Tujifunze biblia

Tujifunze biblia Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Tujifunze biblia, Publisher, DAR ES SALAAM, Dar es Salaam.

ukitaka kumjua MUNGU ni lazima usome biblia,unaposoma biblia unamwambia MUNGU nataka kua karibu na ww unapoanza kupata ufahamu kuhusu yeye ndipo utakapo shuhudia ukuu wa MUNGU

•Mtegemee MUNGU kwa kila Jambo• Wacha hatua zako zikaongozwe na Bwana•Kuifuata Sheria yake na maagizo yake ndiko kukabid...
30/10/2022

•Mtegemee MUNGU kwa kila Jambo
• Wacha hatua zako zikaongozwe na Bwana
•Kuifuata Sheria yake na maagizo yake ndiko kukabidhi njia zako kwake.
•Yeye ajuaye njia ikupasayo kupitia, Yeye atakaye chunga mapito Yako, maana tu Kondoo Wake naye ndiye Mchugaji wetu.
•Usidharau maagizo ya MUNGU aliye yote katika vyote

■ Ishi maisha matakatifu■Tii sheria ya BWANA■Nawe utakua mbarikiwa■Maana MUNGU huangalia Neno lake apate kulitimiza.■ hi...
03/05/2022

■ Ishi maisha matakatifu
■Tii sheria ya BWANA
■Nawe utakua mbarikiwa
■Maana MUNGU huangalia Neno lake apate kulitimiza.
■ hivyo k**a amesema ukiwa mtakatifu utabarikiwa basi ni lazima ubarikiwe maana Ahadi zake ni amina na kweli...
UBARIKIWE...

■Usihofu■MUNGU wetu ni MKUU sana tena saana■Akili yetu imejifunga kwenye mambo madogo madogo mazoe haya yanasababisha tu...
21/04/2022

■Usihofu
■MUNGU wetu ni MKUU sana tena saana
■Akili yetu imejifunga kwenye mambo madogo madogo mazoe haya yanasababisha tumfikilie MUNGU katika udogo huo huo.
■Usimuhofu adui yako, bali wewe muangale MUNGU anasemaje, hakuna awaye yeyote atakaye weza kukudhuru ukiwa uweponi kwake..
■kuwa mcha MUNGU
■muhofu MUNGU na si mwanadamu

■Kuza imani yako■ili uzidi hesabiwa haki kwa imani■ si kwa sheria bali kwa imani■ya kwamba KRISTO alikufa kwa ajili ya d...
12/04/2022

■Kuza imani yako
■ili uzidi hesabiwa haki kwa imani
■ si kwa sheria bali kwa imani
■ya kwamba KRISTO alikufa kwa ajili ya dhambi zetu,
■ya kwamba ni Bwana na mwokozi wetu
■ya kwamba tunatakaswa kwa damu iliyo mwagika pale msalabani
■chochea imani yako

●Linda wokovu wako●Shikiria kile unachokifahamu kuhusu YESU kristo, nguvu ya msalaba, nguvu ya ile damu ya mwanakondoo.●...
19/03/2022

●Linda wokovu wako
●Shikiria kile unachokifahamu kuhusu YESU kristo, nguvu ya msalaba, nguvu ya ile damu ya mwanakondoo.
●usiruhusu kupoteza icho unachojua kumuhusu MUNGU
●daima kaa kwenye uwepo wake
●daima ishike sheria yake
●daima uwe mwaminifu kwake.

10/03/2022
● heshimu na thamini uumbaji wa MUNGU● Thamini watu walio umbwa kwa sura na mfano wake, haijalishi ni mbaya au mzuri, ra...
02/03/2022

● heshimu na thamini uumbaji wa MUNGU
● Thamini watu walio umbwa kwa sura na mfano wake, haijalishi ni mbaya au mzuri, rafiki au adui, ndugu au jirani wewe wathamini na uwapende na Yeye ata hukumu wale walio wabaya kwako.
● Mungu anaposema mpende adui yako anamaanisha ata aliye mbaya kwako usimchukie wewe jukumu lako ni kuonesha upendo tu sababu ndio roho aliyo kuumbia nayo..chochote kilicho kinyume na kusudi lake jua icho hakitokani na YEYE.
● Sasa hacha kiburi cha uzima,usidharau asiye nacho wala usinyanyue mabega kwa kupata kwako riziki...
MHUBIRI 9:11
" Nikarudi, na kuona chini ya jua, ya kwamba si wenye mbio washindao katika michezo, wala si walio hodari washindao vitani, wala si wenye hekima wapatao chakula, wala si watu wa ufahamu wapatao mali, wala wenye ustadi wapatao upendeleo; lakini wakati na bahati huwapata wote."..
● Nawe usiye nacho usinung'unike wala kulaumu kwa kukosa kwako bali msifu YEYE aliye chanzo cha uhai wako, Mungu asikii lawama zako bali anasikiliza hoja.
ISAYA 41:21
"Haya, leteni maneno yenu, asema BWANA; toeni hoja zenu zenye nguvu, asema mfalme wa Yakobo."...
ZINGATIA,
UBARIKIWE SANA...

■ Mazingira yasikutishe■husiangalie mazingira ya kazi yako, uchumi wako, familia yako, kuzaliwa kwako n.k , ukadhani huw...
01/03/2022

■ Mazingira yasikutishe
■husiangalie mazingira ya kazi yako, uchumi wako, familia yako, kuzaliwa kwako n.k , ukadhani huwezi kutoka hapo na kupiga hatua. Mwamini MUNGU.
■ wana wa Israel MUNGU alipo watoa utumwani chini ya mkono wa farao hawakuamini k**a ingeliwezekana kuivuka bahari, walitazama mazingira, waliona hawawezi kuvuka bahari kwa hali waliyo kuwa nayo. walicho amini ni kuwa M***a aliwaleta hapo ili waangamie kwa mkono wa Farao
KUTOKA 14:10-12.
Lakini MUNGU tunae mtumikia ni zaidi ya hayo mazingira unayo kumbana nayo..ni zaidi ya matatizo,
Unacho paswa kufanya ni kumtumikia YEYE , shika sheria yake, tunza amri zake moyoni mwako, muabudu YEYE aliye juu ya vyote, kumcha MUNGU ndicho chanzo cha maarifa...
Naye atakupitisha hapo.....
Ukiangalia mazingira ya ulimwengu huu ulio kaa katika yule muovu yata kudanganya tu, yata ua imani yako kwa MUNGU maana ni kweli yanawezekana yakawa yana tisha lakini si kwamba hayawezekani kuyashinda.

UBARIKIWE....

IKIWA UNATAKA KUMPENDEZA MUNGU HAKIKISHA UNAZINGATIA MAMBO HAYA.■ Chukia uovu, yaani usiufanye, usiushuhudie uovu kaa ka...
18/02/2022

IKIWA UNATAKA KUMPENDEZA MUNGU HAKIKISHA UNAZINGATIA MAMBO HAYA.

■ Chukia uovu, yaani usiufanye, usiushuhudie uovu kaa katika kweli, wala usifurahie mwingine akitendewa uovu hata k**a atakua ni adui yako.

■ Acha kiburi kwa wanadamu walio umbwa kwa sura na mfano wa MUNGU, acha kiburi mbele za MUNGU yaani kuto tii sheria ya BWANA ndicho kiburi icho, unajua jambo fulani hali mpendezi MUNGU nawe unalifanya tu...icho nacho ni kiburi

1 YOHANA 2:16
"Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia."

■ Majivuno yakae mbali nawe

WAFILIPI 2:3
"msitende neno lolote kwa kushindana wala kwa majivuno, bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenzie kuwa bora kuliko nafsi yake."

■ usienende katika njia mbovu
Kaa katika wokovu wako wala usiende kushoto wala kulia

ZABURI 1:1
" Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha."

■ chunga kinywa chako kisitamke machukizo mbele za Mungu.

●Mungu anataka uwe hodari katika kutenda kwako, lolote ulilopewa kufanya basi fanya kwa ubora, iwe ni kazi , biashara n....
10/02/2022

●Mungu anataka uwe hodari katika kutenda kwako, lolote ulilopewa kufanya basi fanya kwa ubora, iwe ni kazi , biashara n.k fanya ili kuujenga ufalme wa MUNGU huku duniani, chochote ulicho pewa kufanya fanya kwa ubora
● usiiache sheria ya Bwana hata kidogo, Sheria ipo hapo kukupa muelekeo wa njia unayo paswa kwenda, sheria ni kiongozi mzuri wa kukuongoza kwenye njia anayo taka MUNGU upite.
● ukiiacha sheria(njia) aliyo kuamuru MUNGU utakua umetoka kwenye njia iliyo na kila neema na baraka za MUNGU pamoja na ulinzi wake, ivyo kushambuliwa na ibilisi itakua ni rahisi mno kuliko unavyo dhani, ibilisi hana haki ya kumuadhibu mtakatifu kwa maana mtakatifu analindwa.
● watii sana watumishi wa MUNGU,
●kuna Baraka nyingi sana zimeachiliwa na MUNGU kwa watumishi wake kwaajili yako, usiwadharau sababu umewapita elimu au umri, wewe unacho paswa kufanya ni kuwasikiliza maana MUNGU atashusha maelekezo yake kupitia wao.
● sawa unaweza sema MUNGU anazungumza na wewe sana hivyo huna haja sana ya kuwasikiliza LAKINI kuna jambo moja unapaswa kulielewa, MUNGU ataongea na wewe katika level ya familia yako, uzao wako na ukoo wako atazungumza na wewe mambo mengi sana lakini ni katika level ya watu wa nyumbani mwako,
● lakini Watumishi wake wapo zaidi ya hapo, wao wanabeba kisudi la watu wengi wakiwemo wa familia zao,yaani kusudi lao ni la watu wengi ambao wengine hawawezi hata kuwa fahamu lakini MUNGU amepitisha majibu ya matatizo yao kwa mtumishi wake.
● neema waliyo nayo ni tofauti na yule na uliyo nayo.
● watumishi wanabeba baraka zako nyingi ila kwa kuto kutii kwako utakosa mengi, kwa sababu mbali na kubeba hatma ya familia zao katika utumishi lakini pia wamebeba hatma za watu wasio wa familia zao.
● unacho paswa kufanya ni KUWAHESHIMU NA KUWASIKILIZA KILE WANASEMA maana MUNGU husema nao ili waseme na wewe pia, usiwanyooshe vidole ukawahukumu

●ishike Amri ya MUNGU ukawe na amani na haki●amani unaipata kwa MUNGU wa kweli tu sio kwa mganga wala kwa mwanadamu yeyo...
08/02/2022

●ishike Amri ya MUNGU ukawe na amani na haki
●amani unaipata kwa MUNGU wa kweli tu sio kwa mganga wala kwa mwanadamu yeyote
●Mungu ndiye amani yote
●ukiitaka amani unahitaji kuishika Amri ya MUNGU maana amani yatoka kwake
ISAYA 9:6
"Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani."........
■tunaposema tunajivunia amani nchini jua kuna watu wamejitoa kwaajili ya MUNGU hivyo neema utupata sote waovu na wasio waovu kwa maana MUNGU anaweza funika mabaya ya yetu kwaajili ya wachache walio mpendeza machoni pake

□Mkimbilie MUNGU tu□Tamani kumpendeza YEYE□Shika sheria yake ukawe salama□Ulimwengu huu ni wakupita tu□umejaa taabu nyin...
31/01/2022

□Mkimbilie MUNGU tu
□Tamani kumpendeza YEYE
□Shika sheria yake ukawe salama
□Ulimwengu huu ni wakupita tu
□umejaa taabu nyingi
□kuna uovu mwingi sababu Dunia yote inakaa katika yule mwovu.
1 YOHANA:19
"Twajua ya kuwa sisi tu wa Mungu; na dunia yote pia hukaa katika yule mwovu."
□Ndiyo maana dhambi ina nguvu kubwa ya ushawishi...hivyo jitakase muda wote.
□hatuna muda kabisa
□ni hatari pia kukaa bila ya kufanya jambo kwaajili ya ufalme wa MUNGU utadaiwa...
□fanya kitu kwa ajili ya ufalme jioneshe kuwa na ubalozi wa mbinguni huku duniani.
□ili ukawe na mwisho mwema

□MUNGU hasikii wenye dhambi.□Husipeleke maombi yako kwake ikiwa una dhambi yatakuwa ni makelele tu mbele zake.□Bali jita...
19/01/2022

□MUNGU hasikii wenye dhambi.
□Husipeleke maombi yako kwake ikiwa una dhambi yatakuwa ni makelele tu mbele zake.
□Bali jitakase kwanza uovu wako kabla ya kupeleka hoja zako kwake.
□YESU anakupenda
□husiji hukumu kwa matendo yako ya kale
□ jitakase kisha rekebisha kuanzia sasa, muoneshe kuwa umebadilika, muoneshe kwamba una faa kuaminiwa.

○washuhudiao Mbinguni wako watatu○ Watatu hawa ni 1)BABA (MUNGU BABA)2) NENO (YESU KRISTO) Soma Yohana 1:1-143) ROHO MTA...
13/01/2022


○washuhudiao Mbinguni wako watatu
○ Watatu hawa ni
1)BABA (MUNGU BABA)
2) NENO (YESU KRISTO) Soma Yohana 1:1-14
3) ROHO MTAKATIFU
○na watatu hawa ni umoja
○wote wanasifa ya UUNGU
○ni utatu unaopatana kwa umoja
○utawatofautisha kwa kazi zao duniani na mbinguni

SILAHA YA TATU : NENO LA MUNGU● Neno la MUNGU ni halisi, limebeba nguvu ya Mungu, linasiri za ufalme wa MUNGU, ● ibilisi...
23/12/2021

SILAHA YA TATU : NENO LA MUNGU
● Neno la MUNGU ni halisi, limebeba nguvu ya Mungu, linasiri za ufalme wa MUNGU,
● ibilisi utamshinda kwa neno, maana Neno limebeba kweli yote inayo shuhudiwa na Roho mtakatifu, ibilisi ni muongo maana upindisha ile kweli ili ajiweke kwenye nafasi ya MUNGU apate kuabudiwa k**a MUNGU.
● utamshinda kwa nguvu ya Neno la MUNGU.
NENO NI HALISI
WAEBRANIA 4 :12
"Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.".....
● Tunapaswa kuyaangalia maisha ya KRISTO k**a kielelezo cha mwenendo wa maisha yetu humu duniani, KRISTO ALIKUA MTENDAJI WA NENO.
● Kristo alitenda Neno, aliliishi neno na alilijua neno.
● ndio maana ilikua rahisi kumshinda ibilisi alipo mjaribu kule jangwani
unaweza soma mfano huu tunao upata katika
LUKA 4:3-4
"3 Ibilisi akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, liambie jiwe hili liwe mkate."

"4 Yesu akamjibu, Imeandikwa ya kwamba mtu hataishi kwa mkate tu."....
●Yesu alipokua akijibu kwa kusema "imeandikwa" alikua akirejea maandiko matakatifu, akiyatumia hayo kuharibu hoja za ibilisi, wala hakujibu kwa kubabaika maana alikua analijua Neno,analiishi na analitenda ilo...
● vivyo hivyo mwana wa MUNGU yakupasa kwanza ulijue Neno, uliishi neno na uwe mtendaji wa neno UTAMSHINDA ibilisi na atakuogopa maana imeandikwa

UFUNUO 12:11
" Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa."...
● SOMA SANA BIBLIA , TENGENEZA UHUSIANO MZURI NA ROHO MTAKATIFU AKUFUNULIE SIRI ILIYOPO KWENYE NENO LA MUNGU
● nawe utaliishi na kulitenda maana utajua MUNGU amekukusudia nini hivyo utajiweka mbali na utaperi wa lile joka...

Address

DAR ES SALAAM
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tujifunze biblia posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Tujifunze biblia:

Videos

Share

Category