Dira Digital Tanzania

Dira Digital Tanzania Official page of Dira TV

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk Emmanuel Nchimbi amesema urafiki kati ya CCM na Prosperity Party, chama taw...
01/02/2025

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk Emmanuel Nchimbi amesema urafiki kati ya CCM na Prosperity Party, chama tawala cha Ethiopia, ni hatua muhimu katika kuboresha na kuimarisha uhusiano wa nchi hizo mbili, pamoja na watu wake.

Dk Nchimbi amesema ushirikiano mzuri kati ya Tanzania na Ethiopia umebebwa kwenye misingi imara ya itikadi za kisiasa iliyowekwa na waasisi wa nchi hizo mbili, akitoa wito uongozi wa kizazi cha sasa unawajibika kuimarisha zaidi kwa ajili ya manufaa ya kiuchumi ya wananchi wa pande zote.

Amesema hayo alipokuwa akitoa salamu za CCM kwenye Mkutano Mkuu wa Chama cha PP, uliofanyika mjini Addis Ababa, jana Ijumaa Januari 31, 2025, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi nchini Ethiopia.

“Kwa niaba ya Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, tunawapongeza sana wenzetu wa Prosperity Party, chini ya uongozi wa Rais wa chama, ambaye pia ni Waziri Mkuu wa Ethiopia, Abiy Ahmed.
“Uongozi wake madhubuti umekuwa mojawapo ya chachu na nguzo imara kw

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Februari 01, 2025 ameshiriki katika mazoezi ya pamoja kwenye Tamasha la Michezo la Bunge...
01/02/2025

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Februari 01, 2025 ameshiriki katika mazoezi ya pamoja kwenye Tamasha la Michezo la Bunge Bonanza, lililofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya John Merlin jijini Dodoma.

GEITA: WANANCHI wilayani Chato mkoani Geita wamejitokeza kumchangia Rais Samia Suluhu Hassan kiasi cha Sh milioni 1.4 kw...
01/02/2025

GEITA: WANANCHI wilayani Chato mkoani Geita wamejitokeza kumchangia Rais Samia Suluhu Hassan kiasi cha Sh milioni 1.4 kwa ajili ya kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya uraisi katika uchaguzi mkuu mwaka 2025.

Mchango huo umefanyika katika hafla maalum iliyoandaliwa na Kamati ya Amani ya Wilaya ya Chato inayoundwa na viongozi wa dini mbalimbali kwa ajili ya kuliombea taifa dhidi ya ugonjwa wa Marburg.

Ikumbukwe kuwa hivi karibuni serikali ya Tanzania ilithibitisha kuwepo kwa ugonjwa wa Murburg wilayani Biharamulo mkoani Kagera ambapo ni jirani na Chato.

Katibu wa NEC Itikadi Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa Ndugu CPA Amos Makalla amesema Zanzibar kunajengwa shule au jina ji...
31/01/2025

Katibu wa NEC Itikadi Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa Ndugu CPA Amos Makalla amesema Zanzibar kunajengwa shule au jina jingine Skuli nzuri za kisasa ambazo zinatumia gharama nafuu lakini zinatija kwani ni mfumo wa Ghorofa na zinajitosheleza kwa kila kitu

Mwenezi amesema hayo wakati akikagua Jengo la Skuli ya Kisasa Fuoni ambayo imejengwa kwa Chuma tu Mkoa wa Magharibi ikiwa ni Muendelezo wa ziara yake ya kichama Visiwani Zanzibar.

“Niwaombe waliojenga Skuli hizi za Ghorofa kwa teknolojia waende kule Bara mana kuna uhaba wa maeneo hivyo teknolojia hii itasaidia sana mfano hai mie nilipokuwa RC Dar es salaam na Mwanza shida kubwa ilikuwa ni maeneo hivyo inatahijika teknolojia kurahisisha kupata Miundombinu bora na safi k**a hii ya hapa Zanzibar”

Aidha Mwenezi Makalla amepongeza Dkt Hussein Mwinyi kwa kutekeleza Ilani kwa vitendo.

“Ni teknolojia ambayo kwanza inapunguza gharama hivyo tumpongeze Dkt Hussein Mwinyi kwanza ameteleza Ilani kwa vitendo haya Maskuli anayojenga ni ya mfano kuanzia Pemba mpaka hapa U

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maen...
31/01/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC-Organ) Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akishiriki Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC katika ukumbi wa New Parliament Building, Harare nchini Zimbabwe tarehe 31 Januari, 2025. Mkutano huo pamoja na mambo mengine unajadili hali ya ulinzi na usalama Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Matukio mbalimbali ya kuwasili kwa Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu H...
31/01/2025

Matukio mbalimbali ya kuwasili kwa Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Robert Mugabe, Harare nchini Zimbabwe kwa ajili ya kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa nchi wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaofanyika leo tarehe 31 Januari, 2025.

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akipokelewa na Mhe. Dkt. Girma Amente, Mjumb...
31/01/2025

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akipokelewa na Mhe. Dkt. Girma Amente, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Prosperity Party (PP), chama tawala cha Ethiopia na pia Waziri wa Kilimo wa Serikali ya nchi hiyo, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Bole. Balozi Nchimbi amewasili nchini Ethiopia kwa ajili ya ziara ya kikazi, kufuatia mwaliko wa PP.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Ridhiwani Kikwete (Mb) akifuatilia mdaha...
31/01/2025

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Ridhiwani Kikwete (Mb) akifuatilia mdahalo katika Mkutano wa Kimataifa wa Soko la ajira unaoendelea jijini Riyadh nchini Saudi Arabia, leo tarehe 30 Januari, 2025

Mkutano huo umehudhuriwa pia na Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Zuhura Yunus.

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Stephen Wasira, amesema kuwa Tanzania haitakubali kulazimishwa kuig...
31/01/2025

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Stephen Wasira, amesema kuwa Tanzania haitakubali kulazimishwa kuiga tamaduni za mataifa ya Magharibi, ikiwemo ndoa za jinsia moja, na kusisitiza kuwa CCM itaendelea kuongoza kwa ridhaa ya Watanzania kuepuka mambo hayo.

Akizungumza Januari 29, 2025, katika mkutano wa hadhara mkoani Geita kuelekea Maadhimisho ya Miaka 48 ya CCM, Wasira amesema kuna njama za baadhi ya watu aliowaita ‘vibaraka’ kutaka kupenyeza ajenda za mataifa ya nje, ikiwemo kuhalalisha ndoa za jinsia moja, jambo ambalo CCM haitakubali.

"Wanatumia vibaraka wao, wanataka utamaduni wao utawale mawazo yetu? Mpaka wanafikia mahali wanataka wanaume waoane na wanawake waoane kwa wanawake, hao ndio walio na vibaraka wao ndani ya Tanzania ambao wanasema tumekaa sana, tumewachelewesha wanaume kuoana maana hatukubaliani nao," amesema Wasira.

Aidha, amezungumzia madai kuwa CCM imekaa madarakani muda mrefu na kusema kuwa chama hicho kimeendelea kuleta maendeleo makubwa nchini, ikiwa ni pamoja na kup

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Shiriki...
29/01/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Somalia Mhe. Dkt. Hassan Sheikh Mohamud leo kwenye makazi yake Ikulu, Jijini Dar es salaam leo tarehe 29, Januari 2025.

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Stephen Wasira amewasili mkoani Geita kwa ziara ya kikazi ambapo pamoja ...
29/01/2025

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Stephen Wasira amewasili mkoani Geita kwa ziara ya kikazi ambapo pamoja na mambo mengine atazindua sherehe za maadhimisho ya miaka 48 ya kuzaliwa CCM kwa Mkoa wa Geita.

BAada ya kuwasili mkoano humu Wasira alilakiwa na viongozi wa Chama wa mkoa huo pamoja na serikali wakiongozwa na Mkuu aa Mkoa wa Geita, kisha kupokea taarifa ya Chama na utekelezaji wa Ilani ya CCM katika kikao kilichofanyika ofifisi za CCM za mkoa huo.

Rais wa Marekani, Donald Trump ameagiza kusitishwa usambazaji wa dawa za Ukimwi, malaria na kifua kikuu kwa nchi zinazop...
29/01/2025

Rais wa Marekani, Donald Trump ameagiza kusitishwa usambazaji wa dawa za Ukimwi, malaria na kifua kikuu kwa nchi zinazopewa misaada na Shirika la Maendeleo la Marekani (USAID).

Agizo hilo limetolewa leo Januari 28, 2025 huku hatua hiyo ikilenga kupitia upya miradi mbalimbali ya misaada lakini imeibua wasiwasi mkubwa miongoni mwa wataalamu wa afya na mashirika ya kibinadamu.

Kwa mujibu wa duru za kimataifa, agizo hilo linatarajiwa kuathiri mamilioni ya watu wanaotegemea huduma za matibabu kupitia programu k**a Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kupambana na Ukimwi (PEPFAR).

Mpango huo, ulioanzishwa mwaka 2003, umeokoa zaidi ya maisha ya watu milioni 25 barani Afrika.

Aidha, mashirika yanayotoa msaada, likiwamo la Chemonics, yamesema hatua hiyo itavuruga upatikanaji wa dawa na huduma kwa watu walioko hatarini zaidi.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameshiriki Mkutano wa kumi na nane wa bunge ulioanza leo Januari 28, 2025, bungeni jijini Do...
28/01/2025

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameshiriki Mkutano wa kumi na nane wa bunge ulioanza leo Januari 28, 2025, bungeni jijini Dodoma.

Mkutano huo ni mahsusi kwa ajili ya Kamati za Kudumu za Bunge kuwasilisha Taarifa za Mwaka za shughuli za k**ati kwa kipindi cha Januari 2024 hadi Januari 2025.

DAR ES SALAAM - Rais wa Umoja wa Visiwa vya Comoro, Azali Assoumani, yupo jijini Dar es Salaam tayari kwa ajili ya kushi...
28/01/2025

DAR ES SALAAM - Rais wa Umoja wa Visiwa vya Comoro, Azali Assoumani, yupo jijini Dar es Salaam tayari kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Nishati.

Rais Assoumani alipokelewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Zanzibar, Ally Suleiman Ameir, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.

Mkutano huu unawakutanisha viongozi wa Afrika, wadau wa sekta ya nishati, na washirika wa maendeleo kwa lengo la kujadili mikakati ya kukabiliana na changamoto za nishati barani Afrika.

DAR ES SALAAM - Rais wa Jamhuri ya Burundi, Évariste Ndayishimiye, amewasili jijini Dar es Salaam kushiriki Mkutano wa W...
28/01/2025

DAR ES SALAAM - Rais wa Jamhuri ya Burundi, Évariste Ndayishimiye, amewasili jijini Dar es Salaam kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Nishati unaoendelea katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC).

Rais Ndayishimiye alipokelewa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Sera, Uratibu na Baraza la Wawakilishi, Hamza Hassan Juma, pamoja na viongozi wengine waandamizi wa Serikali.

Mkutano huu wa siku mbili umeanza kwa ngazi ya mawaziri, ukitarajiwa kufikia kilele chake leo Januari 28, ambapo Wakuu wa Nchi za Afrika watajadili mikakati ya kukabiliana na changamoto za nishati na kuchangamkia fursa zilizopo barani.

Matokeo muhimu yanayotarajiwa ni kupitishwa kwa Azimio la Dar es Salaam, linalolenga kuimarisha upatikanaji wa nishati ya uhakika, nafuu, na endelevu kwa maendeleo ya bara la Afrika.

Tanzania imeandaa mkutano mkubwa wa viongozi wa nchi za Afrika kuhusu nishati, maarufu k**a "Mission 300," ambao umefung...
27/01/2025

Tanzania imeandaa mkutano mkubwa wa viongozi wa nchi za Afrika kuhusu nishati, maarufu k**a "Mission 300," ambao umefunguliwa rasmi leo Januari 27, 2025.

Lengo kuu la mkutano huu ni kuharakisha upatikanaji wa umeme kwa Waafrika milioni 300 katika kipindi cha miaka mitano, hatua inayolenga kufungua fursa za maendeleo barani Afrika.

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati wa Tanzania, Dkt. Doto Biteko, katika hotuba yake ya ufunguzi, amesisitiza umuhimu wa azma hii katika kutimiza Ajenda ya Afrika 2063 na Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs).

Ameeleza kuwa Tanzania, ambayo wakati wa uhuru mwaka 1960 ilikuwa na uwezo wa kuzalisha megawati 21 pekee, sasa inazalisha megawati 3,160, huku ikitarajia kufikia megawati 4,000 mwishoni mwa mwaka 2025. Hata hivyo, bado Waafrika milioni 571 hawana huduma ya umeme, jambo linalodhihirisha umuhimu wa mkutano huu.

Mkutano huu umbao unahudhuriwa na zaidi ya marais 25, mawaziri wa nishati, viongozi wa taasisi za kimataifa, na wadau wa sekta binafsi. Miongoni mwao ni Rais wa B

Address

Kinondoni Biafra
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dira Digital Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Videos

Share