Shamba Fm Radio

Shamba Fm Radio Official Page of Shamba Fm Radio. Sikiliza Live Online www.shambafm.co.tz

DAWA ZA KUFUBAZA MAKALI YA VVU BADO ZIPO NA HAZIUZWI - SERIKALISerikali kupitia Wizara ya Afya imetolea ufafanuzi juu ya...
08/02/2025

DAWA ZA KUFUBAZA MAKALI YA VVU BADO ZIPO NA HAZIUZWI - SERIKALI

Serikali kupitia Wizara ya Afya imetolea ufafanuzi juu ya uvumi unaosambaa mitandaoni na mitaani kuhusu kuadimika kwa dawa za kufubaza makali ya Virusi vya UKIMWI ARVS kwa kusema kuwa hakuna ukweli wowote kuhusu hilo kwani dawa hizo zipo za kutosha na wala haziuzwi.

Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Februari 08, 2025, imeelezwa kuwa Watanzania wapuuze taarifa zisizo za kweli kuhusu upatikanaji wa dawa hizo.

Uvumi wa kuadimika kwa dawa hizo, ulianza kufuatia hatua ya Rais wa Marekani Donald Trump kutangaza kuwa Nchi yake itajiondoa kuchangia shirika la afya Ulimwenguni WHO na kusitisha misaada mingine ambayo Marekani imekuwa ikitoa kwa Mataifa yanayoendelea ikiwemo Tanzania kupitia mashirika kadhaa ya Marekani.

MSIPANDISHE BEI ZA BIDHAA MWEZI WA RAMADHANI - RAIS DKT. MWINYIRais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Mwenyekiti w...
07/02/2025

MSIPANDISHE BEI ZA BIDHAA MWEZI WA RAMADHANI - RAIS DKT. MWINYI

Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Mwinyi amewataka Wafanyabiashara kuwa na uadilifu kwenye biashara zao hususan kuelekea kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani na kuepuka kupandisha bei za bidhaa ndani ya mwezi huo.

Rais Mwinyi ameyasema hayo leo Februari 07, 2025 alipozungumza na Waumini wa dini ya Kiislam kwenye Msikiti wa Jibrili Mkunazini, alipojumuika na waumini hao kwenye swala ya Ijumaa.

Waumini wa dini ya Kiislam wanatarajia kuanza mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani Tarehe Mosi ya mwezi ujao.

BEI YA PILIPILI MWENDOKASI YASHUKA – IRINGA MANISPAAWafanyabiashara katika Soko la Mashine Tatu lililopo Manispaa ya Iri...
07/02/2025

BEI YA PILIPILI MWENDOKASI YASHUKA – IRINGA MANISPAA

Wafanyabiashara katika Soko la Mashine Tatu lililopo Manispaa ya Iringa wamesema kuwa bei ya Pilipili Mwendokasi imeshuka bei tofauti na mwezi miezi miwili iliyopita.

Wakizungumza na Shamba Fm leo Februari 07, 2025, wafanyabiashara hao wamesema bei ya Pilipili Mwendokasi kwa sasa ni kuanzia Shilingi 500 kwa lita moja wakati ilikuwa Shilingi 1,000 katika kipindi cha miezi miwili iliyopita.

Wafanyabiashara hao wameeleza kuwa kuharibika kwa bidhaa ikiwa sokoni hapo ndio changamoto kubwa wanayokutana nayo kutokana na kupungua kwa wateja jambo linalopelekea mzigo kukaa kwa muda mrefu.

AIR TANZANIA KUANZA KUTUA IRINGA MWEZI HUUWaziri wa Uchukuzi nchini Prof. Makame Mbarawa amesema kuwa ndege ya Shirika l...
07/02/2025

AIR TANZANIA KUANZA KUTUA IRINGA MWEZI HUU

Waziri wa Uchukuzi nchini Prof. Makame Mbarawa amesema kuwa ndege ya Shirika la Ndege Tanzania inatarajia kuanza safari zake rasmi katika Mkoa wa Iringa ifikapo Februari 22, 2025 na kufanya safari zake mara tatu kwa wiki.

Prof. Mbarawa amesema hayo leo Februari 07, 2025 alipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa uwanja wa ndege uliopo Nduli, Mkoani Iringa ambao umekamilika kwa asilimia 93 na umeshaanza kutumika huku jumla ya mashirika matatu ya ndege yakitarajiwa kuendesha safari zake katika uwanja huo.

‘’Kukamilika kwa uwanja huu kutafungua sana uchumi wa nchi na hapa Iringa wageni wengi hasa watalii watakuja kwenye uwanja wa ndege huu halafu watachukua magari kutokea hapa kwenda kwenye mbuga za wanyama kwa kuwa zamani ilikuwa wanatoka wanakotoka mfano Zanzibar ama Arusha wanakwenda moja kwa moja hadi kwenye Mbuga za wanyama na hiyo ilipelekea wananchi kukosa mapato’’, amesema Prof. Mbarawa.

Aidha, Prof. Mbarawa ameongeza kuwa Uwanja huo utakapokamilka unatarajiwa kufanya kazi masaa 24 huku ujenzi wake ulitengewa bajeti ya Bilioni 68 ambapo Bilioni 63.77 ni kwa ajili ya ujenzi, Bilioni 1.77 kwajili ya kulipa fidia na Bilioni 2.9 kwa ajili ya kumlipa Mkandarasi.

SIMBA VS TMA, YANGA VS COASTAL UNION CRDB FEDERATION CUP 32 BORADroo ya Michuano ya Michuano ya CRDB Federation imefanyi...
07/02/2025

SIMBA VS TMA, YANGA VS COASTAL UNION CRDB FEDERATION CUP 32 BORA

Droo ya Michuano ya Michuano ya CRDB Federation imefanyika hii Leo Februari 07, 2025 ikiwa ni hatua ya 32 bora ambapo inatarajiwa kuchezwa mwanzoni mwa mwezi Machi mwaka huu.

Mabingwa watetezi wa kombe hilo klabu ya Yanga wamepangiwa kucheza na klabu ya Coastal Union ya mjini Tanga, Simba wakipangwa kukutana na TMA Stars kutoka Arusha huku Azam wakiangukia kwa Mbeya City ya Jijini Mbeya.

Mechi nyingine ni pamoja na:

Singida Black Stars (Singida) Vs Leo Tena (Kagera)

Tabora United (Tabora) Vs Transit Camp (Dar es salaam)

Kiluvya United (Morogoro) Vs Pamba Jiji (Mwanza)

TZ Prisons (Mbeya) Vs Bigman (Shinyanga)

Fountain Gate (Manyara) Vs Stand United (Shinyanga)

Kagera Sugar (Kagera) Vs Namungo (Lindi)

Cosmopolitan (Dar es Salaam) Vs KMC ( Dar es salaam)

BEI YA NDIZI MZUZU HAIJAPANDA WALA KUSHUKA - IRINGAWafanyabiashara wa Ndizi Mzuzu kutoka Soko kuu la Manispaa ya Iringa ...
06/02/2025

BEI YA NDIZI MZUZU HAIJAPANDA WALA KUSHUKA - IRINGA

Wafanyabiashara wa Ndizi Mzuzu kutoka Soko kuu la Manispaa ya Iringa wamesema bei ya ndizi haijapanda wala kushuka ukilinganisha na bei iliyokuwa ikiuzwa miezi miwili iliyopita.

Wakizungumza na Shamba Fm leo Februari 06, 2025, Wafanyabiashara hao wamesema bei ya ndizi mzuzu ni kuanzia 1,000 hadi 5,000 kulingana na uhitaji wa mtumiaji.

Wafanyabiashara hao wameeleza kuwa changamoto wanayokumbana nayo kwa sasa ni mzigo kukaa muda mrefu kutokana na kupungua kwa wateja.

06/02/2025

NCHI 25 WAZALISHAJI WA KAHAWA AFRIKA KUKUTANA TANZANIA

Tanzania inatarajia kuwa Mwenyeji wa Mkutano Mkuu wa 03 wa kahawa utakaokutanisha Wakuu wa nchi 25 ( G25) wanaozalisha kahawa ambapo inatarajiwa kuwa kupitia Mkutano huo kutakuwa na mjadala wa mustakabali wa maendeleo ya uzalishaji wa kahawa na kutoa fursa za ajira kwa vijana.

Mkurugenzi wa Bodi ya Kahawa hapa nchini Primus Kimaryo ameyasema hayo jana Februari 05, 2025 Jijini Dar es salaam wakati akizungumza na vyombo vya habari huku akieleza kuwa Mkutano huo utaangazia namna za kukuza mnyororo wa thamani wa kahawa za Afrika.

“Mkutano huu unakutanisha wakuu wa nchi 25 zinazozalisha kahawa barani Afrika ambapo utatoa mustakabali wa mwelekeo wa zao la kahawa katika kutoa ajira kwa vijana wetu k**a mnavyofahamu Afrika kuna nchi 25 zinazozalisha kahawa na asilimia 90 ya kahawa hii inaenda nje ya bara la Afrika ikiwa haijaongezwa thamani”, amesema Kimaryo.

Mkutano huo utafanyika kwa siku mbili kuanzia Februari 21 hadi Februari 22 mwaka huu 2025 katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere JNICC Jijini Dar es Salaam .

TANZANIA KUJIIMARISHA ILI KUJITEGEMEAWaziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa amesema kuwa mabadiliko ya sera nchini Mare...
06/02/2025

TANZANIA KUJIIMARISHA ILI KUJITEGEMEA

Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa amesema kuwa mabadiliko ya sera nchini Marekani chini ya uongozi wa Rais Donald Trump yanaweza kusababisha Tanzania kuathirika na kusema kuwa mkakati wa Serikali ni kutumia rasilimali za ndani kujiimarisha.

Waziri Mkuu Majaliwa ameyasema hayo leo Februari 06, 2025 Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Mbozi, George Mwanisongole aliyetaka kufahamu kuhusu mpango wa serikali kulingana na mabadiliko ya sera za nje ya nchi ya Marekani ambazo zinatajwa kuathiri sera za elimu, afya na uchumi hasa miradi inayofadhiliwa na USAID, EP4R na programu ya kupunguza makali ya Virusi vya Ukimwi nchini Tanzania.

‘’Muhimu kwetu ni kuhakikisha kwamba tunajiimarisha kwa kuwa na uwezo wa ndani ili kuhakikisha kwamba hatuendelei kuwa wategemezi, ni lazima tujiimarishe kwenye mipango yetu, bajeti zetu ziweze kumudu kutekeleza maeneo yote muhimu ikiwamo maeneo hayo ya afya, elimu na maji", amesema Waziri Mkuu Majaliwa.

Ameongeza kuwa Marekani imeshatangaza na kuna uwezekano pia nchi nyingine ikatangaza kukawa na mabadiliko na sisi tuendelee kujiimarisha kupitia kukuza uchumi wetu kupitia vyanzo vya fedha na mapato ya ndani.

M23 WAUTEKA MJI MWINGINE CONGO Wakati kukitazamiwa mjadala wa mazungumzo ya kutafuta suluhu katika eneo la Mashariki mwa...
06/02/2025

M23 WAUTEKA MJI MWINGINE CONGO

Wakati kukitazamiwa mjadala wa mazungumzo ya kutafuta suluhu katika eneo la Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), matarajio hayo huenda yakafifia kutokana na kitendo cha Wanamgambo wa kundi la M23 kuuteka mji mwingine wa Nyabibwe.

Kutekwa kwa mjio huo unaopatikana kusini mwa Kivu eneo linalotajwa kuwa na madini mengi kunavunja makubaliano ya usitishaji wa mapigano ambayo kundi hilo la M23 lilitangaza mapema Jumatatu ya wiki hii.

Kwa mujibu wa Mtandao wa habari wa Reuters, Waziri wa Mawasiliano wa DRC, Patrick Muyaya, ameliambia shirika hilo kuwa waasi wamevunja usitishaji wa mapigano na sasa wanapambana na jeshi la serikali karibu na Nyabibwe huku Kiongozi wa Muungano wa waasi wa Congo River Alliance M23 ikiwa ndani yake, Corneille Nangaa amethibitisha kwamba wapiganaji wake wameingia Nyabibwe.

MIAKA 48 YA CCM NI YA UMOJA KWA TAIFA - DKT. SAMIAMwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Dkt. Samia Suluhu Hassan...
05/02/2025

MIAKA 48 YA CCM NI YA UMOJA KWA TAIFA - DKT. SAMIA

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema mafanikio ya chama hicho kwa miaka 48 ni kuendelea kuwaunganisha watu na Taifa kwa ujumla.

Dkt. Samia ameyasema hayo leo Februari 05, 2025 Jijini Dodoma kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 48 ya kuzaliwa kwa CCM ambapo amesema ndani ya miaka hiyo chama kimeendelea kubaki katika misingi ya umoja hivyo kufanya kiendelee kuaminiwa na kutumainiwa ndani na nje ya nchi.

Katika hatua nyingine Dkt. Samia ameongeza kuwa kuaminika kwa CCM hakujatokea kwa bahati mbaya bali ni jitihada za kushughulikia matatizo ya wananchi na kutekeleza kwa vitendo ahadi zilizomo kwenye Ilani za Uchaguzi ya chama hicho.

Chama cha Mapinduzi leo hii kimetimiza miaka 48 tangu kuanzishwa kwake Februari 05, 1977 baada ya Muungano wa Vyama viwili vya TANU na ASP.

MRUNDI JELA KWA KUISHI TANZANIA BILA KIBALIMahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijiji Dar es Salaam, imemhukukumu kutumikia ...
05/02/2025

MRUNDI JELA KWA KUISHI TANZANIA BILA KIBALI

Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijiji Dar es Salaam, imemhukukumu kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela na kulipa faini ya Shilingi laki tano (500,000) raia wa Burundi Ferdnand Ndikuriyo (27) baada ya kukutwa na hatia ya kuishi Tanzania bila kibali.

Hukumu hiyo imetolewa leo Februari 05, 2025 na Hakimu Mkazi Mkuu Yusto Ruboroga, ambapo baada ya upande wa mashtaka kuthibitisha shtaka dhidi ya mtuhumiwa, Hakimu Ruboroga amesema kuwa mshtakiwa ni mkosaji wa mara ya pili hivyo anatakiwa kupewa adahabu kali ili iwe fundisho kwake na watu wengine wanaojihusisha na vitendo hivyo ambavyo ni kinyume na sheria.

Ndikuriyo ambaye ni maarufu kwa jina la chuma cha chuma alik**atwa kwa kosa hilo Septemba 18, 2024 katika eneo la Las Vegas Casino, Upanga Wilayani Ilala Jijiji Dar es Salaam.

KUKOSA USINGIZI NI TATIZO LA AFYA YA AKILIImeelezwa kuwa changamoto ya kukosa usingizi inayowakabili baadhi ya watu ni s...
05/02/2025

KUKOSA USINGIZI NI TATIZO LA AFYA YA AKILI

Imeelezwa kuwa changamoto ya kukosa usingizi inayowakabili baadhi ya watu ni sehemu ya tatizo la afya ya akili na hupelekea madhara makubwa ya kimwili na akili.

Hayo yameelezwa na Mwanasaikolojia Moses Mmuya wakati akizungumza na Shamba Fm leo Februari 05, 2025 Shamba Fm ambapo ameeleza kuwa dalili za changamoto hiyo ni pamoja wasiwasi uliopitiliza na kuwashwa kwa mwili wa mwathirika wa changamoto hiyo.

Kwa upande wake Daktari Noel Kivamba kutoka Zahanati ya Iringa Lutheran iliyopo Mtaa wa Tumaini amethibitisha kuwepo kwa changamoto hiyo kwa sasa huku akieleza sababu zake kuwa ni pamoja na matumizi ya dawa mbalimbali pamoja na matumizi ya vifaa vya umeme k**a simu na kumpyuta kabla ya kulala.

Akizungumzia kuhusu tiba ya changamoto hiyo, Mwanasaikolojia Mmuya ameeleza kuwa ni pamoja na kufanya mazoezi pamoja na kupata msaada wa kisaikolojia ili kuepuka madhara zaidi.

DKT. CHIKWE KUKAIMU NAFASI ILIYOACHWA WAZI BAADA YA DKT. NDUGULILE KUFARIKIShirika la Afya Ulimwenguni WHO limetangaza k...
05/02/2025

DKT. CHIKWE KUKAIMU NAFASI ILIYOACHWA WAZI BAADA YA DKT. NDUGULILE KUFARIKI

Shirika la Afya Ulimwenguni WHO limetangaza kumteua Dkt. Chikwe Ihekweazu kuwa Kaimu Mkurugenzi wa shirika hilo katika Kanda ya Afrika ambapo atahudumu mpaka mwezi Mei mwaka huu utakapofanyika uchaguzi wa kumpata mtu wa kujaza nafasi hiyo.

Uteuzi huo umefanyika leo Februari 05, 2025 ambapo Dkt Chikwe ambaye ni raia wa Nigeria anaingia katika nafasi hiyo iliyotakiwa kuwa chini ya aliyekuwa Mkurugenzi mteule Dkt. Faustine Ndugulile kutoka nchini Tanzania kufariki dunia Novemba 27, 2024 nchini India alipokuwa akipatiwa matibabu.

Kuelekea uchaguzi huo unaotarajiwa mwezi Mei mwaka huu, tayari Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, alimpendekeza Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Taifa Muhimbili Profesa Mohamed Janabi kugombea nafasi hiyo iliyoachwa na Dkt. Ndugulile.

𝗝𝗘 𝗪𝗘𝗪𝗘 𝗡𝗜 𝗙𝗨𝗡𝗗𝗜? 𝗨𝗡𝗚𝗘𝗣𝗘𝗡𝗗𝗔 𝗞𝗨𝗣𝗔𝗧𝗔 𝗞𝗔𝗭𝗜 𝗡𝗬𝗜𝗡𝗚𝗜 𝗡𝗔 𝗭𝗘𝗡𝗬𝗘 𝗠𝗔𝗟𝗜𝗣𝗢 𝗠𝗔𝗭𝗨𝗥𝗜? 𝗝𝗜𝗨𝗡𝗚𝗘 𝗦𝗔𝗦𝗔 𝗡𝗔 𝗙𝗨𝗡𝗗𝗜𝗦𝗠𝗔𝗥𝗧 𝗕𝗨𝗥𝗘 𝗣𝗜𝗚𝗔 * 149 * 46 *5...
05/02/2025

𝗝𝗘 𝗪𝗘𝗪𝗘 𝗡𝗜 𝗙𝗨𝗡𝗗𝗜?

𝗨𝗡𝗚𝗘𝗣𝗘𝗡𝗗𝗔 𝗞𝗨𝗣𝗔𝗧𝗔 𝗞𝗔𝗭𝗜 𝗡𝗬𝗜𝗡𝗚𝗜 𝗡𝗔 𝗭𝗘𝗡𝗬𝗘 𝗠𝗔𝗟𝗜𝗣𝗢 𝗠𝗔𝗭𝗨𝗥𝗜?

𝗝𝗜𝗨𝗡𝗚𝗘 𝗦𝗔𝗦𝗔 𝗡𝗔 𝗙𝗨𝗡𝗗𝗜𝗦𝗠𝗔𝗥𝗧 𝗕𝗨𝗥𝗘 𝗣𝗜𝗚𝗔

* 149 * 46 *5 #

𝗙𝗮𝗶𝗱𝗮 𝘇𝗮 𝗞𝘂𝗷𝗶𝘂𝗻𝗴𝗮 𝗻𝗮 𝗙𝘂𝗻𝗱𝗶𝘀𝗺𝗮𝗿𝘁:

1. 𝗞𝘂𝘁𝗮𝗻𝗴𝗮𝘇𝗮 𝗸𝗮𝘇𝗶 𝘂𝗻𝗮𝘇𝗼𝗳𝗮𝗻𝘆𝗮 𝗻𝗮 𝗸𝘂𝗸𝘂𝗮𝗻𝗴𝗮𝗻𝗶𝘀𝗵𝗮 𝗻𝗮 𝗪𝗔𝗧𝗘𝗝𝗔 𝗻𝗰𝗵𝗶 𝗻𝘇𝗶𝗺𝗮.

2. 𝗞𝘂𝗽𝗮𝘁𝗮 𝗖𝗛𝗘𝗧𝗜 𝗸𝘂𝘁𝗼𝗸𝗮 𝗩𝗘𝗧𝗔 𝗸𝗮𝗺𝗮 𝗵𝘂𝗸𝘂𝘀𝗼𝗺𝗲𝗮 𝘂𝗳𝘂𝗻𝗱𝗶 𝘂𝗻𝗮𝗼𝘂𝗳𝗮𝗻𝘆𝗮. 𝗛𝗶𝗶 𝗶𝘁𝗮𝗸𝘂𝘀𝗮𝗶𝗱𝗶𝗮 𝗸𝘂𝗽𝗮𝘁𝗮 𝗮𝗷𝗶𝗿𝗮 𝗮𝘂 𝘁𝗲𝗻𝗱𝗲𝗿 𝘇𝗮 𝗸𝗮𝘇𝗶 𝘇𝗮 𝗦𝗲𝗿𝗶𝗸𝗮𝗹𝗶 𝗮𝘂 𝗺𝗮𝗸𝗮𝗺𝗽𝘂𝗻𝗶.

3. 𝗞𝘂𝗽𝗮𝘁𝗮 𝗠𝗮𝗳𝘂𝗻𝘇𝗼 𝘆𝗮 𝗙𝘂𝗻𝗱𝗶𝗦𝗺𝗮𝗿𝘁 𝗶𝗹𝗶 𝗸𝘂𝗯𝗼𝗿𝗲𝘀𝗵𝗮 𝘂𝗳𝘂𝗻𝗱𝗶 𝘄𝗮𝗸𝗼.

4. 𝗞𝘂𝗽𝗮𝘁𝗮 𝗠𝗶𝗸𝗼𝗽𝗼 𝘆𝗮 𝗙𝗘𝗗𝗛𝗔, 𝗩𝗶𝘁𝗲𝗻𝗱𝗲𝗮 𝗸𝗮𝘇𝗶 𝗽𝗮𝗺𝗼𝗷𝗮 𝗻𝗮 𝗕𝗜𝗠𝗔.

5. 𝗞𝘂𝘀𝗵𝗶𝗿𝗶𝗸𝗶 𝗠𝗔𝗞𝗢𝗡𝗚𝗔𝗠𝗔𝗡𝗢 𝘆𝗮 𝗺𝗮𝗳𝘂𝗻𝗱𝗶 𝘆𝗮𝗻𝗮𝘆𝗼𝗳𝗮𝗻𝘆𝗶𝗸𝗮 𝗻𝗰𝗵𝗶 𝗻𝘇𝗶𝗺𝗮.

𝗙𝘂𝗻𝗱𝗶 𝗵𝘂𝘂 𝗻𝗶 𝗪𝗮𝗸𝗮𝘁𝗶 𝘄𝗮𝗸𝗼 𝘄𝗮 𝗸𝘂𝘄𝗮 𝗙𝘂𝗻𝗱𝗶𝗦𝗺𝗮𝗿𝘁.





Klabu ya wananchi Yanga ya Jijini Dar es salaam imeachana na Kocha wake Sead Ramovic kwa makubaliano ya pande zote mbili...
04/02/2025

Klabu ya wananchi Yanga ya Jijini Dar es salaam imeachana na Kocha wake Sead Ramovic kwa makubaliano ya pande zote mbili.

Taarifa hiyo imetolewa kupitia mitandao rasmi ya kijamii ya Klabu hiyo.

UNYWAJI WA MAJI YA BARIDI SANA SI SALAMA KIAFYA – AFISA LISHE   Unywaji wa maji ya baridi baada ya kula unatajwa kuwa si...
04/02/2025

UNYWAJI WA MAJI YA BARIDI SANA SI SALAMA KIAFYA – AFISA LISHE

Unywaji wa maji ya baridi baada ya kula unatajwa kuwa siyo salama kwa afya kwa kuwa hupelekea ugumu katika mmeng'enyo wa chakula.

Akizungumza na Shamba Fm leo Februari 04, 2025 Afisa Lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Veina Selemani amesema kuwa unywaji maji hayo husababisha madhara mbalimbali ya kiafya k**a kupata choo kigumu au kukosa kabisa pamoja na kikohozi.

Veina ameongeza kwa kutoa elimu zaidi juu ya umuhimu na wakati sahihi wa kunywa maji ikiwa ni pamoja na kunywa maji yakiwa si ya baridi wala ya moto lakini pia kunywa maji nusu saa au saa moja kabla au baada ya kula.

Wakati Afisa lishe akiyasema hayo, Shamba Fm imezungumza na baadhi ya Wananchi kutaka kujua uelewa wao juu ya suala hilo na kubaini kuwa wengi wao hawajui madhara ya maji ya baridi, huku wakitumia nafasi hiyo kuwaomba wataalam wa afya kuendelea kutoa katika jamii ili kuwaepusha na Madhara.

JESHI LA ZIMAMOTO LATOA TAHADHARI YA MVUA KUBWA NCHINIBaada ya Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) kutabiri uwepo wa mv...
04/02/2025

JESHI LA ZIMAMOTO LATOA TAHADHARI YA MVUA KUBWA NCHINI

Baada ya Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) kutabiri uwepo wa mvua za wastani na juu ya wastani katika baadhi ya Mikoa, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limetoa tahadhari ya uwepo wa majanga yatakayotokana na mvua hizo.

Tahadhari hiyo imetolewa leo Februari 4, 2025 jijini Dodoma na Msemaji wa jeshi hilo, Naibu Kamishna wa Zimamoto na Uokoaji Puyo Nzalayaimisi ambapo amewaasa wananchi kuchukua tahadhari ikiwa ni kuondoka kwenye maeneo ya mabonde, kutovuka kwenye maji yanayotembea kwa kasi na kutovuka kwenye madaraja yaliyofunikwa na maji.

Mvua zinazoendelea kunyesha katika mikoa mbalimbali hapa nchini tayari zimeleta athari kwa baadhi ya maeneo ambapo Alfajiri ya Februari 04 Mkoani Mtwara watu zaidi ya 40 wameokolewa kwenye mafuriko yaliyosababishwa na mvua.

MECHI YETU DHIDI YA KAGERA NI NGUMU – SINGIDA BSKlabu ya Singida Black Starts imekiri kuwa mchezo wake wa ligi kuu dhidi...
04/02/2025

MECHI YETU DHIDI YA KAGERA NI NGUMU – SINGIDA BS

Klabu ya Singida Black Starts imekiri kuwa mchezo wake wa ligi kuu dhidi ya Kikosi cha Kagera Sugar utakaopigwa Ijumaa ya Januari 07, 2025 Mkoani Singida utakuwa mgumu kutokana na Kila timu kuhitaji alama tatu.

Akitoa taarifa kuhusu mchezo huo Leo Februari 04, 2025 Afisa habari wa Klabu ya Singida Black Stars Hussein Masanza amesema anafahamu kuwa mchezo huo utakuwa mgumu kutokana na klabu ya Kagera Sugar kuwa katika nafasi ngumu hivyo wanapambana kwa nguvu zaidi kujinasua kwenye mazingira hayo.

Masanza ameongeza kuwa kutokana ugumu huo wao wamejiandaa vyema huku wakitazamia kutumia vizuri faida ya kuwa uwanja wa nyumbani.

Address

Utalii Road
Iringa

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Shamba Fm Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Shamba Fm Radio:

Videos

Share

Category