Nukta Fakti

Nukta Fakti NuktaFakti ni ukurasa rasmi ulioanzishwa na tovuti ya Nukta Habari kufuatilia habari za uzushi Tanzania.

Nukta Fakti is the first Swahili fact-checking initiative in Tanzania under Nukta Africa, a fast growing digital media and technology company. We debunk misinformation and disinformation to minimise more harm to our society. We believe in improving people's lives through quality content which is free from disinformation. Share with us any doubtful information for verification and we will do it for you.

Truth stands independent of belief it is based on facts, not popularity. No matter how widely a falsehood is accepted, i...
10/02/2025

Truth stands independent of belief it is based on facts, not popularity. No matter how widely a falsehood is accepted, it doesn’t become true. In an age of misinformation, fact-checking is essential to ensure accuracy and informed decision-making. Let’s prioritize truth over trends and facts over fiction.

09/02/2025

Wizara ya Afya ya Tanzania imekanusha taarifa inayosambaa mitandaoni kuwa imetangaza bei mpya ya dawa za kupunguza makal...
06/02/2025

Wizara ya Afya ya Tanzania imekanusha taarifa inayosambaa mitandaoni kuwa imetangaza bei mpya ya dawa za kupunguza makali ya Virusi vya Ukimwi (ARV),

Taarifa hiyo inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii ikiiga muekano wa machapisho ya Millard Ayo, inasema kuwa dawa hizo kwa sasa zinauzwa Sh7,600, baada ya kusitishwa kwa msaada wa dawa hizo kutoka Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Marekani (USAID) jambo ambalo si kweli.

Huenda umekutana na taarifa inayobainisha kuwa Bilionea na mfanyabiashara, Mohammed Dewji  Dewji amezindua sarafu mpya y...
06/02/2025

Huenda umekutana na taarifa inayobainisha kuwa Bilionea na mfanyabiashara, Mohammed Dewji Dewji amezindua sarafu mpya ya kidijitali iitwayo Tanzania Coin ($Tanzania), habari hiyo si ya kweli na unapaswa kuipuuza.

Taarifa hiyo ilichapishwa na kusambaa kupitia akaunti yake ya mtandao wa X zamani Twitter jana Februari 5, 2025 ambapo sehemu ya chapisho hilo lilisomeka "Nataka kuifanya Tanzania kuwa rejea ya kupitishwa kwa cryptocurrency, k**a vile alivyofanya kwa El Salvador."

Ujumbe huo ulifuatwa na chapisho jingine likisema, "Ni heshima kuwaletea watu ubunifu huu. Mustakabali wa fedha za kidijitali unaanza hapa."

Chapisho hilo lilifuatana na kiungo cha tovuti kinachodai kuelekeza watu kwenye maelezo ya jinsi ya kuwekeza kwenye sarafu hiyo na baadae ilichapishwa video ya mtu anayefanana na Mohamed Dewji akithibitisha kuwa akaunti yake haijaibiwa na yaya ndiye aliyeanzisha sarafu hiyo.

Wakati Nukta Fakti ikiendelea kutafuta ufumbuzi wa taarifa hiyo saa mbili baadae kupitia akauti yake ya Instagram Mohammed Dewji alikanusha vikali taarifa hizo na kufichua kuwa akaunti yake ya X imedukuliwa.

Katika ujumbe wake aliandika, "Akaunti yangu ya X imevamiwa. Tafadhali puuzia posti zozote au meseji zisizo za kawaida. Tunalifanyia kazi kwa haraka ili kurejesha usalama wa akaunti. Kaeni makini."

24/10/2024

SERIKALI YAJIPANGA KUKABILIANA NA TAARIFA POTOFU KUELEKEA UCHAGUZI

27/09/2024

RAIS SAMIA: VIONGOZI KANUSHENI TAARIFAPOTOFU ZINAPOSAMBAZWA MITANDAONI

Katika baadhi ya tamaduni wanawake wenye makalio makubwa hutafsiriwa k**a warembo zaidi, hali hiyo imesababisha kuwepo n...
13/08/2024

Katika baadhi ya tamaduni wanawake wenye makalio makubwa hutafsiriwa k**a warembo zaidi, hali hiyo imesababisha kuwepo na msukumo wa baadhi ya wanawake kutaka kuongeza maumbile yao ili kuongeza mvuto.

Msukumo huo umesababisha kuenea kwa taarifa potofu zinazoelezea mbinu za kuongeza makalio ambazo baada ya uchambuzi wa kina zimebainika kuwa si kweli.

Mathalani, hivi karibuni kumekuwa na video mbalimbali katika mitandao ya kijamii k**a vile tiktok na WhatsApp inayoeleza kuwa mchanganyiko wa mafuta ya vaseline na kitunguu maji huongeza makalio kwa wanawake, jambo hilo si kweli.

Ukweli ni huu

Vaseline ni aina ya mafuta ya jeli yenye mchanganyiko wa petroli, ambayo hutumika sana kwa madhumuni mbalimbali ya kiafya ikiwemo urembo.

Vaseline ni jina la biashara linalotumika kwa bidhaa hii ilyopo chini ya Kampuni ya Unilever ya Marekani lakini jina la kisayansi ni ‘petroleum jelly’.

Kwa mujibu wa tovuti ya vaseline ambao ndio wazalishaji wa mafuta hayo, vaseline hutumika katika kuimarisha ngozi, kulainisha ngozi kavu, midomo, na kusaidia kuponya ngozi iliyojeruhiwa.

Kitunguu maji ni aina ya mboga inayojulikana kwa jina la kisayansi Allium cepa na huwa na rangi nyeupe, nyekundu au manjano na mara nyingi hutumika k**a kiungo katika mapishi mbalimbali.

Huenda umewahi kukutana na taarifa nyingi kuhusiana na njia mbalimbali za kung’arisha meno au kuyafanya yawe meupe kwa k...
10/08/2024

Huenda umewahi kukutana na taarifa nyingi kuhusiana na njia mbalimbali za kung’arisha meno au kuyafanya yawe meupe kwa kutumia viungo, chakula au matunda.

Kwa muda mrefu imekuwa ikiaminika kuwa maganda ya ndizi yanaweza kusaidia kung’arisha meno ambapo wasambazaji wa taarifa hizo kupitia mitandao ya kijamii hususan Tiktok na Youtube ambapo katika moja ya video muandaaji anasikika akisema maganda ya ndizi husaidia kuponya magonjwa ya fizi na hug’arisha meno jambo ambalo si kweli.

Nukta Fakti imezungumza na madaktari pamoja na wataalamu wa kinywa ambao wamethibitisha kuwa jambo hilo kuwa ni uvumi wakisisitiza matumizi ya maganda ya ndizi hayana mahusiano ya moja kwa moja kung’arisha meno au kuyafanya yawe meupe.

08/08/2024

Kuku wa mapambo anayeuzwa Shilingi milioni moja

Tumia viwango hivi kubadili fedha za kigeni leo Agosti 5, 2024
05/08/2024

Tumia viwango hivi kubadili fedha za kigeni leo Agosti 5, 2024

Huenda umekutana na taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii inayowataka watu kuchukua tahadhari na kutotumia vido...
29/07/2024

Huenda umekutana na taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii inayowataka watu kuchukua tahadhari na kutotumia vidonge vya Paracetamol P 500 kwa kuwa vina virusi vya Machupo, taarifa hiyo si ya kweli.

Ujumbe huo ulioanza kusambaa katika mitandao ya WhatsApp, pamoja na Facebook kuanzia Julai 26,2024 umeambatanishwa na picha inayoonesha mtu aliyetapakaa na vidonda mwilini ikiwa na maneno yanayosomeka;

“ONYO LA HARAKA! Kuwa mwangalifu usichukue paracetamol ambayo inakuja imeandikwa P 500. Ni paracetamol mpya nyeupe sana na inayong'aa, madaktari wanashauri kuwa ina virusi vya "Machupo",

Ukweli huu hapa

Nukta Fakti imefanya uchunguzi ili kujiridhisha na kuthibitisha madai hayo na kugundua yafuatayo;

Ukweli ni kwamba ujumbe huo umekuwa ukisambaa katika makundi sogozi ya WhatsApp, na sio mpya k**a wengi wanavyodhani kwa kuwa umeshatokea katika nchi mbalimbali barani Afrika, ikiwemo hapa Tanzania, pamoja na Afrika Kusini.

Aidha, Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania (TMDA) ilitoa taarifa kwa umma tarehe 21 Agosti 2019 ikikanusha taarifa hiyo ya upotoshaji. Taarifa hiyo ilibainisha kuwa hakuna virusi vyovyote vinavyoitwa Machupo, na hakuna uwezekano wa virusi kuishi kwenye vidonge vya paracetamol.

Pia, bidhaa ya P-500® (Paracetamol) iliyotengenezwa na Apex Laboratories Private Limited, India, haijasajiliwa nchini Tanzania, na TMDA haijawahi kutoa kibali cha uingizaji wa bidhaa hiyo.

Hata hivyo, Julai 27, 2024 TMDA ilitoa tena ufafanuzi mwingine kutilia mkazo taarifa iliyotoa mwaka 2019 ambapo imesisitiza dawa zenye kiambata hai cha paracetamol inayotumika kutibu homa na maumivu zilizopo katika soko nchini kwa majina mbalimbali ya kibiashara zimesajiliwa baada ya kuthibitishwa kuwa zinakidhi vigezo vya usalama, ubora na ufanisi unaotakiwa na hivyo, ni salama kwa matumizi yaliyoainishwa.

25/07/2024

Ukweli kuhusu video ya utekaji watoto Dar es Salaam

08/07/2024

Sio Kweli: Gen Z wachoma moto ndege ya Rais wa kenya

Ufuatiliaji na uchunguzi uliofanywa na Nukta Fakti umebaini kuwa hakuna ndege yoyote ya Rais wa Kenya aina ya Jet iliyochomwa moto.

Kwa msaada wa Google Reverse Image, imebainika kuwa picha na video hizo zinaonyesha eneo la Uhuru Park, katikati ya mji wa Nairobi, hivyo sio eneo ambalo kuna kiwanja cha ndege ambapo ndege inaweza kutua bali ni eneo la mapumziko.

Pia, ndege hiyo ambayo ipo katika eneo la Uhuru Park ni ndege chakavu aina ya Boeing 737 ambayo imegeuzwa kuwa mgahawa.

Picha za Google za Agosti 30, 2022, zinaonyesha ndege hiyo ikiwa katika eneo hilo.

Historia ya Uhuru Park
Bustani ya Uhuru Park ilitangazwa rasmi na kufunguliwa kwa umma na Rais wa kwanza wa Kenya, Mzee Jomo Kenyatta, tarehe 23 Mei 1969 k**a ishara ya uhuru wa nchi.

Aidha, ni makazi ya mnara wa wapigania uhuru wa Mau-Mau unaoheshimu waathiriwa wa mateso wakati wa enzi ya ukoloni.

Tofauti ya Ndege
Ndege ya Rais wa Kenya ni tofauti kabisa na ile inayoonekana kwenye video. Ndege ya Rais wa Kenya ina rangi nyeupe yenye maandishi ya "Republic of Kenya" (Jamhuri ya Kenya).

Hii inaweza kuthibitishwa kwa video mbalimbali za ndegehiyo, ikiwemo zile za mwaka 2019 na 2023.

Habari za zamani
Pia, kuna habari za picha ya ndege hiyo hiyo iliyosambaa mwaka 2012 ikisema kuwa ndege ya rais wa Kenya imetua kwa dharura.

Habari hiyo ilifanyiwa uthibitisho na PesaCheck na kubainika kuwa sio tukio la kweli.

Kwa hivyo, madai ya kuchomwa kwa ndege ya rais wa Kenya ni ya uongo na yamebainishwa k**a uzushi.

Gen Z ni kina nani?

Gen Z inasimama badala ya maneno Generation Z au Zoomer. Ambapo inarejea kuanzia kizazi kilichofuata baada ya millennia, na kinajumuisha watu waliyozaliwa kati ya mwaka 1995 na 2010.

08/07/2024

Debunked: Kenyan MP’s did not eat in the bush following bill protest

Recently there has been a video trending on X (Formerly Twitter) with men in suits eating in bushes claiming that these ...
08/07/2024

Recently there has been a video trending on X (Formerly Twitter) with men in suits eating in bushes claiming that these men are kenyan parliamentarians who run after the kenya bill protest, therefore the claims are not correct.

The video, posted by the X account , captioned: “Kenyan parliamentarians, after running for their lives ended up eating in the bush 🤣🤣🤣. Nigerian youths ooooo.

This will be benediction for Nigerian APC government, parliamentarians, low and high ministers, Ambassadors, ect ect. Kenya’s current dispensation is Just a friendly “good morning” compared to what’s looming and Awaits the so called giant of them all.”

According to Google Reverse Image Search, the video was taken during the funeral of Francis Koka, the father of Silvestry Koka, a Member of Parliament in Tanzania who died on May 22, 2024 and was buried on June 1, 2024.

One of the people shown in the video is Freeman Mbowe, a Former Member of Parliament and the Chairperson of Chadema, an opposition party in Tanzania.

Moreover, the search shows that the video was first posted on June 1, 2024, by Mbowe’s son, James Mbowe, on X and Instagram.

The posts document their participation in Mr. Koka’s funeral at Mkolowonyi Marangu, Kilimanjaro, Tanzania, in accordance with Chagga funeral traditions.

This incident highlights the importance of verifying information before sharing it online. Not everything we see on the internet is true, and fact-checking is essential.

Kwa wiki ya pili sasa nchi ya Kenya imekuwa haina utulivu kutokana na maandamano ya kupinga muswada mpya wa Sheria ya Fe...
04/07/2024

Kwa wiki ya pili sasa nchi ya Kenya imekuwa haina utulivu kutokana na maandamano ya kupinga muswada mpya wa Sheria ya Fedha nchini humo yanayoongozwa na vijana wa kizazi kipya maarufu k**a ‘Gen Z’.

Hata hivyo, watu wenye nia ovu wametumia fursa ya maandamano hayo kuandaa taarifa nyingi za uzushi ambazo zimekuwa zikisambazwa katika kurasa mbalimbali za mitandao ya kijamii k**a Facebook, Instagram, X (zamani Twitter) pamoja na TikTok.

Miongoni mwa taarifa hizo ni ile inayoendelea kusambaa hivi sasa kwenye mitandao ya X na TikTok, ikidai kuwa vijana wa kizazi kipya wanaoongoza maandamano maarufu wa Gen Z wamechoma moto ndege ya rais wa Kenya aina ya Jet.
Ukweli Huu Hapa!

Ufuatiliaji na uchunguzi uliofanywa na Nukta Fakti umebaini kuwa hakuna ndege yoyote ya Rais wa Kenya aina ya Jet iliyochomwa moto.

Kwa msaada wa Google Reverse Image, imebainika kuwa picha na video hizo zinaonyesha eneo la Uhuru Park, katikati ya mji wa Nairobi, hivyo sio eneo ambalo kuna kiwanja cha ndege ambapo ndege inaweza kutua bali ni eneo la mapumziko.

Pia, ndege hiyo ambayo ipo katika eneo la Uhuru Park ni ndege chakavu aina ya Boeing 737 ambayo imegeuzwa kuwa mgahawa.

Picha za Google za Agosti 30, 2022, zinaonyesha ndege hiyo ikiwa katika eneo hilo.

Address

4th Floor, Dabe House, Mwananyamala Road
Dar Es Salaam
76762

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Nukta Fakti posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Nukta Fakti:

Videos

Share

Category