JIKADIRIE! Ukitamani kuwa tajiri halafu upewe siri za utajiriπ€£
#reelsinstagram
#reels
#viral
#viralvideo
#viralreels
Jumla ya Wananchi laki Moja na elfu ishirini na Moja Mkoani Kilimanjaro wamefikiwa na huduma ya msaada wa kisheria ya Samia Legal Aid Campaign, Migogoro 740 ikipokelewa na Migogoro 94 ya ndani ikitatuliwa huku Migogoro zaidi ya 600 ikiendelea kufanyiwa kazi.
Akizungumzia wakati wa kupokea ripoti hiyo Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu ameeleza kuwa Serikali ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro itaendelea kutatua changamoto za kisheria kwa mashauri zaidi ya 600 ya Wananchi wake na kutoa ripoti hiyo Wizara ya Katiba na Sheria.
Akieleza kuhusu kazi hiyo kwa kipindi chote Murumbe James Daudi Mratibu wa huduma ya msaada wa kisheria Mkoa wa Kilimanjaro kutoka Wizara ya Katiba na Sheria mara baada ya kuhitimisha huduma hiyo iliyofanyika kuanzia Januari 29,2025 hadi Februari 7,2025 amesema kuwa bado Migogoro mingi iliyoripotiwa ni migogoro ya ardhi na mingi imekuwa ya muda mrefu zaidi ya miaka 20 hadi 30 hivyo akiwataka wananchi wa Mkoa huo kujaribu kutumia njia ya usuluhishi au mabaraza ya usuluhishi ili kuepuka kesi za ardhi.
Murumbe ameongeza kuwa sababu ya Migogoro hiyo ni kutokana na uelewa mdogo wa wananchi kuhusu masuala ya kisheria hasa juu ya ardhi ya namna ya kutwaa ardhi au kuhamisha kwenda kwa mtu mwingine.
#samiasuluhu
#reels
#viral
#forum
#instagram
Baraza la Madiwani Halmashauri ya Manispaa ya Moshi Mkoani Kilimanjaro limepitisha bajeti ya shilingi Bilioni 53.2 kwa Mwaka 2025/2026 fedha zitakazo tumika kukamilisha miradi mikubwa ya kimkakati na matumizi mengine.
Akizungumza wakati akitoa taarifa ya bajeti hiyo Mkurugenzi Mtendaji Manispaa ya Moshi Mwajuma Nasombe ameeleza kuwa ipo miradi mikubwa ya kimkakati itakayoenda kutekelezwa ili kuzidi kupata mapato zaidi.
Ametaja miradi hiyo ya kimkakati kuwa ni pamoja na umaliziaji wa uwanja wa Mpira Majengo wenye hadhi na vigezo hitajika kutoka FIFA ,Ujenzi wa ukumbi wa kisasa wa shughuli mbalimbali za kijamii pamoja na Ukarabati wa vibanda eneo la Uhuru Park lililopo ndani ya Manispaa hiyo.
"Mbali na miradi inayoenda kukamilisha,tunaenda kujenga ukumbi wa kisasa wa Sherehe na matukio mengine ya kijamii eneo la Shantytown,ukumbi huo wa nje utakuwa na eneo maalum la kisasa kwaajili ya fungate "Honeymoon" kwa maharusi " Nasombe.
Katika kukabiliana na majanga ya moto Mkoani Kilimanjaro Jeshi la zimamoto na uokoaji limepokea gari jipya kutoka Mji dada wa Marburg Nchini Ujerumani ili kusaidia wakati wa matukio ya ajali ya moto na uokozi mwingine.
Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na uokoaji ambaye ni Kaimu Kamanda wa zimamoto na uokoaji Mkoa wa Kilimanjaro Jeremiah Mkomagi amesema kuwa gari hilo litakuwa msaada mkubwa katika kuboresha huduma za uokoaji na kupambana na majanga ya moto katika mkoa wa Kilimanjaro.
Pia aliwataka wananchi kushirikiana na jeshi la zimamoto kwa kutoa taarifa za dharura mapema na kuhakikisha tahadhari za moto zinachukuliwa kwa umakini.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Kiseo Nzowa, ameonya kuhusu athari za ujenzi holela katika juhudi za uokoaji wakati wa majanga ya moto.
Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano ya gari la zimamoto kutoka Marburg, Ujerumani, Nzowa alieleza kuwa mipango mibovu ya ujenzi inasababisha changamoto kubwa kwa vikosi vya uokoaji kufika kwa haraka katika maeneo yenye dharura.
Aidha, alitoa pongezi kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa jitihada zao za kutoa elimu ya kuzuia moto, hasa kwa wanafunzi waliowasilisha maonesho ya mbinu za kudhibiti moto katika hafla hiyo.
Nzowa alisema kuwa elimu hiyo ni muhimu kwa kizazi kijacho ili kuhakikisha jamii inakuwa na uelewa wa namna ya kujikinga na majanga ya moto na jinsi ya kutoa msaada wa haraka panapotokea dharura.
Ametoa wito kwa taasisi na wananchi kuendelea kushirikiana na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ili kuhakikisha usalama wa mkoa wa Kilimanjaro unadumishwa kwa viwango vya juu.
πΉCc @nuhu_suleimantz
Kila Mzazi anatamani katika familia yake pawepo na chipukizi kama la huyu Mtoto atakaye simama kwaajili ya kumtumikia Mungu.
Unanini la kusema juu ya video hii?
Isaya 11:1-2
Basi litatoka chipukizi katika shina la Yese, na tawi litakalotoka katika mizizi yake litazaa matunda.
[2]Na roho ya BWANA atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha BWANA;
πππππππ πππππ
πππππππ ππππππ ππππππππ ππππ ππ πππππππ
#Instagram @kilimanjarorevivalradio
#facebook @ Kilimanjaro revival fm
#Video
#meta
#viral
#explorepage
#reels
#reels
Laigwanan Mkuu wa Jamii ya Maasai Tanzania Isack Ole Kisongo Meijo ameonesha hali ya kushangwaza na ukweli wa binadamu wa kwanza ni upi kama siyo Masai aliyepatikana katika bonde la Olduva Gorge Ngorongoro huku akieleza kuwa Yesu anaweza kuwa ni Masai.
Sikiliza hesabu zake za dunia kuumbwa hadi leo na mtu wa kwanza ni nani.
πππππππ πππππ
πππππππ ππππππ ππππππππ ππππ ππ πππππππ
#Instagram @kilimanjarorevivalradio
#facebook @ Kilimanjaro revival fm
#maasai
#maasaimara
#maasaimara
#olduvai
#ngorongoro
#ngorongorocrater
#ngorongoroconservationarea
#ngorongoronationalpark
#leigwanani
Vijana waoaji kuna ujumbe wenu hapa maridhawa kutoka kwa Mtumishi wa Mungu @pastorcharlesprosperity ikiwa unataka kuoa na inavyopaswa kuwa na adabu katika Mahusiano.
Cc @pastorcharlesprosperity
πππππππ πππππ
πππππππ ππππππ ππππππππ ππππ ππ πππππππ
#Instagram @kilimanjarorevivalradio
#facebook @ Kilimanjaro revival fm
Anaandika Mtumishi wa Bwana @carloskirimbai
Hivi ulikuwa unajua kuwa ngono ni tendo la kiagano? Na je ulikuwa unajua kuwa ngono sio tendo la kimwili tu ni tendo la kinafsi na kiroho pia? Mwanadamu ni roho, anayo nafsi na anakaa ndani ya mwili.
Tendo la ngono linaunganisha sio miili miwili tu bali na nafsi mbili na pia roho mbili. Kitendo cha kingono kinapelekea sio kubadilishana tu vimiminika vya kimwili kama jasho, damu na kadhalika bali pia inapelekea kubadilisha vitu vya nafsi na roho pia.
Yule mtu unayefanya naye ngono anaondoka na sehemu ya ulivyo kiroho, kinafsi na kimwili na kadhalika wewe unaondoka na sehemu ya alivyo kiroho, kimwili na kinafsi. Miili ni rahisi kuachana baada ya tendo ila nafsi na roho zinaendelea kuambatana na kubadilishana vitu muda mrefu baada ya kitendo husika kwa sababu ya muunganiko na mwambatano wa nafsi na roho ambao umetokea.
Ukimpa mtu mwili wako umempa na roho yako na nafsi yako pia na umeingia agano na yeye na wengine wote ambao aliwahi kufanya nao ngono. Kama ambavyo kuna maambukizi ya magonjwa yanaweza kutokea wakati wa kitendo cha ngono kadhalika kuna maambukizi katika upeo wa nafsi na roho hutokea pia yanaweza kutokea wakati wa kitendo cha ngono kadhalika kuna maambukizi katika upeo wa nafsi na roho hutokea pia.
Kama ambavyo mwanamume anaweza akampandia mwanamke kitu kimwili kupitia kitendo cha ngono kadhalika unaweza kupandiwa kitu cha kinafsi na kiroho kupitia kitendo cha ngono. Tusichukulie ngono kirahisi sana maana wengi ni waathirika wa shida za kiroho na za kinafsi na mlango ambao adui aliutumia ni mlango wa ngono. Watu wanaishi kwa matumaini sio tu kwa sababu ya athari za kimwili, bali kuna watu ambao hawana athari zozote za kimwili ila wameathirika sana kwenye nafsi na roho zao.
Na kwa kadiri unavyoshiriki na watu wengi kwa kadiri hiyo hiyo athari zake. Ukifanya ngono na mtu hufanyi tu naye bali na wote aliyofanya nao na ambao wamefanya na hao na kadhalika. Ngono hukuunganisha na mtandao mpana sana wa kimw
Msikilize Mhanga wa ukeketaji akizungumza ndani ya Kipindi Cha Jamvi letu @kilimanjarorevivalradio namna alivyorejeshewa kiungo chake kwa kufanyiwa upasuaji na namna anavyo furahia maisha yake mapya baada ya kurejeshewa kiungo hicho hali inayompelekea kujiamini kama Wanawake wengine wasiyofanyiwa ukeketaji.
πππππππ πππππ
πππππππ ππππππ ππππππππ ππππ ππ πππππππ
#Instagram @kilimanjarorevivalradio
#facebook @ Kilimanjaro revival fm
Host: @reyma_255
πΉ @nuhu_suleimantz
" Tumeendelea kufikiria njia tofauti ili tuweze kumasaidia yule mtu ambaye tayari ameathirika na ukeketaji, kwa sasa @nafgemtanzania kwa kushirikiana hospitali ya @kcmc1971 na madaktari kutoka Ujerumani, tumeanzisha approach mpya ya kumasaidia Mwanamke aliyekeketwa anaweza kurudishiwa sehemu zake zilizoondolewa" Nailejileji Papakinyi.
Nailejileji Papakinyi kutoka sShirika la NAFGEM akizungumza na Kilimanjaro Revival FM katika kipindi cha Jamvi Letu.
#ukatiliwakijinsia
#ukatili
#violenceagainstwomen
#violence
#haki
#right
Bweni la Wasichana katika shule ya Sekondari ya Kaloleni Islamic iliyopo Kata ya Kaloleni Manispaa ya Moshi,Mkoani Kilimanjaro limenusurika kuteketea kwa moto baada ya chumba kimoja cha Bweni hilo kushika Moto na kuteketeza vifaa na malazi ya Wanafunzi.
Akizungumzia tukio hilo lililotokea Februari 4,2025 Mkuu wa Shule hiyo Muhamed Mgeto amesema kuwa moto huo ambao chanzo chake hakijajulikana uliteketeza chumba kimoja cha bweni hilo na kusababisha vifaa na mali nyingine za Wanafunzi kuteketea kwa moto.
Akidhibitisha kutoke kwa ajali hiyo ya moto Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na uokoaji ambaye ni Kaimu Kamanda wa zimamoto na uokoaji Mkoa wa Kilimanjaro Jeremiah Mkomagi amesema kuwa bado wanachunguza kiundani chanzo cha matukio ya moto katika shule hiyo kutokana na kuwa siyo mara ya kwanza matukio ya moto kuripotiwa.