Sweet fm radio 90.5 mbeya

Sweet fm radio 90.5 mbeya Sweet fm radio 90.5 Mbeya . Karibu tukuhudumie kwa gharama nafuu na rafiki kwa wafanyabiashara wote

Jeshi la Polisi mkoa wa Rukwalinawashikilia vijana 13, akiwemo mwanamke mmoja, kwa tuhuma za kujihusisha na utapeli wa k...
11/03/2025

Jeshi la Polisi mkoa wa Rukwa

linawashikilia vijana 13, akiwemo mwanamke mmoja, kwa tuhuma za kujihusisha na utapeli wa kimtandao.

Akizungumza Kamanda wa Polisi mkoa wa Rukwa, SACP Shadrack Masija, amesema watuhumiwa hao walik**atwa wakiwa na laini 36 za mitandao mbalimbali pamoja na zaidi ya simu kumi, ambazo inadaiwa walizitumia katika kutekeleza uhalifu huo.

Kamanda Masija amepongeza juhudi za Jeshi la Polisi katika kuendelea kudhibiti uhalifu wa mtandao na ametoa wito kwa wananchi kuacha mara moja kujihusisha na vitendo vya utapeli wa kimtandao, Pia amewataka wananchi kuwa makini na taarifa zao za kifedha na binafsi ili kuepuka kuingia katika mtego wa matapeli.

Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wa kina ili kubaini mtandao mpana wa uhalifu huo na hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya wahusika.

Takriban vikundi vitatu vya wapiganaji wakundi la wazalendo wanaoliunga mkono Jeshi la Serikali ya Jamhuri Kidemokrasia ...
11/03/2025

Takriban vikundi vitatu vya wapiganaji wa

kundi la wazalendo wanaoliunga mkono Jeshi la Serikali ya Jamhuri Kidemokrasia ya Congo (FARDC) Kivu Kaskazini wameasi na kujiunga na muungano wa makundi ya waasi wa Alliance Fleuve Congo (AFC/M23).

Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini DRC, taarifa iliyosainiwa na kiongozi wa wazalendo, Shukuru Bulenda, vikundi hivyo vilivyoasi ni pamoja na Mai-Mai Kabidon (FPP-AP), sehemu ya Mai-Mai Kifuafua na kikundi cha Nduma Defense of Congo- Renovated (NDC-R/M).

Vikundi hivyo, vinadaiwa kujiunga na AFC/M23, juzi Machi 9, 2025.

Wakati mapigano yakiendelea, Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imesema iko tayari kujadiliana na serikali ya Rais Felix Tshisekedi wa DRC juu ya namna ya kukabiliana na makundi ya waasi nchini humo, kwa sharti la kunufaika na madini ya nchi hiyo.

“Ni lazima tujenge kizazi cha watoto wanaojiamini na wenye uwezo wa kujenga hoja, vijana ambao watatambua kuwa ukubwa wa...
08/03/2025

“Ni lazima tujenge kizazi cha watoto wanaojiamini na wenye uwezo wa kujenga hoja, vijana ambao watatambua kuwa ukubwa wa hoja yake si ukali wa sauti yake wala maneno yake, bali ni hoja yenyewe na utulivu na ufasaha wa kuiwakilisha hoja yenyewe. Kusema hoja kwa kufoka ni kupotosha hoja.” - Rais Samia Suluhu

  Alhamisi Februari 06, 2025
06/02/2025



Alhamisi Februari 06, 2025

“Moja kati ya ahadi zetu wana CCM inasema kwamba tutaitumikia nchi yetu na watu wake wote, ahadi ambayo tunaitekeleza kw...
05/02/2025

“Moja kati ya ahadi zetu wana CCM inasema kwamba tutaitumikia nchi yetu na watu wake wote, ahadi ambayo tunaitekeleza kwa vitendo na imefanya CCM iendelee kuaminiwa na wananchi kwa kuipa dhamana ya kuongoza Serikali zote mbili.” - Rais Samia Suluhu, Mwenyekiti wa CCM Taifa katika Maadhimisho ya Miaka 48 ya CCM

  Moto ambao chanzo chake hakijajulikana umeunguza kiwanda kidogo cha kutengeneza samani za ndani maeneo ya Mabibo Hoste...
05/02/2025

Moto ambao chanzo chake hakijajulikana umeunguza kiwanda kidogo cha kutengeneza samani za ndani maeneo ya Mabibo Hostel, Wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam leo Jumatano Februari 5, 2025.

Jeshi la Zimamoto na Uokozi na baadhi ya wasamaria wema pamoja na majirani wa jengo hilo wameendelea na jitihada za kuuzima moto huo kwa kutumia maji kutoka kwenye mabomba yaliyopo karibu na eneo hilo.

Rais wa Rwanda Paul Kagame amesema kuwa hajui k**a Wanajeshi wa nchi yake wako Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya ...
05/02/2025

Rais wa Rwanda Paul Kagame amesema kuwa hajui k**a Wanajeshi wa nchi yake wako Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), ambako mapigano kati ya kundi la waasi la M23 na Wanajeshi wa Congo yameua zaidi ya watu 900 na kujeruhi maelfu katika siku za hivi karibuni.

Sehemu kubwa ya Jumuiya ya Kimataifa inaamini kuwa Rwanda inawaunga mkono waasi wa M23, waliodai kuuteka mji wa Goma Mashariki mwa Congo wiki iliyopita.

Wataalamu wa umoja wa mataifa wanaamini kuwa takribani wanajeshi 3,000 - 4,000 wa Rwanda wanawasimamia na kuwaunga mkono wapiganaji wa M23 Mashariki mwa DRC, wakiwazidi Wanajeshi wa kundi hilo la waasi nchini humo.

Takribani miili 900 imeopolewa kutoka mitaa ya Goma tangu ghasia kuzuka, kulingana na takwimu za hivi punde za Umoja wa Mataifa.

“Kufikia Januari 31, takriban miili 900 imepatikana kutoka mitaani,” ilisema Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu masuala ya Kibinadamu katika ripoti ya Jumatatu, ikinukuu Shirika la Afya Ulimwenguni.

Rais Donald Trump amesema Marekani itachukua na kumiliki Ukanda wa Gaza baada ya kuwahamisha Wapalestina kwenda maeneo m...
05/02/2025

Rais Donald Trump amesema Marekani itachukua na kumiliki Ukanda wa Gaza baada ya kuwahamisha Wapalestina kwenda maeneo mengine, chini ya mpango wa maendeleo ambao unaweza kugeuza eneo hilo kuwa Riviera ya Mashariki ya Kati.

Trump amesema utawala wake utaongoza maendeleo katika Ukanda huo ili kutoa ajira na makazi yasiyo na kikomo kwa watu wa eneo hilo.

05/02/2025
  Jumatano Februari 05, 2025
05/02/2025



Jumatano Februari 05, 2025

  Ijumaa Januari 31, 2025
31/01/2025



Ijumaa Januari 31, 2025

  Alhamisi Januari 30, 2025
30/01/2025



Alhamisi Januari 30, 2025

MakarashaDay: Dimba la Sokoine lililopo jijini Mbeya lipo tayari kwa sherehe ya leo ya KenGold ambao wanakwenda kutambul...
29/01/2025

MakarashaDay: Dimba la Sokoine lililopo jijini Mbeya lipo tayari kwa sherehe ya leo ya KenGold ambao wanakwenda kutambulisha ‘vyuma’ vyao vipya waliowaongeza kwenye dirisha dogo la usajili.

Mbali na sherehe zitakazofanyika katika dimba la Sokoine, saa 10:00 jioni itashuhudiwa mechi ya kirafiki kati ya KenGold dhidi ya wageni wao Real Nakonde FC

Rais Donald Trump ametoa agizo la kusitisha utoaji wa mikopo na ruzuku zote za Serikali kuu ya Marekani hatua ambayo ina...
29/01/2025

Rais Donald Trump ametoa agizo la kusitisha utoaji wa mikopo na ruzuku zote za Serikali kuu ya Marekani hatua ambayo inatarajiwa kuathiri Sekta muhimu k**a Elimu, Afya, Makazi na misaada ya maafa Nchini humo.

Hatua hii imeibua wasiwasi miongoni mwa Viongozi wa Serikali za mitaa na Mashirika yasiyo ya kiserikali wakihofia athari za kiuchumi na kijamii zitakazotokana na kusitishwa kwa fedha hizo pia Wakosoaji wanasema kuwa hatua hii inaweza kusababisha kusimama kwa huduma muhimu zinazotegemea ruzuku na mikopo ya Serikali kuu.

Kwa upande wake Ikulu imetetea uamuzi huo kupitia Ofisi ya Usimamizi na Bajeti ikisema kuwa hatua hiyo inalenga kufanya mapitio ya kina ya matumizi ya fedha za Serikali na kuhakikisha kuwa zinaendana na vipaumbele vya utawala wa Rais Trump.

Hata hivyo Mawakili Wakuu wa Serikali kutoka majimbo kadhaa wametangaza mpango wa kufungua kesi kupinga hatua hiyo wakidai kuwa itaathiri vibaya maisha ya Wananchi wa kawaida hasa wale wanaotegemea huduma za kijamii zinazofadhiliwa na Serikali kuu.

Wakati mjadala ukiendelea Wadadisi wa masuala ya siasa wanasema kuwa hatua hii ni sehemu ya juhudi za utawala wa Trump kupunguza matumizi ya Serikali na kuelekeza rasilimali kwenye vipaumbele vingine vya kiutawala.

Kuapishwa kwa Rais wa Marekani Donald Trump kumeleta mabadiliko mengi ikiwemo kufukuzwa kwa wahamiaji wasio na vibali ku...
29/01/2025

Kuapishwa kwa Rais wa Marekani Donald Trump kumeleta mabadiliko mengi ikiwemo kufukuzwa kwa wahamiaji wasio na vibali kutoka sehemu mbalimbali.

Hadi Januari 2024, takribani watu milioni 14 wanahesabika kuishi nchini Marekani bila vibali cha kuishi.

Hata hivyo, 40% ya watu hao wana vibali vya kuishi kwa muda, wakati 60% hawana, kulingana na The New York Times.

Orodha hiyo iliyochapishwa Novemba 2024 inaonyesha kuwa zaidi ya watu milioni moja (1,445, 549) ndio wanaopaswa kufukuzwa, kwa kuwa hawana vibali vyovyote.

Kati ya hao, 301 ni Watanzania kwa upande wa Warundi wakiwa ni 462.

  Jumatano Januari 29, 2025
29/01/2025



Jumatano Januari 29, 2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na wakuu wa nchi mbalimba...
28/01/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na wakuu wa nchi mbalimbali mara baada ya kuwasili katika kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu masuala Nishati tarehe 28 Januari, 2025.

Address

Ghana Hill
Mbeya
3445

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sweet fm radio 90.5 mbeya posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sweet fm radio 90.5 mbeya:

Videos

Share

Category