Kilimanjaro Revival Fm

Kilimanjaro Revival Fm Most Credible Christian Radio broadcast from Moshi-Kilimanjaro."Power Of Revival"

Rais Wa Kwanza wa Taifa la Namibia Dkt. Sam Stafiishuna Nujoma(95) amefariki baada ya kuugua kwa muda.Taarifa ilyotolewa...
09/02/2025

Rais Wa Kwanza wa Taifa la Namibia Dkt. Sam Stafiishuna Nujoma(95) amefariki baada ya kuugua kwa muda.

Taarifa ilyotolewa leo Februari 09,2025 na Rais wa Namibia Dkt. Nangolo Mbumba imeeleza kuwa Dkt. Nujoma alilazwa hospitalini kwa zaidi ya wiki tatu akipatiwa matibabu na hatimaye jana tarehe 08, Februari saa 23:45 usiku alifariki.

Dkt. Mbumba ameandika "Misingi ya Jamhuri ya Namibia imetikisika. Kwa zaidi ya wiki tatu zilizopita, Rais wa Kwanza wa Jamhuri ya Namibia na Baba Mwanzilishi wa Taifa letu alikuwa amelazwa hospitalini kwa ajili ya matibabu na uangalizi wa kitabibu kutokana na maradhi. Kwa bahati mbaya, safari hii, shujaa huyu mashuhuri wa nchi yetu hakuweza kupona ugonjwa wake."

Kwa hivyo, kwa huzuni na majonzi makubwa, ninawatangazia Wanamibia, ndugu zetu wa Afrika, na ulimwengu kwa ujumla, kuhusu kifo cha mpigania uhuru wetu anayeheshimiwa na kiongozi wa mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Sam Shafiishuna Nujoma. Rais Nujoma alifariki dunia akiwa na umri wa miaka 95, mnamo tarehe 8 Februari 2025 saa 23:45 huko Windhoek, Namibia." ameandika Dkt. Mbumba

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la TAG Kilimanjaro Revival Temple (KRT) Moshi Mjini, Mchungaji Ron Swai, ameongoza waumini ...
09/02/2025

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la TAG Kilimanjaro Revival Temple (KRT) Moshi Mjini, Mchungaji Ron Swai, ameongoza waumini wa kanisa hilo katika maombi maalum ya kuwaombea viongozi wa serikali, akimuomba Mungu aendelee kuwabariki, kuwajalia nguvu, hekima na umoja katika kulitumikia taifa.

Maombi hayo yamefanyika katika ibada ya kwanza iliyofanyika Februari 9,2025 ndani ya Kanisa hilo, ambapo waumini wamemwomba Mungu awape viongozi wa nchi ya Tanzania, uadilifu, na maono sahihi kwa ajili ya maendeleo ya taifa.

Mchungaji Ron Swai amewahimiza waumini hao na Watanzania wote kuendelea kuwaombea viongozi wa serikali mara kwa mara, akisisitiza kuwa maombi yana nguvu kubwa katika kuleta mabadiliko chanya katika jamii na taifa kwa ujumla kwani viongozi watakuwa na hofu ya Mungu katika kutekeleza majukumu yao na utoaji haji kwa wananchi.

𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐀 πŠπ”π“π”π…π”π€π“πˆπ‹πˆπ€ πŠπ€π“πˆπŠπ€ πŒπˆπ“π€ππƒπ€πŽ π˜π„π“π” π˜π€ πŠπˆπ‰π€πŒπˆπˆ

@ Kilimanjaro revival fm

Cc

Huko mtandaoni Watani wa jadi   na  wameendeleza utani wao wa Ummma....𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐀 πŠπ”π“π”π…π”π€π“πˆπ‹πˆπ€ πŠπ€π“πˆπŠπ€ πŒπˆπ“π€ππƒπ€πŽ π˜π„π“π” π˜π€ πŠπˆπ‰π€...
06/02/2025

Huko mtandaoni Watani wa jadi na wameendeleza utani wao wa Ummma....

𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐀 πŠπ”π“π”π…π”π€π“πˆπ‹πˆπ€ πŠπ€π“πˆπŠπ€ πŒπˆπ“π€ππƒπ€πŽ π˜π„π“π” π˜π€ πŠπˆπ‰π€πŒπˆπˆ

@ Kilimanjaro revival fm

Timu ya   imekubali kuwa haikuwa siku yao baada ya mchezo wao kumalizika 1-1 dhidi ya  baada ya Chasambi kumwaga kahawa ...
06/02/2025

Timu ya imekubali kuwa haikuwa siku yao baada ya mchezo wao kumalizika 1-1 dhidi ya baada ya Chasambi kumwaga kahawa ya ghali mezani

Lionel Ateba 57'
Ladack Chasambi 75'

Kiwamba Cha Leo kinatoka kwa Mtumishi wa Mungu   𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐀 πŠπ”π“π”π…π”π€π“πˆπ‹πˆπ€ πŠπ€π“πˆπŠπ€ πŒπˆπ“π€ππƒπ€πŽ π˜π„π“π” π˜π€ πŠπˆπ‰π€πŒπˆπˆ    @ Kilimanjaro r...
06/02/2025

Kiwamba Cha Leo kinatoka kwa Mtumishi wa Mungu

𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐀 πŠπ”π“π”π…π”π€π“πˆπ‹πˆπ€ πŠπ€π“πˆπŠπ€ πŒπˆπ“π€ππƒπ€πŽ π˜π„π“π” π˜π€ πŠπˆπ‰π€πŒπˆπˆ

@ Kilimanjaro revival fm

BREAKING: Bweni la Wasichana katika shule ya Sekondari ya Kaloleni Islamic iliyopo Kata ya Kaloleni Manispaa ya Moshi,Mk...
04/02/2025

BREAKING: Bweni la Wasichana katika shule ya Sekondari ya Kaloleni Islamic iliyopo Kata ya Kaloleni Manispaa ya Moshi,Mkoani Kilimanjaro limenusurika kuteketea kwa moto baada ya chumba kimoja cha Bweni hilo kushika Moto na kuteketeza vifaa na malazi ya Wanafunzi.

TAARIFA zaidi zitakujia,endelea kufuatilia Mitandao yetu ya kijamii.

Shalom Mpendwa katika Bwana! Mstari wetu wa wiki unatoka kitabu Cha Zaburi 40:13-15 ikiwa unashukuru kwa kuponywa au kut...
02/02/2025

Shalom Mpendwa katika Bwana!

Mstari wetu wa wiki unatoka kitabu Cha Zaburi 40:13-15 ikiwa unashukuru kwa kuponywa au kutaka msaada ni nafasi yako ya kukiri MANENO haya wiki nzima kumbuka kisasi ni Kazi ya Mungu wewe unapaswa kuomba na kumshukuru kwa Kila jambo unalopitia,mitego uliyotegewe ili uanguke kwa nafasi yako, biashara,ndoa,Mahusiano,afya, uchumi,kibali chako nk.Mwambie Mungu akusaidie ili wanaofanya hila Waaibike, wafedheheke pamoja,
Wanaoitafuta nafsi yako waiangamize.
Warudishwe nyuma, watahayarishwe,
Wapendezwao na shari yako.

Amen

 :  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa amethibitisha kutambuliwa kwa Mili ya watu watatu waliofarika kw...
01/02/2025

: Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa amethibitisha kutambuliwa kwa Mili ya watu watatu waliofarika kwa ajali ya gari iliyohusisha gari dogo aina ya Toyota RAV4 na Basi la Kampuni ya Esther Luxury iliyotokea leo Februari Moshi 2025 katika eneo la Kaanani Kiboriloni Mjini Moshi.

Kamanda amewataja waliofariki kuwa ni Paul Sita (25) mkazi wa Dar es salaam ambaye alikuwa ni dereva wa gari dogo, Exaud Mbise (65) na Apaikunda Ayo (61), wote wakazi wa Mkoa wa Arusha.

Kamanda Maigwa amesema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva wa gari dogo kujaribu kuyapita magari mengine, bila kuchukua tahadhari na kugongana uso kwa uso na basi la abiria la kampuni ya Esther luxury.

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imetangaza mfumo mpya wa kidijitali wa uombaji leseni za udereva, lengo likiwa ni kuond...
01/02/2025

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imetangaza mfumo mpya wa kidijitali wa uombaji leseni za udereva, lengo likiwa ni kuondoa vishoka wa leseni na vyeti vya udereva.

Mfumo huu unatajwa kuwa utaongeza ufanisi na kuhakikisha uwazi katika utoaji wa leseni za udereva.

Akizungumza na wakufunzi zaidi ya 20 wa shule za udereva katika Mkoa wa Kilimanjaro, kuhusu mfumo mpya wa kidijitali wa uombaji leseni za udereva, Afisa Msimamizi wa Kodi Mwandamizi na Mkuu wa Kitengo cha Elimu na Mawasiliano kutoka TRA kilimanjaro, Odupoi Papaa, amesema mfumo huo utawezesha kila mtu mwenye chombo cha moto kuchagua huduma anayoihitaji pasipo kwenda ofisi za TRA.

"Tumeweka nafasi ya wakufunzi na vyuo kujisajili katika mfumo wa TRA na Kupitia mfumo huu mwombaji wa leseni ya udereva ataweza kuona chuo Moja Kwa Moja katika mfumo huo na kuchagua aina ya leseni inayotolewa katika chuo hicho
Na hii ni mwarobaini Kwa vishoka wanaotengeneza vyeti feki vya udereva" Amesema Papaa .

Sambamba na Hilo Odupoi amesisitiza wale wanaotaka kubadilisha jina la umiliki wa gari kufanya hivyo kabla Mfumo huo kuanza kutumika ambapo mfumo huo unatarajiwa kuanza Rasmi mwezi februari.

Mkaguzi msaidizi wa Jeshi la Polisi, kutoka Ofisi ya Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa wa Kilimanjaro, Allen Chittunda, pia ameeleza kuwa mfumo huu unalenga kupunguza matatizo yanayotokana na vyeti feki na kuongeza usalama barabarani.

Kwa upande mwingine, Mkufunzi Mwandamizi wa Madereva kutoka VETA Moshi, Mwalimu Karim Mponda, amesema kuwa mfumo huo utasaidia wanafunzi kuchagua chuo kulingana na kiwango cha daraja wanachotaka kufikia katika mafunzo yao.
Cc ✍️

Watu watatu wamefariki dunia katika ajali ya barabarani iliyotokea leo Februari mosi katika eneo Kanaan Kiboriloni mkoan...
01/02/2025

Watu watatu wamefariki dunia katika ajali ya barabarani iliyotokea leo Februari mosi katika eneo Kanaan Kiboriloni mkoani Kilimanjaro.

Ajali hiyo iliyohusisha basi la kampuni Esther Luxury Coach na gari ndogo aina Toyota RAV 4 imetokea majira ya saa 12:30 asubuhi baada ya gari hizo kugongana uso kwa uso.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Godfrey Mzava waliofariki dunia ni watu waliokuwa kwenye gari ndogo yenye namba za usajili T 592 EKU.

Hongera Peter  Abdallah   Mtangazaji wa  kwa ushindi wa tuzo hii muhimu kwako na kwetu Mtangazaji Bora wa Mwaka katika t...
29/01/2025

Hongera Peter Abdallah Mtangazaji wa kwa ushindi wa tuzo hii muhimu kwako na kwetu Mtangazaji Bora wa Mwaka katika tuzo za CHAMUITA.

Ushindi wetu sote!

  kesho itakuwa  Mubashara katika viwanja vya Stendi ya Mabasi Moshi katika Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia ...
28/01/2025

kesho itakuwa Mubashara katika viwanja vya Stendi ya Mabasi Moshi katika Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (Mama Samia Legal Aid campaign ) Mgeni rasmi akiwa ni Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Damas Ndumbaro




Rais wa Kenya William Ruto ameangazia kuzorota kwa hali ya usalama nchini DR Congo baada ya waasi wanaoungwa mkono na Rw...
28/01/2025

Rais wa Kenya William Ruto ameangazia kuzorota kwa hali ya usalama nchini DR Congo baada ya waasi wanaoungwa mkono na Rwanda kuingia katika mji muhimu wa Goma.

Ruto amesema kuwa Rais wa DR Congo FΓ©lix Tshisekedi na Rais wa Rwanda Paul Kagame wamekubali kuhudhuria mkutano wa dharura siku ya Jumatano kujadili mzozo huo.

Ruto aliwaambia waandishi wa habari kwamba: "Hali ilivyo, sioni uwezekano makabiliano ya kijeshi yakiwa suluhisho la changamoto inayokabili mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.

"Majadiliano ya moja kwa moja kati ya kundi la M23 na washikadau wengine mashariki ya mwa DRC ni muhimu."

Kwa sasa Kenya inaongoza Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) yenye wanachama wanane, ikiwemo DR Congo na Rwanda.

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan leo anatarajiwa kuongoza wakuu wa nchi wengine wa Afrika katika majadiliano ya pam...
28/01/2025

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan leo anatarajiwa kuongoza wakuu wa nchi wengine wa Afrika katika majadiliano ya pamoja kwenye Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika 'Mission 300'.

Mijadala hiyo itaendelea leo kwenye siku ya pili ya mkutano huo wa nishati unaofanyika jijini Dar es Salaam nchini Tanzania.

Siku ya jana mijadala ilihusisha mawaziri wa mataifa mbalimbali, viongozi wa sekta binafsi, wadau wa masuala ya maendeleo ya nishati na fedha. Na leo wakuu wa nchi watakuwa sehemu ya mkutano huo.

Wakuu wa nchi mbalimbali wanaendelea kuwasili nchini Tanzania asubuhi hii kwaajili ya siku ya pili ya mkutano huo hii leo.

Baadhi ya marais waliowasili ni pamoja na Rais wa Sierra Leone, Malawi, Somalia, Zambia, Ethiopia, Djibout, Madagascar, Mauritania, Gambia, Burundi, Congo,Comoros, Ghana, Botswana.

Kiwamba cha leo kimemfikia Mchungaji Nelson Mwasha kutoka Kanisa la Kilimanjaro Revival Temple   ambaye anasema mafaniki...
28/01/2025

Kiwamba cha leo kimemfikia Mchungaji Nelson Mwasha kutoka Kanisa la Kilimanjaro Revival Temple ambaye anasema mafanikio hayana tabia ya kumrukia mtu,bali huja kwa kufanya kazi kwa bidii!

quotes.to.win

28/01/2025
Shalom! Wiki hii tunasimama na neno hili kutoka Waraka wa tatu wa Yohana 1:2Ni maombi yetu kuona unafanikiwa katika mamb...
27/01/2025

Shalom! Wiki hii tunasimama na neno hili kutoka Waraka wa tatu wa Yohana 1:2
Ni maombi yetu kuona unafanikiwa katika mambo Yako yote ikiwemo Uchumi,Ndoa,Elimu,Afya, Mahusiano imara nk.

Address

Moshi

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kilimanjaro Revival Fm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Kilimanjaro Revival Fm:

Videos

Share