JAMII FM RADIO

JAMII FM RADIO JAMII FM ni kituo cha redio cha kijamii kilichoanza kutoa huduma mwezi Septemba 2016 kwa lengo la kuwapa jamii jukwaa la kuzungumzia maendeleo yao.

JAMII FM RADIO haitawajibika kwa maoni yatakayotolewa yenye kukiuka sheria za nchi. JAMII FM is a Community Radio that was launched in September 2016 for the purpose of giving community members particularly from rural areas access to information and means of communication. The programmes are basically focused on issues that directly or indirectly reflects community livelihood including people with

special needs. Through Jamii FM Radio, educational and developmental information is disseminated and exchanged; important local issues are aired; a free market place of ideas and opinions is opened up and people are given the opportunity to express themselves. Broad participation by community members is always encouraged in Program production. JAMII FM RADIO gives voice to the voiceless. Vision
The VISION of Jamii FM is to see the community of Lindi and Mtwara Regions particularly from rural areas have access to information and increased capacity to play a meaningful role for their own development through media. Mission
The MISSION is to enable local communities to use media as a tool for enhancing participatory communication in order to achieve sustainable rural development. Location
JAMII FM Radio Station is located at Naliendele area 9km from Mtwara Town along Mtwara-Newala road. The station is opposite to Naliendele Agriculture Research Institute. Coverage:
JAMII FM RADIO owns its 60 metres transmission tower that enables to reach the huge population from both Mtwara and Lindi regions, from Mtwara Municipal up to Nanyamba, Tandahimba, Newala, Nachingwea, Lindi and some parts along the boarder with neighbouring country-Mozambique. Programme Schedule
0600 – 1000hrs – Dira ya Asubuhi
1000 – 1300hrs – Kapu la Jamii
1300 – 1600hrs – Mchakamchaka
1600 -- 1610hrs – Habari (News Bulletin)
1610 – 1800hrs – Sauti ya Jamii
1800 – 1900hrs – Radio France International (RFI)
1900 – 1910hrs – Habari (News Bulletin)
1910 – 2000hrs – Dimba la Michezo (Sports)
2000 – 2100hrs – Makala Maalum
2100 – 2200hrs – Usiku Mwema
2200 – 0000hrs – Love Boat
0000 – 0600hrs – Music Mix

Location
https://www.google.co.tz/maps/place/Jamii+Fm+Radio/@-10.3559624,40.1615128,17z/data=!3m1!4b1!4m5!3m4!1s0x188d5a1f07878dd3:0x3a55ced2bafdf73e!8m2!3d-10.3559624!4d40.1637015?hl=en&hl=en

Kwenye mkoa wako, ni mbinu gani inatumika kuhamasisha watu kwenda kupiga kura??
25/10/2025

Kwenye mkoa wako, ni mbinu gani inatumika kuhamasisha watu kwenda kupiga kura??

Vikundi kumi vya jogging Mtwara Mikindani vimeshiriki mbio fupi kuhamasisha ushiriki wa wananchi katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025, zikiwa na kaulimbiu “Mazoezi kwa Afya, Uchaguzi wa Amani ni Msingi wa Maendeleo.” Na Musa Mtepa MTWARA-Vikundi kumi vya jogging kutoka…

Zikiwa zimesalia siku 6 Kuelekea siku ya Uchaguzi Mkuu Oktoba 29,2025 Mkoa wa Mtwara upo salama kwa Wananchi kupiga kura...
23/10/2025

Zikiwa zimesalia siku 6 Kuelekea siku ya Uchaguzi Mkuu Oktoba 29,2025 Mkoa wa Mtwara upo salama kwa Wananchi kupiga kura kwa amani na utulivu.

Akizungumza na Jamii FM Radio Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara Kamishna msaidizi mwandamizi Issa Juma Suleiman amesema Mkoa uko salama kuelekea uchaguzi Mkuu na Baada ya uchaguzi.

Kamanda Suleiman amesema kila mwananchi wa Mtwara anapaswa kufahamu umuhimu wa kumlinda na kuimarisha Amani, utulivu na usalama kwa kipindi cha uchaguzi na baada ya uchaguzi.

Ameongeza kuwa kwasasa Mkoa wa Mtwara hauna kiashiria chochote cha maandamano na amewatoa hofu wananchi kuwa ikifika oktoba 29, 2025 wajitokeze kwa wingi kwenda kupiga kura na kurudi Nyumbani ili kusibiri matokeo.

Kamanda Suleiman amewaasa vijana kuacha mihemko ya uvunjifu wa amani na wala wasiwasikilize watu wasioitakia amani nchi yetu, na atakayekiuka Jeshi la Polisi halitasita kumchukulia hatua za kisheria.


21/10/2025

Dkt Samia: Msiogope hakuna maandamano siku ya uchaguzi

Mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt Samia Suluhu Hassan amewahakikishia Watanzania kuwa, siku ya Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, hakutakuwa na maandamano zaidi ya kushuhudiwa wananchi wakienda kupiga kura.

Amelisisitiza hilo, akisema kwa kuwa yeye ndiye Amiri Jeshi Mkuu na ndiye Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, siku hiyo hakutashuhudiwa maandamano wala tishio lolote la kiusalama.

Dkt Samia ametoa hakikisho hilo, leo Jumanne Oktoba 21, 2025 alipozungumza katika mkutano wake wa kampeni uliofanyika katika Viwanja vya Leader Club, Kinondoni, jijini Dar es Salaam.

“Ninaye ongeza hapa ndiye Rais wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa nchi hii. Nataka niwaambie maandamano yatakayokuwepo ni watu kwenda vituoni kupiga kura.

“Hakuna maandamano mengine yatakayokuwepo, hakuna tishio la kiusalama litakalokuwepo, anayesema ni Amiri Jeshi Mkuu wa nchi hii, niwaombe ndugu zangu, twendeni mkapige kura,” amesema.

Amesema kila mwananchi anapotoka kwenda kupiga kura anapaswa kuambatana na mwenzake aliyeandikishwa, kisha arudi nyumbani kwa usalama.

Umejiaanda na msimu mpya wa korosho 2025/2026??
20/10/2025

Umejiaanda na msimu mpya wa korosho 2025/2026??

Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) imetangaza kuwa minada ya korosho kwa msimu wa 2025/2026 itaanza Oktoba 31, 2025. Wakulima wametakiwa kuzingatia ubora wa korosho na kuepuka kuuza kwa kangomba, huku minada ikiendeshwa kwa njia ya mtandaoni chini ya usimamizi wa…

Dkt Samia aahidi ujenzi Barabara Kibiti-MtumbaMgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt Samia Suluhu Ha...
20/10/2025

Dkt Samia aahidi ujenzi Barabara Kibiti-Mtumba

Mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt Samia Suluhu Hassan amesema katika miaka mitano ijayo, Serikali yake itajenga Barabara ya Bungu-Nyamisati, Kibiti-Mtumba na Rufiji-Mbwela.

Dkt Samia ametoa ahadi hiyo leo, Jumatatu Oktoba 20, 2025 alipozungumza na wananchi wa Kibiti mkoani Pwani, katika mkutano wake wa kampeni za urais.

Ameahidi kujenga Barabara ya Bungu-Nyamisati, Kibiti-Mtumba, Rufiji-Mbwela na kuboresha barabara za ndani zikiwemo kilomi 42 za maeneo korofi ili zitumike misimu yote.

Dkt Samia amesema miradi ya maji 23 imekamilishwa wilayani humo na kuongeza upatikanaji wa huduma hiyo kutoka asilimia 47 hadi 74 na kwamba ataendelea kuboresha kuhakikisha wananchi wanapata maji zaidi Kibiti.

20/10/2025
18/10/2025

Dkt Samia aahidi Barabara, soko Namanyere

Mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt Samia Suluhu Hassan amesema katika miaka mitano ijayo, atajenga kwa kiwango cha lami, Barabara ya Namanyere-Kizwite-Chelanganya katika Mji wa Namanyere mkoani Rukwa.

Sambamba na mradi huo, ameahidi kujenga soko la kisasa na stendi ya mabasi zinazoendana na hadhi ya Mji wa Namanyere mkoani humo.

Dkt Samia ametoa ahadi hizo leo, Jumamosi Oktoba 18, 2025 katika mkutano wake wa kampeni za urais, uliofanyika Namanyere mkoani Rukwa.

Amesema Serikali yake itajenga Namanyere-Kizwite-Chelanganya na kuweka taa 270 za barabarani ili kuwawezesha wafanyabiashara wa eneo hilo, kufanya shughuli zao kwa saa 24.

Sambamba na barabara hiyo, amesema pia atajenga Barabara ya Mjimwema-Itekesya, kwa kiwango cha changarawe, huku akiwahakikishia wananchi wanaodai fidia zitalipwa baada ya uhakiki.

Kuhusu maji, amesema vyanzo vilivyopo wilayani Nkasi havikidhi mahitaji, hivyo wanakuja na mradi wa maji unaotoka Ziwa Tanganyika.

Pia, ameahidi kujenga stendi ya mabasi na soko la kisasa linaloendana na hadhi ya Mji wa Namanyere mkoani humo, ili kukuza fursa za biashara na uchumi kwa wananchi.

16/10/2025

TANGAZO: Kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025

WENJE ATIMKIA CCMAliyekuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Kanda ya Ziwa, Mbunge Mstaafu na Mjum...
13/10/2025

WENJE ATIMKIA CCM

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Kanda ya Ziwa, Mbunge Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama hicho Bw. Ezekia Dibogo Wenje ametangaza kukihama Chama hicho na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi CCM, akisema "Kwa miaka 15 iliyopita nimekuwa Ligi daraja la Kwanza na sasa nimeamua kujiunga na Ligi Kuu."

Wenje ametangaza maamuzi hayo leo Jumatatu Oktoba 13, 2025 kwenye Mkutano wa Kampeni za Mgombea Urais wa Chama Hicho Dkt. Samia Suluhu Hassan, Chato Mkoani Geita na kupokelewa na Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Asharose Migiro, akimpongeza pia Dkt. Samia na Chama Cha Mapinduzi kwa kuendelea kusimamia amani na utulivu wa Tanzania suala ambalo limewezesha upigaji wa hatua kubwa za maendeleo na ustawi.

Aidha Wenje ameeleza pia kuhusu madai kuwa serikali ya Chama Cha Mapinduzi CCM imekizuia Chadema kushiriki uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, akisema maamuzi ya Vikao vya Chama hicho pamoja na kuhofia kushindwa vibaya dhidi ya Chama Cha Mapinduzi ndiyo yaliyokiondoa Chama hicho kuweza kushiriki katika uchaguzi Mkuu ujao.

"Tarehe 20 Januari mwaka huu tulikutana tukafanya kitu kinaitwa Baraza kuu la Chama. Baraza likatoa mapendekezo tukapeleka kwenye Mkutano Mkuu wa Chadema, wote tukakubaliane Chadema hatushiriki Uchaguzi.Tulishauriwa mpaka na wazee wa maana duniani akiwemo Raila Odinga naye, akawaambia duniani hapa wampe mfano wowote Afrika wa Chama ambacho kiliwahi kususia uchaguzi halafu bado kikaendelea kuwepo. Kwahiyo Mhe. Rais mimi nimechoka kukunja ngumi na kwa miaka 15 nimekuwa kwenye ligi daraja la kwanza na leo nimeamua kuja ligi kuu rasmi." Amekaririwa Bw. Wenje

Wanafunzi wa Dar es Salaam Independent School (DIS) watembelea Jamii FMLeo, Oktoba 7, 2025, wanafunzi wa Kidato cha Pili...
07/10/2025

Wanafunzi wa Dar es Salaam Independent School (DIS) watembelea Jamii FM

Leo, Oktoba 7, 2025, wanafunzi wa Kidato cha Pili kutoka Dar es Salaam Independent School (DIS) wametembelea kituo chetu cha kurushia matangazo Jamii FM Radio, kilichopo Mtwara.

Ziara hii imelenga kuwapa wanafunzi ujuzi wa vitendo kuhusu ulimwengu wa vyombo vya habari, hususan redio na mitandao ya kijamii.

Akizungumza wakati wa ujio huo, Amua Rush*ta Meneja na Mtaalamu wa Masuala ya TEHAMA kutoka Jamii FM amesema kuwa wanafunzi hao wamekuja kujifunza namna mitandao ya kijamii inavyoathiri vyombo vya habari vya jadi (Traditional Media), pamoja na jinsi jamii inavyoweza kupata taarifa sahihi kupitia vyombo vya habari vinavyoaminika.

Ziara k**a hizi ni sehemu ya juhudi za DIS katika kuhamasisha vijana kujifunza, kuhoji, na kuelewa dunia ya habari kwa undani zaidi.

Unafahamu nini kuhusu uaminifu kwa vyombo vya habari katika kuleta habari bila kuwa na chembe ya uongo
07/10/2025

Unafahamu nini kuhusu uaminifu kwa vyombo vya habari katika kuleta habari bila kuwa na chembe ya uongo

Wanafunzi wa Kidato cha Pili wa Dar es Salaam Independent School wametembelea Jamii FM Radio Mtwara kujifunza kuhusu vyombo vya habari na athari za mitandao ya kijamii , ikiwa ni sehemu ya somo la Mtazamo wa Kidunia (Global Perspective) Na…

kwenye eneo lako, unapata nafasi ya kuwatembelea watoto wanaoishi katika vituo vya kulelea watoto?
02/10/2025

kwenye eneo lako, unapata nafasi ya kuwatembelea watoto wanaoishi katika vituo vya kulelea watoto?

Nabii Ncolous Suguye ametoa msaada wa viti mwendo na chakula kwa watoto wenye mahitaji maalum katika Kituo cha Upendo na Shule ya Msingi Rahaleo, Mtwara, kabla ya kuanza mkutano wa Injili utakaofanyika Oktoba 2, 2025, katika viwanja vya Sabasaba Na…

Address

Naliendele, Mtwara/
Mtwara

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when JAMII FM RADIO posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to JAMII FM RADIO:

Share

Category