WANAWAKE DODOMA WAIUNGA MKONO SERIKALI KUSAIDIA MAKUNDI MAALUMU
Taasisi ya kikundi cha wanawake ya Jijini Dodoma ijulikanayo kama WE CAN imetoa msaada wa mahitaji muhimu kwa Wanafunzi wa Shule ya Msingi Buigiri yenye Wanafunzi Wasioona pamoja na wenye ulemavu wa ngozi.
Akizungumza leo tarehe 02 Februari 2025 mara baada ya kukabidhi msaada huo Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Bi. Emmah Kelvin Komba amesema wametoa misaada hiyo ikiwa ni kuunga jitihada zinazofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuyashika mkono makundi maalumu ya watu wenye uhitaji ikiwamo watoto, walemavu na hata Wazee.
Kwa Upande wake Mkuu wa Shule hiyo Mwalimu Samwel Sospeter ameishukuru taasisi kwa kuwakumbuka watoto hao kwa kuwapatia mahitaji muhimu kama nguo chakula na kuchangia kuboresha miundombinu ikiwemo taa za umeme.
Kadhalika Mkuu huyo amesema wanajivunia kuwa na Viongozi katika Ngazi za juu za Serikali waliosoma katika Shule hiyo akiwamo Dkt. Abdallah Saleh Possi ambaye ni Mwakilishi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Ofisi ya Umoja wa Mataifa na Mashirika mengine ya Kimataifa mjini Geneva.
Vilevile Wanafunzi wa Shule hiyo wameishukuru Taasisi hiyo kwa mchango na kuwaomba wawe mabalozi kwa wadau wengine katika kuwasadia watoto Hao.
TAZAMA KILICHOZUNGUMZWA NA WANACHAMA WA CHADEMA KANDA YA SERENGETI BAADA YA KUWASILI NA KUPOKELEWA MKOANI SHINYANGA.
⛔ Ni wajumbe wa mkutano mkuu ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kanda ya Serengeti wakipiga shangwe baada ya kuwasili Mkoani Shinyanga na kupokelewa na baadhi ya wanachama wa Chama hicho.
LIVE🔴: MISA YA KRISMASI KUTOKA PAROKIA YA MTAKATIFU LUKA ILIYOPO WILAYA YA BARIADI MKOANI SIMIYU AMBAYO INAO NGOZWA NA ASKOFU WA JIMBO KATOLIKI SHINYANGA MHASHAMU LIBERATUS SANGU.
Hello Radio farajatz inakutakia kheri ya Christmas 🎄 na mwaka mpya wewe ni familia yetu hakika tuungane kwa pamoja kuijenga jamii 🙏❤️🙏
CCM KATAVI YAMTAKA MENEJA RUWASA KUKAMILISHA MRADI WA MIL 250 NDANI YA MIEZI MIWILI .
Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi imemtaka meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wilaya ya Mlele Mhandisi Charles Mengo kukamilisha haraka upanuzi wa mradi wa maji Chamalendi wenye gharama ya Shilingi 250, 189,071. 41 unaotekelezwa kwa fedha ya Programu ya P for R.
Hayo yamejiri tarehe 10 Desemba 2024 wakati kamati hiyo ilipofanya ziara ya ukaguzi mradi wa maji safi na Salama uliopo katika kata ya Chamalendi katika jimbo la Kavuu Mkoani Katavi kujionea maendeleo ya mradi huo.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo Ndg. Wolfgang Mizengo Pinda amesema kuchelewa kukamilika kwa mradi huo ni kutokana na kutelekezwa kwa mradi huo na kuzidi kuongeza adha ya Maji kwa wananchi wa kitongoji cha Maimba kilichopo Chamalendi.
Aidha Mjumbe wa kamati ya siasa wilaya ya Mlele na Mbunge wa Jimbo la Kavuu mhe. Geophrey Pinda amesikitishwa na ucheleweshwaji wa mradi huo kukamilika ilihali fedha bado zipo kukalimisha mradi huo na kuahidi kukita kambi hadi mradi utakapokamilika
Naye Mwenyekiti wa halmashauri ya Mlele Mheshimiwa Silas Ilumba ametoa wito kwa meneja huyo kuharakisha ujenzi ili kuweka salama maisha ya wananchi hao kwani wamekuwa wakitumia maji ya mtoni ambayo yapo hatarini kutokana na uwepo wa wanyama wakali kama vile mamba na viboko.
Kukamilika kwa mradi huo utaboresha huduma ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa wakazi 1,239 wa kata ya Chamalendi ambao hawanufaiki moja kwa moja na huduma iliuopo kwa sasa.
WANANCHI KIJIJI CHA LUCHIMA KATA YA MAJIMOTO HALMASHAURI YA WILAYA YA MPIMBWE MKOANI KATAVI WAMPONGEZA RAIS SAMIA KWA MRADI WA KISIMA.
Wananchi wa Kijiji cha Luchima kilichopo kata ya Majimoto katika halmashauri ya wilaya ya Mpimbwe Mkoani Katavi wamempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha Mradi wa kisima cha Maji safi na Salama ambacho kitapunguza adha ya uhaba wa maji Kijijini hapo.
Hayo yamejiri mapema leo tarehe 8 Desemba 2024 Wakati Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Mbunge wa Jimbo hilo Mhe. Geophrey Mizengo Pinda alipotembelea kujionea uchimbaji wa kisima cha hicho.
Jumla ya Visima 900 vya Maji Safi na Salama vinatarajiwa kuchimbwa katika majimbo yote ya Mkoani Katavi ambapo Jimbo la Kavuu litachimbiwa visima vitano (5).
ASKOFU SANGU AWASISITIZA WANANCHI KWENDA KUPIGA KURA KUCHAGUA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA.
Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu amepiga kura kuchagua viongozi wa serikali za Mitaa,Vijiji na Vitongoji katika kituo cha Shule ya Msingi Bugoyi "A" kilichopo Mtaa wa Mbuyuni Mjini Shinyanga.
TAZAMA VIDEO 📸 YA ASKOFU SANGU AKIENDA KUPIGA KURA NA KUWAHAMASISHA WANANCHI KWENDA KUPIGA KURA 👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇
AHUKUMIWA MIAKA 7 JELA KWA KOSA LA KUMTUHUMU MWENZAKE UCHAWI
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga SACP Janeth Magomi amethibitisha taarifa ya kukamatwa na kuhukumiwa kifungo cha miaka saba (7) Jela kwa mtu mmoja aliyeshtakiwa kwa kosa la kumuita mwenzake mchawi.
KWA TAARIFA ZAIDI FUATILIA VIDEO HAPO CHINI 👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇
WAMIAJI HARAMU, FUSU LENYE MBEGU ZA PAMBA MIFUKO 210 LADAKWA NA JESHI LA POLISI MKOANI SHINYANGA.
Jeshi la Polisi Mkoani Shinyanga limefanikiwa kuwakamata wahamiaji haramu saba watatu kati yao walikamatwa mnamo tarehe 13.11.2024 katika Kijiji cha Mseki kata ya Bulungwa Wilayani Kishapu na wengine wanne walikamatwa mnamo tarehe 17.11.2024 katika Kijiji cha Nyamilangano Wilayani Ushetu.
Mnamo tarehe 15.11.2024 Jeshi la Polisi walifanikiqa kukamata watuhumiwa wanne na Gari Moja aina ya Fuso likiwa limebeba mbegu za Pamba mifuko 210 katika Kijiji cha Mwamishoni kata ya Bubiki Wilayani Kishapu.
KWA TAARIFA ZAIDI FUATILIA VIDEO HAPO CHINI 👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇
🔴LIVE:- ASKOFU WA JIMBO KATOLIKI SHINYANGA MHASHAMU LIBERATUS SANGU AKIONGOZA MISA TAKATIFU YA DOMINIKA YA KRISTO MFALME NA KILELE CHA KONGAMANO LA VIJANA KIJIMBO KATIKA PAROKIA YA MTAKATIFU MARIA MAMA WA MUNGU NINDO HALMASHAURI YA WILAYA YA SHINYANGA VIJIJINI (Kuendelea tazama sehemu ya pili juu)