UFM Radio TZ

UFM Radio TZ UFM is the leading radio station in Tanzania which is Part of Azam Media Ltd, a company owned by the

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Jerry Silaa amesema uwepo wa Kituo cha Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano kat...
23/01/2025

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Jerry Silaa amesema uwepo wa Kituo cha Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano katika eneo la Horohoro, kinachounganisha Tanzania na nchi ya Kenya, kutachochea shughuli za kiuchumi kati ya nchi hizo mbili pamoja na nchi nyingine za jirani.

Waziri Silaa amesema hayo leo wakati akikagua mradi wa ufikishaji wa mkongo wa Taifa wa Mawasiliano Mombasa kupitia kituo cha Horohoro kilichopo wilaya ya Mkinga, mkoani Tanga.

Mradi huo wa utawezesha mkongo wa taifa kuunganishwa na mikongo mingine saba ya baharini iliyopo katika pwani ya Mombasa.

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) CPA Moremi Marwa amesema hadi kufikia Desemba 2024 jumla ya Kilomita 13,991 za mkongo zimejengwa zikiunganisha mikoa yote ya Tanzania Bara.

Klabu ya Manchester United imeungana na Totenham pamoja na Juventus kutaka huduma ya mshambuliaji wa Paris Saint Germain...
11/01/2025

Klabu ya Manchester United imeungana na Totenham pamoja na Juventus kutaka huduma ya mshambuliaji wa Paris Saint Germain Randal Kolo Muani.

Wakati vilabu hivyo vikimpigia hesabu Muani, kwa mujibu wan mwandishi Ben Jacobs klabu yake ya PSG inampango wa kumuweka chambo kwa Aston Villa ili impate Jhon Duran.

Siku za hivi karibuni mshambuliaji huyo amehusishwa kuhama kwa miamba hiyo ya ufaransa kutoka na ufinyu wa nafasi chini ya kocha Luis Enrique.

Jambo hilo limewavuta karibu mashetani wekundu kumuhitaji Muani kwa mkopo ili kuongeza makali kwenye safu ya ushambuliaji inayosuasua chini ya Ruben Amorim.

Aliyekuwa mshambuliaji wa Liverpool na FC Barcelona Luis Suarez amesaidia kumuokoa  mwanaume mmoja aliyetaka kujiua.Kwa ...
11/01/2025

Aliyekuwa mshambuliaji wa Liverpool na FC Barcelona Luis Suarez amesaidia kumuokoa mwanaume mmoja aliyetaka kujiua.

Kwa kunukuu vyombo vya habari nchini Uruguay vimedokeza Suarez aliyekuwa ufukweni na mkewe Sofia Balbi, ghafla alipewa taarifa kuhusu mtu huyo aliyetaka kujitoa uhai.

Baada ya kupewa taarifa hiyo ,Mshambulizi huyo mwenye umri wa miaka 37, alikwenda kumtazama mzee huyo mwenye miaka 49 aliyekuwa anatishia kuruka juu ya mti wenye urefu wa mita sita.

Picha jongefu zilizorushwa kwenye taarifa ya habari zimemuonesha mchezaji huyo akimsihi mtu huyo ashuke na alifanikiwa kushuka baada saa 20 alizokaa juu ya mti.

Mwanamke aliyejitambulisha kwa jina moja la Andrea, ambaye anafanya kazi kwenye shirika la uokozi, alimtaja Suarez moja ya mashujaa waliofanikisha operesheni hiyo.

Usikose kusikiliza kipindi cha Morning Express Jumatatu ya Januari 13, 2025, tutakuwa mubashara na mkuu wa Wilaya ya Ila...
11/01/2025

Usikose kusikiliza kipindi cha Morning Express Jumatatu ya Januari 13, 2025, tutakuwa mubashara na mkuu wa Wilaya ya Ilala Mh. Edward Mpogolo.

Masuala ya mengi yatatolewa ufafanuzi wa kina.

Arusha 96.5
Shinyanga 98.7
Dodoma 101.7

Klabu ya Azam FC imemsajili kiungo mshambuliaji, Zidane Sereri kutoka Dodoma Jiji, kwa mkataba wa miaka 5.Kwa mujibu wa ...
11/01/2025

Klabu ya Azam FC imemsajili kiungo mshambuliaji, Zidane Sereri kutoka Dodoma Jiji, kwa mkataba wa miaka 5.

Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa kwenye ukurasa rasmi wa mchezaji huyo atadumu kwenye viunga vya Azam Complex hadi mwaka 2030.

Rais Mteule Wa Ghana John Mahama anatarajiwa kuapishwa kesho baada ya kusinda katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwishoni ...
06/01/2025

Rais Mteule Wa Ghana John Mahama anatarajiwa kuapishwa kesho baada ya kusinda katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwishoni mwa mwaka jana

Mahama alimshinda Makamu wa Rais wa nchi hiyo, Mahamudu Bawumia aliyekuwa akiwania nafasi hiyo kupitia chama tawala cha New Patriotic Party (NPP).

Rais huyo mteule anatarajiwa kuchukua nafasi ya Rais Nana Akufo-Addo, ambaye anaachia ngazi baada ya kuitumikia mihula miwili madarakani.

Akitoa Hotuba yake ya mwisho ya Hali ya Taifa Bungeni, Rais huyo amejivunia kushika wadhifa wa Urais wa taifa hilo akidai ni heshima kuu maishani mwake.

Aidha amesema anafurahi kukabidhi Ghana ambayo ipo salama, iliyoungana na yenye msingi thabiti katika kushik**ana na misingi ya kidemokrasia na kuheshimu utawala wa sheria.

Kiongozi Mkuu wa Jeshi la Sudan Abdel Fattah al-Burhan amepongeza pendekezo la Uturuki la kutatua mgogoro kati ya vikosi...
06/01/2025

Kiongozi Mkuu wa Jeshi la Sudan Abdel Fattah al-Burhan amepongeza pendekezo la Uturuki la kutatua mgogoro kati ya vikosi vyake na vikosi vya Msaada wa Haraka RSF.

Mwezi uliopita, Rais wa nchi hiyo Recep Tayyip Erdogan amesema nchi yake itasaidia kurejesha amani na utulivu katika taifa hilo lililokumbwa na vita barani Afrika.

Burhan amemwomba naibu waziri wa mambo ya nje wa Uturuki Burhanettin Duran kuwasilisha ujumbe kuhusu serikali yake kuunga mkomo mpango huo.

Akizungumza katika Mkutano uliofanyika Port Sudan, Waziri wa mambo ya nje wa Sudan Ali Youssef ameeleza nchi hiyo inahitaji ndugu na marafiki k**a Uturuki.

Erdogan alizungumza kwa njia ya simu na Burhan na kuahidi nchi yake kutafuta kusuluhisha mvutano kati ya Sudan na Umoja wa Falme za Kiarabu.

Chanzo: AFP

Korea Kaskazini imerusha kombora la masafa marefu kuelekea Bahari ya Mashariki, katika eneo la maji ambalo pia hujulikan...
06/01/2025

Korea Kaskazini imerusha kombora la masafa marefu kuelekea Bahari ya Mashariki, katika eneo la maji ambalo pia hujulikana k**a Bahari ya Japan.

Jeshi la Korea Kusini limethibitisha kufanyika kwa jaribio hilo, ingawa hakulitaja jina, wakati huu kukiwa na mfululilizo wa matukio yake ambayo yanakosolewa mataifa ya magharibi.

Duru zinaeleza urushaji huo umefanyika leo, wakati Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken akiwa ziarani Korea Kusini, kwa mazungumzo na baadhi ya mawaziri wake.

Kombora hilo la masafa marefu ni la kwanza kurushwa na Korea Kaskazini mwaka huu baada ya Novemba mwaka jana kufanya majaribio ya silaha yenye nguvu zaidi.

Hilo lilikuwa jaribio la kwanza la silaha kwa Rais wa Korea Kaskazini Kim Jong Un tangu kutuhumiwa kutuma wanajeshi kuisaidia Urusi kupambana na Ukraine.

Zaidi ya safari za ndege 1,300 zimeahirishwa nchini Marekani kufuatia msimu wa baridi kali inayosababisha ucheleweshwaji...
06/01/2025

Zaidi ya safari za ndege 1,300 zimeahirishwa nchini Marekani kufuatia msimu wa baridi kali inayosababisha ucheleweshwaji wa safari hizo.

Kwa mujibu wa takwimu zilizochapishwa kwenye tovuti ya kufuatilia safari za ndege FlightAware imedokeza zaidi ya safari 672 zimechelewa, huku 1,343 zikiahirishwa.

Viwanja vya ndege vilivyopo Washington DC, ukiwemo Uwanja wa Ndege wa Kitaifa wa Ronald Raegan, vimeathirika kutokana na mrundikano mkubwa wa theluji.

Chanzo :FlightAware

Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau huenda akajiuzulu wiki hii huku akikabiliwa na upinzani unaoongezeka ndani ya Chama...
06/01/2025

Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau huenda akajiuzulu wiki hii huku akikabiliwa na upinzani unaoongezeka ndani ya Chama chake cha Liberal.

Gazeti la The Globe and Mail limenukuu vyanzo vitatu ambavyo vinavyojua mambo ya ndani ya chama hicho, ambapo huenda tangazo hilo likatolewa leo.

Kwa mujibu wa gazeti hilo uamuzi huo utawasilishwa mbele ya Kikao cha Kamati Kuu ya Chama cha Liberal keshokutwa lakini haijabainika ikiwa Trudeau atasalia mamlakani mpaka lini.

Umaarufu wa Trudeau umepungua katika miezi ya hivi karibuni, huku Serikali yake ikinusurika kura za kutokuwa na imani naye na wakosoaji wakitaka ajiuzulu.

Ameapa kuongoza chama cha Liberals kwenye uchaguzi uliopangwa kufanyika Oktoba 2025, lakini amekabiliwa na shinikizo zaidi kutoka kwa Rais Mteule wa Marekani, Donald Trump.

CAFCC FT  ’ | Simba SC 2-1 CS Sfaxien.Arusha 96.5Shinyanga 98.7Dodoma 101.7
15/12/2024

CAFCC

FT ’ | Simba SC 2-1 CS Sfaxien.

Arusha 96.5
Shinyanga 98.7
Dodoma 101.7

Baada ya michezo mitatu hatua ya makundi barani Afrika, klabu ya Yanga SC imevuna alama Moja pekee.Alama hiyo wameipata ...
14/12/2024

Baada ya michezo mitatu hatua ya makundi barani Afrika, klabu ya Yanga SC imevuna alama Moja pekee.

Alama hiyo wameipata leo dhidi ya TP Mazembe kufuatia sare ya bao
1-1.

kwa namna ulivyoiona Yanga hii leo, Kocha Ramovic ataivuka hatua ya makundi ?

Arusha 96.5
Shinyanga 98.7
Dodoma 101.7
Dar es salaam 107.3

FT |  TP Mazembe 1-1 Young Africans SCArusha 96.5Shinyanga 98.7Dodoma 101.7Dar es salaam 107.3
14/12/2024

FT |

TP Mazembe 1-1 Young Africans SC

Arusha 96.5
Shinyanga 98.7
Dodoma 101.7
Dar es salaam 107.3

Kabla ya mchezo picha hii inayoonesha mashabiki waliovaa jezi za Yanga Sc na Simba Sc zimechapishwa kwenye ukurasa wa In...
14/12/2024

Kabla ya mchezo picha hii inayoonesha mashabiki waliovaa jezi za Yanga Sc na Simba Sc zimechapishwa kwenye ukurasa wa Instagram wa klabu ya TP Mazembe na kuambatanishwa na ujumbe unaosomeka “Kunguru tayari wako Hekaluni “



Arusha 96.5
Shinyanga 98.7
Dodoma 101.7
Dar es salaam 107.3

82 |  TP Mazembe 1-0 Young Africans SCArusha 96.5Shinyanga 98.7Dodoma 101.7Dar es salaam 107.3
14/12/2024

82 |

TP Mazembe 1-0 Young Africans SC

Arusha 96.5
Shinyanga 98.7
Dodoma 101.7
Dar es salaam 107.3

HT’ |  TP Mazembe1-0 Young Africans SCArusha 96.5Shinyanga 98.7Dodoma 101.7Dar es salaam 107.3
14/12/2024

HT’ |

TP Mazembe1-0 Young Africans SC

Arusha 96.5
Shinyanga 98.7
Dodoma 101.7
Dar es salaam 107.3

Upinzani nchini Korea kusini umetangaza ushindi baada ya kukamilika kwa kura ya maoni ya kutokuwa na imani na Rais Yoon ...
14/12/2024

Upinzani nchini Korea kusini umetangaza ushindi baada ya kukamilika kwa kura ya maoni ya kutokuwa na imani na Rais Yoon suk Yeol tangu jaribio lake la kuiweka nchi chini ya utawala wa jeshi kugonga mwamba.

Kura hiyo ya maoni inafanya kufika mwisho kwa mtafaruko wa kisiasa uliozuka baada ya Rais Yoon kutangaza nchi ipo chini ya utawala wa kijeshi Disemba 3 mwaka huu.

Kwenye hotuba yake iliyorushwa mubashara baada ya kukamilika kwa shughuli ya upigaji kura, Yoon amesema yu tayari kuachia ngazi ,lakini hajaomba radhi kwa jaribio lake lililoitumbukiza korea kusini kwenye mtihani.

Kati ya wabunge 300, 204 wamepiga kura ya kuondolewa kwa madai ya uasi, 85 wakipiga kura ya kupinga. Watatu hawakupiga kura, huku kura nane zikibatilishwa.

Pamoja na kufunguliwa mashtaka, Yoon amesimamishwa kazi huku Mahak**a ya Kikatiba ya Korea Kusini ikijadili kuhusu kura hiyo.

Hata hivyo Mahak**a ina siku 180 kutoa uamuzi kuhusu mustakabali wa Yoon.
Iwapo itaunga mkono kuondolewa kwake, Yoon atakuwa rais wa pili katika historia ya Korea Kusini kung’olewa Mamlakani.

Waziri Mkuu Han Duck-soo ambaye sasa ni kiongozi wa mpito wa taifa hilo amewaambia waandishi wa habari "atatumia nguvu zote kuhakikisha utawala wa haki."

Chanzo: AFP

Mwandishi

Address

1 Mandela Road
Dar Es Salaam
12301

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when UFM Radio TZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to UFM Radio TZ:

Videos

Share

Category