EBONY Digital

EBONY Digital The best Swahili Radio Station from the Southern Highlands of Tanzania. Frequency; Iringa 88.1, Njombe 91.9, Mbeya & Songwe 94.5, Dar es Salaam 106.9

Frequency; Iringa 87.8, Mbeya 94.7, Dar 106.9, Njombe 88.2, Songea 102.2 MHz

Rais wa Kenya, William Ruto, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), ametangaza kuwa kutakuwa na ...
27/01/2025

Rais wa Kenya, William Ruto, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), ametangaza kuwa kutakuwa na mkutano usiokuwa wa kawaida wa EAC katika saa 48 zijazo. Mkutano huo utahudhuriwa na Marais Felix Tshisekedi wa DRC na Paul Kagame wa Rwanda. Mkutano huu unafanyika wakati waasi wa M23 na washirika wao wa Rwanda wanakaribia mji wa Goma. Hali hii imesababisha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kutoa wito wa kuondolewa kwa majeshi ya nje kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Nchi kadhaa, ikiwa ni pamoja na Ufaransa, Marekani, na Uingereza, zimeikosoa Rwanda kwa kuhusika katika mzozo huo.




Kamishna wa Elimu nchini Dkt. Lyabwene Mtahabwa, amesema kufuatia taarifa ya Serikali kuhusu agizo la baadhi ya Watumish...
27/01/2025

Kamishna wa Elimu nchini Dkt. Lyabwene Mtahabwa, amesema kufuatia taarifa ya Serikali kuhusu agizo la baadhi ya Watumishi wa Umma kufanyia kazi nyumbani, Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia inaelekeza shule zote za Msingi, Sekondari na Vyuo katika Mkoa wa Dar es Salaam kufungwa kwa siku mbili tarehe 27 na 28 Januari 2025.




KUMEKUCHA MWANAFAMILIA UHALI GANI HALI YA HEWA ASUBUHI HII IKOJE
27/01/2025

KUMEKUCHA MWANAFAMILIA UHALI GANI HALI YA HEWA ASUBUHI HII IKOJE




Benki ya NMB imetenga Shilingi Bilioni 100 kwa ajili ya Mikopo kwa Miradi na Biashara za kusambaza Nishati Safi ya kupik...
26/01/2025

Benki ya NMB imetenga Shilingi Bilioni 100 kwa ajili ya Mikopo kwa Miradi na Biashara za kusambaza Nishati Safi ya kupikia kwa Watanzania.

Benki ya NMB pia itatumia jukwaa la NMB kijiji day na kwa kushirikiana na kampuni ya Taifa Gas kupeleka Elimu ya matumizi ya Nishati safi ya kupikia kwa vijiji 2,000 mwaka 2025.

Uzinduzi wa Mikopo hii umefanyika mbele ya Mgeni Rasmi, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko, akiongozana na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba huku Uwakilishi wa Benki ya NMB umeongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu wetu Bi. Ruth Zaipuna, aliyeambatana na Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara ndugu Filbert Mponzi.






RPC ALLAN BUKUMBI NA GUSA 2025 SISI NI FAMILIA
25/01/2025

RPC ALLAN BUKUMBI NA GUSA 2025 SISI NI FAMILIA




Mwanasiasa maarufu na mbunge wa zamani wa Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa amesema kuwa hana mpango wa kujiunga tena ...
25/01/2025

Mwanasiasa maarufu na mbunge wa zamani wa Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa amesema kuwa hana mpango wa kujiunga tena na Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA k**a inavyodaiwa na baadhi ya watu

Msigwa ametoa kauli hiyo leo Jumamosi January 25, 2025 akizungumza katika matembezi maalum yaliyoandaliwa na CCM mkoa wa Iringa kuunga mkono uamuzi wa mkutano mkuu kumpitisha Dkt Samia Suluhu Hassab kuwa mgombea urais wa CCM 2025.

Amesema kuwa anaridhishwa na utekelezaji wa miradi unaofanywa na CCM na baada ya kupima amethibitisha kuwa hakuna chama kingine kinaweza kuongoza nchi zaidi ya CCM




 NA GUSA 2025 SISI NI FAMILIA
25/01/2025

NA GUSA 2025 SISI NI FAMILIA




Chama cha mapinduzi CCM Iringa wafanya matembezi ya amani kuunga mkono azimio la Chama kumteua Dkt Samia Suluhu Hasan ku...
25/01/2025

Chama cha mapinduzi CCM Iringa wafanya matembezi ya amani kuunga mkono azimio la Chama kumteua Dkt Samia Suluhu Hasan kugombea Urais mwaka 2025 kupitia chama hicho.

Maandamano hayo yamefanyika kutoka kuanzia Samora kuelekea ofisi za ccm Mkoa




Kupitia Morning Extra Wakili Msomi Emmanuel Chengula Kada Wa CHADEMA Atakua na Mjadala Katika Studio Zetu Kuhusu Chama C...
24/01/2025

Kupitia Morning Extra Wakili Msomi Emmanuel Chengula Kada Wa CHADEMA Atakua na Mjadala Katika Studio Zetu Kuhusu Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Una swali Lolote Uliza Hapa.






24/01/2025

UJUMBE WA GUSA KWA VIONGOZI
Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Iringa Kamishna Allan Bukumbi, AmeGUSA kwa Kuahidi Kuwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Iringa Litaendelea Kushirikiana na Ebony FM Katika Utekelezaji wa Kampeni ya GUSA 2025 Inayolenga Kutoa Elimu kwa Wazazi, Walezi na Jamii kwa Ujumla Kuhusu Umuhimu wa Malezi Bora ya Watoto, Haki za Watoto na Athari za Ukatili Dhidi ya Watoto.
Kampeni ya GUSA 2025 ni Mwendelezo wa Ebony FM Kurudisha kwa Jamii Faida Yake Katika Kipindi cha Mwanzo wa Mwaka na Kutokana na Changamoto ya Malezi Duni na Migogoro ya Kifamilia Vinavyoshuhudia Hivi Sasa Vimeisukuma Ebony FM Kuanzisha Kampeni ya Utoaji wa Elimu ya Malezi Bora Kupitia Vipindi Yetu Bure Kwaajili ya Kuhakikisha Ulinzi na Usalama wa Watoto Ambao ni Taifa la Kesho.
Asante Songwe kwa Kuendelea KuGUSA Jamii.


Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani linawashikilia watuhumiwa watatu waliojificha katika msitu kati ya Kimalamsale na Serenget...
24/01/2025

Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani linawashikilia watuhumiwa watatu waliojificha katika msitu kati ya Kimalamsale na Serengeti B, Kata ya Dutumi, Wilaya ya Kipolisi Mlandizi, wakiwa na mtoto mchanga wa miezi saba ambaye alichukuliwa katika tukio la uvamizi la Januari 15, 2025. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, ACP Salim Morcase, alisema mtoto huyo amepelekwa Hospitali ya Tumbi kwa uchunguzi zaidi. Watuhumiwa walik**atwa usiku wa kuamkia leo na uchunguzi unaendelea, ikiwemo kumtafuta mtuhumiwa mwingine ambaye hajapatikana. Gari la Toyota IST, pete ya ndoa ya Johana mke wa Melkizedeki, simu, na kompyuta mpakato vilipatikana katika operesheni ya kuwasaka watuhumiwa.

Tukio la uvamizi lilitokea Januari 15, 2025, ambapo Melkizedeki Sostenes, mfanyabiashara, alishambuliwa nyumbani kwake na watu wanne waliokuwa na mapanga na nondo. Walimshambulia, kumkata mkono wa kushoto, na kumuibia gari lake, ambalo limepatikana. Watuhumiwa walimfunga kamba Melkizedeki, kumtumbukiza kwenye shimo la majitaka, na kumchukua mkewe, Johana Gabriel, na mtoto wao Merysiana Melkizedeki, ambaye alipatikana akiwa hai.




FRANK VEGULLAH NA GUSA 2025 SISI NI FAMILIA
24/01/2025

FRANK VEGULLAH NA GUSA 2025 SISI NI FAMILIA




UTEUZI, UHAMISHO NA MABADILIKO YA VIONGOZI MBALIMBALI
24/01/2025

UTEUZI, UHAMISHO NA MABADILIKO YA VIONGOZI MBALIMBALI




 NA GUSA 2025
24/01/2025

NA GUSA 2025




Benki ya NMB imetunukiwa tuzo 3 na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), ikiwa ni sehemu ya juhudi za TRA kuthamini mchango ...
24/01/2025

Benki ya NMB imetunukiwa tuzo 3 na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), ikiwa ni sehemu ya juhudi za TRA kuthamini mchango wa walipa kodi katika maendeleo ya Taifa.

Tuzo hizo zinazoitambua Benki ya NMB k**a mlipa Kodi Mkubwa Zaidi na Bora Zaidi nchini Tanzania kwa mwaka wa kifedha 2023/2024 ni Taasisi inayolipa kodi kubwa na inayozingatia misingi na kanuni bora za ulipaji kodi (sekta ya kibenki), Mchangiaji bora wa ukusanyaji kodi nchini na Taasisi inayolipa kodi kubwa zaidi nchini na kuzingatia kanuni za ulipaji kodi (sekta zote nchini).

Tuzo hizi zimetolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwenye Siku ya Shukrani na tuzo kwa Mlipa Kodi na kupokelewa kwa niaba ya Benki na Afisa Mtendaji Mkuu Bi. Ruth Zaipuna.




GUSA 2025 SISI NI FAMILIA
24/01/2025

GUSA 2025 SISI NI FAMILIA




Hivi unajua kwa mwaka 2025 Kanye West (), ameripotiwa kuwa mwanamuziki tajiri zaidi duniani mwaka 2025, akiwa na utajiri...
24/01/2025

Hivi unajua kwa mwaka 2025 Kanye West (), ameripotiwa kuwa mwanamuziki tajiri zaidi duniani mwaka 2025, akiwa na utajiri unaokadiriwa kufikia dola bilioni 2.77 Sawa Na Kiasi Cha Tsh. Trilioni 7/= .

Thamani hii kubwa inatokana zaidi na mafanikio ya kazi yake ya muziki pamoja na umiliki wake wa kipekee wa brand ya YEEZY, ambayo inaendelea kufanya vizuri sokoni.




Address

Uhindini
Iringa
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when EBONY Digital posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to EBONY Digital:

Videos

Share

Category