Wolta Media

Wolta Media Wolta Media Kwa Mtazamo Mpana.

➡️VIMONDO  👉SEHEMU II...    K**a kimondo ni kikubwa zaidi, ni sehemu zake za nje tu zinazochomwa, na kiini kinaanguka kw...
07/06/2020

➡️VIMONDO 👉SEHEMU II...
K**a kimondo ni kikubwa zaidi, ni sehemu zake za nje tu zinazochomwa, na kiini kinaanguka kwenye uso wa Dunia. Mara nyingi kimondo kinapasuka hewani na kumwaga vipande vyake.
Kati ya vimondo kumi vikubwa kabisa duniani ambavyo mabaki yake yanaonekana, kimojawapo ni Kimondo cha Mbozi nchini Tanzania. Cha kwanza kabisa kinapatikana Namibia kikiwa na urefu wa mita 2.7.

JE! UNAIJUA MVUA YAKE
Vipande vya vimondo-anga mara nyingi hupatikana kwenye anga-nje na kuonekana k**a wingu lililotawanyika sana. Wakati Dunia linapopita eneo la wingu la aina hiyo vipande vidogo vya vimondo-anga huingia katika angahewa kwa kasi kubwa na kuungua. Mvua ya vimondo huonekana k**a kuongezeka kwa mianga ya vimondo angani kwa kipindi cha siku kadhaa, ilhali idadi kubwa ya vimondo huwaka kwa siku chache tu.

Mvua ya vimondo kwa kawaida unasababishwa na mabaki ya nyotamkia. Wingu la vipande hivyo linazunguka Jua kwenye obiti inayokutana na obiti ya Dunia, kwa hiyo kuna mawingu ya namna hiyo yanayorudi kila mwaka. Vipande vya wingu husogea angani kwa pamoja; vikigusana na angahewa la Dunia mianga yake inaonekana kutokea katika sehemu fulani ya anga. Hivyo mvua ya vimondo hupewa jina kutokana na eneo la kundinyota ambako inaonekana, k**a vile Perseidi na Leonidi Perseidi huwa na jina la Perseus (Farisi) ikionekana kila mwaka mnamo 12 Agosti na Leonidi huitwa hivyo kutokana na Leo (Simba ikionekana mnamo 17 Novemba.

👉 HATARI ZA VIMONDO
Kimondo ni hatari kwa vyombo vya angani kwa sababu ya kasi yake kubwa. Hata punje ndogo yaweza kusababisha uharibifu mwingi.

Duniani kuna hatari fulani lakini hali halisi si kubwa ingawa vimondo vinaingia kila saa katika angahewa. Lakini theluthi mbili za uso wa Dunia ni bahari na sehemu kubwa ya nchi kavu haina watu. Katika miaka yote ya karne ya 20 kuna taarifa 21 pekee za nyumba kugongwa na kimondo.
..Inaendelea sehemu ya Tatu k**a umeikosa sehemu ya kwanza Nenda Kiswahili Lifestyle Hacs Vlogger - Cyprian S.

➡️ VIMONDO 👉 SEHEMU IKimondo ni kiolwa kidogo cha angani kinachozunguka Jua katika anga-nje. Kikiingia katika angahewa l...
07/06/2020

➡️ VIMONDO 👉 SEHEMU I
Kimondo ni kiolwa kidogo cha angani kinachozunguka Jua katika anga-nje. Kikiingia katika angahewa la Dunia kinaonekana k**a mwali wa moto angani.
👉MAJINA NA UKUBWA
Kimsingi hakuna tofauti kati ya kimondo na asteroidi: ni suala la ukubwa tu. Violwa vidogo kuanzia ukubwa wa punje ya mchanga hadi kufikia kipenyo cha mita kadhaa huitwa vimondo. Vikubwa zaidi huitwa asteroidi. Hivyo kimondo ni kidogo kuliko asteoridi na kikubwa kushinda vumbi la anga-nje.
Katika lugha nyingi kuna majina tofauti kutaja hali mbalimbali za vimondo.

Kimondo-anga (Kiingereza meteoride) ni kimondo wakati kipo kwenye anga-nje; ni vipande vya mwamba au metali vinavyopatikana katika anga-nje, kwa kawaida kutokana na kuvunjika kwa asteroidi au nyotamkia (kometi).
Kimondo (ing. meteor) ni hali ya kimondo-anga kinapopita kwenye angahewa ya Dunia pamoja na mwangaza unaoonekana, hasa kwenye anga la usiku. Wakati kinapopita katika angahewa ya Dunia, kinawaka kutokana na joto la msuguano na molekuli za hewa; kinaonekana k**a mstari mfupi wa nuru. Waswahili wa Kale waliita hali hii "kinga cha shetani".
Kimondo-nchi (ing. meteorite) ni mabaki ya kimondo-anga yaliyofika kwenye uso wa ardhi k**a mawe bila kuungua kabisa hewani.
Kugonga angahewa ya Dunia
Obiti (ing.orbit) ya kimondo inaweza kuingiliana na njia ya Dunia au sayari nyingine. Kimondo kikikaribia kiolwa cha angani kikubwa zaidi kinavutwa na graviti yake.

Kikikaribia Dunia yetu kinaingia katika angahewa na kuanguka chini kwa kasi kubwa sana. Njiani kinapashwa moto kutokana na msuguano wa hewa dhidi yake. Kiasi cha joto kinatosha kuchoma kabisa kimondo kidogo hewani. Hii inaonekana na macho matupu k**a mstari wa moto angani unaowaka kwa sekunde 1-2. Hii ni hali ya kimondo inayoitwa pia "meteori". Waswahili wa Kale waliita "Vinga vya sheitani" walieleza miali hiyo ya moto angani kuwa malaika angani wanaozuia mashetani kupanda juu kwa kuwarushia vipande vya kuni vilivyowaka.
👉Itaendelea...Masaa Mawili Yajayo.Nenda LikKiswahili Lifestyle Hacs Vlogger - Cyprian S.S.

🗣️ Je! Unaupa uzito gani ukuaji wa mwanao kimawazo? 👨‍👩‍👦• Siku hizi mtoto 👶hulelewa na walimwengu sio tena wazazi💑 wake...
06/06/2020

🗣️ Je! Unaupa uzito gani ukuaji wa mwanao kimawazo? 👨‍👩‍👦
• Siku hizi mtoto 👶hulelewa na walimwengu sio tena wazazi💑 wake na Jamii inayomzunguka pekee.

Utandawazi umefanya Leo mtoto anaweza kulelewa na Jamii ambayo hakuishi nayo, kwa mfano Mwanao anakua kwa kuishi tamaduni za nchi zingine zenye Nguvu Kiteknolojia katikati ya Wanajamii wa Utamaduni walimwokulia Wazazi wake.

Thamani ya Mawazo ataipata mtoto pale mzazi atakapojikita na kuuthamini utashi wa Mtoto.

_👉 UTASHI NI UWEZO WA KUTAMBUA JEMA NA BAYA.

Lipi bora na Lipi lisilo bora, lenye manufaa na lisilonalo, Yaani hata apate kufahamu mangapi bado ana nafasi ya Kutambua na kuchambua.

Utashi unaboresha hali ya Mwanao kujitambua na Kujiamini.

👉 Usipende kuulinganisha Uwezo wa Mwanao na wajirani ila Mfundishe kwamba binadamu tumeumbwa kusaidiana na sio kuigana!
💪🏼

▶️ "Unapofika Muda Mzazi anatambua kwamba wazazi wake Walikua Sahihi,wakati huo tayari yeye ana mtoto anaefikiria Mzazi ...
05/06/2020

▶️ "Unapofika Muda Mzazi anatambua kwamba wazazi wake Walikua Sahihi,wakati huo tayari yeye ana mtoto anaefikiria Mzazi wake hayupo sahihi"
☑️

LIJENDARI ANAYESHIKILIA REKODI YA DUNIA KATIKA MBIO ZA MITA 1500 KWA DAKIKA 3:32:16.👏👏👏  ▶️Mwaka 1974 alishinda nafasi y...
05/06/2020

LIJENDARI ANAYESHIKILIA REKODI YA DUNIA KATIKA MBIO ZA MITA 1500 KWA DAKIKA 3:32:16.👏👏👏
▶️Mwaka 1974 alishinda nafasi ya Kwanza na Kuwashangaza wengi kwa kutengeneza rekodi hiyo katika Mashindano ya British Commonwealth ( Jumuia ya Madola). Huku akienda kasi Mwanzo Mpaka mwisho, tofauti na mtindo uliozoeleka wa kuanza taratibu.

▶️ Mwaka 1975 alishinda pia Mashindano ya Mbio Jamaica na Kuvunja rekodi ya Bingwa aliyezoeleka huko.

▶️Mwaka 1980 Kampuni ya watu ilimpa Dola 8,000/= na hapo ndipo ukawa mwanzo wa uwekezaji wake.

▶️ Kwasasa ni Mwenyekiti wa k**ati ya michezo ya Riadha Tanzania. Kuna Taasisi mbalimbali ziliitwa Kwa Jina lake k**a ishira ya Ushujaa wake.

[Katika Picha ya Mwaka 1974 New Zealand]
- Filbert bayi ( Mwenye nguo za bluu) akisimama na wenzake wawili walioshika Nafasi ya Pili Ben Jipcho wa Kenya na nafasi ya Tatu John Walker wa New Zealand.

The Greatest Last Place Finish Ever 🤔MTANZANIA ALIYESHIRIKI MEXICO CITY OLYMPIK 1968 KUTOKA MBULU.Anaitwa John Steven Ak...
03/06/2020

The Greatest Last Place Finish Ever 🤔
MTANZANIA ALIYESHIRIKI MEXICO CITY OLYMPIK 1968 KUTOKA MBULU.
Anaitwa John Steven Akhwari.
PICHA: 1.AKIWA AMEBEBA TUZO ADIMU aliyotunukiwa Mwaka 2018.
2. Akikimbia kumaliza shindano la riadha KM 42.

Alimaliza shindano Akiwa Mshindi wa Mwisho No.57 baada ya kukimbia kwa Saa 3:25:27 wakati mshindi wa Kwanza Raia wa Ethiopia Mamo Wolde Alikimbia kwa Saa 2:20:26.

Anaishi Mbulu sasa na ana Familia yenye Watoto sita.

Umaarufu wake unatokana na Msimamo na Uvumilivu aliouonyesha katika shindano hilo kwani alikua ameumia Mguu, Na alipomaliza mashindano alipoulizwa sababu ya Msimamo wake Alijibu "Nchi yangu Tanzania haikunituma huku Mexico kuanza mashindano bali kuyamaliza".

Alizaliwa Mwaka 1938 Mbulu - Manyara Tanzania.

 14-May, 2020 Virusi vya Corona. Je! kalenda ya kombe la Dunia 2022 kuathirika?Virusi vya corona huenda vikaathiri kalen...
14/05/2020


14-May, 2020
Virusi vya Corona. Je! kalenda ya kombe la Dunia 2022 kuathirika?Virusi vya corona huenda vikaathiri kalenda ya soka ya kimataifa kwa "miaka miwili au mitatu", amesema mwanachama wa k**ati ya Uefa.

Lars-Christer Olsson, rais wa ligi za Ulaya, amesema itakuwa suala la kusubiri na kuona hali itakavyokuwa ili kuweza kutathmini athari za janga la corona ikiwemo kombe la Dunia nchini Qatar 2022.
Uamuzi wa iwapo hilo linawezekana au la utafanywa mwezi Mei.
Olsson amesema ni kheri msimu wa sasa usimalizike badala ya kuchelewa kuanza msimu ujao".

Kufuatia kusitishwa kwa michezo ya soka na nchi mbalimbali na michuano ya Euro 2020 na Euro 2021, aliulizwa katika warsha iliyofanyika kwenye mtandao je kalenda ya soka itaathirika kwa kiasi gani.

"Nafikiri pengine miaka miwili au mitatu," amesema.

Awali, alikuwa ameiambia BBC Radio 5 katika kipindi cha asubuhi kwamba hakuna maridhiano kati ya nchi kwa michuano ya ndani ya nchi, kwasababu kila nchi inakabiliwa na hali tofauti kwa misingi ya ugonjwa wa corona na hatua za serikali.

Ligi mbili za juu Ufaansa Ligue 1 na Ligue 2, hazitarejelelewa msimu huu baada ya Ufaransa kupiga marufuku michezo yote ikiwemo ile inayochezwa bila mashabiki hadi Septemba.

Ligi ya Uholanzi ilisitishwa wiki jana huku kukiwa hakuna aliyepandishwa daraja wala kushushwa ama kutangazwa mshindi.

Alipoulizwa endapo wana hitimisho la kutosha kwa mashindano yao kuendelea ikiwa baadhi ya klabu zinazoshiriki k**a PSG na Ajax, hazitakuwa zimecheza kwa miezi mingi amesema: "Ni jambo gumu kulizungumzia lakini katika hali yeyote ile, hili ni jambo lisilo la kawaida ambalo utatuzi wake nao utakuwa si wa kawaida."

ℹ️ SAMMS STUDiOS  "Kuwa Chanzo cha Mabadiliko unayotamani kuyatazama Duniani"Posted by Cyprian Stephens.
08/05/2020

ℹ️ SAMMS STUDiOS
"Kuwa Chanzo cha Mabadiliko unayotamani kuyatazama Duniani"

Posted by Cyprian Stephens
.

ℹ️ SAMMS STUDiOS | IDEOLOGIESMaana ya Maisha yako hupimwa thamani uliyowapatia binadamu wenzako na dunia, Lakini siku zo...
08/05/2020

ℹ️ SAMMS STUDiOS | IDEOLOGIES
Maana ya Maisha yako hupimwa thamani uliyowapatia binadamu wenzako na dunia, Lakini siku zote kumbuka kumwomba Mungu maana Udhaifu wetu yeye pekee anaweza kuudhoofisha!

Admin Cyprian Stephens

STAFF.Cyprian Stephens aka cpryChief Operations Officer SAMMS STUDiOS ...                                       ̇d19    ...
08/05/2020

STAFF.
Cyprian Stephens aka cpry
Chief Operations Officer
SAMMS STUDiOS
...
̇d19

Address

Karatu

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wolta Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Wolta Media:

Share


Other Karatu media companies

Show All

You may also like