Global Publishers

Global Publishers Global Publishers & General Enterprises Limited is a registered private company dealing in publishing of weekly Swahili newspapers in Tanzania

Publishers of Swahili Weekly Newspapers, namely UWAZI, IJUMAA, CHAMPIONI, SPOTI XTRA, RISASI, AMANI and IJUMAA WIKIENDA. Own Global TV Online, +255 Global Radio, Social Media and www.globalpublishers.co.tz

Serikali ya Brazil imeilaumu Serikali ya Marekani chini ya Rais Donald Trump kutokana na kuwasafirisha wahamiaji wa  nch...
26/01/2025

Serikali ya Brazil imeilaumu Serikali ya Marekani chini ya Rais Donald Trump kutokana na kuwasafirisha wahamiaji wa nchi hiyo kuwafudisha nchini kwao huku wakiwa wamefungwa pingu na minyororo na kueleza kuwa kitendo hicho siyo cha kibinadamu.

Rais Luiz Inacio Lula da Silva amesema kitendo hicho kimewakasirisha kwa sababu ni manyanyaso kwa raia wa Brazil na kinyume cha haki za binadamu.

Juzi Ijumaa, Januari 24, 2025, raia 88 wa Brazil walirejeshwa kwao kufuatia amri ya Rais Donald Trump ya kutaka wahamiaji wote kurudi kwenye nchi zao.

Waziri wa Sheria wa Brazil, Ricardo Lewandowski alitoa tamko Ijumaa kuwa ndege iliyowabeba wahamiaji hao, ililazimika kutua kwa dharura kwenye Uwanja wa Manaus nchini Brazil ambapo ndipo walipobaini kwamba wahamiaji hao walikuwa wamefungwa pingu ambapo ilibidi Jeshi la Polisi la Brazil liingilie kati.

Baada ya polisi kuingilia kati, ndipo wahamiaji hao walipofunguliwa pingu na kubadilishiwa ndege kisha kusafirishwa mpaka Uwanja wa Ndege wa Belo Hotizonte kisha kila mmoja kusafirishwa kurudi kwao.

26/01/2025

MJAMZITO anaweza kupata vidonda vya tumbo kabla au baada ya ujauzito. Umakini unahitajika sana katika kumchunguza mama mjamzito ili kuelewa nini kitakuwa ndiyo chanzo cha vidonda vya tumbo kwake. Mwanamke ambaye ulikuwa unaumwa vidonda vya tumbo hat

26/01/2025

Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Dkt. Akinwumi Adesina, amewasili nchini kwa ajili ya kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Nishati, utakaofanyika tarehe 27 hadi 28 Januari 2025 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha J

26/01/2025

 Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, amesema Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi inachukua hatua za haraka kushughulikia msongamano wa magari kwenye Barabara Kuu kutoka Mwanza Mjini hadi Usagara kwa kuijenga kwa njia nne.Ulega amesema hayo mkoani Mw

26/01/2025

UJENZI wa daraja la kimkakati la Kigongo Busisi mkoani Mwanza unatarajiwa kukamilika mwezi ujao huku likitarajiwa kubadili hali ya kimaisha na mwonekano wa eneo la Kanda ya Ziwa.Akizungumza katika daraja hilo jana, Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, a

26/01/2025

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Polisi Dar es Salaam imetangaza kuwa Barabara tisa Jijini Dar es Salaam, zimefungwa kwa siku sita kuanzia Januari 25 hadi Januari 30, 2025 ili kupisha misafara ya viongozi wanaokuja kutoka nchi mbalimbali kuhudhuria mk

26/01/2025

Nafasi za kazi kila siku Tanzania, Serikalini, Makampuni na Taasisi mbalimbali tembelea website yetu ya Global Publishers muda wote bonyeza hapa Publishers muda wote bonyeza hapa

Wananchi wa Kitongoji cha Tengwe, Kijiji cha Manga kilichopo Kata ya Mkata, wamekumbwa na changamoto ya kukosa umeme kwa...
25/01/2025

Wananchi wa Kitongoji cha Tengwe, Kijiji cha Manga kilichopo Kata ya Mkata, wamekumbwa na changamoto ya kukosa umeme kwa siku mbili mfululizo kufuatia mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali, ambayo ilisababisha kuanguka kwa nguzo 14 za umeme.

Akizungumza na vyombo vya habari, Meneja wa TANESCO Wilaya ya Handeni, Mwalimu M***a Chowo, amesema jitihada za kurekebisha miundombinu hiyo zinaendelea.

Aidha, aliwahakikishia wananchi kuwa tatizo hilo litamalizika hivi karibuni ili kurejesha huduma ya umeme katika maeneo husika.

🔴 Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.

Waziri wa Afya, Jenista Mhagama leo Januari 25, 2025 amekutana na ujumbe kutoka Kituo cha Kuratibu na Kuzuia Magonjwa (C...
25/01/2025

Waziri wa Afya, Jenista Mhagama leo Januari 25, 2025 amekutana na ujumbe kutoka Kituo cha Kuratibu na Kuzuia Magonjwa (Centre for Disease Control na Prevention- CDC) Kanda ya Afrika Mashariki, ukiongozwa na Mkurugenzi wa Kanda Afrika Dkt. Lucy Mazyanga na kujadili namna ya kufanya kazi kwa karibu na timu ya ufundi nchini Tanzania ili kubaini maeneo ya kipaumbele ambayo yanaweza kuungwa mkono na Afrika CDC.

Kikao hicho kimefanyika katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es Salaam kufuatia tamko la hivi karibuni la uwepo wa Mlipuko wa Ugonjwa wa Virusi vya Marburg mkoani Kagera Januari 20, 2025.

Winga wa Manchester United, Anthony Matheus dos Santos ametimkia nchini Hispania ambako anaenda kujiunga na Real Betis k...
25/01/2025

Winga wa Manchester United, Anthony Matheus dos Santos ametimkia nchini Hispania ambako anaenda kujiunga na Real Betis kwa mkopo baada ya kutokuwa na wakati mzuri Old Trafford.

Antony amewasili nchini Hispania ambako anatarajiwa kukamilisha hatua za mwisho kabla ya kuanza kucheza katika Ligi ya Hispania, La Liga ambapo inaelezwa kuwa klabu hiyo imekubali kuwa inamlipa mshahara wake wa pauni 200,000 kwa wiki.

Anthony alijiunga na Manchester United akitokea Ajax kwa dau la pauni milioni 86 mwaka 2022.

25/01/2025

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, leo Januari 25, 2025 amesema kuwa Tanzania inazalisha umeme megawati 3,410 zaidi ya mahitaji ya kawaida ikilinganishwa na matumizi ya megawati 1

Mapambano makali yameshuhudiwa usiku wa kuamkia leo, Jumamosi ya Januari 25, 2025 kati ya majeshi ya Jamhuri ya Kidemokr...
25/01/2025

Mapambano makali yameshuhudiwa usiku wa kuamkia leo, Jumamosi ya Januari 25, 2025 kati ya majeshi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo dhidi ya waasi wa M23 waliokuwa wakitaka kuuteka Mji wa Goma.

Hapo jana, Januari 24, 2025 waasi wa M23 walitangaza nia yao ya kuushikilia Mji wa Goma wenye wakazi zaidi ya milioni 1 ambapo usiku walianza mashambulizi lakini Jeshi la DR Congo likapambana nao usiku kucha na kufanikiwa kuwazuia.

Maafisa wa Jeshi la Congo wameeleza kwamba walijipanga kikamilifu wakiwa na silaha nzito na kufanikiwa kuwasambaratisha M23 kabla hawajaingia kwenye mji huo.

Milio ya risasi na makombora ilisikika usiku kucha lakini kulipopambazuka, hali ya utulivu ilionekana kurejea na wananchi kuonekana wakiendelea na shughuli zao, japo kwa uchache tofauti na siku nyingine.

Mapambano ya mara kwa mara yanazidi kushamiri tangu Januari ilipoanza, hasa maeneo ya Mashariki yenye utajiri mkubwa wa madini.

Klabu ya Yanga imepata ushindi mnono wa magoli 5-0 dhidi ya Copco FC katika mchezo wa CRDB Federation Cup ambao umemaliz...
25/01/2025

Klabu ya Yanga imepata ushindi mnono wa magoli 5-0 dhidi ya Copco FC katika mchezo wa CRDB Federation Cup ambao umemalizika katika Dimba la KMC Complex Mwenge jijini Dar es Salaam.

Yanga imepata ushindi huo katika mchezo wake wa kwanza tangu ilipotolewa kwenye hatua ya makundi katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika.

HT|   Young Africans SC 1-0 Copco FC 🔴 Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika k...
25/01/2025

HT|

Young Africans SC 1-0 Copco FC

🔴 Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.



Kundi la wanamgambo wa Hamas leo, Jumamosi, limewaachia huru wanajeshi wanne wa k**e wa Israel kwa kushirikiana na Shiri...
25/01/2025

Kundi la wanamgambo wa Hamas leo, Jumamosi, limewaachia huru wanajeshi wanne wa k**e wa Israel kwa kushirikiana na Shirika la Msalaba Mwekundu, katika mpango wa kubadilishana wafungwa 200 wa Kipalestina waliokuwa gerezani nchini Israel.

Hii ni mara ya pili mabadilishano haya kufanyika tangu kutekelezwa kwa usitishaji wa vita wiki iliyopita, hali iliyositisha mapigano huko Gaza kwa angalau wiki sita. Wanamgambo wa Hamas waliwataja wanajeshi hao kuwa ni Karina Ariev, Daniella Gilboa, Naama Levy, na Liri Alba.

Wanajeshi hao walikuwa wakishikiliwa kwa kipindi cha miezi 15 kabla ya kuachiwa huru. Walionekana wakiwa wamevalia sare za kijeshi za Israel na kuwapungia mkono umati wa watu walipowasili.

Uachiliaji huu umetafsiriwa k**a hatua chanya inayolenga kuimarisha usitishaji wa vita na kuweka msingi wa mazungumzo ya amani ya kudumu kati ya Israel na Palestina.

🔴 Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.


HF|   Young Africans SC 1-0 Copco FC 🔴 Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika k...
25/01/2025

HF|

Young Africans SC 1-0 Copco FC

🔴 Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.



Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa ameeleza kuwa Kikosi maalum cha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa Ku...
25/01/2025

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa ameeleza kuwa Kikosi maalum cha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa Kushirikiana na Wananchi kinaendelea na Operesheni ya kuwatafuta na kuwaokoa Wavuvi katika Ziwa Rukwa ambapo kufikia leo tarehe 25 Januari 2015 saa tisa mchana, miili ya Wavuvi nane imepatika.

Bashungwa akiwa ameambata na Waziri Wa Mifugo na Uvuvi, Dkt. Ashatu Kijaji, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Edwin Mhede kutoa pole kwa Wananchi wa Nankanga, ameeleza kuwa kufuatia upepo mkali uliotokea mnamo tarehe 23 Januari 2025 na kuwakuta Wavuvi 550 wakiwa katika shughuli zao ambapo jitiada za awali zilifanikiwa kuwaokoa Wavuvi 540 wakiwa salama.

“Kwa taarifa tulizozipata sasa, pamoja na jitihada nzuri za mafanikio tuliyopata ya kuokoa ndugu zetu 540 ambao tumewaokoa kutoa ziwani kutokana na takwimu tulizokuwa nazo jana, lakini bahati mbaya kwa taarifa nilizo nazo sasa kutoka kwa wanaonendelea ukoaji ziwani tumewapoteza ndugu zetu saba” ameeleza Bashungwa saa sita mchana.

Bashungwa ameeleza zoezi za ukoaji linaendelea likiongozwa na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji CGF John Masunga ambae anatumia helkopta kuwasiliana Vikosi maalum vya uokoaji ambao wanashirikiana na Wananchi ambao wana jumla ya vyombo 19.

Bashungwa ametoa wito kwa Wananchi na Watanzania kufuatilia na kuzingatia taarifa zinatolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa kwa sababu Rais, Dkt. Samia ameiwezesha mamlaka ya Hali ya Hewa kuwa na vifaa vya kisasa vinavyotoa taarifa za uhakika kwa wakati.

Kwa upande wake, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, CGF John Masunga ameeleza kuwa Oparesheni ya Ukoaji itaendelea vizuri kwa kuhakikisha wavuvi wote waliokuwa ziwani wanapatikana wakiwa hai au kupata miili yao.

Address

P. O. Box 7534
Dar Es Salaam
255

Opening Hours

Monday 09:00 - 19:00

Telephone

+255719401968

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Global Publishers posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Global Publishers:

Videos

Share

HAKUNA KILICHO BORA K**A KUNYWA MAZIWA NIYAPENDAYO

Ongeza cowbell, punguza matatizo, watoto uwa na furaha zaidi baada ya kunywa maziwa Bora ya cowbell. Maziwa Bora yenye mafuta yatokanayo na mimea. Sisitiza Cowbell 1kg , kwa matumizi ya familia yako. Ni wajibu wetu kukupatia ufahamu katika maswala mbalimbali, tuunge mkono kwa kunywa maziwa Bora ya @cowbelltanzania.