Rais wa Iran ziarani Urusi
Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amewasili jijini Moscow muda huu kwa mazungumzo na Rais wa Urusi Vladimir Putin.
🇷 🇦 🇩 🇮 24/7 🇺 🇵 🇩 🇦 🇹 🇪 🇸
Moto
LOS ANGELES: Moto unaoendelea kusambaa katika sehemu za Los Angeles, mpaka sasa umesababisha vifo vya watu 11, ukiteketeza mamia ya majengo, na kusababisha kuhamishwa kwa makumi ya maelfu ya watu.
Licha ya juhudi za maelfu ya wafanyakazi wa zima moto, moto mkubwa zaidi bado haujazuiliwa.
Mamlaka inasema wanatarajia idadi ya vifo itaongezeka.
🇷 🇦 🇩 🇮 24/7 🇺 🇵 🇩 🇦 🇹 🇪
Syra war
WAASI WAUTEKA MJI WA DARAA, WAVUNJA SANAMU LA HAFEZ AL ASSAD
DARAA: Vikosi vya upinzani nchini Syria vimechukua udhibiti wa mji wa Daraa kusini magharibi mwa Syria, na kuingia karibu na mji mkuu Damascus. Waasi hao sasa wanapambana na vikosi vya Rais Bashar al-Assad kutoka pande mbili; kaskazini na kusini, katika jaribio la kuuteka mji mkuu Damascus. Daraa ni mahali ambapo uasi wa Syria ulianza mwaka 2011.
Sanamu ya Hafez al-Assad, Rais wa zamani wa Syria imeanguka tena katikati ya Daraa baada ya kutekwa kwa mji huo.
🇷 🇦 🇩 🇮 24/7 🇺 🇵 🇩 🇦 🇹 🇪 🇸
Syria War
IRAN YASISITIZA KUUNGA MKONO UTAWALA WA ASSAD
DAMASCUS: Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi amewasili katika mji mkuu wa Syria Damascus ili kuthibitisha uungaji mkono thabiti wa Iran kwa Syria huku kukiwa na mashambulizi ya kushtukiza ya makundi ya kigaidi yanayoungwa mkono na mataifa ya kigeni katika nchi hiyo ya Kiarabu.
Akiongoza ujumbe Iran, Araghchi amewasili Damascus leo Jumapili kuwasilisha ujumbe wa Tehran kwa serikali ya Syria.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Tehran kabla ya kuelekea Syria, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran alisema, “Leo ninaondoka kuelekea Damascus ili kufikisha ujumbe wa Jamhuri ya Kiislamu kwa serikali ya Syria. Tunaunga mkono kwa dhati jeshi na serikali ya Syria.
Ameongeza kuwa Iran haitofautishi kati ya utawala wa Israel na Magaidi wanaoipinga Serikali ya Syria.
"Tunaamini kwamba kufuatia kushindwa kwa utawala wa Israel, adui anajaribu kutekeleza malengo yake maovu ya kueneza ukosefu wa usalama katika eneo kupitia makundi hayo hayo ya kigaidi," mwanadiplomasia huyo mkuu wa Iran alisisitiza.
Araghchi alisema jeshi la Syria, kama ilivyokuwa zamani, litapata ushindi mbele ya makundi hayo ya kigaidi.
🇷 🇦 🇩 🇮 24/7
Khamenei
WARANT YA KUKAMATWA NETANYAHU HAITOSHI
TEHRAN: Kiongozi mkuu wa Iran Ayatollah Ally Khamenei amesisitiza kuwa waranti ya ICC ya kukamatwa kwa Waziri mkuu wa Israel Binyamin Netanyahu haitoshi.
Khamenei amesema katika hotuba yake kwamba Waziri Mkuu wa Israel Binyamin Netanyahu anastahili hukumu ya kifo kwa kile alichokifanya.
"Wametoa waranti wa kukamatwa kwake, haitoshi," alisema Khamenei, akizungumza na kundi la wanajeshi wa Basij ambalo ni tawi la Jeshi la Ulinzi wa mapinduzi ya Kiislamu (IRGC)
Badala yake, kiongozi huyo wa Iran alitoa wito wa "hukumu ya kifo kwa Netanyahu" -- ambayo ICC haiwezi kutekeleza.
"Hukumu ya kifo ya viongozi hawa wa uhalifu inapaswa kutolewa," alisema Khamenei.
Baada ya kauli hiyo kali ya Ayatollah, kundi ya wanajeshi waliokuwa wakisikiliza hotuma yake lilitoa kutoa kauli mbiu za kuunga mkono Makundi ya Wapiganaji wa Palestina, huku wakipaza sauti zao kwa kusema "kifo kwa Amerika" na "kifo kwa Israeli".
🇷 🇦 🇩 🇮 24/7
Lindsey Graham
NEW YORK: Seneta wa chama cha Republican nchini Marekani Lindsey Graham ametishia kuwawekea vikwazo washirika wa Marekani iwapo watajaribu kusaidia Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kumkamata Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu.
"Kwa mshirika yeyote - Canada, Uingereza, Ujerumani, Ufaransa - ukijaribu kusaidia ICC, tutakuwekea vikwazo," alisema Seneta huyo wa South Carolina apohojiwa na shirika la habari la Fox.
Alipoulizwa kuhusu aina ya vikwazo hivyo, Graham alisisitiza tishio lake, akisema Marekani inapaswa "kupondaponda" uchumi wa nchi zinazounga mkono juhudi za ICC.
Siku ya Alhamisi, Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu ilitoa waranti wa kukamatwa kwa Netanyahu na Waziri wa zamani wa Ulinzi Yoav Galant kwa tuhuma za uhalifu wa kivita katika Ukanda wa Gaza. Israel imekuwa ikipinga mara kwa mara mahakama ya ICC kusikiliza kesi zinazohusiana na Palestina kwa ujumla. Rais wa Marekani Joe Biden aliutaja uamuzi wa ICC kuwa "wa kuchukiza."
🇷 🇦 🇩 🇮 24/7
Oreshnik Hypersonic missile
MOSCOW: Shambulizi la kombora la masafa ya kati "Oreshnik" dhidi ya sekta ya Ulinzi ya Ukraine huko Dnepropetrovsk lilifanikiwa, huku vichwa vyote vya makombora (War Heads) vikifikia malengo yaliyokusudiwa. Wizara ya Ulinzi ya Urusi imethibitisha ikisema kwamba shambulizi hilo limefanyika ili kukabiliana na utumiaji wa silaha za masafa marefu za Marekani na Uingereza. Kombora la kibalistiki la Oreshnik lina speed mara kumi ya sauti na haliwezi kuzuiwa na mfumo wowote wa Ulinzi anga Duniani
Shambulizi hilo limefanyika huku Wanajeshi 82 wa Ukraine wakijisalimisha, 52 katika hao wakitokea katika eneo la Kursk. Kwa upande mwingine, wizara hiyo imesema Mfumo wa ulinzi wa anga wa Urusi umedungua makombora mawili ya Storm Shadow na ndege zisizo na rubani 642 za Ukraine.
🇷 🇦 🇩 🇮 24/7
Iran defence system
Mfumo wa kujihami na mashambulizi ya anga wa Iran AD-120 surface-to-air missile ukizuia makombora aliyovurumishwa na Israel jijini Tehran usiku wa kuamkia leo.
Iran imesema makombora ya Israel yalidhibitiwa vyema, machache yaliyofanikiwa kupenya yameleta athari ndogo.
🇷 🇦 🇩 🇮 24/7
Abbas Araghch
Licha ya vitisho kutoka Israel kuwa ndege yeyote kutoka Iran isithubutu kuingia kwenye anga ya Lebanon, ndege ya Serikali ya Iran iliyombeba Waziri wa Mambo ya nje Abbas Araghch sambamba na misaada ya kibinadamu iliwasili jijini Beirut, mji mkuu wa Lebanon jana.
Waziri huyo wa masuala ya kigeni wa Iran anayeendelea na ziara yake nchini Lebanon amesema kuwa ikiwa Israel itathubutu kilipiza kisasi kwa kuishambulia Iran, Iran itajibu kwa shambulizi kubwa zaidi.
🇷 🇦 🇩 🇮 24/7
KHAMENEI
Kiongozi mkuu wa Iran Ayatollah Ally Khamenei akiingia kwenye msikiti wa Imam Khomeini jijini Tehran jana October 4, 2024 kwa ajili ya kutoa khutba ya swala ya Ijumaa ikiwa ni kumbukumbu ya kumuenzi Sayyid Hassan Nasrallah, kiongozi wa kundi la Wapiganaji la Hizbullah aliyeuwa kwa shambulizi la bomu lilifanywa na Jeshi la Israel nchini Lebanon September 27, 2024.
🇷 🇦 🇩 🇮 24/7
Hali ilivyokua huko Israel.
By:Abdull Najad Faiq
Nchini Israel.
By:Abdull Najad Faiq