Famara Media

Famara Media Famara Media - Inform, Entertain and Educate.

Mchungaji Mfupi kuliko wote Afrika Leonard Switbert wa kutoka Mbeya ameelezea kisa cha kumpata mchumba wake Elizabeth ka...
14/02/2025

Mchungaji Mfupi kuliko wote Afrika Leonard Switbert wa kutoka Mbeya ameelezea kisa cha kumpata mchumba wake Elizabeth katika siku ya wapendanao via FamaraMedia.

Tufuatilie: YouTube (Famara Media) Instagram (FamaraMedia) Twitter (X) FamaraMedia & Facebook (Famara Media).Mchungaji Leonard mzaliwa wa Mkoani Mbeya ana mc...

07/02/2025

Maneno mazito kutoka kwa Dada wa Taifa . Sikiliza mpaka mwisho.

07/02/2025

Tanzania ni Nchi ambayo ukipata Stress umetaka wewe na sio vinginevyo!!

Majina mapya

Emmanuel Keyeke 'NTANDU"
Mohamed Cumaro "HANGO"
Josephate BADA "KINGU"

NB..... Hata waitwe kina MAKOYE bado hayavutii😁

Elizabeth John Chenge (40) Mido ya  Mechi 3 Goli 1Assist 3Keep on going to the World.....We are proud of you.
05/02/2025

Elizabeth John Chenge (40) Mido ya

Mechi 3
Goli 1
Assist 3

Keep on going to the World.....We are proud of you.

Asante Mungu!! 2025 Mapambano yanaendelea..
05/02/2025

Asante Mungu!! 2025 Mapambano yanaendelea..

03/02/2025
FTArsenal 5 - 1 Manchester City Nb...Mlete mwingine!
02/02/2025

FT

Arsenal 5 - 1 Manchester City

Nb...Mlete mwingine!

02/02/2025

FT | Tabora United 0 - 3 Simba SC

Kwa ushindi huu tumpe Simba SC kombe mapema au bado.?

01/02/2025

YANGA KILELENI BAADA YA USHINDI WA LEO | NANI WA KUMSHUSHA?

Yanga wamerudi kwa kishindo kwenye ligi kuu baada ya kutupwa nje kwenye michuano ya klabu bingwa barani Afrika.

Yanga chini ya Kocha Mjerumani Sead Ramovic imeingia kwa nguvu sana katika mechi hiyo katika uwanja wa KMC ambao ni uwanja wa nyumbani wa Yanga.

Kagera Sugar wameonekana kukosa utulivu toka mechi inaanza. Wamekuwa na makosa mengi kuanza beki, viungo na washambuliaji.

Kagera Sukari wamekosa utulivu wakiwa na mpira kitendo ambacho kimewapa Yanga uzuri wa kutengeneza nafasi nyingi za kufunga.

Kidogo Yanga wamerudishwa ile kujiamini ingawa Master Azizi Ki yeye bado ana ugomvi na penalty maana leo amepoteza penalti ya pili.

Kwa matokeo ya leo, Yanga anakalia usukani wa ligi kwa kufikisha pointi 42 huku hasimu wake Simba SC wakitarajia kucheza kesho Jumapili uwanja wa Ally Hassan Mwinyi dhidi ya Tabora United.

Nb... Kafungwa Kagera Sugar ila vilio vinasikika msimbazi😁

-Hali imekuwa mbaya kwa maafisa wa uhamiaji walitoa uraia kwa wachezaji watatu wa Singida Black Stars, Emmanuel Keyekeh ...
26/01/2025

-Hali imekuwa mbaya kwa maafisa wa uhamiaji walitoa uraia kwa wachezaji watatu wa Singida Black Stars, Emmanuel Keyekeh (Ghana), Arthur Bada (Ivory Coast) na Damaro Mohamedi (Guinea) kuwa raia wa Tanzania. Maafisa hao wamehojiwa kujua walitumia vigezo gani kuwapa uraia wa Tanzania wachezaji hao.

-Uraia wa wachezaji hao unaweza kusitishwa ili kupisha uchunguzi ili kujua k**a walifuata taratibu zote na wamekidhi vigezo vyote vya kupewa uraia wa Tanzania. Pia wamedai kuwa hawajapokea barua yoyote kutoka Simba ya kuwaombea wachezaji wao 9 uraia wa Tanzania na wao wanashangaa kuona barua inasambaa kwenye mitandao ya kijamii.

26/01/2025

Huyu ndio mdogo wangu ninayemfahamu....

TUNDU ANTIPAS LISSU || THE INDOMITABLE LION | CHADEMA CHAIRMAN. youtu.be/0UNY4F1MmR4?si…
23/01/2025

TUNDU ANTIPAS LISSU || THE INDOMITABLE LION | CHADEMA CHAIRMAN.

youtu.be/0UNY4F1MmR4?si…

Aliyekuwa Mchambuzi wa masuala ya soka pale AZAM TV, Dominick Salamba amefunguka kuwa anashangwaza namna waamuzi wa Shir...
23/01/2025

Aliyekuwa Mchambuzi wa masuala ya soka pale AZAM TV, Dominick Salamba amefunguka kuwa anashangwaza namna waamuzi wa Shirikisho la soka Afrika (CAF) wanavyopambana kuibeba Simba kuliko Yanga
“Kinachoshangaza ni kwamba pamoja na utandawazi wa sasa, kwanini waamuzi wa CAF wanafanya makosa mengi? Inafikirisha sana ukitazama mechi za Simba marefa wanakuwa upande wao, lakini ukitazama mechi za Yanga inaumiza sana ni k**a huyu aliyekataa penati halali la Yanga dhidi ya MC Alger juzi.
Aliwaza nini kutoweka penati na mchezaj kashika ndani ya boksi? Picha za marudio zinaonyesha alishika mpira. Na sheria iko wazi. K**a umeshika kwenye boksi ni penati. Ukikataa na timu ikatolewa k**a vile inaumiza sana.”

Chanzo: Champion_tz

16/01/2025

Mwanamuziki John Lennon aliamua kumuacha mke wake Cynthia na kwenda kuanzisha mahusiano mapya na Yoko Ono ambae ni msanii mkubwa mwenye asili ya Japan mwaka 1966, na kweli mwaka 1969 akamuoa Yoko Ono.

Mke wake Cynthia alibaki na mtoto wao wa kiume mwenye miaka mi 5 tu anaeitwa Julian Lennon (ambae ni mwanamuziki mkubwa kwa sasa na Baba yake baada ya kuuwawa 1980 ilikua hajamuweka Julian kwenye wosia wa urithi, yani hakurithishwa chochote) lakini tuachane na hilo ni stori nyingine.

Basi Cynthia alibaki na mtoto wake Julian na maisha yakawa magumu sana kwa upande wake akafikiria nini afanye? Akaamua aziuze kumbukumbu zake zote za mapenzi ya miaka mingi tangu utoto (teens) na John Lennon ambae alikua ni msanii mkubwa wakati huo, akauza barua zote za mapenzi na michoro waliyokua wanapeana kabla hajaachwa na John Lennon.

Barua zilizokua zimebeba ujumbe wa hisia k**a "Nakupenda Cynthia" fikiria ni maumivu kiasi gani Cynthia kubaki na barua zenye kumbukumbu k**a hizi, Cynthia alifanikiwa kuziuza kumbukumbu hizo kwa gharama kubwa kwakua Ex-husband wake alikua ni msanii mkubwa.

Lakini baada ya muda Cynthia alishangaa ametumiwa zawadi kupitia mail alipopokea zawadi hizo zilikua zimetoka kwa Paul McCartney ambae ni msanii mkubwa rafiki wa mume wake waliekua wanaimba wote kwenye bendi moja na alipofungua ndani kuangalia zawadi hizo alikuta ni zile barua zake za kumbukumbu alizoziuza na zilikuja na karatasi ya ujumbe kutoka kwa McCartney aliyokua ameandika "Daima usiuze kumbukumbu zako"

Hivyo ndivyo ilivyo Kumbukumbu zote zinafaa kutunzwa kwa matumizi ya baadae iwe mbaya au nzuri, k**a ni nzuri zitunze k**a kielelezo cha furaha na k**a ni mbaya zitunze k**a funzo. Hii ni entertainment plus education.

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limeifungia klabu ya Simba Sc kuingiza mashabiki kwenye mechi yao ya mwisho ya hatua ya ...
14/01/2025

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limeifungia klabu ya Simba Sc kuingiza mashabiki kwenye mechi yao ya mwisho ya hatua ya Makundi ya kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Constantine Jumapili hii Januari 19, 2025.

Hii ni kutokana na vurugu zilizotokea kwenye mchezo dhid ya SC Sfaxien ya Tunisia uliopigwa Desemba 2024 hvyo mechi dhid ya SC Constantine itachezwa bila mashabiki katika dimba la Benjamin Mkapa.

13/01/2025

Hawa ndio MTIBWA SUGAR... wanataka kurudi Ligi Kuu NBC. Weka mbali na watoto.

This is Simba SC!! Hongera sana kufuzu. Umeipa heshima Tanzania na Afrika Mashariki. Weka Neno moja la pongezi kwa Simba...
12/01/2025

This is Simba SC!! Hongera sana kufuzu. Umeipa heshima Tanzania na Afrika Mashariki. Weka Neno moja la pongezi kwa Simba SC.

Address

Nyamagana
Mwanza
994

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Famara Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Famara Media:

Videos

Share