Liverpool habari

Liverpool habari Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Liverpool habari, News & Media Website, Dar es Salaam.

Kocha wa Liverpool, Arne Slot, ametoa taarifa kuhusu majeruhi ndani ya kikosi chake kuelekea mechi yao ya Ligi Kuu ya Ui...
03/01/2025

Kocha wa Liverpool, Arne Slot, ametoa taarifa kuhusu majeruhi ndani ya kikosi chake kuelekea mechi yao ya Ligi Kuu ya Uingereza dhidi ya Manchester United.

Joe Gomez hatakuwa sehemu ya kikosi kwa majuma kadhaa kutokana na hali yake ya majeraha ambayo bado haijaimarika. Hata hivyo, kuna habari njema kwa mashabiki wa Liverpool kwani Conor Bradley na Ibrahima Konatรฉ (Ibou) wanatarajiwa kushiriki mazoezi kwa mara ya kwanza leo baada ya kupona majeraha yao.

Hii ni mechi muhimu kwa Liverpool, na mashabiki wanatarajia kuona kikosi kikiwa na nguvu kamili ili kupambana na wapinzani wao wa jadi, Manchester United.

Tunaendelea kuomba afya njema kwa wachezaji wote wa kikosi na matumaini ya ushindi mkubwa!

Mambo bado magumu, naona Real Madrid wameamua  kukomaa na Trent.
03/01/2025

Mambo bado magumu, naona Real Madrid wameamua kukomaa na Trent.

Heri ya Mwaka Mpya 2025 kutoka Liverpool Habari!Tunapofunga pazia la mwaka 2024 na kufungua ukurasa mpya wa 2025, tunape...
31/12/2024

Heri ya Mwaka Mpya 2025 kutoka Liverpool Habari!

Tunapofunga pazia la mwaka 2024 na kufungua ukurasa mpya wa 2025, tunapenda kuchukua fursa hii kuwashukuru wapenzi wote wa Liverpool kwa upendo wenu, sapoti, na mshik**ano wa hali ya juu.

Mwaka huu umekuwa wa changamoto na mafanikio, na kila hatua tumechukua pamoja. Tumeshuhudia mechi kali, mabao ya kipekee, na nyakati za furaha ambazo zitaendelea kukumbukwa milele. K**a mashabiki wa Liverpool, umoja wetu umekuwa nguvu yetu kubwa.

Tunatumaini mwaka 2025 utakuwa wa baraka zaidi, mafanikio, na furaha kwa kila mmoja wenu. Pia tunatamani kikosi chetu kipendwa cha Liverpool kionyeshe mchezo wa hali ya juu na kutimiza ndoto zetu kubwa za kutwaa vikombe na kuleta furaha zaidi Anfield na duniani kote.

Heri ya mwaka mpya kwa familia yako na marafiki! Liverpool Habari itaendelea kuwa nawe kila hatua, tukikuletea habari zote muhimu, maoni, na uchambuzi wa kina kuhusu timu yetu pendwa.

YNWA โ€“ Youโ€™ll Never Walk Alone!
Imetoka kwa familia ya Liverpool Habari.

[๐ŸŸข] NEW: Liverpool bado wana matumaini kuwa Trent Alexander-Arnold atachagua kuendelea kuitumikia klabu yake ya utotoni....
31/12/2024

[๐ŸŸข] NEW: Liverpool bado wana matumaini kuwa Trent Alexander-Arnold atachagua kuendelea kuitumikia klabu yake ya utotoni. Mazungumzo kuhusu mkataba mpya yanaendelea kwa sasa.

[Chanzo: ]

Ameandika mshambuliaji wa zamani wa Liverpool, Michael Owen"Hatua ya Real Madrid kuweka wazi nia yao ya kumsajili Trent ...
31/12/2024

Ameandika mshambuliaji wa zamani wa Liverpool, Michael Owen

"Hatua ya Real Madrid kuweka wazi nia yao ya kumsajili Trent Alexander-Arnold inatoa dalili kuwa huenda ni suala la muda tu kabla ya nyota huyo kujiunga nao. Ikiwa Liverpool walikuwa na uhakika wa kumshawishi kusaini mkataba mpya, ni vigumu kuamini kwamba Madrid wangechukua hatua rasmi leo" . Mwisho wa kunukuu.

Inaonekana mazungumzo ya siri kati ya Madrid na wawakilishi wa Trent yamekuwa yakiendelea kwa muda, na sasa klabu hiyo imejihakikishia uwezekano wa kumpata mchezaji huyo. Ikiwa Liverpool hawatachukua hatua ya haraka na thabiti, kuna uwezekano mkubwa wa kumwona Trent akisaini mkataba na Real Madrid ifikapo Julai 2025.

Habari hii ni pigo kubwa kwa Liverpool na mashabiki wao, kwani Trent si tu beki wa kiwango cha juu, bali pia ni mmoja wa nyota muhimu wa klabu hiyo. Tunatarajia kuona jinsi hali hii itakavyobadilika katika miezi ijayo.

Pia, leo Liverpool imekataa ofa kutoka Real Madrid kwa ajili ya Trent ambaye amebakisha mwaka mmoja kwenye mkataba wake.
31/12/2024

Pia, leo Liverpool imekataa ofa kutoka Real Madrid kwa ajili ya Trent ambaye amebakisha mwaka mmoja kwenye mkataba wake.

Liverpool inakabiliwa na changamoto kubwa ya kuhakikisha Trent Alexander-Arnold anasaini mkataba mpya, hasa ikizingatiwa...
31/12/2024

Liverpool inakabiliwa na changamoto kubwa ya kuhakikisha Trent Alexander-Arnold anasaini mkataba mpya, hasa ikizingatiwa kwamba hadi sasa hakuna makubaliano yaliyofikiwa kati ya klabu na mchezaji huyo.

Real Madrid, wakitambua hali hii, wameendelea kuweka shinikizo wakilenga kumnasa Trent k**a mchezaji huru ifikapo Julai 2025. Ikiwa Liverpool haitafanikiwa kufikia muafaka na mlinzi huyo wa kulia, nafasi ya Madrid kupata huduma yake bila gharama ya usajili itakuwa kubwa zaidi.

Kwa upande mwingine, Liverpool inajua umuhimu wa Trent si tu k**a mchezaji wa kikosi, bali pia k**a kiungo muhimu wa falsafa yao ya mchezo. Mkataba mpya hautakuwa rahisi, lakini klabu ina kila sababu ya kufanya kila linalowezekana kumshawishi aendelee kuwa sehemu ya historia yao.

Je, mazungumzo haya yataleta mwanga mpya kwa Liverpool, au Real Madrid watafaidika na hali hii? Ni suala linalosubiriwa kwa hamu kubwa.

๐Ÿ“ Kauli ya Arne Slot kuhusu kutokuwepo kwa Federico Chiesa kwenye kikosi cha Liverpool kwenye baadhi ya mechi zilizopita...
30/12/2024

๐Ÿ“ Kauli ya Arne Slot kuhusu kutokuwepo kwa Federico Chiesa kwenye kikosi cha Liverpool kwenye baadhi ya mechi zilizopita:

๐Ÿ”ดโš ๏ธ Arne Slot amesema:
"Tunafanya kazi ya kuhakikisha anafikia kiwango bora cha utimamu wa mwili, na mara tu inapowezekana, tutamjumuisha kwenye timu."

"Tuliona ni bora Federico apate mazoezi ya ziada badala ya kuungana nasi kwa sasa."

Unadhani hatua hii ni bora kwa maendeleo ya Chiesa?

Liverpool hadi sasa imebakiwa na mabeki wa kati wawili pekee, ambao ni nahodha Virgil van Dijk na kijana mwenye kipaji J...
30/12/2024

Liverpool hadi sasa imebakiwa na mabeki wa kati wawili pekee, ambao ni nahodha Virgil van Dijk na kijana mwenye kipaji Jerome Quansah. Hii ni baada ya Joe Gomez kuondolewa uwanjani dakika ya 37 ya kipindi cha kwanza jana kutokana na majeraha ya misuli ya paja.

Kwa upande mwingine, Ibrahima Konatรฉ bado hajarejea kikosini, na hali hii imesababisha Liverpool kuwa na upungufu mkubwa katika safu ya ulinzi.

Je, Liverpool inapaswa kuingia sokoni Januari hii ili kuimarisha safu ya ulinzi?
K**a jibu ni ndiyo, ungependekeza mchezaji gani asajiliwe? Na k**a hapana, una maoni gani kuhusu suluhisho la muda mfupi kwa changamoto hii?

Tuma maoni yako na tuendelee kujadili jinsi Liverpool inaweza kujipanga katika kipindi hiki kigumu!

# Liverpoolhabari

ARNEEEE!! SLOOOOOTTT!! NA TIMU YENYE UTAMU WA ASALI.Mpira umemalizikaWestham 0 Liverpool 5.Diaz 30'Gapko 40'Salah 44'TAA...
29/12/2024

ARNEEEE!! SLOOOOOTTT!! NA TIMU YENYE UTAMU WA ASALI.

Mpira umemalizika
Westham 0 Liverpool 5.
Diaz 30'
Gapko 40'
Salah 44'
TAA 54'
Jota 84'

Gonga like salamu ziwafikie nyumbu hiyo tarehe 5 Januari, 2025.

Mvunjaji Rekodi: Mohamed Salah Anaandika Historia MpyaMohamed Salah, nyota wa Liverpool, anaendelea kuvunja rekodi na ku...
29/12/2024

Mvunjaji Rekodi: Mohamed Salah Anaandika Historia Mpya

Mohamed Salah, nyota wa Liverpool, anaendelea kuvunja rekodi na kuandika historia mpya katika Ligi Kuu ya Uingereza. Msimu huu, Salah ameweka kiwango cha kipekee cha kufunga au kusaidia kufunga mabao mara 1.54 kwa kila dakika 90 anapokuwa uwanjani. Hii ni rekodi ya juu zaidi kuwahi kufikiwa katika historia ya Ligi Kuu ya Uingereza.

Pira la utatoa hutoi limepigwa kipindi cha kwanza dhidi ya Westham na kupelekea Liverpool kuwa mbele kwa magoli matatu(3...
29/12/2024

Pira la utatoa hutoi limepigwa kipindi cha kwanza dhidi ya Westham na kupelekea Liverpool kuwa mbele kwa magoli matatu(3) kwa sifuri (0)

Magoli ya
Diaz 30'
Gapko 40'
Salah 44'

Hapo vipi?
29/12/2024

Hapo vipi?

Leo tunacheza dunia yote ipo kimya.Mchezo wa kumi nane(18) kwetu ndani ligi kuu ya Uingereza dhidi ya Westham Utd katika...
29/12/2024

Leo tunacheza dunia yote ipo kimya.
Mchezo wa kumi nane(18) kwetu ndani ligi kuu ya Uingereza dhidi ya Westham Utd katika dimba la London Stadium. Mechi itachezwa muda wa saa mbili na robo usiku(8:15pm).

Liverpool hadi sasa kwenye msimamo inaongoza kwa jumla ya alama sita(6) kabla ya mechi za leo.

Je nini utabiri wako kwenye mchezo huu?

Mohamed Salah: Mwanajeshi Shupavu wa AnfieldFikiria Mohamed Salah k**a jenerali shupavu wa vita, akiongoza jeshi la Live...
27/12/2024

Mohamed Salah: Mwanajeshi Shupavu wa Anfield

Fikiria Mohamed Salah k**a jenerali shupavu wa vita, akiongoza jeshi la Liverpool dhidi ya maadui wa Ligi Kuu ya Uingereza na mashindano mengine. Katika msimu huu wa vita, Salah ameonyesha uwezo wa kipekee kwenye uwanja wa vita, akiwa na silaha kali za kufunga na kutoa msaada kwa wenzake.

โš”๏ธ Magoli 19: K**a mshale unaopenya ngome za maadui, kila bao lake ni sawa na mshindi wa vita muhimu.

๐Ÿ›ก๏ธ Pasi za magoli 15: Ni k**a mkakati wa kijeshi unaoweka wenzake kwenye nafasi bora za kushambulia na kushinda vita.

Historia inaweza kumfananisha na jenerali maarufu wa vita k**a Napoleon Bonaparte, ambaye licha ya changamoto kubwa, alijulikana kwa mipango ya kushinda maadui wake. Salah, k**a Napoleon, hutumia mbinu za haraka na maamuzi mazuri, kuhakikisha Liverpool inaibuka mshindi dhidi ya kila mahasimu wake.

Je, Salah ataweza kudumisha ubora huu hadi mwisho wa msimu na kuipeleka Liverpool kwenye kilele cha ushindi? Muda utaamua, lakini kwa sasa, ni dhahiri kuwa huyu ni shujaa wa kweli wa Anfield

# Liverpoolhabari

Alama tatu(3) muhimu dhidi ya Leicester. Alama saba(7) kileleni, huku tukiwa na mchezo mmoja mkononi.Mpira umemalizika k...
26/12/2024

Alama tatu(3) muhimu dhidi ya Leicester. Alama saba(7) kileleni, huku tukiwa na mchezo mmoja mkononi.

Mpira umemalizika kwa Liverpool kuibuka na ushindi wa mabao matatu(3) kwa moja(1). Magoli ya Gapko 45+1', Jones 49' na Salah 82'.

Mpira ni mapumziko Liverpool 1 Leicester 1Gapko 45+1'
26/12/2024

Mpira ni mapumziko
Liverpool 1 Leicester 1
Gapko 45+1'

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255656707428

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Liverpool habari posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Liverpool habari:

Videos

Share