Serikali imetangaza kwamba ili kuwapunguzia wananchi adha ya foleni wakati wa mkutano wa viongozi wa Afrika unaonza keshokutwa, wageni watakuwa wakitumia njia ya mwendokasi kwenda na kurudi Uwanja wa Ndege.
Akizungumza na waandishi wa habari jioni hii, Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, alisema abiria wanaokwenda na kurudi kutoka mjini wataendelea kutumia barabara ya kawaida.
“Nchi yetu imepata bahati ya ugeni mkubwa kuanzia keshokutwa kutokana na Mkutano wa Afrika wa Masuala ya Nishati. Rais wetu Samia Suluhu Hassan ametupa heshima kubwa kama taifa kuleta viongozi wa Afrika na Dunia kuja kwetu.
"Sasa ili kuounguza adha kwa wananchi, serikali yenu umeamua wageni watumie njia ya Mwendokasi wakitoka na kwenda Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere na wananchi waendelee kutumia barabara ya kawaida," alisema.
Katika hatua nyingine, Ulega leo amekagua maandalizi ya kimiundombinu ya mkutano huo, ikiwemo kufungwa kwa taa za mwanga barabarani ambazo zimeanza kubadili mwonekano wa jiji la Dar nyakati za usiku.
Mkutano wa Nishati wa Bara la Afrika utakutanisha viongozi wakuu wa Afrika kujadili namna ya kuongeza upatikanaji wa umeme kwa wananchi wa Afrika utafanyika kati ya Januari 27 na 28 mwaka huu.
#VIDEO Baadhi ya Wananchi wa kata ya Lwambi Jijini Mbeya wamedai kuugua ugonjwa wa tumbo na kuhara baada ya kutumia maji ambayo yanayodhaniwa kuchanganyika na kinyesi. #Kurasa #EastAfricaTV
#VIDEO Wananchi waishio Kawe Mtaa wa Makazi mapya pembezoni mwa Mto Mbezi, wameiomba Serikali kuwajengea kingo kwenye Mto huo ili kupunguza madhara ya kubomoka nyumba nyingine mvua zitakapoanza. #Kurasa #EastAfricaTV
#VIDEO Baadhi ya Wananchi wa kata ya Lwambi Jijini Mbeya wamedai kuugua ugonjwa wa tumbo na kuhara baada ya kutumia maji ambayo yanayodhaniwa kuchanganyika na kinyesi. #Kurasa #EastAfricaTV
#VIDEO Upandaji miti umesaidia kukuza kipato, kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kuhifadhi vyanzo vya maji katika kijiji cha Itimbo Wilayani Kilolo Mkoani Iringa. #Kurasa #EastAfricaTV
Msimamo wa kisheria na maoni ya Mwanasheria @advocate_nziku kitendo cha muimbaji Goodluck Gozbert kuchoma moto gari lake.
#Trending #GoodluckGozbert ✍ @shneida_infos
#VIDEO Serikali imetenga zaidi ya shilingi bilioni 56 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa vivuko vitano vitakavyosaidia kuondoa kero ya usafiri kwa maeneo tofauti nchini.
Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, amesema kwamba uwekezaji huo ni mkubwa kuwahi kufanyika kwa wakati mmoja katika historia ya Tanzania.
Ulega ameyasema hayo wakati alipotembelea kukagua maendeleo ya ujenzi na ukarabati wa vivuko hivyo unaofanywa na kampuni ya kizalendo ya Songoro Marine mjini Mwanza.
Kwa mujibu wa waziri huyo, vivuko vine kati ya hivyo vinatarajiwa kuanza kufanya kazi kazi kufikia mwezi Aprili mwaka huu.
#EastAfricaTv
#VIDEO Ujenzi wa daraja la kimkakati la Kigongo Busisi mkoani Mwanza unatarajiwa kukamilika mwezi ujao huku likitarajiwa kubadili hali ya kimaisha na mwonekano wa eneo la Kanda ya Ziwa.
Akizungumza katika daraja hilo jana, Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, amesema ujenzi wa daraja hilo umefikia asilimia 96 hivi sasa na kama mambo yatakwenda kama yalivyo, utafikia asilimia 100 na kukamilika kabisa kufikia mwishoni mwa mwezi ujao.
Alitumia nafasi hiyo kumpongeza Rais Samia Suluhu Hassan ambaye alisema alikuta ujenzi wa daraja hilo ukiwa umefikia kiasi cha asilimia 25 tu mwaka 2021 na sasa ametumia zaidi ya shilingi bilioni 611 kufika lilipo sasa.
Daraja hilo linatarajiwa kurahisisha usafiri katika eneo zima la kanda ya ziwa kwa kupunguza muda wa usafiri kuvuka kutoka eneo hilo kutoka saa mbili za sasa hadi dakika tano baada ya kukamilika kwa daraja.
#EastAfricaTv
#VIDEO Msanii wa nyimbo za Gospel nchini Goodluck Gozbert amaeingia kwenye trend za mitandao ya kijamii nchini mara baada ya kuonekana akichoma moto gari yake ambayo inasadikiwa alipewa miaka 3 iliyopita na nabii mkuu Geor Davie #EastAfricaTV
✍ @iboysean
#BURUDANI Muigizaji na Muimbaji @mimi_mvrs11 akijibu kuhusu #ZariTheBossLady kusema watanzania kupenda sana UMBEA😀
#FridayNightLive @tbway360 @billsepengaa
#BURUDANI Ulinzi uongezeke kwa Chuga Queen @mimi_mvrs11 asije akakimbilia South Africa sababu ni nchi ambayo anatamani kuishi hapa duniani.
#FridayNightLive @tbway360 @billsepengaa
#BURUDANI Beautful @mimi_mvrs11 amefunguka sehemu ya mwili wake ambayo anatamani kufanya Surgery.
#FridayNightLive @tbway360 @billsepengaa