07/09/2024
Geita Gold FC wafanya jambo kubwa kwa jamii...watoa misaada kwa wagonjwa hospitalini Geita. Hongera sana.
Famara Media - Inform, Entertain and Educate.
(3)
Geita Gold FC wafanya jambo kubwa kwa jamii...watoa misaada kwa wagonjwa hospitalini Geita. Hongera sana.
Alfa na Omega Band wazindua Albam "Shukurani".
Alfa na Omega Band kutoka Mwanza....
MVP | JEAN CHARLES AHOUA.
1 - Goli
3 - Assist
2 - Mechi
Hadi sasa amehusika na magoli 4..
Simba wamefunga goli 7 na kati ya hizo 7 MVP Ahoua amehusika na goli 4.
Na bado gari halijachanganya vizuri. Tuendelee kuvuta pumzi na subira, huenda kuna mazuri huko mbele.
DEBORAH FERNANDEZ MAVAMBO βοΈ
2000 BORN CENTRAL MIDFIELDER . Ni yuleyule dhidi ya Apr kwenye Simba Day , ni yule ambaye alifanya Mashabiki wa Simba watikise kichwa na kusema hapa Timu ipo dhidi ya Yanga, Ni yuleyule dhidi ya Tabora United na ni huyu wa leo dhidi Fountain .
Top Top Top Performance kutoka kwake Top Top Top MIDFIELDER , Mpira anaufanya uwe kitu chepesi sana pale kati ya Dimba.
Hana papara k**a kijana aliyebalekhe akiiona kwa mara yakwanza.Vitu vingi anafanya Slow but Sure π«‘ .
Say his name !
DEBORAH FERNANDEZ MAVAMBOπ
MWIGULU NCHEMBA AMRUHUSU YUSUF KAGOMA AENDE SIMBA SC.
"Nafahamu undani wa Suala la Yusuf Kagoma, ni kweli Kagoma alisaini mkataba Yanga, na baadae akasaini Simba, Najua kutokwenda kwake Yanga na badala yake kusaini Simba hata sio Masuala ya Fedha"
"Tutatumia muda sana tukitaka kuchimba haya. Kagoma ni mtoto wetu, Yanga ni Club kubwa sana na ina mambo muhimu ya kuyawekea nguvu kuyafanikisha kuliko kuweka nguvu Kagoma aisicheze licha ya ukweli kwamba alistahili achezee Yanga"
"Nimewaomba viongozi wa Yanga wasamehe yote,waondoe shauri dhidi ya Kagoma,wamwachie awe huru akaitumikie Simba kwa Maslahi mapana ya mpira wa nchi na kwa faida ya Mchezaji mwenyewe"
Β©οΈ Mwigulu Nchemba.
Waziri wa fedha Tanzania na mlezi wa klabu ya Singida Black Stars.
Kila Mwalimu alikuja na mpango kazi wake kuhakikisha anapata alama tatu katika mchezo wa Leo
1: Mecky alihitaji kuwa na umiliki wa mchezo (performance) Wakiwa na idadi kubwa ya wachezaji kwenye phase Zote tatu, huku wakitumia pasi fupifupi na long balls Kwa uchache.
2: Goran akichagua kutumia eneo la pembeni mwa uwanja (akimtumia Zaidi John Nakibinge) + Mipira mirefu (Drop balls) kwakua ana Okutu + Boateng, ambapo alifanikiwa japo sio Kwa kiasi kikubwa.
Dodoma Jiji walikua Bora sana with ball, Toka vizuri nyuma Hadi kwenye Final third ya Pamba Jiji, walitengeneza nafasi, mtihani kwao ulikua ni ubora wa Yona Amosi kuokoa michomo, ndicho walichokikosa Dodoma Jiji (Goli tu) lakini walijitahidi kufanya vitu vingi Kwa usahihi.
Turning point ya Pamba ulikua ni Mabadiliko ya George mpole second half yaliifanya Pamba Jiji kurejea mchezoni, walioonekana kufanya mashambulizi ya hatari langoni mwa Dodoma, nafikiri Pamba Kuna vitu wanahitaji kuboresha:-
1: Maamuzi sahihi, kitu gani tufanye katika nyakati zipi (wakiwa na mpira na bila mpira) chaguzi za pasi zao, nani Yuko sehemu sahihi, namfikishia vipi mpira.
2: Usahihi wa matendo Yao, wanaonekana kukosa sana utulivu wanapokaribia final third ya mpinzani, Kuna muda wanahitaji kumantain possession ili kupata nafasi sahihi, lakini walichagua kushoot.
3: Eneo la ulinzi wanakua beaten sana katika zile 1v1 situations, wanaacha sana mianya (distance Kati ya mchezaji na mchezaji).
NOTE:
1: John Nakibinge mchezaji Bora Pamba wakiwa na mpira, shida Maamuzi yake ya mwisho, anahitaji utulivu, kunyanyua macho yake, Kasi yake dribbling π.
2: Milandu alikua na game nzuri sana, alikua anawaweka Dodoma sehemu salama, aliwapa wakati mgumu sana J. Mwashinga na Kasindi.
3: Yona Amosi anajua Nini anatakiwa kufanya akiwa golini, saves after Saves... Ana clear makosa, remember the Name π§€.
4: George mpole anamdai muda Zaidi Goran!
5: Makocha unafurahia performance ya team, unaumia umekosa goli tu.
NBC Premier League 2024/2025
FT | Pamba Jiji FC 0 - 0 Dodoma Jiji FC
CCM KIRUMBA.
π¨BODI YA LIGI MJITAFAKARI K**A MNATOSHA KUONGOZA SOKA LETU.
Anaandika Fabiano Mwaipopo - Mdau wa Soka.
π·Uhuni unaondelea kwenye ligi yetu Kwa kichaka Cha *UDHAMINI* kuufumbia macho inahitaji uwe na moyo usio na haya wa soni na wenye tabia zote za "WAPIGA DILI MICHEZONI " na nisawa na kusema hamtoshi kuogoza mpira wetu, Bali mmetanguliza agenda zenu binafsi nyuma ya mpira.
Kiongozi mkuu wa yanga ni Eng. HERSI SAID
Kiongozi mkuu wa uwekezaji wa gsm ni Eng. HERSI SAID
π·Anayeingia mikataba ya uwekezaji ya kibiashara ya GSM ni mfanyakazi wake mkurugenzi mkuu wa uwekezaji wa GSM ambaye ni Eng. HERSI SAID
Aliyesaini mikataba ya GSM na hizo timu sita za ligi KUU ya NBC ni Eng. HERSI SAID
π·Kifupi Eng. HERSI SAID ni mfanyakazi mkuu wa yanga iliyopo ligi ya NBC , pia ni mfanyakazi mkuu wa uwekezaji wa GSM na ndio aliyeingia kandarasi na timu sita kwenye ligi ya NBC
π·Hivi viongozi wa tff mnaweza vipi kutuambia k**a MNATOSHA KUONGOZA mpira wetu kwa upuuzi k**a huu? Mliona ligi gani Duniani wakaruhisu huu upuuzi , nimeita upuuzi maana ni jambo la kihuni na ambalo halikubaliki kwenye mpira , kuanzia sheria Hadi kanuni za CAF na fifa , najua nyiemmejificha kwenye kipengele Cha kanuni zetu hazijasema k**a ni kosa kufanya hivyo , je ? Mnasubiri Nini hizo kanuni kuzifanyia amendment? Mbona kanuni za fee ya wachezaji wa kigeni mmebadilisha kutoka 4ml Hadi 8ml mlishindwaje kufanyia maboresho na Hilo??
mwanafa
WAJUE WATU MWAMBA KATIKA SOKA LA MWANZA.
Soka la Mwanza limekuwa linapiga hatua kutoka hatua moja kwenda hatua nyingine. Inaweza kuonekana hatua ni ndogo ila ndio ukuaji. Ni hatua ambazo zimechagizwa na watu wengi wenye moyo na wasiokua na moyo.
Soka la Mwanza limepitia milima na mabonde, mazuri na machungu yote watu wa mpira Mwanza tumeyapitia. Kuna wakati watu walitoa machozi jasho na damu kupambana kwa ajili ya hatima ya soka la Mwanza.
Wapo watu wengi sana wamefanya kazi nzuri ambao tuna sababu ya kuwazungumzia. Majina nguli k**a kina Manishi Luparelia, Jumbe Magati, Jackson Songora, Marehemu Nasibu Mabrouk, Vedastus Lufano, Aleem Alibhai, Israel Mtambalike, Paresh Kotecha na wengine wengi ambao nafasi isingetosha kuandika majina yao hapa.
Watu huwa wamepambana sana kusababisha soka la Mwanza linakuwa kubwa siku hadi siku. Zipo nyakati waliona ugumu na zipo nyakati waliona wepesi kutokana na majukumu walionayo katika kusukuma soka mkoa Mwanza.
Zipo timu nyingi za Soka hapa Mwanza ambazo mashujaa hawa walijitoa kuhakikisha zinafanya vizuri katika kuleta furaha kwa wana Mwamza. Zipo timu k**a Pamba, Toto Africans, Mbao FC, Alliance na hata Gwambina. Zote hizi likuchukua muda na gharama za watu hawa kuzifikisha katika nchi ya Kanani.
Kwa umoja wao walizifikisha ligi kuu na kwa bahati mbaya zikateremka zote kwa awamu na msimu tofauti. Timu zote nilizozitaja hapo juu kwa Msimu tofauti zilikuwa ligi kuu na kushuka baada ya kupata pointi chache kati ya timu zilizokuwa zinashiriki misimu hiyo.
Baada ya timu hizo kushuka, kazi ikawa kazi. Miaka kadhaa watu wengi mkoani Mwanza wamepambana sana kuzirudisha ligi kuu kwa kushirikiana hatimaye kwa neema ya Mungu kupitia Komredi Said Mohamed Mtanda Pamba Jiji FC ikapamba Ligi kuu ya NBC.
Itaendelea....
ππππππ ππππππ
π πππππππππππππ
Feb 2022 TFF walitoa taarifa ya Kusaini mkataba wa miaka miwili na GSM Group k**a Mdhamini mwenza wa Ligi Kuu NBC
Mkataba huu ulitakiwa kuhusisha Timu zote 16, Klabu za ligi Kuu zikatia sani ya makubaliano ya mkataba huo isipokua Klabu mbili ambazo ni
Azam FC & Simba SC
Baada ya Upande wa klabu ambazo ziligomea mkataba huo kutoa hoja za msingi, TFF wakakaa kimya na wakahairisha zoezi la kulazimisha Klabu kuweka logo ya GSM katika jezi zao
Nimekumbuka tukio hili, Leo ni August 17 2024
Kwanini TFF hawakutoa taarifa ya kurudisha Pesa za GSM kwamba mkataba umevunjwa? Kwamba ulivunjwa kimyakimya? Kwanini ?
Baada ya Tukio hili hadi leo, Klabu za ligi Kuu 7 kati ya 16 tayari zina udhamini wa GSM na wanaelekea kumaliza zote
Mimi naamini huu mkataba bado unaishiβοΈ
Β© Ayubu Taarifa
KAULI ZA KOCHA WA PAMBA JIJI FC KOPONOVIC ZINAFIKIRISHA SANA.
Pamba Jiji FC jana wameanza Kampeni ya kushiriki michuano ya Ligi kuu NBC kwa kucheza na Tanzanian Prisons. Ilikuwa mechi ya kwanza ya ufunguzi wa pazia la ligi kuu yenye msisimko mkubwa.
Timu zote mbili zilikuwa na wachezaji wazoefu na wenye kuifahamu ligi vizuri. Ukiangalia Pamba wachezaji walioanza kikosi cha kwanza wachezaji karibia wote waba uzoefu na ligi kuu.
Kipa Yona Amos alikuwa Tanzania Prisons, Kenneth Kunambi alikuwa Ihefu FC, Ibrahim Abraham alikuwa Tanzania Prisons, Christopher Oruchum alikuwa Namungo na Justine Omar alikuwa Dodoma Jiji FC.
Hata wengine wote waliobakia kwenye kikosi wamesajili kutoka timu kubwa kubwa. Na wamecheza ligi kuu ya Tanzania na wanajua ugumu wake ulivyo. Kocha Goran Koponovic anaijua ligi kuu na anaijua Tanzania maana sio mara ya kwanza kufundisha soka la Tanzania.
Ukiangalia Tanzania Prisons pia wana wachezaji wazoefu wa ligi kuu. Wamecheza mechi nyingi na wanajua ugumu wake na uimara wake. Kocha Mbwana Makata anaijua ligi kuu maana amecheza k**a Mchezaji miaka mingi huko nyuma na sasa ni Kocha wa Tanzania Prisons.
Matokeo ya mechi ya jana kwa kila timu kupata pointi moja moja yalikuwa sahihi kutokana na ugumu wa mchezo ulivyokuwa. Wachezaji kutokuwa makini katika ukabaji na umaliziaji ulisababisha timu kutokupata matokeo ya ushindi.
Uzoefu wa muda mrefu wa Tanzania Prisons uliwapa kuwa makini katika kujilinda na uchanga wa Pamba Jiji FC katika mchezo wa kwanza dhidi ya Tanzania Prisons ulisababisha kuondoka na pointi moja.
Pamoja na yote ila kauli ya Kocha wa Pamba Jiji FC Goran Koponovic ilinipa kufikiria sana. Kwamba TFF walizuia wachezaji waliokuwa kwenye utaratibu wa mchezo wa jana kwa sababu hawana leseni. Goran anasema amebadilisha kikosi karibia mara tano. Kitendo ambacho kiliharibu utaratibu wa mchezo wao jana.
Alienda mbali Kocha Kopunovic kuilaumu TFF kwa kutoitendea haki Pamba na yeye binafsi k**a Kocha.
Itaendelea.....
Nafikiri ilikua ni jambo Moja tu Tanzania Prisons SC wamekikosa katika dk 90' za mchezo, ni kuuweka mpira wavuni tu ndicho kilichosekana Kwa Tanzania Prisons, walijaribu kutengeneza nafasi, zuia vizuri ila goli tu ndicho walichokikosa.
Nafikiri kipindi Cha kwanza Pamba Jiji FC walikua na mchezo mzuri, walikua wanacheza vizuri kutoka nyuma Lakini mtihani ilikua namna team inatoka katikati kwenda mbele, namna gani mipira inafika alipo Erick Okutu + baadhi ya nyakati Kuna Maamuzi sahihi + utulivu ulikosekana.
Note:
Yona Amosi alimaliza msimu akiwa na saves 35, Leo kaanza alipoishia Saves 3 za Maana, k**a sio uimara wake nadhani Pamba alikua anaokota mipira wavuni.
John Nakibinge good game, speed, dribbling, Justin Omary defending π.
Oscar Mwajanga ni vile alikosa msaada, Segeja 8+ mins 1 shot mwanzo mzuri.
MBONA k**a kulikua na uoga π, ukishinda mechi ya kwanza unashuka daraja... Kikombe kimekimbiwa.
FT: Pamba Jiji 0 Vs 0 Tanzania Prisons SC
Happy Birthday Adrishinah.....Long Iive with full of blessings and happiness.
Ukiwasikiliza wachambuzi kuhusu Chama ndio utajua k**a watu hawataki amani nchi hiiπ
β‘οΈMsimu uliopita hakuna nyota anaemuingia Chama Yanga.
β‘οΈKipindi cha usajili - Yanga wamelamba dume kumsajili Chama
β‘οΈLeo hii kabla ya ligi kuanza - Nilisema usajili wa Chama hauna maana na hana furaha Yanga
Ndio maana mwili unasisimka nikiitwa mchambuziπ€
Yes, we are coming very broad and loud....Let us make it happen.
Chama kubwa, Famara Online TV.
Everest Hagila....Mjumbe wa Bodi ya Pamba Jiji Football Club....
National Safari....
SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa Orodha mpya ya Vilabu Bora Afrika kuelekea msimu mpya 2024/25
1. Al Ahly (Egypt) β 87 points
2. Esperance (Tunisia) β 61 points
3. Wydad AC (Morocco) β 60 points
4. Mamelodi Sundowns (South Africa) β 54 points
5. Zamalek (Egypt) β 48 points
6. RS Berkane (Morocco) β 42 points
7. Simba (Tanzania) β 39 points
8. Petro de Luanda (Angola) β 39 points
9. TP Mazembe (DR Congo) β 38 points
10. CR Belouizdad (Algeria) β 36 points
Chama lako namba ngapi hapo __!!π
Mzee Said Soud ni Mwenyeji wa Tanga, shabiki mkubwa wa Yanga na Coastal Union.
Bahati mbaya sana TFF wamemuamini kuwa Menyekiti wa Kamati ya Hadhi za Wachezaji, k**ati ambayo ameitumia KUIMUZA Simba kwa muda mrefu sasa.
Tokea ameingia yeye k**a Mjumbe wa Kamati ya Utendaji na Mwenyekiti wa Kamati amekuwa akishirikiana na marafiki zake k**a nyenzo za kuiumiza Simba.
Hakujawahi kuwa na haki kwa Simba na yeye analijua hilo na amekuwa akijitapa hadharani kuwa ni RAFIKI MKUBWA WA RAIS WA TFF, Wallace Karia na HAKUNA WA KUMFANYA LOLOTE.
Amezoea maisha ya migogoro tokea enzi za FAT ni Coastal tu ndio yenye maendeleo Tanga tokea amekuwa Mwenyekiti wa Mkoa wa Tanga na MIGOGORO HAIJAWAHI KWISHA.
Yeye amekuwa chanzo cha migogoro, lakini ni mjanja na MNAFIKI MKUBWA.
Leo kwenye Kamati suala la Simba na KMC kuhusiana na Awesu limekuwa kubwa zaidi ya kawaida kwa kuwa tu AMEINGIZA CHUKI UPYA dhidi ya Simba na kusababisha liwe kubwa zaidi, wakati tayari yakifikiwa makubaliano.
Inaonekana Simba na KMC wangeelewana k**a si k**ati hiyo chini ya Mzee Said anayeutumia vibaya MGONGO WA KARIA.
Karia awe makini, kafanya makubwa katika mpira wa Tanzania, lakini babu huyu anakwenda kumharibia kwa kisingizio cha UTANGA, kumbe ni mapenzi yaliyopindukia ya Yanga na HASIRA NA CHUKI ZISIZOISHA DHIDI YA SIMBA.
Wanasimba tusikubali kuonewa hivi, TUNA NGUVU...Huyu Mzee ni ADUI YETU NAMBA MOJA na roho mbaya yake HAIWEZI KUIZIDI HAKI YA SIMBA...TUMKATAE.
Baada ya hapa, UTAWASIKIA CHAWA wa GSM wakiingia kazini kumtetea kwa kuwa NIMEMGUSA BABU YAO KIPENZI.
Pamba Day ni 10 AGOSTI 2024 CCM Kirumba Mwanza.
COPCO FC WATWAA KOMBE LA FAHARI SUPER CUP 2024.
Timu ya Copco Football Club ya kutoka Buswelu Wilaya ya Ilemela Mkoa wa Mwanza imeibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Mweta Sports Club ya kutoka Kisesa Wilayani Magu katika uwanja wa Red Cross Kisesa.
Akizungumzia baada ya kumalizika mtanange huo Mgeni Rasmi Mheshimiwa Mary Francis Masanja ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum alisema amefarijika na vipaji vya timu zote na kuomba uongozi wa timu hizo kuvisaidia vipaji hivyo ili vilete faida kwa wahusika na taifa kwa ujumla.
"Nimefarijika na michuano hii, nimependa vipaji vya wachezaji. Hakika kuna vipaji vingi na vizuri sana. Vijana wanajua sana na wana vipaji na uzuri bado wana umri mdogo. Wakiendelezwa watakuwa na faida kwa timu zetu za taifa na wao wenyewe kujiletea vipato"
Aidha Mheshimiwa Masanja amewaasa wana Mwanza kujitokeza kwa wingi katika uwanja wa CCM Kirumba tarehe 10, 2024 kushuhudia timu yao ya Pamba Jiji FC ambao ndio Fahari ya Mwanza na Kanda ya Ziwa.
"Nitoe wito kwa wana Mwanza na Kanda ya Ziwa, wajitokeza kwa wingi uwanja wa CCM Kirumba tarehe 10, 2024 kuiona timu yao Pamba Jiji FC. Ni timu ya wana Mwanza na Kanda ya Ziwa na tunajivunia kuwa nayo. Tafadhali nunueni tiketi mapema wote ili mje kupata raha ya Pamba"
Mratibu wa michuano hiyo ambaye ni Mkurugenzi wa Kituo cha Mweta Sports Centre, Wilbert Mweta amesema michuano hiyo kwa msimu huu ilikuwa mizuri na kuwaasa wachezaji wote kuendelea kujituma ili wafikie lengo kamili ya kuwa wachezaji wakubwa.
Timu ya Copco Football Club imetwaa Kombe pamoja na zawadi ya shilingi milioni moja na medali. Huko Mweta Sports Club wakipata zawadi wa shilingi laki tano na medali.
Huu ni msimu wa tatu kwa michauno hii ya Fahari Super Cup, ambao kwa msimu miwili ya mwanzo kombe lilichukuliwa na Mweta Sports Club. Msimu wa tatu Copco Football Club wametwaa ushindi.
https://youtu.be/sjIvyWZPK1U?si=odQTvgxk69_USv1K
BABA AMNYONGA MWANAE NA YEYE KUJIUWA Katika hali isiyokuwa ya kawaida mwanume mmoja aitwaye Kisumo Emmanuel [38] mkazi wa Kijiji cha Sayaka wilayani Magu mko...
Nyamagana
Mwanza
994
Be the first to know and let us send you an email when Famara Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.
Send a message to Famara Media:
Mkutano Mkubwa wa Injili Mwanza, CCM Kirumba 24-28 Julai 2024 kuanzia saa 2 asubuhi hadi 11 jioni. Ni Pasta Ezekiel kutoka Kenya ambaye Bwana anamtumia kwa ishara na miujiza mikubwa atahubiri na kufanya maombi na maombezi kwa wagonjwa na wote wenye shida mbalimbali. Njoo upokeee muujiza wako kutoka kwa Mungu Mtenda miujiza. 0717583492 0785514127
#usajili | π πππππ ππππππππππ - Klabu za Ihefu SC na Geita gold FC Kwa pamoja zilifanya mazungumzo na meneja wa mshambuliaji Fiston abdulrazack juu ya uwezekano wa kumpata mshambuliaji huyo. Lakini mazungumzo hayo yalivunjika kutokana na klabu hizo kutoa ofa ambayo haikumridhisha Fiston. Coastal union nao wameonesha Nia ya kumhitaji mshambuliaji huyo, mazungumzo yanaendelea.
Khalid Aucho amempiga kiviko Ibrahim Ajibu kwenye mechi ya NBC Premier League baina Coastal Union vs Yanga. Mwamuzi Emmanuel Mwandembwa amempa Aucho kadi ya njano kutokana na mchezo usio wa kiungwana. Kitendo kama hiki kwenye mechi huwa kikitokea mwamuzi anatakiwa atoe kadi ya njano au kadi nyekundu au atoe msamaha? Karibu tuyajenge.
#NBCPL Namba 10 Analysed by @sistiinho Kwenye #MzizimaDerby leo nimeondoka na Perfomance bora ya namba 10 wa pande zote; - Stephanie Aziz Ki (Yanga Sc) - Feisal Salum (Azam Fc) π₯ Kwenye STRUCTURE za timu zao walitumikia nafasi zinazofanana β’ Aziz kwenye 4-2-3-1 ya Yanga alicheza; - Mbele ya viungo wawili wa kati, Aucho na Mudathir (double Pivot) - Katikati ya viungo wawili wa pembeni, Pacome na Max - Nyuma ya Mzize (Zone 14) β’ Feisal kwenye 4-2-3-1 ya Azam alicheza; - Mbele ya viungo wawili wakati, Bajana na Akamiko (double pivot) - Katikati ya viungo washambuliaji wa pembeni, Sillah na Sopu - Nyuma ya Dube (zone 14) π₯ Wote kwa pamoja walifanya MAJUKUMU yanayofanana kiuchezaji uwanjani π Majukumu ya Aziz Ki β’ Yanga ikishambulia - Alikuwa anaji-position nyuma ya viungo wa Azam, Akamiko na Bajana - Pia kuna nyakati Azam walikuwa wakitengeneza rest defence ya 2+3, mabeki wao wawili wa pembeni huingia ndani kuungana na Bajana mbele ya mabeki wawili wa kati, Ki Aziz alikuwakukabana nao - Alikuwa na jukumu la kusaidia timu kupenya β’ Yanga ikizuia - Wakianza kuzuia kuanzia mbele na muundo wa 4-2-3-1, Aziz Ki huwa kwenye mstari wa pili wa uzuiaji nyuma ya mshambuliaji, dhidi ya kiungo wa chini wa Azam - Kama Azam wakijenga shambulizi na viungo wawili wa chini Mudathir husaidia kuongengezeka usawa wa Ki (4-1-4-1) - Yanga wakizuia kwenye nusu yao, Ki huungana na Mzize kwenye mstari wa kwanza wa uzuiaji (4-4-2 low & mid block) π Majumukumu ya Feisal β’ Azam ikishambulia - Anaji-position nyuma ya viungo wa Yanga, dhidi ya Aucho na Muda - Pia kuna nyakati Yanga walikuwa wakitengeneza rest defence ya 2+1, Muda husogea mbele, Lomalisa na Job hupanda, Fei alikuwa dhidi ya Aucho mbele ya CB's - Alikuwa na jukumu la kusaidia timu kupenya β’ Azam ikizuia - Wakianza kuzuia kuanzia mbele na muundo wa 4-2-3-1, Fei huwa kwenye mstari wa pili wa uzuiaji nyuma ya mshambuliaji, dhidi ya kiungo wa chini wa Yanga - Azam ikizuia kwenye nusu yao muundo huwa
Singida Fountain Gate imemtambulisha rasmi kocha mpya, Ricardo Ferreira kutoka nchini Brazil π§π· kuchukua nafasi ya Mjerumani aliyehepa... Ana rekodi ya kufundisha vilabu vikubwa barani Afrika kwa mafanikio vikiwemo Al Hilal, Al Merrikh SC na Ismaily SC. Kocha Ricardo amesaini kandarasi ya mwaka mmoja sambamba na Msaidizi wake, Andrews Barbosa (Deco).
Jana nimeweka picha na maelezo ya huyu mwamba hapa Jukwaani. Nimaambulia matusi ya kutosha. Nikasema isiwe tabu acha nitafute video yake kisha niiweke hapa msikilize alichokisema huyu Mwamba. Kazi hii imefanya na chombo cha habari cha Soka 6. Sisi Famara Media tumechukua kwao. Ndio maana tumeweka kitu kinaitwa Credit: Soka 6 ((Chanzo Soka 6). "Msipende kusikia yake mnayoyataka tu, pia pendeni kusikiliza msiyoyataka".
#NgaoYaJamii | Plan B ya Gamondi ilivyowaua Azam Usiku @sistiinho π₯ Kwa dakika zaidi ya 60, baada ya mpango na uchaguzi wa wachezaji wa eneo la ushambuliaji kutoleta matokeo, benchi la ufundi la Yanga walikuja na suluhisho kwa majina na mpango na likalipa, uliofeli ni upi? - Kwenye mfumo wa 4-2-3-1, eneo la Yanga la mbele lilikuwa na viungo washambuliaji watatu, Skudu/Ngushi, Max na Farid nyuma ya mshambuliaji Kennedy Musonda - Hawa kwenye eneo la walishindwa kubadili Scoreboard mbele ya wazuiaji wa Azam ambao walizuia na mfumo wa 5-3-2 eneo hilo - Mabeki watatu wa kati,Manyama na Lusajo waliwa-track washambuliaji wa pembeni wa Yanga (Skudu/Ngushi na Max Farid ambao walifanya rotation za nafasi bila mafanikio), Sebo aki-deal na Musonda - Akamiko na Bajana walihakikisha hakuna space kubwa mbele ya mabeki wao kuruhusu viungo wa Yanga kuwa free kwenye Zone 14 - Sidibe na Chilambo walilinda Yao na Lomalisa kupita pembeni π₯Baada ya tathmini (Ongoing match analysis) Gamondi na timu yake walikuja na suluhisho hili kutokana na ubora na udhaifu wa Azam; π Udhaifu wa kipa na mabeki wa Azam under-pressure - Kipindi cha kwanza Yanga hawaku-apply pressure kubwa kwenye theluthi ya kwanza ya Azam wakijenga shambulizi - Baada ya wachezaji wa nyuma wa Azam, mebeki na kipa kuonyesha udhaifu kukaa na mpira wakiwa kwenye shinikizo (Press Resistance), Yanga wakaanza ku-Press kuanzia mbele, Bao la Mzize na moment zingine kadhaa yanashuhudia hili π Rotation ya Mzize na Ki Aziz mbele ba nyuma ya mabeki - Mzuze kwa ubora wake akilipa goli mgongo, Yanga walimtumia kama "Target Man", mipira mingi ya juu ilielekezwa kwake na ku-link kwa wenzake huku Ki Aziz akishambulia nafasi anayoiacha nyuma, hii ilisaidia kuwa-draw out of position mabeki wa Azam waliofanya man marking - Shuti la Mzize lililogonga mwamba na hata Movement ya goli la Aziz Ki lilihusisha u-Target Man wa Mzize yanashuhudia π Aziz Ki kuivunja Double Pivot ya Azam - Kiungo pacha ya Bajana n
BREAKING: Mkuu wa Mkoa wa Kagera Albert Chalamila amesema Ndege ya Precision Air iliyopata ajali wakati wa kutua Bukoba leo ilikuwa imebeba Watu 43 ambapo hadi sasa wameokolewa 26 tu na kupelekwa hospital ya Rufaa ya mkoa Kagera. Japo Mkuu wa Mkoa hajasema Watu hao waliokolewa vipi na muda gani, Mashuhuda wanasema huenda waliokolewa sekunde chache baada ya ajali kabla sehemu kubwa ya Ndege hiyo kufunikwa na maji, tunaendelea kufuatilia zaidi ili kupata taarifa kamili kutoka kwa Mamlaka. Kwa upande mwingine RC Chalamila amewaomba Wananchi kuendelea kuwa watulivu maana mawasiliano na Marubani walioko ndani ya ndege bado yanaendelea. Ndege hiyo ni ATR 42 yenye namba za usajili 5H BWF ambayo ilikua ikitokea Dar es salaam kuelekea Bukoba na ilikua na safari ya kurudi Dar es salaam kupitia Mwanza. Chanzo: Millard Ayo.
Kutoka Ukurasa wa Club Africain ya Tunisia leo kabla ya mechi yao Playoff baina ya Yanga na Club Africain. Umeona nini hapoo!!! Mimi nimeona wafu wanazozana...
JICHO LA MGALILAYA MECHI YA CHAMPIONS LEAGUE YANGA VS AL HILAL. 1. Mechi dume ya mabingwa wawili wa nchi mbili. Wanaume kweli kweli iliyoamuliwa Kwa sare ya 1-1. 2. HILAL wametuachia funzo Jinsi gani mechi ya ugenini inapaswa kuchezewa. Hawakuwa na mambo mengi ila walitimiza malengo Yao. 3. Yanga bado hawajajua Jinsi ya kuutumia uwanja wa nyumbani. Uwanja wa nyumbani huwezi kupata nafasi kumi ukaitumia Moja ambayo ni nusu nafasi. 4. Kuna kosa Nabi amelifanya la kumuacha Mwamnyeto nje. Kwa umbo lake na washambuliaji wa HILAL ambao sio wanyumbulifu Sana hii mechi ilimfaa. Kutokana na maumbo madogo ya mabeki wa YANGA walilazimika kuzuia kuzingatia wingi wa namba na hakukuwa na mtu Mmoja ambaye wangeweza kuamini ataruka juu na ikibidi kutumia Nguvu atataumia Nguvu. 5. Mayele anapaswa kupewa heshima anayostahili. Pamoja na kukosa nafasi mbili za wazi zaidi alifunga goli kwenye mazingira magumu. Kwa lugha ya kimpira tunasema alileta goli pasipokuwa na goli. 6. Mechi iliyotuonyesha Bado wachezaji wa Ligi yetu Kuna vitu wanapaswa kujifunza na kuanza Sasa kuachana na mpira wa kufurahisha majukwaa. 7. Kuna Muda wachezaji wa YANGA kuchukua maamuzi wakiwa na mpira mguuni na walipokuja kuyachukua Tayari walikuwa wamechelewa. 8. Daira ni mojawapo ya makipa wachache Duniani ambao wakati unaamini tumefungwa ndio anakudhihirishia Kwa nini yupo pale. Kama sio yeye pengine kingekuwa kinazungumzwa kitu kingine tofauti saa hizi. 9. Natamani kuwaona Yanga watakavyocheza kule Sudan baada ya kutoka vyumbani Harf time. Kuna kitu nataka Aidha nikiamini au nikifute kichwani mwangu. 10. HILAL wametuonyesha nini maana ya wachezaji Bora na wachezaji wenye majina makubwa. 11. Tujifunze kuheshimu mafanikio ya wengine na kuyachukulia Kwa Mtazamo chanya kutafuta Jinsi ya kuwafikia. Kuwabeza mdomoni haitusaidii chochote. Ukweli ni kwamba HILAL ni timu Bora kuliko timu zote zinazocheza Ligi yetu. 12. Mechi Bado haijaisha imemalizika kipindi kimoja Cha dakika 90 Bado zingine 90 kule Khatum
Hii kitaalamu inaitwaje?? ππ Mimi siwezi hii kabisaa unaweza kuvunjika mgongo bure kisa eti unajipima uzito!!