BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA

BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA BOMBA FM RADIO broadcasting live from MBEYA CITY - TANZANIA.(Iringa,Mbeya,Rukwa,Njombe & Ruvuma). Tus

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe Dkt.Samia Suluhu Hasaan amesema kufuatia ziara ya kikazi iliyofanywa na Rais...
22/06/2024

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe Dkt.Samia Suluhu Hasaan amesema kufuatia ziara ya kikazi iliyofanywa na Raisi wa Ginne-Bissau Mhe.Embalo wamejadiri mambo mengi ikiwa ni pamoja na kukuza ushirikiano na Nchi nyinge barani Afrika.

Rais Samia amesema katika sekta kilimo Tanzania na Ginne-Bissau zitashirikian kukuza thamni ya Zao la kororsho huku wakijadiri pia kukuza uchumi wa Bluu.

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hasaan amempokea Mgeni wake Rais Umaro Sissoco Embalo wa Jamhur...
22/06/2024

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hasaan amempokea Mgeni wake Rais Umaro Sissoco Embalo wa Jamhuri ya Ginne-Bissau aliyekuja Kwaajiri ya ziara ya kikazi.Mapokezi hayo yamefanyika Leo Juni,22 katika Ikulu ya Dar es salaam.

Wakulima wa zao la Pareto Mkoani Mbeya wametakiwa kulima kilimo Bora Ili kuongeza zaidi uzalishaji na kujiongezea kipato...
22/06/2024

Wakulima wa zao la Pareto Mkoani Mbeya wametakiwa kulima kilimo Bora Ili kuongeza zaidi uzalishaji na kujiongezea kipato ili wanufaike na kilimo hicho.

Akizungumza wakati wa mahojiano na Rdio Bomba FM Afisa kilimo na uvuvi kutoka halmashauri ya Wilaya ya Mbeya Gidion Mapunda amewataka wananchi kuzingatia ubora wa Pareto Kwani zao hilo linafanya vizuri kwa Sasa kwenye soko la kimataifa.

Hata hivyo amewaasa wakulima kuacha kufanya udanganyifu wa kuchanganaya maua ya zao hilo na vitu vingine ili kuongeza uzito Kwa lengo la kupata Fedha zaidi.Pia amewasihi wakulima kufuata njia nzuri za ukaushaji wa maua ya zao hili ili Taifa la Tanzania liendelee kujizolea umaarufu zaidi katika ushindani wa Soko.

Mwisho amesema Kwa kushirikiana na maafisa ugani katika kata zote Mkoa wa Mbeya wataendelea kutoa Elimu kwa wakulima mbali mbali katika maeneo ya Mkoa wa Mbeya Ili kuwasaidia wananchi kufanya kilimo Bora na kuwakomboa wananchi kutoka katika kilimo kisicho tija.

✍️

Tunaianza Weekend kwa kusanuana. Eti mdau unaweza tuambia biashara za hao watu kutokana na Viatu vyao??It's Frahiday 😂😂😂...
21/06/2024

Tunaianza Weekend kwa kusanuana. Eti mdau unaweza tuambia biashara za hao watu kutokana na Viatu vyao??

It's Frahiday 😂😂😂😂

Tunawatakia sikukuu njema ya Eid al - Adha.
17/06/2024

Tunawatakia sikukuu njema ya Eid al - Adha.

Msimamizi wa Chumba cha Habari hapa Bomba fm   ametangaza kuuaga u bachelor na sasa ni Bwana harusi Mtarajiwa Karibu new...
17/06/2024

Msimamizi wa Chumba cha Habari hapa Bomba fm ametangaza kuuaga u bachelor na sasa ni Bwana harusi Mtarajiwa
Karibu news Room Shemeji ni wazi sasa News Room iko salama zaidi

BOMBA Fm tunaungana na Wakuu wa nchi na serikali Duniani kote, 😁😁pokea Pongezi hizi na endeleeni kuishi katika Ubora😂🙏

Michuano ya Bomba Bonanza imehitimishwa hii leo huku kikosi cha Wanzani Fc kikiibuka Bingwa wa michuano hiyo.Mshindi wa ...
11/06/2024

Michuano ya Bomba Bonanza imehitimishwa hii leo huku kikosi cha Wanzani Fc kikiibuka Bingwa wa michuano hiyo.

Mshindi wa Kwanza - Wanzani Fc
Mshindi wa Pili - Ilasilo Fc
Mshindi wa Tatu - Galula Fc

Baada ya Wilaya ya Songwe Bomba Bonanza inaelekea wapi, baki hapahapa tutakujuza.

Ni maji kweli haya au kamnyeso Eti     kwakuwa nyie ni mashuhuda leteni maneno hapa😁😁
09/06/2024

Ni maji kweli haya au kamnyeso Eti
kwakuwa nyie ni mashuhuda leteni maneno hapa😁😁

Ni mwendo wa Shangwe na vibe hapa Dimba la Itindi Ni Bomba Bonanza 2024 wilaya ya Songwe Mkoani Songwe
09/06/2024

Ni mwendo wa Shangwe na vibe hapa Dimba la Itindi
Ni Bomba Bonanza 2024 wilaya ya Songwe Mkoani Songwe

Nani Kuicheza Fainal ya Bomba Bonanza 2024
09/06/2024

Nani Kuicheza Fainal ya Bomba Bonanza 2024

Mchezo Wenye hadhi ni Nusu Fainal ya Bomba Bonanza kata ya Galula wilaya ya Songwe Mkoani Songwe.Na kesho itapigwa Faina...
09/06/2024

Mchezo Wenye hadhi ni Nusu Fainal ya Bomba Bonanza kata ya Galula wilaya ya Songwe Mkoani Songwe.
Na kesho itapigwa Fainal hapa

Mashabiki wa kariakoo wako hapa kushuhudia Bomba Bonanza 2024 kata ya Galula wilaya ya Songwe Leo inapigwa Nusu Fainal y...
09/06/2024

Mashabiki wa kariakoo wako hapa kushuhudia Bomba Bonanza 2024 kata ya Galula wilaya ya Songwe

Leo inapigwa Nusu Fainal ya kigaidi kabisa hapa

📷

WATUMISHI TUMIENI MUDA WA ZIADA KUKUZA VIPAJI VIWASAIDIE KATIKA MAISHA YENUWatumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbey...
08/06/2024

WATUMISHI TUMIENI MUDA WA ZIADA KUKUZA VIPAJI VIWASAIDIE KATIKA MAISHA YENU

Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya wametakiwa kutumia muda wa ziada kukuza vipaji walivyonavyo ili viwe msaada katika maisha yao.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya Dkt. Godlove Mbwanji, wakati akihitimisha wiki ya Tamasha la Michezo na Vipaji liloshirikisha watumishi kutoka Hospitali hapo.

Dkt. Mbwanji ameitaka jamii kuwa na tabia ya kutenga muda wa ziada kwaajili ya kufanya mazoezi kwa lengo la kuimarisha afya na kupelekea kuepukana na magonjwa mbalimbali ikiwemo magonjwa yasiyoambukiza.

Dkt. Uwesu mchepange ni Mwenyekiti wa Kamati ya Tamasha la Michezo na Vipaji MZRH, amesema lengo la tamasha hilo kwa watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya ni kuwaleta watumishi pamoja na kuibua vipaji mbalimbali walivyonavyo.

Kwa upande wao washiriki wa tamasha hilo la michezo na vipaji MZRH wameushukuru uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya chini ya Dkt. Godlove Mbwanji, kwa kuwa imekuwa sehemu ya burudani pamoja na kuwaimarisha kiafya na hivyo kuepukana na magonjwa yasiyoambukiza.

Tamasha hilo limefanyika kwa muda wa wiki moja chini ya udhamini wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya likihusisha michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, kuvuta Kamba, maonyesho ya mavazi, maigizo, mpira wa pete, mpira wa wavu, ambapo washindi wamekabidhiwa zawadi ya pesa taslimu pamoja na vikombe.

Bomba Bonanza linaendelea kutimua Vumbi kata ya Galula wilayani Songwe mkoani Songwe
08/06/2024

Bomba Bonanza linaendelea kutimua Vumbi kata ya Galula wilayani Songwe mkoani Songwe

Mchezo wa kwanza umemaliza kwa team ya Nyumbani kutupwa nje ya mashindano
08/06/2024

Mchezo wa kwanza umemaliza kwa team ya Nyumbani kutupwa nje ya mashindano

Ni Bomba Bonanza Kata ya GALULA wilayani Songwe mkoani SongweHuku linapigwa Bonanza la siku 4 kuanzia Jana Tareh 7 hadi ...
08/06/2024

Ni Bomba Bonanza Kata ya GALULA wilayani Songwe mkoani Songwe

Huku linapigwa Bonanza la siku 4 kuanzia Jana Tareh 7 hadi tareh 10

RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI, miongoni mwa walioteuliwa ni Zuhura Yunus aliyekuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu.
06/06/2024

RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI, miongoni mwa walioteuliwa ni Zuhura Yunus aliyekuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu.

RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI, miongoni mwa walioteuliwa ni Zuhura Yunus aliyekuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu.
06/06/2024

RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI, miongoni mwa walioteuliwa ni Zuhura Yunus aliyekuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu.

RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI.Zuhura Yunus aliyekuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu naye yumo.
06/06/2024

RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI.
Zuhura Yunus aliyekuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu naye yumo.

Utasikia mengi kuhusu Mfuko wa Mawasiliano kwa wote  ikiwemo kuhusu mradi wa ujenzi wa minara 758 nchini.
05/06/2024

Utasikia mengi kuhusu Mfuko wa Mawasiliano kwa wote ikiwemo kuhusu mradi wa ujenzi wa minara 758 nchini.



Mbeya: Watu 13 wamefariki Dunia na wengine kujeruhiwa katika eneo la Mbembela Jijini Mbeya katika barabara kuu ya Mbeya ...
05/06/2024

Mbeya:

Watu 13 wamefariki Dunia na wengine kujeruhiwa katika eneo la Mbembela Jijini Mbeya katika barabara kuu ya Mbeya – Tunduma, ambapo Gari namba T.979 CVV likiwa na Tela namba T.758 BEU Scania ikiendeshwa na Dereva aliyefahamika kwa jina la Ross Mwaikambo [40] likitokea Shamwengo likiwa limepakia kokoto, aligongana na Gari namba T.167 DLF Toyota Coaster kisha kugongana na Gari namba T.120 DER Toyota Harrier iliyokuwa ikiendeshwa na Dokta.Robert Francis Mtungi [48] Mkazi wa Isyesye.

Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya BENJAMIN KUZAGA, Lori hilo liliendelea kugonga Guta namba MC 660 BCR kisha kugonga Pikipiki namba MC 889 CKX na kusababisha vifo vya watu kumi na tatu (13) kati yao wanawake 5, wanaume 8 na majeruhi kumi na nane [18] kati yao wanawake 4 na wanaume 14.

Majeruhi wamepelekwa katika Hospitali ya Rufaa Mbeya kwa matibabu na miili ya marehemu imepelekwa Hospitalini hapo kwa hifadhi na kusubiri kutambuliwa.

Chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa Dereva wa Lori kushindwa kulimudu gari kwenye mteremko.

Kamanda KUZAGA amesema tayari wanamshikilia Dereva wa Gari hilo ambaye anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya akiwa chini ya ulinzi.

Ndani ya mizuka ya Burudani🔥🔥
05/06/2024

Ndani ya mizuka ya Burudani🔥🔥

Leo ndani ya MIZUKA YA BURUDANI atapita queen wa Bongo fleva
04/06/2024

Leo ndani ya MIZUKA YA BURUDANI atapita queen wa Bongo fleva

Ni siku 4 nzito Pale kata ya Galula wilaya ya Songwe Mkoani Songwe Tutaisimamisha songwe kuanzia tareh 7 hadi tareh 11/6...
03/06/2024

Ni siku 4 nzito Pale kata ya Galula wilaya ya Songwe Mkoani Songwe

Tutaisimamisha songwe kuanzia tareh 7 hadi tareh 11/6/2024

Wakazi wa Songwe kaa tayari

SUGU ashinda Uchaguzi Chadema kanda ya Nyassa,1. Joseph Mbilinyi (Sugu) kura 54 sawa na 51%2. Peter Msigwa (Baba Jimmy) ...
29/05/2024

SUGU ashinda Uchaguzi Chadema kanda ya Nyassa,
1. Joseph Mbilinyi (Sugu) kura 54 sawa na 51%
2. Peter Msigwa (Baba Jimmy) kura 52 sawa na 49%

Hongera sana TAITA

SONGWE.Baada ya Halmashauri ya Wilaya ya Songwe kuzindua Stendi mpya ya mabasi katika kijiji cha Kaloleni, kumekuwa na m...
21/05/2024

SONGWE.
Baada ya Halmashauri ya Wilaya ya Songwe kuzindua Stendi mpya ya mabasi katika kijiji cha Kaloleni, kumekuwa na malalamiko ya Wananchi wakidai kuongezwa kwa vituo vidogovidogo vya kushushia abiria.

Wakizungumza na Bomba Fm baadhi ya Wananchi wameeleza kuwa kutoka stendi ilipo hadi kituo kinachofuata eneo zilipo Ofisi za Halmashauri kuna umbali mrefu na kuiomba Halmashauri iongeze vituo vidogo ambavyo vitawasaidia abiria kushuka hususani katikati ya mji wa Mkwajuni au eneo la stendi mpya iliyokuwa ikitumika awali.

Pia wamesema wapo Wananchi ambao hupata huduma za matibabu katika Hospitali ya Mwambani ambayo imekuwepo kwa muda mrefu sasa, hivyo kutokuwepo kwa vituo vingine itawawia vigumu kuanza kuchukua usafiri mwingine kwenda hospitalini hapo ambao ni gharama.

Kutokana na malalamiko hayo, Mwandishi wetu Heneliko Malo akamtafuta Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe ABRAHAM SAMBILA ambaye ameeleza kuwa bado hawajapata malalamiko kutoka kwa Wananchi na kwamba wenye malalamiko wanatakiwa wafike Ofisi ya Halmashauri ili waweze kusikilizwa na halmashauri ifanyie kazi.

"hao wanaolalamika mbona sisi kwetu hawafiki wanawafuata nyinyi watu wa Bomba Fm, si waje kwa Mkurugenzi k**a kuna hitaji Mkurugenzi atalileta kwenye vikao tuone k**a hoja hiyo ni ya msingi basi tuweze kuona ni namna gani k**a kuna hitaji kuweka vituo vingine, lakini hivyo vituo tulivyoviweka vimekubaliwa na wadau wote na watu wamefurahia sana kupata ile stendi na utaratibu tuliouweka" alisema Abraham Sambila.

Stendi hiyo ya Wilaya imejengwa kwa kutumia mapato ya ndani ya Halmashauri ambapo awamu ya kwanza ya ujenzi imekalimika na kusubiri awamu wa pili.

(Imeandikwa na Heneliko Malo)

Leo Mei,15 ni maadhimisho ya Siku ya Familia Duniani na kwa kulitambua hilo Bomba FM Mbeya tunapenda kuwatakia maadhimis...
15/05/2024

Leo Mei,15 ni maadhimisho ya Siku ya Familia Duniani na kwa kulitambua hilo Bomba FM Mbeya tunapenda kuwatakia maadhimisho mema wanafamilia wetu wa 104.1 MhZ (Wasikilizaji,Wadau na Wapenzi wa Bomba FM Mbeya).

Idadi ya vifo kutokana na mvua iliyosababisha mafuriko katika jimbo la Rio Grande do Sul nchini Brazil imeongezeka na ku...
13/05/2024

Idadi ya vifo kutokana na mvua iliyosababisha mafuriko katika jimbo la Rio Grande do Sul nchini Brazil imeongezeka na kufikia watu 143.

Mamlaka nchini Brazil imesema watu wengine 125 hawajulikani waliko katika jimbo hilo la kusini mwa Brazil ambapo viwango vya maji kwenye mito inaripotiwa kupanda. Idara ya hali ya hewa imesema mvua zinazoendelea kunyesha "zinatia wasiwasi."
Mnamo siku ya Jumamosi, serikali ilitangaza kitita cha dola bilioni 2.34 kwa matumizi ya dharura ili kushughulikia janga hilo ambalo limesababisha zaidi ya watu 538,000 kuyahama makazi yao.
Rais wa Brazil Luiz Inacio Lula da Silva amesema serikali kuu itajenga upya miundombinu yote iliyoharibiwa na mvua katika jimbo hilo la Rio Grande do Sul.
Kwa upande wake, Rais Joe Biden wa Marekani amesema utawala wake unawasiliana na Brazil kwa lengo la kutoa msaada kwa waathiriwa wa mafuriko.................
Story by

Leo ikiwa ni maadhimisho ya Siku ya Mama Duniani, Bomba FM Mbeya tunapenda kuwatakia wasikilizaji wetu hasa akina mama K...
12/05/2024

Leo ikiwa ni maadhimisho ya Siku ya Mama Duniani, Bomba FM Mbeya tunapenda kuwatakia wasikilizaji wetu hasa akina mama Kheri ya siku hii muhimu.

MBEYA.Waziri Mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Khasim Majaliwa amewaagiza Wakuu wa Mikoa yote Nchini...
11/05/2024

MBEYA.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Khasim Majaliwa amewaagiza Wakuu wa Mikoa yote Nchini kuhakikisha wanawaagiza wakuu wa Wilaya kutenga maeneo ya wazi Kwaajili ya mazoezi Kwa wananchi na Wanamichezo Ili kukabiliana na magonjwa yasiyoambukizwa.

Majaliwa wameyasema hayo leo 11,Aprili,2024 alipokuwa mgeni rasmi katika kilele cha mbio za Tulia Marathon zilizofanyika katika Uwanja wa kumbu kumbu ya Sokoine Jijini Mbeya.

Ameongeza kuwa Kwa mujibu wa takwimu kutoka wizara ya Afya wananchi wengi wanapoteza maisha kutokana na magonjwa yasiyo yakuambukizwa k**a Kisukari na Presha hivyo maeneo hayo yatasaidia wananchi kuepukana na magonjwa hayo.

"Sio lazima ukimbie Kilometa 21,10,au 5 ndipo ionekane umefanya mazoezi hata ukikimbia Kilometa 1 tuu inatosha sana lakini kikubwa usiuweke mwili katika hali ya kubweteka tuutukifanya hivi magonjwa haya hatutoyapata" Amesema Majaliwa Khasim Majaliwa (Mb) Waziri Mkuu wa Tanzania
Aidha Kwa upande wake Naibu Waziri wa Sanaa na Michezo Mhe. Hamis Mwinjuma

Address

P O Box 579
Mbeya
255

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 17:00
Saturday 08:00 - 00:30

Telephone

+255753451045

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA:

Videos

Share

Category

Nearby media companies


Other Radio Stations in Mbeya

Show All

You may also like