Watetezitv

Watetezitv WATETEZI TV is a Not-For-Profit online Tv under the Tanzania Human Rights Defenders Coalition(THRDC). Watetezi Tv operates in lieu of all applicable laws.

It will not be responsible to any subscriber who will post anything contrary to the applicable laws

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, DK Samia Suluhu Hassan amezindua Tume ya Rais ya Kutathmini kuhusu masuala ya m...
20/02/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, DK Samia Suluhu Hassan amezindua Tume ya Rais ya Kutathmini kuhusu masuala ya mgogoro wa ardhi eneo la Hifadhi ya Ngorongoro pamoja na Tume ya Rais ya Kutathmini zoezi la uhamaji wa hiari wa wakazi wa eneo la Hifadhi ya Ngorongoro.

Uzinduzi huo umefanyika leo Februari 20,2025 Ikulu Jijini Dar es Salaam, ambapo tume hiyo iliundwa rasmi Desemba 23,2024 ikiwa ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa Desemba 1,2025 wakati alipokutana na wakazi wa Ngorongoro.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia M***a Basuka kwa tuhuma za kumuua rafiki yake Issa Mohammed, kwa kumpiga ngu...
20/02/2025

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia M***a Basuka kwa tuhuma za kumuua rafiki yake Issa Mohammed, kwa kumpiga ngumi ya kichwa wakibishania zamu ya kupika kwenye nyumba waliyopanga.

Akizungumza leo Februari 20,2025 Kaimu K**anda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Wilbert Siwa, limetokea Februari 18,2025 katika eneo la Manyanya wilayani Chunya, amesema tukio hilo limetokea baada ya kuibuka ugomvi baina yao uliotokana na kubishania zamu ya kupika, ambapo mtuhumiwa alikua na zamu ya kuchota maji na marehemu akiwa na zamu ya kupika.

"Chanzo cha Tukio hili ni Mzozo uliotokea wakiwa katika chumba walichopanga, ulitokea wakibishania zamu ya kupika chakula ambapo marehemu alikuwa na zamu ya kupika chakula cha jioni na mtuhumiwa alikuwa na zamu ya kuchota maji." Ameeleza k**anda Siwa.

Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu imeamuru kutolewa kwa amri ya Mwanasiasa Mkongwe, Dkt. Wibroad Slaa (76) kufikishwa maha...
19/02/2025

Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu imeamuru kutolewa kwa amri ya Mwanasiasa Mkongwe, Dkt. Wibroad Slaa (76) kufikishwa mahak**ani ifikapo Machi 4, mwaka huu ili uweze kutolewa uamuzi wa kesi hiyo itakuwa inasikilizwa kwa njia gani.

Uamuzi huo ulitolewa leo mahak**ani hapo na Hakimu Mkazi Mkuu, Ushindi Swalo kesi hiyo ilipotajwa mahak**ani hapo leo Februari 19,2025.

Awali, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Job Mrema alidai kuwa shauri hilo lilipelekwa kwa ajili ya kutajwa na kueleza kuwa kwa kuwa shauri hilo lipo katika taratibu nyingine za kirufaa zinaendelea katika Mahak**a ya Rufaa ya Tanzania, hivyo aliiomba mahak**a ipange tarehe nyingine ya shauri hilo kutajwa.

Rufaa katika kesi hiyo ilikatwa na Mkurugenzi wa Mash*taka juu ya uamuzi uliotolewa na Mahak**a Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam wa kuamuru shauri namba 993/2025 kurudishwa mahak**ani hapo ili liweze kutolewa uamuzi juu ya dhamana ya Dkt. Slaa ambayo hapo awali iliwekewa pingamizi na upande wa mash*taka.

Baada ya Mrema kueleza hayo upande wa utetezi ukiongozwa na Wakili Melkion Sanga ulidai kuwa katika kikao kilichopita ilitolewa amri ili msh*takiwa aweze kufikishwa mahak**ani siku ya leo na kujua mwenendo wa kesi yake inavyoendelea.

Sanga alidai kuwa kwa kuwa msh*takiwa hakufikishwa mahak**ani aliiomba mahak**a itoe ahirisho fupi ili aweze kufikishwa mahak**ani k**a ilivyoamuriwa katika kikao kilichopita, pia alidai kuwa amri ya mahak**a ilivyotolewa ilitakiwa ifuatwe kwa msh*takiwa kufikishwa mahak**ani hapo.

Itakumbukwa ni takribani siku 40 zimepita tokea Dkt. Willbroad Slaa alipotiwa kizuizini na kufunguliwa kesi ambapo wadau mbalimbali wanaotetea haki za binadamu wamekuwa wakipaza sauti na kutaka mshtakiwa apatiwe haki ya dhamana wakidai kuwa shauri linalomkabili alimkoseshi haki ya dhamana.

Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umesema umesikitishwa sana na kitendo cha kutokusomwa kwa wakat...
19/02/2025

Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umesema umesikitishwa sana na kitendo cha kutokusomwa kwa wakati kwa maamuzi madogo ya Mahak**a Kuu ya Tanzania katika kesi ya kikatiba Na. 36 ya Mwaka 2019, kati ya Onesmo Olengurumwa ambaye ni Mtetezi wa haki za binadamu na Mratibu Kitaifa wa THRDC dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Shauri hilo linapinga uhalali wa kikatiba wa vifungu na 178, 243, 244, 245, 246, 247, 248, 249, 250, 256, 257,258 na 259 vya Sheria ya Mwenendo ya Makosa ya Jinai, Sura ya 20 ambavyo vinaruhusu mtuhumiwa kufunguliwa kesi katika Mahak**a za Chini (Committal Proceedings) wakati upelelezi ukiwa haujakamilika kwa makosa ambayo Mahak**a Kuu ndio ina mamlaka ya kusikiliza kesi
hizo.

Shauri hilo ambalo liko mbele ya Mhe. Jaji Manyanda, lilipangwa kwaajili ya uamuzi mdogo kwa mara ya kwanza tarehe 28 Novemba 2024 lakini uamuzi haukusomwa kwasababu haukuwa tayari na uliahirishwa hadi Desemba 10, 2024 pia uliahirishwa hadi Desemba, 20, 2024 ukaahirishwa tena hadi Januari 14, 2025 na siku hiyo pia uamuzi haukusomwa na kuahirishwa hadi Februari 06, 2025 pia haukusomwa tena hadi Februari 18, 2025 ambapo haukusomwa tena

"Februari 18, 2025 uamuzi huo mdogo haujasomwa kwasababu Jaji hakuwepo mahak**ani na ndipo msajili amepanga uamuzi mdogo wa kesi hiyo usomwe Februari 25, 2025. Mpaka leo ahirisho hilo la kusomwa kwa uamuzi mdogo ni la tano(05) bila sababu za msingi" Imeeleza taarifa iliyotolewa na THRDC.

THRDC imesema Kucheleweshwa kusomwa kwa wakati kwa maamuzi ya Mahak**a katika kesi hiyo ni kinyume cha Kanuni zinazo ongoza mashauri ya kikatiba nchini, ambapo kwa mujibu wa kanuni ya 9(1) ya Kanuni za Sheria ya Haki Msingi na Wajibu (Mwenendo na Utaratibu) za Mwaka 2014.

THRDC imesikitishwa na ukiukwaji huo wa sheria na utaratibu wa kimahak**a na imesema jambo hilo lina fifisha imani ya umma kwa mahak**a na kuathiri utawala wa sheria, kwani haki iliyocheleweshwa ni haki iliyonyimwa.

Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ)  kimeeleza kusikitishwa na tukio la hivi karibuni ...
18/02/2025

Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ) kimeeleza kusikitishwa na tukio la hivi karibuni lililotokea Unguja, ambapo imedaiwa kuwa Bi. Khadija Shaaban Ali (34) alimshambulia na kumjeruhi mke mwenzake kwa kumpiga visu, Bi Maimuna Said Suleiman (38), tukio lililomsababishia maumivu na majaraha makubwa.

Hayo yameelezwa kwenye Taarifa iliyotolewa leo February 18,2025 na TAMWA- ZANZIBAR ambapo imesema tukio hilo ni kinyume cha haki za binadamu.

Aidha TAMWA imeshangazwa na kitendo cha Mume wa wanawake hao kuondoka na kuwaacha wake zake wakiwa kwenye ugomvu uliopelekea bi Khadija kumjeruhi mke mwenzake.

"Kwa mujibu wa ripoti kutoka vyombo mbalimbali vya habari, ikiwemo ZBC Radio kupitia kipindi cha Habari za Mawio kilichorushwa hewani tarehe 11 Februari 2025 ni kuwa wanawake hao walikuwa wamepakiwa katika gari moja na mume wao hadi nyumbani kwa mke mdogo huko Chukwani, mkoa wa mjini magharibi.
Kwa mujibu wa mawio mume aliingia ndani na kuwaacha wake zake hao wawili peke yao na ndipo mkasa huo ukaanza kutokea, ambapo taarifa zinadai kuwa Bi Maimuna alianza kupigwa kwa visu na kupiga makelele ya kuomba msaada lakini hata mumewe hakuweza kutoka kwa wakati." Imeeleza taarifa hiyo.

"TAMWA, ZNZ inasikitishwa na tukio hilo la Bi Khadija kumshambulia mke mwenziwe vibaya na kumsababishia madhara makubwa ya kimwili.
TAMWA ZNZ inasikitika zaidi na kitendo hicho cha mume wa wake hao kuondoka na kuwaacha peke yao bila ya hadhari zozote wakati yeye anawajua tabia zao vya kutosha." Imeongeza taarifa hiyo.

TAMWA imesisitiza kuchukuliwa kwa hatua kali za kisheria dhidi ya wote waliohusika na kadhia hiyo ili iwe funzo kwa watu kujichukulia sheria mikononi mwao.

Wakati mapigano yakiendelea kushamiri mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na maelfu ya wakaazi wakilazi...
18/02/2025

Wakati mapigano yakiendelea kushamiri mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na maelfu ya wakaazi wakilazimika kuyakimbia makazi yao, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) limetoa wito wa kuchukuliwa hatua za dharura ili kuokoa mwaka wa masomo kwa maelfu ya watoto waliokosa fursa ya elimu.

Kwa mujibu wa UNICEF, hata kabla ya kuongezeka kwa mzozo huu, mfumo wa elimu katika eneo hilo ulikuwa tayari unakabiliwa na changamoto kubwa, hasa kutokana na idadi kubwa ya wakimbizi waliotawanyika katika maeneo mbalimbali. Taarifa zinaonyesha kuwa zaidi ya watu milioni 6.5, wakiwemo watoto milioni 2.6, wameathiriwa na hali ya uhamaji katika eneo hilo.

Tangu mwanzoni mwa mwaka huu, mapigano makali yamesababisha kufungwa kwa zaidi ya shule 2,500 katika mikoa ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini, huku shule nyingi zikiharibiwa na nyingine zikibadilishwa kuwa makazi ya wakimbizi. Kwa sasa, takribani watoto 795,000 hawana fursa ya kupata elimu, idadi ambayo imeongezeka kutoka 465,000 mwezi Desemba 2024. Ikiwemo mkoa wa Ituri, idadi ya watoto wasio na fursa ya masomo mashariki mwa DRC imefikia zaidi ya milioni 1.6.

Athari za Mzozo kwa Elimu ya Watoto

Mwakilishi wa UNICEF nchini DRC, Jean Francois Basse, amesema kuwa hali hii ni dharura kwa watoto na inahitaji hatua za haraka. “Hii ni hali ya dharura kwa watoto,” alisema Basse, akisisitiza kuwa shule ni muhimu si tu kwa elimu, bali pia kwa ulinzi wa watoto dhidi ya hatari za kuajiriwa na makundi ya kijeshi pamoja na unyanyasaji wa kingono.

Hata baada ya shule za Goma kufunguliwa mnamo Februari 9, idadi ya wanafunzi waliorejea shuleni imesalia kuwa ndogo kutokana na hofu ya usalama. Wazazi wengi wameeleza wasiwasi wao kuhusu usalama wa watoto wao, hali inayosababisha wengi wao kusita kuwapeleka watoto shuleni.

Mbali na kutoa elimu, UNICEF imesisitiza kuwa shule pia zinatoa msaada wa kisaikolojia kwa watoto waliokumbwa na madhila makubwa wakati wa vita.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limefanikiwa katika operesheni maalum dhidi ya uhalifu na wahalifu, iliyofanyika kuanzia ...
18/02/2025

Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limefanikiwa katika operesheni maalum dhidi ya uhalifu na wahalifu, iliyofanyika kuanzia Januari hadi Februari 2025, ambapo watuhumiwa mbalimbali walik**atwa na kufikishwa mahak**ani.

Akitoa taarifa hiyo, K**anda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Justine Masejo, amesema kuwa katika operesheni hiyo, walifanikiwa kuwak**ata watuhumiwa 15 wa makosa ya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia, kati yao 10 wakihusishwa na tuhuma za ubakaji na wengine watato (5) kwa ulawiti.

Kwa mujibu wa K**anda Masejo, baada ya kufikishwa mahak**ani, watuhumiwa watatu wa ubakaji wamehukumiwa kifungo cha maisha jela, mmoja kifungo cha miaka 30. Aidha, kwa makosa ya ulawiti, mtuhumiwa mmoja amepewa kifungo cha maisha, huku mwingine akihukumiwa kifungo cha miaka 30. Kesi za watuhumiwa wengine bado zipo katika hatua mbalimbali za kisheria.

Mapambano Dhidi ya Dawa za Kulevya

Katika misako dhidi ya dawa za kulevya, Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha lilik**ata watuhumiwa 26 wakiwa na kilogramu 196.4 za mirungi, na watuhumiwa 22 wakiwa na kilogramu 32 za bangi. Aidha, hekari 10 za mashamba ya bangi ziliteketezwa. Watuhumiwa wote wa dawa za kulevya tayari wamefikishwa mahak**ani kwa hatua zaidi.

Mapambano Dhidi ya Ujangili

K**anda Masejo pia ameeleza kuwa katika mapambano dhidi ya ujangili, watuhumiwa wawili walik**atwa wakiwa na kilogramu 20 za nyama ya nungunungu. Watuhumiwa hao tayari wamefikishwa mahak**ani na kesi zao zinaendelea.

Uk**ataji wa Pombe Haramu na Wizi

Katika operesheni hiyo, watuhumiwa 38 walik**atwa wakiwa na lita 172 za pombe haramu aina ya Moshi, pamoja na mitambo minne ya kutengeneza pombe hiyo. Wote wamefikishwa mahak**ani kwa hatua za kisheria.

Aidha, jumla ya watuhumiwa 202 wa makosa ya wizi walik**atwa na kesi zao zinaendelea kushughulikiwa kwa mujibu wa sheria.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limewahimiza wananchi kutojihusisha na vitendo vya uhalifu, huku likiwataka madereva wa vyombo vya moto kufuata sheria za usalama barabarani ili kuepusha ajali na madhara mengine.

Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imesema kumekuwa na ongezeko kubwa la wananchi wanaotoa notisi za kuishtaki serika...
18/02/2025

Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imesema kumekuwa na ongezeko kubwa la wananchi wanaotoa notisi za kuishtaki serikali, ambapo idadi imefikia zaidi ya 500 kwa mwaka.

Hali hiyo imedaiwa kuonesha kuwa baadhi ya viongozi na watumishi wa umma wanakiuka misingi ya utawala wa sheria.

Akizungumza Februari 17, 2025, katika uzinduzi wa K**ati ya Ushauri wa Kisheria na Kliniki ya Sheria bila Malipo, Mkurugenzi wa Huduma za Uratibu na Ushauri wa Kisheria, Neema Ringo, ambaye ni mwakilishi wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, amesema ongezeko hilo linadhihirisha kuwa wananchi wengi wanakwazwa na namna wanavyohudumiwa na viongozi au watumishi wa umma katika utekelezaji wa majukumu yao.

“Ongezeko hili linaonesha kuwa kuna maeneo ambayo viongozi na watendaji wa serikali hawazingatii utawala wa sheria au hawatoi mwongozo wa kutosha kwa wananchi kuhusu taratibu za kufuata. Hii inawafanya wananchi kuhisi haki zao zinakiukwa, na kwa kweli, baadhi yao wanakuwa na madai ya msingi, hivyo kutoa notisi za kuishtaki serikali,” amesema Ringo.

Kutokana na hali hiyo, alisema serikali imeanzisha k**ati hizo za ushauri wa kisheria ambazo zitasimamiwa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kushirikiana na ofisi za Wakuu wa Wilaya na Mikoa. K**ati hizo zitakuwa kiunganishi kati ya wananchi na serikali kwa lengo la kusikiliza malalamiko na kutoa ushauri wa kisheria kabla ya wananchi kufikia hatua ya kufungua mash*taka mahak**ani.

“K**ati hizi zitatoa fursa kwa wananchi kueleza changamoto zao na kupata mwongozo wa kisheria kwa wakati, kabla ya kufikia hatua ya kuishtaki serikali. Pia zitawasaidia wananchi kuelewa taratibu za kisheria ili wasipoteze haki zao kwa kuchelewa kuchukua hatua stahiki,” ameongeza Ringo.

Mahak**a Kuu Kanda ya Bukoba imepokea ripoti ya kitabibu inayothibitisha kuwa mshtakiwa wa kwanza katika kesi ya mauaji ...
18/02/2025

Mahak**a Kuu Kanda ya Bukoba imepokea ripoti ya kitabibu inayothibitisha kuwa mshtakiwa wa kwanza katika kesi ya mauaji ya mtoto mwenye ulemavu wa ngozi, Padri Elipidius Rwegoshora, ana akili timamu na yuko katika hali nzuri kiafya.

Ripoti hiyo, iliyotolewa na Hospitali ya Gereza la Isanga mkoani Dodoma, ilisomwa mnamo Februari 17, 2025 mahak**ani hapo wakati wa kusikilizwa kwa maelezo ya awali ya kesi hiyo yenye namba 25513/2024.

Jaji Gabriel Malata alisema ripoti hiyo, yenye kumbukumbu namba 11927/2024 na iliyosainiwa na Dk. Enock Changarawe, haikuonyesha dalili zozote za matatizo ya afya ya akili kwa Padri Rwegoshora.

Kesi hiyo inamuhusisha pia baba mzazi wa mtoto aliyeuawa, Asimwe Novath, pamoja na wash*takiwa wengine akiwemo Novath Venant, Nurdini Amada Masudi, Ramadhani Selestine, Rweyangira Burukadi Alphonce, Dastan Bruchard, Faswiu Athuman, Gozbert Alikad, na Desdery Everist.

Tukio hilo la mauaji limeendelea kuzua taharuki na mjadala kuhusu usalama wa watu wenye ulemavu wa ngozi nchini. Mahak**a sasa inatarajiwa kutoa mwelekeo wa hatua zinazofuata baada ya kupokea maelezo ya awali kutoka kwa pande zote.

Wanafunzi wawili wa shule ya Msingi na Sekondari wakazi wa Kitongoji cha Kezaria Kata ya Ikuti Wilaya ya Rungwe Mkoani M...
16/02/2025

Wanafunzi wawili wa shule ya Msingi na Sekondari wakazi wa Kitongoji cha Kezaria Kata ya Ikuti Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya wamefariki dunia huku watatu wakijeruhiwa baada ya kupigwa na radi iliyoambatana na mvua kubwa majira ya mchana Februari 15,2025.

Akizungumza na Watetezi TV kwa njia ya simu Dkt Baraka Mwasankumbo Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Ikuti amewataja waliofariki kuwa ni Tumsifu Hosiana Mbughi(14)jinsi ya k**e mwanafunzi wa kidato cha pili Sekondari ya Ikuti na Bryan Ngairo(11)jinsi ya kiume mwanafunzi wa darasa la sita Shule ya Msingi Kinyika.

Waliojeruhiwa ni pamoja na Hubiri Hosiana Mbughi (5),Tumepewa Hosiana Mbughi (3) na Neema Lusajo Kalinga(11) na baada ya kupatiwa matibabu hali zao zinaendelea vema wameruhusiwa kurejea mwakwao.

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kezaria Simeon Kabula Seme amesema alipata taarifa za tukio hilo majira ya saa 8:00 mchana ndipo alipofika eneo la tukio ambapo majirani waliwawahisha Kituo cha Afya Ikuti na kuthibitika vifo vya wanafunzi wawili na majeruhi watatu na kwamba walikuwa kwenye masomo ya ziada (tuition) ndipo wakakutwa na ajali.

Diwani wa Kata ya Ikuti Charles Kalinga amefika msibani kwa kwa ajili ya kuwafariji wafiwa na kuwaona majeruhi Kituo cha Afya Ikuti.

Hata hivyo ameishukuru ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe na ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwa kufika mapema eneo la tukio wakati huo akiomba Serikali kufunga vyombo vya kudhibiti radi kutokana na kuwepo kwa matukio ya mara kwa mara katika Kata yake.

"Hivi karibuni Afisa Utumishi alinusurika kifo alipokuwa akitekeleza majukumu yake ofisi ya Mtendaji Kata ilhali mtu mmoja alifariki baada ya kupigwa na radi miaka miwili iliyopita"alisema Kalinga.

K**anda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Benjamin Kuzaga kwa sasa yupo nje ya Mkoa hivyo Kaimu K**anda atakuwa kwenye nafasi nzuri ya kulizungumzia suala hilo.

“Kauli mbiu ni bila mabadiliko hakuna uchaguzi. K**a hawataki kuleta mageuzi kwa hiari wataleta mageuzi kwa shuruti. Tuj...
15/02/2025

“Kauli mbiu ni bila mabadiliko hakuna uchaguzi. K**a hawataki kuleta mageuzi kwa hiari wataleta mageuzi kwa shuruti. Tujiandae kuzuia uchaguzi k**a hawataki kuleta mageuzi.” –

Tundu Lissu, Mwenyekiti CHADEMA akizungumza na wananchi wa Manyoni leo Februari 15,2025.

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kanda ya Kaskazini, Godbless Lema, amezungumzia dhan...
15/02/2025

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kanda ya Kaskazini, Godbless Lema, amezungumzia dhana ya 'NO REFORM NO ELECTION' kuwa ni dhana inayolenga mabadiliko kwenye mfumo wa uchaguzi na utawala bora, kwani Uchaguzi ndo unaoamua mfumo wa maisha kwa kila mwananchi.

Kupitia ukurasa wake wa X, leo Februari 15, 2025 Lema ameandika yafuatayo;

"Kuna FIKRA unaziona unashangaa sana. Kufikiri NO REFORMS NO ELECTION ni jambo linalohusu UCHAGUZI ni kutokujua maana halisi ya mabadiliko na kusudi tunalo litaka. Mifumo takribani yote ya utawala wa Nchi inaamuliwa na viongozi wanaotokana na UCHAGUZI. Kufanya mzaha na uchaguzi ni kufanya mzaha na biashara, ujasiriamali,afya ,elimu usalama na future ya wajukuu na vitukuu vya Nchi hii.

Utakuwa ni Ubinafsi Mkubwa kujali maslahi ya Urais,Ubunge na Udiwani ktk kuamua dhana hii kuliko mtazamo mpana wa afya na ustawi wa Nchi yetu. Ubunge na Urais sio ajira ni utumishi , hivyo misingi ktk kutafuta kazi hizi lazima uongozwe na ukweli na haki. Ukishiriki uchaguzi unashindwa unaibiwa kura usiposhiriki pia unashindwa , kwa hiyo matokeo yanafanana either way , kwa hiyo kubadilisha matokeo ni kuchukua hatua tofauti. Hivyo basi kila mtu anahusika ktk kufikiri FIKRA hii mpya ya No Reforms no Election . NI wajibu wa wananchi wote."

Mtandao  wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umesaini mkataba wenye thamani ya Euro €1,500,000 kutoka Umoja...
15/02/2025

Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umesaini mkataba wenye thamani ya Euro €1,500,000 kutoka Umoja wa Ulaya (European Union) kwa ajili ya mradi wa miaka minne utakaoanza kutekelezwa kuanzia mwaka 2025 hadi 2028. Mradi huo unaoitwa “Kulinda Utawala wa Sheria, Nafasi ya Asasi za Kiraia, na Uwajibikaji Tanzania kupitia Mashirikiano yaliyoboreshwa”

Mradi huu utatekelezwa kwa kushirikiana na mashirika mengine matatu ambayo ni Jumuiya ya Wanasheria wa Afrika Mashariki (EALS), Chama cha wanasheria wa Afrika (PALU) , na Chama cha Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA).

Lengo la mradi huu ni kuboresha utawala bora, kuimarisha nafasi ya kiraia, na kukuza uwajibikaji nchini Tanzania.

Walengwa wakuu wa mradi huu ni Asasi za Kiraia (CSOs), Vyama vya Wanasheria, na Taasisi za Serikali. Mradi unalenga kuwawezesha walengwa hao kwa kuboresha uwezo wao wa kushawishi mabadiliko chanya ya kisheria, kujenga mashirikiano ya kimkakati, na kutetea haki za jamii zenye mahitaji maalumu. Kupitia shughuli k**a mafunzo, usaidizi wa kiutendaji, na mazungumzo ya kimkakati, mradi huu utaimarisha ushirikiano, imani ya umma, na kusaidia utawala bora.

Utekelezaji wa mradi utaanza rasmi mapema mwaka huu, ukilenga kukuza haki za binadamu, kuimarisha uwajibikaji, na kuhakikisha mageuzi endelevu katika sekta muhimu nchini Tanzania.

*Imetolewa na*
*THRDC*

Ujumbe wa Maaskofu wa Kanisa Katoliki na Protestanti nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo umekutana na waasi wa M23 k...
13/02/2025

Ujumbe wa Maaskofu wa Kanisa Katoliki na Protestanti nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo umekutana na waasi wa M23 katika juhudi za kutafuta amani nchini humo.

Wajumbe hao wa makanisa waliongozwa na Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki katika jimbo la Kivu Kaskazini, Askofu Ngumbi Ngengele ambapo walitilia mkazo haja ya kushirikiana ili kuhakikisha amani inarejea Goma na maeneo mengine yanayoathiriwa na machafuko hayo.

Askofu Donatien Nshole, katibu Mkuu wa Kongamano la Maaskofu wa Kongo,CENCO , amesema kuna mambo mengi ya kujadili kuhusu mgogoro huo iwapo pande husika zitageukia meza ya mazungumzo kwa kutafuta amani.

"Tulielewa kuwa kuna mambo mengi ambayo yanaweza kutatuliwa ikiwa Wakongo wataketi katika meza moja ya mazungumzo ili kuutatua mgogoro huu. Pia kwetu mazungumzo hayo yalilenga kuwaonesha hofu ya Wakongomani kuhusu kuligawa taifa hili la Kongo. Kuhusu uporaji haramu wa maliasili huko pia tulikuwa na majibu ya uhakika na kwamba hawana lengo la kuigawa DRC vipande vipande", alisema Nshole.

Kwa zaidi ya saa tatu wajumbe hao wa Kanisa Katoliki na Wakristo wa madhehebu mbalimbali nchini DRC walijadili njia za amani katika Mgogoro huo unaosambaa mashariki mwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Kwa mujibu wa Askofu Donatien N'SHOLE, baada ya kikao hicho na viongozi wa M23, wajumbe hao walionyesha matumaini kuhusu usitishwaji wa mapigano na kuanzishwa kwa safari za ndege kwenye uwanja wa ndege wa Goma, jambo ambalo linaweza kusaidia kurejesha hali ya kawaida na kuimarisha uchumi wa wakazi.

Chanzo DW

Serikali ya Kenya imetangaza kwamba Nyati wa majini wanaweza kutumika k**a mlo, licha ya kwamba wanyama hao hawapo nchin...
13/02/2025

Serikali ya Kenya imetangaza kwamba Nyati wa majini wanaweza kutumika k**a mlo, licha ya kwamba wanyama hao hawapo nchini humo kwa sasa.

Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo Dk Allan Azegele alifichua kuwa hatua hiyo inafuatia miaka ya maandalizi na ushirikiano wa kimataifa.
"Mpango huu umekuwa ukiendelezwa tangu 2018 wakati Kenya na Brazili zilipoanzisha itifaki ya kuagiza/kusafirisha nje wakati wa Maonyesho ya Kimataifa ya Mifugo ya Uberaba katika Jimbo la Minas Gerais," Dkt Azegele alinukuliwa na gazeti la Daily Nation Online akisema.

Mlo wa nyati wa majini unatarajiwa kuleta mafao katika sekta ya nyama na maziwa nchini Kenya na kile ambacho wataalamu wanakitaja kuwa bidhaa bora zaidi.

"Nyama ya nyati wa nyumbani ni nyembamba, yenye afya, na ina mafuta kidogo ikilinganishwa na nyama nyekundu ya jadi ya ng'ombe, kondoo na mbuzi," Dk Azegele alibainisha.

"Maziwa yao, ambayo yana kiwango kikubwa cha mafuta na protini kuliko maziwa ya ng'ombe, yanafaa zaidi kwa kuzalisha bidhaa za maziwa k**a vile jibini, mtindi na siagi."

Ili kuhakikisha mabadiliko ya haraka, serikali imetaja kipindi cha majaribio cha miaka miwili ambapo ni Kituo cha Rasilimali za Jenetiki ya Wanyama nchini (KAGRC) pekee na wakulima walioidhinishwa kufuga nyati hao.

Tamko hilo chini ya Sheria ya Kudhibiti Nyama, ililotolewa kupitia Notisi ya Gazeti namba 977 la Januari 31, 2025, na Katibu wa Baraza la Mawaziri wa Kilimo na Maendeleo ya Mifugo Mutahi Kagwe, linaonyesha mwanzo wa kuanzishwa kwa uangalifu wa mifugo hawa wa bara Asia Kusini kwenye mandhari ya kilimo cha Kenya.

Chanzo BBC

“Mafanikio ya Mwanaume yapo kwenye amani ya Mke wake yaani k**a Mkeo hana amani hauwezi kupiga hatua na ukiona umeendele...
13/02/2025

“Mafanikio ya Mwanaume yapo kwenye amani ya Mke wake yaani k**a Mkeo hana amani hauwezi kupiga hatua na ukiona umeendelea Mwanaume wakati Mkeo ana majonzi na yule Mke ndio Mungu alikupangia, maendeleo yako ni ya ushirikina, yaani k**a kuna Mwanaume ameendelea halafu Mke wake ana majonzi na manung’uniko, hana amani kwenye ndoa hayo maendeleo ni ya ushirikina”

“Hakuna maendeleo yanayotoka kwa Mungu k**a ndoa haina amani kwahiyo niwaombe Wananchi wa Arusha tumpe amani na furaha Mwanamke na tukifanya hivyo hata ukatili wa kijinsia utapungua, niwaombe pia tumtangulize Mungu hata kwenye ndoa na itatusaidia kupunguza migogoro hata Wizara ya Mama yangu Gwajima haitokuwa na migogoro mingi”

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Makonda akiongea leo Jijini Arusha kwenye kikao cha maandalizi ya maadhimisho ya wiki ya Wanawake Duniani ambayo kitaifa yatafanyika Arusha.

Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kinondoni imeelezwa kuwa vijana sita, wakiwemo mabondia wawili, walipanga kumteka mfanyabiashar...
12/02/2025

Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kinondoni imeelezwa kuwa vijana sita, wakiwemo mabondia wawili, walipanga kumteka mfanyabiashara Deogratus Tarimo kwa lengo la kumlawiti na kumsababishia maumivu.

Kesi hiyo, inayowakabili washtakiwa Fredrick Nsato (21), bondia Isaack Mwaifuani (29), Benk Mwakalebela (40), bondia Bato Twelve (32), dereva teksi Nelson Msela (24), na Anitha Temba (27) maarufu k**a Jack, imeendelea kusikilizwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Ramadhani Rugemalira.

Wakili wa Serikali Mkuu, Nassoro Katuga, amesema kuwa Anitha alihusika katika kumshawishi Tarimo kukutana naye hotelini kwa madai ya kujadili biashara, ambapo alinaswa kwenye mtego wa wash*takiwa waliokuwa na mpango wa utekaji.

Ilidaiwa kuwa Novemba 11, 2024, Tarimo alipofika hotelini, Anitha alimwelekeza kusubiri katika kaunta ya baa. Baada ya muda mfupi, washtakiwa Mwaifuani, Mwakalebela, na Twelve waliwasili katika gari aina ya Toyota Raum namba T 237 EGE na kujitambulisha k**a polisi.

Walipomvuta Tarimo kuelekea kwenye gari, alipiga kelele, hali iliyowafanya kumwachia na kumtishia kuwa wangempata tena. Taarifa zilifikishwa katika Kituo cha Polisi Gogoni na uchunguzi ukaanza, hatimaye kusababisha kuk**atwa kwa wash*takiwa hao.

"Tunaposema bila mabadiliko hakuna uchaguzi tuna maana gani? Tuna maaana kwamba kusipokuwa na mabadiliko yanayohitajika ...
12/02/2025

"Tunaposema bila mabadiliko hakuna uchaguzi tuna maana gani? Tuna maaana kwamba kusipokuwa na mabadiliko yanayohitajika ya mfumo wa uchaguzi, tutafanya kila tunaloweza, kwa nguvu tulizonazo kuhakikisha kwamba uchaguzi mkuu haufanyiki mwaka huu, hatuzungumzii kususia uchaguzi, hatutasusia, tutaenda kuwaambia Watanzania, na tutaiambia jumuiya ya kimataifa, na tutawaambia walimwengu kwamba k**a CCM na serikali yake haipo tayari kufanya mabadiliko kwenye mfumo wa uchaguzi ili kuhakikisha chaguzi huru na za haki, uchaguzi wa mwaka huu usifanyike kabisa, ndiyo maana ya 'No Reform No Election' bila mabadiliko hakuna uchaguzi."

"Ninataka niwe wazi hapa, huu siyo uamuzi wa Mwenyekiti mpya wa CHADEMA Tundu Lissu, huu ni msimamo wa CHADEMA k**a ulivyowekwa na vikao vyake vya juu vya kikatiba: K**ati Kuu, Baraza Kuu, Mkutano Mkuu wa Taifa" - Lissu.

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa, Tundu Lissu akizungumza na wanahabari Makao Makuu ya chama hicho mkoani Dar es Salaam, leo Februari 12, 2025.

Address

P. O Box 105926
Dar Es Salaam
00225

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Watetezitv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Watetezitv:

Videos

Share

Category