Nondo za Mhe. Dkt. Charles Kimei, Mbunge wa Jimbo la Vunjo akichangia Bajeti ya Wizara ya Fedha na Mipango leo tarehe 17 June 2022.
MHE. DKT. KIMEI (MB) AHOJI SERIKALI ITAANZA LINI UJENZI WA SOKO LA KIMATAIFA LOKOLOVA.
Leo tarehe 30/05/2022, Mhe. Dkt. Charles Stephen Kimei, Mbunge wa Jimbo la Vunjo katika kipindi cha maswali na majibu kwa Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara ameuliza swali la msingi pamoja na maswali ya nyongeza.
Swali la msingi;
"Ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Soko la Kimataifa katika Eneo la Lokolova mpakani mwa Tanzania na Kenya??.
Majibu ya Serikali kupitia kwa Naibu Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara Mhe. Exaud S. Kigahe Alisema;
" Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Moshi imetenga eneo lenye ukubwa wa Ekari 140 katika Eneo la Lokolova kwa ajili ya ujenzi wa Soko la mpakani..."
"Hatua inayofuata ni kupata Hatimiliki ya Eneo hilo na hatimaye kutenga Fedha kwa ajili ya Miundombinu ya Soko husika".
Aidha , Mhe. Mbunge, aliweza kuuliza maswali mawili ya ngongeza kama ifuatavyo (Tizama video). 👇
TULIAHIDI, TUNATEKELEZA KWA VITENDO. VIVA MHE. RAIS SAMIA SULUHU HASSAN, VIVA MHE. DKT. CHARLES KIMEI (MB),. TUNAENDELEA KUMTUA MAMA NDOO KICHWANI. 👏👏👏🙏
1/4: Viongozi wa Dini ya Kiislamu Jimbo la Vunjo wakitoa maoni baada ya kupokea sadaka ya Mhe. Dr. Kimei (MB).
MKUU WA WILAYA YA MOSHI MHE. ABBAS KAYANDA AMETOA MAELEKEZO KWA IDARA YA MAJI (MUWSA) KUUNGANISHA BOMBA LA MAJI LILILOHUJUMIWA KWA KUKATWA KWA MAKUSUDI MARA MBILI KATIKA KIJIJI CHA MATALA KATA YA MWIKA KUSINI JIMBO LA VUNJO, PIA WANANCHI WOTE WALIOLIPA PESA ZA KUUNGANISHIWA MAJI WAUNGANISHIWE HARAKA SANA.
MKUU WA WILAYA YA MOSHI MHE. ABBAS KAYANDA AMETOA ONYO KALI KWA WAHUJUMU WA MIRADI YA MAENDELEO. ONYO HILO AMELITOA AKIWA KIJIJI CHA MATALA, KATA YA MWIKA KUSINI JIMBO LA VUNJO AMBAPO MIUNDOMBINU YA MAJI IMEKUWA IKIHARIBIWA KWA MAKUSUDI ILI KUKWAMISHA JITIHADA ZA SERIKALI.
VUNJO: Naibu Waziri TAMISEMI, Mhe. David Silinde apongeza Ujenzi wa Shule Mpya ya Sekondari Kata ya NJIAPANDA.
Mhe. Dkt. Charles Kimei (Mb) aendelea kuzisemea kero za Barabara kwa manufaa ya wananchi wa Jimbo la Vunjo 👏👏👏🙏 #SautiYaWanavunjo #MtumishiWaWananchi
Swali la Mhe. Dkt. Charles Kimei (MB) kuhusu Ukarabati wa Vyuo vya Ufundi vilivyopo Jimbo la Vunjo. 👍
Maswali ya Mhe. Dkt. Charles Kimei (MB) kuhusu Ahadi ya Kituo cha Afya (OPD-HIMO).
Mhe. Dkt. Charles Kimei (MB) kwenye hafla ya kupokea madarasa 85 iliyofanyika Vunjo:
1. Amemshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwakumbuka wananchi wa Jimbo la Vunjo kuwapa Fedha za Ujenzi wa Madarasa, Tsh 1.7 Bilioni.
2. Amempongeza Mkuu wa Wilaya, Mwenyekiti wa Halmashauri, Mkurugenzi, Wakuu wa Shule na Kamati zote zilizosimamia Ujenzi.
3. Ameridhishwa na thamani ya pesa iliyotumika katika ujenzi.
Mhe. Dkt. Charles Kimei (MB) kuzindua VUNJO EMPOWERMENT FOUNDATION ikiwa na Malengo yafuatayo:
1. Kuwawezesha Vijana na wajasiriamali Wanawake.
2. Kusaidia wajasiriamali kupata ufadhili wa miradi na biashara zao.
3. Kuanzisha programu mbalimbali za kutoa Elimu ili kusaidia wajasiriamali Vijana na Wanawake waweze kusaidika katika Taasisi za kifedha.
Mhe. @drcharleskimei (MB): "HEWA YA UKAA KUPAISHA UCHUMI WANANCHI WA JIMBO LA VUNJO. TAASISI YA @carbontanzania IPO TAYARI KUSHIRIKIANA KUFANIKISHA AZMA HII. KAZI KUBWA NI KUENDELEA KUTUNZA MISITU YETU YA ASILI."
Mhe. Dkt. Kimei (MB) asisitiza umuhimu wa kujengwa kwa kiwango cha Lami Barabara ya Pofo-Mandaka-Kilema KM 9 (Road Code 34053). Amuomba Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kusaidia Barabara hii ya Kimkakati ambayo ipo katika ilani ya Uchaguzi.
Source: ITV Tanzania. Ujenzi wa Madarasa 22 Manispaa ya Moshi mambo mazuri.
Mayor Juma Raibu Priscus Tarimo (Mb).
Mhe. Dkt. Kimei (MB) ameishukuru Serikali kupitia RUWASA kwa kutekeleza ukarabati wa Mradi wa Maji Kata ya Kilema Kaskazini. Mradi huu unanufaisha Vijiji vya Makami Juu, Makami Chini, Kyou na Ruwa. Mradi huu unahusisha ujenzi wa tenki la lita laki moja, vilula 21, kulaza mabomba KM 7.5, kujenga chanzo cha maji mto Mshiri. Mradi huu umegharimu zaidi ya kiasi cha shilingi Milioni 150,000,000/=. Mradi huu ukikamilika utaondoa tatizo la maji kata za Kilema Kaskazini, Kilema Kati, Kilema Kusini.
"SERIKALI INA MPANGO GANI KUHAKIKISHA VITUO VYA POLISI VYA KILEMA, KAHE, KIRUA NA MARANGU KATIKA JIMBO LA VUNJO VINAPEWA USAFIRI WA MAGARI?". DKT. KIMEI KWA USHIRIKIANO (MB)
Mbunge wa Moshi Mjini Mh. Priscus J. Tarimo akichangia kwenye mpango wa taifa 2022/2023, amejikita kwenye issue za kitaifa zaidi:-
1. Kilimo kuongezewa budget ili kilete tija ( kwa sasa kimepata chini ya asilimia moja bilioni 294.1)
2. Kutumia fursa ya kijiografia kwenye mifugo (soko la nyama DRC lina zaidi ya dola milioni 70),
3.Uwekezaji mkubwa kwenye huduma za afya uweze kuchangia kwenye uchumi haswa huduma za kibingwa (utalii tiba) kwa kuangalia India inavyofanya (soko litakuwa na thamani ya zaidi ya dola bilion 287 duniani ifikapo 2027
4. Upimaji wa ardhi kama chanzo cha mapato lakini kupanga vyema maeneo yetu pamoja na matumizi bora ya ardhi (kodi ya ardhi)
5. Miradi mikubwa ya serikali wapewe wazawa chini ya ufuatiliaji maalumu ili sehemu kubwa ya fedha ibaki nchini.