Jambo FM Tanzania

Jambo FM Tanzania The official page for Jambo FM Radio

Ukurasa rasmi wa Jambo FM Radio


📻 92.7 Shinyanga
(1)

09/01/2026

Mbunge wa Jimbo la Meatu, Salum Khamis Saluma ametekeleza ahadi yale kwa Chama Cha mpira wa miguu wilaya ya Meatu (MEDIFA) ya kutoa jezi seti sita, mipira na kombe kwa ajili ya michuano ya moira wa miguu vijana mkoa wa Simiyu.

Vifaa hivyo vimepokelewa na Christian Nkunga, katibu wa MEDIFA aliyeambatana na katibu wake msaidizi, Bw. Sanga walipofika Makao Makuu ya Ibadakuli, Shinyanga.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amemteua aliyekuwa Naibu waziri wa Wizara ya Habari, S...
08/01/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amemteua aliyekuwa Naibu waziri wa Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Paul Christian Makonda kuwa Waziri wa Wizara hiyo ambayo aliyekuwa waziri wake Prof. Palamagamba Kabudi ameteuliwa kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Ikulu (Kazi Maalum).

Pia Rais amemteua Patrobas Katambi kuwa Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani akichukua nafasi ya Simbachawene ambaye utauzi wake umetenguliwa.

Aliyekuwa katibu wa Rais, Bw. Waziri Rajab Salum ameteuliwa kuwa Balozi na wataapishwa tarehe 13 Januari, 2026 Ikulu ya Chamwino, Dodoma.

07/01/2026

Kifahamu kisiwa kidogo zaidi duniani "Migingo Island" chenye watu wengi kilichopo Ziwa Victoria ambacho ukubwa wake ni k**a nusu uwanja wa mpira wa miguu ila kina wakazi wanaofikia elfu moja.

Ni kwa nini imekuwa ngumu kwa nchi ya Kenya na Uganda kufikia makubaliano juu ya nani anapaswa kudhibiti kisiwa hiki?

Sponsored by

06/01/2026

Huzuni imetanda katika Kata ya Tumbi, Manispaa ya Tabora, baada ya mwili wa kijana mmoja dereva wa pikipiki kupatikana umefariki na kutupwa katika msitu wa Matitumbi.

Marehemu ametambulika kwa jina la Sigela Hamisi Maulidi (23), mkazi wa eneo hilo, ambaye aliripotiwa kupotea kwa siku tatu mfululizo.

Kwa mujibu wa viongozi wa eneo hilo, kijana huyo alionekana mara ya mwisho tarehe 4 ya mwezi huu majira ya saa moja usiku, baada ya kupokea simu kutoka kwa mtu aliyedhaniwa kuwa abiria. Tangu wakati huo hakurejea nyumbani wala kuwasiliana na ndugu zake.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Tumbi, Rajabu Hamsini, akizungumza pamoja na Mwenyekiti wa Kitongoji husika Mollo John, wamesema juhudi za kumtafuta zilianza mara moja kwa kushirikiana na familia ya marehemu pamoja na madereva wenzake wa bodaboda.

Hatimaye, leo mwili wake uligundulika msituni ukiwa umefungwa mikono kwa kamba na miguu ikiwa imefungwa kwa mipira, huku pikipiki yake ikiwa haijulikani ilipo.

Baba mzazi wa marehemu, Hamisi Maulidi, amesema mwanawe aliondoka nyumbani usiku huo bila kubeba abiria yoyote, hali iliyozua maswali zaidi juu ya mazingira ya tukio hilo la kikatili.

Akitoa tahadhari kufuatia tukio hilo, Mwenyekiti wa Maafisa Usafirishaji Mkoa wa Tabora, Mrisho Shime, amewataka madereva wa bodaboda kuwa waangalifu zaidi, hasa kuepuka kubeba abiria wasiowafahamu au zaidi ya mmoja, hasa nyakati za usiku na maeneo ya nje ya mji.

Wakati huo huo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora limefika eneo la tukio na kuchukua mwili wa marehemu kwa ajili ya uchunguzi wa kina, huku uchunguzi wa kubaini waliohusika na tukio hilo ukiendelea.

✍️ Pascal Tuliano

05/01/2026

Watu watatu wa familia moja wamefariki dunia katika eneo la Nyarusurya, Manispaa ya Musoma mkoani Mara, baada ya moto mkubwa kuteketeza nyumba yao usiku wa kuamkia leo.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Mara,Augustin Magere amesema moto huo ulianzia sebuleni na kusambaa kwa kasi hadi kwenye vyumba vinne vya nyumba hiyo, hali iliyosababisha vifo vya watu watatu wa familia moja.

Mashuhuda wa tukio hilo pamoja na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Nyarusurya,Iddy Jafari wamesema juhudi za kuuzima moto huo zilikuwa ngumu kutokana na moto kuenea kwa kasi wakati familia hiyo ikiwa imelala.

Kwa mujibu wa wakazi wa eneo hilo, moto huo ulizuka majira ya usiku wa manane na kuteketeza mali mbalimbali, huku familia hiyo ikimpoteza baba, mama na mtoto.

✍️ Adam Msafiri

03/01/2026

Ahsante 2025 kutoka gridi ya maisha fresh namba 101.5 Simiyu, Saada Almasi Mwandishi wa habari na mwakilishi wa Jambo Media mkoani Simiyu.

ASANTE 2025 🙏.

03/01/2026

Kutoka 102.5 mkoani Simiyu, Mkurugenzi wa Mji wa Bariadi Bw. Idd Ndabona na ASANTE 2025 na ahadi ya maisha fresh kwa Wanabariadi kwa mwaka wa 2026.

ASANTE 2025 🙏.

03/01/2026

ASANTE 2025 za Kamanda wa jeshi la polisi kutoka 106.9 Geita, SACP Safia Jongo kwenda kwa wanamaisha fresh wote wa mkoa wa Geita kwa kudumisha amani na kushirikiana na jeshi la polisi katika kudhibiti matukio ya kihalifu.

ASANTE 2025 🙏.

03/01/2026

Kutoka 95.3 mkoani Katavi, SACP Kaster Ngonyani na ASANTE 2025 kwa wananchi wa mkoa wa Katavi zilizoambatana na ahadi ya usalama wa raia na mali zao kwa mwaka 2026.

ASANTE 2025 🙏

02/01/2026

Moto mkubwa umezuka na kuteketeza eneo maarufu la starehe maarufu kwa jina la "Suzy Lounge" pamoja na nyumba ya kulala wageni katika mamlaka ya mji mdogo wa Katoro, wilayani Geita mkoani Geita na kusababisha hasara baada ya mali kuteketea.
Tukio hilo limetokea Januari 02, 2026 huku chanzo cha awali cha moto huo kikielezwa kuwa ni hitilafu ya umeme, na hakuna taarifa za majeruhi zilizothibitishwa hadi sasa.

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema moto huo ulizuka ghafla baada ya umeme kukatika na kurejea, hali iliyosababisha mlipuko kabla ya moto kuenea kwa kasi na kueleza kwamba mali zote zimeteketea kabisa, huku baadhi yao wakiomba serikali kuweka kito cha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji katika mji huo.

Akizungumza kuhusiana na tukio hilo, Mkurugenzi wa Suzy Lounge, Peter Cheyo, amesema moto huo ulitokea baada ya umeme kukatika na kurejea ghafla, hali iliyosababisha mlipuko na kuanzisha moto ulioteketeza mali zote zilizokuwemo ndani ya ‘lounge’ hiyo.

Akithibitisha tukio hilo, Mkuu wa Kituo cha Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Geita, Mrakibu Msaidizi Wambura Fider, amesema walipata taarifa za tukio hilo kwa kuchelewa, na baada ya uchunguzi umebaini chanzo cha moto ni hitilafu ya umeme, huku akibainisha kuwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limefanikiwa kuokoa baadhi ya mali na kuzuia moto kufika sehemu ya Nyumba ya kulala wageni ambako vyumba viwili pekee vilifikiwa na moto huo,



Aidha amesema zipo jitihada zinafanyika ili kusogeza karibu huduma ya zimamoto na uokoaji katika Mji wa Katoro ili kuboresha huduma za uokoaji.

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Katoro, Mh. Eng. Khija Ntemi amefika eneo la tukio na kutoa pole kwa waathirika wa janga hilo, huku akiahidi kufuatilia na kupeleka huduma ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji katika mji mdogo wa Katoro

✍️

02/01/2026

Mzigo huu hapa 'Jambo Long Life Milk' maziwa halisi ya ng'ombe yaliyoandaliwa kwa ubora wa hali ya juu yanayoweza kudumu muda mrefu yakiwa na ladha na virutubisho asilia.

Jipatie ya kwako na familia yako, yanapatikana madukani na kwenye supermarkets.



02/01/2026

anaamini kwenye upande wa series movie mwaka 2025 umekuwa wa muigizaji na mtayatishaji wa filamu kutoka nchini Marekani, Tyler Perry.

Full Episode ya Series 10 bora zaidi kwa mwaka 2025 tumekuwekea kwenye chaneli yetu ya Youtube 'Jambo FM Radio Tanzania'.

Sponsored by Jambo Long Life Milk kutoka

Hosts:
🎥

Address

P. O. BOX 71
Shinyanga

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jambo FM Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Jambo FM Tanzania:

Share

Category