JAMII FM RADIO

  • Home
  • JAMII FM RADIO

JAMII FM RADIO JAMII FM ni kituo cha redio cha kijamii kilichoanza kutoa huduma mwezi Septemba 2016 kwa lengo la kuwapa jamii jukwaa la kuzungumzia maendeleo yao.

JAMII FM RADIO haitawajibika kwa maoni yatakayotolewa yenye kukiuka sheria za nchi. JAMII FM is a Community Radio that was launched in September 2016 for the purpose of giving community members particularly from rural areas access to information and means of communication. The programmes are basically focused on issues that directly or indirectly reflects community livelihood including people with

special needs. Through Jamii FM Radio, educational and developmental information is disseminated and exchanged; important local issues are aired; a free market place of ideas and opinions is opened up and people are given the opportunity to express themselves. Broad participation by community members is always encouraged in Program production. JAMII FM RADIO gives voice to the voiceless. Vision
The VISION of Jamii FM is to see the community of Lindi and Mtwara Regions particularly from rural areas have access to information and increased capacity to play a meaningful role for their own development through media. Mission
The MISSION is to enable local communities to use media as a tool for enhancing participatory communication in order to achieve sustainable rural development. Location
JAMII FM Radio Station is located at Naliendele area 9km from Mtwara Town along Mtwara-Newala road. The station is opposite to Naliendele Agriculture Research Institute. Coverage:
JAMII FM RADIO owns its 60 metres transmission tower that enables to reach the huge population from both Mtwara and Lindi regions, from Mtwara Municipal up to Nanyamba, Tandahimba, Newala, Nachingwea, Lindi and some parts along the boarder with neighbouring country-Mozambique. Programme Schedule
0600 – 1000hrs – Dira ya Asubuhi
1000 – 1300hrs – Kapu la Jamii
1300 – 1600hrs – Mchakamchaka
1600 -- 1610hrs – Habari (News Bulletin)
1610 – 1800hrs – Sauti ya Jamii
1800 – 1900hrs – Radio France International (RFI)
1900 – 1910hrs – Habari (News Bulletin)
1910 – 2000hrs – Dimba la Michezo (Sports)
2000 – 2100hrs – Makala Maalum
2100 – 2200hrs – Usiku Mwema
2200 – 0000hrs – Love Boat
0000 – 0600hrs – Music Mix

Location
https://www.google.co.tz/maps/place/Jamii+Fm+Radio/@-10.3559624,40.1615128,17z/data=!3m1!4b1!4m5!3m4!1s0x188d5a1f07878dd3:0x3a55ced2bafdf73e!8m2!3d-10.3559624!4d40.1637015?hl=en&hl=en

JESHI LA POLISI WAANZA UCHUNGUZI VIDEO YA MTOTO KUPEWA POMBE Jeshi la Polisi Tanzania limeeleza kusikitishwa na video in...
06/09/2025

JESHI LA POLISI WAANZA UCHUNGUZI VIDEO YA MTOTO KUPEWA POMBE



Jeshi la Polisi Tanzania limeeleza kusikitishwa na video inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii, inayoonesha mwanamke mmoja akimnywesha pombe mtoto mdogo.

Kitendo hicho kinatajwa kuwa ni ukatili wa hali ya juu dhidi ya mtoto, na ni kosa la jinai linalokiuka sheria za nchi.

Kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi hilo iliyotolea leo September 6,2025, tukio hilo linakiuka Sheria ya Mtoto, Sura ya 13 pamoja na marekebisho ya mwaka 2023 kifungu cha 9(3) na 13, na pia Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura ya 16 kifungu cha 169A, k**a ilivyorekebishwa mwaka 2023.

Jeshi la Polisi limesema uchunguzi wa kina umeanza mara moja, ili kubaini iwapo tukio hilo limetokea ndani ya mipaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na kuhakikisha mhusika anapatikana na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Jeshi hilo pia linatoa wito kwa yeyote anayemfahamu mwanamke huyo kutoa taarifa kwa njia yoyote ile iliyo rahisi kwake, au kupitia namba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi, 0699 998899.

Aidha, mwanamke huyo ametakiwa kujisalimisha mwenyewe katika kituo chochote cha Polisi mara tu atakapoona taarifa hii.

Jeshi la Polisi linakemea vikali vitendo vya ukatili dhidi ya watoto, na linaendelea kusisitiza kuwa litaendelea kuchukua hatua kwa mujibu wa sheria ili kulinda haki na ustawi wa watoto wote nchini.

Karibu upate ELIMU Kupitia Radio yetuChildren in Crossfire
06/09/2025

Karibu upate ELIMU Kupitia Radio yetu
Children in Crossfire

JWTZ yaadhimisha miaka 61 kwa shughuli za kijamii na michezo Mtwara
01/09/2025

JWTZ yaadhimisha miaka 61 kwa shughuli za kijamii na michezo Mtwara

JWTZ limeadhimisha miaka 61 tangu kuanzishwa kwake kwa kushiriki shughuli za kijamii ikiwemo uchangiaji damu na mpira wa kirafiki dhidi ya Jeshi la Polisi, katika viwanja vya Nangwanda Sijaona, Mtwara Na Musa Mtepa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ) leo…

Ijumaa hii usikose kututegea sikio
28/08/2025

Ijumaa hii usikose kututegea sikio

KIPAZA 🎤Unaridhika na huduma ya Dj's wanavyopiga muziki katika kumbi za starehe kwa % ngapi hapo ulipo?  TROWBACK THURSD...
28/08/2025

KIPAZA 🎤
Unaridhika na huduma ya Dj's wanavyopiga muziki katika kumbi za starehe kwa % ngapi hapo ulipo?

TROWBACK THURSDAY REQUEST NGOMA KALI YA KITAMBO WASHTUE WANA👊🏽
SHOW JAMIIFM RADIO 🎼
90.5 MHZ MTWARA 📻

🎤

KIPAZA 🎤Kwanini baadhi ya watu wamekua  wakitumia kiasi kikubwa cha pesa kwenye maswala ya sherehe na unyago kuliko kuwe...
22/08/2025

KIPAZA 🎤
Kwanini baadhi ya watu wamekua wakitumia kiasi kikubwa cha pesa kwenye maswala ya sherehe na unyago kuliko kuwekeza kwenye elimu?

SIKILIZA KIPINDI CHA MCHAKAMCHAKA HAPA JAMII FM RADIO 90.5 MHZ MTWARA 📻

Online radio link
👉🏾 radiotadio.co.tz/jamiifm

Budah 🎤

Wanachama CCM Msimbati watishia kujiondoa uanachama
18/08/2025

Wanachama CCM Msimbati watishia kujiondoa uanachama

Wanachama zaidi ya 150 wa CCM Msimbati wamelalamikia kuondolewa kwa jina la Rashidi Linkoni aliyeshinda kura za maoni, wakitishia kurudisha kadi zao, huku viongozi wa wilaya wakisisitiza maamuzi ya k**ati ya siasa Na Musa Mtepa Zaidi ya wanachama 150 wa…

Inasemekena Mitandao ya kijamii na malezi duni inasababisha mmomonyoko wa maadili Mtwara, wewe una lipi la kusema juu ya...
18/08/2025

Inasemekena Mitandao ya kijamii na malezi duni inasababisha mmomonyoko wa maadili Mtwara, wewe una lipi la kusema juu ya jambo hili

Kongamano limebainisha kuwa malezi duni, matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii na kuiga tamaduni za kigeni vinachangia mmomonyoko wa maadili na ongezeko la ukatili dhidi ya watoto, likitoa wito kwa jamii kurejesha malezi imara Na Musa Mtepa Matumizi mabaya ya…

KIPAZA 🎤Kuna Mstari una sema "Tuliza moyo wako, Kubali mapungufu yako, Rahisisha mahitaji yako, ongeza kipato chako, Chu...
18/08/2025

KIPAZA 🎤
Kuna Mstari una sema "Tuliza moyo wako, Kubali mapungufu yako, Rahisisha mahitaji yako, ongeza kipato chako, Chunga tamaa mbaya".

Wimbo wa msanii gani?
🎼

MchakaMchaka Show
JAMIIFM RADIO 90.5 MHZ MTWARA

WANDISHI WA HABARI WAKUMBUSHWA KUZINGATIA WELEDI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025Waandishi wa habari nchini wametakiwa kuwa m...
15/08/2025

WANDISHI WA HABARI WAKUMBUSHWA KUZINGATIA WELEDI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025

Waandishi wa habari nchini wametakiwa kuwa makini na kuzingatia weledi wa taaluma yao, hususani wakati huu wa kuelekea katika kipindi cha uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29,2025.

Wito huo umetolewa Agosti 15, 2025, na mkufunzi Amua Rush*ta wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari wa kituo cha Jamii FM Redio kuhusu ulinzi na usalama katika kipindi cha uchaguzi.

Mafunzo haya ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari ni sehemu ya mradi wa usalama wa mwandishi wa habari kuelekea uchaguzi mkuu 2925, yanayosimamiwa na umoja wa Klabu za waandishi wa habari nchini (UTPC).

Bw. Amua amesema kuwa waandishi wanapaswa kuchukua tahadhari wanapokuwa kazini ili kuepuka hatari zinazoweza kujitokeza.

Amesema mafunzo hayo yamejikita katika maeneo matatu makuu: kuzingatia taratibu wakati wa kuhudhuria mikutano ya vyama vya siasa, kujikinga na uhalifu mtandaoni kupitia vifaa vya kidijitali, na kuimarisha ustawi wa kisaikolojia kwa waandishi wa habari wakiwa kazini.

Waandishi wa habari wa Jamii FM Redio, Shaibu Omari na Msafiri Kipila, wameeleza kufurahia mafunzo hayo, wakisema yamegusa moja kwa moja namna ya kuboresha usalama wao na kufuata taratibu sahihi wakati wa mchakato wa uchaguzi.





KIPAZA🎤Unampa ushauri gani muhimu wa kuzingatia kijana mwenzako anayejitafuta katika maisha  ili aweze kujipata?Trowback...
14/08/2025

KIPAZA🎤
Unampa ushauri gani muhimu wa kuzingatia kijana mwenzako anayejitafuta katika maisha ili aweze kujipata?

Trowbackthursday Request ngoma ya kitambo unayoikubali sana then watag wana.

MCHAKAMCHAKA SHOW JAMIIFM RADIO 90.5 MHZ MTWARA.
🎤

MBARONI KWA WIZI WA PIKIPIKI MKOANI LINDIJeshi la Polisi mkoa wa Lindi linamshikilia Hamis Malimu Swahiba (25), mkazi wa...
14/08/2025

MBARONI KWA WIZI WA PIKIPIKI MKOANI LINDI

Jeshi la Polisi mkoa wa Lindi linamshikilia Hamis Malimu Swahiba (25), mkazi wa Rufiji mkoa wa Pwani, kwa tuhuma za kuiba pikipiki aina ya Boxer yenye namba za usajili MC.339 FCJ.

Tukio hilo lilitokea tarehe 12 Agosti 2025 katika eneo la Somanga, wilayani Kilwa, ambapo inadaiwa kuwa mtuhumiwa alitoroka na pikipiki hiyo baada ya dereva wake, Salumu Mohamed (20), kuiacha kwa muda nje ya duka akiwa ameiacha na funguo zake kwa lengo la kupata chenji ya kumrudishia mtuhumiwa.

Baada ya tukio hilo, Jeshi la Polisi lilianzisha msako mkali uliowezesha kuk**atwa kwa mtuhumiwa tarehe 13 Agosti 2025 katika eneo hilo hilo la Somanga, akiwa katika harakati za kuisafirisha pikipiki hiyo kuelekea mkoa mwingine kwa lengo la kuwauzia watu wasiojulikana.

Jeshi la Polisi linaendelea na upelelezi, na mara baada ya kukamilika, mtuhumiwa atafikishwa mahak**ani kujibu mashtaka dhidi yake.

Aidha, Polisi wamewataka madereva bodaboda kuwa waangalifu na abiria wasiowafahamu, kuepuka kuwaamini kiholela, na kuhakikisha wanatoa funguo za pikipiki kila wanaposimama ili kujiepusha na matukio ya aina hiyo.

Address

Naliendele, Mtwara/

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when JAMII FM RADIO posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to JAMII FM RADIO:

  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share