13/01/2026
HAKI BILA UPENDELEO NI MSINGI WA TAIFA - SAMIA
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema maendeleo ya Taifa na ustawi wa wananchi hayawezi kupatikana bila uwepo wa mahak**a huru, yenye uwezo na inayosimamia haki kwa uadilifu na uwazi.
Akizungumza leo Januari 13, 2026 wakati akifungua mkutano mkuu wa mwaka wa Chama cha Mahakimu na Majaji Tanzania (TMJA) unaofanyika kwa siku mbili katika viwanja vya Mahak**a jijini Dodoma, Rais Samia amesema Serikali itaendelea kulinda na kuheshimu uhuru wa mahak**a k**a mhimili muhimu wa utawala bora.
Hata hivyo, Rais Samia amesisitiza kuwa uhuru wa mahak**a unapaswa kwenda sambamba na uwajibikaji, nidhamu, utii wa sheria na uzalendo, ili mahak**a ibaki kuwa chombo cha haki kwa wote, si kwa wachache.
Ameeleza kuwa wananchi wana matarajio makubwa kwa mhimili huo, wakitamani kuona haki inatendeka bila hofu, upendeleo wala uonevu, kwa kuzingatia misingi ya Katiba, sheria na utu wa binadamu.
“Watanzania wana matumaini makubwa sana na nyinyi, wangependa kuaona mahak**a inayosimamia haki kwa uwazi kwa kuzingatia misingi ya kikatiba sheria na utu,” amesema Rais Samia.
Katika kauli iliyosisitiza uzito wa wajibu wa mhimili wa mahak**a, Rais Samia amegusia changamoto ya wananchi kufungwa kwa kesi zisizo na msingi, akitahadharisha dhidi ya vitendo vinavyodhoofisha imani ya jamii kwa mfumo wa haki.
“Huko mahabusu kuna mtu anafungwa kwa kesi ya kubambikiwa, sasa engineering gani imeitaka mahak**ani hadi mtu anafungwa kwa kesi ya kubambikiwa… Akitoka anasema sikuwa na kesi nilibambikiwa tu,” amehoji.
Kwa ujumla, Rais Samia ametoa wito kwa mahakimu na majaji kuendelea kuisimamia haki kwa weledi na dhamira ya dhati, akisisitiza kuwa haki inayotendeka kwa uwazi ndiyo nguzo ya amani, umoja na maendeleo ya Taifa.