Zanzibarleo Online

Zanzibarleo Online Pata habari za uhakika na kuaminika kutoka Gazeti namba 1 visiwani Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.

KATIBU Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Neema Msitha, amesema mafanikio yaliyopatikana katika sekta ya mich...
19/02/2025

KATIBU Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Neema Msitha, amesema mafanikio yaliyopatikana katika sekta ya michezo ndani ya kipindi cha miaka minne, yanamchango mkubwa wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza na waandishi wa habari, jijini Dodoma Msitha alisema kuwa katika kipindi hicho, kumekuwa na ongezeko kubwa la ufadhili, ujenzi wa miundombinu ya kisasa na ushirikiano wa kimataifa, hatua ambazo zimechangia mafanikio katika sekta ya michezo.

Alisema miongoni mwa miradi ya miundombinu iliyotekelezwa ni ukarabati wa Uwanja wa Benjamin Mkapa uliogharimu shilingi bilioni 31, ujenzi wa uwanja mpya wa michezo jijini Arusha wenye gharama ya shilingi bilioni 338, pamoja na ujenzi wa uwanja mpya wa michezo Dodoma utakaogharimu shilingi bilioni 310.

"Serikali imewekeza shilingi bilioni 21 katika ujenzi wa viwanja vya mazoezi k**a Gymkhana, Leaders Club, TIRDO, Law School na uwanja wa Farasi", alisema Neema.

KAMBI ya matibabu uliyoitishwa na madaktari bingwa wa Tanzania nchini Comoro imeanza kwa mwitikio mkubwa kwa raia wa nch...
18/02/2025

KAMBI ya matibabu uliyoitishwa na madaktari bingwa wa Tanzania nchini Comoro imeanza kwa mwitikio mkubwa kwa raia wa nchi hiyo kujitokeza kwa wingi.

Mamia ya raia wa Comoro wenye matatozo mbalimbali ya kiafya wamejitokeza kupata huduma zinazotolewa kwa ushirikiano na madakatari wazawa katika kisiwa cha Ngazija.

Madaktari hao wanatoa huduma za uchunguzi na matibabu kwa wagonjwa wanaosumbuliwa na maradhi ya mifupa, figo na vibofu vya mkojo, mifupa, saratani, moyo na mengineyo ambapo takribani wagonjwa 417 wameandikishwa katika siku ya kwanza.

Akizungumza katika kikao cha tathmini ya uendeshaji wa kambi hiyo inayoratibiwa ubalozi wa Tanzania nchini Comoro na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Kaimu Mkuu wa msafara,Dk. Salehe Mwinchete, alieleza kuwa ushirikiano waliopewa na madaktari wenyeji ni mkubwa na raia wa Comoro wamejitokeza kwa wingi na hilo limewatia moyo kuwa siku zinazofuata hali itakuwa bora zaidi.

JUMLA ya wananchi  mia mbili na sita  (206)  wenye matatizo ya mtoto wa jicho wamefanyiwa matibabu kwa njia ya upasuaji ...
18/02/2025

JUMLA ya wananchi mia mbili na sita (206) wenye matatizo ya mtoto wa jicho wamefanyiwa matibabu kwa njia ya upasuaji kufuatia kambi maalumu ya Madaktari Bingwa kutoka Hospitali ya Rufaa Mnazi Mmoja iliyofanyika katika Hospitali ya Wilaya ya Chake Chake Vitongoji Kisiwani Pemba .

Kambi hiyo ya wiki moja iliyowekwa na Wizara ya Afya kupitia shirika la Living Stone Chartable Trust la Uiengereza, iliendeshwa na madaktari bingwa wa maradhi hayo.

Akizungumzia kambi hiyo, Mratib wa huduma za macho Zanzibar Dr. Fatma Juma Omar alisema jumla ya watu 403 walijitokeza kwa uchunguzi wa awali ambapo watu 206 walipatiwa matibabu kwa njia ya upasuaji na wengine kupata matibabu mengine ya kawaida pamoja na ushauri wa daktari.

Alieleza kambi hiyo ilihusisha Uchunguzi wa maradhi mbali mbali ya macho pamoja na kufanyiwa upasuaji kwa kutolewa mtoto jicho.

WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Amali, imesema ifikapo mwezi Machi mwaka huu wanafunzi wote wa skuli za umma wataanza kuso...
18/02/2025

WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Amali, imesema ifikapo mwezi Machi mwaka huu wanafunzi wote wa skuli za umma wataanza kusoma mkondo mmoja kwani kazi ya ujenzi wa miundombinu imeanza kukamilika.

Vile vile, serikali hivi sasa imeweka mpango wa kuzivunja skuli za zamani na kujenga za horofa, ili kupata madarasa mengi yatayowafanya wanafuzi kuingia mkondo mmoja.

Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Ali Abdulgulam Hussein, aliyasema katika mkutano wa 18 wa kikao cha 10 cha Baraza la Wawakilishi kinachoendelea kufanyika huko Chukwani nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.

Soma zaidi: https://zanzibarleo.co.tz/smz-kuzivunja-skuli-za-zamani-mkondo-mmoja-kuanza-rasmi-machi/

CHUO Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kilichipo mkoani Morogoro, kimebaini mkojo wa paka unaweza kutumika kufukuza pan...
17/02/2025

CHUO Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kilichipo mkoani Morogoro, kimebaini mkojo wa paka unaweza kutumika kufukuza panya wanaoshambulia mazao ya wakulima hali ambayo itamsaidia mkulima kulima na kuvuna mazao yake hasa mahindi bila kikwazo.

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kudhibiti Viumbe Hai Waharibifu wa Chuo hicho, Prof. Allen Malisa, ambapo alieleza utafiti uliofanywa na chuo hicho umebaini mkojo wa paka unafaa kuwadhibiti panya.

Alisema baada ya kupata changamoto kutoka kwa wakulima wakiwemo wa Mikese juu ya mazao yao, waliamua kufanya utafiti wa mkojo wa paka unavyoweza kuwafukuza panya mashambani.

Alisema walik**ata paka kadhaa na kuchukua mkojo wao ambapo wameuchanganya na unga wa mahindi na kuwapa panya.

Utafiti huo unaonesha kuwa kutumia mkojo wa paka kunaleta tija kulinganisha na njia nyengine za kufukuza panya, na mkojo wa paka jike unafanya kazi vizuri zaidi kufukuza panya kuliko mkojo wa paka dume.

Alisema utafiti wa kutumia mkojo wa paka unatumika kuwafukuza panya shambani tu na siyo kuwaua.

Aliwataka wananchi hususani wakulima kufuga paka kwa wingi kwani mkojo wake ni ‘dili’, hivyo wanaweza kuuuza na kujipatika kipato au wao wenywe kuutumia kufukuza panya.

ANGOLA imerekodi visa 3,402 vya kipindupindu na vifo 114 tangu mripuko huo uanze mapema Januari, kulingana na taarifa ya...
13/02/2025

ANGOLA imerekodi visa 3,402 vya kipindupindu na vifo 114 tangu mripuko huo uanze mapema Januari, kulingana na taarifa ya kila siku ya Wizara ya Afya kwa vyombo vya habari hapo jana.

Tangu Februari 1, Angola imekuwa ikiripoti zaidi ya visa 100 vipya vya kipindupindu kila siku, na kufikia 295 Februari 8.

Hata hivyo, upimaji wa kimaabara kuthibitisha maambukizi bado ni mdogo, huku tangu kuzuka kwa ugonjwa huo Januari 7, ugonjwa huo umeenea katika majimbo mengi, huku Luanda na mkoa jirani wa Bengo ndio watu wake walioathirika zaidi.

Zaidi ya watu 925,000 wamechanjwa dhidi ya kipindupindu, ikiwa ni pamoja na asilimia 86 ya watu wanaolengwa, kulingana na taarifa ya Wizara ya Afya kuhusu magonjwa.

JESHI la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi linatarajia kumfikisha mahak**ani Febuari 13, mwaka mtuhukiwa Khadija Shaaban Al...
13/02/2025

JESHI la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi linatarajia kumfikisha mahak**ani Febuari 13, mwaka mtuhukiwa Khadija Shaaban Ali (34) mkaazi wa Chukwani kwa tuhuma za kumjeruhi mke mwenzake kwa kisu sehemu mbali mbali za mwili.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya Habari, Kamanda wa Polisi mkoa wa Mjini Magharibi, SACP Richard Thadei Mchomvu, alisema bado wanamshikilia mwanadada huyo anayetuhumiwa kufanya tukio hilo na kumuhoji na kubaini kuwa tukio hilo limechochowa na wivu wa mapenzi.

Akizungumzia mume wa wanandoa hao, alisema ndie aliyetoa msaada kufanikisha mke wake kufikishwa polisi bila ya kukimbia na kumtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Khadija Shaaban Ali (34) makaazi wa Chukwani.

“Katika tukio hilo Maimuna Said Suleiman (38) alijeruhiwa kwa kukatwa kwa visu maeneo mbali mbali ya mwili wake na mke mwenzake aliyetambulika kwa jina la Khadija Shaaban Ali (34) wakaazi wa Chukwani mnamo Febuari 9, mwaka huu majira ya saa 7 za mchana”, alieleza SACP Mchomvu.

Alibainisha siku ya tukio wote watatu walikuwepo pamoja wakiwa kwenye gari na walipofika nyumbani kwa mke mdogo ghafla mke mkubwa anatoka kwenye gari alitoa kisu kuanza kumshambulia mke mdogo wakati mume wao akiwa ameshaingia ndani ya nyumba

Soma zaidi: https://zanzibarleo.co.tz/aliyemjeruhi-mke-mwezake-kufikishwa-mahak**ani-leo/

WANAFUNZI wa darasa la tatu wanatarajia kufanya mitihani ya upimaji wa kitaifa mwaka huu ikiwa ni utekelezaji wa mtaala ...
12/02/2025

WANAFUNZI wa darasa la tatu wanatarajia kufanya mitihani ya upimaji wa kitaifa mwaka huu ikiwa ni utekelezaji wa mtaala mpya wa elimu ulioanza kutekelezwa mwaka 2022.

Akizungumza na gazeti hili Mkurugenzi Mtendaji Baraza la Mitihani Zanzibar, Dk. Rashid Abdul-azizi Mukki, alisemai mitihani hiyo tawaandaa vyema wanafunzi katika kukabiliana na masomo yao ya mbele kuona wanafanya vizuri hasa katika mitihani ya taifa.

Alifafanua kuwa tayari usaili kwa wanafunzi wa darasa la tatu umeanza na na utafungwa Februari 28 ili kuwa na takwimu sahihi za wanafunzi wote watakaofanya mitihani hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kitengo cha habari na uhusiano Baraza la Mitihani Zanzibar hivi karibuni inaeleza kuwa mitihani hiyo itafanyika mwezi wa Oktoba na Novemba mwaka huu.

Address

Maisara
Zanzibar

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Zanzibarleo Online posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Zanzibarleo Online:

Videos

Share