Zamaradi TV

Zamaradi TV NEWS, ENTERTAINMENT and LIFESTYLE channel that has varieties of programs including Series, Talk Shows

TAARIFA: KIFO CHA MWASISI WA TAIFA LA NAMIBIA, MHESHIMIWA DK. SAM NUJOMADk. Nujoma alikuwa shujaa wa ukombozi, mpigania ...
09/02/2025

TAARIFA: KIFO CHA MWASISI WA TAIFA LA NAMIBIA, MHESHIMIWA DK. SAM NUJOMA

Dk. Nujoma alikuwa shujaa wa ukombozi, mpigania haki, na mpenda Afrika aliyeacha alama isiyofutika katika historia ya bara hili. Akiwa mpenzi na rafiki wa Tanzania, alihifadhiwa hapa wakati wa harakati za kupigania uhuru wa Namibia. Maisha yake yalikuwa ya utumishi, yakibadilisha hatima ya taifa lake na kuhamasisha vizazi kusimama kidete kwa ajili ya uhuru, usawa, na haki.

Kwa niaba ya Serikali na wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tunatoa pole zetu za dhati kwa Mheshimiwa Dk. Nangolo Mbumba, Rais wa Namibia, wananchi wa Namibia, Mama Mwanzilishi wa Taifa, Mheshimiwa Kovambo Nujoma, familia ya Dk. Nujoma, watoto wake, marafiki na wapambanaji wa SWAPO.

Pumzika kwa amani, shujaa wa Afrika.

MAJALIWA: ANWANI ZA MAKAZI KUIBADILI TANZANIA KIDIGITALIDodoma, Februari 08, 2025 – Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema ...
08/02/2025

MAJALIWA: ANWANI ZA MAKAZI KUIBADILI TANZANIA KIDIGITALI

Dodoma, Februari 08, 2025 – Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema mfumo wa anwani za makazi nchini ni hatua kubwa katika mapinduzi ya kidigitali, ambayo yataimarisha utoaji wa huduma kwa wananchi, biashara mtandao, na usalama wa taifa.

Akizungumza katika kilele cha Wiki ya Anwani za Makazi kilichofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete (JKCC) jijini Dodoma, Majaliwa ameeleza kuwa utekelezaji wa mfumo huo umefanikisha ukusanyaji wa taarifa za makazi milioni 12.3, ambazo sasa zinahifadhiwa katika Mfumo wa Kitaifa wa Anwani za Makazi (National Physical Addressing – NaPA).

“Kama wanachama wa Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa, tunaheshimu mipaka na uhuru wa kila taifa. Pia, tunawajibika kuh...
08/02/2025

“Kama wanachama wa Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa, tunaheshimu mipaka na uhuru wa kila taifa. Pia, tunawajibika kuhakikisha usalama wa raia, wanadiplomasia, na walinda amani katika nchi zetu. Kutojali maisha ya watu na kushambulia balozi na walinda amani ni kinyume na sheria za kimataifa na ni kitendo cha kikatili.”

Mgogoro huu hautaweza kusuluhishwa kwa njia za kijeshi, lazima tukatae kupiga mabomu, ni suluhu za kidiplomasia ndizo zinazohitajika, njia k**a hiyo inahitaji kushirikisha wadau mbalimbali, mtakubaliana nami kuwa mazungumzo ya amani sio udhaifu bali ni kusikilizana na kushauriana"

Tunaona gharama kubwa inayoikabili DRC, mamilioni ya watu wanahama, matishio ya vifo, watoto wanahusishwa katika vikosi vya majeshi, tunahitaji kuchukua hatua kwani usalama wa nchi hiyo unaathiri Dunia nzima na athari zake zinatakiwa zisipuuzwe"- William Ruto, Rais wa Kenya na Mwenyekiti wa EAC kwenye Mkutano wa Pamoja na Wakuu wa Nchi na Serikali wa EAC na SADC, Ikulu Dar es salaam.

RAIS SAMIA ASHIRIKI MKUTANO WA VIONGOZI WA EAC NA SADC KUJADILI USALAMA MASHARIKI MWA DRCRais wa Jamhuri ya Muungano wa ...
08/02/2025

RAIS SAMIA ASHIRIKI MKUTANO WA VIONGOZI WA EAC NA SADC KUJADILI USALAMA MASHARIKI MWA DRC

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Februari 8, 2025, ameshiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaofanyika Ikulu, Dar es Salaam.

Mkutano huo umejikita katika kujadili hali ya usalama Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), ikiwemo hatua za ushirikiano wa kikanda katika kurejesha amani na utulivu kwenye eneo hilo lenye changamoto za kiusalama.

Viongozi wa mataifa wanachama wa EAC na SADC wamesisitiza umuhimu wa mshik**ano wa kikanda katika kukabiliana na migogoro inayosababisha madhara kwa wananchi wa DRC na kutishia ustawi wa kanda nzima. Mkutano huu unatarajiwa kutoa maazimio muhimu yatakayosaidia kurejesha amani katika eneo hilo.

Aliyekuwa Mchezaji wa Real Madrid, Marcelo Viera Da Silva ametangaza kuachana na soka rasmi (amestaafu) baada ya kucheza...
06/02/2025

Aliyekuwa Mchezaji wa Real Madrid, Marcelo Viera Da Silva ametangaza kuachana na soka rasmi (amestaafu) baada ya kucheza kwa kipindi kirefu.

Marcelo alipita kwenye vila tofauti na kupata mafanikio vikiwemo.

Fluminense, Real Madrid, Olympicos, Fluminense

🏆 ×5 Champions league
🏆 ×6 La Liga
🏆 ×4 Fifa Club world cup
🏆 ×3 UEFA super cup
🏆 ×2 Copa Del Rey
🏆 × 5 Spanish super cup
🏆 × Copa Libertadores
🏆 ×1 Confederation cup

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Dkt. Sami katika sherehe za maadhimisho ya ...
05/02/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Dkt. Sami katika sherehe za maadhimisho ya Miaka 48 ya Kuzaliwa kwa CCM leo 05 Februari 2025

Matukio yote ya hapa Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodma utaendelea kuyapata kupitia kurasa za mitandao yetu ya kijamii ya

Baadhi ya Wasanii wakiwa katika Maadhimisho ya miaka 48 ya Dodoma yamejaa historia, utamaduni, na maendeleo! Hizi ni baa...
05/02/2025

Baadhi ya Wasanii wakiwa katika Maadhimisho ya miaka 48 ya Dodoma yamejaa historia, utamaduni, na maendeleo! Hizi ni baadhi ya picha zikionesha shamrashamra na matukio muhimu ya siku hii maalum.

BAADHI YA MATUKIO KATIKA PICHA YA MAADHIMISHO YA MIAKA 48 DODOMAMaadhimisho ya miaka 48 ya Dodoma yamejaa historia, utam...
05/02/2025

BAADHI YA MATUKIO KATIKA PICHA YA MAADHIMISHO YA MIAKA 48 DODOMA

Maadhimisho ya miaka 48 ya Dodoma yamejaa historia, utamaduni, na maendeleo! Hizi ni baadhi ya picha zikionesha shamrashamra na matukio muhimu ya siku hii maalum.

RASMI: Klabu ya Yanga yatangaza kuachana na kocha Sead Ramovic!Je, unadhani hii ni hatua sahihi kwa Wananchi? Nani unadh...
04/02/2025

RASMI: Klabu ya Yanga yatangaza kuachana na kocha Sead Ramovic!

Je, unadhani hii ni hatua sahihi kwa Wananchi? Nani unadhani anafaa kuchukua nafasi yake? 🟢🟡

Klabu ya Simba leo imetembelea bunge la Tanzania, ikiongozwa na menejinenti, wachezaji na benchi la ufundi. Simba itasaf...
04/02/2025

Klabu ya Simba leo imetembelea bunge la Tanzania, ikiongozwa na menejinenti, wachezaji na benchi la ufundi.

Simba itasafiri kuelekea manyara kwa ajili ya mchezo dhidi ya Fountain Gate Fc katika muendelezo wa Ligi kuu Tanzania bara.

✍️

Baada ya ushindi wa bao 4 kwa 0 dhidi ya Al Wasl, katika ligi kuu ya Saudi Arabia, nahodha wa timu hiyo na mfungaji bora...
03/02/2025

Baada ya ushindi wa bao 4 kwa 0 dhidi ya Al Wasl, katika ligi kuu ya Saudi Arabia, nahodha wa timu hiyo na mfungaji bora wa muda amefikisha goli la 923, baada ya kufunga mabao mawili kwenye mchezo huo

Yamesalia mabao 77 kufikisha mabao 1,000 katika kipindi chake Cha uchezaji wa soka la ushindani.

Je, atafikia idadi hiyo kabla ya kuachana na soka?

✍️

Marcus Rashford amejiunga na Aston Villa kwa mkopo kutoka Man United.Asilimia 75 ya mshahara unalipwa na Villa, pamoja n...
03/02/2025

Marcus Rashford amejiunga na Aston Villa kwa mkopo kutoka Man United.

Asilimia 75 ya mshahara unalipwa na Villa, pamoja na kipengele kumnunua cha £40m mwezi Juni.

Neno moja kwa mashabiki wa Man United..!

✍️

Mwanadada nyota wa muziki ulimwenguni, Queen Beyonce ametangaza ujio wa ziara ya muziki kwa mwaka 2025 yenye lengo ya ku...
02/02/2025

Mwanadada nyota wa muziki ulimwenguni, Queen Beyonce ametangaza ujio wa ziara ya muziki kwa mwaka 2025 yenye lengo ya kuendelea kutangaza Album yake ya nane COW BOY CARTER.

Queen B ametangaza ujio wa ziara hiyo kupitia chapisho aliloliweka katika mtandao wake wa Instagram ingawa bado tarehe za ziara hiyo bado hazijatangazwa.

Hii inakuja mara baada ya kuahirisha show yake Jijini Los Angeles Januari 14 mwaka huu.

Yanga Sc imepanda kileleni mwa msimamo wa Ligi soka Tanzania bara baada ya kuwafunga Kagera Sugar mabao 4 kwa bila na ku...
01/02/2025

Yanga Sc imepanda kileleni mwa msimamo wa Ligi soka Tanzania bara baada ya kuwafunga Kagera Sugar mabao 4 kwa bila na kufikisha alama 42.

Kesho ni zamu ya mnyama Simba Sc dhidi ya Tabora United.

✍️

Waandaaji wa  wametangaza mabadiliko ya tarehe za matukio muhimu kwa mwaka 2025. All Star Comedy Festival sasa Itafanyik...
31/01/2025

Waandaaji wa wametangaza mabadiliko ya tarehe za matukio muhimu kwa mwaka 2025. All Star Comedy Festival sasa Itafanyika tarehe 16 Februari 2025, huku ikisogezwa hadi 22 Februari 2025.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na The Plug, BASATA, na Bodi ya Filamu, mabadiliko haya yamelenga kuongeza muda wa upigaji kura na kuboresha maandalizi, ili kuhakikisha matukio haya yanafanyika kwa ubora wa hali ya juu.

Mashabiki wa vichekesho wanahimizwa kufuatilia akaunti rasmi ya kwa taarifa zaidi kuhusu tuzo hizi zinazotambua na kusherehekea vipaji vya wachekeshaji nchini.

Real Madrid itakutana na Man City kwenye hatua ya mtoano kufuzu Raundi ya 16 Bora Klabu Bingwa Ulaya 2024/25Feb 11/12Man...
31/01/2025

Real Madrid itakutana na Man City kwenye hatua ya mtoano kufuzu Raundi ya 16 Bora Klabu Bingwa Ulaya 2024/25

Feb 11/12
Man City vs Real Madrid

Feb 18/19
Real Madrid vs Man City

✍️

Abel Makkonen Tasfaye maarufu k**a The Weeknd ameachia album yake ya sita HURRY UP TOMORROW ambayo ina jumla ya track 22...
31/01/2025

Abel Makkonen Tasfaye maarufu k**a The Weeknd ameachia album yake ya sita HURRY UP TOMORROW ambayo ina jumla ya track 22 chini ya lebo ya XO Republic.

Album hiyo imejumuisha wasanii mbalimbali ambao wamefanikisha zoezi la zima la ukamilikaji licha ya wasanii hao kutokutajwa rasmi. Wasanii hao ni pamoja na Anitta, Florence and the machine, Travis Scott, Pl***oy Carti na Lana Del Rey huku production nzima ikisimamiwa na Travis Scott pamoja na The Weeknd mwenyewe.

Tayari album hiyo inapatikana kwenye digital platform zote za muziki, stream na enjoy muziki mzuri 🔥

Msanii Wa Nigeria “Tems” Amesitisha Show Yake Nchini Rwanda Kufuatia Mgogoro Na DR Congo. Tems Ameomba Radhi Kwa Kutanga...
31/01/2025

Msanii Wa Nigeria “Tems” Amesitisha Show Yake Nchini Rwanda Kufuatia Mgogoro Na DR Congo. Tems Ameomba Radhi Kwa Kutangaza (Promote) Show Hiyo Akidai Kuwa Hakuwa Anafahamu Chochote Kile Kinachoendelea Kati Ya Rwanda Na Congo.

“Sikufahamu Chochote kuhusu mgogoro huu. Wala Sikukusudia Kupuuzia Masuala Halisi Ya Dunia. Moyo wangu uko pamoja na wale walioathirika, na ninaomba amani.” - Tems.

Show Ya Tems ilitakiwa kufanyika Machi 22, 2025 Mjini Kigali Nchini Rwanda, Ikiwa Ni Sehemu Ya Ziara Yake Ya Dunia Ya “Born In The Wild” .

Address

Shabaha Street
Dar Es Salaam
255

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Zamaradi TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Zamaradi TV:

Videos

Share

Category