Kicora FM

Kicora FM 98.9 FM Kigoma
Jitambue! Wewe Ni Nyota!
📧 [email protected]
📱 +255 743251694

W***Y ESSOMBA ONANA.Klabu ya Simba imempa mkono wa kwaheri aliyekuwa kiungo wake W***y Essomba Onana raia wa Cameroon.Ny...
16/08/2024

W***Y ESSOMBA ONANA.

Klabu ya Simba imempa mkono wa kwaheri aliyekuwa kiungo wake W***y Essomba Onana raia wa Cameroon.

Nyota huyo wa Cameroon alijiunga na Simba SC mwezi julai 2023 na kwenye NBC premium league msimu wa 2023/2024 alifunga jumla la magoli manne (4) na pasi moja ya goli assist(1)

✍🏾

UFUNGUZI WA NBC PREMIUM LEAGUE LEO PAMBA JIJI VS TANZANIA PRISON'S.Kocha mkuu wa kikosi cha Pamba jiji ya Mwanza Goran K...
16/08/2024

UFUNGUZI WA NBC PREMIUM LEAGUE LEO PAMBA JIJI VS TANZANIA PRISON'S.

Kocha mkuu wa kikosi cha Pamba jiji ya Mwanza Goran Kopuvonic anaanza maisha yake ya soka ndani ya Pamba jiji huku akikutana na maafande wa jelajela Tanzania Prisons wakiongozwa na kocha wao Mbwana Makata.

Goran Kopuvonic amesema itakuwa mechi yakuvutia sana kwasababu pia kocha wa Tanzania Prisons aliyekuwa kocha wa Pamba jiji amempongeza kwa kuipandisha timu hii ligi kuu ...

NBC premium league msimu wa 2024/2025 leo utepe kukatwa rasmi katika uwanja wa CCM Kirumba Mwanza.

✍🏾

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI AKABIDHI MAKASHA YA KUHIFADHIA SAMAKI.Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Hamisi Ulega baada ya...
15/08/2024

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI AKABIDHI MAKASHA YA KUHIFADHIA SAMAKI.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Hamisi Ulega baada ya kufungua rasmi shughuli za Uvuvi katika ziwa Tanganyika pia amekabidhi Makasha 500 kwa akina mama wafanyabiashara wa samaki ili kupunguza upotevu wa samaki zinazoharibika.




UVUVI ZIWA TANGANYIKA SASA RUKSA.Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mheshimiwa Abdallah Hamisi Ulega amefungua rasmi shughuli za ...
15/08/2024

UVUVI ZIWA TANGANYIKA SASA RUKSA.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mheshimiwa Abdallah Hamisi Ulega amefungua rasmi shughuli za Uvuvi katika ziwa Tanganyika baada ya Kufungwa takribani miezi mitatu.

Waziri Ulega amefanya zoezi hilo la ufunguzi katika Mwalo wa Katonga manispaa ya Kigoma Ujiji Mkoani Kigoma Agosti 15 , 2024 na kubainisha kuwa shughuli za Uvuvi zilisimamishwa kwa miezi hiyo mitatu kwa lengo la kulinda rasilimali za Uvuvi kwenye ziwa hilo.

Ulega ameongeza kuwa uamuzi huo wa Kufunga ziwa ni utekelezaji wa mkataba wa kikanda wa nchi wanachama wa mamlaka wa Tanganyika (LTA) unaoweka hatua za Usimamizi wa Uvuvi Endelevu katika Ziwa Tanganyika.

Aidha , Waziri Ulega ametumia nafasi hiyo kuwaeleza wavuvi kuwa Kufunguliwa kwa shughuli za Uvuvi kuendane na matumizi sahihi ya zana halali zinazokubalika kwa mujibu wa kanuni na sheria za Uvuvi.





Ni kesho ndani ya KICORA Radio    #2024
15/08/2024

Ni kesho ndani ya KICORA Radio



#2024

COUSTAL UNION SAFARINI.Msafara wa kikosi Cha coastal union mangushi umewasili jijini Addis Ababa Ethiopia, ukiwa safarin...
14/08/2024

COUSTAL UNION SAFARINI.

Msafara wa kikosi Cha coastal union mangushi umewasili jijini Addis Ababa Ethiopia, ukiwa safarini kwenda Angola kuifuata Fc Bravos kwenye mchezo wa kombe la shirikisho Afrika ( CAFCC)

Kocha mkuu wa coustal union David oruma amesema wanaenda Angola akiamini mchezo wake wa kwanza atafanya vizuri kuiwakikisha vyema bendera ya Tanzania.

Huku akiamini wamekuwa na mda mrefu bila kuingia katika michuano ya kombe la shirikisho barani afrika...

✍🏾

Serikali ya Tanzania, kupitia Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa kushirikiana na Wizara ...
14/08/2024

Serikali ya Tanzania, kupitia Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa kushirikiana na Wizara ya Ujenzi, inatekeleza Mradi wa Uendelezaji wa Bonde la Msimbazi kwa kiasi cha dola za Marekani milioni 260, ambapo kiasi cha dola milioni 200 ni mkopo nafuu kutoka Benki ya Dunia, dola milioni 30 ufadhili wa Serikali ya Uholanzi na dola milioni 30 ni mkopo kutoka Serikali ya Hispania.

Aidha, Wakala ya Barabara za Vijijini na Mjini Tanzania (TARURA) na Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) ndiyo watekelezaji wa Mradi wa Uendelezaji wa Bonde la Msimbazi kwa niaba ya wizara husika.

✍🏾

SIMBA QUEENS CECAFA.Kocha mkuu wa kikosi Cha simba queens Juma mgunda amesema maandalizi ya timu kuelekea michuano ya CE...
14/08/2024

SIMBA QUEENS CECAFA.

Kocha mkuu wa kikosi Cha simba queens Juma mgunda amesema maandalizi ya timu kuelekea michuano ya CECAFA yamekamilika na kikosi kipo tayari kwaajili ya mashindano..

Mbali na hayo kocha juma mgunda anakili wazi kuwa michuano itakuwa migumu kwasabu Kila timu inayoingia kwenye michuano hiyo ni bingwa katika nchi yake..

Lakini nipende kuwaambia simba queens sports club ni bingwa wa michuano hii ya kombe la CECAFA kwasabu naiamini timu yangu ya simba queens sports club naenda kuludi na kombe.

✍🏾

Shirikisho la soka Afrika (CAF) limetoa rodha mpya ya vilabu bora Afrika kuelekea msimu mpya 2024/25 huku Young Africans...
14/08/2024

Shirikisho la soka Afrika (CAF) limetoa rodha mpya ya vilabu bora Afrika kuelekea msimu mpya 2024/25 huku Young Africans akiwa hayupo miongoni mwa vilabu kumi Bora Barani Afrika

1. Al Ahly (Egypt) – 87 points
2. Esperance (Tunisia) – 61 points
3. Wydad AC (Morocco) – 60 points
4. Mamelodi Sundowns (South Africa) – 54 points
5. Zamalek (Egypt) – 48 points
6. RS Berkane (Morocco) – 42 points
7. Simba (Tanzania) – 39 points
8. Petro de Luanda (Angola) – 39 points
9. TP Mazembe (DR Congo) – 38 points
10. CR Belouizdad (Algeria) – 36 points

✍🏾

FAIDA KUU ZA TANGAWIZI.Wengi tumekuwa tukitumia tangawizi k**a kiungo kwenye vyakula pasipo kuzifahamu faida zake katika...
14/08/2024

FAIDA KUU ZA TANGAWIZI.

Wengi tumekuwa tukitumia tangawizi k**a kiungo kwenye vyakula pasipo kuzifahamu faida zake katika afya zetu...

Hizi hapa ndizo faida kuu kumi za tangawizi ..

1. Huondoa sumu mwilini kwa haraka sana
2. Huondoa uvimbe mwilini
3. Kuna viua vijisumu (antibiotics) vya asili viwili kwenye tangawizi
4. Ni dawa nzuri Kwa kansa ya kwenye damu ( leukaemia)
5. Huua virusi vya homa
6. Huongeza msukumo wa damu mwilini
7. Huzuia damu kuganda
8. Husafisha utumbo mpana
9. Huzuia tatizo la miguu kuwaka moto
10. Husaidia mfumo wa mmeng'enyo wa chakula Kwa haraka zaidi.

✍🏾

Kocha Jackline Juma ameingia katika vitabu vya historia kwa kuwa kocha wa kwanza Mwanamke kwenye ligi kuu nchini Kenya. ...
14/08/2024

Kocha Jackline Juma ameingia katika vitabu vya historia kwa kuwa kocha wa kwanza Mwanamke kwenye ligi kuu nchini Kenya.

Mwanamke huyu ni kocha wa Talanta FC, na inaelezwa kuwa ni mmoja kati ya makocha watatu wanawake wenye CAF License A Kenya nzima.

✍🏾

Wananchi wapatao 4870 wamepatiwa huduma za Ultrasound ikiwemo wajawazito katika Hospitali ya Wilaya ya Songwe ikiwa ni m...
13/08/2024

Wananchi wapatao 4870 wamepatiwa huduma za Ultrasound ikiwemo wajawazito katika Hospitali ya Wilaya ya Songwe ikiwa ni miaka mitatu tangu kuanza rasmi kutoa huduma kwa Hospitali hiyo hali iliyo kupunguza rufaa kwa wagonjwa.

Hayo yamebainishwa na Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Dkt. Ntufye Kapesa wakati akielezea hali ya utoaji wa huduma za matibabu kwenye hospitali hiyo.

Dkt. Ntufye amesema mbali ya Utrasound vilevile hospitali imekuwa ikitoa huduma za mionzi (X-Ray) ambapo imeweza kuwahudumia wangonjwa zaidi ya 1760.

Katika hatua nyingine Dkt. Ntufye amesema kuwa, Hospitali ya Wilaya ya Songwe kupitia jengo la dharura lenye vifaa vya kisasa lililoanza kutoa huduma toka Oktoba, 2023 limeweza kuhudumia wagonjwa 890 wa dharura hadi sasa.

Dkt. Ntufye ametumia fursa hiyo kuishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kupeleka watumishi kwenda kusoma na kujifunza namna ya kutumia vifaa hivyo.

✍🏾

ASILIMIA 10 PEKEE KUKAMILIKA UJENZI WA DARAJA LA JPMUjenzi wa Daraja la Magufuli linalounganisha Kigongo na Busisi umefi...
13/08/2024

ASILIMIA 10 PEKEE KUKAMILIKA UJENZI WA DARAJA LA JPM

Ujenzi wa Daraja la Magufuli linalounganisha Kigongo na Busisi umefikia asilimia 90, hatua ambayo ni muhimu katika kukamilisha mradi huo mkubwa wa miundombinu nchini Tanzania. Daraja hili, lenye urefu wa kilomita 3.2, litakuwa daraja refu zaidi Afrika Mashariki, likirahisisha usafiri na kukuza shughuli za kiuchumi kati ya Mwanza na maeneo ya jirani.

Mafanikio haya yamepatikana kutokana na juhudi za serikali na wadau mbalimbali, ambapo ujenzi umeendelea kwa kasi huku ukizingatia viwango vya kimataifa. Kukamilika kwa daraja hili kutaleta mapinduzi makubwa katika usafirishaji na kuchochea maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi wa kanda ya ziwa na taifa kwa ujumla.

✍🏾

HIFADHI YA MAJI YAGUNDULIWA KATIKA MIAMBA YA SAYARI YA MARSWanasayansi wamegundua hifadhi ya maji kwenye sayari ya Mars ...
13/08/2024

HIFADHI YA MAJI YAGUNDULIWA KATIKA MIAMBA YA SAYARI YA MARS

Wanasayansi wamegundua hifadhi ya maji kwenye sayari ya Mars - ndani ya miamba ya sayari hiyo .

Ugunduzi huo unatokana na uchambuzi mpya wa data kutoka kwa chombo Cha NASA kilichochunguza matukio katika sayari hiyo mnamo 2018

Chombo Hicho kilitumia kipima mtetemo ambacho kilirekodi mitetemeko ya miaka minne - mitetemeko ya mars kutoka ndani kabisa ya sayari nyekundu

Kuchambua matetemeko hayo - na jinsi sayari inavyosonga kulibaini ishara za uwepo wa maji

✍🏾

MWANAFUNZI NCHINI MAREKANI ADAIWA KUMUUA MWALIMU WAKE KWA RISASIKatika tukio la kushtua huko Detroit, Michigan, mtoto wa...
13/08/2024

MWANAFUNZI NCHINI MAREKANI ADAIWA KUMUUA MWALIMU WAKE KWA RISASI

Katika tukio la kushtua huko Detroit, Michigan, mtoto wa k**e mwenye umri wa miaka 8 anadaiwa kumpiga risasi na kumuua mwalimu wake wa mazoezi ya viungo, Jim Turner (56). Tukio hili la kusikitisha lilitokea Agosti 12, 2024, baada ya mtoto huyo kuingiza silaha ya baba yake shuleni.

Kulingana na taarifa, wakati darasa la mazoezi likiendelea, mwalimu huyo alimpeleka mtoto huyo ofisini kwake kwa sababu zisizojulikana. Hata hivyo, dakika chache baadae, milio ya risasi ilisababisha wanafunzi kukimbia kwa hofu huku mwalimu Turner akipoteza maisha.

Polisi na mamlaka husika wanachunguza kwa kina tukio hili ili kubaini sababu ya mtoto huyo kuchukua hatua hiyo. Shule imetoa taarifa ya rambirambi na msaada wa kisaikolojia kwa wanafunzi na walimu walioathirika.

✍🏾

KAZINI KWA FREDDY NA MKWALA KUNA KAZI...Klabu ya simba sports imekamilisha uhamisho wa mshambuliaji LIONEL ATEBA. Kwa mk...
13/08/2024

KAZINI KWA FREDDY NA MKWALA KUNA KAZI...

Klabu ya simba sports imekamilisha uhamisho wa mshambuliaji LIONEL ATEBA. Kwa mkataba wa miaka miwili Kwa ada ya Dola $200,000/=
Sawa na Tsh 542,000,000/=

Ateba mwenye umri wa miaka (25) Raia wa Cameroon alijiunga na usm Alger mnamo January 2024 Kwa dau la Dola laki tatu akitokea Dynamo douala ya nyumbani kwao Cameroon...

Amecheza mechi kumi na sita (16) akiifungia usm Alger bao Moja (1) na assist (8)

Lionel ateba kimbinu ndani ya uwanja anapenda sana kutoa pasi ya mwisho kuzalisha goli Bali sio kufunga ...

✍🏾

“Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika mwaka wa Fedha 2024/2025 imetenga fedha ya TZS bilioni 7.3 kwa ajili ya ununuzi wa vif...
13/08/2024

“Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika mwaka wa Fedha 2024/2025 imetenga fedha ya TZS bilioni 7.3 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa na kuwakopesha vijana (wa programu ya BBT) wanaofanya kazi katika maeneo hayo punde wanapohitimu mafunzo ili kuwawezesha kujiajiri.” – Ridhiwani Kikwete, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu)

Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) - Mloganzila imefanya huduma ya Ubingwa Bobezi ya upasuaji wa kupandikiza figo kwa wa...
13/08/2024

Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) - Mloganzila imefanya huduma ya Ubingwa Bobezi ya upasuaji wa kupandikiza figo kwa wagonjwa wawili ambapo figo imevunwa kutoka kwa mchangiaji kwa kutumia utaalam na njia ya kisasa ya tundu dogo (Hand Assisted Laparascopic Donor Nephrectomy)

Utaalam huu unatumika Muhimbili pekee kwa hapa nchini.

✍🏾

"Mkuu wa Mmoa wa Kigoma Anawatakia wananchi wote wa mikoa ya kigoma na Tabora maadhimisho ya sikukuu ya nane nane 2024"
08/08/2024

"Mkuu wa Mmoa wa Kigoma Anawatakia wananchi wote wa mikoa ya kigoma na Tabora maadhimisho ya sikukuu ya nane nane 2024"

Kicorafmtz tunawatakia nanenane njema
08/08/2024

Kicorafmtz tunawatakia nanenane njema

WANANCHI TUMIENI HUDUMA YA MAJITAKA YA KUWASAMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Kigoma (KUWASA) inatoa wito kwa w...
06/08/2024

WANANCHI TUMIENI HUDUMA YA MAJITAKA YA KUWASA

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Kigoma (KUWASA) inatoa wito kwa wananchi kutunza mazingira kwa kutumia huduma ya maji taka ambayo inawezesha kuacha mazingira yakiwa safi na salama.

Wito huo umetolewa na Meneja wa Usafi wa Mazingira KUWASA, Bi Yasinta Jovini, wakati akizungumza kupitia kipindi cha Morning Jam cha Redio Kicora Fm 98.9 ambapo amesisitiza huduma ya maji taka inayotolewa na Mamlaka imekidhi vigezo vya kimataifa.

Bi Yasinta ameeleza kuwa KUWASA inalo gari la kisasa ambalo linafanya kazi ya kukusanya maji taka na kuyapeleka katika mabwawa maalumu. Hivyo, wananchi wanatakiwa kutumia utaratibu huo rasmi ambao utaepusha kuharibu na kuchafua mazingira.

Aidha, amesisitiza kuwa suala la utunzaji wa mazingira ni shirikishi, hivyo wananchi wanatakiwa kuhakikisha wanapofanya ujenzi wa nyumba miundombinu ya maji taka inawekwa sehemu ambayo ni rahisi kufikika ili kurahisisha zoezi la kuyaondoa pindi inapohitajika kufanya hivyo.

Kicorafmtz tunakutakia kheri ya wiki ya unyonyeshaji duniani 1-7/8/2024        Kauli mbiu "Tatua changamoto :Saidia Unyo...
03/08/2024

Kicorafmtz tunakutakia kheri ya wiki ya unyonyeshaji duniani 1-7/8/2024

Kauli mbiu "Tatua changamoto :Saidia Unyonyeshaji kwa mtoto"

Kicorafmtz inakutakia kheri ya wiki ya unyonyeshaji duniani                         kaulimbiu "Tatua changamoto : Saidia...
03/08/2024

Kicorafmtz inakutakia kheri ya wiki ya unyonyeshaji duniani

kaulimbiu
"Tatua changamoto : Saidia Unyonyeshaji kwa Mtoto"

Leo Ijumaa tarehe 2/8/2024 shekhe mkamba atakuwa live kicora radio katika kipindi cha Ijumaa kareem atazungumzia kuhusu ...
02/08/2024

Leo Ijumaa tarehe 2/8/2024 shekhe mkamba atakuwa live kicora radio katika kipindi cha Ijumaa kareem atazungumzia kuhusu umuhimu wa ibaada ya kuchinja

Karibu ujifunze mambo mbalimbali kuhusu ibaada ya kuchinja nautaruhusiwa kuhoji ama kuuliza maswali mbalimbali kuhusu ibaada ya kuchinja

IJUE BILI YAKO KWA KUSIKILIZA MORNING JAM YA  K**A UNA SWALI LOLOTE ULIZA HAPA NA   WATAKUPA MAJIBU   💦
19/07/2024

IJUE BILI YAKO KWA KUSIKILIZA MORNING JAM YA
K**A UNA SWALI LOLOTE ULIZA HAPA NA WATAKUPA MAJIBU


💦

*WAJIBU NA HAKI ZA MTUMIAJI WA HUDUMA YA MAJI*Mkurugenzi wa huduma kwa wateja wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa mazingi...
16/07/2024

*WAJIBU NA HAKI ZA MTUMIAJI WA HUDUMA YA MAJI*

Mkurugenzi wa huduma kwa wateja wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa mazingira Kigoma (KUWASA), Ndugu Boniphace Kohoye, ametoa wito kwa watumiaji wa huduma ya maji kutambua haki na wajibu wao ili kuboresha matumizi ya huduma hiyo.

Akizungumza kupitia kipindi cha Radio cha Morning Jam,Kicora Fm Kohoye ametaja baadhi ya haki za mtumiaji huduma ikiwemo Haki ya Kutoa Maoni na Malalamiko na kusema Kila mteja anayo haki ya kueleza jambo lolote ambalo anaona halijamridhisha katika kupatiwa huduma ya maji.Mteja anaweza kutoa maoni au malalamiko yake kwa KUWASA kwa lengo la kuboresha huduma.

Haki nyingine ambayo ameitaja ni Kupata Ufafanuzi."Mteja anayo haki ya kupata ufafanuzi kutoka KUWASA kuhusu huduma anazopokea. Hii inajumuisha haki ya kuuliza maswali na kupata majibu kuhusu bili za maji, ubora wa maji, na matatizo mengine yanayohusiana na huduma za maji"alisema Boniphace Kohoye Mkurugenzi wa huduma kwa wateja KUWASA.

Aidha kwa upande wa wajibu wa mtumiaji wa huduma ya Maji Kohoye ameeleza moja ya wajibu ni Kulipa Ankara za Maji kwa wakati ambapo amesisitiza Watumiaji wa maji wanawajibika kulipa ankara za maji au bili kwa wakati. Hii inasaidia KUWASA kutekeleza majukumu yake na kuendelea kutoa huduma bora.

Aidha Mteja anao wajibu wa kutoa taarifa zozote zinazoweza kusaidia Mamlaka kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi. Taarifa hizi zinaweza kujumuisha ripoti za uvujaji wa maji, wizi wa maji, au matatizo mengine yanayohusiana na huduma ya maji.

Ndugu Kohoye akizungumza kupitia kipindi cha redio cha Morning Jam kilichorushwa na Kicora FM, alisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya watumiaji wa maji na Mamlaka ya KUWASA ili kuhakikisha huduma bora na endelevu kwa jamii.

UTEUZIRaus wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amemteua na kumuapisha Suleiman Abubakar Mombo kuwa mkurugenzi mkuu wa ...
11/07/2024

UTEUZI

Raus wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amemteua na kumuapisha Suleiman Abubakar Mombo kuwa mkurugenzi mkuu wa idara ya usalama wa Taifa.

cc.

MARUFUKU KUTOA RUSHWA UKITAKA HUDUMA YA MAJIMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Kigoma (KUWASA) imetoa wito kwa wa...
08/07/2024

MARUFUKU KUTOA RUSHWA UKITAKA HUDUMA YA MAJI

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Kigoma (KUWASA) imetoa wito kwa watu wote wanaotaka kuunganishiwa huduma ya maji kwa mara ya kwanza kutojihusisha na vitendo vya rushwa. Badala yake, wanahimizwa kufika ofisini na kufuata taratibu zilizowekwa.

Akizungumza katika Kipindi cha Morning Jam cha Redio Kicora, mkoani Kigoma, Mkuu wa Kitengo cha Maunganisho Mapya, Alfred Chagu, amesema kuwa Mamlaka imeboresha utoaji wa huduma kwa wateja ili kuhakikisha hakuna rushwa inayotolewa ili kupata huduma hiyo.

Chagu amesema kuwa maboresho yaliyofanywa yanajumuisha kuhakikisha mteja anapojaza fomu na kulipia, huduma ya maji inafungiwa ndani ya siku saba baada ya vipimo kukamilika. Aliongeza kuwa kila wiki, takribani wateja 50 wanapatiwa vifaa na huduma hiyo.

Pia alieleza kuwa vifaa vyote vya maunganisho mapya, kuanzia mita (dira) ya maji pamoja na viunganisho vingine, vinatolewa na Mamlaka pekee. Hivyo, hairuhusiwi kwa mteja kununua vifaa mtaani bali anatakiwa kulipia na kupewa na Mamlaka, na fundi atafika kuunganisha bila malipo ya ziada.

Alfred Chagu ametoa wito kwa wateja wote wapya kufuata taratibu zilizowekwa, ikiwemo kujaza fomu na kulipia kwa wakati. Pia aliwasihi wateja kutoa ushirikiano kwa mafundi wanapofika katika maeneo yao ili kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji.
💦

.waziri9

Manager wa kicora tunakutakia miaka mingi ya  kuishi duniani
11/05/2024

Manager wa kicora tunakutakia miaka mingi ya kuishi duniani

Happy International Workers' Day to all our dedicated listeners.
01/05/2024

Happy International Workers' Day to all our dedicated listeners.

Address

Kigoma

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kicora FM posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Kicora FM:

Videos

Share

Category


Other Radio Stations in Kigoma

Show All

You may also like