Sweet fm radio 90.5 mbeya

Sweet fm radio 90.5 mbeya Sweet fm radio 90.5 Mbeya . Karibu tukuhudumie kwa gharama nafuu na rafiki kwa wafanyabiashara wote

UZINDUZI WA KAMPENI YA ELIMU KWA UMMA KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI.
04/06/2024

UZINDUZI WA KAMPENI YA ELIMU KWA UMMA KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI.




KAMPENI YA UCHANGIAJI DAMU.Kuokoa maisha kwa wahitaji kwa kuchangia damu kwa hiariKampeni hii inaendelea hadi juni 14, 2...
04/06/2024

KAMPENI YA UCHANGIAJI DAMU.
Kuokoa maisha kwa wahitaji kwa kuchangia damu kwa hiari
Kampeni hii inaendelea hadi juni 14, 2024 kwa vituo vyote vyakutolea huduma ya afya mkoa wa Mbeya


Wananchi, Young Africans Sc wametwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania bara kwa mara ya 30 kihistoria kufuatia ushindi...
13/05/2024

Wananchi, Young Africans Sc wametwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania bara kwa mara ya 30 kihistoria kufuatia ushindi wa 2-1 dhidi ya Wakata Miwa, Mtibwa Sugar katika dimba la Manungu Complex, Morogoro.

FT: Mtibwa Sugar 1-3 Yanga Sc
⚽ Inanfya 33’
⚽ Musonda 63’
⚽ Nasry Kombo (og) 66’
⚽ Mzize 81’

Yanga Sc imefikisha pointi 71 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote.

MSIMAMO top 🔝3️⃣
🏆 Yanga Sc — mechi 27 — pointi 71
🥈 Azam Fc — mechi 27 —pointi 60
🥉 Simba Sc —mechi 26— pointi 57

TAARIFA KWA UMA
13/05/2024

TAARIFA KWA UMA

𝐌𝐖𝐀𝐌𝐁𝐀 Joseph Guede mchezaji bora 𝐍𝐈𝐂 𝐈𝐍𝐒𝐔𝐑𝐀𝐍𝐂𝐄 𝐏𝐋𝐀𝐘𝐄𝐑 𝐎𝐅 𝐓𝐇𝐄 𝐌𝐎𝐍𝐓𝐇 kwa Mwezi wa Aprili    🔥🔥💚💛
07/05/2024

𝐌𝐖𝐀𝐌𝐁𝐀 Joseph Guede mchezaji bora 𝐍𝐈𝐂 𝐈𝐍𝐒𝐔𝐑𝐀𝐍𝐂𝐄 𝐏𝐋𝐀𝐘𝐄𝐑 𝐎𝐅 𝐓𝐇𝐄 𝐌𝐎𝐍𝐓𝐇 kwa Mwezi wa Aprili


🔥🔥💚💛

“Nyumbani kwetu sisi. Furaha yetu kwetu ni kuona vizazi vyetu k**a walivyofurahi kuona kizazi cha Salum Manula” Golikipa...
07/05/2024

“Nyumbani kwetu sisi. Furaha yetu kwetu ni kuona vizazi vyetu k**a walivyofurahi kuona kizazi cha Salum Manula” Golikipa wa Simba SC, Aishi Salum Manula.

Manula haonekani dimbani kutokana na kusumbuliwa na majeraha aliyoyapata kwenye majukumu ya Taifa Stars kwenye mchezo dhidi ya Bulgaria.

TAARIFA KWA UMMA KATIZO LA UMEME
07/05/2024

TAARIFA KWA UMMA KATIZO LA UMEME

Mamlaka husika nchini Uingereza zimeanza kuwashikilia wahamiaji k**a sehemu ya maandalizi ya kuwahamishia nchini Rwanda ...
02/05/2024

Mamlaka husika nchini Uingereza zimeanza kuwashikilia wahamiaji k**a sehemu ya maandalizi ya kuwahamishia nchini Rwanda katika muda wa wiki 9 hadi 11 zijazo. Serikali ya Uingereza ilitangaza taarifa hiyo jana ikiashiria hatua muhimu katika mkakati wa uhamiaji unaotekelezwa na Waziri Mkuu Rishi Sunak.

Maofisa wa idara ya uhamiaji ya Uingereza katika mpango huo tajwa wameonakana wakiingia katika nyumba mbalimbali na kuwatoa watu wakiwa na pingu mikononi.

Serikali ya Uingereza imeeleza kuwa timu za utendaji ndani ya Wizara ya Mambo ya Ndani zimekuwa zikifanya kazi kwa kasi kuwaweka kizuizini kwa usalama na haraka watu walioorodheshwa katika mkakati huo wa Waziri Mkuu Sunak ili kupatiwa hifadhi huko Rwanda.

Ripoti kutoka taasisi ya kujitolea ya kuhudumia wakimbizi ya Care4Calais imethibitisha kuwa zoezi la kuwak**ata na kuwashikilia raia hao wanaotazamiwa kupelekwa Rwanda lilianza Jumatatu.

Wakati huo huo picha zilizorushwa jana katika mitandao ya kijamii na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Uingereza zimewaonyesha raia hao wakiwa chini ya udhibiti wa maofisa husika wa uhamiaji.

  Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) nchini imesema kwamba mgandamizo mdogo wa hewa katika Bahari ya Hindi mashariki...
02/05/2024

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) nchini imesema kwamba mgandamizo mdogo wa hewa katika Bahari ya Hindi mashariki mwa pwani ya Mtwara umeendelea kuimarika na kuwa kimbunga Hidaya chenye nguvu ya kati, kikiwa umbali wa takribani kilomita 506 mashariki mwa pwani ya Mtwara.

TMA imesema mwenendo wa mifumo ya hali ya hewa baharini inaonesha uwezekano mkubwa wa kimbunga Hidaya kusogea karibu kabisa na pwani ya Tanzania kuanzia usiku wa leo tarehe 02 Mei 2024 na kuendelea kuwepo hadi tarehe 06 na kwamba kimbunga hicho kinatarajiwa kupungua nguvu baada ya tarehe 6 Mei 2024.

“Uwepo wa kimbunga “HIDAYA” karibu na pwani ya nchi yetu unatarajiwa kutawala na kuathiri mifumo ya hali ya hewa hapa nchini ikiwa ni pamoja na kusababisha vipindi vya mvua kubwa na upepo mkali katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Dar es Salaam, Tanga, Morogoro, visiwa vya Unguja na Pemba na maeneo ya jirani hususan tarehe 3 Mei 2024 kwa maeneo ya pwani ya kusini (Lindi na Mtwara) na kusambaa katika maeneo mengine ya ukanda wa pwani kuelekea tarehe 4 hadi 6 Mei 2024,” imeeleza taarifa ya TMA


Na mchango umechangia Tsh . 120,000
02/05/2024

Na mchango umechangia Tsh . 120,000

  Ni Ihefu vs Yanga nusu fainali. FT: Yanga 3-0 Tabora United. Nusu fainali nyingine itakuwa ni; Azam /Namungo vs Coasta...
01/05/2024

Ni Ihefu vs Yanga nusu fainali.

FT: Yanga 3-0 Tabora United.

Nusu fainali nyingine itakuwa ni; Azam /Namungo vs Coastal Union.

Nyota wa klabu ya Simba, Clatous Chama amefungiwa michezo mitatu (3) na kutozwa faini ya Sh. 1,000,000 kwa kosa la kumka...
01/05/2024

Nyota wa klabu ya Simba, Clatous Chama amefungiwa michezo mitatu (3) na kutozwa faini ya Sh. 1,000,000 kwa kosa la kumkanyaga kwa makusudi mchezaji Nickson Kibabage wa klabu ya Yanga wakati mchezo wa Derby ya Kariakoo kati ya timu hizo uliopigwa Aprili 20, 2024 katika dimba la Benjamin Mkapa.

CHAMA atakosa mechi tatu zinazofuata za Simba Sc ukiwemo mchezo wa Derby ya Mzizima kati ya Simba Sc dhidi ya Azam fc unaotarajiwa kupigwa Mei 9, 2024. Michezo mwingine atakayokosa ni pamoja na mechi dhidi ya Mtibwa Sugar na Tabora United.

  Wananchi wametakiwa kuendelea kuchukua tahadhari kufuatia taarifa ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kuripoti u...
01/05/2024

Wananchi wametakiwa kuendelea kuchukua tahadhari kufuatia taarifa ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kuripoti uwepo wa mgandamizo mdogo wa hewa katika Bahari ya Hindi mashariki mwa pwani ya Mtwara.

Taaarifa ya TMA inaeleza kuwa mifumo ya hali ya hewa iliyopo kwa sasa inaonesha kuwa mgandomizo huo mdogo wa hewa ambao unatarajiwa kuimarika na kufikia hadhi ya Kimbunga kamili hadi kufikia kesho tarehe 2 Mei 2024.

Wakati mgandamizo huo mdogo wa hewa ukiendelea kuimarika, unatarajiwa pia kusogea kuelekea baadhi ya maeneo ya pwani ya nchi yetu kuanzia usiku wa kuamkia siku ya Ijumaa tarehe 3 Mei 2024.

Aidha, mgandamizo huo mdogo wa hewa unatarajiwa kuendelea kuwepo katika maeneo ya ukanda wa pwani ya nchi yetu hadi tarehe 6 Mei 2024. Hata hivyo, mgandamizo huo mdogo wa hewa unatarajiwa kupungua nguvu baada ya tarehe 6 Mei 2024.

Uwepo wa mgandamizo huo mdogo wa hewa unatarajiwa kutawala na kuathiri mifumo ya hali ya hewa hapa nchini ikiwa ni pamoja na kusababisha vipindi vya mvua kubwa na upepo mkali katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani, Morogoro, Dar es Salaam na maeneo ya jirani.

Makamu wa Rais wa Tanzania Dkt. Philip Mpango amesema Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amemuagiza awaambie Wafa...
01/05/2024

Makamu wa Rais wa Tanzania Dkt. Philip Mpango amesema Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amemuagiza awaambie Wafanyakazi wa Tanzania kuwa endapo hali ya uchumi wa Taifa itaendelea kuwa stahimilivu na kudumu k**a ilivyo sasa basi Wafanyakazi wawe na matumaini kwamba atasema jambo hivi karibuni kuhusu nyongeza ya mishahara.

Akiongea leo wakati wa Maadhimisho ya Mei Mosi, Dkt. Mpango amesema “Kuhusu nyongeza ya mishahara k**a mlivyosema kwenye risala yenu mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali ilipandisha kima cha chini cha mishahara kwa 23.3% kutoka Tsh. 300,000 hadi Tsh. 370,000 kwa mwezi lengo likiwa ni kuwezesha Watumishi wenye mishahara ya kima cha chini kumudu gharama za maisha kadri inavyowezekana”

“Makundi mengine ya Watumishi nayo yaliguswa na ongezeko hilo la mishahara kwa viwango tofauti kwa kuzingatia ukomo wa bajeti ya mishahara iliyotengwa, k**a ambavyo tumekuwa tukisema Serikali itaendelea kuhuisha viwango vya mishahara kwa kuzingatia uwezo wa kiuchumi na kibajeti pamoja na ujuzi na utendaji wa Waajiriwa, haya ni muhimu ili kuepuka kuchochea mfumuko wa bei, kuhatarisha uhimilivu wa deni la Taifa na athari nyingine kwenye utulivu wa uchumi wa Taifa kwa ujumla”

“Haya yote lazima yazingatiwe katika mchakato wa kuongeza mshahara hususani katika kipindi ambapo uchumi wa Dunia umekumbwa na misukosuko mingi ikiwemo Vita za Urusi na Ukraine na vita vya Mashariki ya Kati inayohusisha Palestina, Israel, Lebanon, Syria na Iran na kufanya kuvurugika kwa bei ya ugavi na kupanda sana kwa bei ya chakula ,mbolea, mafuta n.k”

“Kama hiyo haitoshi Dunia imekumbwa na majanga mengine ikiwemo mvua kubwa na maporomoko ya ardhi ambayo yamesababisha uharibifu mkubwa wa miundombinu, magonjwa na hata vifo, changamoto zote hizi zimeathiri uchumi wetu lakini bado pamoja na haya yote tathmini tulizofanya ndani na zilizofanywa na IMF, Benki ya Dunia n.k zimeonesha uchumi wa Taifa umekuwa stahimilivu kwa kiasi cha kuridhisha na Nchi yetu inakopesheka”

“Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mama wa Taifa ameniagiza niwaambie Wafanyakazi wa Tanzania kuwa endapo hali hiyo itadumu Wafanyakazi wawe na matumaini kwamba atasema jambo hivi karibuni“

Heri ya Sikukuu ya wafanyakazi👏
01/05/2024

Heri ya Sikukuu ya wafanyakazi👏

  Moja ya story kubwa kule Marekani ni kubuma kwa show ya rapa wa Migos Quavo ukumbi wa Hartford Healthcare Ampitheater,...
29/04/2024

Moja ya story kubwa kule Marekani ni kubuma kwa show ya rapa wa Migos Quavo ukumbi wa Hartford Healthcare Ampitheater, Connecticut Marekani wikiendi hii.

Ukumbi huo una uwezo wa kuchukua mashabiki 5700 lakini waliojiotokeza kushuhudia show hiyo ya Quavo walikuwa watu zaidi ya 100 tu.

Taarifa hiyo imeibua muendelezo wa bifu zito linaloendelea kati ya Quavo na Chris Brown, ambapo inasemekana amenunua tiketi za show hiyo ili kumfelisha Quavo.

Tukio k**a hilo liliwahi kutokea kwa 50 Cent kununua tiketi za mbele kwenye show ya Ja Rule na kukaa peke yake ili kuonekana show hiyo haikuingiza watu.

“Serikali ya Awamu ya Sita kupitia Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania, sasa imeweka mpango wa kuwasomesha vijana watano k...
29/04/2024

“Serikali ya Awamu ya Sita kupitia Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania, sasa imeweka mpango wa kuwasomesha vijana watano kila mwaka kwa kuwapa ufadhili nje ya nchi ili kusudi waweze kujifunza teknolojia ya nyuklia katika kiwango ambacho sisi hapa nchini hatujafikia.” - Profesa Lazaro Busagala, Mkurugenzi wa Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania

Wanaobeza Muungano ni ‘mbilikimo’Mbunge wa Viti Maalumu, Mwantum Dau Haji amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kudum...
23/04/2024

Wanaobeza Muungano ni ‘mbilikimo’

Mbunge wa Viti Maalumu, Mwantum Dau Haji amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kudumisha muungano na kuwataka Watanzania wote kudumisha muungano huo.

Mwantum amesema hayo Bungeni jijini Dodoma wakati akichangia Bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

“Changamoto zilizobakia katika Muungano sio kubwa sana na hizi Rais wangu atazimaliza moja baada ya nyingine, tuendelee na Muungano wetu na wale wanaobeza Muungano basi hawa tuseme hawaoni, hawana macho na tunasema hawa ni mbilikimo,” amesema Mwantum

Comment ziwe fupi fupi
23/04/2024

Comment ziwe fupi fupi

23/04/2024
Mh.Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza kwa njia ya mtandao na mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania nje ya nchi walipokuwa ...
22/04/2024

Mh.Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza kwa njia ya mtandao na mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania nje ya nchi walipokuwa kwenye mkutano unaojadili kuhusu mkakati wa Diplomasia ya Umma na Tathmini ya Kiutendaji (Retreat) uliofanyika Kibaha mkoani Pwani leo.

Mwili wa aliyekuwa Mtangazaji wa Clouds Media Group, Gardner G. Habash ukiwa katika viwanja vya Leaders kwa ajili ya wao...
22/04/2024

Mwili wa aliyekuwa Mtangazaji wa Clouds Media Group, Gardner G. Habash ukiwa katika viwanja vya Leaders kwa ajili ya waombolezaji kutoa heshima za mwisho.

Mazishi ya Gardner yanatarajiwa kufanyika Aprili 23 mwaka huu Kijiji cha Kikelelwa wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro.

WATU 13 WAFARIKI KWENYE AJALI LINDIWatu 13 wamefariki dunia na wengine 6 kujeruhiwa baada ya basi dogo la abiria aina ya...
22/04/2024

WATU 13 WAFARIKI KWENYE AJALI LINDI

Watu 13 wamefariki dunia na wengine 6 kujeruhiwa baada ya basi dogo la abiria aina ya Hiace kugonganga uso kwa uso na roli la mafuta kwenye eneo la Somanga lililopo wilayani Kilwa mkoani Lindi.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Lindi ACP John Imori amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo huku majeruhi wakiendelea na matibabu kwenye kituo cha afya Tingi na Hospitali ya wilaya ya Kilwa.

  Jumatatu Aprili 22, 2024
22/04/2024



Jumatatu Aprili 22, 2024

MICHEZO: Msimu wa 2023/24 ni mchungu kwa Wanasimba, hiyo ni baada ya Simba kufungwa magoli 2-1 dhidi ya Yanga, ikimaanis...
20/04/2024

MICHEZO: Msimu wa 2023/24 ni mchungu kwa Wanasimba, hiyo ni baada ya Simba kufungwa magoli 2-1 dhidi ya Yanga, ikimaanisha imefungwa mechi zote mbili dhidi ya Wapinzani wao wa Jadi katika Ligi Kuu Msimu huu

Magoli ya Stephane Aziz Ki (20) kwa penati 20 na Joseph Guede (38) yameifanya Simba ambayo imepata goli lake kupitia kwa Freddy Kouablan (73) kujiweka mbali katika mbio za ubingwa

Yanga ina pointi 58 katika mechi 22 na inaongoza msimamo wa Ligi Kuu, Azam FC nafasi ya pili kwa pointi 51 mechi 23, Simba ni ya tatu ikiwa na pointi 46 katika michezo 21

Ukipewa dakika mbili za kuongea unaongea nini???
20/04/2024

Ukipewa dakika mbili za kuongea unaongea nini???

Kipindi cha pili kimeanza.
20/04/2024

Kipindi cha pili kimeanza.

Address

Ghana Hill
Mbeya
3445

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sweet fm radio 90.5 mbeya posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sweet fm radio 90.5 mbeya:

Videos

Share

Category

Nearby media companies


Other Radio Stations in Mbeya

Show All

You may also like