
07/10/2025
Wanafunzi wa Dar es Salaam Independent School (DIS) watembelea Jamii FM
Leo, Oktoba 7, 2025, wanafunzi wa Kidato cha Pili kutoka Dar es Salaam Independent School (DIS) wametembelea kituo chetu cha kurushia matangazo Jamii FM Radio, kilichopo Mtwara.
Ziara hii imelenga kuwapa wanafunzi ujuzi wa vitendo kuhusu ulimwengu wa vyombo vya habari, hususan redio na mitandao ya kijamii.
Akizungumza wakati wa ujio huo, Amua Rush*ta Meneja na Mtaalamu wa Masuala ya TEHAMA kutoka Jamii FM amesema kuwa wanafunzi hao wamekuja kujifunza namna mitandao ya kijamii inavyoathiri vyombo vya habari vya jadi (Traditional Media), pamoja na jinsi jamii inavyoweza kupata taarifa sahihi kupitia vyombo vya habari vinavyoaminika.
Ziara k**a hizi ni sehemu ya juhudi za DIS katika kuhamasisha vijana kujifunza, kuhoji, na kuelewa dunia ya habari kwa undani zaidi.