Casa

Casa MEDIA

  Waandamanaji kadhaa wameuawa kwa risasi nchini Kenya baada ya kuwazidi nguvu askari na kuingia bungeni.Aidha imeelezwa...
25/06/2024

Waandamanaji kadhaa wameuawa kwa risasi nchini Kenya baada ya kuwazidi nguvu askari na kuingia bungeni.

Aidha imeelezwa baadhi ya waandamanaji hao waliopenya bungeni wameanza kula chakula cha wabunge kisha waendelee kuandamana.


  Klabu ya Simba SC, imetangaza kuachana rasmi na aliyekuwa beki kisiki wa klabu hiyo Henock Inonga Baka.Umeipokeaje "Th...
24/06/2024

Klabu ya Simba SC, imetangaza kuachana rasmi na aliyekuwa beki kisiki wa klabu hiyo Henock Inonga Baka.

Umeipokeaje "Thank You" ya Inonga🤷 kwa Furaha😃 au kwa masikitiko na majonzi makubwa🥹?

  Wajumbe wa Sekretarieti ya K**ati Maalum ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar wamepitisha pendekezo la kuishauri K**a...
23/06/2024

Wajumbe wa Sekretarieti ya K**ati Maalum ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar wamepitisha pendekezo la kuishauri K**ati Maalumu kuridhia kuongeza muda wa Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi kuongoza nchi katika muhula wake wa kwanza kwa kipindi cha miaka saba badala ya mitano.

Hayo yamesemwa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dk Mohamed Said Dimwa wakati akifunga mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana (UVCCM) Wilaya Dimami kichama Zanzibar uliofanyika Ofisi za Wilaya hiyo Kiembesamaki.

Dkt. Dimwa amesema uamuzi wa kumuongezea muda wa kuongoza Dkt. Mwinyi unatokana na kuridhishwa na kasi yake ya kiutendaji katika kutekeleza Ilani ya CCM ya mwaka 2020-2025 kwa zaidi ya asilimia 100 ndani ya kipindi miaka mitatu na miezi kadhaa tangu aingie madarakani.

Katika maelezo yake, Dkt. Dimwa amesema CCM Zanzibar imeona Serikali kuingia katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ni hasara na matumizi mabaya ya fedha za walipa kodi kwa kuwa ni wananchi wanahitaji maendeleo endelevu, hivyo Rais Mwinyi anafaa kuongezewa muda ili Zanzibar iwe nchi ya visiwa iliyoendelea kiuchumi katika ukanda wa Afrika mashariki.

"Wajumbe wa sektetarieti tumejadili na kutathimini kwa kina juu ya utendaji wa Rais Mwinyi, tukajiridhisha hakuna mbadala wake na anastahiki aongoze nchi kwa kipindi cha miaka saba ili apate muda mzuri wa kufanya Mapinduzi ya kimaendeleo katika nyanja za kiuchumi na kijamii,” amesema Dkt. Dimwa.

K**a ulimsikia  akieleza kuwa 'Muziki wa Samia' ndio itakuwa album yake ya mwisho kwenye muziki wake basi unachotakiwa k...
20/06/2024

K**a ulimsikia akieleza kuwa 'Muziki wa Samia' ndio itakuwa album yake ya mwisho kwenye muziki wake basi unachotakiwa kujua ni kwamba amefuta hiyo kauli! Anaeleza ndani tayari ana album inaitwa 'World Cup' yenye collabo za kimataifa kutoka kila pande ya Dunia •

Klabu ya Simba imemtangaza mchezaji Lameck Lawi aliyekuwa Coastal Union kuwa mchezaji wao mpya✍️Beki huyo wa kati alikuw...
20/06/2024

Klabu ya Simba imemtangaza mchezaji Lameck Lawi aliyekuwa Coastal Union kuwa mchezaji wao mpya✍️

Beki huyo wa kati alikuwa kwenye kiwango bora kwa misimu miwili mfululizo✅

Mangungu jembe sio jembe!?😅 Mnawapa % ngapi kwa usajili huu!?

🚨 MUITO OBRIGADO LUIS MIQUISSONKlabu ya Simba imetangaza kuachana na nyota Luis Miquisson baada ya kutoridhishwa na kiwa...
19/06/2024

🚨 MUITO OBRIGADO LUIS MIQUISSON
Klabu ya Simba imetangaza kuachana na nyota Luis Miquisson baada ya kutoridhishwa na kiwango cha nyota huyo wa Kimataifa wa Msumbiji mzaliwa wa Tete!

Miq alijiunga na klabu hiyo akitokea Misri alikotemwa na klabu ya Al Ahly ya Misri na sasa si faida tena kwa klabu hiyo. Miquisson huenda akajiunga na UD De Songo ya pale pale Msumbiji.

Kipi utakikumbuka kwa Luis Miquisson!?
Mnyama k**a yupo Serious!?🤔🥷

Jeshi la Polisi linawashikilia watu tisa kwa tuhuma za kuhusika na tukio la mauaji ya mtoto aliyekuwa na ulemavu wa ngoz...
19/06/2024

Jeshi la Polisi linawashikilia watu tisa kwa tuhuma za kuhusika na tukio la mauaji ya mtoto aliyekuwa na ulemavu wa ngozi (albino), Asimwe Novart mwenye umri wa miaka miwili na nusu.



Mtoto huyo aliporwa na watu wasiofahamika kutoka kwa mama yake Mei 30, 2024 katika kijiji cha Bulamula Wilaya ya Muleba mkoani Kagera. Mwili wa mtoto huyo ulipatikana Juni 17, 2024 ukiwa hauna baadhi ya viungo katika kijiji cha Makongora.

Taarifa iliyotolewa leo na Msemaji wa Jeshi la Polisi, David Misime imeeleza kuwa Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na raia wema walianza msako mkali kuanzia Mei 31, 2024 hadi usiku wa kuamkia leo Juni 19, 2024 ambapo watuhumiwa tisa wamek**atwa wakiwa na viungo vinavyodhaniwa ni vya mtoto Asimwe Novart wakitafuta mteja.

Watuhumiwa waliok**atwa ambao kwa mujibu wa polisi wameeleza jinsi walivyoshiriki katika tukio hili ni pamoja baba mzazi wa mtoto huyo, Novart Venant.

Wengine ni Desideli Evarist ambaye ni mganga wa jadi, mkazi wa Nyakahama na Elipidius Rwegoshora, Paroko Msaidizi wa Parokia ya Bugandika ambaye anadaiwa kumfuata na kumshawishi baba mzazi wa mtoto huyo wafanye biashara ya viungo vya binadamu.

Paroko huyo msaidizi anatuhumiwa pia kwamba ndiye aliyemtafuta mganga wa jadi na kulipia gharama zote za uganga.

Watuhumiwa wengine ni Dastan Kaiza, mkazi wa Bushagara, Faswiru Athuman mkazi wa Nyakahama, Gozibert Alkadi wa Nyakahama K**achumu, Rwenyagira Burka wa Nyakahama K**achumu, Ramadhani Selestine wa K**achumu na Nurdin Hamada ambaye pia ni mkazi wa K**achumu.

Jeshi la Polisi limetoa onyo kali kwa watu wanaoendekeza imani za kishirikina ikiwemo kupiga ramli chonganishi wakiaminishana kwamba wanaweza kupata utajiri kwa njia za kishirikina kuacha tabia hizo.

"Watu waache kudanganyana kwamba kuna utajiri unaopatikana kwa kumiliki viungo vya binadamu mwenye ualbino, si kweli kwa sababu k**a ingekuwa hivyo familia zenye watoto au ndugu wenye ualbino wangekuwa na utajiri mkubwa," amesema Misime.

Uongozi wa  baada ya Jana kuanza na kutoa Thank you kwa John Bocco, leo wametoa mkono wa kwaheri rasmi kwa Kiungo wake S...
18/06/2024

Uongozi wa baada ya Jana kuanza na kutoa Thank you kwa John Bocco, leo wametoa mkono wa kwaheri rasmi kwa Kiungo wake Saido Ntibazonkiza Raia kutoka Burundi baada ya kuitumikia Simba kwa msimu wa Miaka miwili.

Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) imeitaka serikali kupitia Wizara ya Habari, Mawasiliano na Tek...
11/06/2024

Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) imeitaka serikali kupitia Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kuhakikisha inaufungia mtandao wa 'X' zamani ukijulikana k**a 'tweeter' kwa kuwa mtandao huo kutangaza dhamira ya kuruhusu kupokea maudhui yanayokinzana mila, desturi na silka ya Watanzania

Hayo yamezungumzwa na Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Mohamed Ali Mohamed (Kawaida) wakati akizungumza na wanahabari leo, Jumanne Juni 11.2024 jijini Dar es Salaam ambapo amesema hatua ya kuufuta mtandao huo itasaidia kuendelea kulinda maadili ya vijana wa Tanzania kwa kuwa mitandao ya kijamii haipaswi kupewa kipaumbele k**a inachochea uvunjifu wa mila na desturi

Kawaida amesema hivi karibuni mtandao huo (X) umetoa tangazo ukieleza kwamba maudhui yote ya kingono na Yale yanayofanana na hayo yameruhusiwa kupokelewa

  Watu wote tisa waliokuwemo katika ndege iliyombeba Makamu wa Rais wa Malawi Dkt.Saulos Chilima wamefariki dunia baada ...
11/06/2024

Watu wote tisa waliokuwemo katika ndege iliyombeba Makamu wa Rais wa Malawi Dkt.Saulos Chilima wamefariki dunia baada ndege hiyo kuanguka katika msitu wa Chikangawa.

Kufuatia ajali hiyo, Rais Lazarus Chakwera ametoa pole kwa familia na ndugu waliopoteza wapendwa wao na bendera za nchi hiyo zitapepea nusu mlingoti hadi mazishi yatakapofanyika.

Dkt.Chilima amekuwa Makamu wa Rais wa Malawi tangu mwaka 2020.

Uteuzi wa RC Simiyu watenguliwaRais Samia Suluhu Hassan ametengua uteuzi wa mkuu wa mkoa wa Simiyu Dkt. Yahya Nawanda.Ku...
11/06/2024

Uteuzi wa RC Simiyu watenguliwa

Rais Samia Suluhu Hassan ametengua uteuzi wa mkuu wa mkoa wa Simiyu Dkt. Yahya Nawanda.

Kufuatia hatua hiyo, amemteua Kenan Kihongosi kuwa mkuu wa mkoa wa Simiyu.

Kabla ya uteuzi huo Kihongosi alikuwa mkuu wa wilaya ya Momba mkoani Songwe.

Klabu ya Singida black stars(Ihefu)Imefikia  Makubaliano ya Awali ya kumsajili Kwa  mwaka mmoja PATRICK AUSSEMS Kuwa koc...
07/06/2024

Klabu ya Singida black stars(Ihefu)
Imefikia Makubaliano ya Awali ya kumsajili Kwa mwaka mmoja PATRICK AUSSEMS Kuwa kocha mkuu wa Timu hiyo msimu wa 2024/2025

Kwa sasa kocha AUSSEMS Anaendelea na Zoezi la Usajili kwa Ushirikiano na Menejimenti.

Aliyekuwa CEO wa klabu ya Simba, Barbara Gonzalez inaelezwa kuwa amekubali kurejea ndani ya klabu hiyo na kuridhi mikoba...
07/06/2024

Aliyekuwa CEO wa klabu ya Simba, Barbara Gonzalez inaelezwa kuwa amekubali kurejea ndani ya klabu hiyo na kuridhi mikoba ya Salim Abdalah 'Try Again' ili kuiongoza Bodi ya klabu hiyo.

Rais wa heshima wa Simba, Mohammed Dewj ‘MO’inaelezwa kuwa amewapigia wajumbe wa upande wake akiwataka waandike barua za kujiuzulu kwa lengo la kuunda safu mpya ya uongozi wawili hao wanadaiwa kugomea agizo hilo hadi sasa.

Inaelezwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Klabu ya Simba kwa sasa, Salim Abdallah 'Try Again' na mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi, Rashid Shangazi wamegomea uamuzi wa Rais wa heshima wa klabu hiyo akiwataka waandike barua ya kujiuzulu.

“Hadi sasa Try Again na Shangazi hawajaandika barua lakini wengine wote tayari k**a mambo yataenda sawa kesho au keshokutwa Barbara Gonzalez atatangazwa kuwa Mwenyekiti na CEO anatafutwa,”

Barbara arejee au?

Nyota wa Azam FC, Feisal Salum akiondoka kwa huzuni mbele ya Kombe la Shirikisho la CRDB lililotwaliwa na Yanga baada ya...
03/06/2024

Nyota wa Azam FC, Feisal Salum akiondoka kwa huzuni mbele ya Kombe la Shirikisho la CRDB lililotwaliwa na Yanga baada ya timu yake kupoteza katika fainali ya pige nikupige iliyoamriwa kwa mikwaju ya penati katika dimba la New Amaan Complex, Zanzibar.

Yanga ilishinda kwa penati 6 dhidi ya 5 za Azam

Klabu ya Yanga Sc imetwaa kombe la shirikisho la Benki ya CRDB kwa mara ya nne (4) baada ya kuifunga Azam FC, jumla ya p...
02/06/2024

Klabu ya Yanga Sc imetwaa kombe la shirikisho la Benki ya CRDB kwa mara ya nne (4) baada ya kuifunga Azam FC, jumla ya penati 6-5 katika fainali iliyochezwa katika Dimba la Amaan, visiwani Zanzibar leo Juni 2, 2024.

✍🏽

  REAL MADRID imetwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa mara ya 15 kufuatia ushindi wa 2-0 dhidi miamba ya Ujerumani...
01/06/2024

REAL MADRID imetwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa mara ya 15 kufuatia ushindi wa 2-0 dhidi miamba ya Ujerumani, Borussia Dortmund kwenye fainali iliyopigwa katika dimba la Wembley, London.

FT: Dortmund 🇩🇪 0-2 🇪🇸 Real Madrid
⚽ Carvajal 73’
⚽ Vini Jr 82’

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa Ndege wa Jeshi wa Seoul, Jam...
31/05/2024

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa Ndege wa Jeshi wa Seoul, Jamhuri ya Korea kwa ajili ya Ziara Rasmi ya Kikazi tarehe 31 Mei, 2024.

 : Nyota wa timu ya Al Ahly Hussein El-Shahat amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela na kulipa faini ya Pauni 100,000 ...
31/05/2024

: Nyota wa timu ya Al Ahly Hussein El-Shahat amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela na kulipa faini ya Pauni 100,000 za Misri kwa kosa la kumpiga beki wa kulia wa Pyramids Mohamed El-Chibi wakati wa mchezo uliochezwa July 23, 2023 baada ya Al Ahly kuchapwa mabao 3-0 msimu uliopita.

El-Chibi alimshutumu El-Shahat kwa kumpiga makofi, matusi na vitisho mbele ya mamilioni ya watazamaji waliokuwa kwakitazama mchezo huo, mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo, El-Shahat alimuomba msamaha El-Chibi ana kwa ana.

Uamuzi wa mahak**a nchini Misri ulitoa kauli ifuatayo "mahak**a ya Jiji la Nasr inamhukumu Hussein El-Shahat kifungo cha mwaka mmoja jela na faini ya Pauni 100,00, na kufungiwa kwa muda wa miaka mitano kujihusisha na soka"

Katika ufafanuzi wa adhabu hiyo, El-Shahat kwa kipindi hicho cha mwaka mmoja atakuwa chini ya uangalizi, hatakiwi kufanya kosa lolote, aidha ndani ya kipindi cha miaka mitano Shahat hataruhusiwa kushika wadhifa wowote wala kuwa mwanachama wa timu yeyote ya michezo na hatma yake itasalia kwenye uangalizi.

Wahitimu 188,787 kati ya 197,426 waliofaulu mitihani ya kidato cha nne, wamechaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha t...
30/05/2024

Wahitimu 188,787 kati ya 197,426 waliofaulu mitihani ya kidato cha nne, wamechaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha tano na sita pamoja na vyuo mbalimbali kwa mwaka 2024.

“Wanafunzi waliochaguliwa baada ya kukidhi vigezo wapo wenye mahitaji maalumu 812 na kupangiwa kujiunga na kidato cha tano katika shule mbalimbali nchini pamoja na vyuo vya kati katika fani mbalimbali,”amesema Mchengerwa.

Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Rais Tawala za Miko ana Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa amesema hayo leo Alhamisi Mei 30, 2024 wakati akitangaza uchaguzi wa wanafunzi.

Mchengerwa amesema wanafunzi 131,986 wakiwamo wasichana 66,432 na wavulana 65,554 wenye sifa, wamechaguliwa kujiunga na shule za sekondari za kidato cha tano 622 zikiwamo shule mpya 82 zinazoanza mwaka huu wa 2024.

“Wanafunzi 1,462 wakiwamo wasichana 669 na wavulana 793 walipangwa katika shule za sekondari nane zinazopokea wanafunzi wenye ufaulu wa juu zaidi ambazo ni Kilakala, Mzumbe, Ilboru, Kisimiri, Msalato, Kibaha, Tabora Boys na Tabora Girls,”amesema Mchengerwa.

Pia, amesema wanafunzi 6,576 wakiwamo wasichana 3,449 na wavulana 3,127 wamepangwa katika shule za sekondari za kutwa za kidato cha tano huku wanafunzi 123,948 wakiwamo wasichana 62,636 na wavulana 61,312 wamepangiwa katika shule za sekondari za bweni za kitaifa za kidato cha tano.

-Muonekano Mpya wa kombe CRDB Bank Federation Cup kombe ambalo litatolewa kwa bingwa wa msimu huu 2023/24 kati ya Yanga ...
30/05/2024

-Muonekano Mpya wa kombe CRDB Bank Federation Cup kombe ambalo litatolewa kwa bingwa wa msimu huu 2023/24 kati ya Yanga SC dhidi Azam FC kwenye fainali ya FA Cup ambayo itachezwa Jumapili June 02 kwenye dimba la New Amaan Complex, Zanzibar

 : Mlinda mlango wa klabu ya Yanga SC Djigui Diara ametwaa tuzo ya mchezaj bora wa Afrika kwa msimu wa 2023\2024, katika...
30/05/2024

: Mlinda mlango wa klabu ya Yanga SC Djigui Diara ametwaa tuzo ya mchezaj bora wa Afrika kwa msimu wa 2023\2024, katika tuzo zilizotolewa nchini Mali. Tuzo hizo maalum zilizotolewa nchini Mali ni kwa wachezaji wa nchini humo wanaocheza ndani ya Bara la Afrika

Diara amechukua tuzo hiyo akiwashinda wachezaji wenzake, Sadio Kanute, Fily Traore, Aliou Dieng na Abdoulaye kanou waliokuwa wakiwania tuzo hiyo. Tuzo hizo maalum hutolewa kwa wachezaji wanaofanya vizuri katika msimu husika.

Ni kweli Diara amestahili tuzo hiyo

  ya Azam Fc imefanikiwa kumsajili Mshambuliaji Jhonier BlancoAlikuwa mfungaji bora wa Ligi Daraja la Kwanza nchini Colo...
30/05/2024

ya Azam Fc imefanikiwa kumsajili Mshambuliaji Jhonier Blanco
Alikuwa mfungaji bora wa Ligi Daraja la Kwanza nchini Colombia (Categoría Primera) akiwa na Fortaleza CEIF, akifunga mabao 13, msimu uliopita 2022/23.

Blanco, alifanikiwa kuisaidia Fortaleza kupanda daraja na kuchukua ubingwa, huku akihitimisha msimu huo kwa rekodi nzuri baada ya kufunga jumla ya mabao 18 kwenye mechi 26 za mashindano yote.

Welcome to Azam FC, 🔝🇨🇴 striker!
Blanco!

 : Afisa habari wa klabu ya Simba Ahmed Ally amesema timu ya samba imejipanga vizuri kushiriki na kufanya vizuri katika ...
29/05/2024

: Afisa habari wa klabu ya Simba Ahmed Ally amesema timu ya samba imejipanga vizuri kushiriki na kufanya vizuri katika kombe la Shirikisho Barani Africa msimu ujao baada ya kuishia nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi kuu bara msimu ulioisha wa 2023\2024.

Simba itaungana na Costal Union katika kombe la Shirikisho huku mabingwa wa Tanzania Yanga SC na Azam FC wakishiriki klabu bingwa Barani Afrika kwa kumaliza nafasi ya pili licha yakuwa na alama sawa na Simba ila wakiwa na tofauti kubwa ya magoli.

Wana-Simba mna maoni gani juu ya kauli ya semaji?

MATOKEO YA MICHEZO YA LEOFT: Simba 2-0 JKT Tanzania (Saido 88’p, Onana 90’+2)FT: Geita Gold 0-2 Azam (Yeison 58’, Feisal...
28/05/2024

MATOKEO YA MICHEZO YA LEO

FT: Simba 2-0 JKT Tanzania (Saido 88’p, Onana 90’+2)

FT: Geita Gold 0-2 Azam (Yeison 58’, Feisal 71’)

FT: Yanga 4-1 TZ Prisons (Aziz Ki 11’, 12’, 79’ Musonda 52’ / Ngassa 5’)

FT: Namungo 3-2 Tabora United (Buswita 19’, 28’p, Manyanya 77’ / Abbas 84’, Moses)

FT: Coastal Union 0-0 KMC

FT: Mashujaa 3-0 Dodoma Jiji (Lusajo 6’, 47’, Ulomi 84’)

FT: Ihefu SC 5-1 Mtibwa Sugar (Bola 5’, Chukwu 16’, Mgunda 41’, 62’, 74’ / Karihe 37’)

FT: Singida FG 2-3 Kagera Sugar (Kidemile 19’, Kaseke 84’p / Mafie 40’, Mbaraka 46’, Mhilu 82”

 : Kaminsheni ya ngumi za kulipwa nchini  TPBRC limesitisha pambano la ngumi baina ya bondia mtanzania Hassani Mwakinyo ...
28/05/2024

: Kaminsheni ya ngumi za kulipwa nchini TPBRC limesitisha pambano la ngumi baina ya bondia mtanzania Hassani Mwakinyo dhidi Pactick Allotey kutoka Ghana kutokana na promota kushindwa kukidhi vigezo. moja ikiwa ni malipo kwa mabondia hao na pili ni ukumbi ambao utachezwa pambano hilo kutofikia viwango.

Mume wa Shilole, Rommy amethibitisha kuachana na msanii huyo kwa madai ya kumpisha kijana mwingine aendeleze gurudumu!."...
28/05/2024

Mume wa Shilole, Rommy amethibitisha kuachana na msanii huyo kwa madai ya kumpisha kijana mwingine aendeleze gurudumu!.

"Mimi na aliyekuwa mwenzangu Zuwena Mohamed (Shilole), naona tumefikia mwisho na si vibaya nikakubali matokeo na kumpisha kijana mwenzangu aendeleze gurudumu hili, na Maisha yaendelee.".

"Nipende kutoa shukrani zangu za dhati kwa vile tulivyoishi siku zote za mapenzi yetu. Wabillah Tawfiq" amesema Rommy 3D.

Agness Simkanga (22) ambaye ni mwanafunzi wa utabibu, ameshinda taji lla urembo kwa mkoa wa  Mwanza ( Miss Mwanza 2024)....
26/05/2024

Agness Simkanga (22) ambaye ni mwanafunzi wa utabibu,
ameshinda taji lla urembo kwa mkoa wa Mwanza ( Miss Mwanza 2024).

  "Msimu ujao Yanga ikifungwa na timu yoyote njooni mchome moto nyumba Yangu" Amesema  wakati akitumbuiza kwenye sherehe...
26/05/2024

"Msimu ujao Yanga ikifungwa na timu yoyote njooni mchome moto nyumba Yangu" Amesema wakati akitumbuiza kwenye sherehe za ubingwa leo pale Jangwani.

Mwanamitindo na Mwanamuziki, Hamisa Mobetto amethibitisha kuachana na mpenzi wake, Kevin Sowax kutokea nchini Togo ambay...
26/05/2024

Mwanamitindo na Mwanamuziki, Hamisa Mobetto amethibitisha kuachana na mpenzi wake, Kevin Sowax kutokea nchini Togo ambaye mwishoni mwa 2023 walionekana pamoja.

Utakumbuka kabla ya Kevin, Hamisa alihusishwa kuwa na uhusiano na Rapa wa Marekani, Rick Ross baada ya kuonekana kuwa na ukaribu katika mitandao ya kijamii na baadaye kukutana Dubai kwa mara ya kwanza.

"Sina mahusiano nipo single, yule (Kelvin) tuliachana muda kidogo umepita, hakukuwa na sababu maalum ila suala mmoja tuseme ilikuwa ni umbali baina yetu, yeye yupo bize, mimi nipo bize." amesema Hamisa.

Utakumbuka katika historia yake, Hamisa ambaye ni mama wa watoto wawili sio mtu wa kuweka sana hadharani mahusiano yake ila kwa Kevin mambo yaliwekwa sana hadharani, picha nilikuwa za kutosha.

𝐏𝐀𝐑𝐀𝐃𝐄 𝐋𝐀 𝐌𝐀𝐁𝐈𝐍𝐆𝐖𝐀Skudu na SHANGWE k**a lote  Parade likiendelea Jijini DSM Katika Mitaa Mbali Mbali
26/05/2024

𝐏𝐀𝐑𝐀𝐃𝐄 𝐋𝐀 𝐌𝐀𝐁𝐈𝐍𝐆𝐖𝐀
Skudu na SHANGWE k**a lote Parade likiendelea Jijini DSM Katika Mitaa Mbali Mbali

Address


Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Casa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

  • Address
  • Alerts
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share