JAMII FM RADIO

JAMII FM RADIO JAMII FM ni kituo cha redio cha kijamii kilichoanza kutoa huduma mwezi Septemba 2016 kwa lengo la kuwapa jamii jukwaa la kuzungumzia maendeleo yao.

JAMII FM RADIO haitawajibika kwa maoni yatakayotolewa yenye kukiuka sheria za nchi. JAMII FM is a Community Radio that was launched in September 2016 for the purpose of giving community members particularly from rural areas access to information and means of communication. The programmes are basically focused on issues that directly or indirectly reflects community livelihood including people with

special needs. Through Jamii FM Radio, educational and developmental information is disseminated and exchanged; important local issues are aired; a free market place of ideas and opinions is opened up and people are given the opportunity to express themselves. Broad participation by community members is always encouraged in Program production. JAMII FM RADIO gives voice to the voiceless. Vision
The VISION of Jamii FM is to see the community of Lindi and Mtwara Regions particularly from rural areas have access to information and increased capacity to play a meaningful role for their own development through media. Mission
The MISSION is to enable local communities to use media as a tool for enhancing participatory communication in order to achieve sustainable rural development. Location
JAMII FM Radio Station is located at Naliendele area 9km from Mtwara Town along Mtwara-Newala road. The station is opposite to Naliendele Agriculture Research Institute. Coverage:
JAMII FM RADIO owns its 60 metres transmission tower that enables to reach the huge population from both Mtwara and Lindi regions, from Mtwara Municipal up to Nanyamba, Tandahimba, Newala, Nachingwea, Lindi and some parts along the boarder with neighbouring country-Mozambique. Programme Schedule
0600 – 1000hrs – Dira ya Asubuhi
1000 – 1300hrs – Kapu la Jamii
1300 – 1600hrs – Mchakamchaka
1600 -- 1610hrs – Habari (News Bulletin)
1610 – 1800hrs – Sauti ya Jamii
1800 – 1900hrs – Radio France International (RFI)
1900 – 1910hrs – Habari (News Bulletin)
1910 – 2000hrs – Dimba la Michezo (Sports)
2000 – 2100hrs – Makala Maalum
2100 – 2200hrs – Usiku Mwema
2200 – 0000hrs – Love Boat
0000 – 0600hrs – Music Mix

Location
https://www.google.co.tz/maps/place/Jamii+Fm+Radio/@-10.3559624,40.1615128,17z/data=!3m1!4b1!4m5!3m4!1s0x188d5a1f07878dd3:0x3a55ced2bafdf73e!8m2!3d-10.3559624!4d40.1637015?hl=en&hl=en

Wanafunzi wa Dar es Salaam Independent School (DIS) watembelea Jamii FMLeo, Oktoba 7, 2025, wanafunzi wa Kidato cha Pili...
07/10/2025

Wanafunzi wa Dar es Salaam Independent School (DIS) watembelea Jamii FM

Leo, Oktoba 7, 2025, wanafunzi wa Kidato cha Pili kutoka Dar es Salaam Independent School (DIS) wametembelea kituo chetu cha kurushia matangazo Jamii FM Radio, kilichopo Mtwara.

Ziara hii imelenga kuwapa wanafunzi ujuzi wa vitendo kuhusu ulimwengu wa vyombo vya habari, hususan redio na mitandao ya kijamii.

Akizungumza wakati wa ujio huo, Amua Rush*ta Meneja na Mtaalamu wa Masuala ya TEHAMA kutoka Jamii FM amesema kuwa wanafunzi hao wamekuja kujifunza namna mitandao ya kijamii inavyoathiri vyombo vya habari vya jadi (Traditional Media), pamoja na jinsi jamii inavyoweza kupata taarifa sahihi kupitia vyombo vya habari vinavyoaminika.

Ziara k**a hizi ni sehemu ya juhudi za DIS katika kuhamasisha vijana kujifunza, kuhoji, na kuelewa dunia ya habari kwa undani zaidi.

Unafahamu nini kuhusu uaminifu kwa vyombo vya habari katika kuleta habari bila kuwa na chembe ya uongo
07/10/2025

Unafahamu nini kuhusu uaminifu kwa vyombo vya habari katika kuleta habari bila kuwa na chembe ya uongo

Wanafunzi wa Kidato cha Pili wa Dar es Salaam Independent School wametembelea Jamii FM Radio Mtwara kujifunza kuhusu vyombo vya habari na athari za mitandao ya kijamii , ikiwa ni sehemu ya somo la Mtazamo wa Kidunia (Global Perspective) Na…

kwenye eneo lako, unapata nafasi ya kuwatembelea watoto wanaoishi katika vituo vya kulelea watoto?
02/10/2025

kwenye eneo lako, unapata nafasi ya kuwatembelea watoto wanaoishi katika vituo vya kulelea watoto?

Nabii Ncolous Suguye ametoa msaada wa viti mwendo na chakula kwa watoto wenye mahitaji maalum katika Kituo cha Upendo na Shule ya Msingi Rahaleo, Mtwara, kabla ya kuanza mkutano wa Injili utakaofanyika Oktoba 2, 2025, katika viwanja vya Sabasaba Na…

Unashiriki vipi kwenye Uzazi wa mpango, wewe na familia yako?
02/10/2025

Unashiriki vipi kwenye Uzazi wa mpango, wewe na familia yako?

Karibu usikilize makala maalum ya dakika 13 inayoangazia Umuhimu wa wanandoa kushiriki elimu ya uzazi wa mpango.Makala hii imeandaliwa kwa ushirikiano kati ya Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) na shirika la WELLSPRING, linalotekeleza mradi wa kutoa elimu…

KIPAZA 🎤Leo ni siku ya kimataifa ya wazee duniani. Tuambie wazee wanachangamoto gani katika jamii,  lakini pia  jamii in...
01/10/2025

KIPAZA 🎤
Leo ni siku ya kimataifa ya wazee duniani.

Tuambie wazee wanachangamoto gani katika jamii, lakini pia jamii ina mtazamo gani juu ya wazee katika kuboresha na kutatua changamoto zao?

MCHAKAMCHAKA SHOW JAMIIFM RADIO MTWARA 90.5 MHZ. 📻🎤

Je unafahamu mahitaji ya mgombea udiwani hasa mwanamke katika Siasa?
29/09/2025

Je unafahamu mahitaji ya mgombea udiwani hasa mwanamke katika Siasa?

Mgombea udiwani Kata ya Chuno kupitia CCM, Mariamu Chimbwahi, amewataka wanawake kuanza uongozi ngazi za chini ili kujijengea uzoefu, huku akihimiza ushirikiano baina yao na kushiriki katika shughuli za kiuchumi ili kujitegemea Na Musa Mtepa Wanawake wametakiwa kujitokeza kugombea nafasi…

Waandishi wa habari mtwara wakaa kitako kulonga mambo yao
27/09/2025

Waandishi wa habari mtwara wakaa kitako kulonga mambo yao

Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora imetoa mafunzo kwa waandishi wa habari mkoani Mtwara, ikiwataka kuzingatia maadili ya taaluma, haki za binadamu na misingi ya utawala bora, hasa kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025. Waandishi wameahidi kutumia mafunzo…

Watoto kuacha shule kwako kunaleta maana gani?
26/09/2025

Watoto kuacha shule kwako kunaleta maana gani?

Mdondoko wa wanafunzi na ukatili wa kijinsia vyatajwa kuchangia ongezeko la vitendo vinavyohatarisha amani katika jamii , huku wazazi wakilaumiwa kwa kulegeza majukumu ya malezi na ufuatiliaji wa watoto wao Na Musa Mtepa Mtwara, Septemba 24, 2025 – Ukatili wa…

KIPAZA 🎤Trowbackthursday   Tuambie wimbo gani wa kitambo unaukubali sana ukipigwa tu unahisi vibe👊🏽MCHAKAMCHAKA SHOW JAM...
25/09/2025

KIPAZA 🎤
Trowbackthursday
Tuambie wimbo gani wa kitambo unaukubali sana ukipigwa tu unahisi vibe👊🏽

MCHAKAMCHAKA SHOW JAMIIFM RADIO MTWARA
90.5 MHZ 📻
Dropisha wimbo wako pendwa hapo 💪🏾

Hali ya Umeme kutengemaa sasa Mtwara
23/09/2025

Hali ya Umeme kutengemaa sasa Mtwara

TANESCO kuongeza uzalishaji wa umeme kwa MW 20 katika kituo cha Hiari, Mtwara, kukabiliana na upungufu wa umeme Lindi na Mtwara. Mashine mpya itakamilika ndani ya mwezi mmoja, ikiongeza uzalishaji hadi MW 70 Na Musa Mtepa Mtwara, Tanzania – Shirika…

MLINZI AKAMATWA KWA TUHUMA ZA WIZI WA PIKIPIKI UWANJA WA NDEGE KILWA MASOKOJeshi la Polisi mkoani Lindi, kwa kushirikian...
20/09/2025

MLINZI AKAMATWA KWA TUHUMA ZA WIZI WA PIKIPIKI UWANJA WA NDEGE KILWA MASOKO

Jeshi la Polisi mkoani Lindi, kwa kushirikiana na wenzao wa Mkoa wa Mtwara, Septemba 20,2025 limemk**ata Shaa Athuman Mohamed (20), mlinzi wa uwanja wa ndege wa Kilwa Masoko, kwa tuhuma za kuiba pikipiki aina ya TVS yenye namba za usajili STN 2790, mali ya kiwanja hicho.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, Kamishna Msaidizi wa Polisi John Imori, mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo mnamo Septemba 16, 2025, akiwa zamu kazini katika uwanja wa ndege huo. Inadaiwa kuwa baada ya kutekeleza wizi huo, alitoweka na pikipiki hiyo na kuiacha kazi bila taarifa.

Kamanda Imori amesema kuwa baada ya tukio hilo, mamlaka ya uwanja huo wa ndege ilifungua jalada la kesi KLM/IR/429/2025 katika Kituo cha Polisi Kilwa kwa kosa la wizi, na kuanza msako mkali wa kumnasa mtuhumiwa.

Mtuhumiwa alik**atwa tarehe 20 Septemba, 2025 katika mtaa wa Mkomaindo, Wilaya ya Masasi mkoani Mtwara, akiwa katika harakati za kujaribu kuiuza pikipiki hiyo. Kuk**atwa kwake kulifanikishwa na mtego uliowekwa na askari polisi, ambao ulipelekea kumtia mbaroni bila shaka.

Baada ya kuk**atwa, Shaa aliwaongoza askari hadi eneo alilokuwa ameificha pikipiki hiyo, ambapo alionyesha namba kamili ya usajili kabla ya mali hiyo kupatikana kichakani.

Mtuhumiwa huyo ambaye ni mfanyakazi wa kampuni ya ulinzi ya INSIGHT aliyekuwa akilinda katika uwanja wa ndege wa Kilwa Masoko, anatarajiwa kufikishwa mahak**ani mara baada ya taratibu za upelelezi kukamilika.

Jeshi la Polisi limewataka wananchi kuendelea kushirikiana na vyombo vya dola kwa kutoa taarifa za uhalifu ili kuimarisha usalama katika maeneo yao.

NINI MADHARA YA KUTOHUFHURIA KLINIKI KWA WAKATI  KWA MAMA  MJAMZITOKushiriki kipindi hiki Piga na tuma ujumbe mfupi wa m...
18/09/2025

NINI MADHARA YA KUTOHUFHURIA KLINIKI KWA WAKATI KWA MAMA MJAMZITO

Kushiriki kipindi hiki
Piga na tuma ujumbe mfupi wa maandishi (SMS)
Kupitia namba ya simu 0717 841 929 au Komenti hapa na ujumbe wako utasomwa Mubashara kwenye kipindi.

Address

Naliendele, Mtwara/
Mtwara

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when JAMII FM RADIO posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to JAMII FM RADIO:

Share

Category