04/09/2024
FT' |
Taifa Stars wanamaliza mchezo kwa sare ya bila kufungana
Tanzania 0-0 Ethiopia
Ukurasa rasmi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC). Verified
FT' |
Taifa Stars wanamaliza mchezo kwa sare ya bila kufungana
Tanzania 0-0 Ethiopia
76'| Taifa Stars bado wanatafuta bado
Tanzania 0-0 Ethiopia
60’ |
Tanzania 0-0 Ethiopia
Live TBC Taifa na Mitandao ya kwa anwani ya TBConline
MAPUMZIKO |
HT: Tanzania 0-0 Ethiopia
Matukio ya picha mbalimbali kutokea Uwanja wa Benjamin Mkapa utakakopigwa mchezo wa kuwania kufuzu fainali za mataifa ya Afrika (AFCON) 2025, Taifa Stars dhidi ya Ethiopia.
Fahamu maisha ya JK akiwa mwanafunzi UDSM
Safari yake ya uongozi ilianza kung'aa wakati anasoma katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) pale alipochaguliwa kuwa Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa chuo hicho, chini ya umoja wao ambao kwa kipindi hicho uliofahamika k**a DUSO (Dar es Salaam University Student Organization) baadaye DARUSO.
Huyu hapa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ambaye Jumapili hii ya Septemba 8, 2024, saa 11:00 jioni kupitia mtandao wa YouTube kwa anwani TBC Online kwenye exclusive ya "5 za JK akiwa Mwanafunzi UDSM" ambapo utapata kufahamu mengi kuhusu maisha yake wakati akiwa mwanafunzi wa UDSM.
Bunge limepokea na kukubali taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu uchambuzi wa sheria ndogo zilizowasilishwa bungeni kwenye mkutano wa 14 na wa 15 pamoja na taarifa za utekelezaji wa maazimio ya Bunge kuhusu sheria ndogo zilizowasilishwa bungeni kwenye mkutano wa 12 na wa 13.
Akiwasilisha taarifa hiyo bungeni Jijini Dodoma, Mwenyekiti wa k**ati hiyo Dkt. Jasson Rweikiza amesema lengo la uchambuzi wa sheria hizo ni kuhakikisha mamlaka zilizokabidhiwa madaraka ya kuweka sheria ndogo hazizidi mamlaka ya utungaji sheria yaliyotolewa na watu kwa wawakilishi wao, kuhakikisha madaraka ya kuweka sheria ndogo katika mfumo wa sheria za nchi yaliyokasimiwa na Bunge na mamlaka mbalimbali hayavunji haki za watu wala hayavuki mipaka pamoja na kuhakikisha sheria zinazotokana na Bunge zinaakisi maslahi ya umma.
Pia amebainisha dosari zilizojitokeza katika uchambuzi wa sheria hizo ambazo ni pamoja na sheria ndogo mbili kuwa na masharti yanayokinzana na Katiba, Sheria ndogo kumi kuwa na masharti yanayokinzana na Sheria Mama na sheria nyingine za nchi, Sheria ndogo 22 kuwa na masharti yasiyo na uhalisia, Sheria ndogo 13 kuwa na makosa ya kutoendana na misingi ya uandishi na sheria ndogo 13 kuwa na dosari katika Majedwali.
Bunge limeazimia mapendekezo ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo ya kuzielekeza mamlaka zilizotunga sheria ndogo zenye dosari ya kukinzana na uhalisia, masharti ya katiba ya nchi, sheria mama na sheria nyingine za nchi zifanyiwe marekebisho ya dosari hizo.
Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Luteni Jenerali Salum Haji Othuman ameishukuru Kamati ya Kudumu ya Bunge, Ulinzi na Mambo ya Nje ya Kisiwa cha Ushelisheli kwa kuthamini mchango wa Jeshi hilo katika harakati za ukombozi barani Afrika.
Luteni Jenerali Othuman ameyasema hayo alipotembelewa na k**ati hiyo Makao Makuu ya JWTZ Msalato Jijini Dodoma.
Kwa upande wake
Mwenyekiti wa
Kamati hiyo ya Kudumu ya Bunge, Ulinzi na Mambo ya Nje ya Kisiwa cha Ushelisheli, Francois Adelaide amesema JWTZ imekuwa imekuwa msaada mkubwa kwa nchi nyingi za kusini mwa Afrika.
Amesema nchi yake itaendelea kukuza diplomasia ya ulinzi na Tanzania hasa kwenye mafunzo, mazoezi na kubadilishana ujuzi katika kukabiliana na uhalifu unaovuka mipaka pamoja na kukabiliana na majanga.
Upo mbali na unaisubiri mechi ya Taifa Stars dhidi ya Ethiopia kwa hamu!?
Basi usijali… TBC inakujali na kukuletea matangazo mbashara kwa redio na Televisheni buuure kabisa kuanzia saa 1:00 usiku!
Una kıla sababu ya kufurahia mbungi hii nyumbani kwako bila bugdha yoyote!
Tuiunge mkono Stars kinyumbanii…!
Kiputeee… Msererekooooo!
Mbungiiii Mwaaa Mwiii🔥🔥🔥
Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel amesema katika mwaka wa fedha wa 2024/2025 Serikali imetenga shilingi Bilioni 21.1 kwa ajili ya kununua vifaa tiba vitakavyowezesha kuboresha huduma za uzazi kwa akina mama wakiwemo wenye ulemavu.
Amesema hayo bungeni Jijini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Stella Ikupa aliyeuliza kuhusu hospitali ngapi nchini zimetenga vyumba vya kujifungulia wanawake wenye ulemavu.
Dkt. Mollel amesema hospitali zote za rufaa za mikoa na hospitali za Kanda ambazo ni pamoja na CCBRT za Mtwara na Chato, KCMC, Meta Mbeya na hospitali 184 za halmashauri zina vyumba vya kujifungulia wanawake wakiwemo wenye ulemavu.
Naibu Waziri Mollel amefafanua kuwa Serikali itahakikisha fedha hizo zilizotengwa kwa ajili ya kuboresha huduma za uzazi kwa akina mama zinaboresha miundombinu ikatika vyumba vya kujifungulia ili kukidhi mahitaji ya akima mama wenye ulemavu.
Serikali kupitia Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Ofisi ya Msajili wa Hazima imeanza kupitia upya hali ya uzalishaji wa viwanda vya Korosho vilivyobinafsishwa kikiwemo Kiwanda cha Tunduru kwa lengo la kuhakikisha wawekezaji wa viwanda hivyo wanavifufua.
Kauli hiyo imetolewa bungeni Jijini Dodoma na Waziri wa Kilimo Hussein Bashe wakati akijibu swali la Mbunge wa Tunduru Kaskazini Hassan Kungu aliyeuliza kuhusu sababu za kutofanya kazi kwa kiwanda cha kubangua korosho wilayani Tunduru mkoani Ruvuma kwa miaka saba sasa.
Waziri Bashe ameeleza kuwa kiwanda hicho cha Tunduru chenye uwezo wa kubangua korosho wastani wa tani 3,500 kilijengwa na Serikali mwaka 1981 lakini kutokana na mabadiliko ya kisera Serikali ilikibinafsisha kwa Kampuni ya Korosho African Limited mwaka 2001.
Kiwanda hicho kiliendelea na shuguhili za ubanguaji korosho mpaka mwaka 2019/2020 kilipositisha shughuli zake kutokana na kubangua korosho kwa hasara kinyume na matarajio.
Waziri Bashe amesema tatizo la wawekezaji kuchukua viwanda na kutoviendeleza lipo katika sekta mbalimbali na kwamba Wizara ya Kilimo na Ofisi ya Msajili wa Hazima wameshaanza mazungumzo ili kupitia upya mikataba ya ubinafsishaji kwa lengo la kuangalia masharti yalikuwaje na k**a wawekezaji hao wanakidhi masharti.
Rais Samia Suluhu Hassan ambaye yupo nchini China, akiwa na ujumbe wake amefanya kikao cha pamoja na Rais Xi Jinping wa nchi hiyo na ujumbe wake.
Kikao hicho kimefanyika katika Ukumbi wa The Great Hall of The People Jijini Beijing leo Septemba 04, 2024.
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linaendelea na vikao vyake Jijini Dodoma ambapo miongoni mwa shughuli za leo ni kupokea taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu uchambuzi wa sheria ndogo zilizowasilishwa bungeni kwenye mkutano wa 14 na 15.
Pia litapokea taarifa za Utekelezaji wa Maazimio ya Bunge kuhusu Sheria Ndogo zilizowasilishwa bungeni kwenye mkutano wa 12 na 13.
Leo ni kumbukizi ya siku ya kuzaliwa ya Paul Alphonce, Mtangazaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).
Tunamtakia maisha marefu.
Unailinda vipi jamii dhidi ya ukatili?
Maoni yako yatasomwa katika Kipindi cha Jambo Tanzania
Unadhibiti vipi matumizi ya simu kwa mtoto?
Maoni yako yatasomwa katika kipindi cha Jambo Tanzania
Unayafahamu majukumu ya Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa?
Maoni yako yatasomwa katika Kipindi cha Jambo Tanzania
Yaliyomo katika kurasa za mbele za magazeti leo Septemba 04, 2024
Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 2) wa Mwaka 2024 umepitishwa na Bunge leo Septemba 3, 2024.
Miongoni mwa marekebisho yaliyopitishwa na Bunge ni pamoja sehemu ya saba ya muswada ambayo inapendekeza marekebisho katika Sheria ya Bohari ya Dawa, Sura ya 70 kifungu cha 16A ili kuondoa masharti ya lazima kwa Bohari ya Dawa (MSD) kuwekeza katika uwekezaji unaoruhusiwa katika Sheria ya Uwekezaji wa Wadhamini, Sura ya 53. Lengo ni kuongeza wigo wa uwekezaji wa MSD na kuiwezesha kujiendesha kibiashara k**a taasisi ya kimkakati kwa kuzingatia maelekezo yatakayokuwa yanatolewa na Msajili wa Hazina na mamlaka nyingine zozote zinazohusika.
Aidha kifungu cha 22 cha muswada huo pamoja na sehemu ya sita iliyokuwa ikipendekeza kufanya marekebisho katika Sheria ya Ardhi, Sura ya 113 vimefutwa.
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limeridhia na kupitisha muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Ushindani wa Mwaka 2024 wenye lengo la kutatua changamoto mbalimbali zilizobainika katika utekelezaji wa masharti ya sheria hiyo.
Akitoa hoja mbele ya Bunge jijini Dodoma, Waziri wa Viwanda na Biashara, Selemani Jafo amesema kuwa marekebisho ya muswada huo yataleta manufaa makubwa kwa Watanzania na si kuwakandamiza.
Aidha, akitolea ufafanuzi kifungu cha 13 kilicholeta mjadala mzito bungeni kutokana na kifungu hicho kufuta kifungu cha 17 cha sheria mama kwa kuweka sharti la wauzaji wa bidhaa au huduma kuonesha bei ya kila bidhaa au huduma, Waziri Jafo amesema kifungu hicho hakitawahusu wafanyabishara wadogo huku akisema kifungu hicho kitatungiwa kanuni hivi karibu kabla ya kuanza kutekelezwa.
Hata hivyo, Bunge liliamua kufuta kifungua hicho cha 13 ili kikafanyiwe marekebisho kutokana na kubainika kuwa na mapungufu ya kushindwa kutoa tafsiri ya “wafanyabishara wadogo” inaowalenga.
Aidha Waziri Jafo, amesema kuwa tayari ameielekeza Tume ya Ushindani (FCC) pindi sheria itakapoanza kutumika waanze kutoa elimu kupitia televisheni, mitandao ya kijamii na majukwaa mengine ili kuongeza uelewa kwa jamii kuhusu utekelezaji wa sheria hiyo, huku akibainisha kuwa kutakuwa na usimamizi mzuri wa utekelezaji wa sheria hii na wala si kwa kutumia mabavu.
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Damas Ndumbaro ameongeza adhabu ya faini aliyolimwa msanii Seif Kisauji maarufu Babu wa TikTok kutoka shilingi milioni 3 hadi milioni 5 akimtaka msanii huyo aombe radhi hadharani kutokana na kosa la kurusha mitandaoni maudhui ya sanaa yanayokiuka maadili.
Waziri Ndumbaro ametoa uamuzi huo leo Septemba 3, 2024 Mtumba Jijini Dodoma baada ya kusikiliza rufaa ya msani huyo ya kupinga adhabu aliyopewa na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) ya kufungiwa kujihusisha na shughuli za sanaa kwa miezi sita pamoja na kulipa faini ya shilingi milioni 3 kutokana na kurusha mtandaoni picha za video zinazokiuka maadili.
Aidha, kufuatia rufaa hiyo, msanii Seif Kisauji amekiri kosa la kusambaza maudhui hayo na kuomba apunguziwe adhabu hatua iliyomfanya Waziri Dkt. Damas Ndumbaro amuondolee adhabu ya kifungo cha cha miezi 6 cha kutojihusisha na shughuli za sanaa lakini akimwongezea kiwango cha faini kutoka milioni 3 hadi 5.
Sheria ya Basata iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2019 kifungu cha 15 A inampa mamlaka Waziri mwenye dhamana ya masuala ya sanaa kusikiliza rufani na kutoa maamuzi.
"Kwa kushauriana na Naibu Waziri, Hamis Mwinjuma (MwanaFA) ambaye ndiye msimamizi wa sekta ya sanaa, nimefuta adhabu ya miezi sita aliyopewa kuanzia leo, lakini ninamtaka azingatie maadili katika kufanya kazi zake" amesisitiza Waziri Ndumbaro.
Awali katika kikao hicho Naibu Waziri Mwinjuma alimtaka msanii huyo, kurudi katika sanaa aliyokuwa akiifanya zamani ambayo ndiyo iliyomfanya jamii imtambue na kuelewa kuwa yeye ni kioo cha jamii hivyo anapaswa kufanya sanaa inayoelimisha na kuburushisha jamii bila kuharibu mila na desturi za Kitanzania.
Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Xavier Daudi amewataka wakurugenzi wa utawala na usimamizi wa rasilimali watu wa wizara pamoja na waratibu wa jinsia, ngazi ya wizara, kuweka mbinu za kuimarisha mfumo wa utoaji haki, kudhibiti uonevu, dhuluma na unyanyasaji.
Naibu Katibu Mkuu amesema hayo leo wakati akifungua Semina Elekezi ya Mwongozo wa Jinsia (2023) kwa wakurugenzi wa utawala na usimamizi wa rasilimali watu wa wizara pamoja na waratibu wa jinsia ngazi ya wizara jijini Dodoma.
Amesema kumekuwepo kwa viashiria vinavyominya haki za watumishi k**a kutokupata stahiki zao kwa wakati, kutopewa nafasi za kujiendeleza, kukataliwa uhamisho, kutopewa likizo na nauli ya likizo kwamba ni mambo yanayo fedhehesha watumishi wa umma.
Amesema ujumuishwaji wa masuala ya jinsia ni muhimu sana maana ni chachu na huleta ufanisi na tija katika utendaji wa kazi. Aidha amesema hatua hiyo huwawezesha watumishi wanaume kwa wanawake kutumia ujuzi, vipaji na vipawa walivyonavyo kutekeleza majukumu yao na kuleta taswira njema katika taasisi zao.
Nyota wa Timu ya Al-Hilal ya Saudi Arabia, Neymar Jr, ameendelea kujifua ili kujiweka sawa kwa ajili ya msimu mpya wa Ligi Kuu ya Roshn Saudi Arabia, baada ya kukaa nje kwa miezi 11.
Baada ya kujiunga na Al-Hilal, Neymar alipata majeraha ambayo yamemweka nje ya uwanja hadi sasa. Timu hiyo ya Al-Hilal, pamoja na mfungaji huyo bora wa muda wote wa Brazil, wamekuwa wakichapisha picha mbalimbali mitandaoni zinazoonyesha Neymar akifanya mazoezi ya utimamu wa mwili, akijiandaa kabla ya kuanza mazoezi ya pamoja na kikosi chake.
Neymar, ambaye ana mkataba wa miaka miwili na matajiri hao wa Jiji la Riyadh, amecheza mechi tano tu kabla ya kupata majeraha akiwa na Timu ya Taifa ya Brazil dhidi ya Uruguay mnamo Oktoba 2023.
Mshambuliaji wa Timu ya Taifa Uruguay, Luis Suárez, ametangaza kustaafu soka la kimataifa.
Akizungumza huku akitokwa machozi wakati wa mkutano na waandishi wa habari mjini Montevideo, Uruguay, Suárez, mwenye umri wa miaka 37, amethibitisha kuwa mechi ya kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Paraguay itakayochezwa Septemba 5, itakuwa ya mwisho kwake akiwa na timu yao ya taifa.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa Liverpool na Barcelona ni mfungaji bora wa muda wote wa Uruguay akiwa na mabao 69 katika michezo 142, tangu aanze kuchezea timu ya taifa katika mechi dhidi ya Colombia mnamo Februari 2007.
"Nimekuwa nikifikiria na kuchambua hili. Ninaamini huu ndio wakati sahihi," amesema Suárez.
Suárez amecheza mashindano makubwa tisa ya kimataifa akiwa na Timu ya Taifa ya Uruguay.
Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Ushindani wa mwaka 2024 umewasilishwa bungeni leo Septemba 03, 2024 kwa lengo la kuufanyia marekebisho yanayopendekezwa, ili kutatua changamoto mbalimbali zilizobainika katika utekelezaji wa masharti ya sheria.
Akiwasilisha Muswada huo bungeni Jijini Dodoma Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Selemani Jafo amesema vifungu vya 5 na 8 vya muswada huo vinapendekezwa kufanyiwa marekebisho kwa kuanzisha dhana ya "Hodhi ya Pamoja" na kuongeza kiwango cha hodhi ya soko kutoka asilimia 35 hadi 40 Ili kuweka vikwazo dhidi ya matumizi mabaya ya hodhi ya soko inayohusisha mtu zaidi ya mmoja na kuendana na mabadiliko ya kiuchumi na maendeleo yanayofanyika katika ngazi ya kitaifa, kikanda na kimataifa.
Aidha, kifungu cha 10A na 11A vinapendekeza kuongezwa ili kuweka masharti yanayozuia makubaliano baina ya watu walio katika ngazi tofauti katika mnyororo wa uuzaji wa bidhaa pamoja na Tume ya Ushindani kuidhinisha muungano wa kampuni wenye manufaa makubwa kwa umma huku kifungu cha 17 pamoja na Jedwali la Marekebisho katika aya B kikipendekezwa kufutwa na kuandikwa upya kwa kuweka sharti la wauzaji wa bidhaa au huduma kuonesha bei ya kila bidhaa au huduma.
Waziri Jafo amesema kuwa vifungu vya 61 na 84 vinapendekezwa kurekebishwa ili
mtu ambaye hajaridhika na maamuzi ya Baraza la Ushindani aweze kukata rufaa Mahak**a Kuu ambayo itasikilizwa na majaji watatu kwa lengo la kutoa fursa kwa mtu ambaye hajaridhika na maamuzi ya Baraza kuweza kutafuta haki kwenye chombo cha juu zaidi cha utoaji haki.
Bunge litaendelea kuujadili muswada huo na kisha kusomwa kwa mara ya tatu kabla ya kupitishwa.
Bodi ya Wakurugenzi ya Azam FC na Kocha Youssouph Dabo wamefikia makubaliano ya pande mbili ya kutoendelea kufanya kazi pamoja kuanzia leo Septemba 03, 2024.
Dabo, aliyehudumu kwenye klabu hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja, anaondoka pamoja na wasaidizi wake wa benchi la ufundi aliokuja nao.
Hatua hiyo imekuja baada ya mwenendo mbaya wa klabu hiyo ya Azam tangu kuanza kwa msimu huu hasa baada ya kuondolewa
kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika kwa kufungwa jumla ya mabao 2-1 na Klabu ya APR ya Rwanda na kutoka sare katika mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu ya NBC.
Dabo atakumbukwa kwa mafanikio yake ndani ya matajiri wa Chamazi, Azam FC, ambapo msimu uliopita wa 2023/2024 aliiwezesha timu hiyo kumaliza msimu katika nafasi ya pili ikiwa na pointi 69, na kuisaidia kufuzu kucheza mashindano ya CAF Champions League (CFL).
Mafunzo kwa Shirikisho la Askari wa K**e na wasimamizi wa sheria duniani yanaendelea katika Jiji la Chicago, Marekani kwa kushirikisha nchi mbalimbali ikiwemo Tanzania.
Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Naibu Kamishna wa Uhamiaji kutoka Tanzania DCI Tatu Burhan amesema mafunzo waliyopatiwa yamejikita katika masuala ya ushirikiano wa kimataifa na utatuzi wa changamoto za wahamiaji wanaoingia katika mataifa mbalimbali na namna bora ya kutatua changamoto hizo.
Amesema mafunzo hayo yamewapa mwanga wa namna bora ya kukabiliana changamoto za wahamiaji ambao wamekuwa wakiingia katika nchi mbalimbali kwa lengo la makazi huku akiweka wazi kuwa suala la wahamiaji ni mtambuka.
Kwa upande wake
Ronald Vitiello ambaye ni
Mkufunzi Kutoka Wizara ya Huduma za Binadamu katika Jiji la Chicago akitoa mada kuhusu mipaka na wahamiaji amesema ni muhimu kwa washiriki wa mafunzo hayo kubadilishana uzoefu wa namna ya kukabiliana na wahamiaji.
Mafunzo hayo yanaendelea huku mada mbalimbali zikiwasilishwa ili kuwajengea uwezo wa kiutendaji washiriki hao ambao ni kutoka nchi 64 duniani.
Bunge kuendelea kujadili Miswada leo
Baadhi ya wabunge wakiwasili bungeni Jijini Dodoma kushiriki kikao cha sita cha mkutano wa 16 wa Bunge hilo.
Shughuli za leo za Bunge ni pamoja na kujadiliwa kwa miswada miwili ambayo ni Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria
ya Ushindani wa mwaka 2024 na Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 2) wa mwaka 2024.
Aidha, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo pamoja na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria zitawasilisha maoni kuhusu miswada hiyo.
Miswada hiyo itasomwa kwa mara ya pili na ya tatu kabla ya kupitishwa na Bunge.
Dar Es Salaam
Be the first to know and let us send you an email when TBConline posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.
Send a message to TBConline:
Mashabiki wa soka na Timu ya Taifa Stars wamelitaka Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuvunja benchi la ufundi ili kutengeneza timu ya Taifa katika muundo utakaoleta ushindi. Hii ni baada ya kukamilika mchezo wa Taifa Stars ikitoka suluhu na Ethiopia 0-0. Je, kuna haja ya kuvunja benchi la ufundi la timu ya Taifa? 🎤 @e_j1official 🎥 @simbeyezekiel
Mwanamuziki na mpenzi wa soka, Foby amesema Taifa Stars haijacheza vizuri dhidi ya Ethiopia kutokana na kutokaa kambini kwa muda mrefu ambao ungesaidia kutengeza muunganiko mzuri wa timu. Foby amesema kukosekana kwa Mbwana Samatta pamoja na Simon Msuva siyo sababu ya timu ya taifa kukosa matokeo mazuri bali wachezaji kukosa muunganiko. Hata hivyo amesisitiza kwamba timu ya Taifa bado ina nafasi ya kufuzu fainali za AFCON 2025 kutokana na ubora wa baadhi ya wachezaji waliopo katika timu ya taifa. 🎤 @e_j1official 🎥 @simbeyezekiel
Mashabiki wa Timu ya Taifa Stars wamesema siyo kila mtu maarufu anaweza kuhamasisha mashabiki kujitokeza uwanjani kuja kuipa nguvu timu ya Taifa. Badala yake wamesema kwamba mashabiki ndio watu wa mpira na watumike wao kuhamasisha tofauti na kutumia wasanii kuhamasisha mashabiki kuja uwanjani. Mchezo umekamilika Taifa Stars dhidi ya Ethiopia kwa matokeo ya 0-0 ikiwa ni mchezo wa kwanza wa kuwania kufuzu fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025. 🎤@e_j1official 🎥 @simbeyezekiel
Shabiki wa Timu ya Taifa Stars amesama mchango wa Rais Samia Suluhu Hassan katika michezo umeonekana kuongeza hamasa hasa kwa namna anavyomwaga pesa kwa kila goli ambalo timu zetu zimekuwa zikicheza katika michuano kimataifa. “Goli la Mama limekuwa na mchango mkubwa sana kwa timu zetu hata kwa timu ya Taifa kwani inawapa morali wachezaji,” amesisitiza shabiki huyo. Ni kuelekea mchezo wa kuwania kufuzu fainali za mataifa ya Afrika (AFCON) 2025, Tanzania ikikipiga leo dhidi ya Ethiopia. Mchezo huo utakuwa mbashara kupitia Televisheni ya Taifa TBC1 na redio, TBC Taifa. @e_j1official @simbeyezekiel
Mashabiki wa Simba na Yanga pamoja na vilabu vingine nchini wamesema leo wameungana kwa kuondoa tofauti zao na kwamba leo lao ni moja tu; kuipa nguvu Taifa Stars kwa pamoja kwani klabu zao zinatumika pia kutoa wachezaji wa kuijenga timu ya Taifa. Ni kuelekea mchezo wa kuwania kufuzu fainali za mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 zitakazofanyika nchini Morocco. Mchezo wa leo Tanzania watakipiga dhidi ya Ethiopia kuanza saa 1:00. 🎤 @e_j1official 🎥 @simbeyezekiel
JK: Maandalizi ya mapema yatatupa heshima Afcon 2027 Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete amesema, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na klabu za Tanzania wanapaswa kuwaandaa wachezaji wazawa ili kujenga timu ya Taifa imara itakayofanya vizuri kwenye michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027. Kikwete amesema, lazima klabu na TFF zikae pamoja na klabu kubwa za Simba, Yanga na Azam ili kuweka mkakati wa kuwajenga wachezaji wanaoweza kuonesha ushindani mkubwa kwenye michuano hiyo. Rais Mstaafu Kikwete ametoa ushauri huo alipofanya mahojiano maalum na TBC Digital kuhusiana na nafasi ya Tanzania kwenye michuano ya Afcon ya mwaka 2027 ambapo Tanzania, Kenya na Uganda wameshinda nafasi ya kuandaa michuano hiyo. Kikwete ambaye ni mpenzi mkubwa wa soka, amesema, kujenga viwanja bora ni jambo moja lakini lazima tuwe na timu yenye uwezo wa kuvitumia viwanja hivyo na kuonesha umahiri mkubwa wa kusakata kabumbu kama waandaji wa michuano hiyo. Amesema, muda wa maandalizi ni sasa ili kuwa na timu bora ya Taifa itakayokuwa na uwezo wa kushindana hata kufika fainali kwenye michuano hiyo na sio kusindikiza wengine. Amepongeza uamuzi wa Serikali kuhakikisha Tanzania inaandaa michuano hiyo kwa kutoa baraka kwa TFF kuomba nafasi ya kuandaa Afcon kwa kushirikiana na Kenya na Uganda na kwamba hiyo ni hatua kubwa na ya kihistoria.
Mashabiki wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars wakitamba wao kuwa wazalendo kwa kuipambania timu ya Taifa hasa kwa kutoa hamasa kwa Watanzania kujitokeza kufuatilia mchezo wa leo dhidi ya Ethiopia. “Toka hasubuhi tumezunguka kwenye vyombo mbalimbali vya habari kama kikundi cha kujitolea kuhamasisha Watanzania kuja uwanjani ili kuwapa nguvu wachezaji wetu. Sisi ni wazalendo wa kweli,” amesema shabiki mmoja wapo. Mchezo huo wa kuwania kufuzu fainali za mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 ni katika ya Taifa Stars na Ethiopia. Mchezo huo utapigwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa kuanzia saa 1:00 usiku na kurushwa na TBC1 na TBC Taifa. 🎤@e_j1official 🎥 @simbeyezekiel
Shabiki wa Timu ya Taifa Stars amesema timu yetu ya Taifa inahitaji uzalendo kwa kuipa nguvu bila kujali kama wanafanya vizuri au vinginevyo akisisitiza kwamba wachezaji ni kama watoto, muda wote wanahitaji kushangiliwa ili wafanye vizuri zaidi. Aidha amewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi katika Dimba la Benjamin Mkapa kuipa sapoti Stars kwa kuishangalia mwanzo mwisho bila kuangalia matokeo itakapocheza dhidi ya Wahabeshi kutoka Ethiopia kuanza saa 1:00 jioni. Mchezo utarushwa bureeeeee na kukuijia sebuleni kwako au kibanda umiza na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kupitia redio na televisheni. 🎤 @e_j1official 🎥 @simbeyezekiel
Kuelekea mchezo wa kuwania kufuzu fainali za mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 timu ya Taifa Stars leo watashuka dimbani kukipiga na Ethiopia katika Uwanja wa Benjamin Mkapa. Shabiki wa Taifa Stars amesema amelipia mashabiki 20 kwa ajili ya kuingia uwanjani ili kuipa nguvu timu ya Taifa dhidi ya Wahabeshi hao kutoka Ethiopia. Mchezo huo utachezwa saa 1:00 na kurushwa bure kabisa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kupitia redio na televisheni. @e_j1official @simbeyezekiel
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas, amesema ujenzi wa Bandari ya Mbamba Bay itakayokuwa makao makuu ya bandari za Ziwa Nyasa utakapokamilika, unatarajia kuongeza ufanisi wa Bandari ya Dar es Salaam na ushoroba wa Mtwara na hivyo kuongeza fursa za ajira na kuinua uchumi wa mkoa huo na Taifa kwa ujumla. Kwa sasa, amesema kazi ya usanifu na ujenzi wa uendelezaji wa bandari hiyo iliyopo wilayani Nyasa mkoani Ruvuma inaendelea kwa gharama ya shilingi bilioni 80.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Gerald Kusaya amehuisha taarifa zake katika Daftari la Kudumu la Mpiga Kura kwenye kituo cha uandikishaji cha Mkendo katika Manispaa ya Musoma mkoani Mara. Zoezi hilo limeanza leo Septemba 04, 2024 na linatarajiwa kukamilika Septemba 10, 2024, ambapo Kusaya amewataka wananchi wa Mara kuhakikisha wanajitokeza kujiandikisha pamoja na kuboresha taarifa zao.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Jumanne Sagini ametaja adhabu mbalimbali ambazo kwa mujibu wa sheria ya makosa ya adhabu zinatolewa kwa mtu aliyetenda makosa ya ubakaji. Amesema kifungu cha 131 kifungu kidogo cha 1 cha sheria ya kanuni ya adhabu sura ya 16 kimeainisha adhabu ya makosa ya kubaka kuwa ni kifungo kisichopungua miaka 30, viboko, na mahakama inaweza kutoa amri ya kumlipa fidia muathirika wa tukio. Aidha, amesema kuwa kifungu cha 131 kifungu kidogo cha 3 cha sheria hiyo kimeainisha kuwa ikiwa muathirika wa tukio ni mtoto mwenye umri wa chini ya miaka 10 adhabu pekee iliyopo ni kifungo cha maisha jela. Naibu Waziri Sagini amesema hayo bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Najma Giga aliyeuliza kama Serikali haioni haja ya kupeleka bungeni Muswada wa Sheria utakaotoa adhabu ya kifo kwa wabakaji watoto walio na umri wa chini ya miaka tisa. Naibu waziri Sagini ameongeza kuwa endapo kosa hilo la ubakaji litatekelezwa na mtoto basi atahukumiwa na mahakama kwa mujibu wa sheria ya watoto.
Timu ya Pamba Jiji FC ya Mwanza inaendelea na maandalizi ya kuwakabili Singida Black Stars Septemba 15 katika Uwanja wao wa nyumbani, CCM Kirumba ulioko jijini Mwanza. Akizungumza na TBC Digital mkoani Mwanza, Msemaji wa Pamba Jiji, Moses William amesema katika mchezo huo mashabiki wa Pamba watarajie kuona mabao mengi zaidi timu yao ikiwabugiza wapinzani na kuwataka siku ya mechi kujitokeza kwa wingi. Halikadhalika, William amesema klabu hiyo haifikirii kuachana na Kocha wao, Goran Kopunovic.
Huku Klabu ya Pamba Jiji ya Mwanza 'Wana TP Lindanda' wakiwa wamerejea Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya kukaa nje kwa miaka 22, wapenzi wa klabu nyingine iliyotikisa Jiji la Mwanza, Toto Africans pia wamehamasika wakihaha ili kuona timu yao ikirejea kukiwasha na kuwapa burudani. Mgongano wa maslahi unatajwa kuwa chanzo cha kupotea kwa klabu ya Toto Africans tangu iliposhuka daraja mwaka 2015 na imekuwa ikijaribu kurudi bila mafanikio huku ukata na kukosekana kwa uongozi imara vikitajwa kuwa sababu. Mwandishi Wetu Jofrey Kobeto aliyepo jijini Mwanza amezungumza na wadau wa timu hiyo ambao wameuomba uongozi wa Mkoa Mwanza kuingilia kati suala hilo ili kurejesha timu hiyo na kuongeza burudani katika jiji hilo linaloaminika kuwa la pili kwa ukubwa nchini Tanzania baada ya Dar es Salaam. Toto Africans Football Club ilianzishwa miaka 1970 na ilikuwa ni moja ya vilabu maarufu kutoka Kanda ya Ziwa Victoria kushiriki katika Ligi ya Tanzania na kutoa mchango mkubwa katika kukuza vipaji vya soka nchini. Historia inaonesha kwamba Toto Africans ilianza kama timu ya wachezaji wa ndani wa Mwanza na polepole ilikuja kuwa klabu yenye nguvu katika soka la Tanzania. Katika miaka ya 1980 na 1990, timu hii ilijijengea jina kama moja ya timu imara katika ligi. Ingawa klabu haijashinda mataji makubwa kama baadhi ya vilabu vikubwa nchini Tanzania, ushiriki wake katika Ligi Kuu na mashindano ya kitaifa ulikuwa ukileta hamasa kubwa jijini Mwanza na Tanzania kwa ujumla na hasa ilipokuwa ikikutana Pamba. Yapo madai kwamba Toto Africans ilikuwa na uhusiano wa kijamii na kisoka na Yanga Afrika sambamba na Klabu ya African Sports ya Tanga ambayo pia kwa muda mrefu imepotea kwenye ramani ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara.
Mchezaji wa timu ya Taifa ya soka ya Tanzania, Dickson Job amesema wao kama wachezaji wamejipanga vema na wako tayari kuikabili Ethiopia katika mchezo wa hapo kesho. "Sisi kama wachezaji tuko tayari kwa asilimia 100. Walimu wetu tayari wamekamilisha kazi yao uwanjani kwenye mazoezi, na kilichobaki ni kumuomba Mwenyezi Mungu atupe afya njema. Tunawahakikishia Watanzania kwamba tutaenda kupambana kwa ajili ya timu yetu ya Tanzania." amesema Job Taifa Stars inashuka katika dimba la Benjamin Mkapa, Dar es Salaam kesho Septemba 04, 2024 katika mchezo wake dhidi ya Ethiopia, kusaka tiketi ya kushiriki Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) mwaka 2025.
Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 2) wa mwaka 2024 umewasilishwa bungeni Jijini Dodoma leo Septemba 03, 2024. Akiwasilisha Muswada huo Mwanasheria Mkuu wa Serikali Hamza Johari amesema muswada huo unapendekeza marekebisho katika Sheria kuu nane ambazo ni Sheria ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu Sura ya 432, Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Jinai Sura ya 20, Sheria ya Serikali Mtandao Sura ya 273, Sheria ya Uhamiaji Sura ya 54, Sheria ya Ardhi Sura ya 113, Sheria ya Bohari ya Dawa Sura ya 70, Sheria ya Viwango Sura ya 130 na Sheria ya Tume ya Mipango Sura ya 127. Amesema miongoni mwa marekebisho yanayopendekezwa ni kurekebisha Sheria ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu Sura ya 432 ili kuimarisha nyanja zote za kuzuia usafirishaji haramu wa binadamu huku Sehemu ya nne ya Muswada in kipendekeza kufanya marekebisho katika Sheria ya Serikali Mtandao Sura ya 273 ili kuweka uwiano wa adhabu na kosa lililotendeka na kuzuia watu kutenda au kujaribu kutenda kosa husika na kifungu cha 57 kinapendekezwa kurekebishwa ili kuongeza adhabu kwa kosa la kuondoa, kuharibu au kubadili data, kumbukumbu za kielektroniki, mifumo au vifaa vya kielektroniki. Sehemu ya tano ya Muswada huo inapendekeza kufanya marekebisho katika Sheria ya Uhamiaji, Sura ya 54 Ili kuondoa mapungufu yaliyojitokeza wakati wa utekelezaji wa sheria, vilevile inapendekezwa kurekebishwa kwa ajili ya kuweka masharti yanayohusu hadhi maalum kwa raia wa nchi nyingine mwenye asili ya Tanzania pamoja na marekebisho katika kifungu cha 20 ambacho kinaweka masharti kuhusu utaratibu wa kuchukua maelezo ya mtu anayeshukiwa. Bunge litaendelea kujadili muswada huo kisha kusomwa kwa mara ya tatu kabla ya kupitishwa.
Mbunge wa Jimbo la Kigamboni Dkt. Faustine Ndugulile kwa mara ya kwanza tangu achaguliwe kuwa Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika amewashukuru Watanzania wote mbele ya Bunge linaloendelea na vikao vyake Jijini Dodoma kwa kumuunga mkono katika mchakato mzima wa uchaguzi hadi kuibuka mshindi katika nafasi hiyo. Dkt. Ndugulile amechaguliwa kuwa Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani Kanda ya Afrika katika mkutano wa 74 wa Kamati ya Shirika la Afya Duniani Kanda ya Afrika uliyofanyika Congo- Brazzaville Agosti 27, 2024 na kuwashinda wagombea wengine kutoka Niger na Senegal.
Naibu Waziri wa Nishati Judith Kapinga ametoa ufafanuzi bungeni Jijini Dodoma kuhusu utaratibu unaotumiwa na Serikali kuwalipa fidia watu wanaoathiriwa na majanga yanayotokana na hitilafu za umeme. Amesema Serikali kupitia taasisi zilizo chini ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) hufanya uchunguzi ili kujiridhisha kama madhara yaliyotokea yamesababishwa na mifumo ya taasisi zake na inapobainika ni kweli, mwananchi anaweza kulipwa fidia kwa kufuata taratibu za kisheria. Naibu Waziri Judith Kapinga ametoa ufafanuzi huo alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Anatropia Lwehikila aliyeuliza kuhusu utaratibu unaotumika kuwalipa fidia watu wanaopata majanga yanayosababishwa na hitilafu za umeme.
Mafunzo kwa Shirikisho la Askari wa Kike na wasimamizi wa sheria duniani yanaendelea katika Jiji la Chicago, Marekani kwa kushirikisha nchi mbalimbali ikiwemo Tanzania. Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Naibu Kamishna wa Uhamiaji kutoka Tanzania DCI Tatu Burhan amesema mafunzo waliyopatiwa yamejikita katika masuala ya ushirikiano wa kimataifa na utatuzi wa changamoto za wahamiaji wanaoingia katika mataifa mbalimbali na namna bora ya kutatua changamoto hizo. Amesema mafunzo hayo yamewapa mwanga wa namna bora ya kukabiliana changamoto za wahamiaji ambao wamekuwa wakiingia katika nchi mbalimbali kwa lengo la makazi huku akiweka wazi kuwa suala la wahamiaji ni mtambuka. Kwa upande wake Ronald Vitiello ambaye ni Mkufunzi Kutoka Wizara ya Huduma za Binadamu katika Jiji la Chicago akitoa mada kuhusu mipaka na wahamiaji amesema ni muhimu kwa washiriki wa mafunzo hayo kubadilishana uzoefu wa namna ya kukabiliana na wahamiaji. Mafunzo hayo yanaendelea huku mada mbalimbali zikiwasilishwa ili kuwajengea uwezo wa kiutendaji washiriki hao ambao ni kutoka nchi 64 duniani.
TBC is your news, entertainment, music fashion website. We provide you with the latest breaking news and videos straight from the entertainment industry.