Radio Free Africa

Radio Free Africa Ukurasa Rasmi wa Radio Free Africa
Tunasikika Nchi Nzima & Kimataifa. Mawasiliano Kutangaza Nasi
📞 +255 625 991 764
📞 +255 718 292 838
(448)

Radio yenye Makao Makuu Jijini Mwanza Tanzania na kusikika katika Mikoa Mbalimbali kupitia Masafa ya FM, Masafa ya Kati 1377 ,Mtandao na Kupitia Ving'amuzi/Visimbuzi mbalimbali. Kazi yake k**a ulivyo wajibu wa vyombo vya Habari, Kuhabarisha, kuelimisha, Kuburudisha.

24/02/2025

Kuelekea maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambayo kitaifa itafanyika Mkoani Arusha mtandao wa Polisi wanawake Arusha umeeleza ulivyojipanga kuimarisha ulinzi, kutoa elimu na kutembelea vituo vya wahitaji pamoja na kuunga Juhudi za Mheshimiwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kutangaza vivutio vya utalii hapa nchini.

Akitoa taarifa hiyo afisa mnadhimu namba moja Mkoa wa Arusha ambaye pia ni mwenyekiti wa Mtandao wa Polisi wanawake Mkoa wa Arusha Kamishina msaidizi wa Polisi ACP Debora Lukololo, amesema kuwa askari wa k**e Mkoa wa Arusha kwa kishirikiana na askari wa k**e mikoa mingine wamejipanga kuimarisha ulinzi kabla na baada ya shereke za maazimisho ya siku ya wanawake duniani ambayo shamrashamra zake zitaanza Machi 01,2025 hadi 08 Mkoani humo.

Ameongeza kuwa maadhimisho hayo yataenda sambamba na utoaji wa elimu, misaada mbalimbali na kutembelea hifadhi za taifa ambapo amewaomba wageni na washiriki wengine kutambua kuwa mtandao wa Polisi wanawake umejipanga vyema kuimarisha ulinzi na Usalama wakati wote wa maadhimisho hayo.

ACP Lukololo amebainisha kuwa katika maadhisho hayo litakuwepo banda maalum la Polisi ambalo litakuwa na wataalamu mbalimbali wa Jeshi hilo watakaosililiza na kutakua changamoto za wananchi huku akitumia fulsa hiyo kuwaomba wananchi wenye changamoto katika masuala ya utalii kufika katika kituo Cha Polisi Cha Diplomasia na Utalii ambacho kinahusika na maswala yote ya Diplomasia na Utalii.

Kwa upande wake Mkuu wa Kikosi cha usalama Barabarani Mkoa wa Arusha Mrakibu Mwandamizi wa Polisi SSP Zauda Mohamed akaweka Wazi mikakati ya Kikosi cha usalama Barabarani kuelekea maadhimisho hayo ya siku ya wanawake duniani ambapo amesema kuwa wamejipanga vyema kuimarisha usalama Barabarani na kutoa elimu kupitia Banda maaalum ambalo litakuwepo katika maadhimisho hayo.

Mkuu wa dawati la Jinsia na watoto Mkoa wa Arusha Mrakibu wa Polisi SP Happness Temu akabainisha kuwa watatumia fursa hiyo ya siku ya wanawake duniania kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya ukatili wa kijinsia.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Serikali inaendelea kubuni mbinu mbalimba...
24/02/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Serikali inaendelea kubuni mbinu mbalimbali za kukabiliana na wanyamapori wakali na waharibifu huku akiiielekeza Wizara ya Maliasili na Utalii kuangalia namna ya kupitia upya kanuni za malipo ya kifuta jasho/machozi.

Ameyasema hayo leo Februari 24,2025 katika ziara alipokuwa akizungumza na wananchi kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto Mkoani Tanga

"Tunaendelea kuongeza Askari Wanyamapori na kubuni mbinu mbalimbali za kufukuza wanyama ikiwemo kutumia ndegenyuki(drones)" Rais Samia amesisitiza.

Mkutano huo umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali wakiwemo Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb), Naibu Waziri, Mhe. Dunstan Kitandula (Mb), Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi pamoja na baadhi ya Watendaji kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii na Taasisi zake.

24/02/2025

“Tanga oyeee!, Korogwe safi?. Niwakumbushe kwamba ile homa yetu ya kila miaka mitano joto linaanza kupanda. Na diyo maana mnasikia wengine wanasema huko, lakini niwakumbushe kile kijambo chetu cha mwezi wa kumi mwaka huu, k**a jina lako halipo kwenye daftari la wapiga kura hutoweza kupata ile haki. Sasa k**a unafurahia maendeleo na miradi inayoletwa Korogwe hakikisha umejiandikisha kwenye daftari na siku ikifika umetoka kwenda kupiga kura,”

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

24/02/2025

“Ndugu zangu wa Korogwe nimekagua ujenzi wa bwawa la umwagiliaji na kuweka jiwe la msingi baada ya kuridhishwa na maendeleo ya bwawa lile. Mradi huu utanufaisha wananchi Zaidi ya 20,000 katika kata saba na vijiji 28. Wakulima sasa watalima bila kutegemea mvua. Ukivuna utasikiliza ushauri wa maafisa kilimo unaendelea kulima kitu kingine au unapanda mazao mengine lakini mradi ndani ya mwaka utavuna mara mbili au mara tatu inategemea utakachokilima,”

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

24/02/2025

“Wanatanga kwa kweli toka jana mimi sina la kusema. Inaonesha kabisa mlikuwa na hamu ya ziara hii, kwa sababu kila ninapokanyaga umati ni mwingi kwelikweli. Nafurahi kuzungumza nanyi katika uwanja huu, uwanja wa chuo cha waalimu. Ni baraka kuwepo hapa kwa sababu mi mwenzenu walimu nawapenda sana,”

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

24/02/2025

“Nikiwa naendelea na ziara yangu mkoani Tanga. Leo ni siku ya wilaya ya Lushoto na wilaya ya Korogwe. Kwa hiyo nipo kwenye wilaya mbili. Na ndio maana mnasikia watu wanaambiwa muda mdogo nendeni haraka. Lakini niseme kabla sikuendelea na hotuba yangu, kwanza niwape wana Lushoto maua yenu kwenye utunzaji wa mazingira. Nataka niwaambie kweli, ukiingia Lushoto hata uvutaji wa hewa unakuwa mwepesi zaidi,”

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

24/02/2025

“Ndugu zangu namshukuru Mungu. Namshukuru Mungu kwa kunifikisha Mkomazi. Lakini kilichonivuta kuja k**a alivyosema Mheshimiwa Waziri nimetoa fedha nyingi sana za ujenzi wa Bwawa hili. Kwa hiyo nikaona nije niangalie yaliyopo. Na k**a yanaendelea lakini nataka kuwaambia nimeridhika na niwatakie kazi njema. Sasa ndugu zangu k**a alivyosema Waziri kwamba kuna mawazo ya siku nyingi ya kujenga mabwawa ya aina hii. Kuna hili la Mkomazi na jingine lipo kule karibu na Dar es Salaam linaitwa Kidunda,”

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

24/02/2025

“Barabara hii mwanangu January amekuwa akiililia sana. Soni, Bumbuli, Korogqwe. Akiililia sana. Na baada ya kusikia kilio chake. Nikasema basi itangazeni. Nataka niwaambie tarehe 6 mwezi ujao tunafungua tenda kutafuta mkandarasi na barabara itaanza kujengwa. Tunakwenda kujenga kilomita 22,”

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

24/02/2025

“Wanyama waharibifu wanaoingia kwenye mashamba ya watu ni changamoto kubwa. Pia nataka nikwambie kwamba serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali kwa ajili ya kuwalinda wananchi ikiwemo kuongeza askari wanyama pori na kubuni mbinu mbalimbali za kufukuza wanyama ikiwemo matumizi ya hizi drone,”

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Katika jitihada za kuimarisha uwezo wa utoaji wa huduma za dharura wakati wa mlipuko wa Ugonjwa wa Marburg, Wizara ya Af...
24/02/2025

Katika jitihada za kuimarisha uwezo wa utoaji wa huduma za dharura wakati wa mlipuko wa Ugonjwa wa Marburg, Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Chama cha Madaktari wa Magonjwa ya Dharura Tanzania (EMAT) imeendesha mafunzo maalum kwa watumishi wa afya waliopo mstari wa mbele katika Hospitali ya Wilaya ya Biharamulo.

Mafunzo haya ya siku tano yamehusisha watumishi waliopo kwenye kambi ya Marburg, wakipewa elimu ya kina, ujuzi wa kitabibu, na mbinu za kisasa za utambuzi, matibabu, na udhibiti wa maambukizi ya ugonjwa huu hatari. Lengo kuu la mafunzo haya ni kuhakikisha watumishi wa afya wanaimarisha utayari wa kukabiliana na dharura zinazotokana na Marburg na kuongeza ufanisi wa huduma kwa wagonjwa au wanaohisiwa kuwa na maambukizi.

Akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mafunzo hayo, Mkuu wa Timu ya Matibabu, Dkt. Michael Kiremeji, alieleza kuwa mafunzo haya ni nyenzo muhimu katika juhudi za kuzuia kuenea kwa ugonjwa huo.

"Mafunzo haya yanalenga kuhakikisha wahudumu wa afya wanakuwa na ujuzi wa hali ya juu wa kushughulikia wagonjwa wa Marburg kwa haraka, kupunguza hatari ya maambukizi katika vituo vya afya, na kulinda jamii dhidi ya mlipuko wa ugonjwa huu," alisema Dkt. Kiremeji.

Serikali inaendelea kuwekeza katika ujenzi wa mifumo madhubuti ya udhibiti wa magonjwa ya mlipuko, ikiwemo kutoa mafunzo kwa watumishi wa afya, kuimarisha upatikanaji wa vifaa tiba, na kuelimisha jamii kuhusu tahadhari dhidi ya Marburg.


Cc

 Leo anatuhusu kwenye     HOSTED BY  @vio_de_navigatorMusic :dj_bonny255Gfx by   💪🏿🔥🔥24.2.2025 📻
24/02/2025

Leo anatuhusu kwenye
HOSTED BY @vio_de_navigator
Music :dj_bonny255
Gfx by
💪🏿🔥🔥
24.2.2025

📻

24/02/2025

🙌🙌🔥🔥🔥😂😂😂🔥🔥🔥8&9 Machi Furahisha itatapikaaaaaa😂😂🔥🔥🔥 *Chief Hangaya Utamaduni Festival 2025*🔥

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika matukio tofautitofauti wakati wa hafla ya U...
24/02/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika matukio tofautitofauti wakati wa hafla ya Uzinduzi wa jengo la Halmashauri ya Bumbuli Mkoani Tanga ikiwa ni sehemu ya Ziara ya kikazi Mkoani humo leo Februari 24, 2025.

23/02/2025

"Nimejuzwa kwamba Hospitali ile mpaka sasa imeshapokea wajawazito 900, ambao 300 kati yao walijifungua kwa operation. Sasa tufikirie tusingekuwa na hospitali ile 300 hawa wangekimbizwa nadhani Tanga Mjini au Hospitali ya Mkoa ya karibu k**a ipo, lakini nadhani wangekwenda Tanga Mjini. Sasa 300 hawa si wote, wasingefika hospitali. Wengine tungewapoteza njiani,"

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

23/02/2025

"Hospitali ile tumeona maendeleo yake, tumeona ilivyo kamilika. Lakini kwa sababu hospitali ile iko barabarani si mbali na barabarani. Na tukiweka lami kipande kinachotoka barabarani na hospitali patakuwa karibu mno. Kwa hiyo tumeamua kujenga sasa eneo la kutibu au kupasua mifupa. Na kwa maana hiyo namuelekeza Waziri wa Tamisemi alete hapa fedha milioni 240 ili kujenga sasa eneo la mifupa,"

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

23/02/2025

"Serikali yenu imeiangalia kwa jicho la karibu sana mkoa wa Tanga. Serikali imeleta trilioni 3.1 k**a alivyosema mkuu wa mkoa kwa shughuli mbalimbali za kimaendeleo. Sasa kuja kwangu leo ni kuja kuangalia kazi iliyofanywa na fedha hii iliyokuja Tanga,"

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alipowasili Uwanja wa Shule ya Msingi Mkata Mashar...
23/02/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alipowasili Uwanja wa Shule ya Msingi Mkata Mashariki kwenye Mkutano wa hadhara na Wananchi wa Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga ikiwa ni Siku ya kwanza ya ziara Mkoani humo leo February 23, 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Matukio tofautitofauti na viongozi mbalimba...
23/02/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Matukio tofautitofauti na viongozi mbalimbali aliposhiriki Mashindano ya Dunia ya Quran Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Benjamin Mkapa Dar es Salaam leo Februari 23, 2025.

Address

7-C, Ilemela Industrial Area, Airport Road
Mwanza
POBOX1732

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio Free Africa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Radio Free Africa:

Videos

Share