Shamba Fm Radio

Shamba Fm Radio Official Page of Shamba Fm Radio. Sikiliza Live Online www.shambafm.co.tz

DODOMA JIJI VS SINGIDA BS NANI KUCHUKUA ALAMA TATU LEOLigi Kuu ya NBC Tanzania bara inarejea leo Januari 16, 2025 kwa mc...
16/01/2026

DODOMA JIJI VS SINGIDA BS NANI KUCHUKUA ALAMA TATU LEO

Ligi Kuu ya NBC Tanzania bara inarejea leo Januari 16, 2025 kwa mchezo mmoja ambapo klabu ya Dodoma jiji itakuwa nyumbani kumenyana na Singida BS kwenye uwanja wa Jamhuri uliopo Dodoma majira ya saa moja usiku.

Hadi sasa Dodoma jiji inashika nafasi ya pili kutoka mwishoni kwenye ligi kuu mara baada ya kucheza michezo nane huku ikiwa na alama sita, Singida ikiwa na alama nane kwenye michezo mitano ya ligi.

Dodoma inahitaji alama tatu kujinasua kwenye mstari wa kushuka daraja huku upande wa Singida ikihitaji alama tatu ili kusogea kwenye nafasi za timu nne bora juu ya msimamo wa ligi.

Utabiri wako ukoje kuelekea mchezo huo.



MUSEVENI AONGOZA MATOKEO YA AWALI UGANDA ASILIMIA 61.7.Matokeo ya awali ya Uchaguzi Mkuu nchini Uganda uliofanyika jana ...
16/01/2026

MUSEVENI AONGOZA MATOKEO YA AWALI UGANDA ASILIMIA 61.7.

Matokeo ya awali ya Uchaguzi Mkuu nchini Uganda uliofanyika jana Januari 15, 2026, yameanza kutangazwa yakionesha Rais Yoweri Museveni akiongoza katika vituo 133 vya kupigia kura vilivyohesabiwa hadi sasa.

Kwa mujibu wa matokeo hayo, Museveni ameongoza kwa kupata kura 14,232 sawa na asilimia 61.7, huku mpinzani wake mkuu Bobi Wine akipata kura 7,753 sawa na asilimia 33.6. Jumla ya kura zilizohesabiwa hadi sasa ni 23,496.

Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo hayo, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Uganda, Jaji Simon Byabak**a, amesema zoezi la kuhesabu kura bado linaendelea katika vituo vingine, huku matokeo zaidi yakitarajiwa kutangazwa leo.

Jaji Byabak**a ameongeza kuwa siku ya uchaguzi kwa ujumla ilikwenda vizuri, licha ya kuwepo changamoto za kiufundi ikiwemo hitilafu ya majina ya baadhi ya wapiga kura pamoja na mashine za kupigia kura kushindwa kufanya kazi katika baadhi ya maeneo. Hata hivyo, amesema changamoto hizo zilitatuliwa kwa kufuata taratibu za kisheria, ikiwa ni pamoja na kutumia daftari la wapiga kura ili kuendeleza zoezi la upigaji kura.

Tume ya Uchaguzi imewahakikishia wananchi kuwa mchakato unaendelea kwa uwazi na haki hadi matokeo ya mwisho yatakapokamilika na kutangazwa rasmi.



Michuano ya AFCON imefikia hatua ya nusu fainali ambapo leo Januari 14, 2025 mechi mbili katika hatua hiyo zitapigwa.Mch...
14/01/2026

Michuano ya AFCON imefikia hatua ya nusu fainali ambapo leo Januari 14, 2025 mechi mbili katika hatua hiyo zitapigwa.

Mchezo wa kwanza wa nusu fainali utakuwa ni kati ya Senegal dhidi ya Misri ambao utapigwa saa 20:00 usiku huku mechi ya pili ikiwa ni ya Nigeria dhidi ya Morocco itakayopigwa saa 23:00 usiku.

Mechi zote mbili tutazitangaza hapa 88.5 Shamba FM huku uchambuzi ukianza saa moja kabla ya mchezo husika.

Unaiona fainali ikichezwa kati ya Mataifa yapi?,tuandikie.



Michuano ya AFCON imefikia hatua ya nusu fainali ambapo leo Januari 14, 2025 mechi mbili katika hatua hiyo zitapigwa.Mch...
14/01/2026

Michuano ya AFCON imefikia hatua ya nusu fainali ambapo leo Januari 14, 2025 mechi mbili katika hatua hiyo zitapigwa.

Mchezo wa kwanza wa nusu fainali utakuwa ni kati ya Senegal dhidi ya Misri ambao utapigwa saa 20:00 usiku huku mechi ya pili ikiwa ni ya Nigeria dhidi ya Morocco itakayopigwa saa 23:00 usiku.

Mechi zote mbili tutazitangaza hapa 88.5 Shamba FM huku uchambuzi ukianza saa moja kabla ya mchezo husika.

Unaiona fainali ikichezwa kati ya Mataifa yapi?,tuandikie.



MAHABUSU AJINYONGA KITUO CHA POLISI MOSHI KATIJeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro linafanya uchunguzi wa tukio la kifo c...
14/01/2026

MAHABUSU AJINYONGA KITUO CHA POLISI MOSHI KATI

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro linafanya uchunguzi wa tukio la kifo cha mtuhumiwa aitwaye Michael Lambau (18), mkazi wa mtaa wa Karikacha, Kata ya Rau, Manispaa ya Moshi, aliyefariki dunia kwa kujinyonga akiwa mahabusu katika Kituo cha Polisi Moshi Kati.

Akizungumza kuhusu tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, SACP Simon Maigwa, alisema mtuhumiwa huyo alikuwa anashikiliwa kwa tuhuma za kosa la shambulio la kudhuru mwili.

Kwa mujibu wa Kamanda Maigwa, mtuhumiwa alik**atwa Januari 13, 2026, akituhumiwa kumshambulia Brian Felix, ambaye ni baba yake mdogo, kwa kumpiga kwa kutumia mabapa ya panga. Inadaiwa kuwa mtuhumiwa huyo alijinyonga siku hiyo hiyo akiwa mahabusu.

Aidha, Kamanda Maigwa alieleza kuwa mtuhumiwa huyo pia alikuwa akitafutwa kwa tuhuma za kufanya kosa la mauaji ya baba yake mzazi, tukio lililotokea Novemba 22, 2025, ambapo anadaiwa kumchoma shingoni kwa kutumia kitu chenye ncha kali kabla ya kutoroka.

Jeshi la Polisi limeeleza kuwa linaendelea na uchunguzi wa kina kubaini mazingira kamili ya tukio hilo na hatua zaidi zitachukuliwa kwa mujibu wa sheria.



ASASI ZA KIRAIA ZAFUNGWA SIKU MBILI KABLA YA UCHAGUZISiku mbili tu kabla ya Uchaguzi Mkuu, Serikali ya Uganda imezima ba...
13/01/2026

ASASI ZA KIRAIA ZAFUNGWA SIKU MBILI KABLA YA UCHAGUZI

Siku mbili tu kabla ya Uchaguzi Mkuu, Serikali ya Uganda imezima baadhi ya asasi maarufu za kiraia, ikiwemo Chapter Four Uganda, ACFIM, HRNJ-U, National NGO Forum na National Coalition of Human Rights Defenders. Hatua hii imesababisha hofu na sintofahamu kuhusu uwazi wa uchaguzi.

Mashirika haya yalikuwa yakifuatilia uchaguzi, kutetea haki za binadamu na kuhakikisha usalama wa waandishi wa habari. Ripoti za awali ziligundua matumizi mabaya ya fedha za umma katika kampeni za uchaguzi uliopita, jambo lililozua mjadala mkubwa.

Aidha, mmoja wa viongozi wa juu wa asasi hizi, Dkt. Sarah Bireete, ameshikiliwa na vyombo vya usalama kwa madai ya kutoa elimu kwa wananchi kuhusu haki za kiraia. Hali hii inachukuliwa na wadau k**a jaribio la kuwatisha wanaharakati.

Wadau wa haki za kiraia wameeleza mshik**ano wao na mashirika yaliyolengwa, wakiwataka viongozi wa serikali kuheshimu uhuru wa asasi huru na kuhakikisha demokrasia inatekelezwa bila vitisho.

Kiongozi wa Upinzani, Bobi Wine, amesema kuwa madai ya serikali ya “uhatarishaji wa taifa” si sahihi, bali ni kisingizio cha kufunika vitendo vya ukandamizaji, ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka.



AHADI ZA KISHIRIKINA ZA AFCON ZAMPELEKA MGANGA JELAMganga wa kienyeji maarufu kwa jina la Sinayogo nchini Mali amejikuta...
13/01/2026

AHADI ZA KISHIRIKINA ZA AFCON ZAMPELEKA MGANGA JELA

Mganga wa kienyeji maarufu kwa jina la Sinayogo nchini Mali amejikuta matatani baada ya kudaiwa kuwatapeli mashabiki wa soka kwa ahadi za kishirikina za kuiwezesha timu ya taifa ya Mali kuvuka hatua za juu katika mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025/26.

Katika sakata hilo, Sinayogo alijitangaza kuwa na uwezo wa kutumia nguvu za kiroho kuhakikisha Mali inashinda au angalau kufika hatua za nusu fainali, kauli iliyowashawishi mashabiki wengi kuchanga fedha kwa matumaini ya ushindi. Kupitia mbinu hiyo, alifanikiwa kukusanya zaidi ya euro 33,500 sawa na zaidi ya shilingi milioni 97 za Kitanzania.

Hata hivyo, hali ilibadilika ghafla baada ya Mali kuondolewa kwenye michuano hiyo kufuatia kipigo cha bao 1–0 dhidi ya Senegal katika hatua ya robo fainali. Baada ya matokeo hayo, umati wa mashabiki waliokata tamaa na wenye hasira ulifurika nje ya nyumba ya mganga huyo wakidai majibu na kurejeshewa fedha zao.

Polisi walilazimika kuingilia kati kumtoa Sinayogo salama na kumweka chini ya ulinzi. Kwa sasa anashikiliwa na kitengo maalumu cha uhalifu wa mtandao (cybercrime) kwa tuhuma za udanganyifu na kuvunja imani ya umma, huku uchunguzi ukiendelea kubaini mtandao mzima wa sakata hilo.



SILINDE ARIDHISHWA NA MIRADI YA UMWAGILIAJI TABORA, SINGIDANaibu Waziri wa Kilimo, Mhe. David Silinde (Mb), ameonesha ku...
13/01/2026

SILINDE ARIDHISHWA NA MIRADI YA UMWAGILIAJI TABORA, SINGIDA

Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. David Silinde (Mb), ameonesha kuridhishwa na kasi na matokeo ya miradi ya ujenzi na upanuzi wa miundombinu ya umwagiliaji inayoendelea katika mikoa ya Tabora na Singida, akisema miradi hiyo ni chachu ya mapinduzi ya kilimo na ongezeko la kipato kwa wakulima.

Akizungumza wakati wa ziara yake ya ukaguzi iliyofanyika Januari 11, 2026, Mhe. Silinde alitembelea Skimu ya Umwagiliaji ya Mwamapuli mkoani Tabora, ambapo alishuhudia mafanikio makubwa ya wakulima wa mpunga wanaonufaika kupitia Chama cha Ushirika cha Umwagiliaji Maji Mwamapuli (AMCOS) chenye wanachama 970.

Kupitia uwekezaji wa umwagiliaji, wakulima hao wamefanikiwa kuongeza uzalishaji wa mpunga kutoka wastani wa tani 2.5 hadi tani 7.5 kwa hekta moja, hali iliyotajwa kuchangiwa na upatikanaji wa maji ya uhakika, matumizi sahihi ya pembejeo na ufuataji wa kanuni bora za kilimo.

Zaidi ya hayo, chama hicho kimejiimarisha kiuchumi kwa kumiliki zana za kisasa za kilimo ikiwemo trekta, rotaveta, mashine za kuvunia na kukoboa mpunga, jambo lililopunguza gharama za uzalishaji na kuongeza ufanisi mashambani.

Wakulima wa Mwamapuli wameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwaunga mkono kupitia ruzuku ya mbolea na upanuzi wa skimu ya umwagiliaji, ambao pia umeongeza manufaa kwa vikundi vya Mahambasi A, Mahambasi B, Makomero A na Makomero B kupitia ujenzi wa mitaro na barabara za mashambani.

Kwa mujibu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, upanuzi wa Skimu ya Mwamapuli umeongeza eneo la umwagiliaji kutoka hekta 630 hadi hekta 2,565, na unatarajiwa kuwanufaisha wakulima wapatao 5,000, hatua itakayoongeza uzalishaji wa chakula na kipato cha wananchi.



SAMIA AAGIZA MIGOGORO YA ARDHI ISIKILIZWE MAHAKAMANIRais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema migogoro ya ardhi ina...
13/01/2026

SAMIA AAGIZA MIGOGORO YA ARDHI ISIKILIZWE MAHAKAMANI

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema migogoro ya ardhi inapaswa kushughulikiwa kupitia mahak**a badala ya mabaraza ya ardhi, akieleza kuwa mfumo huo utaimarisha upatikanaji wa haki kwa wananchi na kuongeza ufanisi katika utoaji wa maamuzi.

Akizungumza leo Januari 13, 2026 jijini Dodoma wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa Chama cha Mahakimu na Majaji Tanzania (TMJA), uliofanyika katika viunga vya Makao Makuu ya Mahak**a ya Tanzania, Rais Samia amesema Serikali inalenga kuhamishia usikilizwaji wa migogoro hiyo katika Mahak**a za Mwanzo.

Ameeleza kuwa hatua hiyo itahitaji uwekezaji mkubwa, ambapo Serikali imeanza maandalizi ya kutenga bajeti ya kutosha katika mwaka wa fedha ujao kwa ajili ya ujenzi wa Mahak**a za Mwanzo nchi nzima. Rais Samia amefananisha mpango huo na ujenzi wa vituo vya afya, akisisitiza kuwa lengo ni kusogeza huduma za haki karibu zaidi na wananchi.

Kwa mujibu wa Rais Samia, maboresho hayo yataondoa ucheleweshaji wa mashauri ya ardhi, kuongeza uwazi katika maamuzi na kupunguza migogoro inayodumu kwa muda mrefu, hatua inayotarajiwa kuleta utulivu na amani katika jamii.



VIVURUGE RU ZUKU YA PEMBEJEO VADHIBITIWA TAGAMENDAUongozi wa Kijiji cha Tagamenda umefanikiwa kuvuruga mbinu za baadhi y...
13/01/2026

VIVURUGE RU ZUKU YA PEMBEJEO VADHIBITIWA TAGAMENDA

Uongozi wa Kijiji cha Tagamenda umefanikiwa kuvuruga mbinu za baadhi ya wakulima wasio waaminifu waliokuwa wakitumia mianya ya Daftari la Ruzuku ya Pembejeo kujinufaisha binafsi.

Akizungumza na redio ya Shamba FM Januari 12, 2025, Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Jeradi Kivike, amesema wakulima hao walikuwa wakijiandikisha kwa majina zaidi ya moja au kuandika ukubwa wa mashamba usio sahihi kwa lengo la kujipatia pembejeo nyingi, hususan mbolea na mbegu, ili kuziuza baadaye kwa bei ya juu.

Kutokana na hali hiyo, Kivike amesema kijiji kimeanzisha utaratibu maalumu wa kufanya uchunguzi wa kina ili kuwabaini wote waliohusika na vitendo hivyo, hatua itakayosaidia kurejesha haki kwa wakulima waaminifu na kulinda lengo la Serikali la kuwasaidia wakulima wadogo.

“Tumeanzisha utaratibu wakufanya uchunguzi kwa kila aliyejiandikisha kwa jina zaidi ya moja na kwa wale walio andikisha Ekari nyingi za mashamba kwa lengo hilohilo pia watafuatiliwa,” amesema Kivike.

Ameongeza kuwa watakaobainika kufanya udanganyifu hawatasamehewa bali watachukuliwa hatua za kisheria ili iwe funzo kwa wengine, Aidha, amewahimiza wakulima kutumia ipasavyo fursa ya pembejeo za ruzuku kwa bei ya punguzo badala ya kuzihujumu, akisisitiza kuwa nafasi k**a hiyo haiji mara mbili.



HAKI BILA UPENDELEO NI MSINGI WA TAIFA - SAMIARais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema maendeleo ya Taifa na ustaw...
13/01/2026

HAKI BILA UPENDELEO NI MSINGI WA TAIFA - SAMIA

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema maendeleo ya Taifa na ustawi wa wananchi hayawezi kupatikana bila uwepo wa mahak**a huru, yenye uwezo na inayosimamia haki kwa uadilifu na uwazi.

Akizungumza leo Januari 13, 2026 wakati akifungua mkutano mkuu wa mwaka wa Chama cha Mahakimu na Majaji Tanzania (TMJA) unaofanyika kwa siku mbili katika viwanja vya Mahak**a jijini Dodoma, Rais Samia amesema Serikali itaendelea kulinda na kuheshimu uhuru wa mahak**a k**a mhimili muhimu wa utawala bora.

Hata hivyo, Rais Samia amesisitiza kuwa uhuru wa mahak**a unapaswa kwenda sambamba na uwajibikaji, nidhamu, utii wa sheria na uzalendo, ili mahak**a ibaki kuwa chombo cha haki kwa wote, si kwa wachache.

Ameeleza kuwa wananchi wana matarajio makubwa kwa mhimili huo, wakitamani kuona haki inatendeka bila hofu, upendeleo wala uonevu, kwa kuzingatia misingi ya Katiba, sheria na utu wa binadamu.

“Watanzania wana matumaini makubwa sana na nyinyi, wangependa kuaona mahak**a inayosimamia haki kwa uwazi kwa kuzingatia misingi ya kikatiba sheria na utu,” amesema Rais Samia.

Katika kauli iliyosisitiza uzito wa wajibu wa mhimili wa mahak**a, Rais Samia amegusia changamoto ya wananchi kufungwa kwa kesi zisizo na msingi, akitahadharisha dhidi ya vitendo vinavyodhoofisha imani ya jamii kwa mfumo wa haki.

“Huko mahabusu kuna mtu anafungwa kwa kesi ya kubambikiwa, sasa engineering gani imeitaka mahak**ani hadi mtu anafungwa kwa kesi ya kubambikiwa… Akitoka anasema sikuwa na kesi nilibambikiwa tu,” amehoji.

Kwa ujumla, Rais Samia ametoa wito kwa mahakimu na majaji kuendelea kuisimamia haki kwa weledi na dhamira ya dhati, akisisitiza kuwa haki inayotendeka kwa uwazi ndiyo nguzo ya amani, umoja na maendeleo ya Taifa.



TRUMP ATISHIA WASHIRIKA WA IRAN KWA USHURU MPYARais wa Marekani, Donald Trump, ametangaza hatua kali ya kiuchumi dhidi y...
13/01/2026

TRUMP ATISHIA WASHIRIKA WA IRAN KWA USHURU MPYA

Rais wa Marekani, Donald Trump, ametangaza hatua kali ya kiuchumi dhidi ya mataifa yanayoendelea kufanya biashara na Iran, akisema nchi hizo zitatozwa ushuru wa asilimia 25 kwa bidhaa zote zitakazoingia katika soko la Marekani.

Kupitia chapisho lake kwenye mtandao wa Truth Social, Trump amesema uamuzi huo unaanza kutekelezwa mara moja, akilenga kuongeza shinikizo kwa Tehran kufuatia madai ya kukandamiza maandamano ya raia wanaopinga Serikali ya kidini nchini Iran. Amesisitiza kuwa agizo hilo ni la mwisho, akionya kuwa hakutakuwa na mazungumzo zaidi kuhusu suala hilo.

Hatua hiyo inaongeza mzigo wa kiuchumi kwa Iran, ambayo uchumi wake unategemea kwa kiasi kikubwa mauzo ya mafuta kwa mataifa mbalimbali ikiwemo China, Uturuki, Iraq, Umoja wa Falme za Kiarabu na India. Kupitia mkakati huo, Washington inalenga kudhoofisha vyanzo vikuu vya mapato ya Tehran bila kutumia nguvu za kijeshi.

Hata hivyo, kauli ya Trump imezua mvutano wa kidiplomasia, ambapo China imeikosoa vikali hatua hiyo. Ubalozi wa China mjini Washington umesema Beijing haitakubali vitisho vya kiuchumi na itachukua hatua zote muhimu kulinda maslahi yake ya biashara, jambo linaloashiria kuongezeka kwa mvutano kati ya Marekani na washirika wakuu wa Iran.



Address

Utalii Road
Iringa

Telephone

+255715729000

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Shamba Fm Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Shamba Fm Radio:

Share

Category