Digital News Tanzania

Digital News Tanzania Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Digital News Tanzania, Media/News Company, Njombe.

MTWANGO  KUNUFAIKA  NA BARABARA ZA LAMIMbunge wa Jimbo la Lupembe Mh Edwini Enosy  Swalle Amesema Tayari Ujenzi  wa Bara...
22/12/2024

MTWANGO KUNUFAIKA NA BARABARA ZA LAMI

Mbunge wa Jimbo la Lupembe Mh Edwini Enosy Swalle Amesema Tayari Ujenzi wa Barabara kwa Kiwango cha Lami yenye thamani ya zaidi shilingi bilioni moja Inayo fika Katika Kituo cha Afya Mtwango Umeanza Rasmi Huku Mkandarasi akiwa na Mkataba wa Miezi Sita ya Kuhakikisha Barabara Hiyo Inakuwa Imekamilika.

Swalle Amesema Hayo Mara Baada ya Kutembelea Mradi Huo na kuukagua akiwa ameongozana na Baadhi ya Viongozi Ili Kuona Maendeleo ya Mradi Huo Ambao Unatekelezwa Kwa Fedha za Mapato ya Ndani Huku Akiwataka Wananchi Kuwa na Subira Pindi Miradi Hiyo Inapo Tekelezwa Kwenye Maeneo Yao.

Aidha Amemuagiza Mkandarasi Aliye Pata Tenda Hiyo Kuhakikisha Barabaraba hiyo Inakuwa na Karavati za Uhakika Kutokana na Thamani ya Fedha Iliyo Tolewa na Serikali.

Kutokana na Hali Hiyo Kituo Hiki Kimezungumza na Mkandarasi Mzawa Aliye pata Tenda Hiyo ambapo Amekiri Kwenda Kufanya Kazi na Kukamilisha Barabara Hiyo Kwa Mujibu wa Mkataba.

Akiwa Katika ziara ya Kikazi Katika Kata ya Mtwango Moja ya Changamoto Ambazo Wananchi Waliomba Serikali zipatiwe Ufumbuni ni Pamoja na Miundombinu ya Barabara ikiwemo Barabara hii ya kuelekea kituo Cha afya cha kata ya Mtwango.

JUMUIYA YA WAZAZI MKOA WA NJOMBE YARIDHISWA NA KAZI ZA RAIS SAMIA/HUYU TUNAENDA NAYE 2025Kufuatia Kuridhishwa na kazi zi...
17/12/2024

JUMUIYA YA WAZAZI MKOA WA NJOMBE YARIDHISWA NA KAZI ZA RAIS SAMIA/HUYU TUNAENDA NAYE 2025

Kufuatia Kuridhishwa na kazi zinazofanywa na Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr Samia Suluhu Hassani Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Njombe ikiongozwa na Wajumbe wa Baraza wa Jumuiya hiyo Wamesema kuwa Wanaungana na Tamko la Chama Makao Makuu na Vikao mbalimbali vya chama linalosema kwamba kuelekea Uchaguzi mkuu 2025 fomu ya Urais ndani ya Chama hicho itachukuliwa na Mwenyekiti wa sasa ambae ni Rais Samia Suluhu Hassani.

Tamko hilo la Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Njombe limetolewa katika kikao cha kawaida cha Baraza hilo ambapo akizungumza kwa niaba ya Wajumbe wa Baraza hilo Mjumbe wa Baraza kuu Taifa Ndugu Rabson Mahenge amesema kuwa hakuna ubishi juu ya kazi zilizofanywa na Serikali ya awamu ya Sita ndani ya nchi hii hivyo k**a Jumuiya ya Wazazi mkoa wa Njombe wanaona kwamba hakuna sababu ya kutoa form nyingi za Urais ndani ya Chama hicho.

Aidha akizungumzia Miradi mbalimbali ya Maendeleo iliyotekelezwa hapa nchini ikiwemo Mkoa wa Njombe Mjumbe wa Baraza kuu Taifa Ndugu Rabson Mahenge amesema kuwa Miradi k**a ya Afya,Elimu,Miundombinu ya Barabara,Maji,Umeme,ndio sababu iliyopelekea Jumuiya ya Wazazi mkoa wa Njombe kuamua kwenda na Rais Samia Pakee katika Uchaguzi wa Urais Mwaka 2025.

Pamoja na hayo katika kikao hicho cha Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Njombe Wajumbe Wamejadiri namna ya Kuimarisha uhai wa Chama pamoja na Kuwapongeza Wanachama wa chama hicho kwa kushinda Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa kishindo huku pia wakiadhimia Ujenzi wa nyumba za Watumishi wa Jumuiya hiyo unaanza ili kuweka mazingira rafiki kwa Watumishi wa Jumuiya ya Wazazi mkoani Njombe

KUTOKA CHUO KIKUU DODOMA TANZANIA Mbunge wa Jimbo la Lupembe na  Wakili wa Mahak**a kuu Mh Edwin Enosy Swalle hii  leo t...
06/12/2024

KUTOKA CHUO KIKUU DODOMA TANZANIA

Mbunge wa Jimbo la Lupembe na Wakili wa Mahak**a kuu Mh Edwin Enosy Swalle hii leo tar 6/12/2204 ametunukiwa Shahada ya Uzimili (Master Of Laws in Corporate- LL.M ) kutoka Chuko Kikuu Cha Dodoma.

Mbunge wa Jimbo la Lupembe Mkoani Njombe Mh Edwin Enosy Swalle hii leo emeendelea kushiriki mikutano ya kampeni za uchag...
22/11/2024

Mbunge wa Jimbo la Lupembe Mkoani Njombe Mh Edwin Enosy Swalle hii leo emeendelea kushiriki mikutano ya kampeni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika Jimbo la Lupembe mkoani Njombe.

Akiwa katika kijiji cha Mfriga Mbunge Tarafa ya Lupembe Mbunge Swalle ametoa Computer moja (laptop)yenye thamani ya shilingi laki saba (700000)kwa chama cha Ushirika (SACCOS)Katika kijiji cha Mfriga Jimbo la Lupembe.

Mbunge Swalle amesema kuwa ametoa Computer hiyo ili isaidie kufanya shughuli mbalimbali katika chama hicho ambacho kinahudumia Wananchi wa Mfriga.

HOSPITALI YA WILAYA YA MAKETE YANUFAIKA NA MGAO WA MASHUKA KUTOKA KWA NEEMA MGAYA MBUNGE VITI MAALUMU MKOA WA NJOMBEMbun...
16/11/2024

HOSPITALI YA WILAYA YA MAKETE YANUFAIKA NA MGAO WA MASHUKA KUTOKA KWA NEEMA MGAYA MBUNGE VITI MAALUMU MKOA WA NJOMBE

Mbunge Viti Maalumu Mkoa wa Njombe Neema Mgaya ametembelea na Kutoa Msaada wa Mashuka ya Kulalia Wagonujwa katika Hospitali ya Wilaya ya Makete.

Akizungumza na Wagonjwa katika Hospitali ya Wilaya ya Makete akiwa ameambatana na Viongozi wengine wa Umoja wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi (UWT) Wilaya ya Makete ambapo emesema kuwa ameamua kufanya hivyo baada ya Kuridhishwa na Uwekezaji Mkubwa unaofanywa na Serikali katika Sekta ya Afya kote nchini hivyo ameamua kuunga mkono jitihada hizo kwa kutoa Mashuka ya Kulalia Wagonjwa katika Hospitali hiyo ya Wilaya.

"Ndugu zangu niwape pole kwa changamoto ya Kuugua lakini Mimi k**a Mbunge wenu wa Viti Maalumu nimekuja hapa kuwaona na kuwapa Pole lakini sijaja Mikono Mitupu bali nimekuja na Zawadi kutoka kwa Rais Samia,Zawadi hizo ni Mashuka ya kujifunika pindi mkiwa hapa Hospitalini,Sisi Wabunge wenu Tunaridhishwa na Utendaji wa Serikali hivyo tumeamua kwa dhati kumuunga mkono Rais Dr Samia Suluhu Hassan katika Utendaji wake na ndio maana leo nimewaletea Mashuka"Amesema Neema Mgaya Mbunge viti maalumu Mkoa wa Njombe.

Ikumbukwe kuwa Mbunge wa Viti maalumu Neema Mgaya amekuwa na Mwendelezo wa Kugawa Mashuka ya Kulalia Wagonjwa katika Maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Njombe hususani katika Zahanati,Vituo vya Afya pamoja na Hospitali ambapo amesema kuwa anaamini Mashuka hayo yanaenda kuacha alama kubwa kwa Wananchi wa Mkoa wa Njombe.

MNUNGE  WA LUPEMBE AKUTANA NA VIONGOZI WA CHAMA CHA WALIMU BUNGENI JIJINI DODOMA.Mbunge wa Jimbo la Lupembe Mh Edwin Eno...
05/11/2024

MNUNGE WA LUPEMBE AKUTANA NA VIONGOZI WA CHAMA CHA WALIMU BUNGENI JIJINI DODOMA.

Mbunge wa Jimbo la Lupembe Mh Edwin Enosy Swalle hii leo November 5 akiwa Bungeni Jijini Dodoma amekutana na kufanya mazungumzo na Viongozi wa Chama cha Walimu Wilaya ya Njombe ambapo pamoja na Mambo Mengine Viongozi wa CWT WIlauya ya Njombe Walimweleza changamoto mbalimbali zinazowakabiri Walimu kwa ujumla wake huku na yeye akizipokea kwa niaba ya Wabunge Wengine wa wanaotoka katika Majimbo yaliyopo ndani ya Wilaya ya Njombe.

Ujumbe huu wa Chama cha Walimu ulioelekea Bungeni Jijini Dodoma Uliongozwa na Mwenyekiti wa CWT Wilaya ya Njombe Mwl. Varian Ngalyoma ambapo Pamona na Mambo Mengine wamemueleza baadhi ya changamoto ambazo zinawakabiri Walimu ambapo Wanatarajia Changamoto hizo zitachukuliwa na Wabunge wanaotoka katika Majimbo yaliyopo ndani ya Wilaya ya Njombe na kuzipeleka Serikalini kwaajili ya kutafuta Majawabu.

Mbunge wa jimbo la lupembe Mh Edwin Enosy  swalle amesema wananchi wa kata ya ikondo wanaenda kuondokana na adha ya Mawa...
03/11/2024

Mbunge wa jimbo la lupembe Mh Edwin Enosy swalle amesema wananchi wa kata ya ikondo wanaenda kuondokana na adha ya Mawasiliano iliyo wakabili kwa zaidi ya miaka 40 na kwamba tayari serikali imesha anza ujenzi wa mnara wa mawasiliano ili kuwanusuru wannachi wake na masuala ya kiuchumi.

Swalle amesema hayo akiwa katika Parokia ya Matembwe jimbo la lupembe Mkoani Njombe ambapo amesema kutokana na Changamoto ya mawasiliano inayo wakabili wananchi kwa miaka mingi na kuzorotesha uchumi wao hatimaye serikali tayari imeshapeleka wakandarasi katika kata hiyo ya ikondo tayari kwa kuanza Ujenzi wa mnara huo.

Awali Paroko wa palokia ya Matembwe iliyopo katika Jimbo la Lupembe amewataka wananchi kushiriki shughuli za maendeleo katika maeneo yao na kwamba kufanya hivyo kuna leta tija kwa wananchi na Serikali yao huku baaadhi ya madiwani wakiwasihi wananchi kwenda kuchagua Viongozi watakao wafaa kwa miaka mitano ijayo.

Kutokana na hali hiyo kituo hiki kimelazimika kuzungunza na wananchi wa jimbo la lupembe ambao wamekiri ya kwamba kujengwa kwa mnara wa Mawasiliano katika kata ya Ikondo kunaenda kufufua uchumi wa wananchi hao na maendeleo ya kata hiyo.

Itakumukwa siku tatu zilizopita wakati mbunge swalle akiuliza swali Bungeni juu ya Umuhimu wa kupeleka mawasiliano ya simu kwa Wananchi wa ikondo, serikali ikasema tayari imeshapeleka wakandarasi kuanza Ujenzi wa mnara huo ili kutasaidia wananchi wa kata hiyo kuendelea na shughuli mbalimbali za Kiuchumi ndani ya kata hiyo kwa kuwa naawasiliano safi.

SERIKALI KUANZA UJENZI WA MNARA WA MAWASILIANO KATA YA IKONDO.Serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania imesema kuwa ipo ...
02/11/2024

SERIKALI KUANZA UJENZI WA MNARA WA MAWASILIANO KATA YA IKONDO.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania imesema kuwa ipo katika hatua za Mwisho kujenga mnara wa Mawasiliano katika kata ya Ikondo ili kuiondoa changamoto za Mawasiliano katika kata hiyo na Maeneo Jirani ndani ya Jimbo la Lupembe.

Serikali imesema hayo kufuatia Swali la Mbunge wa Lupembe Mh Edwin Enosy Swalle alipohoji na kutaka Kufahamu nilini Serikali itajenga mnara wa Mawasiliano ili kupunguza Changamoto hiyo kwa Wananchi Wanaotoka katika Vijiji vya Nyave,Idyadya,Itova,na Vijiji Vingine katika eneo hilo ikiwemo Ikondo Swali ambalo limejibiwa na Naibu Waziri wa Maji kwa Niaba ya Waziri wa Habari ambapo amesema kuwa Serikali imeshafanya hatua zote ili kuanza Ujenzi wa Mnara wa Mawasiliano katika eneo hilo huku akisema kuwa tayari Wakanadarasi Wameshafika site na Wapo tayari kuanza Ujenzi wa Mnara wa mawasiliano katika kata ya Ikondo.

"Kwanza kabisa nianze kwa Kumpongeza Advocate Edwin Enosy Swalle Mbunge wa Lupembe kwa kazi kubwa na kwa namna anavyowapigania Wananchi wa Jimbo lake la Lupembe na ambayo amepambania kuhusu hii kata ya Ikondo lakini bahati nzuri na Salamu Njema kwako na Wananchi wako ni kwamba leo baada ya kuwa nimepatiwa taarifa na Mh Waziri wa Habari Mh Jerry William Silaa ni kwamba kata ya Ikondo Wakandarasi Wameshafika Site na Wako tayari kuanza kujenga mnara wa Mawasiliano katika eneo hilo.Mh. Eng.Kundo Andrea Mathew Naibu Waziri wa Maji akijibu Swali la Mbunge Wa Lupembe kwa Niaba ya Waziri wa Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

19/10/2024
Mwenyekiti Wa UWT Wilaya ya Njombe Beatrice Malekela amewataka Wanawake wa Wilaya ya Njombe kuwa mstari wa Mbele katika ...
19/10/2024

Mwenyekiti Wa UWT Wilaya ya Njombe Beatrice Malekela amewataka Wanawake wa Wilaya ya Njombe kuwa mstari wa Mbele katika zoezi la kujiandikisha katika Daftari la Mkazi ili ukifika mda wa kuchagua viongozi wa Serikali za mitaa na Vijiji Waweze kutumia fursa hiyo kuchagua Viongozi wao pamoja na Kuchaguliwa kuwa Viongozi wa Serikali za Vijiji na miitaa ikiwa Wanasifa za kugombea.

Ikiwa zoezi  la Wananchi kujiandikisha katika Daftari la Mkazi linaendelea kote Nchini ambapo linatarajiwa kukamilika ha...
19/10/2024

Ikiwa zoezi la Wananchi kujiandikisha katika Daftari la Mkazi linaendelea kote Nchini ambapo linatarajiwa kukamilika hapo October 20 mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Njombe Neema Mgaya amewataka Wananchi wa Mkoa wa Njombe kuhakikisha Wanajiandikisha katika Daftari la Mkazi katika maeneo yao ili kupata fursa mhimu ya kuwachagua Viongozi watakao waongoza kwa miaka mitano ijayo

Mbunge wa Jimbo la Lupembe Mheshimiwa  Edwin Enosy Swalle amekabidhi tofari  3500 kwaajiri ya ujenzi  wa Ofisi ya chama ...
19/10/2024

Mbunge wa Jimbo la Lupembe Mheshimiwa Edwin Enosy Swalle amekabidhi tofari 3500 kwaajiri ya ujenzi wa Ofisi ya chama cha Mapinduzi kata ya Igongolo ambapo amesema kuwa k**a Mbunge wa Jimbo la Lupemnbe atahakikisha anashiriki kikamilifu katika shughuli mbalimbali za chama kuanzia ngazi za Matawi mpaka.

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Antony Mtaka hii leo  amezindua Rasmi Zoezi la Wananchi  kujiandikisha kwenye Daftari la kudumu l...
11/10/2024

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Antony Mtaka hii leo amezindua Rasmi Zoezi la Wananchi kujiandikisha kwenye Daftari la kudumu la Mpiga kura katika Ofisi za Mtaa wa Lunyanywi Halmashauri ya Mji wa Njombe ambapo amewataka Wananchi katika mkoa huo kutumia fursa hii mhimu ya kujiandikisha ili Wapate Fursa ya kuwachagua viongozi wanaowataka.

Wakati Walimu nchini Tanzania wakiadhimisha Siku ya Walimu Duniani Serikali Nchini Tanzania imesema kuwa inaendelea kush...
05/10/2024

Wakati Walimu nchini Tanzania wakiadhimisha Siku ya Walimu Duniani Serikali Nchini Tanzania imesema kuwa inaendelea kushughulikia Changamoto mbalimbali zinazowakabiri Waalimu ili kuhakikisha Wanafanya kazi katika Mazingira Wezeshi na Mazingira Rafiki.

Serikali imetoa Kauli hiyo mapema leo kupitia kwa Waziri wa Elimu Pro Aldof Mkenda alipozungumza na Waandishi wa habari ambapo amesema kuwa Serikali inaheshimu na kuthamini mchango wa Walimu hapa Nchini hivyo itaendelea kushughulikia madai mbalimbali ya Walimu ili kuhakikisha Wanafanya kazi kwa Weredi.

Aidha amesema kuwa Serikali ya awamu ya sita inayoonhozwa na Rais Samia imeendelea kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia ikiwemo Ujenzi wa Madarasa kupitia fedha za Boost pamoja na Sequip ambapo amesema kuwa Ukamilishwaji wa Miradi hiyo unawafanya Walimu kupata mazingira mazuri ya kutekeleza majukumu yao.

Aidha Waziri wa Elimu amesema kuwa Serikali iko katika Mpango wa kuandaa Mwongozo wa Utoaji Motisha kwa Walimu ili kuongeza ufanisi katika utendaji wa Walimu hapa Nchini.
Baadhi ya Walimu Waliozungumza na Kituo hiki wamesema kuwa kwa miaka ya hivi karibuni eameshuhudia Serikalini ikijibu kwa vitendo baadhi ya changamoto zao hivyo wanaipongeza Serikali ya awamu ya sita kwa kuboresha miundombinu pamona na kuwa kiungo mhimu katika kutatua changamoto zao.

Mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Njombe Neema Mgaya amewataka Wananchi wa Kata ya Uwemba kuhakikisha Wanajiandaa na Uchagu...
30/09/2024

Mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Njombe Neema Mgaya amewataka Wananchi wa Kata ya Uwemba kuhakikisha Wanajiandaa na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambao unatatraji kufanyika siku chache zijazo.

Mbunge huyo ametoa hamasa hiyo kwa Wananchi wa kata ya uwemba akiwa katika Kijiji cha Ikisa Halmashauri ya Mji wa Njombe ambapo amesema kuwa uchaguzi ni tukio mhimu kwa Wananchi na Serikali hivyo ni mhimu wakajitokeza kujiandikisha ili wapate fursa ya kuwachagua Viongozi wanaowataka lakini pia na wao kupata Fursa Ya kuchaguliwa.

"Ndugu zangu Wananchi wa Ikisa Rais Wetu Samia Suluhu Hassan amekuwa akiweka kipaumbele sekta hii ya afya na ndio maana ...
30/09/2024

"Ndugu zangu Wananchi wa Ikisa Rais Wetu Samia Suluhu Hassan amekuwa akiweka kipaumbele sekta hii ya afya na ndio maana Mtaona anajenga zahanati,Vituo vya afya kila mahali Hapa Nchini lakini pia analeta Vifaa tiba pamoja na Watumishi, hivyo sisi wasaidizi wake tupo kwaajiri ya kumsaidia na ndio maaana leo nimekuja kuwaona ndugu zangu lakini sijaja mikono mitupu nimeleta Mashuka ili mkija kupata Matibabu mjifunike na Mpate huduma bora kutoka Kwa Wataalamu wetu"Neema Mgaya Mbunge Viti maalumu Mkoa wa Njombe.

Address

Njombe

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Digital News Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share