Sport STAR TV

FOUNTAIN GATE FOOTBALL CLUB WALIFANYA UZEMBE.Simba sports club waliwahi kufanya hivyo wakati wanacheza na Azam football ...
06/02/2025

FOUNTAIN GATE FOOTBALL CLUB WALIFANYA UZEMBE.

Simba sports club waliwahi kufanya hivyo wakati wanacheza na Azam football club pale Songea, walipokutana na Young Africans sports club wachezaji wa Yanga ilikua kila ikitokea faulo kwanza wanashika mpira mkononi mpaka mwamuzi aweke ukuta.

Simba sports club toka kipindi cha kwanza walikua hawampi nafasi mwamuzi Abel William toka Arusha ya kufanya maamuzi yake baada ya faulo kutokea kuna muda ilitokea faulo Abel William akatoa njano wakati anataka kuandika ili kuweka kumbukumbu zake Simba wakaanza haraka sana.

Nini walitakiwa kufanya Fountain Gate football club..?

Baada ya faulo kutokea alitakiwa mchezaji mmoja akasimame mbele ya mpira eneo la faulo ili kumfanya mwamuzi Abel William awaamuru wakapange ukuta wao lakini hawakufanya hivyo Simba wakaanza haraka k**a kawaida yao na kuwaadhibu kirahisi sana.

Mwamuzi Abel William aliwahi kuvurunda katika mchezo wa Lipuli na Ruvu Shooting msimu wa 2020 ikapelekea Afisa habari wa wakati huo Masau Bwire akalalamika sana siku hiyo.

Kuna namna wachezaji mnapaswa kuwa wajanja mnapokutana na timu ambayo wachezaji wake ni wajanja wajanja sana.

Cosmasy William Choga | Sport STAR TV

Klabu ya Yanga imemtangaza kocha Miloud Hamdi raia wa Algeria na Ufaransa kuwa kocha mkuu wao mpya akichukua nafasi ya S...
04/02/2025

Klabu ya Yanga imemtangaza kocha Miloud Hamdi raia wa Algeria na Ufaransa kuwa kocha mkuu wao mpya akichukua nafasi ya Sead Ramovic ambae anaondoka.

Miloud Hamdi alikua kocha mkuu wa Singida Black Stars ya Singida pia amewahi kuzifundisha timu za CS Constantine, USM Alger, JS Kabylie zote za Algeria na RS Berkane ya Morocco.

Sport STAR TV habari

PHILIP MULRYNE KUTOKA MCHEZAJI HADI PADRE.Philip Mulryne kabla ya kuwa padre alikuwa mwanasoka wa ligi kuu ya England. A...
04/02/2025

PHILIP MULRYNE KUTOKA MCHEZAJI HADI PADRE.

Philip Mulryne kabla ya kuwa padre alikuwa mwanasoka wa ligi kuu ya England. Alicheza Norwich City FC na Manchester FC. Alizaliwa mwaka 1978 kwao Ireland.

Baada ya maisha ya soka, Philip alianza masomo ya Seminari huko Ireland kwa kusoma Falsafa miaka miwili, kisha kwenda Gregorian University, Italia, kuongeza maarifa juu ya maisha ya upadre kwa ujumla.

Alijiunga na Shirika la Dominican Order (OP: Ordo Praedicatorum) hukohuko Italia na mwaka 2016 akawa Shemasi. Kipindi cha matazamio kabla ya kuwa padre rasmi. Mwaka 2017 akawa padre na kuachana na maisha ya soka k**a ilivyo kwa mwanasoka wa zamani wa Ufaransa, FLORENT MALOUDA kuamua kuingia jeshini huko kwao French Guyana baada ya maisha ya soka.

Chaguo lako, utunze!
____________________
Kizito Mpangala, Jalimu.

Sport STAR TV Kizito Mpangala

"Bosi wa Kengold alinipigia simu akaniambia nataka uje unisaidie kubakisha timu ligi kuu, sijapona vizuri lakini kidogo ...
04/02/2025

"Bosi wa Kengold alinipigia simu akaniambia nataka uje unisaidie kubakisha timu ligi kuu, sijapona vizuri lakini kidogo kidogo nitakua sawa.

K**a bosi akikubali kuniongeza mkataba hata k**a timu imeshuka mimi nipo tayari kucheza daraja la kwanza kwani zote ni ligi. Kabla nilianza kucheza madaraja ya chini". Bernard Morrison mchezaji wa Kengold.

Sport STAR TV habari.

Usajili wa moto moto kutoka masaa matano tu yaliyopita ni Mathys Tel amejiunga na Tottenham Hotspur  akitokea Bayern Mun...
04/02/2025

Usajili wa moto moto kutoka masaa matano tu yaliyopita ni Mathys Tel amejiunga na Tottenham Hotspur akitokea Bayern Munich ya Germany πŸ‡©πŸ‡ͺ. Mchakato mzima umesukwa na nyota wa zamani Harry Kane.

Good morning Sport STAR TV fans

"Mimi binafsi nilimuelewa sana Mwanafa pale aliposema tuache kuwadekeza wachezaji wetu, ukikaa na kufatilia makipa wetu ...
03/02/2025

"Mimi binafsi nilimuelewa sana Mwanafa pale aliposema tuache kuwadekeza wachezaji wetu, ukikaa na kufatilia makipa wetu kila msimu unaona wanarudi katika msimu mpya k**a ambavyo walimaliza.

Huoni wakionyesha ushawishi wa kusema tuzuie makipa hawa wa kigeni ambao wanakuja na kuonyesha uwezo mkubwa katika ligi yetu na kimataifa pia, hivyo naweza kusema sioni sababu ya msingi kutaka makipa wa kigeni wasiwepo nchini kwetu". Cosmasy William Choga

Sport STAR TV habari

"Sisi Young Africans sports club tunajiandaa kucheza na Kengold football club sio Bernard Morrison, muhimu kwetu tunacho...
03/02/2025

"Sisi Young Africans sports club tunajiandaa kucheza na Kengold football club sio Bernard Morrison, muhimu kwetu tunachoangalia ni alama tatu ". Ally Kamwe afisa habari wa Young Africans Sports club.

Una nyongeza yoyote...?

Sport STAR TV habari

"Sioni cha kusema Christina Mwagala amepozwa na mdomo hapana, kiuhalisia ukiitazama Tabora United ilivyo ana haki ya kus...
03/02/2025

"Sioni cha kusema Christina Mwagala amepozwa na mdomo hapana, kiuhalisia ukiitazama Tabora United ilivyo ana haki ya kusema yote anayoweza kusema ina watu haswa shida ni kuwa imekutanana na nani hapo ndio tatizo

Tabora United kwa timu za daraja la kati watasumbua sana sio ajabu kwao wakimaliza nafasi nne za juu katika ligi. Wachezaji wa Tabora United wana uwezo mkubwa kuanzia nyuma". Cosmasy William Choga

Sport STAR TV habari.

Rasmi Seleman Mwalimu ameuzwa kinako klabu ya Wydad Casablanca ya Morocco πŸ‡²πŸ‡¦ akitokea Singida Black Stars, kwenye ligi y...
31/01/2025

Rasmi Seleman Mwalimu ameuzwa kinako klabu ya Wydad Casablanca ya Morocco πŸ‡²πŸ‡¦ akitokea Singida Black Stars, kwenye ligi ya Tanzania alikua katika kikosi cha Fountain Gate football club katika mzunguko wa kwanza.

Katika makubaliano baina ya Singida Black Stars na Wydad Casablanca ikiwa Selemani atauzwa kwenda klabu nyingine Singida Black Stars itapata asilimia kumi ya mauzo yake.

Yapi maoni yako..?

Tanzania yapewa Nigeria πŸ‡³πŸ‡¬, Tunisia πŸ‡ΉπŸ‡³ na Uganda kunako Afcon. Je Tanzania itavuna alama ngapi katika mataifa hayo..?
27/01/2025

Tanzania yapewa Nigeria πŸ‡³πŸ‡¬, Tunisia πŸ‡ΉπŸ‡³ na Uganda kunako Afcon. Je Tanzania itavuna alama ngapi katika mataifa hayo..?

The   Last 16 draw will take place on Wednesday at 18:00.Teams qualified so far: βœ… Marumo Gallantsβœ… Chippa Unitedβœ… Durba...
27/01/2025

The Last 16 draw will take place on Wednesday at 18:00.

Teams qualified so far:
βœ… Marumo Gallants
βœ… Chippa United
βœ… Durban City
βœ… Baroka
βœ… Cape Town Spurs
βœ… Mamelodi Sundowns
βœ… Orlando Pirates
βœ… Mpheni Home Defenders
βœ… Polokwane City
βœ… Kaizer Chiefs

BREAKINGKwa mjibu wa Eric Ndagijimana mwandishi wa habari za michezo nchini Rwamda ameripoti Kocha Mkuu wa Kaizer Chiefs...
27/01/2025

BREAKING

Kwa mjibu wa Eric Ndagijimana mwandishi wa habari za michezo nchini Rwamda ameripoti Kocha Mkuu wa Kaizer Chiefs ya South America Africa ,Nasreddine Nabi πŸ‡ΉπŸ‡³ anahitaji huduma ya beki wa kushoto wa klabu ya Simba SC πŸ‡ΉπŸ‡Ώ Nahodha, πŸ‡ΉπŸ‡ΏMohamed Husseini.

Imeelezwa Nabii πŸ‡ΉπŸ‡³ alimtaka kwenye dirisha hili la usajili.

Sport STAR TV

"Iringa kuwa na timu inawezekana lakini uwezekano huo ni lazima iwe ya mtu binafsi k**a Azam football club sio kuwa chin...
20/01/2025

"Iringa kuwa na timu inawezekana lakini uwezekano huo ni lazima iwe ya mtu binafsi k**a Azam football club sio kuwa chini ya wanachama k**a ilivyokua kwa timu zilizopoteana". Cosmasy William Choga

Sport STAR TV

Cosmasy William Choga  kupitia ukurasa wake wa Facebook amehoji swali hili huku akimtania mtangazaji Nazareth Upete soma...
20/01/2025

Cosmasy William Choga kupitia ukurasa wake wa Facebook amehoji swali hili huku akimtania mtangazaji Nazareth Upete soma kisha shiriki kutoa maoni.

"Egypt πŸ‡ͺπŸ‡¬ sijui waliwakosea nini South Africa πŸ‡ΏπŸ‡¦ linapokuja suala la mpira wa miguu, mara zote wanapenda kuwanyanyasa. Nazareth Upete ombeni msamaha." Ameandika.

Unadhani Egypt πŸ‡ͺπŸ‡¬ huwa inakwama wapi kwa timu za South Africa..?

Mwamuzi  kutoka Tanzania Ahmed arajiga ndio alikua  Pilato wa mchezo wa kombe la Shirikisho kati Ya RS Berkane dhidi ya ...
20/01/2025

Mwamuzi kutoka Tanzania Ahmed arajiga ndio alikua Pilato wa mchezo wa kombe la Shirikisho kati Ya RS Berkane dhidi ya Stellenbosch

Ulionaje uwezo wake...??

I've just reached 20K followers! Thank you for continuing support. I could never have made it without each and every one...
20/01/2025

I've just reached 20K followers! Thank you for continuing support. I could never have made it without each and every one of you. πŸ™πŸ€—πŸŽ‰

Ibrahim Bacca ameingia kambani mara mbili Yanga ikichapa Tanzania Prisons nne na sasa amefunga magoli manne msimu huu.At...
22/12/2024

Ibrahim Bacca ameingia kambani mara mbili Yanga ikichapa Tanzania Prisons nne na sasa amefunga magoli manne msimu huu.

Atafikisha mabao mangapi..?

Abdallah Mwinyimkuu mwamuzi wa mechi ya leo Young Africans Sports club vs Tanzania Prisons ya Mbeya. Unampa asilimia nga...
22/12/2024

Abdallah Mwinyimkuu mwamuzi wa mechi ya leo Young Africans Sports club vs Tanzania Prisons ya Mbeya. Unampa asilimia ngapi za ufanisi kazini hii leo..?

Sport STAR TV

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sport STAR TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sport STAR TV:

Videos

Share

Category