Famara Media

Famara Media Famara Media - Inform, Entertain and Educate.

MGONGANO WA MASLAHI WATIKISA UCHAGUZI FRAT MKOA: WADAU WA SOKA WAPAZA SAUTI.Kumekuwepo na sintofahamu kubwa ndani ya mch...
07/01/2026

MGONGANO WA MASLAHI WATIKISA UCHAGUZI FRAT MKOA: WADAU WA SOKA WAPAZA SAUTI.

Kumekuwepo na sintofahamu kubwa ndani ya mchakato wa uchaguzi wa FRAT Mkoa, kufuatia uteuzi wa Wakili Musa Nyamwelo kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya FRAT Mkoa, hali inayodaiwa kukiuka misingi ya haki, uwazi na kuepuka mgongano wa maslahi.

Wadau wa soka wamehoji vikali uteuzi huo wakibainisha kuwa Wakili Nyamwelo kwa sasa ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya MZFA, jambo linalozua maswali mazito kuhusu uwezekano wa Conflict of Interest katika mchakato mzima wa uchaguzi.

Kwa mujibu wa wadau hao, haijawahi kutokea katika historia ya soka la Tanzania, mtu mmoja kushika nafasi za juu za Kamati za Uchaguzi katika ngazi mbili tofauti kwa wakati mmoja. Mfano umetolewa wa Wakili Kiomoni Kibamba, ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi TFF na wakati huo huo hawezi kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi MZFA.

MKANGANYIKO NDANI YA KAMATI TENDAJI FRAT
Taarifa zinaeleza kuwa ndani ya Kamati Tendaji ya FRAT Mkoa kulikuwapo na mjadala mpana, ambapo wajumbe wengi walikubaliana kuwa Wakili Madukwa aendelee kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi, nafasi ambayo amekuwa akiishikilia hata katika uchaguzi uliopita uliofanyika Bwalo la Mgambo.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa Kamati Tendaji FRAT Mkoa, Emmanuel Mataba, anadaiwa kumteua Wakili Nyamwelo bila ridhaa ya wajumbe wa Kamati Tendaji, hatua iliyozua mpasuko na malalamiko makubwa miongoni mwa wajumbe.

TUHUMA ZA NJAMA NA MALALAMIKO YA NDANI
Taarifa zisizo rasmi (“za chini chini”) zinaeleza kuwa uteuzi wa Wakili Nyamwelo unadaiwa kuwa na lengo la kuwakata wagombea wengine ili kumwachia nafasi mgombea mmoja abakie peke yake, hali inayodaiwa kuhatarisha uhalali wa uchaguzi.

Aidha, baadhi ya wajumbe wa Kamati Tendaji ya FRAT Mkoa wanaomaliza muda wao wanadaiwa kupinga vikali uteuzi huo, wakieleza kuwa haukufuata taratibu za kikatiba na haukuhusisha jopo lote la Kamati Tendaji. Malalamiko hayo tayari yameripotiwa ngazi za juu kwa ajili ya uamuzi.

Jowi!!! Endelea kupumzika Baba....Baba while you were away!! there some ODM Leaders wali practice Siasa mbaya kwenye Cha...
07/01/2026

Jowi!!! Endelea kupumzika Baba....Baba while you were away!! there some ODM Leaders wali practice Siasa mbaya kwenye Chama yako.

Today, January 7, we mark what would have been the 81st birthday of the Right Honourable Raila Odinga, a patriot whose life was defined by courage, sacrifice, and an unyielding love for Kenya.

Baba taught us, time and again, that the country must always come before self, that no ambition is greater than our unity, and no victory more important than our peace.

He believed deeply in Kenya and never lost faith that our best days lie ahead. Whether in struggle or reconciliation, he chose stability over chaos, unity over division, and hope over despair.

As we remember him on his birthday, we celebrate not just the man but the enduring lessons he left us: To close ranks for the common good, to rise above partisanship, and to keep faith in the Kenyan dream.

06/01/2026

Kumbe DCP ni Mali ya Cleo Malala na Hezron Obaga? Riggy G ni Master of Ceremony "MC" tu.😁

05/01/2026

Sisi ndio Arsenal...Parade la nguvu kwa mashabiki wa Arsenal Sudan Kusini..😀 Mtafukuza makocha sana. Sisi haooo.

Tanzania imefungwa 1 - 0 na Morocco katika mechi ya raundi ya 16 na kuondolewa kwenye mashindano ya Afcon 2025 pale Moro...
04/01/2026

Tanzania imefungwa 1 - 0 na Morocco katika mechi ya raundi ya 16 na kuondolewa kwenye mashindano ya Afcon 2025 pale Morocco.

Gumzo kubwa ni maamuzi ya refarii uwanjani yameancha maswali mengi yasiokuwa majibu..Wengi wanasema amewaumiza Tanzania huko akiipendelea Morocco.

Wewe umeonaje mechi na maamuzi ya refarii huyu raia wa Mali?

04/01/2026

1 Mambo ya Nyakati 18:13

Naye BWANA akampa Daudi kushinda, kila alikokwenda.

02/01/2026

Francis Kahata, who has been training with KCB FC for the past few weeks, is likely to sign for the Bankers when the mid-season transfer window opens on Monday.

02/01/2026

Junior Khanye on Hugo Broos 👀😳

“If Hugo Broos loses to Cameroon on Sunday, he may be forced to leave Bafana Bafana.

"Because the pressure from former players, the media, and the fans would be overwhelming, along with the relentless questioning.”😬

MAKILAGI SPORTS WEAR YATOA SHUKRANI KWA WATEJA WAKE.Duka la vifaa vya michezo la Makilagi Sports Wear, lililopo katika o...
02/01/2026

MAKILAGI SPORTS WEAR YATOA SHUKRANI KWA WATEJA WAKE.

Duka la vifaa vya michezo la Makilagi Sports Wear, lililopo katika ofisi za Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, limetoa shukrani za dhati kwa wateja wake wote waliounga mkono huduma na bidhaa zake kwa kipindi cha mwaka 2025.

Akizungumza mwanzoni mwa mwaka mpya 2026, Mkurugenzi wa Makilagi Sports Wear, Bi. Sophia Makilagi, amesema mafanikio yaliyopatikana yametokana na imani na ushirikiano mkubwa kutoka kwa wateja wao wa ndani ya Mkoa wa Mwanza na nje ya mkoa.

Bi. Makilagi amesema katika mwaka 2025, duka hilo lilifanikiwa kuuza bidhaa mbalimbali za michezo zikiwemo jezi, mipira pamoja na vifaa vya mazoezi kwa wadau wengi wa michezo, hali iliyochangia ukuaji na uimara wa biashara hiyo.

“Tunamshukuru Mungu kwa kutuvusha salama mwaka 2025 na kutuwezesha kuanza mwaka mpya 2026 kwa mafanikio. Tunatoa shukrani za dhati kwa wateja wetu wote waliotufikia dukani pamoja na wale waliokuwa mbali waliotuamini kwa kuagiza bidhaa zetu. Tunaomba ushirikiano huu uendelee na uwe mkubwa zaidi katika mwaka huu wa 2026,” amesema Bi. Makilagi.

Katika wateja waliotoa mchango mkubwa kwa kununua mizigo kwa wingi mwaka 2025, Bi. Makilagi amewataja Mwenyekiti wa Copco FC, Simon Romli, Nyaitato Stephano Mwenyekiti wa Alliance Sports Academy Augustino Yassaya Mbogo ambaye ni Katibu wa CCM Wilaya ya Ngorongoro, pamoja na Wilbert Mweta Mkurugenzi wa Mweta Sports Centre, akisema walionesha mfano mzuri wa kuunga mkono biashara za ndani.

Aidha, Makilagi Sports Wear imeeleza mpango wake wa kuwaandalia Vyeti vya Shukrani wadau hao k**a sehemu ya kutambua mchango wao katika kusaidia kukuza duka hilo na maendeleo ya vifaa vya michezo Mkoa wa Mwanza.

Cc

01/01/2026

Hello

01/01/2026

Happy New Year 2026.

Address

Nyamagana
Mwanza
994

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Famara Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Famara Media:

Share