Kicora FM

Kicora FM 98.9 FM Kigoma
Jitambue! Wewe Ni Nyota!
📧 [email protected]
📱 +255 754 570 369 & +255 756 736 484

Kicora team tunakutakia kheri ya krisimasi
24/12/2024

Kicora team tunakutakia kheri ya krisimasi

Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) taifa Freeman Mbowe hatimaye ametangaza rasmi kugombea nafasi ...
21/12/2024

Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) taifa Freeman Mbowe hatimaye ametangaza rasmi kugombea nafasi ya Uenyekiti wa chama hicho taifa .

Mbowe ameyasema hayo leo nyumbani kwako Mikocheni Jijini Dar es Salaam wakati akifanya mkutano na wahariri vyombo vya habari nchini.

"Nimetafakair kwa kina sana nimesema mara nyingi nilitamani kuondoka lakini siwezi kuondoka katikati ya minyukano iliyopo CHADEMA nipo nitakuwepo nitagombea... anayetaka kugombea tukutane kwenye boksi". Mbowe

Mkuu wa wilaya ya kigoma Dr.Rashidi chuachua amehuhuria fainali ya main fm cup siku ya leo december 9,2024 katika viwanj...
09/12/2024

Mkuu wa wilaya ya kigoma Dr.Rashidi chuachua amehuhuria fainali ya main fm cup siku ya leo december 9,2024 katika viwanja vya kawawa ujiji mkoani kigoma huku akiwaomba wananchi kutumia nishati safi za kutumia mitungi ya gesi.

Ameyasema hayo baada ya mchezo wa fainali kumalizika timu ya mnalani boda fc kupata ushindi wa bao moja kwa sufuri dhidi ya Mlole sc na kuwataka wananchi kupambana na uchafuzi wa mazingira ili kutumia gesi .

Raisi wa shirikisho la mpira wa miguu tanzania Wallace karia amesema anataka kuona ligi ya Tanzania kwasasa inapiga hatu...
07/12/2024

Raisi wa shirikisho la mpira wa miguu tanzania Wallace karia amesema anataka kuona ligi ya Tanzania kwasasa inapiga hatua kimiundombinu ili msimu unaokuja ligi hiyo ipande kutoka nafasi ya sita mpaka nafasi tatu za juu .

Ameyasema hayo leo tarehe 7,December 2024 katika ukumbi wa Tanganyika hotel Mkoani kigoma huku agenda ikiwa kuangalia tathimini ya mwaka mzima wamefanikiwa wapi na matarajio yao ni yapi k**a Tff msimu unaokuja 2025 Ligi kuu bara na NBC championship na madaraja mengine ya mpira wa miguu.



07/12/2024


Pichani ni Katibu mkuu wizara ya elimu, sayansi na teknolojia Mheshimiwa Prof. Carolyne Nombo na Mkuu wa mkoa wa Kigoma ...
04/12/2024

Pichani ni Katibu mkuu wizara ya elimu, sayansi na teknolojia Mheshimiwa Prof. Carolyne Nombo na Mkuu wa mkoa wa Kigoma Mheshimiwa Thobias Andengenye walipohudhuria katika kongamano la 34 la wanazuoni wa chuo kikuu huria cha Tanzania (OUT) lililofanyika katika kituo cha chuo hicho mkoani Kigoma

Mkuu wa mkoa wa Kigoma Mheshimiwa Thobias Andengenye amewataka wahitimu wa chuo kikuu huria cha Tanzania (OUT) kujitofau...
04/12/2024

Mkuu wa mkoa wa Kigoma Mheshimiwa Thobias Andengenye amewataka wahitimu wa chuo kikuu huria cha Tanzania (OUT) kujitofautisha na wahitimu wa vyuo vingine ili kukabiliana na changamoto ya ajira na ushindani nchini.

Mheshimiwa Andengenye ameyasema hayo leo Desemba 04 2024 wakati akihutubia kongamano la 34 la wanazuoni wa chuo kikuu huria cha Tanzania (OUT) lililofanyika katika kituo cha chuo hicho mkoa wa Kigoma kuelekea mahafali ya 43 ya chuo yanayotarajiwa kufanyika Desemba 5 2024 mkoani hapa.

Mheshimiwa Andengenye ameongeza kuwa chuo kikuu huria cha Tanzania (OUT) kimekuwa msaada mkubwa kwa watanzania na watu kutoka nje ya Tanzania.

Mahafali ya 43 ya chuo hicho itafanyika kesho Desemba 5 2024 katika uwanja wa kawawa mkoani Kigoma na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri mkuu wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa.


Katibu mkuu wizara ya elimu, sayansi na teknolojia Prof. Carloyne Nombo amesema serikali itaendelea kushirikiana na chuo...
04/12/2024

Katibu mkuu wizara ya elimu, sayansi na teknolojia Prof. Carloyne Nombo amesema serikali itaendelea kushirikiana na chuo kikuu huria cha Tanzania ( OUT) katika kuboresha huduma za elimu ili kufikia malengo yaliyowekwa.

Prof.Nombo ameyasema hayo leo Desemba 04 2024 katika kongamano la 34 la kitaaluma la wanazuoni kuelekea mahafali ya 43 ya chuo hicho lililofanyika katika chuo hicho kituo cha Kigoma

Mahafali ya 43 ya chuo kikuu huria cha Tanzania ( OUT) kitaifa itafanyika Desemba 05 2024 katika uwanja wa kawawa mkoani Kigoma.



Kai

Mbunge wa Kigamboni (CCM) Dkt.Faustine Ndugulile amefariki dunia leo jumatano Novemba 27 2024 nchini India wakati alipok...
27/11/2024

Mbunge wa Kigamboni (CCM) Dkt.Faustine Ndugulile amefariki dunia leo jumatano Novemba 27 2024 nchini India wakati alipokuwa akitapiwa matibabu.

Dkt. Ndugulile kabla ya kifo chake alikuwa Mkurugenzi wa shirika la Afya Duniani ( WHO) Kanda ya Afrika ambapo alipaswa kuanza majukumu yake mwezi Februari 2025.


Siku ya leo tutakuwa live na bando mc kupigia kipindi cha burudani Mahak**a ya burudani Host Helbert Charles nikiwa na d...
25/11/2024

Siku ya leo tutakuwa live na bando mc kupigia kipindi cha burudani Mahak**a ya burudani Host Helbert Charles nikiwa na dj tigger
Charles

Timu ya taifa ya Tanzania "taifa stars" imefuzu kushiriki mashindano ya  kombe la mataifa ya Afrika AFCON yatakayofanyik...
19/11/2024

Timu ya taifa ya Tanzania "taifa stars" imefuzu kushiriki mashindano ya kombe la mataifa ya Afrika AFCON yatakayofanyika mwakani nchini Morocco.

Taifa stars imefuzu baada ya ushindi wa bao 1 kwa sifuri dhidi ya timu ya taifa ya Guinea bao lililofungwa na Simon Msuva dakika ya 61 ya mchezo.



🇹🇿

Timu ya taifa ya Tanzania "taifa stars" leo majira ya saa 16:00 jioni itakuwa na kibarua kizito dhidi ya timu ya taifa y...
19/11/2024

Timu ya taifa ya Tanzania "taifa stars" leo majira ya saa 16:00 jioni itakuwa na kibarua kizito dhidi ya timu ya taifa ya Guinea kusaka tiketi ya kufuzu AFCON 2024 mchezo utakaochezwa uwanja wa Benjamin Mkapa.

Taifa stars katika mchezo huo wa leo inahitaji ushindi pekee ili kufuzu AFCON mwakani itakayofanyika nchini Morocco.

Katika msimamo wa kundi H Jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo inaongoza kundi ikiwa na alama 12 Guinea nafasi ya pili alama 9 Tanzania nafasi ya tatu alama 7 na Ethiopia nafasi ya mwisho alama 1.

Aidha serikali ya Tanzania imetangaza mechi hiyo haitakuwa na kiingilio ili kuongeza hamasa zaidi kwa washabiki kujitokeza kwa wingi kushuhudia mchezo huo muhimu kwa stars.




Mkrugenzi na msimamizi wa uchaguzi wa serikali za mitaa manispaa ya Kigoma ujiji Kisena Mabuba ametoa wito kwa wananchi ...
18/11/2024

Mkrugenzi na msimamizi wa uchaguzi wa serikali za mitaa manispaa ya Kigoma ujiji Kisena Mabuba ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kusikiliza sera za wagombea kutoka vyama mbalimbali kuelekea uchaguzi was serikali za mitaa.

Mabuba amesema hayo leo katika kipindi cha Morningjam cha KICORA radio na ameongeza kuwa ratiba za kampeni kutoka vyama vyote vya kisiasa ameshaipokea kwaajili ya utaratibu maalumu kuepuka migongano katika sehemu mbalimbali .

Mabuba amesema kampeni za uchagzuzi wa serikali za mitaa zitaanza tarehe 20-26 mwezi novemba 2024 ,kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa kumi na mbili jioni , na tarehe 27 itakuwa siku ya uchaguzi.


18/11/2024

Maandalizi ya kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa yamepamba moto , ndani ya Morning jam usikose kusikiliza kipindi hi...
16/11/2024

Maandalizi ya kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa yamepamba moto , ndani ya Morning jam usikose kusikiliza kipindi hiki maalum .

Uchaguzi wa serikali za mitaa utafanyika novemba 27 2024 .Jitokeze kupiga kura.

Klabu ya Yanga SC imevunja mkataba na aliyekuwa kocha mkuu wa klabu hiyo Angel Miguel Gamondi kwa makubaliano ya pande z...
15/11/2024

Klabu ya Yanga SC imevunja mkataba na aliyekuwa kocha mkuu wa klabu hiyo Angel Miguel Gamondi kwa makubaliano ya pande zote mbili.

Aidha klabu ya Yanga SC pia imesitisha mkataba na kocha wake msaidizi wa kikosi cha kwanza Msenegal Mousa Ndaw

Klabu ya Yanga mara baada ya taarifa hiyo imetangaza kuanza mchakato wa haraka wa kutafuta walimu wapya kuchukua nafasi ya Gamondi na Ndaw .


Address

Kigoma

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kicora FM posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Kicora FM:

Videos

Share

Category