Kilimanjaro Revival Fm

Kilimanjaro Revival Fm Most Credible Christian Radio broadcast from Moshi-Kilimanjaro."Power Of Revival"

Shalom!Barikiwa na neno hili la wiki linalokutaka kuwa mwangalifu kwa kila unalotenda kwako na kwa mwenzako,Maana ya waz...
20/01/2025

Shalom!
Barikiwa na neno hili la wiki linalokutaka kuwa mwangalifu kwa kila unalotenda kwako na kwa mwenzako,Maana ya wazi juu ya maneno haya wapendwa ni kuwa kila ubaya,uchochezi na uchonganishi ambao unaufanya baina ya watu,kikundi au jamii fulani huwa na matokeo hasi kwa maana ya maangamizo.

Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye leo amepitishwa kuwa Mgombea Urais (CCM) kwe...
19/01/2025

Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye leo amepitishwa kuwa Mgombea Urais (CCM) kwenye Uchaguzi wa mwaka huu 2025, amemtangaza Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Emmanuel Nchimbi kuwa Mgombea mwenza wake wa Urais.

Akiongea leo January 19,2025 kwenye Mkutano Mkuu Maalum Jijini Dodoma, Rais Samia amesema Dkt. Nchimbi ataendelea kuwa Katibu Mkuu wa CCM kwa sasa hadi Uchaguzi Mkuu utakapofanyika.

Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango amemwandikia barua ya kuomba apumzik...
19/01/2025

Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango amemwandikia barua ya kuomba apumzike Umakamu wa Rais ambapo amesema baada ya kutafakari ameridhia ombi hilo lakini kwa sasa Dkt. Mpango ataendelea kuwa Makamu wa Rais hadi utakapofanyika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu 2025.

Akiongea leo January 19,2025 kwenye Mkutano Mkuu Maalum Jijini Dodoma, Rais Samia amesema “Dkt. Philip Mpango ndiye Makamu wa Rais miezi ya karibuni hapa amekuja kuniona kuniomba apumzike, ana sababu kadhaa lakini sio za kazi, anasema yeye sasa ana miaka 68 na angependa kuishi zaidi kwahiyo naomba nipumzisheni, nikambishia bishia Wiki iliyopita hapa akanikabidhi barua yangu hii ( ya kujiuzulu) na barua sikumjibu, nilipoenda kwenye K**ati Kuu nikawaeleza hiyo hali na kwa pamoja wote tukakubali tumpumzishe”

Mkutano Mkuu Maalum wa CCM unaofanyika Jijiji Dodoma kwa pamoja umeazimia jina la Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Tan...
19/01/2025

Mkutano Mkuu Maalum wa CCM unaofanyika Jijiji Dodoma kwa pamoja umeazimia jina la Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa ndiye atakayegombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya CCM.

“Tunaiagiza Halmshauri Kuu ya CCM Taifa kutekeleza jukumu lake leo, na kwakuwa Katiba ya CCM inasema Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ndio ina Mamlaka kuchagua Mgombea wa Urais Zanzibar, tunaelekeza kikao hicho kukutana leo ili kutekeleza jukumu lake hilo”

Yanga SC inashindwa kufuzu hatua ya Robo fainali ya ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kulazimishwa sare dhidi ya MC Alger...
18/01/2025

Yanga SC inashindwa kufuzu hatua ya Robo fainali ya ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kulazimishwa sare dhidi ya MC Alger ya Algeria.

FT: Yanga SC 0-0 MC Alger

MSIMAMO KUNDI A
1. Al Hilal - 10pts
2. MC Alger - 9pts
3. Yanga SC - 8pts
4. TP Mazembe - 5pts

Al Hilal ya Sudan na MC Alger zinafuzu hatua ya robo fainali katika mashindano hayo, huku Yanga na Mazembe wakiishia hatua ya makundi.

Mwanasiasa mkongwe na Waziri wa zamani Mzee Stephen Wasira,  amependekezwa kugombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti Tanzania...
18/01/2025

Mwanasiasa mkongwe na Waziri wa zamani Mzee Stephen Wasira,  amependekezwa kugombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti Tanzania Bara wa chama hicho leo Jumamosi Januari 18, 2025.

Imeelezwa kuwa zaidi ya wanawake 6,000 hufariki dunia kila mwaka nchini kutokana na ugonjwa wa saratani ya mlango wa kiz...
16/01/2025

Imeelezwa kuwa zaidi ya wanawake 6,000 hufariki dunia kila mwaka nchini kutokana na ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi.

Hayo yameeleza na Daktari bingwa wa magonjwa ya akina mama, Baraka Shao kutoka hospitali ya Rufaa kanda ya Kaskazin (KCMC) wakati akizungumza na Kilimanjaro Revival Radio ambapo amesema kuwa ugonjwa huo huanza taratibu hadi kupelekea kifo.

Aidha ameeleza kuwa saratani ya shingo ya kizazi husababishwa na virusi vya Human Papilloma (HPV), virusi ambavyo vinaweza kuambukizwa kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine kwa kujamiiana.

Dkt. Shao ameeleza mambo mengine ambayo yanaweza kuongeza uwezekano wa kupata saratani ya shingo ya kizazi ikiwa ni pamoja na kupata maambukizi ya magonjwa ya zinaa, Magonjwa ya Upungufu wa Kinga Mwilini k**a UKIMWI, Matumizi ya vidonge vya kudhibiti uzazi kwa muda mrefu (miaka mitano au zaidi) na kuvuta sigara.

Vilevile amesema kuwa saratani ya shingo ya kizazi kwa kawaida haina dalili za moja kwa moja na huchukuwa miaka kadhaa kuonyesha dalili zake za kwanza.

"Ishara za saratani ya mlango wa kizazi ni pamoja na kutokwa na damu ukeni baada ya kujamiiana, Kutokwa na damu ukeni wakati wa hedhi au baada ya kukoma hedhi, Hedhi nzito na/au ndefu kuliko wastani, Kutokwa na majimaji, damu na harufu mbaya ukeni na maumivu ya kiuno wakati wa kujamiiana". amesema.

Hatahivyo, Muuguzi afya ya jamii Tatu Msangi kutoka hospitali ya rufaa Kanda ya Kaskazini (KCMC) amewasihi wanawake kufanya uchunguzi wa saratani ya mlango wa kila baada ya miezi sita ili Wataalum wa afya watakapo baini uwepo wa ugonjwa huo, kuanza matibabu katika hatua za mwanzoni.

Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO lilitangaza kuwa mwezi Januari ni mwezi wa kuhamasisha jamii kuhusu satarani ya shingo ya kizazi.
✍️

AFYA: Inashauriwa kuwa Mwanadamu anapaswa kupata haja kubwa mara mbili hadi mara tatu kwa siku au mara mbili hadi tatu k...
16/01/2025

AFYA: Inashauriwa kuwa Mwanadamu anapaswa kupata haja kubwa mara mbili hadi mara tatu kwa siku au mara mbili hadi tatu kwa wiki.

Daktari Thobias Wajama ameeleza kuwa swali kubwa watu wanalosumbuka nalo ni mara ngapi kwa binadamu kupata haja kubwa kwa siku na kueleza kuwa zipo sababu zinazoweza kupelekea binadamu kukosa choo.

K**a ikitokea mtu akakosa choo kwa muda wa siku nne au zaidi mfululizo hiyo ni shida anapaswa kumuona Daktari ,kukosa choo kwa siku tatu siyo siku za kustua na kwenda hospitali ila ikiwa siku nne au zaidi mfululizo hapo ndio shida fika hospitali kwa ushauri zaidi" Wajama.

Ameeleza kuwa sababu zinazopelekea mtu kukosa haja kubwa au choo kigumu ni pamoja na lishe mbovu,Vyakula vilivyosindikwa sana, sukari, nafaka iliyokobolewa, pombe,msongo wa mawazo,kutoshughulisha mwili, matumizi ya baadhi ya vidonge,ukuaji wa bakteri wabaya kwenye mfumo wa chakula na sababu nyingine nyingi.

Heri ya siku mpya!Tumekusogezea kurasa zambele za mageti ya Tanzania leoJanuari 16,2025.Sikiliza uchambuzi wake ndani ya...
16/01/2025

Heri ya siku mpya!

Tumekusogezea kurasa zambele za mageti ya Tanzania leoJanuari 16,2025.

Sikiliza uchambuzi wake ndani ya ukiwa naye na

Sikiliza live kupitia website ya www.kilimanjarorevivalfm.or.tz

Wizara ya Afya nchini imeeleza kupokea tetesi za uwepo wa ugonjwa wa Marburg katika Mkoa wa Kagera na kuanza kufanyia ka...
15/01/2025

Wizara ya Afya nchini imeeleza kupokea tetesi za uwepo wa ugonjwa wa Marburg katika Mkoa wa Kagera na kuanza kufanyia kazi tetesi hizo.

Kufuatia tetesi hizo, Wizara imeeleza kuchukua hatua kadhaa za haraka ikiwemo,kutuma timu ya wataalamu; kufanya uchunguzi wa suala hilio, kuchukua sampuli na kufanya vipimo vya maabara.

Taarifa iliyo tolewa na Waziri wa Afya Jenista Mhagama imeeleza kuwa hadi kufika leo, tarehe 15 Januari 2025, majibu ya uchunguzi wa kimaabara kutoka kwa wahisiwa wote waliochukuliwa sampuli hizo hayajathibisha uwepo wa virusi vya Marburg.

Ameeleza kuwa Wizara inapenda kuwahakikishia wananchi pamoja na jumuiya ya kimataifa, likiwemo Shirika la Afya Duniani (World Health Organisation - WHO), kuwa imeimarisha mifumo ya ufuatiliaji wa magonjwa na itaendelea kutoa taarifa zaidi.

Mkuu wa Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro Kasilda Mgeni  ameagiza Jeshi la Polisi kuk**ata waliohusika kuwapa ujauzito W...
15/01/2025

Mkuu wa Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro Kasilda Mgeni ameagiza Jeshi la Polisi kuk**ata waliohusika kuwapa ujauzito Wanafunzi wanne wa shule tofauti za msingi na sekondari katika kata za Kalemawe na Bendera,kuk**atwa mara moja na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Kasilda ametoa maagizo hayo wakati wa ziara yake ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi, pamoja na kuhamasisha wazazi kuwapeleka watoto shule,akihimiza umuhimu wa kuwasaidia watoto wanaoanza chekechea, darasa la kwanza, na waliofaulu kujiunga na kidato cha kwanza ili kufanikisha ndoto zao.

Akiongea katika ziara hiyo Kasilda amesisitiza kuwa vitendo vya kuwapa mimba wanafunzi vinaharibu ndoto za watoto wa k**e na juhudi za serikali ya awamu ya sita, ambayo imejikita kuboresha mazingira ya elimu kwa wanafunzi wote, hasa wa k**e.

"Mazingira rafiki ya elimu yanayoboreshwa na serikali yetu yanahitaji msaada wa jamii. Vitendo k**a hivi havikubaliki, vinaharibu maisha ya watoto wetu na kukiuka maadili yetu. Wahusika wote watawajibishwa kwa mujibu wa sheria," alisema kwa msisitizo.

Mhe. Kasilda pia aliwataka wazazi, walezi, na jamii kwa ujumla kuhakikisha watoto wanalelewa kwa maadili mema na kulindwa dhidi ya vitendo vya ukatili vinavyoweza kuathiri maendeleo yao ya kielimu na maisha yao kwa ujumla. Aliagiza hatua za haraka zichukuliwe dhidi ya wazazi wanaowaficha wanaume waliowapa mimba wanafunzi, akiwataja wazazi hao kuwa washiriki wa uhalifu kwa kuficha wahalifu.

"Hata wazazi walioshirikiana na wanaume hao kwa kupokea pesa au manufaa yoyote hawatapona, nimeagiza nao wasakwe na kufikishwa mahak**ani kwa kosa la kuficha wahalifu," aliongeza.

Wananchi walioshiriki mkutano huo walionesha kuridhishwa na hatua za haraka zilizochukuliwa na Mhe. Kasilda, huku wakiahidi kushirikiana na serikali kwa kutoa taarifa za wahusika wa ukatili dhidi ya wanafunzi.

Kwa upande wao, baadhi ya walimu wakuu wa shule hizo walieleza kuwa changamoto kubwa ni ushirikiano mdogo kutoka kwa wazazi wa wahanga, ambao mara nyingi huficha ukweli na kuweka vikwazo katika upatikanaji

Wale Wana ndoa ujumbe huu unawahusu na siyo kukariri Mithali 21:19Ni afadhali kukaa katika nchi ya nyika; Kuliko na mwan...
14/01/2025

Wale Wana ndoa ujumbe huu unawahusu na siyo kukariri Mithali 21:19
Ni afadhali kukaa katika nchi ya nyika;
Kuliko na mwanamke mgomvi, mchokozi. Au ukaongeza na Mithali 21:9
Ni afadhali kukaa katika pembe ya darini,
Kuliko katika nyumba pana pamoja na mwanamke mgomvi.

Wote kwa pamoja jitahidi msiwe wagomvi kuboresha kinga za mwili na kuepeuka kuzipinguza k**a alivyoshauri .janabi







Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Mhe. Ester Mahawe amefariki dunia leo Januari 14, 2025 katika hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Ka...
14/01/2025

Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Mhe. Ester Mahawe amefariki dunia leo Januari 14, 2025 katika hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini -KCMC Mkoani Kilimanjaro alipokuwa anapatiwa Matibabu.

Taarifa ya kifo chake imetangazwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Mohamed Mchengerwa kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan "Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Mkuu wa Wilaya ya Mbozi mkoani Songwe Mhe. Ester Mahawe. Kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ninatoa pole kwa familia, Mkuu wa Mkoa wa Songwe, wafanyakazi na wananchi wote wa wilaya ya mbozi, ndugu, jamaa na mafariki kwa msiba huu. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi' amesema waziri Mchengerwa.

Aidha kupitia ukurasa wa Instagram wa Rais Mhe.Rais ametoa pole kwa familia na Wananchi wa Mbozi kufuatia kifo hicho.

“Ukawaida ni mkoa uliopakana na    kutokujikubali upande wa kaskazini, kukosa maamuzi upande wa kusini, mawazo ya kale u...
14/01/2025

“Ukawaida ni mkoa uliopakana na kutokujikubali
upande wa kaskazini, kukosa maamuzi upande wa kusini, mawazo ya kale upande wa mashariki na ukosefu wa maono upande wa magharibi”
-John Mason-

Nehemia 2:20Ndipo nikawajibu, nikawaambia, Mungu wa mbinguni, yeye atatufanikisha; kwa hiyo sisi, watumishi wake, tutaon...
13/01/2025

Nehemia 2:20
Ndipo nikawajibu, nikawaambia, Mungu wa mbinguni, yeye atatufanikisha; kwa hiyo sisi, watumishi wake, tutaondoka na kujenga; lakini ninyi hamna sehemu, wala haki, wala kumbukumbu, katika Yerusalemu.

Waziri Mkuu,   Kassim Majaliwa akitia saini mbele ya Rais Yoweri Museveni wa Uganda (kushoto) na Wakuu wa Nchi na Serika...
11/01/2025

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitia saini mbele ya Rais Yoweri Museveni wa Uganda (kushoto) na Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika baada ya kushuhudia Tamasha la Kahawa Afrika (Africa Coffee Festival) lililolenga kuhamasisha uongezaji thamani katika mazao yanayolimwa Afrika likiwemo zao la kahawa. Tukio hilo lilifanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Speke Resort, Munyonyo, Kampala Uganda ambako alimwakilisha Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika Mkutano Maalum wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika kuhusu Mpango wa Maendeleo ya Kilimo Afrika, Januari 11, 2025.

  inakukaribisha katika maombi ya mfungo wa siku 21 kuombea familia,Kanisa na Taifa ili Mungu aachilie Rehema na Neema z...
11/01/2025

inakukaribisha katika maombi ya mfungo wa siku 21 kuombea familia,Kanisa na Taifa ili Mungu aachilie Rehema na Neema zake!



Address

Moshi

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kilimanjaro Revival Fm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Kilimanjaro Revival Fm:

Videos

Share