Mratibu Kitaifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) Wakili Onesmo Olengurumwa ameunga mkono kauli ya Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Emanuel Nchimbi kuonya juu ya Asasi za Kiraia kutojihusisha na masuala ya siasa.
Wakili Olengurumwa amesema ni makosa makubwa kisheria kwa Asasi hizo kushiriki kwa njia yoyote ile katika mambo yanayohusu siasa au wagombea na kuwa alichokisema Dr. Nchimbi ni Sahihi.
“Kwa hiyo tunachosema ni kwamba ,alichosema Nchimbi ni sahihi kwa upande wao kwamba si sahihi na wote ambao wataonekana wanafanya shughuli hizo,ni kwamba wanafanya makosa “ amesema Wakili Olengurumwa
“ Yeyote yule anayetaka kuingia kwenye uchaguzi ni lazima ahakikishe kwamba anapotaka kuingia kwenye uchaguzi ajiondoe kwanza kwenye NGO na kuachia wengine lakini pia asitumie kwa namna moja ama nyingine lakini pia asitumie shughuli za Asasi kufanya kampeni ndani ya Chama au pengine baadaye wakati wa uchaguzi” ameongeza Olengurumwa.
Hili ni angalizo kwa wote ,lakini pia wapo ambao wanafungua NGOs kipindi hiki na Kwenda kufanya miradi mbalimbali ambayo lengo kubwa sio kuisaidia jamii,bali ni lengo la kufanya kampeni hili ni kosa,nadhani vyote hivi vinapaswa kuangaliwa sio na vyama vya siasa pekee bali pia viongozi wote wanaohusika na mashirika , wasajili wasaidizi katika ngazi za wilaya ,kitaifa kuhakikisha tunalinda uadilifu wa Asasi hizi kipindi hiki cha uchaguzi” ameeleza Wakili Olengurumwa.
Awali Dr. Nchimbi alitoa kauli ya onyo hilo akifungua mafunzo ya watendaji wa kata na makatibu tawi wa mkoa wa Dodoma.
Waandishi wa habari wametakiwa kutumia kalamu zao vizuri na kuandika habari kwa usahihi ili kuepusha upotoshaji wa umma unaozua taharuki.
Hayo yameelezwa na Msemaji Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa Habari Maelezo, Gerson Msigwa , ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo alipozungumza na Wahariri na Wanahabari jijini Dar es Salaam Februari 19,2025.
Msigwa amesema vyombo vya habari vimekuwa na mtindo wa kuandika vichwa vya habari ambavyo vinapotosha kwa lengo la kuwavuta watu wengi kufuatilia habari, huku vikisahau kuwa vinaweza kuleta madhara kwa jamii.
Akitoa mfano kuhusu suala hilo, amezungumzia upotoshaji ambo ulitokea kuhusu Marekani kusitisha misaada ya program za UKIMWI, na kutaja kuwa vipo vyombo vya habari vilizua taharuki kwa kuandika kuwa dawa za kufubaza makali ya VVU zitaadimika hivyo kufanya baadhi ya watumiaji wa dawa hizo kuingiwa na hofu juu ya afya zao.
Msigwa amewataka wanaofanya hivyo kuacha mara moja jambo hilo kwani linapotosha jamii.
Afya za Wananchi na mifugo katika eneo la Songwe viwandani kata ya Songwe wilaya ya Mbeya mkoa wa Mbeya, zipo hatarini kutokana na kuvuta hewa chafu na utitirishwaji holela wa maji machafu kutoka kwenye kiwanda cha kuzalisha wanga cha East Africa starch Limited kilichopo katika eneo hilo.
Wakizugumza na Watetezi Tv wananchi wa eneo hilo wamedai kuwa harufu mbaya na utitirishaji maji machafu katika makazi yao vilianza tangu mwaka jana baada ya kiwanda wa hicho kuanza uzalishaji.
Wananchi kutoka eneo hilo la Songwe wameleza kuwa wamefanya jitihada kadhaa ikiwa ni pamoja na kukutana viongozi wa serikali Kijiji cha Songwe pamoja na Kiwanda hicho lakini hakuna hatua zilizochukuliwa huku wakiendelea kuteseka na harufu mbaya pamoja maji machafu kutiririka katika makazi.
Mwandishi wa Watetezi Tv amefika katika kiwanda hicho na kuelezwa na walinzi kuwa viongozi hawapo na hata walipo pigiwa simu hazikupokelewa huku Meneja wa Baraza la Taifa la hifadhi na usimizi wa mazingira NEMC Josia Mlunya amekiri kupokea malalamiko ya wananchi juu ya hali hiyo.
Wananchi hao wamesema kuwa mbali harufu mbaya lakini pia wamekuwa wakishindwa kupumua na wakati mwingine wakitema mate hovyo kutokana na changamoto za harufu hivyo wanaziomba mamlaka kuliangalia hilo ili kuweza kuwanusuru na hali hiyo.
Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa, Tundu Lissu, amesema ratiba ya uchaguzi imetungwa na watu na inaweza kubadilishwa kwa mujibu wa katiba.
Hayo ameyasema jana, Alipozungumza kwenye kipindi cha Dk.45 kinachoruswa na ITV.
Tundu Lissu amesema hayo ikiwa ni ufafanuzi kuhusu kauli mbiu ya chama hicho "NO REFORM NO ELECTION" Kwamba uchaguzi hautafanyika kama hakutakuwa na mabadiliko, Ambapo baadhi ya watu wamekuwa wakitafsiri kuwa kauli hiyo inaashiria kususia uchaguzi.
Tundu Lissu amesema chama hicho hakitasusia uchaguzi bali kama hakutakuwa na mabadiliko uchaguzi hautafanyika, na suala la kuahirisha uchaguzi linawezekana kikatiba.
Video Credit | ITV
Ili kupunguza ajali za Barabarani ambazo zimekuwa zikitokea katika maeneo mbalimbali ya miji na kuua watu kwa nyakati tofauti, huku baadhi ya ajali hizo zikihusisha magari makubwa ya mizigo (Malori) ambayo mara kadhaa yameripotiwa kugonga magari madogo ya abiria, pikipiki na watembea kwa miguu, Mamlaka ya udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imeshauriwa kuweka utaratibu utakaozuia Malori kutumia barabara za mijini nyakati za mchana na badala yake kuzitumia usiku.
Ushauri huo umetolewa na Mratibu Kitaifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) Wakili Onesmo Olengurumwa @olengurumwa2 leo Februari 17,2025 ikiwa ni siku chache tangu kutokea kwa ajali iliyoua watu takribani 3 katika eneo la Kimara Jijini Dar es salaam ambapo Lori kubwa liliparamia waendesha pikipiki na watembea kwa miguu na kusababisha vifo na majeruhi.
Olengurumwa amesema haki ya kuishi ni haki kuu na ya msingi anayostahili binadamu, hivyo ajali zinazotokea na kukatisha uhai wa watu zinakatili haki hiyo hivyo ni lazima hatua stahiki zichukuliwe ili kudhibiti ajali hizo.
"Ajali zimekuwa zikisababisha haki ya kuishi kwa Watanzania wengi, kupotea kila siku ya Mungu, na ajali zimekuwa kwa sura nyingi zinasababishwa na changamoto nyingi barabarani pengine miundombinu mibovu, uzembe wa mtu mmoja mmoja na kingine ni sisi kama Taifa tumeshindwa kupangilia vizuri matumizi mazuri ya barabara zetu". Amesema Olengurumwa.
Olengurumwa amependekeza kuwa kuna ulazima wa LATRA kupanga utaratibu utakaopunguza ajali hizo, ambapo moja ya hatua inayopaswa kuchukuliwa ni kuzuia Malori kutumia barabara za mijini wakati wa mchana, ili kuzuia ajali na foleni za barabarani zisizo za lazima lakini pia ameshauri mabasi ya abiria yasiwe na utaratibu wa kusafiri usiku kwani muda huo hakuna udhibiti stahiki wa usalama barabarani.
BAADA ya kukaa na maradhi ya macho yaliyomsababishia kutokuona kwa muda wa miaka sita bila kupata matibabu, Hassan Sijale Tendo, Mkazi wa Mtaa wa Ikhanga kata ya Iganzo Jijini Mbeya amewaangukia Watanzania na kuomba kumsaidia kiasi cha shilingi lakini saba (750,000) ili aweze kupata tiba na kuendelea na maisha yake ya utafutaji.
Akizugumza na watetezi tv akiwa nyumbani kwake mtaa wa Ikhanga, Hassan ambaye ni mwenyekiti mstaafu wa CCM Kata ya Iganjo, Jijini Mbeya, amesema kuwa hali ya upofu wa macho ilimpata wakiwa katika kikao cha kujadili hatma ya ofisi ya chama ambayo iliuzwa na kujengwa kituo cha mafuta eneo la Igawilo jijini Mbeya, na kabla ya kikao hicho alikuwa akiona kama kawaida lakini baada ya hapo akapoteza uwezo wa kuona.
Wakizugumza na watetezi tv watoto wa Hassan wamesema baada ya baba yao kupata changamoto hiyo walijaribu kuhangaika katika maeneo mbalimbali kwa ajili ya kupata tiba lakini wameshindwa kutokana na ukata wa pesa hivyo wanawaomba watanzania kiasi cha shilingi laki saba na nusu ili kumuwezesha baba yao kupata matibabu.
Unaombwa kuchangia chochote kupitia namba za Hassan Sijale Tendo;
📞+255764677594 (HASSAN SIJALE)
Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa, Tundu Antipas Lissu amesema hawatakuwa tayari kuona uchaguzi unafanyika bila mabadiliko wanayoyahitaji, hivyo wapo tayari kushinikiza mabadiliko kwa namna yoyote itakayotakiwa kufanyika.
Hayo ameyasema leo Februari 15,2025 kwenye hafla ya mapokezi ya mwenyekiti huyo iliyofanyika nyumbani kwao Ikungi mkoani Singida, ambapo amepokelewa na maelfu ya wafuasi wa chama hicho.
Tundu Lissu ameendelea kusisitiza kauli mbiu ya chama hicho "NO REFORM NO ELECTION" ambapo amesema kuwa kama chama Tawala CCM) hakitakubali kwa hiari mabadiliko ya uchaguzi basi watashurutisha mabadiliko kwa njia mbalimbali ikiwemo maandamano.
Akizungumzia mabadiliko hayo, ametaja suala la Tume huru ya uchaguzi ambayo amesema kuwa tume hiyo sio huru kwani ni tume ambayo inaundwa na Rais ambaye ni mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi (CCM) ambaye ndiye mwenye mamlaka ya kuteua watendaji wote wa tume hiyo, Mkurugenzi wa uchaguzi na wasimamizi wa uchaguzi.
Aidha Tundu Lissu ameongeza kuwa, kumekuwa na sababu zinazotolewa na chama tawala kuwa ni vigumu kufanya mabadiliko yoyote kwa sasa kwani hakuna muda wa kutosha kufanya hivyo kwa sasa mpaka uchaguzi utakapomalizika, Lissu ameikana sababu hiyo na kudai kuwa hicho sio kikwazo cha kufanya mabadiliko uchaguzi kwani katiba inaruhusu kufanya mabadiliko ya tarehe ya uchaguzi endapo kutakuwa na hali ya hatari.
Kufuatia taarifa zilizosambaa mitandaoni kuhusu serikali ya Tanzania kungia makubaliano ya na mwekezaji wa Saudi Arabia kwenye bandari ya Bagamoyo, Waziri Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji Prof. Kitila Mkumbo, amekanusha taarifa hizo na kusema kuwa si za kweli.
Akizungumza bungeni, leo Februari 14,2025, Prof. Kitilamkumbi amesema serikali haijingia mkataba na mwekezaji yoyote katika mradi wa Bagamoyo ikiwemo bandari.
"Serikali haijaingia makubaliano wala Mkataba na Mwekezaji yeyote katika mradi wa Bagamoyo nilioutaja ukiwemo wa Bandari, hivyo taarifa zinazosambaa katika mitandao ya kijamii kwamba Kampuni moja ya Saudi Arabia imepata mkataba wa uwekezaji wa kujenga na kuendesha Bandari ya Bagamoyo sio za Kweli.." amesema Prof. Kitila Mkumbo.
Jana Februari 13,2025 zilisambaa taarifa mitandaonu kuwa Saudi Arabia imepata idhinisho la kuendesha Bandari ya Bagamoyo (Tanzania) ambayo ni moja ya bandari kubwa zaidi Afrika Mashariki na kati huku ikitajwa kuwa ni katika hatua inayolenga kuimarisha biashara na uwekezaji.
Habari hiyo ilimuibua Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Wakili Mwabukusi, ambaye aliitaka serikali kutoa ufafanuzi juu ya suala hilo ili liwe wazi kwa watanzania wote.
"Kumekuwa na ripoti zinazosambaa Kuonesha kuwa Saudi Arabia, kupitia Kampuni ya Uwekezaji na Maendeleo ya Afrika ya Saudi (SADC), imetwaa umiliki na haki za uendeshaji wa Bandari ya Bagamoyo nchini Tanzania.
Taarifa hizi zilianza kusambaa baada ya kauli iliyotolewa na Hassan Al-Huwaizi, Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyabiashara wa Saudi, na zilichapishwa na vyombo vya habari kama Saudi Press Agency na Argaam. (argaam.com)
Nirai yetu kwamba serikali ifafanue kuwa, Umma ujue iwapo kweli kuna mazungumzo kati ya maafisa wa Tanzania na wawekezaji wa Saudi kuhusu jambo hili.
Ni imani yetu kwamba makubaliano yeyote yatazingatia sheria namba 5 na Namba 6 kuhudu ulinzi wa Raslimali zetu za Asili" alisema Mwabukusi.
Video ya Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe ACP Alli Kitumbo innaendelea kusambaa kwenye mitandao ya kijamii inayomuonesha akitoa wito wa kutojidhuru kwa wenza watakaoingia kwenye migogoro na kuachwa na wenza wao.
Video hii inayomuonesha akizungumza na waandiahi wa habari inaendelea kupata umaarufu katika mitandao ya kijamii ikitumika kufikisha ujumbe kwa wale watakaochwa hasa katika siku ya wapendanao ya Valentine.
Kumekuwa na matukio ya kudhuru au kujidhuru kwa baadhi ya watu ambao wametengwa au kuachwa na wenzao katika mikoa mbalimbali nchini.
Je una mtazamo wowote juu ya ujumbe huu uliotolewa na ACP ALLI KITUMBO?
Kwa miongo mingi, Afrika imekuwa mpokeaji mkubwa wa misaada kutoka kwa mataifa yaliyoendelea na taasisi za kimataifa. Ingawa misaada hii huwasilishwa kama njia ya kusaidia maendeleo, kuna mjadala kuhusu kama kweli ina nia njema au ni njia ya kunyonya rasilimali za bara hili.
Mtego wa Rasilimali
Afrika ina utajiri mkubwa wa madini, mafuta, gesi, na ardhi yenye rutuba. Hata hivyo, mikataba mingi ya uchimbaji inafaidisha makampuni ya kigeni badala ya wananchi. Mfano ni madini ya coltan kutoka DRC, ambayo yanatumika kutengeneza simu duniani, lakini wenyeji wanabaki maskini.
Mikopo Inayoua Uchumi
Nchi nyingi za Afrika hukopa fedha kutoka China, IMF, na Benki ya Dunia kwa miradi ya miundombinu. Hata hivyo, mikopo hii mara nyingi huambatana na masharti magumu, yanayoweza kusababisha mataifa haya kupoteza udhibiti wa mali zao muhimu, kama ilivyoshuhudiwa Kenya na Zambia.
Misaada Isiyo na Faida kwa Waafrika
Misaada mingi huwanufaisha watoa misaada kuliko Waafrika. Mfano, nchi za Magharibi hutoa chakula cha msaada kutoka kwa makampuni yao, badala ya kusaidia wakulima wa Afrika kuzalisha zaidi. Hali hii inachochea utegemezi badala ya kujenga uchumi imara.
Je, Afrika Inaweza Kujitegemea?
Ndiyo, lakini ni lazima ichukue hatua madhubuti:
✅ Kuimarisha uwajibikaji – Serikali ziwe wazi kuhusu mikataba ya rasilimali.
✅ Kuwekeza kwenye viwanda – Malighafi zisafishwe na kuchakatwa ndani ya Afrika.
✅ Elimu na teknolojia – Kujenga uwezo wa ndani badala ya kutegemea nje.
✅ Kushirikiana kikanda – Kuimarisha biashara kati ya nchi za Afrika.
✅ Kusimamia mikopo vyema – Kuiga mataifa kama Malaysia yaliyojijenga bila kutegemea misaada kwa kiwango kikubwa.
Hitimisho
Misaada inaweza kusaidia, lakini Afrika lazima iwe macho isigeuzwe soko au chanzo cha mali ghafi pekee. Ni wakati wa bara hili kutumia utajiri wake kwa maendeleo ya wananchi wake, si wageni!
Una maoni gani kuhusu misaada kwa Afrika? Ni msaada wa kweli au ni mtego? ⬇️
#Afrika #Misaada #Uchumi #Rasil
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu amesema mfumo wa Uchaguzi wa Tanzania umeharibiwa kiasi cha kufanya kusiwepo na uchaguzi huru na wa haki kutokana na namna mfumo huo ulivyojengwa kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambao unampa mamlaka kubwa ya uteuzi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuteua watendaji wa Tume Huru ya Uchaguzi bila kuulizwa na yeyote.
Akizungumza mbele ya wanahabari leo Februari 12,2025 jijini Dar es salaam, amesema kutokana na mfumo huo, hakuwezi kuwa na uchaguzi huru na haki kwani Rais ambaye ni mwenyekiti wa chama ndiye mdhibiti wa mfumo mzima wa uchaguzi.
"Mfumo wetu wa uchaguzi ni mfumo unaodhibitiwa na Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, na zanzibar unadhibitiwa na rais wa Zanzibar.
Rais wa Jamhuri ya muungano ndiye anayeteua Mwenyekiti wa tume, Makamu mwenyekiti wa tume, Mkuurugenzi Mkuu wa Uchaguzi na wajumbe wote wa Tume, Na anawateua bila kulazimika kushauriana na mtu yeyote yule." Amesema Lissu
Tundu Lissu amerejelea uchaguzi wa mwaka 2019/2020 ambapo amesema makosa yaliyotokea wakati ule hayawezi kurekebishwa kama hakutakuwa na mabadiliko ya mfumo wa uchaguzi, na kwa sasa chama hicho kimekuja na kauli mbiu ya "No Reform No Election" (Hakuna mabadiliko hakuna uchaguzi).
Lissu amesisitiza kuwa kauli mbiu hiyo hailengi kususia uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu, bali unalenga kutofanyika kwa uchaguzi endapo hakutakuwa na mabadiliko.
Umoja wa Ulaya (EU) unapanga kufanya mapitio makubwa ya mgao wa misaada yake ya kigeni ili kuhakikisha inalingana na maslahi yake ya kimkakati katika mazingira ya kimataifa yanayobadilika kwa kasi. Hatua hii inalenga kubadili mfumo wa msaada wa jumla na kuelekeza rasilimali kwa mataifa yenye umuhimu wa kipekee kwa EU.
Sababu Kuu za Mabadiliko
1. Mazingira Mapya ya Kisiasa
• Vita vya Ukraine vinaingia mwaka wa tatu, na EU inahitaji kuongeza bajeti yake ya ulinzi.
• Marekani, chini ya Rais Donald Trump, imebadili mkakati wake kwa kusitisha baadhi ya misaada ya kigeni na kuvunja USAID.
• Ushindani kati ya EU, Marekani, na China unaongezeka, hasa katika kuwania ushawishi kwenye mataifa yanayoendelea.
2. Msukumo wa EU Kuwa na Mkakati wa Kibiashara
• EU inataka misaada yake ilenge mataifa yanayounga mkono sera zake kimataifa badala ya kuwa msaada wa jumla.
• Kipaumbele kitawekwa kwenye upatikanaji wa malighafi muhimu, kama vile madini ya thamani yanayohitajika kwa sekta ya teknolojia.
• Mabadiliko haya pia yanahusiana na juhudi za kudhibiti uhamiaji holela kuelekea barani Ulaya.
3. Changamoto za Bajeti ya EU
• Bajeti ya EU ni takriban 1% ya GDP, lakini mahitaji yanaongezeka kutokana na:
✅ Kuongezeka kwa bajeti ya ulinzi
✅ Ufadhili wa mpango wa mabadiliko ya kijani
✅ Malipo ya deni la €30 bilioni kila mwaka kutoka mfuko wa kufufua uchumi baada ya COVID-19
Hatua Zinazofuata
Kamisheni ya Ulaya inatarajia kuwasilisha mpango wa bajeti ya miaka saba (2028-2034) ifikapo Julai 2025. Mpango huu utajumuisha:
✅ Vigezo vipya vya misaada kwa kila nchi ili kuimarisha uwajibikaji
✅ Mfuko wa ushindani kusaidia teknolojia za kimkakati
✅ Masharti ya kuheshimu utawala wa sheria kwa nchi zitakazonufaika na misaada ya EU
Mabadiliko haya yanaifanya EU kujitofautisha na Marekani chini ya Trump na kujiimarisha dhidi ya ushindani wa China, ikilenga kuwa mshirika wa kuaminika zaidi duniani.