SokaLetu

SokaLetu ⚽Pata Habari za Kimichezo.
⚽Pata update zote za mechi kali
⚽Pata Uchambuzi wa mechi zote
⚽Bongo Soka

🚨   KLABU ya Yanga inasemekana inaelekea kukamilisha usajili mmoja mkubwa ambao inatarajia kuutangaza hivi karibuni na k...
02/01/2025

🚨 KLABU ya Yanga inasemekana inaelekea kukamilisha usajili mmoja mkubwa ambao inatarajia kuutangaza hivi karibuni na kushtua nchi, huku taarifa zikisema imeingilia kati dili la Simba la kumwania straika anayeongoza kwa mabao mpaka sasa kwenye Ligi Kuu, Elvis Rupia.

Awali Simba ilitajwa kuwa kwenye mchakato wa kumsajili mshambuliaji huyo raia wa Kenya na tayari mazungumzo yalishaanza baina ya pande hizo.

Ofisa Habari wa Klabu ya Yanga Ali Kamwe, alisema kipindi hiki cha dirisha dogo Yanga inafanya usajili wa kuboresha kikosi chake na wanamalizia vitu vichache tu ili kuweza kumtangaza mmoja wa wachezaji ambaye atakuwa gumzo kwenye usajili kipindi hiki.

Hata hivyo, habari kutoka ndani ya klabu hiyo zinasema kuwa ilikuwa kwenye harakati za mwisho kupata saini ya Rupia na ndio wanatarajia kumtangaza wakati wowote kuanzia sasa akitokea Singida Black Stars.

Follow

🚨 KLABU ya Tabora United imemsajili mlinda mlango raia wa Gabon 🇬🇦, Jean-Noël Amonome ambae ameshawahi kucheza klabu za ...
02/01/2025

🚨 KLABU ya Tabora United imemsajili mlinda mlango raia wa Gabon 🇬🇦, Jean-Noël Amonome ambae ameshawahi kucheza klabu za Amazulu na AS Arta Solar ya Djibouti 🇩🇯.

Jean-Noël Amonome ndiye mlinda mlango namba moja wa timu ya taifa ya Gabon 🇬🇦.

Follow

🚨   Klabu ya Simba inaripotiwa kuanza mazungumzo rasmi na klabu ya Azam kuhusu usajili wa kiungo wa kati wa Azam Feisal ...
02/01/2025

🚨 Klabu ya Simba inaripotiwa kuanza mazungumzo rasmi na klabu ya Azam kuhusu usajili wa kiungo wa kati wa Azam Feisal Salum ili kunasa saini yake katika dirisha hili dogo la usajili.

Taarifa zinaeleza kuwa Feisal ni pendekezo la kwanza la kocha mkuu Fadlu Davids, ambaye anataka kuongeza nguvu kwenye eneo la ushambuliaji la klabu hiyo kuelekea duru la pili la ligi.

Bado matajiri wa Azam hawajatoa jibu lolote kwa wekundu wa Msimbazi licha ya Simba kuweka ofa ya zaidi ya milioni 500 mezani ili kununua sehemu ya mkataba wa kiungo huyo ndani ya Azam.

K**a mambo yakienda sawa kati ya Azam na Simba basi huwenda tukashuhudia Feisal akiibukia mitaa ya Msimbazi na kuweka historia ya kucheza klabu zote za Kariakoo akiwa kwenye ubora wake.

Follow

🚨 “Wakati watu wanashangilia kuingia mwaka mpya wa 2025 sisi tulikuwa tunafanya taratibu za kukamilisha usajili wa Elie ...
02/01/2025

🚨 “Wakati watu wanashangilia kuingia mwaka mpya wa 2025 sisi tulikuwa tunafanya taratibu za kukamilisha usajili wa Elie Mpanzu kwenye Michuano ya Kimataifa.

Kwaiyo taarifa rasmi tu ni kwamba Elie Mpanzu yuko halali kuitumikia Simba SC kwenye Michuano ya Kimataifa, kwanzia mechi ya tarehe 5 Dhidi ya Sfaxien.’’

- Amesema Ofisa habari wa klabu ya Simba SC, AHMED ALLY.

Follow

🚨 KLABU ya Kengold Fc imefikia makubaliano na Obrey Chirwa juu ya kupata saini yake  kwa mkataba wa miezi sitaKengold im...
01/01/2025

🚨 KLABU ya Kengold Fc imefikia makubaliano na Obrey Chirwa juu ya kupata saini yake kwa mkataba wa miezi sita

Kengold imeshafanya utaratibu wa usafiri kuhakikisha Chirwa anafika jijini Mbeya ili kusaini mkataba.

Follow

🚨 Wakati staa wa zamani wa Yanga na Simba, Bernard Morrison akitua KenGold, benchi la ufundi la timu hiyo limeandaa prog...
01/01/2025

🚨 Wakati staa wa zamani wa Yanga na Simba, Bernard Morrison akitua KenGold, benchi la ufundi la timu hiyo limeandaa programu maalumu kwa nyota huyo raia wa Ghana.

Pia limesema kabla ya kumsainisha tayari walishazungumza naye kumpa masharti ya timu hiyo na matarajio yao ni kuona anawapa kitu cha maana ndani ya uwanja.

Morrison asiyeishiwa vituko ndani na nje ya uwanja, amesaini mkataba wa miezi sita kuitumikia timu hiyo iliyopo mkiani mwa Ligi Kuu Bara ikiwa na pointi sita.

Kocha Mkuu wa timu hiyo, Omary Kapilima amesema utukutu wa nyota huyo, hautakuwa na athari yoyote kwani ameingia mazingira tofauti na aliyokuwapo awali ya Yanga na Simba.

Amesema mbali na staa huyo, timu hiyo imesheheni nyota kadhaa wakiwamo wa kigeni kutoka Zambia na DR Congo na nyota wengine wenye uwezo na uzoefu akiwamo beki Kelvin Yondani.

"Tulishazungumza naye kumpa masharti yetu tukakubaliana naye, tunajua uwezo na uzoefu alionao utatupa kitu duru la pili kuona tunaondoka mkiani,"

"Hayuko peke yake, wapo mastaa wengine kutoka Zambia na DR Congo na waliocheza timu kubwa hapa nchini k**a Yondani, hivyo tunaenda kuanza upya Ligi" amesema Kapilima.

Kocha huyo ameongeza licha ya ratiba kusogezwa hadi Machi 1, kwao ni faida kwani watapata muda kutengeneza timu kutokana na maingizo mapya akisisitiza wachezaji wote kurejea kambini Januari 3.

Follow

🚨 Klabu ya soka ya  Kengold imemsajili mchezaji wa kimataifa kutoka Ghana  Bernard Morrison k**a mchezaji huru kwa mkata...
31/12/2024

🚨 Klabu ya soka ya Kengold imemsajili mchezaji wa kimataifa kutoka Ghana Bernard Morrison k**a mchezaji huru kwa mkataba wa miezi sita.

Morrison ambaye alikuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu akiuguza majeraha wakati akiitumikia FAR Rabart ya Nchini Morocco, sasa yuko fiti kuwatumikia wachimba madini KenGold.

Morrison amewahi kuvitumikia vilabu vya Orlando Pirates, Club ya Young Africans, Simba Sc, As Vita na FAR Rabart.

Follow

🚨 Kocha Mkuu wa Manchester United, Ruben Amorim, amekiri kuwa anajisihisi “aibu” kuongoza timu hiyo katika hali yake ya ...
31/12/2024

🚨 Kocha Mkuu wa Manchester United, Ruben Amorim, amekiri kuwa anajisihisi “aibu” kuongoza timu hiyo katika hali yake ya sasa, akisema Mashetani hao Wekundu wamejikuta wakipambana kujinusuru kushuka daraja.

“Ni aibu kidogo kuwa kocha wa Manchester United na kupoteza mechi nyingi. Hilo liko wazi kabisa, kwa hivyo tunapaswa kupambana. Huu ni wakati mgumu sana, moja ya nyakati ngumu zaidi katika historia ya Manchester United, na tunapaswa kukabiliana nayo kwa uaminifu,” amesema Amorim.

Mchezo unaofuata wa Manchested United EPL utafanyika ugenini Januari 5 dhidi ya vinara wa ligi hiyo, Liverpool.

Follow

🚨   Taarifa za ndani zinaeleza kuwa klabu ya Yanga ipo kwenye mazungumzo na golikipa wa Simba Sc Aishi Salum Manula kwaa...
31/12/2024

🚨 Taarifa za ndani zinaeleza kuwa klabu ya Yanga ipo kwenye mazungumzo na golikipa wa Simba Sc Aishi Salum Manula kwaajili ya kumsajili k**a golikipa namba mbili wa klabu hiyo.

Mpaka sasa mazungumzo yanaenda vizuri na Aishi Manula inawezakana akakubali kabisa kujiunga na klabu ya Yanga kwa mkataba wa miaka miwili.

Follow

🚨 Shirikisho la Mpira wa miguu nchini (TFF) imesimamisha ligi kuu Tanzania Bara kuanzia Disemba 29,2024 mpaka Machi 1,20...
31/12/2024

🚨 Shirikisho la Mpira wa miguu nchini (TFF) imesimamisha ligi kuu Tanzania Bara kuanzia Disemba 29,2024 mpaka Machi 1,2025 kupisha michuano ya Mapinduzi Cup pamoja na Michuano ya CHAN itayoanza Mwezi january Mwaka Ujao.

Follow

🚨 “Taarifa kuhusu timu yetu ni kwamba baadhi ya Wachezaji wetu waliyokuwa majeruhi hivi sasa wamerejea kwenye kikosi che...
31/12/2024

🚨 “Taarifa kuhusu timu yetu ni kwamba baadhi ya Wachezaji wetu waliyokuwa majeruhi hivi sasa wamerejea kwenye kikosi chetu, Djigui Diarra, Maxi Nzengeli na Kennedy Musonda wamerejea Rasmi, Yao Kouassi yeye Yupo 50% kurejea huku Clatous Chama na Aziz Andabwile wakiwa wanaendelea na Mazoezi ya Utimamu wa mwili ili kujiunga rasmi na wenzao kwaajili ya maandalizi ya mchezo wetu dhidi ya TP Mazembe’’

-Amesema Afisa habari wa klabu ya Yanga ALLY KAMWE.

Follow

🚨 KOCHA Mkuu wa Simba, Fadlu Davids, amesema baada ya kumalizika kwa mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania Bara, anata...
31/12/2024

🚨 KOCHA Mkuu wa Simba, Fadlu Davids, amesema baada ya kumalizika kwa mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania Bara, anatarajia kwenda kukaa na viongozi wa klabu hiyo kuangalia nini kifanyike kwa ajili ya kukiongezea nguvu kikosi chake.

“Nakwenda kukaa na viongozi kuangalia nini kifanyike, nani anapatikana sokoni ili tumwongeze, kazi bado ni kubwa, nyuma, katikati na mbele kote kunahitaji maboresho angalau ya mchezaji mmoja mmoja, ukiangalia ushindani kwenye Ligi Kuu ni mkubwa, kuna Azam FC, Singida Black Stars, Tabora United na Yanga pamoja na sisi wote tuna uwezo wa kuchukua ubingwa, hivyo lazima tuendelee kuongeza uimara kwenye kikosi chetu,’’ alisema kocha huyo.

Follow

🚨 Joshua Mutale anatarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa wiki tatu akiuguza majeraha ya gotiMutale alipata majeraha hayo katik...
31/12/2024

🚨 Joshua Mutale anatarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa wiki tatu akiuguza majeraha ya goti

Mutale alipata majeraha hayo katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya JKT Tanzania uliopigwa Disemba 24 Simba ikiibuka na ushindi wa bao 1-0

Unaweza kusema Mutale amekuwa na mwanzo mbaya Msimbazi kwani ameandamwa na mfululizo wa majeruhi

Huenda akakosa mechi zote tatu zilizobaki kuhitimisha hatua ya makundi kombe la Shirikisho la CAF (CAF CC)

Hata hivyo ongezeko la Elie Mpanzu katika kikosi cha Simba pamoja na uwepo wa winga kinda Ladark Chasambi wanamuhakikishia kocha Fadlu Davids huduma bora zaidi.

Follow

🚨 Afisa wa Bodi ya Ligi kuu ya NBC, Karim Boimanda amethibitisha kupokea barua kutoka kwa Simba SC  juu ya kutaka kuhama...
31/12/2024

🚨 Afisa wa Bodi ya Ligi kuu ya NBC, Karim Boimanda amethibitisha kupokea barua kutoka kwa Simba SC juu ya kutaka kuhama uwanja wa KMC Complex na kwenda uwanja wa Azam Complex .

Simba Sc wametuma barua ya kuhama uwanja wa KMC Complex ili kuweza kuhamia uwanja wa Azam Complex .

Follow

🚨 Mashabiki wa klabu ya Yanga wanamuona beki mpya aliyetua hivi karibuni kutoka Singida Black Stars, Israel Mwenda mazoe...
30/12/2024

🚨 Mashabiki wa klabu ya Yanga wanamuona beki mpya aliyetua hivi karibuni kutoka Singida Black Stars, Israel Mwenda mazoezini tu, lakini bado hajaweza kuruhusiwa kuanza kucheza lakini imefahamika kwamba tatizo ni winga wa zamani wa timu hiyo aliyewahi kupita pia Simba, Augustine Okrah.

Mwenda bado hajaanza kuichezea timu hiyo akiishia mazoezini tu huku kwenye mechi akiishia jukwaani tu na kuwa mchezaji mtazamaji.

Taarifa za uhakika kutoka ndani ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ni kwamba Yanga haiwezi kumtumia Mwenda hadi pale itakapomalizana na Okrah, aliyeishtaki klabu hiyo Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) kufuatia kuvunjiwa mkataba aliokuwa nao.

Okrah anaidai Yanga malimbikizo ya ada ya usajili ambayo hakumaliziwa hadi alipositishiwa mkataba mwishoni mwa msimu uliopita akiitumikia kwa muda wa miezi sita.

Hata hivyo, uongozi wa Yanga unafanya juhudi za kuindoa kesi hiyo ili klabu yao iweze kuendelea na matumizi ya Mwenda na mastaa wengine ambao watasajiliwa.

Follow

🚨 Klabu ya Yanga SC imeendeleza desturi ya magoli mengi kwenye mchezo mmoja baada ya kuifunga Fountain Gate FC magoli 5 ...
29/12/2024

🚨 Klabu ya Yanga SC imeendeleza desturi ya magoli mengi kwenye mchezo mmoja baada ya kuifunga Fountain Gate FC magoli 5 kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya NBC.

Yanga SC ya Ramovic imeshafunga magoli 18 kwenye michezo 5 iliyokwisha cheza tangu aichukue timu hiyo.

Pacome Zouzoa mchezaji bora wa mechi akihusika kwenye magoli 3 kati ya 5 yaliyofungwa leo. Mudathir Yahya kwa mara ya kwanza msimu huu simu zimeanza kuita, na Clement Mzize mwenye kiwango bora kwa sasa amefunga na kusaidia goli moja leo.

Ni Clean Sheet ya 3 mfululizo kwa Mshery tangu ameanza kuaminiwa na Ramovic.

FT: Yanga 5-0 Fountain Gate FC

Follow

🚨 BODI YA LIGI hii Leo imempa onyo kali Mkurugenzi wa Ufundi wa klabu ya Yanga, Abdihamid Moalin kwa kitendo cha kukaa k...
29/12/2024

🚨 BODI YA LIGI hii Leo imempa onyo kali Mkurugenzi wa Ufundi wa klabu ya Yanga, Abdihamid Moalin kwa kitendo cha kukaa kwenye benchi la Ufundi kwenye mechi tatu za Ligi Kuu kinyume na utaratibu.

Lakini pia Bodi kwasasa imepokea rasmi taarifa kutoka TFF kuwa Moalin atakuwa Kocha Msaidizi namba mbili, hivyo mechi zote za ligi kuu atakuwa anakaa kwenye bench la ufundi kihalali.

Follow

🔥🔥🔥 🥰🥰🥰
29/12/2024

🔥🔥🔥 🥰🥰🥰

Address

Bagamoyo
Dar Es Salaam
BAGAMOYO

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when SokaLetu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Videos

Share