Radio Furaha FM

Radio Furaha FM RADIO FURAHA KUTANGAZA INJILI KWA WATU WOTE.RADIO INAYOFANYA VIPINDI VYA KIJAMII, MATANGAZO, BURUDAN

Usawa upo au haupo
18/03/2025

Usawa upo au haupo

 HABARI KUBWA KUTOKA TFFDABI YANGA SC VS SIMBA SC YAOTA MBAWA
08/03/2025



HABARI KUBWA KUTOKA TFF

DABI YANGA SC VS SIMBA SC YAOTA MBAWA





Neema kwa Waimbaji wa Nyimbo za Injili Iriiiinga!! Tuzooo  Elct Dira Chafumbwe Chasco Radio Furaha FM Injinji
05/03/2025

Neema kwa Waimbaji wa Nyimbo za Injili Iriiiinga!! Tuzooo

Elct Dira Chafumbwe Chasco Radio Furaha FM Injinji

 Timu ya soka ya Shirika la Umeme Tanzania, Mkoa wa Iringa TANESCO FC imejipanga kikamilifu kwa ajili ya kushiriki na ku...
05/02/2025



Timu ya soka ya Shirika la Umeme Tanzania, Mkoa wa Iringa TANESCO FC imejipanga kikamilifu kwa ajili ya kushiriki na kufanya vizuri kwenye ligi ya mabingwa wa mkoani iringa inayotarajiwa kuanza hivi karibuni.

Timu hiyo inalenga kuonyesha uwezo wake na kushindana kwa nguvu ili kuhakikisha inapata matokeo mazuri katika michuano hiyo.

Msemaji wa timu hiyo, Bw. Emmanuel Kisigo, amesema kuwa maandalizi yanaendelea vizuri na wachezaji wako kwenye hali nzuri ya ushindani. alisisitiza kuwa timu imeimarisha mazoezi na mikakati yake ili kuhakikisha inakuwa na safu imara katika kila idara ya uwanja.

Akizungumza na Furaha Michezo, Bw. Kisigo alieleza kuwa kikosi chao kimefanya maboresho muhimu kwa lengo la kukabiliana na changamoto zinazoweza kujitokeza wakati wa ligi.

Aidha, alisema kuwa ari ya wachezaji ni kubwa na kila mmoja ana dhamira ya kushiriki kwa bidii kuhakikisha timu inapata ushindi.

Tanesco inatarajia kukutana na timu mbalimbali zenye ushindani mkubwa, lakini uongozi wa timu una imani kwamba maandalizi waliyofanya yatawasaidia kupata matokeo mazuri.

"Mbinu za kiufundi na mshik**ano wa wachezaji zimeimarishwa ili kuongeza ufanisi ndani ya uwanja."

Mashabiki wa tanesco wamehimizwa kuendelea kuipa sapoti timu yao kwa kuwa motisha yao ni sehemu muhimu ya mafanikio.

"Wadau wa michezo wanatarajia kuona ligi yenye ushindani mkubwa, huku tanesco ikitarajia kuwa miongoni mwa timu zitakazofanya vizuri katika mashindano hayo."




 Yanga SC yaendeleza vichapo baada ya kuichabanga KenGold kutoka jijini Mbeya 6-1 mchezoambao umevurumishwa uwanja wa KM...
05/02/2025



Yanga SC yaendeleza vichapo baada ya kuichabanga KenGold kutoka jijini Mbeya 6-1 mchezoambao umevurumishwa uwanja wa KMC jijini Dar es Salaam.



 Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimebaini changamoto ya ajira nchini na kimeanza kuchukua hatua kwa kuboresha sera za elimu i...
05/02/2025



Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimebaini changamoto ya ajira nchini na kimeanza kuchukua hatua kwa kuboresha sera za elimu ili kuhakikisha zinatoa majibu sahihi katika sekta ya ajira.

Hatua hii inalenga kuandaa mazingira mazuri kwa vijana kupata ujuzi unaohitajika kwenye soko la ajira na kuimarisha uchumi wa taifa.
Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, alizungumza kuhusu jambo hilo wakati wa kilele cha maadhimisho ya miaka 48 ya chama hicho yaliyofanyika jijini Dodoma. Alisisitiza kuwa chama kinatambua changamoto za sasa na kinaendelea kuboresha mifumo yake ili kujenga taifa lenye maendeleo endelevu.

Aidha, Mhe. Dkt. Samia alieleza kuwa ili kuwa na mustakabali mzuri wa chama na taifa kwa ujumla, ni muhimu kuboresha jumuiya zilizopo ndani ya CCM. Alisema jumuiya hizo zinapaswa kujengwa kwa misingi ya itikadi thabiti na kuandaliwa kwa uongozi bora ili kudumisha mshik**ano na maadili ya chama.

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi, aliahidi kutekeleza kwa vitendo ilani ya chama kwa manufaa ya wananchi. Alisema serikali inaendelea kuwaletea wananchi maendeleo kwa kuhakikisha miradi mbalimbali ya kijamii na kiuchumi inatekelezwa ipasavyo.

Naye Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, alisisitiza umuhimu wa kila mwanachama kuwa mwadilifu na kuzingatia demokrasia ndani ya chama. Alisema uadilifu na uongozi wa haki ni nguzo muhimu katika kuimarisha chama na kuhakikisha kinaendelea kuwa imara kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania wote.







 Askofu Blaston Gavile Atoa Wito wa Ushirikiano Kati ya Jamii na Serikali kwa MaendeleoIringa Askofu wa Kanisa la Kiinji...
01/02/2025



Askofu Blaston Gavile Atoa Wito wa Ushirikiano Kati ya Jamii na Serikali kwa Maendeleo
Iringa
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Iringa, Dkt. Blaston Gavile, ametoa wito kwa jamii kushirikiana na serikali ili kuleta maendeleo endelevu.
Askofu Gavile ametoa rai hiyo katika ibada maalum ya kumuingiza kazini Mkuu wa Jimbo Mpya la Kusini Mashariki, Mchungaji Medson Chengula, ambayo imefanyika katika Usharika wa Idete, Wilaya ya Kilolo, mkoani Iringa.
``Maendeleo hayawezi kupatikana kwa juhudi za mtu mmoja, tunahitaji mshik**ano wa pamoja,” amesema Askofu Gavile
Katika hotuba yake, Askofu Gavile amesisitiza umuhimu wa mshik**ano kati ya wananchi na serikali katika kutekeleza miradi ya maendeleo pamoja na miundombinu bora k**a vile barabara,maji,umeme pamoja na mawasiliano kwa ustawi wa jamii.

Katika kuhakikisha maendeleo yanapatikana kwa wakati Askofu Gavile alieleza kuwa ushirikiano wa pamoja kati ya viongozi wa dini, serikali na wananchi wote ni muhimu wote kushirikian kwa pamoja.

Aidha, ameataka waumini na jamii kwa ujumla kujikita katika kazi za maendeleo, akisisitiza kuwa mafanikio ya jamii yanategemea mshik**ano na juhudi za pamoja.

Ibada hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa dini, waumini, pamoja na viongozi wa serikali, ambapo wote walikubaliana kuwa mshik**ano ndiyo njia pekee ya kufanikisha maendeleo katika jamii.







 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amefungua rasmi Bunge Bonanza 2025 ambalo limeanza ...
01/02/2025



Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amefungua rasmi Bunge Bonanza 2025 ambalo limeanza kwa matembezi, kisha mazoezi ya viungo na mashindano ya kukimbia na michezo mingine ikiwemo mpira wa miguu itafuata.

Bonaza hilo pia linashirikisha vilabu vya Simba na Yanga.







 Ufaransa inatarajia kupendekeza rasimu ya azimio kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ambayo inalenga "kuongeza sh...
01/02/2025



Ufaransa inatarajia kupendekeza rasimu ya azimio kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ambayo inalenga "kuongeza shinikizo kwa Rwanda" kuondoa wanajeshi wake mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Balozi wa Ufaransa wa Umoja wa Mataifa Nicolas de Riviere amesema.

"Natumai azimio hili linaweza kupitishwa hivi karibuni," alisema, akiongeza kuwa hafikirii azimio hilo lingetishia vikwazo vyovyote katika hatua hii.

"Tunachohitaji ni ujumbe mzito na wa wazi wa Baraza la Usalama katika mfumo wa azimio, unaohimiza hatua ya sasa kusitisha na kuhimiza uondoaji wa wanajeshi wa kigeni, na kutaka kuanzishwa tena kwa mazungumzo," de Riviere aliongeza.

Rasimu ikishasambazwa kwa wajumbe 15, baraza litajadili lugha kabla ya kura kuratibiwa. Azimio la baraza hilo linahitaji angalau kura tisa za kuunga mkono na hakuna kura ya turufu ya Marekani, Urusi, Uchina, Uingereza au Ufaransa kupitishwa.

Ujumbe wa Ufaransa kwenye Umoja wa Mataifa ulisema baadaye Ijumaa kwamba ili kuunga mkono juhudi za upatanishi, Ufaransa pia ilikuwa katika "mawasiliano ya karibu na washirika wake katika Umoja wa Mataifa huko New York ili kuhimiza kuanzishwa tena kwa mazungumzo kati ya DRC na Rwanda, yaliyowezeshwa na Angola ndani ya Umoja wa Mataifa- yanayofahamika k**a mchakato wa Luanda."

Chanzo: BBC Swahili











 Kutoka Harare, Zimbabwe.//Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na...
31/01/2025



Kutoka Harare, Zimbabwe.
//
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC-Organ) Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akishiriki Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC katika ukumbi wa New Parliament Building, Harare nchini Zimbabwe tarehe 31 Januari, 2025. Mkutano huo pamoja na mambo mengine unajadili hali ya ulinzi na usalama Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).












 TBT: MWAKA MMOJA TANGU MTUNZA HAZINA KKKT - DAYOSISI YA IRINGA CPA HENZRON NZIKU AINGIZWE KAZINIMtunza Hazina wa saba w...
28/01/2025



TBT: MWAKA MMOJA TANGU MTUNZA HAZINA KKKT - DAYOSISI YA IRINGA CPA HENZRON NZIKU AINGIZWE KAZINI

Mtunza Hazina wa saba wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Iringa CPA Henzron Nziku aliingizwa kazini rasmi Jumapili Januari 28, 2024 katika Usharika wa Kanisa Kuu (Iringa Mjini), Jimbo la Magharibi, Ibada iliongozwa na Baba Askofu Dkt. Blaston Tuluwene Gavile akichukua nafasi ya Ndugu Vicenti Masanula ambaye alistaafu rasmi Septemba 3, 2023.













  : Muonekano wa makundi yote sita baada ya kufanyika kwa droo ya   usiku huu jijini Rabat nchini Morocco. Kundi “A” Mor...
27/01/2025



: Muonekano wa makundi yote sita baada ya kufanyika kwa droo ya usiku huu jijini Rabat nchini Morocco.

Kundi “A” Morocco, Comoro, Zambia na Mali

Kundi “B” Misri, Afrika Kusini, Angola na Zimbabwe, Angola

Kundi “C” Tunisia, Nigeria, Uganda na Tanzania

Kundi “D” Senegal, DR Congo, Benin na Botswana

Kundi “E” Burkina Faso, Algeria, Sudan na Guinea ya Ikweta,

Kundi “F” Ivory Coast, Cameroon, Gabon na Msumbiji


 Hongera Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kumbukizi yako ya kuzaliwa. Tunakuta...
27/01/2025



Hongera Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kumbukizi yako ya kuzaliwa. Tunakutakia utumishi mwema na uliotukuka.












 Umoja wa kuwawezesha vijana kiuchumi, Tuna Finance Hub wa Chuo Kikuu cha Iringa kinachomilikiwa na KKKT-Dayosisi ya Iri...
20/01/2025



Umoja wa kuwawezesha vijana kiuchumi, Tuna Finance Hub wa Chuo Kikuu cha Iringa kinachomilikiwa na KKKT-Dayosisi ya Iringa umekusudia kuwakomboa vijana kifikra katika maendeleo ya kiuchumi.

Mwanzilishi wa Tuna Finance Hub, Helman Minazi, ametoa rai hiyo katika mafunzo jumuishi ya vijana wa vyuo vya Iringa ambayo yamelenga kuwapa vijana maarifa ya kifedha, kuona na kutumia fursa za maendeleo zinazowazunguka.

Baadhi ya vijana wamekiri kuwa mafunzo hayo yatawasaidia kuimarisha kipato chao na kuondoa utegemezi.







DC KHERI JAMES:  WANANCHI ZINGATIENI MBINU BORA ZA KILIMO NA UFUGAJI. Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Kheri James, amewataka w...
16/01/2025

DC KHERI JAMES: WANANCHI ZINGATIENI MBINU BORA ZA KILIMO
NA UFUGAJI.

Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Kheri James, amewataka wananchi wa wilaya hiyo kuzingatia kanuni bora za kilimo na ufugaji ili kuimarisha uzalishaji na maendeleo ya kijamii.

Akizungumza katika uzinduzi wa mradi wa ulata water project wa kijiji cha Ulata Boresha Afya uynaotekel;ewa na Shirika la World Vision uliofanyika kijiji Kiponzelo kata ya Maboga Iringa Vijijini .

DC Kheri alieleza kuwa, shughuli za kilimo na ufugaji ni uti wa mgongo wa uchumi wa wakazi wengi wa Wilaya ya Iringa, na hivyo ni lazima zitekelezwe kwa ufanisi.
Aidha, aliwahimiza wafugaji kufuata mbinu bora za ufugaji ambazo zitasaidia kuongeza uzalishaji wa mifugo na kupunguza athari za magonjwa.

DC Kheri alibainisha kuwa ufugaji bora unahitaji usimamizi wa mara kwa mara wa mifugo, matumizi ya malisho ya kutosha, na kuzingatia matibabu ya mifugo ili kuongeza tija.
Vilevile, DC Kheri alitumia nafasi hiyo kuwaasa wananchi kujifunza kutoka kwa wataalamu wa kilimo na ufugaji wanaopatikana katika eneo hilo. Alisisitiza kuwa serikali inatoa huduma hizo bure kupitia maafisa wa kilimo na mifugo, hivyo ni jukumu la kila mwananchi kuhakikisha wanazitumia ipasavyo.
Mwisho, DC Kheri alitoa wito kwa wananchi kuimarisha ushirikiano katika vikundi vya kijamii vinavyoshughulikia masuala ya kilimo na ufugaji. Alisema ushirikiano huo utawezesha kupatikana kwa misaada mbalimbali, k**a vile pembejeo za kilimo, mafunzo, na masoko kwa mazao na bidhaa za mifugo.
-MWISHO-

WANANCHI WA KILOLO WANUFAIKA NA MITI YA SHIRIKA LISILO LA KISERIKALI."Wananchi wa kijiji cha Itimbo, kata ya Ihimbo wila...
16/01/2025

WANANCHI WA KILOLO WANUFAIKA NA MITI YA SHIRIKA LISILO LA KISERIKALI.

"Wananchi wa kijiji cha Itimbo, kata ya Ihimbo wilayani Kilolo, wamenufaika na msaada wa miti uliotolewa na Shirika la One Acre Fund," wamesema wakazi wa kijiji hicho wakati wa kupokea miti hiyo.
Wameeleza kuwa miti hiyo itawasaidia kuongeza kipato na pia kuchangia jitihada za kutunza mazingira katika eneo lao.

Wakatae Nyamba, msimamizi wa miradi ya miti ya malipo na hewa ya ukaa kutoka wilaya ya Kilolo, alisema, "Tunatoa miti kwa wananchi kwa lengo la kurutubisha ardhi na pia kuwasaidia kupata kipato kutokana na mazao ya miti k**a matunda." Aliongeza kuwa hatua hiyo inalenga kuongeza thamani ya ardhi huku ikihamasisha utunzaji wa mazingira.
Kwa mujibu wa Dorcus Tinga, Afisa Habari wa Shirika la One Acre Tanzania LTD, shirika hilo limepanga kusambaza miti milioni nne mwaka huu katika mikoa ya Iringa, Mbeya, Njombe, na Songwe. "Mpango huu unalenga kuboresha maisha ya wananchi kupitia kilimo endelevu na mazingira rafiki," alisema Dorcus.

Afisa Misitu kutoka kitengo cha Maliasili wilaya ya Kilolo, Bw. Aige Mwilafi, alisema, "Kila mwaka tunalenga kupanda miti zaidi ya milioni 12 kwa kushirikiana na Shirika la One Acre Fund." Alibainisha kuwa ushirikiano huo pia unahusisha utoaji wa elimu kwa wananchi ili kufanikisha jitihada za upandaji miti na kuhakikisha wanapata manufaa ya kiuchumi na kimazingira.

Wananchi wamehimizwa kushiriki kikamilifu katika kuhifadhi miti hiyo ili kuhakikisha manufaa yake yanadumu kwa vizazi vijavyo. "Shirika la One Acre Fund limekuwa mshirika muhimu katika kuimarisha mazingira na kuboresha maisha ya jamii mbalimbali nchini," alihitimisha Bw. Mwilafi.

14/01/2025

Ni Ibada ya Uzinduzi ugawaji miche katika bustani ya miti Ofisi kuu KKKT DIRA.

January 14,2025

Elct Dira

Upi umuhimu wa kumuandaa Mtoto kabla ya shule kufunguliwa?Tuandikie tutasoma Ujumbe wako kwenye Makala ya Mtazamo Mseto ...
14/01/2025

Upi umuhimu wa kumuandaa Mtoto kabla ya shule kufunguliwa?

Tuandikie tutasoma Ujumbe wako kwenye Makala ya Mtazamo Mseto


Address

Gangilonga/DIRA, P. O BOX 511
Iringa

Opening Hours

Monday 00:30 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00

Telephone

+255756492515

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio Furaha FM posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Radio Furaha FM:

Videos

Share