BWorld Tv

BWorld Tv Ukurasa huu ni kwa ajili ya kupashana habari zote za ulimwengu, kubadilishana fikra na majadiliano kw

15/04/2024

Kwenye mashambulizi ambayo waliyafanya Iran kwenda nchini Israeli, takribani makombora 9 ya balistiki yalifanikiwa kuzifumua kambi kadhaa za kijeshi zilizopo nchini Israeli.
Shambulio moja lilitua kwenye kituo cha anga cha Nevatim kilichopo kwenye Mji wa Negev ambacho kilipigwa makombora 5 ya balestiki.
Makombora hayo yalifanikiwa kuharibu njia kuu ya ndege,
ndege ya usafirishaji ya C-130, na vifaa kadhaa vya kuhifadhi silaha.
Shambulio lingine lilifanyika kwenye kituo cha anga cha Ramon, ambacho pia kipo kwenye Mji wa Negev.
Kituo hiki Kilipigwa na angalau makombora 4 ya balestiki na
Kusababisha uharibifu ambao haujajulikana mpaka sasa.
Taarifa hizi zimetolewa na wachambuzi wa masuala ya kivita
wa Marekani kwa kupitia kituo cha habari cha ABC News.
Kwa upande wa Israeli,
Wizara ya Ulinzi imetoa picha na video za ukarabati wa sehemu iliyoharibika kwenye njia ya ndege iliyopo kwenye
kambi ya Nevatim ambayo ilipiga na makombora ya Iran.
Kwa lugha rahisi ni kwamba, ndege zisizo na rubani ambazo zilitumwa na Iran ndizo ambazo zilidunguliwa na Israeli,
Kwa upande wa Makombora machache ya Balestiki na Hypersonic ambayo waliyatuma, yalifanikiwa kugonga kwenye maeneo husika.
Huku Taifa la Israel wakiendelea kuficha uharibu zaidi ulio tokea lakini taarifa zimeanza kuvujishwa ndani ya maeneo husika.
Credit to siasa makini

Katika kuendeleza vita vya mahasimu wa Kirusi na Marekani mapema Wadukuzi wa Kirusi (KILLNET HACKERS) Wamedukua tovuti y...
18/11/2022

Katika kuendeleza vita vya mahasimu wa Kirusi na Marekani mapema Wadukuzi wa Kirusi (KILLNET HACKERS) Wamedukua tovuti ya Ikulu ya Marekani (WhiteHouse). Wadukuzi hao walifanikiwa kuchunguza baadhi ya nyaraka za SIRI za Ofisi Ya Rais wa Marekani (Tovuti hiyo ilipotea kwa muda wa dakika kadhaa).

Waandamanaji wamesema wataendelea kubaki katika Makazi ya Rais na Waziri Mkuu hadi Viongozi hao watakapojiuzulu rasmi. K...
11/07/2022

Waandamanaji wamesema wataendelea kubaki katika Makazi ya Rais na Waziri Mkuu hadi Viongozi hao watakapojiuzulu rasmi. Kwa mujibu wa Spika wa Bunge la Nchi hiyo, Rais Gotabaya Rajapaksa atajiuzulu Julai 13, 2022

Rais Rajapaksa hajaonekana na hakutoa kauli ya kujiuzulu mwenyewe moja kwa moja. Baadhi ya Ripoti zinadai yupo katika Meli ya Kijeshi

Utulivu umeonekana kurejea katika Mji Mkuu wa Colombo. Baadhi ya Maafisa wa Vyombo vya Usalama wenye silaha wameonekana nje ya Makazi ya Rais, lakini hawajazuia Wananchi kuingia

Vyanzo vya kijeshi vinasema kwamna Rais kwa sasa yuko kwenye meli ya Wanamaji katika maji ya Sri Lanka.
Kaka yake, Waziri Mkuu wa zamani Mahinda Rajapaksa, yuko kwenye kambi ya wanamaji nchini humo, duru zinasema.
Maelfu walifika Colombo Jumamosi wakimtaka ajiuzulu baada ya miezi kadhaa ya maandamano.

Rais amelaumiwa kwa usimamizi mbaya wa uchumi wa nchi, ambao umesababisha uhaba wa chakula, mafuta na dawa kwa miezi kadhaa.
Waziri Mkuu wa sasa Ranil Wickremesinghe pia alisema atajiuzulu kufuatia maandamano ya Jumamosi, ambapo makazi yake ya binafsi yalichomwa moto.

Nondo za Wazee wetu.
11/05/2022

Nondo za Wazee wetu.

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeviagiza vyombo vyote vya utangazaji na mitandao ya kijamii nchini kutorusha vi...
06/05/2022

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeviagiza vyombo vyote vya utangazaji na mitandao ya kijamii nchini kutorusha video ya wimbo uitwao 'Mtasubiri Sana' ulioimbwa na msanii Nasib Abdul maarufu Diamond Platnumz kwa kushirikiana na Zuhura Othuman Soud maarufu Zuchu, hadi hapo wasanii hao watakaporekebisha sehemu ya video ya wimbo huo ambayo imeleta ukakasi.

Kwa mujibu wa TCRA, katika video ya wimbo huo kuna kipande kimeonesha wahusika wapo kanisani wanaimba kwaya lakini baadae wakaacha na kuelekea kwingine, kitendo kilicholeta ukakasi miongoni mwa waumini wa madhehebu ya dini na kuleta hisia kuwa ni dharau juu ya dini/madhehemu fulani.

Taarifa ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Dkt. Jabiri Bakari imeeleza kuwa uamuzi huo umefikiwa baada ya TCRA kupokea taarifa kutoka Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) ya kuzuia usambazaji wa video ya wimbo huo unaopigwa katika mitandao ya kijamii na vyombo vya utangazaji.

Mahak**a Kuu imemuachia huru aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, Lengai Ole Sabaya na wenzake wawili baa...
06/05/2022

Mahak**a Kuu imemuachia huru aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, Lengai Ole Sabaya na wenzake wawili baada ya kubaini kulikuwa na mapungufu katika mwenendo mzima wa kesi, pamoja na kutofautiana kwa mashahidi.

Sabaya na wenzake walikata rufaa kupinga hukumu ya kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha iliyotolewa na Mahak**a ya Hakimu Mkazi Arusha.

Mbali na Sabaya, wengine ni Sylvester Nyegu na Daniel Mbura.

Hata hivyo, Sabaya ataendelea kukaa mahabusu kutokana na kukabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi.

Rais wa Urusi Vladimir Putin ameonya kuwa nchi zozote zinazoingilia Ukraine zitakabiliwa na jibu la haraka."Ikiwa mtu ku...
27/04/2022

Rais wa Urusi Vladimir Putin ameonya kuwa nchi zozote zinazoingilia Ukraine zitakabiliwa na jibu la haraka.

"Ikiwa mtu kutoka nje atajaribu kuingilia kati Ukraine," alisema akizungumza hivi sasa na wabunge wa Urusi, "jibu letu litakuwa haraka sana."

"Tuna zana zote [za kujibu] ambazo hakuna mtu anayeweza kujivunia. Na hatutakuwa na majisifu juu yao, tutatumia ikiwa ni lazima," alisema.

Kiongozi huyo wa Urusi aliongeza kwamba aina ya maamuzi juu ya majibu ambayo yatatolewa tayari yamefanywa, lakini hakutoa maelezo zaidi.

Marekani Jumanne imesema itatoa kiasi cha hadi dola milioni 10 kwa atakaetoa habari kuhusu watu 6 wanaotambulishwa k**a ...
27/04/2022

Marekani Jumanne imesema itatoa kiasi cha hadi dola milioni 10 kwa atakaetoa habari kuhusu watu 6 wanaotambulishwa k**a maafisa wa ujasusi wa jeshi la Russia, ambao waliendesha mashambulizi ya mtandaoni yaliyoathiri miundombinu muhimu ya Marekani.
Maafisa hao wanafanya kazi katika kitengo cha idara kuu ya ujasusi ya Russia kinachohusika na masuala ya mtandaoni ( GRU) ambao walihusika katika shambulio la mwaka wa 2017 kwenye ngazi ya kimataifa la kusambaza kirusi kilichoharibu kompyuta za makampuni kadhaa ya kibinafsi ya Marekani, ikiwemo mfumo wa hospitali, wizara ya mambo ya nje ya Marekani imesema.

Shambulio hilo la mtandaoni maarufu “NotPetya” la 2017 lilidumaza sehemu ya miundombinu ya Ukraine na kuharibu kompyuta katika nchi kote ulimwenguni, ikiwemo Ufaransa, Ujerumani, Italy na Marekani, na kusababisha hasara inayokadiriwa kuwa ya mabilioni ya dola.

Russia ilikanusha kuhusika katika shambulio hilo.

26/04/2022

Tizama video ya ajali ya njombe iliyouwa watu tisa hapo hapo.

Rais wa Nigeria amesema nchi hiyo iko katika "mshtuko na kiwewe" kufuatia vifo vya takriban watu 100 kutokana na mlipuko...
24/04/2022

Rais wa Nigeria amesema nchi hiyo iko katika "mshtuko na kiwewe" kufuatia vifo vya takriban watu 100 kutokana na mlipuko katika kiwanda haramu cha kusafisha mafuta kinyume cha sheria.

Rais Muhammadu Buhari alielezea tukio hilo katika jimbo la Imo, kusini mwa Nigeria k**a " janga la kitaifa".

Wahasiriwa wengi waliteketea kiasi chakutoweza kutambulika.

Polisi sasa wanamsaka mmiliki wa kiwanda hicho kisicho halali cha kusafisha mafuta.

Uharibifu unaokumba uvuvi na kilimo unaosababishwa na sekta ya mafuta kwa miongo kadhaa iliyopita na umetokana na nchi hiyo kushindwa kugawana mali yake. Hali ambayo kumesababisha baadhi ya watu kutafuta njia nyingine za kupata pesa.

Usafishaji haramu wa mafuta unavutia sana katika sehemu za Delta yenye mafuta mengi ya Niger kwasababu inaoonekana kuwa rahisi kuepuka mkono washeria, licha ya juhudi za kukomesha mwenendo huo.

Makumi ya watu wanadhaniwa walikuwa wakifanya kazi katika kiwanda hicho wakati kilipokumbwa na moto

Idadi ya vifo imeongezeka kulingana na wafanyakazi wa kutoa huduma za dharura. Ifeanyi Nnaji wa Shirika la Kitaifa la Usimamizi wa Dharura aliambia BBC Igbo kwamba idadi ya waliouawa sasa imefikia 109.

Posted  •  MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Rukwa Irene Alex Ndyamk**a amefariki dunia leo Aprili 24 katika Hospitali ya Tu...
24/04/2022

Posted • MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Rukwa Irene Alex Ndyamk**a amefariki dunia leo Aprili 24 katika Hospitali ya Tumbi alikokuwa akipatiwa matibabu, Spika wa Bunge amesema katika taarifa iliyotolewa na Idara ya Habari ya Bunge.

Dk. Tulia Ackson amesema: “Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Mhe. Irene Alex Ndyamk**a. Natoa pole kwa familia ya Marehemu, ndugu, jamaa, waheshimiwa wabunge na wananchi wa mkoa wa Rukwa. Mwenyezi Mungu awape moyo wa uvumilivu na subira katika kipindi hiki kigumu.”

Mtoto Salah Jackson (5) mwenye ulemavu wa viungo, mkazi wa kijiji cha Makiwaru, mkoani Kilimanjaro amefariki dunia kutok...
24/04/2022

Mtoto Salah Jackson (5) mwenye ulemavu wa viungo, mkazi wa kijiji cha Makiwaru, mkoani Kilimanjaro amefariki dunia kutokana na njaa na kisha mama yake mzazi kumzika kimya kimya usiku wa manane.

Mtoto huyo anadaiwa kuzikwa na mama yake mzazi aitwaye Rebecca Siowi (30) usiku wa kuamkia Aprili 22, 2022 nyumbani kwa bibi yake walikokuwa wakiishi yeye pamoja na mama yake baada ya mume kumtelekeza na watoto watano.

Tukio hilo liligundulika baada ya mtoto huyo kutoonekana jioni ya Aprili 21 nyumbani alikokuwa akiishi kwa bibi yake, ambapo bibi yake huyo alifanya jitihada za kumtafuta mjukuu wake huyo bila mafanikio ndipo Aprili 22 alipobainika kuwa amezikwa.

Akizungumzia tukio hilo leo Aprili 23, 2022 Kamanda wa polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa amekiri kuwepo kwa tukio hilo, akisema baada ya kupata taarifa ya tukio hilo kutoka kwa wananchi walifika eneo la tukio kuona sehemu alipozikwa mtoto huyo.

Kamanda Maigwa amesema walipofika eneo la tukio walilazimika kuomba kibali cha kuufukua mwili wa mtoto huyo ili kujua sasababu hasa za kifo cha mtoto huyo kutokana na maneno ambayo yalikuwa yakisemwa mtaani.

"Tulifukua mwili jana na kuupeleka hospitali kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi na majibu ya daktari yalipotoka yalionyesha kwamba huyu mtoto alikufa kutokana na njaa,” amesema Kamanda Maigwa

Akizungumzia tukio hilo, jirani wa familia hiyo, Maria Nko amesema hata k**a mtoto huyo alikufa kwa njaa mama yake huyo hakupaswa kumzika mwanaye k**a mbwa tena usiku wa manane.

Tafsiri ya Demokrasia katika uwanda mpana wa vichwa vya wafuasi wa Marekani ni kufuata yale ambayo wao wanayataka. Ni k*...
24/04/2022

Tafsiri ya Demokrasia katika uwanda mpana wa vichwa vya wafuasi wa Marekani ni kufuata yale ambayo wao wanayataka. Ni k**a vile wao ndo wanafanya maamuzi na kuandaa agenda mbalimbali za kutaka dunia iende kwa spidi gani.

Waziri wa Mambo ya Nje Kutoka Russia, SERGEY LAVROV amefafanua kwa ukubwa wake siku ya jana kwa kujaribu kukumbusha mambo mbalimbali ambayo yamefanywa na Marekani bila kufuata Demokrasia na sheria za haki za binadamu.

Migogoro ya kisiasa ambayo ilisababisha vita katika Mataifa ya Iraq, Syria, Libya, Yemen, Afghanistan na sehemu zingine ni moja ya mifano ambayo Waziri huyu aliizungumzia kuhusu namna Marekani wanatengeneza matatizo katika dunia hii kwa kutumia mhimili wa Demokrasia.

Mataifa dhaifu yanafuata maelekezo ya Marekani na kupangiwa nini cha kufanya katika masuala mbalimbali ya kimaendeleo, uchumi na siasa lakini Russia wametengeneza mifumo yao ya kujitegemea tangu miaka ya nyuma jambo ambalo linaleta chuki na uhasama mkubwa dhidi ya Marekani.

MWISHO: Waziri Sergey Lavrov alisisitiza kwa kutoa msimamo wa Russia kwa dunia katika mambo matatu:

1. Hawatakuja kufanya jambo lolote kwa ushawishi wa Marekani isipokuwa kwa maridhiano ya pande zote.

2. Mataifa yenye kuhitaji Ushirikiano na Russia yapo huru kuja kufanya biashara kwa bei nafuu katika kipindi hiki cha Vita.

3. Wanatambua Ushawishi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa, wamejipanga kukabiliana na kila fitna ambayo itawakabili.

Kisa kipya cha ugonjwa wa Ebola kimethibitishwa kaskazini magharibi mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Taasisi ...
24/04/2022

Kisa kipya cha ugonjwa wa Ebola kimethibitishwa kaskazini magharibi mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Taasisi ya Kitaifa ya Utafiti wa Tiba ya Kijamii ilisema katika taarifa yake Jumamosi jioni.

Mwanaume mwenye umri wa miaka 31 alifariki kutokana na ugonjwa huo katika mji wa Mbandaka, mji mkuu wa jimbo la Equateur nchini DRC, taasisi hiyo ilisema.

Mgonjwa alianza kuonyesha dalili mnamo Aprili 5, lakini hakutafuta matibabu kwa zaidi ya wiki moja. Alilazwa katika kituo cha matibabu ya Ebola Aprili 21 na alifariki baadaye siku hiyo, Shirika la Afya Duniani (WHO) lilisema katika taarifa yake.

Mlipuko wa awali wa Ebola nchini ulitangazwa zaidi ya miezi minne iliyopita, mnamo Desemba 2021.

24/04/2022

VIDEO: Mwijaku na Baba Levu wachuana,asema anashika viuno vya wanawake mwezi mtukufu.

Rais wa awamu ya tatu wa Kenya, Mwai Kibaki amefariki  dunia akiwa na umri wa miaka 90.Kibaki alikuwa  Rais wa Kenya kwa...
22/04/2022

Rais wa awamu ya tatu wa Kenya, Mwai Kibaki amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 90.

Kibaki alikuwa Rais wa Kenya kwa muda wa miaka kumi kuanzia mwezi Desemba mwaka 2002 hadi mwezi Aprili mwaka 2013.

Kabla ya kuwa Rais wa Kenya alikuwa Makamu wa Rais wa Taifa hilo kwa muda wa miaka kumi kuanzia mwaka 1978 hadi mwaka 1988 wakati huo Rais akiwa Hayati Daniel Arap Moi.

Ali'zaliwa Novemba 15 mwaka 1931 katika eneo la Gaituyaini nchini Kenya.

Rais Uhuru Kenyatta. wa Kenya amelihutubia Taifa kufuatia msiba huo na kusema kuwa wamepoteza mtu muhimu.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Ronald Fenty ambaye ni Baba...
22/04/2022

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Ronald Fenty ambaye ni Baba wa Msanii Maarufu Robyn Rihanna Fenty alipofika katika Ukumbi wa Paramount Pictures kwa ajili ya kuangalia Filamu ya Tanzania Royal Tour, leo Aprili 22, 2022.

Filamu hiyo inafanyiwa uzinduzi Los Angeles, Marekani ikiwa ni mara ya pili kufanyiwa kuzinduliwa Nchini humo baada ya awali kuzinduliwa Aprili 28, 2022 Jijini New York

Uzinduzi huo umefanyika usiku wa Aprili 21 kwa Marekani lakini kwa Tanzania tayari ni tarehe 22 Aprili 2022.

Address

Zanzibar

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when BWorld Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Videos

Share

Category


Other TV Channels in Zanzibar

Show All

You may also like