Famara Media

Famara Media Famara Media - Inform, Entertain and Educate.
(3)

Geita Gold FC wafanya jambo kubwa kwa jamii...watoa misaada kwa wagonjwa hospitalini Geita. Hongera sana.
07/09/2024

Geita Gold FC wafanya jambo kubwa kwa jamii...watoa misaada kwa wagonjwa hospitalini Geita. Hongera sana.

28/08/2024

Alfa na Omega Band wazindua Albam "Shukurani".

28/08/2024

Alfa na Omega Band kutoka Mwanza....

28/08/2024
MVP | JEAN CHARLES AHOUA.1 - Goli3 - Assist2 - MechiHadi sasa amehusika na magoli 4.. Simba wamefunga goli 7 na kati ya ...
25/08/2024

MVP | JEAN CHARLES AHOUA.

1 - Goli
3 - Assist

2 - Mechi

Hadi sasa amehusika na magoli 4..

Simba wamefunga goli 7 na kati ya hizo 7 MVP Ahoua amehusika na goli 4.

Na bado gari halijachanganya vizuri. Tuendelee kuvuta pumzi na subira, huenda kuna mazuri huko mbele.

DEBORAH FERNANDEZ MAVAMBO ✍️2000 BORN CENTRAL MIDFIELDER . Ni yuleyule dhidi ya Apr kwenye Simba Day , ni yule ambaye al...
25/08/2024

DEBORAH FERNANDEZ MAVAMBO ✍️

2000 BORN CENTRAL MIDFIELDER . Ni yuleyule dhidi ya Apr kwenye Simba Day , ni yule ambaye alifanya Mashabiki wa Simba watikise kichwa na kusema hapa Timu ipo dhidi ya Yanga, Ni yuleyule dhidi ya Tabora United na ni huyu wa leo dhidi Fountain .

Top Top Top Performance kutoka kwake Top Top Top MIDFIELDER , Mpira anaufanya uwe kitu chepesi sana pale kati ya Dimba.

Hana papara k**a kijana aliyebalekhe akiiona kwa mara yakwanza.Vitu vingi anafanya Slow but Sure 🫑 .

Say his name !

DEBORAH FERNANDEZ MAVAMBOπŸ™Œ

MWIGULU NCHEMBA AMRUHUSU YUSUF KAGOMA AENDE SIMBA SC."Nafahamu undani wa Suala la Yusuf Kagoma, ni kweli Kagoma alisaini...
24/08/2024

MWIGULU NCHEMBA AMRUHUSU YUSUF KAGOMA AENDE SIMBA SC.

"Nafahamu undani wa Suala la Yusuf Kagoma, ni kweli Kagoma alisaini mkataba Yanga, na baadae akasaini Simba, Najua kutokwenda kwake Yanga na badala yake kusaini Simba hata sio Masuala ya Fedha"

"Tutatumia muda sana tukitaka kuchimba haya. Kagoma ni mtoto wetu, Yanga ni Club kubwa sana na ina mambo muhimu ya kuyawekea nguvu kuyafanikisha kuliko kuweka nguvu Kagoma aisicheze licha ya ukweli kwamba alistahili achezee Yanga"

"Nimewaomba viongozi wa Yanga wasamehe yote,waondoe shauri dhidi ya Kagoma,wamwachie awe huru akaitumikie Simba kwa Maslahi mapana ya mpira wa nchi na kwa faida ya Mchezaji mwenyewe"

©️ Mwigulu Nchemba.

Waziri wa fedha Tanzania na mlezi wa klabu ya Singida Black Stars.

Kila Mwalimu alikuja na mpango kazi wake kuhakikisha anapata alama tatu katika mchezo wa Leo1: Mecky alihitaji kuwa na u...
24/08/2024

Kila Mwalimu alikuja na mpango kazi wake kuhakikisha anapata alama tatu katika mchezo wa Leo

1: Mecky alihitaji kuwa na umiliki wa mchezo (performance) Wakiwa na idadi kubwa ya wachezaji kwenye phase Zote tatu, huku wakitumia pasi fupifupi na long balls Kwa uchache.

2: Goran akichagua kutumia eneo la pembeni mwa uwanja (akimtumia Zaidi John Nakibinge) + Mipira mirefu (Drop balls) kwakua ana Okutu + Boateng, ambapo alifanikiwa japo sio Kwa kiasi kikubwa.

Dodoma Jiji walikua Bora sana with ball, Toka vizuri nyuma Hadi kwenye Final third ya Pamba Jiji, walitengeneza nafasi, mtihani kwao ulikua ni ubora wa Yona Amosi kuokoa michomo, ndicho walichokikosa Dodoma Jiji (Goli tu) lakini walijitahidi kufanya vitu vingi Kwa usahihi.

Turning point ya Pamba ulikua ni Mabadiliko ya George mpole second half yaliifanya Pamba Jiji kurejea mchezoni, walioonekana kufanya mashambulizi ya hatari langoni mwa Dodoma, nafikiri Pamba Kuna vitu wanahitaji kuboresha:-

1: Maamuzi sahihi, kitu gani tufanye katika nyakati zipi (wakiwa na mpira na bila mpira) chaguzi za pasi zao, nani Yuko sehemu sahihi, namfikishia vipi mpira.

2: Usahihi wa matendo Yao, wanaonekana kukosa sana utulivu wanapokaribia final third ya mpinzani, Kuna muda wanahitaji kumantain possession ili kupata nafasi sahihi, lakini walichagua kushoot.

3: Eneo la ulinzi wanakua beaten sana katika zile 1v1 situations, wanaacha sana mianya (distance Kati ya mchezaji na mchezaji).

NOTE:
1: John Nakibinge mchezaji Bora Pamba wakiwa na mpira, shida Maamuzi yake ya mwisho, anahitaji utulivu, kunyanyua macho yake, Kasi yake dribbling πŸ‘.

2: Milandu alikua na game nzuri sana, alikua anawaweka Dodoma sehemu salama, aliwapa wakati mgumu sana J. Mwashinga na Kasindi.

3: Yona Amosi anajua Nini anatakiwa kufanya akiwa golini, saves after Saves... Ana clear makosa, remember the Name 🧀.

4: George mpole anamdai muda Zaidi Goran!

5: Makocha unafurahia performance ya team, unaumia umekosa goli tu.

NBC Premier League 2024/2025FT | Pamba Jiji FC 0 - 0 Dodoma Jiji FC CCM KIRUMBA.
24/08/2024

NBC Premier League 2024/2025

FT | Pamba Jiji FC 0 - 0 Dodoma Jiji FC

CCM KIRUMBA.

🚨BODI YA LIGI MJITAFAKARI K**A MNATOSHA KUONGOZA SOKA LETU.Anaandika Fabiano Mwaipopo - Mdau wa Soka.πŸ”·Uhuni unaondelea k...
23/08/2024

🚨BODI YA LIGI MJITAFAKARI K**A MNATOSHA KUONGOZA SOKA LETU.

Anaandika Fabiano Mwaipopo - Mdau wa Soka.

πŸ”·Uhuni unaondelea kwenye ligi yetu Kwa kichaka Cha *UDHAMINI* kuufumbia macho inahitaji uwe na moyo usio na haya wa soni na wenye tabia zote za "WAPIGA DILI MICHEZONI " na nisawa na kusema hamtoshi kuogoza mpira wetu, Bali mmetanguliza agenda zenu binafsi nyuma ya mpira.

Kiongozi mkuu wa yanga ni Eng. HERSI SAID

Kiongozi mkuu wa uwekezaji wa gsm ni Eng. HERSI SAID

πŸ”·Anayeingia mikataba ya uwekezaji ya kibiashara ya GSM ni mfanyakazi wake mkurugenzi mkuu wa uwekezaji wa GSM ambaye ni Eng. HERSI SAID

Aliyesaini mikataba ya GSM na hizo timu sita za ligi KUU ya NBC ni Eng. HERSI SAID

πŸ”·Kifupi Eng. HERSI SAID ni mfanyakazi mkuu wa yanga iliyopo ligi ya NBC , pia ni mfanyakazi mkuu wa uwekezaji wa GSM na ndio aliyeingia kandarasi na timu sita kwenye ligi ya NBC

πŸ”·Hivi viongozi wa tff mnaweza vipi kutuambia k**a MNATOSHA KUONGOZA mpira wetu kwa upuuzi k**a huu? Mliona ligi gani Duniani wakaruhisu huu upuuzi , nimeita upuuzi maana ni jambo la kihuni na ambalo halikubaliki kwenye mpira , kuanzia sheria Hadi kanuni za CAF na fifa , najua nyiemmejificha kwenye kipengele Cha kanuni zetu hazijasema k**a ni kosa kufanya hivyo , je ? Mnasubiri Nini hizo kanuni kuzifanyia amendment? Mbona kanuni za fee ya wachezaji wa kigeni mmebadilisha kutoka 4ml Hadi 8ml mlishindwaje kufanyia maboresho na Hilo??








mwanafa








WAJUE WATU MWAMBA KATIKA SOKA LA MWANZA.Soka la Mwanza limekuwa linapiga hatua kutoka hatua moja kwenda hatua nyingine. ...
21/08/2024

WAJUE WATU MWAMBA KATIKA SOKA LA MWANZA.

Soka la Mwanza limekuwa linapiga hatua kutoka hatua moja kwenda hatua nyingine. Inaweza kuonekana hatua ni ndogo ila ndio ukuaji. Ni hatua ambazo zimechagizwa na watu wengi wenye moyo na wasiokua na moyo.

Soka la Mwanza limepitia milima na mabonde, mazuri na machungu yote watu wa mpira Mwanza tumeyapitia. Kuna wakati watu walitoa machozi jasho na damu kupambana kwa ajili ya hatima ya soka la Mwanza.

Wapo watu wengi sana wamefanya kazi nzuri ambao tuna sababu ya kuwazungumzia. Majina nguli k**a kina Manishi Luparelia, Jumbe Magati, Jackson Songora, Marehemu Nasibu Mabrouk, Vedastus Lufano, Aleem Alibhai, Israel Mtambalike, Paresh Kotecha na wengine wengi ambao nafasi isingetosha kuandika majina yao hapa.

Watu huwa wamepambana sana kusababisha soka la Mwanza linakuwa kubwa siku hadi siku. Zipo nyakati waliona ugumu na zipo nyakati waliona wepesi kutokana na majukumu walionayo katika kusukuma soka mkoa Mwanza.

Zipo timu nyingi za Soka hapa Mwanza ambazo mashujaa hawa walijitoa kuhakikisha zinafanya vizuri katika kuleta furaha kwa wana Mwamza. Zipo timu k**a Pamba, Toto Africans, Mbao FC, Alliance na hata Gwambina. Zote hizi likuchukua muda na gharama za watu hawa kuzifikisha katika nchi ya Kanani.

Kwa umoja wao walizifikisha ligi kuu na kwa bahati mbaya zikateremka zote kwa awamu na msimu tofauti. Timu zote nilizozitaja hapo juu kwa Msimu tofauti zilikuwa ligi kuu na kushuka baada ya kupata pointi chache kati ya timu zilizokuwa zinashiriki misimu hiyo.

Baada ya timu hizo kushuka, kazi ikawa kazi. Miaka kadhaa watu wengi mkoani Mwanza wamepambana sana kuzirudisha ligi kuu kwa kushirikiana hatimaye kwa neema ya Mungu kupitia Komredi Said Mohamed Mtanda Pamba Jiji FC ikapamba Ligi kuu ya NBC.

Itaendelea....

πŒππ€ππ†πŽ 𝐇𝐀𝐔𝐉𝐀𝐅𝐀 π“π”π‹πˆπƒπ€ππ†π€ππ˜π–π€Feb 2022 TFF walitoa taarifa ya Kusaini mkataba wa miaka miwili na GSM Group k**a Mdhamini m...
17/08/2024

πŒππ€ππ†πŽ 𝐇𝐀𝐔𝐉𝐀𝐅𝐀 π“π”π‹πˆπƒπ€ππ†π€ππ˜π–π€

Feb 2022 TFF walitoa taarifa ya Kusaini mkataba wa miaka miwili na GSM Group k**a Mdhamini mwenza wa Ligi Kuu NBC

Mkataba huu ulitakiwa kuhusisha Timu zote 16, Klabu za ligi Kuu zikatia sani ya makubaliano ya mkataba huo isipokua Klabu mbili ambazo ni

Azam FC & Simba SC

Baada ya Upande wa klabu ambazo ziligomea mkataba huo kutoa hoja za msingi, TFF wakakaa kimya na wakahairisha zoezi la kulazimisha Klabu kuweka logo ya GSM katika jezi zao

Nimekumbuka tukio hili, Leo ni August 17 2024

Kwanini TFF hawakutoa taarifa ya kurudisha Pesa za GSM kwamba mkataba umevunjwa? Kwamba ulivunjwa kimyakimya? Kwanini ?

Baada ya Tukio hili hadi leo, Klabu za ligi Kuu 7 kati ya 16 tayari zina udhamini wa GSM na wanaelekea kumaliza zote

Mimi naamini huu mkataba bado unaishi✍️

Β© Ayubu Taarifa

KAULI ZA KOCHA WA PAMBA JIJI FC KOPONOVIC ZINAFIKIRISHA SANA.Pamba Jiji FC jana wameanza Kampeni ya kushiriki michuano y...
17/08/2024

KAULI ZA KOCHA WA PAMBA JIJI FC KOPONOVIC ZINAFIKIRISHA SANA.

Pamba Jiji FC jana wameanza Kampeni ya kushiriki michuano ya Ligi kuu NBC kwa kucheza na Tanzanian Prisons. Ilikuwa mechi ya kwanza ya ufunguzi wa pazia la ligi kuu yenye msisimko mkubwa.

Timu zote mbili zilikuwa na wachezaji wazoefu na wenye kuifahamu ligi vizuri. Ukiangalia Pamba wachezaji walioanza kikosi cha kwanza wachezaji karibia wote waba uzoefu na ligi kuu.

Kipa Yona Amos alikuwa Tanzania Prisons, Kenneth Kunambi alikuwa Ihefu FC, Ibrahim Abraham alikuwa Tanzania Prisons, Christopher Oruchum alikuwa Namungo na Justine Omar alikuwa Dodoma Jiji FC.

Hata wengine wote waliobakia kwenye kikosi wamesajili kutoka timu kubwa kubwa. Na wamecheza ligi kuu ya Tanzania na wanajua ugumu wake ulivyo. Kocha Goran Koponovic anaijua ligi kuu na anaijua Tanzania maana sio mara ya kwanza kufundisha soka la Tanzania.

Ukiangalia Tanzania Prisons pia wana wachezaji wazoefu wa ligi kuu. Wamecheza mechi nyingi na wanajua ugumu wake na uimara wake. Kocha Mbwana Makata anaijua ligi kuu maana amecheza k**a Mchezaji miaka mingi huko nyuma na sasa ni Kocha wa Tanzania Prisons.

Matokeo ya mechi ya jana kwa kila timu kupata pointi moja moja yalikuwa sahihi kutokana na ugumu wa mchezo ulivyokuwa. Wachezaji kutokuwa makini katika ukabaji na umaliziaji ulisababisha timu kutokupata matokeo ya ushindi.

Uzoefu wa muda mrefu wa Tanzania Prisons uliwapa kuwa makini katika kujilinda na uchanga wa Pamba Jiji FC katika mchezo wa kwanza dhidi ya Tanzania Prisons ulisababisha kuondoka na pointi moja.

Pamoja na yote ila kauli ya Kocha wa Pamba Jiji FC Goran Koponovic ilinipa kufikiria sana. Kwamba TFF walizuia wachezaji waliokuwa kwenye utaratibu wa mchezo wa jana kwa sababu hawana leseni. Goran anasema amebadilisha kikosi karibia mara tano. Kitendo ambacho kiliharibu utaratibu wa mchezo wao jana.

Alienda mbali Kocha Kopunovic kuilaumu TFF kwa kutoitendea haki Pamba na yeye binafsi k**a Kocha.

Itaendelea.....

Nafikiri ilikua ni jambo Moja tu Tanzania Prisons SC wamekikosa katika dk 90' za mchezo, ni kuuweka mpira wavuni tu ndic...
16/08/2024

Nafikiri ilikua ni jambo Moja tu Tanzania Prisons SC wamekikosa katika dk 90' za mchezo, ni kuuweka mpira wavuni tu ndicho kilichosekana Kwa Tanzania Prisons, walijaribu kutengeneza nafasi, zuia vizuri ila goli tu ndicho walichokikosa.

Nafikiri kipindi Cha kwanza Pamba Jiji FC walikua na mchezo mzuri, walikua wanacheza vizuri kutoka nyuma Lakini mtihani ilikua namna team inatoka katikati kwenda mbele, namna gani mipira inafika alipo Erick Okutu + baadhi ya nyakati Kuna Maamuzi sahihi + utulivu ulikosekana.

Note:
Yona Amosi alimaliza msimu akiwa na saves 35, Leo kaanza alipoishia Saves 3 za Maana, k**a sio uimara wake nadhani Pamba alikua anaokota mipira wavuni.

John Nakibinge good game, speed, dribbling, Justin Omary defending πŸ‘.

Oscar Mwajanga ni vile alikosa msaada, Segeja 8+ mins 1 shot mwanzo mzuri.

MBONA k**a kulikua na uoga 😁, ukishinda mechi ya kwanza unashuka daraja... Kikombe kimekimbiwa.

FT: Pamba Jiji 0 Vs 0 Tanzania Prisons SC



Happy Birthday Adrishinah.....Long Iive with full of blessings and happiness.
15/08/2024

Happy Birthday Adrishinah.....Long Iive with full of blessings and happiness.

Ukiwasikiliza wachambuzi kuhusu Chama ndio utajua k**a watu hawataki amani nchi hiiπŸ˜€βž‘οΈMsimu uliopita hakuna nyota anaemu...
15/08/2024

Ukiwasikiliza wachambuzi kuhusu Chama ndio utajua k**a watu hawataki amani nchi hiiπŸ˜€

➑️Msimu uliopita hakuna nyota anaemuingia Chama Yanga.
➑️Kipindi cha usajili - Yanga wamelamba dume kumsajili Chama

➑️Leo hii kabla ya ligi kuanza - Nilisema usajili wa Chama hauna maana na hana furaha Yanga

Ndio maana mwili unasisimka nikiitwa mchambuzi🀭

Yes, we are coming very broad and loud....Let us make it happen.
15/08/2024

Yes, we are coming very broad and loud....Let us make it happen.

Chama kubwa, Famara Online TV.
15/08/2024

Chama kubwa, Famara Online TV.

15/08/2024

Everest Hagila....Mjumbe wa Bodi ya Pamba Jiji Football Club....

National Safari....
15/08/2024

National Safari....

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa Orodha mpya ya Vilabu Bora Afrika kuelekea msimu mpya 2024/251. Al Ahly (Egypt) ...
15/08/2024

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa Orodha mpya ya Vilabu Bora Afrika kuelekea msimu mpya 2024/25
1. Al Ahly (Egypt) – 87 points
2. Esperance (Tunisia) – 61 points
3. Wydad AC (Morocco) – 60 points
4. Mamelodi Sundowns (South Africa) – 54 points
5. Zamalek (Egypt) – 48 points
6. RS Berkane (Morocco) – 42 points
7. Simba (Tanzania) – 39 points
8. Petro de Luanda (Angola) – 39 points
9. TP Mazembe (DR Congo) – 38 points
10. CR Belouizdad (Algeria) – 36 points
Chama lako namba ngapi hapo __!!πŸ‘‡

Mzee Said Soud ni Mwenyeji wa Tanga, shabiki mkubwa wa Yanga na Coastal Union.Bahati mbaya sana TFF wamemuamini kuwa Men...
11/08/2024

Mzee Said Soud ni Mwenyeji wa Tanga, shabiki mkubwa wa Yanga na Coastal Union.

Bahati mbaya sana TFF wamemuamini kuwa Menyekiti wa Kamati ya Hadhi za Wachezaji, k**ati ambayo ameitumia KUIMUZA Simba kwa muda mrefu sasa.

Tokea ameingia yeye k**a Mjumbe wa Kamati ya Utendaji na Mwenyekiti wa Kamati amekuwa akishirikiana na marafiki zake k**a nyenzo za kuiumiza Simba.

Hakujawahi kuwa na haki kwa Simba na yeye analijua hilo na amekuwa akijitapa hadharani kuwa ni RAFIKI MKUBWA WA RAIS WA TFF, Wallace Karia na HAKUNA WA KUMFANYA LOLOTE.

Amezoea maisha ya migogoro tokea enzi za FAT ni Coastal tu ndio yenye maendeleo Tanga tokea amekuwa Mwenyekiti wa Mkoa wa Tanga na MIGOGORO HAIJAWAHI KWISHA.

Yeye amekuwa chanzo cha migogoro, lakini ni mjanja na MNAFIKI MKUBWA.

Leo kwenye Kamati suala la Simba na KMC kuhusiana na Awesu limekuwa kubwa zaidi ya kawaida kwa kuwa tu AMEINGIZA CHUKI UPYA dhidi ya Simba na kusababisha liwe kubwa zaidi, wakati tayari yakifikiwa makubaliano.

Inaonekana Simba na KMC wangeelewana k**a si k**ati hiyo chini ya Mzee Said anayeutumia vibaya MGONGO WA KARIA.

Karia awe makini, kafanya makubwa katika mpira wa Tanzania, lakini babu huyu anakwenda kumharibia kwa kisingizio cha UTANGA, kumbe ni mapenzi yaliyopindukia ya Yanga na HASIRA NA CHUKI ZISIZOISHA DHIDI YA SIMBA.

Wanasimba tusikubali kuonewa hivi, TUNA NGUVU...Huyu Mzee ni ADUI YETU NAMBA MOJA na roho mbaya yake HAIWEZI KUIZIDI HAKI YA SIMBA...TUMKATAE.

Baada ya hapa, UTAWASIKIA CHAWA wa GSM wakiingia kazini kumtetea kwa kuwa NIMEMGUSA BABU YAO KIPENZI.

Pamba Day ni 10 AGOSTI 2024 CCM Kirumba Mwanza.
04/08/2024

Pamba Day ni 10 AGOSTI 2024 CCM Kirumba Mwanza.

04/08/2024
COPCO FC WATWAA KOMBE LA FAHARI SUPER  CUP 2024.Timu ya Copco Football Club ya kutoka Buswelu Wilaya ya Ilemela Mkoa wa ...
04/08/2024

COPCO FC WATWAA KOMBE LA FAHARI SUPER CUP 2024.

Timu ya Copco Football Club ya kutoka Buswelu Wilaya ya Ilemela Mkoa wa Mwanza imeibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Mweta Sports Club ya kutoka Kisesa Wilayani Magu katika uwanja wa Red Cross Kisesa.

Akizungumzia baada ya kumalizika mtanange huo Mgeni Rasmi Mheshimiwa Mary Francis Masanja ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum alisema amefarijika na vipaji vya timu zote na kuomba uongozi wa timu hizo kuvisaidia vipaji hivyo ili vilete faida kwa wahusika na taifa kwa ujumla.

"Nimefarijika na michuano hii, nimependa vipaji vya wachezaji. Hakika kuna vipaji vingi na vizuri sana. Vijana wanajua sana na wana vipaji na uzuri bado wana umri mdogo. Wakiendelezwa watakuwa na faida kwa timu zetu za taifa na wao wenyewe kujiletea vipato"

Aidha Mheshimiwa Masanja amewaasa wana Mwanza kujitokeza kwa wingi katika uwanja wa CCM Kirumba tarehe 10, 2024 kushuhudia timu yao ya Pamba Jiji FC ambao ndio Fahari ya Mwanza na Kanda ya Ziwa.

"Nitoe wito kwa wana Mwanza na Kanda ya Ziwa, wajitokeza kwa wingi uwanja wa CCM Kirumba tarehe 10, 2024 kuiona timu yao Pamba Jiji FC. Ni timu ya wana Mwanza na Kanda ya Ziwa na tunajivunia kuwa nayo. Tafadhali nunueni tiketi mapema wote ili mje kupata raha ya Pamba"

Mratibu wa michuano hiyo ambaye ni Mkurugenzi wa Kituo cha Mweta Sports Centre, Wilbert Mweta amesema michuano hiyo kwa msimu huu ilikuwa mizuri na kuwaasa wachezaji wote kuendelea kujituma ili wafikie lengo kamili ya kuwa wachezaji wakubwa.

Timu ya Copco Football Club imetwaa Kombe pamoja na zawadi ya shilingi milioni moja na medali. Huko Mweta Sports Club wakipata zawadi wa shilingi laki tano na medali.

Huu ni msimu wa tatu kwa michauno hii ya Fahari Super Cup, ambao kwa msimu miwili ya mwanzo kombe lilichukuliwa na Mweta Sports Club. Msimu wa tatu Copco Football Club wametwaa ushindi.

Address

Nyamagana
Mwanza
994

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Famara Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Famara Media:

Videos

Share

Nearby media companies


Other Mwanza media companies

Show All

You may also like