Zamaradi TV

Zamaradi TV NEWS, ENTERTAINMENT and LIFESTYLE channel that has varieties of programs including Series, Talk Shows

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro ameongeza adhabu ya faini kutoka shilingi milioni 3 hadi ...
03/09/2024

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro
ameongeza adhabu ya faini kutoka shilingi milioni 3 hadi milioni 5 kwa msanii Seif Kisauji maarufu (Babu wa TikTok) akimtaka msanii huyo aombe msamaha hadharani kutokana na kosa la kurusha maudhui ya sanaa yanayokiuka maadili mtandaoni.

Waziri Ndumbaro ametoa uamuzi huo leo Septemba 3, 2024 Mtumba Jijini Dodoma baada ya kusikiliza rufaa ya msanii huyo ya kupinga adhabu aliyopewa na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) ya kufungiwa kujihusisha na shughuli za sanaa kwa miezi 6 pamoja na kulipa faini ya shilingi milioni 3 kutokana na kurusha mtandaoni picha za video zinazokiuka maadili.

Aidha, kufuatia rufaa hiyo, msanii Seif Kisauji amekiri kosa la kusambaza maudhui hayo na kuomba apunguziwe adhabu hatua iliyomfanya Waziri Mhe.Dkt. Damas Ndumbaro amuondolee adhabu ya kifungo cha cha miezi 6 cha kutojihusisha na shughuli za sanaa huku akimuongezea kiwango cha faini kutoka milioni 3 hadi 5.

“Sheria ya BASATA iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2019 kifungu cha 15 A inampa mamlaka Mhe. Waziri kusikiliza rufaa na kutoa maamuzi, hivyo kwa kushauriana na Naibu Waziri Mhe. Hamis Mwinjuma ambaye ndiye msimamizi wa sekta ya sanaa, nimefuta adhabu ya miezi sita aliyopewa kuanzia leo, na ninamtaka azingatie maadili katika kufanya kazi zake” amesisitiza Mhe. Ndumbaro.

Awali katika kikao hicho Naibu Waziri wa wizara hiyo, Mhe. Hamis Mwinjuma alimataka Msanii huyo, kurudi katika sanaa aliyokua akiifanya zamani ambayo ndiyo iliyomfanya jamii imtambue na kuelewa kuwa yeye ni kioo cha jamii hivyo anapaswa kufanya Sanaa inayoelimisha na kuburushisha jamii bila kuharibu mila na desturi za Kitanzania.

Kwa upande wake Msanii Seif Kisauji ameishukuru wizara kukubali rufaa yake pamoja na kuridhia msamaha na kumfungulia kufanya sanaa akiahidi kujirekebisha na kufanya sanaa zenye maadili na kuwa Balozi mzuri kwa wasanii wenzake.

Mwanaume mmoja aliyefahamika kwa jina la Damas Stephano (38), Mkazi wa Mtaa wa Mbuyuni, Kata ya Kizota, Dodoma anashikil...
03/09/2024

Mwanaume mmoja aliyefahamika kwa jina la Damas Stephano (38), Mkazi wa Mtaa wa Mbuyuni, Kata ya Kizota, Dodoma anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kumlawiti na kumbaka mtoto wake mwenye umri wa miezi sita hadi kumuua na kisha kumweka mlangoni mwa nyumba ya bibi yake.

Stephano ambaye ni baba mzazi wa mtoto huyo, anadaiwa kufanya tukio hilo jana Jumapili Septemba Mosi majira ya saa tatu usiku.

Akitoa taarifa ya tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, George Katabazi amesema mtuhumiwa amek**atwa na uchunguzi zaidi wa tukio hilo la kushangaza unaendelea.

Bodi ya Wakurugenzi ya Azam FC na Kocha Youssouph Dabo wamefikia makubaliano ya pande mbili ya kutoendelea kufanya kazi ...
03/09/2024

Bodi ya Wakurugenzi ya Azam FC na Kocha Youssouph Dabo wamefikia makubaliano ya pande mbili ya kutoendelea kufanya kazi pamoja kuanzia leo Septemba 03, 2024.

Dabo, aliyehudumu kwenye klabu hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja, anaondoka pamoja na wasaidizi wake wa benchi la ufundi aliokuja nao.

Tumewasikia kilio cheni hii ni kwa wale wa Antenna ambao walikosa kutazama baadhi ya vipindi vya nyuma sasa tumewaletea ...
02/09/2024

Tumewasikia kilio cheni hii ni kwa wale wa Antenna ambao walikosa kutazama baadhi ya vipindi vya nyuma sasa tumewaletea ratiba moya ya Marudio ya Reality zote za nyuma ambazo hamkuwahi kuziona na Ratiba yake ni hiyo kuanzia leo tarehe 2 September.

Twambie kipindi kipi ulikuwa unatamani kirudiwe na umekiona kwenye Ratiba hii!!?

Usikose kuangalia LIVE kupitia channel 413 ZAMARADI TVGRAND FINAL ZA MISS GRAND 2024 kuanzia saa 1:00 usiku moja kwa moj...
31/08/2024

Usikose kuangalia LIVE kupitia channel 413 ZAMARADI TV
GRAND FINAL ZA MISS GRAND 2024 kuanzia saa 1:00 usiku moja kwa moja kutokea Masaki WEREHOUSE ambapo warembo 15 wanawania CROWN ya Miss Grand 2024

Je? Ni nani ataibuka kidedea usiku wa leo?

Usikose kufuatilia Zamaradi tv na mitandao yetu ya kijamii kwa habari mbali mbali

Cc

Msanii  na Mzazi mwezake kwenye sherehe ya mtoto wao Henzo ambaye ametimiza miaka 2 leo.
25/08/2024

Msanii na Mzazi mwezake kwenye sherehe ya mtoto wao Henzo ambaye ametimiza miaka 2 leo.

Picha za Baba na Mama Henzo  pamoja na Mtoto wao wa katika tukio la kulishana cake. Tukio hili lipo LIVE  channel namba ...
25/08/2024

Picha za Baba na Mama Henzo pamoja na Mtoto wao wa katika tukio la kulishana cake.

Tukio hili lipo LIVE channel namba 413 kwenye antenna na Dish kwenye Kisimbuzi cha Azama Pekee.

Kesho Jumapili tarehe 25/08/2024 kuanzia saa NANE kamili mchana macho na masikio yako yaelekeze  channel namba 413 AZAM ...
24/08/2024

Kesho Jumapili tarehe 25/08/2024 kuanzia saa NANE kamili mchana macho na masikio yako yaelekeze channel namba 413 AZAM pekee kuangalia Birthday ya Henzo mtoto wa Msanii

Usikose kesho ifikapo saa 4 Kamili usiku kutazama washiriki wa  wakiingia kambini rasmi kwa ajili ya kujianda na Fainali...
21/08/2024

Usikose kesho ifikapo saa 4 Kamili usiku kutazama washiriki wa wakiingia kambini rasmi kwa ajili ya kujianda na Fainali za shindano hilo, kwa taarifa na matukio yote kuanzia kesho watakapokuwa kambini hadi siku ya Fainali kaa nasi kwenye kurasa zetu za mitandao ya kijamii na kwenye Channel yetu ta inayopataika kwenye kisimbuzi cha AZAM Pekee.

Kwa taarifa zilizotufikia na zilizothibitishwa na  mwenyewe ni kuwa Baba yake mzazi Mzee Salim Mitimingi hatuko nae tena...
21/08/2024

Kwa taarifa zilizotufikia na zilizothibitishwa na mwenyewe ni kuwa Baba yake mzazi Mzee Salim Mitimingi hatuko nae tena Duniani

Taarifa zaidi zitakujia juu ya msiba huu, tunampa pole sana Sheikh Abdulrazack pamoja na wafiwa wote, na MUNGU aiweke pema roho ya marehemu mzee wetu, Amin.

    cc  channel namba 413 AZAM!!!
16/08/2024



cc channel namba 413 AZAM!!!

Msanii wa Muziki wa kizazi kipya Mandojo amefariki Dunia jijini Dodoma leo.Taarifa ya kifo cha Msanii huyo imethibitishw...
11/08/2024

Msanii wa Muziki wa kizazi kipya Mandojo amefariki Dunia jijini Dodoma leo.

Taarifa ya kifo cha Msanii huyo imethibitishwa na rafiki yake wa karibu Msafiri L pamoja na msanii mkongwe Soggy Doggy

Kwa mujibu wa Msafiri L anasema marehemu Mandojo amefariki baada ya kupigwa na watu akidhaniwa kuwa ni mwizi usiku wa kuamkia Leo.

Tunaendelea kufuatilia zaidi Taarifa hii kwa undani Endelea kufuatilia kurasa zetu
tv

Kwa wewe ambaye hukuamgalia LIVE Shindano la   Jana basi usikose Marudio ya tukio zima ifikapo saa Moja kamili usiku nda...
10/08/2024

Kwa wewe ambaye hukuamgalia LIVE Shindano la Jana basi usikose Marudio ya tukio zima ifikapo saa Moja kamili usiku ndani ya channel namba 413 inapatikana kwenye Dishi na Anntena.

Cc

TOP SIX YA MISS CENTRAL ZONE Washiriki suta ambao wamepita kwenye mchujo usiku huu ambapo kinachofuata ni muda wa wao ku...
09/08/2024

TOP SIX YA MISS CENTRAL ZONE

Washiriki suta ambao wamepita kwenye mchujo usiku huu ambapo kinachofuata ni muda wa wao kujibu maswali na kuchaguliwa Top 5.

Tupo Live Kupitia channel namba 413 katika Dish na Anntena

Cc

Mshiriki namba 10 akituonyesha vazi lake la usiku, katika shindano hilo la Miss Central Zone.Tupo Live Kupitia  channel ...
09/08/2024

Mshiriki namba 10 akituonyesha vazi lake la usiku, katika shindano hilo la Miss Central Zone.

Tupo Live Kupitia channel namba 413 katika Dish na Anntena

Cc

Mshiriki namba 3 akituonyesha vazi lake la usiku, katika shindano hilo la Miss Central Zone.Tupo Live Kupitia  channel n...
09/08/2024

Mshiriki namba 3 akituonyesha vazi lake la usiku, katika shindano hilo la Miss Central Zone.

Tupo Live Kupitia channel namba 413 katika Dish na Anntena

Cc

Mshiriki namba 2 akituonyesha vazi lake la usiku, katika shindano hilo la Miss Central Zone.
09/08/2024

Mshiriki namba 2 akituonyesha vazi lake la usiku, katika shindano hilo la Miss Central Zone.

Muandaji wa Shinda la Miss Central Zone 2024  tayari akiwa ameshawasi kwenye tukio la kumtafuta Miss kanda ya kati usiku...
09/08/2024

Muandaji wa Shinda la Miss Central Zone 2024 tayari akiwa ameshawasi kwenye tukio la kumtafuta Miss kanda ya kati usiku huu.

Una mapa asilimia ngapi kwenye nguo yake ya leo

Tupo Live Kupitia channel namba 413 katika Dish na Anntena

Cc

Wasanii wa Bongo Flave  na  wanatarajiwa kutoa burudani leo usiku kwenye fainali kuu ya Miss Central Zone Inayoafanyika ...
09/08/2024

Wasanii wa Bongo Flave na wanatarajiwa kutoa burudani leo usiku kwenye fainali kuu ya Miss Central Zone Inayoafanyika Mkoani Dodoma katika ukumhi wa Maboye Hall kuanzia saa Moja usiku.

Tukio hili ambalo litarula LIVE kupitia channel yeu ya Zamaradi TV namba 413 kwenye Dish na Antenna

Ticket Available through Nilipe App

Tiketi zinapatikana Nilipe App

Don’t miss out on the chance to witness this spectacular event!






Usikose kuangalia LIVE kupitia channel 413 ZAMARADI TVGRAND FINAL ZA MISS CENTRAL ZONE kuanzia saa 1:00 usiku  moja kwa ...
09/08/2024

Usikose kuangalia LIVE kupitia channel 413 ZAMARADI TV
GRAND FINAL ZA MISS CENTRAL ZONE kuanzia saa 1:00 usiku moja kwa moja kutokea DODOMA ambapo warembo 15 wanawania CROWN ya Miss Central Zone Jee?ni nani ataiwakilisha KANDA YA KATI? usikose kufuatilia Zamaradi tv na mitandao yetu ya kijamii kwa habari mbali mbali

𝐌𝐈𝐒𝐒 𝐂𝐄𝐍𝐓𝐑𝐀𝐋 𝐙𝐎𝐍𝐄 𝐓𝐚𝐧𝐳𝐚𝐧𝐢𝐚 𝟐𝟎𝟐𝟒 ᴊᴏᴜʀɴᴇʏ ᴛᴏ ᴛʜᴇ ᴄʀᴏᴡɴ 𝗙𝗜𝗡𝗔𝗟 𝗖𝗢𝗠𝗣𝗘𝗧𝗜𝗧𝗜𝗢𝗡 𝗡𝗜𝗚𝗛𝗧📍 𝙼𝙰𝙱𝙴𝚈𝙾 𝙷𝙰𝙻𝙻, 𝙳𝙾𝙳𝙾𝙼𝙰📆  𝟿𝚝𝚑 𝙰𝚞𝚐𝚞𝚜𝚝 𝟸𝟶𝟸𝟺⏰ 𝟶𝟽:...
08/08/2024

𝐌𝐈𝐒𝐒 𝐂𝐄𝐍𝐓𝐑𝐀𝐋 𝐙𝐎𝐍𝐄 𝐓𝐚𝐧𝐳𝐚𝐧𝐢𝐚 𝟐𝟎𝟐𝟒 ᴊᴏᴜʀɴᴇʏ ᴛᴏ ᴛʜᴇ ᴄʀᴏᴡɴ


𝗙𝗜𝗡𝗔𝗟 𝗖𝗢𝗠𝗣𝗘𝗧𝗜𝗧𝗜𝗢𝗡 𝗡𝗜𝗚𝗛𝗧

📍 𝙼𝙰𝙱𝙴𝚈𝙾 𝙷𝙰𝙻𝙻, 𝙳𝙾𝙳𝙾𝙼𝙰

📆 𝟿𝚝𝚑 𝙰𝚞𝚐𝚞𝚜𝚝 𝟸𝟶𝟸𝟺

⏰ 𝟶𝟽: 𝟶𝟶 𝙿𝙼 | 𝙴𝙰𝚃

Tickets available .

𝓢𝓽𝓪𝔂 𝓣𝓾𝓷𝓮𝓭

Special Thanks to ours Sponsors and Partners : .esperanza






Zamaradi Tv inawatakiwa Watanzania wote siku ya Nane Nane
08/08/2024

Zamaradi Tv inawatakiwa Watanzania wote siku ya Nane Nane

Naibu Waziri Sanaa Utamaduni na Michezo Mhe Khamis Minjuma akiongozana na baadhi ya wasanii nao wapo katika treni ya ume...
01/08/2024

Naibu Waziri Sanaa Utamaduni na Michezo Mhe Khamis Minjuma akiongozana na baadhi ya wasanii nao wapo katika treni ya umeme SGR kutokea Dar kuelekea Dodoma
Ambapo leo unafanyika rasmi uzinduzi wa treni hizo ikiwa mgeni rasmi ni Mhe. Dk Samia Suluhu Hassan

Steve nyerere akiwa ameongozana na baadhi ya wasanii kutokea kundi la mama Ongea na mwanao  anasema leo mpaka kieleweke ...
01/08/2024

Steve nyerere akiwa ameongozana na baadhi ya wasanii kutokea kundi la mama Ongea na mwanao anasema leo mpaka kieleweke Dar mpaka Dodoma ni miongoni mwa wasanii ambao tayari yupo ndani ya treni ya Umeme SGR Dar es salaam - Dodoma
Ambapo leo unafanyika rasmi uzinduzi wa treni hizo ikiwa mgeni rasmi ni Mhe. Dk Samia Suluhu Hassan

Msanii Alikiba ni miongoni mwa wasanii ambao tayari yupo  ndani ya treni ya Umeme SGR Dar es salaam - Dodoma Ambapo leo ...
01/08/2024

Msanii Alikiba ni miongoni mwa wasanii ambao tayari yupo ndani ya treni ya Umeme SGR Dar es salaam - Dodoma
Ambapo leo unafanyika rasmi uzinduzi wa treni hizo ikiwa mgeni rasmi ni Mhe. Dk Samia Suluhu Hassan

Peter msechu tayari yupo  ndani ya treni ya Umeme SGR Dar es salaam - Dodoma Ambapo leo unafanyika rasmi uzinduzi wa tre...
01/08/2024

Peter msechu tayari yupo ndani ya treni ya Umeme SGR Dar es salaam - Dodoma
Ambapo leo unafanyika rasmi uzinduzi wa treni hizo ikiwa mgeni rasmi ni Mhe. Dk Samia Suluhu Hassan

Msanii luludiva tayari yupo  ndani ya treni ya Umeme SGR Dar es salaam - Dodoma Ambapo leo unafanyika rasmi uzinduzi wa ...
01/08/2024

Msanii luludiva tayari yupo ndani ya treni ya Umeme SGR Dar es salaam - Dodoma
Ambapo leo unafanyika rasmi uzinduzi wa treni hizo ikiwa mgeni rasmi ni Mhe. Dk Samia Suluhu Hassan

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia o...
29/07/2024

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia ombi la kujiuzulu nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ambaye amemwandikia barua ya kuomba kupumzika.

Katika majibu yake Mwenyekiti wa CCM amesema “Ni kweli nilipokuomba utusaidie kwa nafasi ya Makamu Mwenyekiti nilikuahidi utakaa muda mfupi k**a ulivyoomba, na kwa kweli nilipenda uendeleekutusaidia lakini kwa kuwa umeomba sana na ahadi ni deni nalazimika kwa moyo mzito kuridhia kujiuzulu kwako”

Pia Mwenyekiti wa CCM amesisitiza kuwa Chama kitaendelea kutumia uzoefu na maarifa ya Ndugu Kinana kila vitakapohitajika.
Chama Cha Mapinduzi kinamshukuru Ndugu Abdulrahman Kinana kwa mchango wake mkubwa kwa Chama chetu.

Ally Shaban Kamwe leo Julai 28, 2024 ametangaza kujiuzulu nafasi yake k**a Meneja wa idara ya Habari na Mawasiliano wa k...
28/07/2024

Ally Shaban Kamwe leo Julai 28, 2024 ametangaza kujiuzulu nafasi yake k**a Meneja wa idara ya Habari na Mawasiliano wa klabu ya Yanga Sc baada ya kuhudumu kwa kipindi cha miaka miwili kwa mafanikio tangu Septemba 25, 2022.

Akitangaza uamuzi huo kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii Kamwe amesema Mumbuizaji mzuri anatakiwa kujua ni wakati gani wa kuondoka Jukwaani akinukuu maneno ya hekima kutoka katika kinywa cha Patrick Loch Otieno Lumumba,

“Na ni Hekima hi, inanituma mbele yenu Wananchi, Mashabiki na Wanachama wa Klabu yetu pendwa, kuwaambia kuwa, Ni wakati sasa wa kijana wenu kuondoka Jukwaani.

“Nimesimama Miaka miwili juu ya hili Jukwaa, Tumeimba, Tumecheza, Tumefurahi na Alhamdulillah Tumeshinda pamoja kila pambano Lililokuja mbele yetu. Muda wangu umemalizika na Asanteni sana.

“Tutaonana tena Wakati mwingine nikiwa na kitu kizuri cha kuwaonyesha Juu ya Jukwaa.” ameandika Kamwe.

Tayari tupo Live kupitia  channel namba 413 kwenye kisimbuzi cha Azam Pekee na kwenye YouTube channel yetu. Kwa Matukio ...
26/07/2024

Tayari tupo Live kupitia channel namba 413 kwenye kisimbuzi cha Azam Pekee na kwenye YouTube channel yetu.

Kwa Matukio yanayoendekea kwenye shunghuli ya 40 ya mtoto wa na kaa nasi kwenye kurasa zetu za Mitandao ya kijamii

Address

Shabaha Street
Dar Es Salaam
255

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Zamaradi TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Zamaradi TV:

Videos

Share

Category

Nearby media companies


Other TV Channels in Dar es Salaam

Show All