08/03/2023
MFAHAM MWANAMKE NI NANI
MWANAMKE AMEBEBA UHAI
Amebeba uhai wa kila mwanadamu kila mwanadamu unae mwona duniani uhai wake umebebwa na mwanamke💪
Mwanamke ni ukamirifu na msaidizi wa Mwanaume 📕MWANZO 2: 18💥
Mwanamke aliumbwa ktk ukamirifu ili kuziba sehem ya upungufu wa mwanaume.
Kupitia mwanamke watu wote walio kwenye hii dunia walizaliwa 📕MWANZO 3: 20💥 Mwanamke ni mlango wa wanadamu wote duniani, Mungu alimwamini mwanamke tumbo lake liwe sehem ya uumbaji wa watu wote.
Mwanamke ni mlinzi wa mwanamue 📕YEREMIA 31: 22💥 Hivyo ukisoma hapo utagundua mwanamke ananguvu na maarifa mengi ya ulinzi kuliko mwanaume ndiyo maana Mungu amemwamini kumlinda mwanaume, mwanamke anaetambua nafasi yake anaweza kumlinda mumewe na watoto wake.
Mwanamke ndiyo kituchema namba moja duniani kuliko chochote 📕MITHALI 18: 22💥
Ukisoma hapo utagundua mwanamke ana uwezo wa kumfungulia mwanaume kibali cha kukubalika na Mungu 🤔
Mwanamke maombi yake yanasikilizwa na Mungu upesi kuliko kawaida 📕YEREMIA 9: 17💥 ISAYA 58: 12💥
Mwanamke akisimama kwenye nafasi yake anaweza kuokoa ndoa yake watoto wake na jamii nzima ikawa salama.
Kupitia tumbo la mwanamke mmoja MARIAM kumzaa Yesu ulimwengu ulipata wokovu 📕MATHAYO 1: 23💥
Mwanamke ndiyo mwenyewe kujenga nyumba yani ndiyo mwenye ndoa ili nyumba au ndoa isimame inategemea jinsi mwanamke anavyo jitambua kwenye hilo eneo la ndoa au mahusiano 📕MITHALI 14: 1💥 Mungu anamtambua mwanamke k**a ndiyemhusika zaidi wa ndoa 📕MWANZO 2: 24💥 mwanamke akisimama kwenye nafasi yake ndoa haiwezi kuvunjika pia akiamua kuivunja ni mala moja.
Wanawake wengi wamepoteza nafasi zao kwa kudanganywa na elimu za dunia zinazowafundisha kuwa k**a wanaume, na kupoteza thamani yao kubwa ya kuwa mwanamke.
Ndiyo maana ndoa nyingi zinavunjika na watoto wa mitaani kuongezeka,
Mwanamke ndiyo mwenyewe nafasi kubwa ya kuombea ndoa mume na watoto📕YEREMIA 31 : 15💥 akisima kwa maombi na sadaka anamlinda mumewe na watoto wake mpaka wajukuu zake,
Mabinti wengi leo hii wanakosa kuolewa siyo kuwa hakuna wanaume, bali hawajatambua nafasi zao katika ulimwengu wa roho.
Na shetani kwa kuwa anatambua nafasi ya mwanamke ndiyo maana anampiga vita katika maeneo mbali mbali hasa ya ndoa na mahusiano,
Unaweza kuhisi wanaume hakuna ndiyo maana Mabinti hawaolewi, lakini ukweli nikuwa wanaume wengi na vijana wengi wametekwa na shetani kwenye madawa ya kulevya na maeneo mengine yasiyofaa mpaka wamepoteza jukum lao la kuwa baba na waume za watu,
Anapo potea mwanaume mmoja amesababisha binti mmoja kukosa mume, hivo ni wajibu wa Mabinti kusimama kwenye nafasi zao kwa kuomba ili wanaume zao waokolewe kutoka kwenye vifungo vya kuto kuoa na kuwa baba wa familia ili dada zetu waolewe.🤝
Mwanamke ana tumia akili zaidi kuliko mwanaume simanishi wanaume hawana akili ndiyo maana Mungu alisema ishi na mwanamke kwa akili 📕1PETRO 3: 7💥 Ukisoma hapo utagundua wanawake wamepewa akili zaidi kuliko nguvu za mwilini, 📕MWANZO 27: 11 - 17💥 ukisoma hapo utagundua mwanamke anatumia akili kuliko nguvu,
Mwanamke ndiyo heshima ya dunia akipoteza madili inchi inakuwa imepoteza thamani yake mwanamke akiamua kuolewa anaweza kuolewa mda wowote anaotaka ukiona hajaolewa ujue hajatambua nguvu yake na nafasi yake, au kuna sehem amefungwa na shetani ili asijue thamani yake.
Mwanamke yeyote unaehisi umepoteza nafasi yako ndiyo maana ndoa ina sumbua ndiyo maana mahusiano yanakusumbua ndiyo maana huolewi njoo niombe na wewe Mungu akurejeshee thamani yako usimame kwenye nafasi yake kwa jina la Yesu 🙏
Maombezi Whatsapp 0716822126
✍️by Mtumishi Fahim Whatsapp 0716822126
MUNGU AWABARIKI WANAWAKE WOTE AMEEN🙏