Radio Free Africa

Radio Free Africa Ukurasa Rasmi wa Radio Free Africa
Tunasikika Nchi Nzima & Kimataifa. Kazi yake k**a ulivyo wajibu wa vyombo vya Habari, Kuhabarisha, kuelimisha, Kuburudisha.
(449)

Radio yenye Makao Makuu Jijini Mwanza Tanzania na kusikika katika Mikoa Mbalimbali kupitia Masafa ya FM, Masafa ya Kati 1377 ,Mtandao na Kupitia Ving'amuzi/Visimbuzi mbalimbali.

"Kwa niaba ya Marekani, namtakia heri Rais Samia Suluhu Hassan na Watanzania katika kuadhimisha miaka 61 ya kuundwa kwa ...
26/04/2025

"Kwa niaba ya Marekani, namtakia heri Rais Samia Suluhu Hassan na Watanzania katika kuadhimisha miaka 61 ya kuundwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Marekani inathamini sana ushirikiano wetu wa kudumu na Tanzania, ambao unatokana na tamaa yetu ya pamoja ya ustawi na usalama. Katika mwaka ujao, tunatarajia kuimarisha ushirikiano wetu kwenye biashara na uwekezaji kwa manufaa ya pande zote mbili za watu wa Marekani na Tanzania.

Katika siku hii ya miaka 61 ya Muungano, tunaupongeza uongozi wa Tanzania katika Afrika Mashariki na kuthibitisha dhamira yetu ya kujenga dunia yenye amani na ustawi zaidi.

Kwa niaba ya Marekani, namtakia kila la heri Rais Samia Suluhu Hassan na Watanzania katika kuadhimisha miaka 61 ya kuundwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Marekani inathamini sana ushirikiano wetu wa kudumu na Tanzania, ambao unatokana na tamaa yetu ya pamoja ya ustawi na usalama. Katika mwaka ujao, tunatarajia kuimarisha ushirikiano wetu kwenye biashara na uwekezaji kwa manufaa ya pande zote mbili za watu wa Marekani na Tanzania.

Katika siku hii ya miaka 61 ya Muungano, tunaupongeza uongozi wa Tanzania katika Afrika Mashariki na kuthibitisha dhamira yetu ya kujenga dunia yenye amani na ustawi zaidi," Marco Rubio, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ameiwakilisha Tanzania kwenye Maziko ya aliyek...
26/04/2025

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ameiwakilisha Tanzania kwenye Maziko ya aliyekuwa Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki Duniani hayati Baba Mtakatifu Francisko yanayofanyika tarehe 26 Aprili 2025 Vatican.

26/04/2025

SHOWTIME MUSIC CHART FRIDAY  25..4.20252pm-4pm Hosted by   dj_bonny255 Artwork by Artist: ๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡@phynofino@jidejaydee       ...
25/04/2025

SHOWTIME MUSIC CHART FRIDAY
25..4.2025
2pm-4pm


Hosted by

dj_bonny255
Artwork by
Artist: ๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡

@phynofino@jidejaydee @mabantutwaha
๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ“ป

๐Ÿ“ป

Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) imepongezwa kwa utekelezaji mzuri wa miradi ya maendeleo ya elimu kupitia Mfuko wa Elimu...
25/04/2025

Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) imepongezwa kwa utekelezaji mzuri wa miradi ya maendeleo ya elimu kupitia Mfuko wa Elimu wa Taifa pamoja na Mfuko wa Kuendeleza Ujuzi (SDF).

Pongezi hizo zimetolewa leo na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bw. Methusela Ntonda, alipotembelea banda la TEA katika ufunguzi wa Maonesho ya Kitaifa ya Kazi za Utamaduni na Sanaa yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Jijini Dar es Salaam.

Akiwa kwenye banda hilo, Ntonda alipata fursa ya kujionea shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na TEA, zikiwemo taarifa za miradi ya elimu na Mfuko wa Kuendeleza Ujuzi, pamoja na bidhaa zilizotengenezwa na mmoja wa wanufaika aliyepata ufadhili wa kusomea Mafunzo ya Kuendeleza Ujuzi.

Aidha, Ntonda amesema amevutiwa na juhudi za Mamlaka hiyo katika kuboresha miundombinu ya kujifunzia na kufundishia, sambamba na uwezeshaji uliotolewa kwa Watanzania kupitia ufadhili wa mafunzo ya ujuzi.

Bw. Ntonda aliipongeza TEA na kusema uwekezaji uliofanywa kupitia mifuko yote miwili una mchango mkubwa katika kuleta maendeleo ya sekta ya elimu na kukuza maarifa kwa wananchi, hasa vijana. Alisisitiza umuhimu wa kuendeleza jitihada hizo kwa kushirikisha wadau mbalimbali ili kuhakikisha elimu bora na fursa za ujuzi zinapatikana kwa watu wengi zaidi nchini.

Awali, akitoa utambulisho wa Mamlaka hiyo, Afisa Uhusiano na Mawasiliano wa TEA, Bi. Eliafile Solla alisema, TEA ilianzishwa kwa lengo la kusimamia Mfuko wa Elimu wa Taifa, ambapo majukumu yake makuu ni kutafuta rasilimali fedha kutoka kwa wadau wa ndani na nje ya nchi, pamoja na kuzitumia kusaidia juhudi za Serikali katika kuboresha miundombinu ya elimu nchini. Aliongeza kuwa TEA pia ina jukumu la kuratibu na kusimamia utekelezaji wa miradi ya uendelezaji ujuzi kupitia Mfuko wa SDF.

โ€Ž"Siko tayari kuzungumza chochote kwa sasa, kwa kuwa kila kitu kipo chini ya uongozi, nimeomba kwenda nyumbani nina masu...
25/04/2025

โ€Ž"Siko tayari kuzungumza chochote kwa sasa, kwa kuwa kila kitu kipo chini ya uongozi, nimeomba kwenda nyumbani nina masuala binafsi ya kifamilia."
โ€Ž
โ€ŽJohn Noble_Kipa Fountain Gate
โ€Ž
โ€ŽIkumbukwe nyota huyo raia wa Nigeria ambaye leo amekutana uso kwa uso Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere na Mwandishi wa Redio Free Africa, Mareges Nyamaka ni amesimamishwa kwa muda usiojulikana na uongozi wake wa FG ikiwa ni baada ya saa chache mchezo wa FG dhidi ya Yanga SC Kutamatika Uwanja wa Kwaraa, Manyara wenyeji FG wakichapika 4-0



๐Ÿ–Š๏ธ

K**a unatutegea sikio basi maoni Yako ni Sehemu muhimu ya kipindi cha michezo na Burudani Karibu sanaCc
25/04/2025

K**a unatutegea sikio basi maoni Yako ni Sehemu muhimu ya kipindi cha michezo na Burudani

Karibu sana

Cc

Idara ya Uhamiaji Nchini imefanya ukaguzi maalum nchi nzima kwa kipindi cha miezi minne kuanzia Januari hadi Aprili, 202...
25/04/2025

Idara ya Uhamiaji Nchini imefanya ukaguzi maalum nchi nzima kwa kipindi cha miezi minne kuanzia Januari hadi Aprili, 2025 kwa lengo la kuwachukulia hatua za kisheria raia wa kigeni ambao wanaishi nchini bila kuwa na vibali au kufanya kazi/biashara kinyume cha masharti ya vibali vyao.

Taarifa ya leo Aprili 24, 2025 iliyotolewa na Msemaji wa Idara hiyo, SSI. Paul J. Mselle imeeleza kuwa kupitia zoezi hilo, Idara imefanikiwa kuwak**ata jumla ya raia wa kigeni 7,069 kutoka katika mataifa tofauti na hatua mbalimbali zimechukuliwa dhidi yao ambapo raia 1,008 wamefikishwa Mahak**ani huku kati yao 703 wakihukumiwa kifungo gerezani, 257 wamehalalisha ukaazi wao na watuhumiwa 4,796 wameondoshwa nchini wakati watuhumiwa wengine 305 uchunguzi bado ukiendelea.

Taarifa hiyo inaeleza kwamba, Idara ya Uhamiaji kwa ushirikiano na Vyombo vingine vya Usalama wamefanya ukaguzi maalum katika eneo la Kariakoo ambapo jumla ya raia wa kigeni 62 kutoka katika mataifa mbalimbali wamek**atwa na kuondoshwa nchini kwa kosa la kuishi na kufanya biashara bila ya kuwa na vibali na baadhi yao kukiuka masharti yaliyoanishwa katika vibali vyao vya biashara.

Idara ya Uhamiaji imetoa wito kwa raia wa kigeni kuzingatia matakwa ya masharti ya vibali vyao ili kuepuka hatua za kisheria au usumbufu unaoweza kujitokeza wakati huu zoezi la ukaguzi likiendelea.

Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu imepanga kutoa uamuzi kwa njia ya mtandao April 28, 2025 kuhusu hoja za pingamizi za Maw...
24/04/2025

Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu imepanga kutoa uamuzi kwa njia ya mtandao April 28, 2025 kuhusu hoja za pingamizi za Mawakili wa utetezi katika kesi ya uchochezi inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo ndugu, Tundu Lissu.

Kesi imesikilizwa leo kwa njia ya mtandao mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Godfrey Mhini ambapo upande wa Jamhuri kupitia Wakili wa Serikali Mwandamizi, Job Mrema umesema kesi hiyo imeitishwa kwa ajili ya Lissu kusomewa Maelezo ya Awali.

Upande wa Jamhuri kupitia Wakili Mrema ulipouliza kuhusu Mshtakiwa Lissu kuto onekana mtandaoni, Hakimu Mhini alimtaka Askari Magereza ajibu ambapo alisema kwamba Lissu amegoma kusomewa maelezo ya awali kwa njia ya mtandao (visual) ambapo Hakimu Mhini alirihusu kesi kuendelea pasipo Lissu kuonekana.

Kutokana na hatua hiyo, Hakimu Mhini ameahirisha kesi hiyo hadi April 28, 2025 kwa ajili ya kutoa uamuzi wa mapingamizi hayo ya utetezi kwa njia ya mtandao ili kuona k**a kesi hiyo isikilizwe kwa mtandao ama mshatkiwa afikishwe Mahak**ani.

Matokeo ya Sensa ya watu na Makazi ya mwaka 2022, inaonesha kuwa 51% ya watanzania ni wanawake na hivyo kuthibitisha umu...
24/04/2025

Matokeo ya Sensa ya watu na Makazi ya mwaka 2022, inaonesha kuwa 51% ya watanzania ni wanawake na hivyo kuthibitisha umuhimu wao katika maendeleo ya Taifa.

Hata hivyo, kutokana na sababu za kihistoria, wanawake bado wamekuwa katika nafasi za chini kijamii na kiuchumi jambo lililosababisha kuanzishwa kwa Mkakati wa Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi.

Kwa wanawake wanaofanya biashara, changamoto kubwa ni mitaji midogo isiyojitosheleza, matumizi ya nyenzo duni, ujuzi mdogo, masoko kwa bidhaa zao, mila kandamizi na kukosa dhamana inayoweza kuwasaidia kupata mikopo ili kuondokana na changamoto zao.

Kwa kuliona hilo Benki ya TCB k**a mdau mkubwa wa Jukwaa la Uwezeshaji wanawake Kiuchumi wamekuletea akaunti ya 'TABASAMU' maalum kwa wanawake ambayo inapatikana Benki ya TCB pekee.

Pichani ni wawakilishi wa TCB Bank akiwemo Sarah Mwambeje (aliyekaa mbele kushoto) ambae ni Mkufunzi Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi kutoka TCB, Edward Mwoleka Meneja kutoka TCB bank (aliyesimama wa tatu kutoka kushoto).

Wengine ni Naziru Saidi Mtaalamu wa masuala ya Bima (aliyesimama wa kwanza kutoka kushoto) walipokutana na timu ya Sahara Media Group Ltd yenye vituo vya Star tv, Radio Free Africa na Kiss fm ofisi za Dar es salaam chini ya Bureau Chief na Mhariri Michael Noel (aliyesimama wa tatu kutoka kulia) baada ya kujadili namna taasisi hizo zinavyoweza kushirikiana huku Farida Njiku Afisa Masoko akiteuliwa kuwa balozi wa akaunti ya Tabasamu ndani ya Sahara Media Group Ltd.

Wananchi wa Kijiji Cha  Omukakajinja katika Wilaya ya Karagwe mkoani Kagera wakipewa  elimu ya masuala Mbalimbali ya kis...
24/04/2025

Wananchi wa Kijiji Cha Omukakajinja katika Wilaya ya Karagwe mkoani Kagera wakipewa elimu ya masuala Mbalimbali ya kisheria inayotolewa na timu ya wataalamu wa kampeni ya msaada wa kisheria ya MAMA SAMIA inayoendelea kutolewa katika vijiji vya Wilaya hiyo ya Karagwe

Mada zilizowasilishwa na wataalamu hao ni umuhimu wa kuandika wosia,ndoa pamoja na sheria ya ardhi.

Mratibu wa kampeni hiyo ya msaada wa kisheria ya MAMA SAMIA katika wilaya ya Karagwe Gaudensia Mdaki amesema kuwa wamekutana na migogoro mingi ya ardhi na hivyo kuwataka wananchi kufuata Sheria na taratibu za umiliki wa ardhi.

Tunayapa kipaumbele maoni yako unapotusikilzia na kuchangia Jambo lililokugusa Kwenye saa 2 za michezo na Burudani saa 2...
24/04/2025

Tunayapa kipaumbele maoni yako unapotusikilzia na kuchangia Jambo lililokugusa Kwenye saa 2 za michezo na Burudani saa 2 Hadi 4 asubuhi

Cc

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ameipa Simba sapoti ya usafiri wa kwenda Afrika Kusini na ...
23/04/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ameipa Simba sapoti ya usafiri wa kwenda Afrika Kusini na kugharamia malazi kwa timu hiyo katika kipindi chote itakapokuwa huko kwa ajili ya mechi ya marudiano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika dhidi ya Stellenbosch, Aprili 27, 2025.

Mechi hiyo ni ya marudiano ya hatua ya nusu fainali baada ya kwanza iliyofanyika kwenye Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar kumalizika kwa ushindi wa Simba wa bao 1-0.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba, Mohammed Dewji amethibitisha Rais Samia kutoa sapoti hiyo huku akitoa shukrani za klabu hiyo.

โ€œKwa niaba ya Klabu ya Simba Sports Club, napenda kutoa shukrani za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kwa kuiwezesha klabu yetu kushiriki mashindano ya kimataifa.

โ€œTumepokea kwa moyo wa shukrani mchango wa malazi na usafiri kwa ajili ya mchezo wetu wa marudiano wa nusu fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Stellenbosch.

โ€œKlabu ya Simba inatambua na kuthamini kwa dhati juhudi za Rais Samia katika kumarisha sekta ya michezo hapa nchini, hususan mpira wa miguu,โ€ amesema Dewji.

Makamu Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania, CHADEMA, John Heche, amek**atwa leo na Jeshi la Polisi ka...
23/04/2025

Makamu Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania, CHADEMA, John Heche, amek**atwa leo na Jeshi la Polisi katika eneo la Kariakoo, jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka CHADEMA, Heche alikuwa amekwenda kuongoza mkutano wa hadhara ambao tayari ulitangazwa na taarifa yake kuwasilishwa kwa Polisi siku kadhaa zilizopita.

Hata hivyo, Polisi walileta barua saa chache kabla ya mkutano kuanza, wakipinga kufanyika kwake kwa madai kuwa eneo la mkutano Mtaa wa Nyamwezi na Mkunguni lina shughuli nyingi za biashara na mkutano huo ungeathiri shughuli hizo.

"tunashauri mkutano wenu huo wa hadhara ufanyike katika eneo lingine la wazi", ilisema barua ya Polisi kwenda CHADEMA.

Licha ya zuio hilo, Heche alifika eneo la mkutano, ambapo Polisi walimk**ata na kuondoka naye. Taarifa zaidi kuhusu mahali alipo bado zinafuatiliwa na chama hicho.

Mjumbe wa K**ati Kuu ya CHADEMA, Godbless Lema, amethibitisha kuk**atwa kwa Heche kupitia ukurasa wake wa mtandao wa X (zamani Twitter), ingawa Jeshi la Polisi halijatoa taarifa rasmi hadi sasa.

"Taarifa ya Mkutano ilipekekwa Wiki Moja Iliyopita na Mkutano ulianza kutangazwa. Leo Mchana Polisi wameleta barua kuzuia mkutano kufanyika Kariakoo", aliandika Lema.

Kuk**atwa kwa Heche kunakuja wiki chache baada ya Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, kuk**atwa na kufikishwa mahak**ani kwa tuhuma za uhaini mashtaka ambayo hayana dhamana.

Lissu anatarajiwa kufikishwa tena Mahak**a ya Kisutu tarehe 24 Aprili, 2025, ambapo Heche amekuwa akihamasisha wafuasi wa CHADEMA kujitokeza kwa wingi.

Matukio haya yamezua hofu na mijadala mikali kutoka kwa wananchi na viongozi wa dini, wakitaka kuwepo kwa maridhiano ya kitaifa na utulivu wa kisiasa.

Katika kipindi hiki, CHADEMA inaendelea na kampeni yake ya โ€œNo Reform, No Electionโ€, ikisisitiza kuwa hakutakuwa na ushiriki katika uchaguzi wowote bila kufanyika kwa mabadiliko makubwa ya kisiasa na kisheria.

LEO  yupo ๐Ÿ‘‡   HOSTED BY  @vio_de_navigatorMusic :dj_bonny255Gfx by   ๐Ÿ’ช๐Ÿฟ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ22.4 2025 Tuesday ๐Ÿ“ป ๐Ÿ“ป
22/04/2025

LEO yupo ๐Ÿ‘‡
HOSTED BY @vio_de_navigator
Music :dj_bonny255
Gfx by
๐Ÿ’ช๐Ÿฟ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ
22.4 2025 Tuesday

๐Ÿ“ป ๐Ÿ“ป

Matokeo ya droo ya LOTTO na LOTTO PLUS 1 tarehe 21/04/2025.LOTTO: 04, 18, 34, 37, 40, 48Mpira wa Bonasi: 16LOTTO PLUS 1:...
22/04/2025

Matokeo ya droo ya LOTTO na LOTTO PLUS 1 tarehe 21/04/2025.

LOTTO: 04, 18, 34, 37, 40, 48
Mpira wa Bonasi: 16
LOTTO PLUS 1: 02, 03, 06, 36, 38, 49
Mpira wa Bonasi: 30

HONGERA kwa Washindi wote!
Angalia tiketi yako sasa!



Askofu wa Jimbo Katoliki Ifakara, Mhashamu Sulutaris Libena amewataka Watanzania kulinda na kudumisha amani na kuzingati...
20/04/2025

Askofu wa Jimbo Katoliki Ifakara, Mhashamu Sulutaris Libena amewataka Watanzania kulinda na kudumisha amani na kuzingatia makubaliano na maelewano, kwa kuwa ndiyo msingi wa amani wa Taifa lao.

"Sisi k**a nchi tunafurahia amani, tunasema tuna amani na ni kweli tuna amani. Hatuna vita hatuna magomvi, amani iendane na upendo, iwe zao la ukweli na amani inatokana na upendo. Amani inahitaji sana makubaliano na maelewano," amesema Askofu Libena.

Askofu Libena ameyasema hayo leo Aprili 20, 2025, alipokuwa akitoa mahubiri wakati wa ibada ya Pasaka kitaifa katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Andrea Mtume, Jimbo Katoliki lililopo Ifakara, mkoani Morogoro.:

Heri ya   Happy Easter Tag (waambatanishe)  watu wako Hapa unaowatakia pasaka njema.
20/04/2025

Heri ya
Happy Easter

Tag (waambatanishe) watu wako Hapa unaowatakia pasaka njema.

Address

7-C, Ilemela Industrial Area, Airport Road
Mwanza
POBOX1732

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio Free Africa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Radio Free Africa:

Share