Zanzibarleo Online

Zanzibarleo Online Pata habari za uhakika na kuaminika kutoka Gazeti namba 1 visiwani Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.

WAANDISHI wa habari nchini, wametakiwa kuielimisha jamii juu ya ugonjwa wa homa ya nyani ‘Mpox’ hasa katika makundi yana...
21/08/2024

WAANDISHI wa habari nchini, wametakiwa kuielimisha jamii juu ya ugonjwa wa homa ya nyani ‘Mpox’ hasa katika makundi yanayoonekana kuwa hatarini zaidi kupata ugonjwa huo endapo utaingia nchini.

Akitoa elimu ya ya ugonjwa huo kwa waandishi hao katika Ofisi za Kitengo cha Elimu ya Afya Meya Zanzibar, Meneja wa kitengo hicho, Bakar Hamad Magarawa, aliwataka wandishi kuielezea jamii juu dalili za ugonjwa huo na njia za kujikinga nao.

Alisema ugonjwa huo unaosababishwa na kirusi cha ‘Monkeypox’ uligundulika kwa
mara ya kwanza mwaka 1958 nchini Denmark na kuenea katika nchi nyengine ikiwemo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kwa upande wa nchi za Afrika.

Magarawa alieleza kuwa maambukizi ya ugonjwa huo yalianza kutoka kwa mnyama kwenda kwa binaadamu katika nchi zilizo karibu na misitu ya Kitropiki na kwamba uzoefu unaonesha kuwa Zanzibar ni nchi yenye muingiliano wa wageni kutoka nchi tofauti hivyo inakuwa ni miongoni mwa nchi zilizo katika hatari ya kupata ugonjwa huo.

Aidha Magarawa alisema ugonjwa unapatikana kwa njia ya kujamiiana na mwenye maambukizi hasa mapenzi ya jinsia moja, kula au kugusa mizoga ya wanyama, kugusana na mtu mwenye dalili za ugonjwa huo kwa kusalimiana kwa kukumbatiana au kushikana mikono pamoja na kugusa maji maji ya mwili wa mtu mwenye maambukizi.

Alisema dalili za ugonjwa huo zinafanana na maradhi mengine, jambo ambalo ni gumu mtu kujitambua, hivyo aliishauri jamii kuwahi kituo cha afya mara tu anapopata homa, vidonda vya koo, maumivu ya kichwa, maumivu ya mgongo, misuli, uchovu wa mwili, kuvimba kwa mitoki na kuwashwa kwa muendelezo.

Aliongeza kuwa ugonjwa huo hauna matibabu maalum ila jamii inashauriwa kuwahi kituo cha afya kupata matibabu ya dalili za ugonjwa huo ambazo hujitokeza ndani ya wiki mbili baada ya kupata maambukizi.

Tarehe 21 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la  Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.sm...
21/08/2024

Tarehe 21 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la

Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.smsz.co.tz/ au tembelea wakala alie karibu nawe.

Benki ya NMB Tanzania  imejenga Skuli ya Maandalizi katika eneo la Tasani, Makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja.Skuli hiyo y...
20/08/2024

Benki ya NMB Tanzania imejenga Skuli ya Maandalizi katika eneo la Tasani, Makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja.

Skuli hiyo ya Maandalizi iliyopewa jina la Dkt. Samia Suluhu Hassan imefunguliwa rasimi na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan katika muendelezo wa shamrashamra za Tamasha la Kizimkazi.

Rais Samia amewataka walimu watakao kabidhiwa vituo k**a hivyo ni kutekeleza lengo la Serikali kuhakikisha watoto wanapata malezi bora na kupata elimu ya mapema pamoja na kuendelezwa mapema.

Ndege mpya aina ya Boeing B787-8 Dreamliner, ambayo ilishindwa kuondoka chini Marekani kutokana na changamoto za hali ya...
20/08/2024

Ndege mpya aina ya Boeing B787-8 Dreamliner, ambayo ilishindwa kuondoka chini Marekani kutokana na changamoto za hali ya hewa, itawasili leo, tarehe 20 Agosti 2024, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Zanzibar.

Ndege hiyo ya Shirika la ndege Tanzania (ATCL) itatua majira ya saa 10 jioni, ambapo Mgeni Rasmi atakayeipokea ndege hiyo ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe.
Dk. Hussein Ali Mwinyi.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inawakaribisha wananchi wote kushiriki katika sherehe za uzinduzi wa mapokezi ya ndege hiyo.

20/08/2024

Umeenda mnadani kununua samaki halafu umekutana na mzigo k**a huu 😁
Utasemaje neno lako la kwanza? Hebu tuambie kwenye comment

JUMLA ya wagonjwa 15,964 wamegundulikana kuwa na vimelea vya ugonjwa wa malaria katika kipindi cha kuanzia Junuari mosi ...
20/08/2024

JUMLA ya wagonjwa 15,964 wamegundulikana kuwa na vimelea vya ugonjwa wa malaria katika kipindi cha kuanzia Junuari mosi hadi Julai 15, mwaka huu.

Afisa Afya jamii, muhamasshaji programu ya kumaliza maleria zanzibar, Mwinyi Issa Khamis, alieleza hayo wakati akizungumza na mwandishi wa gazeti hili ofisini kwake Mwanakwerewe, wilaya ya Magharibi ‘B’ Unguja.

Alisema takwimu hizo ni za wagonjwa waliofika katika vituo vya afya na hospitali kwa ajili ya matibabu ambapo kati yao wagonjwa 776 wamepatikana Pemba na 15,188 Unguja.

Alifafanua kwa upande wa pemba wilaya ya Chake chake iliongoza kwa kuwa na jumla ya wagonjwa 242 ikifuatiwa na Micheweni iliyoripoti wagonjwa 208, Mkoani 96 na Wete 251 huku wilaya ya Mjini ikiongoza kwa Unguja baada ya kuripotiwa kuwa na wagonjwa 6,217.

Aidha Mwinyi alieleza kuwa wilaya ya Magharibi ‘B’ ilikuwa na wagonjwa 4,195, Mahgariub ‘A’ 1,961, wilaya ya Kati 930, wilaya ya Kaskazini ‘A’ 820, Kaskazini ‘B’ 609, na Kusini 456.

“Katika ripoti tulizokusanya wilaya inayoongoza kwa kuwa na wagonjwa waliogundulika kuwa na vimelea au kuugua ugonjwa wa malaria ni Wilaya ya Mjini ikiwa na wagonjwa 6217 ikifuatiwa na wagonjwa kidogo ni wilaya ya Mkoani ikiwa na wagonjwa 96”, alifafanua Mwinyi.

Hivyo aliwahimiza wananchi kuendelea kuchukua tahadhari kwani ugonjwa wa malaria bado upo Zanzibar ingawa umepungua kwa kiasi kikubwa ikilinganishwa na hapo aali.

Tarehe 20 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la  Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.sm...
20/08/2024

Tarehe 20 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la

Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.smsz.co.tz/ au tembelea wakala alie karibu nawe.

Ndege mpya ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) iliyotarajiwa kutua siku ya leo katika uzinduzi wake na kupokelewa na Rai...
19/08/2024

Ndege mpya ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) iliyotarajiwa kutua siku ya leo katika uzinduzi wake na kupokelewa na Rais wa na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi yashindwa kuwasili katika uwanja wa ndege wa Abeid Amani Karume, Zanzibar.

Sababu inayotajwa kutowasili kwa ndege hiyo k**a ilivyopangwa ni kutokana na changamoto za hali ya hewa.

Ratiba mpya ya kuwasili ndege hiyo itatolewa mapema hapo baadae.

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inaomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza.

19 - 25 August, 2024. Front and back pages of the   newspaper Read the newspaper online. Visit: https://epaper.smsz.co.t...
19/08/2024

19 - 25 August, 2024. Front and back pages of the newspaper

Read the newspaper online. Visit: https://epaper.smsz.co.tz/ or visit an agent near you.

Tarehe 19-25 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la Michezo la   Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: ht...
19/08/2024

Tarehe 19-25 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la Michezo la

Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.smsz.co.tz/ au tembelea wakala alie karibu nawe.

Tarehe 19 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la  Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.sm...
19/08/2024

Tarehe 19 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la

Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.smsz.co.tz/ au tembelea wakala alie karibu nawe.

Tarehe 18 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la  Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.sm...
18/08/2024

Tarehe 18 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la

Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.smsz.co.tz/ au tembelea wakala alie karibu nawe.

Tarehe 17 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la  Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.sm...
17/08/2024

Tarehe 17 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la

Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.smsz.co.tz/ au tembelea wakala alie karibu nawe.

Tarehe 16 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la  Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.sm...
16/08/2024

Tarehe 16 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la

Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.smsz.co.tz/ au tembelea wakala alie karibu nawe.

Tarehe 15 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la  Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.sm...
15/08/2024

Tarehe 15 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la

Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.smsz.co.tz/ au tembelea wakala alie karibu nawe.

NAHODHA wa Yanga Bakar Mwamnyeto amesema kila mchezaji ana kiu ya kupata mataji ndani ya kikosi chao msimu huu 2024/2025...
14/08/2024

NAHODHA wa Yanga Bakar Mwamnyeto amesema kila mchezaji ana kiu ya kupata mataji ndani ya kikosi chao msimu huu 2024/2025 jambo linalowafanya kupambana mwanzo mwisho.

Yanga tayari imenyakua Ngao ya jamii kutoka kwa watani zao Simba walioambulia nafasi ya tatu katika mchezo huo huku ya pili ikitwaliwa na Azam FC.

Akizungumza na Zanzibar Leo Mwamnyeto alisema wachezaji wote wanatambua majukumu yao na kujua umuhimu wa kuwepo kikosini , hivyo watahakikisha wanapambana kupata matokeo ili waweze kutimiza lengo.

"Msimu unakwenda kuanza lakini kikubwa tunamshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa hatua hii ya awali kuanza kupata taji la kwanza katika timu nne shiriki sisi tumelichukua ni jambo la kumshukuru sana Mungu,"alisema Mwamnyeto.

Aidha Mwamnyeto alisisitiza kuwa hata wachezaji wapya walioingia kikosini wana uwezo mkubwa na ndio maana uongozi ukawasajili.

Alisema wanatambua wingi wa mashindano mbalimbali mbele yao kuanzia ligi kuu, FA pamoja na ligi ya mabingwa.

Aliwashukuru mashabiki wa Yanga kwa namna ya kipekee wanavyojitolea kuiunga mkono timu yao, jambo ambalo ni deni kubwa kwa wachezaji kuhakikisha wanawapa burudani zaidi.

"Mashabiki kwetu ndio kila kitu tunatambua mchango wao na tunajua wanahitaji nini ni jukumu letu kuhakikisha tunawapa furaha,"alisema.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema serikali inatarajia kujenga viwanja...
14/08/2024

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema serikali inatarajia kujenga viwanja vipya 16 katika wilaya zote za Unguja na Pemba.

Hayo aliyasema juzi katika maadhimisho ya siku ya vijana kimataifa hafla iliyofanyika ukumbi wa Goldeni Tulip uwanja wa Ndege mjini Unguja.

Alisema mbali na hayo serikali imeimarisha miundombinu ya michezo kwa kufanya ukarabati mkubwa wa uwanja wa Amaan na Gombani.

Alisema miongoni mwa viwanja vinavyotarajiwa kujengwa ni pamoja na kiwanja cha Maisara Mjini Unguja, kwa lengo la kukuza vipaji na kuimarisha ustawi mzuri wa vijana.

Aidha alifahamisha kuwa kwa kushirikiana na shirika la Ujerumani serikali itajenga viwanja vitano vipya vya michezo na kuvifanyia ukarabati viwanja vitatu.

Alisema hatua hiyo itasaidia kukuza michezo kwa vijana na kuinua vipaji ambavyo vitapelekea kupata ajira ndani na nje ya nchi.

Hivyo aliwanasihi vijana kuvitumia viwanja hivyo sambamba na kuvitunza ili vitumike na vizazi vijavyo.

MENEJA wa Inter Miami, Gerardo Martino, amesema, nahodha, Lionel Messi bado hajapona jeraha la kifundo cha mguu alilolip...
14/08/2024

MENEJA wa Inter Miami, Gerardo Martino, amesema, nahodha, Lionel Messi bado hajapona jeraha la kifundo cha mguu alilolipata alipokuwa akiichezea Argentina katika fainali ya Copa America mwezi uliopita.

Martino alikiri kuwa bado hajui ni lini Messi atarejea katika utimamu kamili, lakini, alisema, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 37 alikuwa akipona kwa njia ya kuridhisha.

"Bado hatujui ni lini ataweza kuwa na [timu ya kwanza] kundini. Kwa wakati huu, anaendelea kufanya mazoezi tofauti."

Messi hajacheza tangu apate maumivu kwenye kifundo cha mguu wake wa kulia wakati Argentina iliposhinda 1-0 dhidi ya Colombia kwenye fainali ya Copa America Julai 14.

Mechi yake ya hivi majuzi zaidi akiwa na Inter Miami ilikuwa sare ya 3-3 nyumbani na St. Louis katika MLS.

Messi amefunga mabao 14 na kutoa asisti 11 katika mechi 15 alizocheza kwenye mashindano yote akiwa na Inter Miami mwaka huu.

Miamba hiyo ya Florida inaongoza msimamo wa MLS Eastern Conference wakiwa na pointi 53 kutokana na michezo 25, pointi tano mbele ya Cincinnati inayoshika nafasi ya pili.(AP).

WAZIRI wa Elimu na Mafunzo ya Amali  , Lela Muhamed M***a, amesema serikali imeifanya elimu ya mafunzo ya amali kuwa mio...
14/08/2024

WAZIRI wa Elimu na Mafunzo ya Amali , Lela Muhamed M***a, amesema serikali imeifanya elimu ya mafunzo ya amali kuwa miongoni mwa elimu ya lazima ili kuendeleza ujuzi wa wanafunzi na kuzalisha ajira.

Lela alyaisema hayo katika mahafali ya 11 ya Chuo cha Mafunzo ya Amali Mkokotoni, wilaya ya Kaskazi 'A' Unguja na kueleza kwamba hatua hiyo itawasaidia wanafunzi wengi kuona umuhimu na kusoma fani hizo na kupata ujuzi utakaowasaidia kujiajiri au kuajiriiwa kwa urahisi katika taasisi za serikali na binafsi.

Waziri Lela alifahamisha kuwa serikali ya Mapinduzi Zanzibar na ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zinaendelea na mpango wa kuratibu suala hilo na endapo likikamilika basi fani hizo zitasomwa zaidi na vija wengi ili ziweze kuwasaidia wao na taifa kwa ujumla.

Alisema hatua hiyo itasaidia wahitimu wote wanaomaliza elimu ya sekondari wanakuwa na aina ya ujuzi utakaowawezesha kujiajiri na kuacha kukaa mitaani kukosa la kufanya na kujiingiza katika makundi yasiostahiki.

Alisema tafiti zinaonesha kuwa taifa lolote likihitaji maendeleo lazima kuwe na misingi na miundombinu imara ya kuwawezesha vijana kupata mbinu na ujuzi utakaowasaidia kujiajiri na kujikwamua kiuchumi hatua ambayo itatoa mchango mkubwa katika kuchangia ukuwaji wa uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

Tarehe 14 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la  Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.sm...
14/08/2024

Tarehe 14 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la

Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.smsz.co.tz/ au tembelea wakala alie karibu nawe.

Tarehe 12 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la   LeoSoma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epape...
13/08/2024

Tarehe 12 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la Leo

Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.smsz.co.tz/ au tembelea wakala alie karibu nawe.

Tarehe 12 Agosti, 2024. Kurasa za mbele na nyuma za magazeti yetu.Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper....
12/08/2024

Tarehe 12 Agosti, 2024. Kurasa za mbele na nyuma za magazeti yetu.

Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.smsz.co.tz/ au tembelea wakala alie karibu nawe.

Tarehe 11 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la  Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.sm...
11/08/2024

Tarehe 11 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la

Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.smsz.co.tz/ au tembelea wakala alie karibu nawe.

Tarehe 10 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la  Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.sm...
10/08/2024

Tarehe 10 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la

Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.smsz.co.tz/ au tembelea wakala alie karibu nawe.

Tarehe 9 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la  Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.sms...
09/08/2024

Tarehe 9 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la

Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.smsz.co.tz/ au tembelea wakala alie karibu nawe.

Tunakutakia Kheri Sikukuu ya Wakulima Duniani (Nane Nane).
08/08/2024

Tunakutakia Kheri Sikukuu ya Wakulima Duniani (Nane Nane).

Tarehe 8 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la  Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.sms...
08/08/2024

Tarehe 8 Agosti, 2024. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la

Soma gazeti kupitia mtandao. Tembelea: https://epaper.smsz.co.tz/ au tembelea wakala alie karibu nawe.

SHIRIKA la Mawasiliano   (TTCL) kupitia kampuni Tanzu T-PESA imekuja na huduma ya MALIPO KWA MKUPUA inayowezesha Shirika...
07/08/2024

SHIRIKA la Mawasiliano (TTCL) kupitia kampuni Tanzu T-PESA imekuja na huduma ya MALIPO KWA MKUPUA inayowezesha Shirika, Taasisi au Kampuni kuwalipa wanufaika wake kwa haraka.

Hayo yameelezwa na meneja Biashara Dodoma, Leyla Pongwe ambapo alisema kuwa huduma hiyo inawasaidia wakulima kupitia vyama vyao vya ushirika ambapo chama kinaweza kuwalipa wakulima na wakapokea fedha kupitia simu zao za Mkononi kwa wakati mmoja.

Aidha alisema kupitia maonesho ya kimataifa ya Nanenane TTCL inajivunia kufikisha huduma ya Mawasilino juu ya kilele cha Mlima Kilimanjaro ambapo sasa watalii hawana tena Shida ya internet wanapotembelea mlima huo.

MKURUGENZI wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko kutoka Chuo kikuu cha   (UDOM), Rose Joseph amesema, chuo hicho kimebuni...
07/08/2024

MKURUGENZI wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko kutoka Chuo kikuu cha (UDOM), Rose Joseph amesema, chuo hicho kimebuni teknolojia ya ufugaji samaki ambayo wananchi wanaweza kuitumia kujiongezea kipato na kujikwamua kiuchumi.

Ameyasema hayo jijini Dodoma, wakati akizungumza na waandishi wa habari katika maonesho ya nanenane kitaifa yanayoendelea katika viwanja vya Nzunguni jijini Dodoma.

Alisema ubunifu mwingine ni tekonoloji ya kubaini magonjwa ya mifugo ambayo yamekuwa yakiwakabili wafugaji na kupunguza tija ya mifugo nchini.

“Ubunifu mwingine ni ufugaji wa sunglasses kisasa ambapo mkojo wake unatumika k**a viwatilifu kwenye mimea ya bustani lakini kinyesi chao kinatumika k**a mbolea hivyo kuondoa matumizi ya kemikali”, alisema.

Sambamba na hayo amezungumzia kuhusu kuongeza thamani zao la asali nchini ambao Chuo hicho cha (UDOM) kimekuja na ubunifu wa kuzalisha mvinyo utokanao na asali.

Rose alisema kuwa pamoja na mambo mengine chuo hicho kimekuwa kikijihisisha na ufugaji nyuki na kuzalisha zao la asali.

MAMLAKA ya Ugiriki imek**ata kokeini yenye thamani ya zaidi ya euro milioni 1 (dola milioni 1.10) ambayo ilikuwa imefich...
07/08/2024

MAMLAKA ya Ugiriki imek**ata kokeini yenye thamani ya zaidi ya euro milioni 1 (dola milioni 1.10) ambayo ilikuwa imefichwa kwenye kontena la ndizi lililokuwa kwenye bahari, mlinzi wa pwani alisema.

Kwa mujibu wa walinzi wa pwani walisema dawa hizo, zilizonaswa kwenye meli katika bandari ya Piraeus hapo jana ni juhudi ya usaidizi wa kitengo cha Uchunguzi wa Usalama wa Ndani cha ubalozi wa Marekani mjini Athens.

Mamlaka iligundua takriban kilo 35 (77 lb) za kokeini kwenye vifurushi 30 vilivyofichwa kwenye kontena hilo lililojazwa shehena ya ndizi kutoka Ecuador.

Uzalishaji wa kokaini nchini Amerika ya Kusini umeongezeka katika muongo mmoja uliopita, huku wafanyabiashara wa Balkan wakisaidia kugeuza Ulaya kuwa soko kubwa zaidi la dawa hizo duniani.

Mwezi Mei, mamlaka ya Ugiriki ilisema walikuwa wamesambaratisha kundi la wahalifu la kimataifa linalosafirisha kokeini katika makontena ya kusafirisha bidhaa mbalimbali kutoka Amerika Kusini hadi Ulaya.

Siku chache zilizopita, zilipatikana zaidi ya kilo 109 (pauni 240) za kokeini zilizofichwa kwenye kontena lililokuwa na ngisi kwenye meli nyingine iliyokaguliwa katika bandari ya Piraeus.

Address

Maisara
Zanzibar

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Zanzibarleo Online posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Zanzibarleo Online:

Videos

Share

Nearby media companies