East Africa TV

East Africa TV Official EastAfricaTV page
(865)

Umewahi kupita mara ngapi Mlima Kitonga?   /AIDS
26/01/2025

Umewahi kupita mara ngapi Mlima Kitonga?

/AIDS

Umepita mara ngapi Mlima Kitonga?   /AIDS
26/01/2025

Umepita mara ngapi Mlima Kitonga?

/AIDS

  Watu wanne wamefariki dunia na wengine 20 wamejeruhiwa katika ajali ya barabarani iliyotokea jioni ya jana Jumamosi, J...
26/01/2025

Watu wanne wamefariki dunia na wengine 20 wamejeruhiwa katika ajali ya barabarani iliyotokea jioni ya jana Jumamosi, Januari 25, 2025 eneo la Msolwa, Chalinze Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani.

Ajali hiyo imetokea kati ya saa 10 na 11 jioni ikihusisha lori na basi dogo la abiria aina ya Coaster iliyokuwa inasafirisha msiba kutoka jijini Dar es Salaam kwenda Bukoba, Mkoa wa Kagera.

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Chalinze, Allen Mlekwa amethibitisha kupokea majeruhi na miili ya waliofariki kati ya waliofariki dunia wanaume ni watatu na mwanamke mmoja.

Majeruhi ni 20 kati yao 15 walipewa rufaa kwenda Hospitali ya Tumbi Kibaha.

Miili iliyohifadhiwa ni pamoja na mwili uliokuwa ukisafirishwa, huku majeruhi hao wakiendelea kutibiwa kwenye Hospitali ya Msoga wilayani Bagamoyo.

  Kikosi maalum cha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa kushirikiana na wananchi kinaendelea na operesheni ya kuwatafuta na...
26/01/2025

Kikosi maalum cha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa kushirikiana na wananchi kinaendelea na operesheni ya kuwatafuta na kuwaokoa wavuvi katika ziwa Rukwa ambapo kufikia leo tarehe 25 Januari 2015 saa tisa mchana, miili ya wavuvi nane imepatika.

Akizungumza wakati zoezi la uokoaji likiendelea Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa akiwa ameambata na Waziri Wa Mifugo na Uvuvi, Dkt. Ashatu Kijaji, kata ya Nankanga, ameeleza kuwa kufuatia upepo mkali uliotokea mnamo tarehe 23 Januari 2025 na kuwakuta Wavuvi 550 wakiwa katika shughuli zao ambapo jitihada za awali zilifanikiwa kuwaokoa Wavuvi 540 wakiwa salama.

Bashungwa ameeleza zoezi za ukoaji linaendelea likiongozwa na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji CGF John Masunga ambae anatumia helkopta kuwasiliana na vikosi maalum vya uokoaji ambao wanashirikiana na wananchi wakiwa na jumla ya vyombo 19 huku akiwasisitiza wananchi na Watanzania kufuatilia na kuzingatia taarifa zinatolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa.

  Huyu hapa Sancheza Mapepe aliewaponza Chelsea kwene mechi ya leo.⏰FULLF-TIME⏰Man City 3-1 ChelseaNeno moja kwa Kipa Sa...
25/01/2025

Huyu hapa Sancheza Mapepe aliewaponza Chelsea kwene mechi ya leo.

⏰FULLF-TIME⏰
Man City 3-1 Chelsea

Neno moja kwa Kipa Sanchez ?

  Chelsea wameshindwa kukaza kipindi cha kwanza na kujikuta wakiruhusu goli na matokeo kuwa 1-1.⏰HALF-TIME⏰Man City 1-1 ...
25/01/2025

Chelsea wameshindwa kukaza kipindi cha kwanza na kujikuta wakiruhusu goli na matokeo kuwa 1-1.

⏰HALF-TIME⏰
Man City 1-1 Chelsea

Unadhani mechi itamalizika vipi leo?

25/01/2025

Serikali imetangaza kwamba ili kuwapunguzia wananchi adha ya foleni wakati wa mkutano wa viongozi wa Afrika unaonza keshokutwa, wageni watakuwa wakitumia njia ya mwendokasi kwenda na kurudi Uwanja wa Ndege.

Akizungumza na waandishi wa habari jioni hii, Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, alisema abiria wanaokwenda na kurudi kutoka mjini wataendelea kutumia barabara ya kawaida.

“Nchi yetu imepata bahati ya ugeni mkubwa kuanzia keshokutwa kutokana na Mkutano wa Afrika wa Masuala ya Nishati. Rais wetu Samia Suluhu Hassan ametupa heshima kubwa k**a taifa kuleta viongozi wa Afrika na Dunia kuja kwetu.

"Sasa ili kuounguza adha kwa wananchi, serikali yenu umeamua wageni watumie njia ya Mwendokasi wakitoka na kwenda Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere na wananchi waendelee kutumia barabara ya kawaida," alisema.

Katika hatua nyingine, Ulega leo amekagua maandalizi ya kimiundombinu ya mkutano huo, ikiwemo kufungwa kwa taa za mwanga barabarani ambazo zimeanza kubadili mwonekano wa jiji la Dar nyakati za usiku.

Mkutano wa Nishati wa Bara la Afrika utakutanisha viongozi wakuu wa Afrika kujadili namna ya kuongeza upatikanaji wa umeme kwa wananchi wa Afrika utafanyika kati ya Januari 27 na 28 mwaka huu.

  Wadau wanasema ifike tu mahali huyu Salah ahamishwe ligi kwa sababu anakoelekea ataifanya ligi ya EPL k**a shamba la b...
25/01/2025

Wadau wanasema ifike tu mahali huyu Salah ahamishwe ligi kwa sababu anakoelekea ataifanya ligi ya EPL k**a shamba la bibi, ambapo hii leo baada ya kufunga goli amepanda hadi nafasi ya 7 ya kuwa mfungaji bora wa muda wote EPL akiwa na magoli 176.

⏱️HALF TIME⏱️
Liverpool 3-0 Ipswich Town
Brighton 0-1 Everton
Southampton 1-2 Newcastle
Wolves 0-0 Arsenal
Bournemouth 1-0 Nottingham Forest

25/01/2025

Baadhi ya Wananchi wa kata ya Lwambi Jijini Mbeya wamedai kuugua ugonjwa wa tumbo na kuhara baada ya kutumia maji ambayo yanayodhaniwa kuchanganyika na kinyesi.

25/01/2025

Wananchi waishio Kawe Mtaa wa Makazi mapya pembezoni mwa Mto Mbezi, wameiomba Serikali kuwajengea kingo kwenye Mto huo ili kupunguza madhara ya kubomoka nyumba nyingine mvua zitakapoanza.

25/01/2025

Upandaji miti umesaidia kukuza kipato, kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kuhifadhi vyanzo vya maji katika kijiji cha Itimbo Wilayani Kilolo Mkoani Iringa.

  Kwa ushindi huu,kesho Supu wapi?FT: Yanga SC 5-0 Copco FC
25/01/2025

Kwa ushindi huu,kesho Supu wapi?

FT: Yanga SC 5-0 Copco FC

  Wakati waasi wa M23 wakisonga mbele kuelekea Goma, mji mkubwa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Marekani...
25/01/2025

Wakati waasi wa M23 wakisonga mbele kuelekea Goma, mji mkubwa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Marekani, Uingereza na Ufaransa wamewataka raia wao kuondoka eneo hilo.

Mapigano kati ya jeshi la Congo na waasi yamezusha mzozo wa kibinadamu huku juhudi za kidiplomasia kupatanisha mazungumzo kati ya viongozi wa Congo na Rwanda zimeshindwa.

DRC na Umoja wa Mataifa zinaishutumu nchi jirani ya Rwanda kwa kuchochea uasi wa miaka mitatu wa M23 kwa kutumia wanajeshi wake na silaha. Rwanda inakanusha hili.
Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na M23 walipambana nje ya Goma Ijumaa huku Uingereza, Marekani na Ufaransa zikiwataka raia kuondoka katika mji huo ulioko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, zikionya hali inaweza kuwa mbaya zaidi.

Tangu mazungumzo ya amani kushindikana, wapiganaji wa M23 wanaoungwa mkono na wanajeshi wa Rwanda wametateka maeneo mengi mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) katika wiki za hivi karibuni, na kusababisha mgogoro wa kibinadamu kuukumba mji mkuu wa jimbo hilo, ambao ni makazi ya watu wapatao milioni mbili.

 HT: Yanga SC 1-0 Copco FC (Sheikhan Ibrahim 35’)
25/01/2025



HT: Yanga SC 1-0 Copco FC (Sheikhan Ibrahim 35’)

Address

Mikocheni Light Industrial Area
Dar Es Salaam
0255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when East Africa TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to East Africa TV:

Videos

Share