Globify

Globify Issa Halili,
Founder & CEO of GLOBLIFY
+255782621022

GLOBIFY is a global digital media network, marketplace and platform that provides dynamic solutions and digital services based on programs and contents which inform, engage and entertain the world.

Globify tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwenu wadau kwakuwa nasi mwaka 2024. Msaada wenu, ushirikiano, na juhudi ...
01/01/2025

Globify tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwenu wadau kwakuwa nasi mwaka 2024. Msaada wenu, ushirikiano, na juhudi zenu zimekuwa nguzo muhimu ya mafanikio yetu. Tumefanikiwa kwa pamoja, na tunathamini sana mchango wenu katika kila hatua. Tuna furaha kubwa kuwa na ninyi k**a wadau wetu na tunatarajia kuendelea kushirikiana katika mwaka mpya, tukielekea kwenye malengo mapya na mafanikio zaidI

Heri ya Mwaka Mpya 2025
Tunawatakia mwaka mpya wenye furaha, afya njema, na mafanikio. Asanteni kwa kuwa sehemu ya safari yetu, na tukiwa pamoja, tutavuka vikwazo na kufikia malengo makubwa zaidi

GLOBIFY

*GLOB8FY HISTORY**IJUE HISTORIA YA PICHA HII*Inawezekana umeiona hii picha mara nyingi, ila leo utaifahamu stori ya kusi...
26/12/2024

*GLOB8FY HISTORY*

*IJUE HISTORIA YA PICHA HII*

Inawezekana umeiona hii picha mara nyingi, ila leo utaifahamu stori ya kusikitisha iliyojificha nyuma ya hii picha, stori inaanzia karne ya 15 katika kijiji kidogo kilichopo pembeni ya jiji la Nuremberg, huko ujerumani.

Kulikua na familia yenye watoto kadhaa, ilikua ni familia maskini ili kupata mkate wao wa kila siku ilibidi Baba yao afanye kazi kwa zaidi ya masaa 18 kwenye machimbo ya makaa ya mawe na walikula chochote walichopata, ila kulikua na watoto wawili katika familia hiyo ambao walikua na ndoto ya kuwa wachoraji wakubwa.

Walifahamu Baba yao hana uwezo wa kuwapeleka chuo wakasomee fani hiyo ya uchoraji, ikawa kila siku usiku wanajadiliana vipi watafikia ndoto zao, siku moja baada ya majadiliano mengi ya usiku wa siku nyingi kupita hawa watoto wawili walikubaliana kuwa watarusha shilingi juu ili wapate mshindi na atakaeshindwa itabidi aende akafanye kazi kwenye machimbo ya makaa ya mawe kwaajili ya kutafuta pesa na kumlipia ada ya chuo atakaeshinda, na baada ya mshindi kumaliza masomo nae atamsomesha mwenzake aliebaki kwa kuuza kazi ya sanaa ya uchoraji atakayokua anaiuza.

Kulivyokucha walirusha shilingi juu mmoja anaeitwa Albrecht Dürer alishinda na akaenda kusoma jijini Nuremberg, Germany. Kaka yake akabaki kufanya kazi ya hatari kwenye machimbo ya makaa ya mawe kwa miaka 4 ili kulipa ada ya Albrecht, na bahati nzuri Albrecht alikua na uwezo mkubwa sana chuo na hadi anamaliza masomo yake alianza kupata pesa kutokana na kazi zake za sanaa.

Baada ya kumaliza masomo Albrecht Dürer alirudi kijijini kwao na akakuta familia imemuandalia sherehe ya heshima kwa mafanikio hayo, wakiwa wanasherehekea Albrecht alisimama mbele ya meza iliyoandaliwa kwa heshima yake na akamshukuru kaka yake kwa kujitoa ili amsomeshe na akasema pia yupo tayari kumlipia ada kaka yake ili nae akasome k**a ilivyokua makubaliano yao, lakini habari ya kusikitisha ni kuwa kaka yake alikataa

Albrecht Dürer akamuuliza kaka yake kwanini unakataa? Kaka yake akajibu " Hapana mdogo wangu mimi sitaenda Nuremberg kusomea sanaa ya uchoraji, nimeshachelewa sana, hii miaka minne niliyofanya kazi kwenye machimbo imeharibu mikono yangu, kila mfupa ulio kwenye vidole vyangu hakuna ambao haujawahi kuvunjika, vidole vya mkono wangu wa kulia kila siku vinazidi kukak**aa, hata kwenye sherehe yako nimepata shida kushika glass kugonga cheers na wewe".

"Siwezi kushika kalamu wala brash, ila nina furaha mikono yangu hii iliyojaa kasoro imeweza kusaidia wewe kufikia ndoto yako".

Albrecht Dürer alilia sana kwaajili ya kaka yake, kaka aliejitoa kuvunjika vidole ili amsomeshe yeye na mwisho hakuhitaji malipo yoyote.

Ni zaid ya miaka 450 sasa imepita tangu siku ya tukio hilo, Albrecht Dürer alichora picha nyingi zilizojaa kwenye makumbusho ila siku moja aliamua achore picha ya mikono ya kaka yake ikiwa imekutana pamoja na inaelekea mbinguni k**a ishara ya kushukuru, na picha yenyewe ndo hii ambayo imekua maarufu hata kwa wasiojua historia yake.

*GLOBIFY*

Heri ya Siku ya Uhuru wa Tanzania!🇹🇿Tunaposherehekea miaka 63 Tuendelee kudumisha umoja, amani na upendo.GLOBIFY
09/12/2024

Heri ya Siku ya Uhuru wa Tanzania!🇹🇿

Tunaposherehekea miaka 63 Tuendelee kudumisha umoja, amani na upendo.

GLOBIFY

GLOBIFY CHARITY ZANZIBAR 08 DEC 2024Watoto Yatima Wana Ndoto, Hebu Tuzisaidie Ziwe Halisi Kupitia Upendo Na Ukarimu Wetu...
22/11/2024

GLOBIFY CHARITY ZANZIBAR 08 DEC 2024

Watoto Yatima Wana Ndoto, Hebu Tuzisaidie Ziwe Halisi Kupitia Upendo Na Ukarimu Wetu.

Watoto Ni Baraka, Lakini Wanahitaji Walezi Na Moyo Wako Wa Ukarimu Ili Kuinuka.

Jiunge Na Globify Charity Ili Kugusa Maisha Yao Moja Kwa Moja Kupitia- https://chat.whatsapp.com/BiYVpSHVGt34tTA2eMQA3z

GLOBIFY CHARITY - LET LOVE CONNECT US

Globify Charity Yatoa Msaada kwa Watoto Yatima Katika Kituo Cha Islamic Yatima FoundationWadau wa Globify Charity, kwa m...
14/10/2024

Globify Charity Yatoa Msaada kwa Watoto Yatima Katika Kituo Cha Islamic Yatima Foundation

Wadau wa Globify Charity, kwa moyo wa upendo na mshik**ano, wametembelea kituo cha watoto yatima cha Islamic Yatima Foundation kilichopo Ilemela, Mwanza. Katika ziara hiyo, walikabidhi mahitaji muhimu kwa watoto hao, yakiwemo magodoro, vyandarua, vifaa vya shule, mahitaji ya vyakula na nguo.

Baada ya kutoa msaada, wadau walipata nafasi ya kutembelea Saanane National Park na kujionea vivutio mbalimbali vya kipekee vinavyopatikana katika hifadhi hiyo ya kitalii.

Uongozi wa Globify Charity unatoa shukrani za dhati kwa wadau wote waliowezesha mafanikio ya tukio hili kupitia michango ya fedha, vifaa, uhamasishaji, na ushiriki wa moja kwa moja katika safari hii ya matendo ya huruma na upendo kwa jamii. Pia, uongozi unatoa shukrani za dhati kwa uongozi wa kituo kwa mapokezi na ushirikiano mzuri. Uongozi unawakaribisha wadau wengine kuungana na Globify ili kupata fursa za uelimishaji na ushiriki katika matukio ya kijamii.

Jiunge nasi kupitia https://chat.whatsapp.com/BiYVpSHVGt34tTA2eMQA3z

Let Love Connect Us.

Ulisoma na mtu gani maarufu!?
08/10/2024

Ulisoma na mtu gani maarufu!?




SHERIA 6 ZA KUFANIKIWA MAISHANI: 1. Tambua mshindani wako ni yule uliyekuwa jana2. Tengeneza pesa na wekeza kabla ya kul...
01/10/2024

SHERIA 6 ZA KUFANIKIWA MAISHANI:

1. Tambua mshindani wako ni yule uliyekuwa jana

2. Tengeneza pesa na wekeza kabla ya kula bata

3. Kwepa watu hasi, maisha ni mafupi

4. K**a usiposaka kile unachokitaka, hutakipata.

5. Ona kufeli k**a mwanzo tu, sio mwisho.

6. Tabia zetu ndizo huamua maisha yetu ya baadae.

GLOBIFY

"Haijalishi ni kiasi gani tunachotoa bali ni upendo kiasi gani tunaowekeza katika kutoa"Kila tendo jema ni sadaka . Toa,...
29/09/2024

"Haijalishi ni kiasi gani tunachotoa bali ni upendo kiasi gani tunaowekeza katika kutoa"

Kila tendo jema ni sadaka . Toa,penda,rudia,tenda wema,tabasamu na uonyeshe utofauti katika kutoa kwako

Jiunge nasi tukawape tabasamu watoto wenye uhitaji
https://whatsapp.com/channel/0029VaER90OEgGfVZhNXv00o/1336

GLOBIFY

MDAU TUAMBIE HAPA NI WAPI!?
24/07/2024

MDAU TUAMBIE HAPA NI WAPI!?





Mchana fulani wa kibabe,chagua sahani moja hapo twende sawa
22/07/2024

Mchana fulani wa kibabe,chagua sahani moja hapo twende sawa





Wakati Mwingine unaweza usione tumaini lolote mbele yako,machozi yatakuwa sehemu ya maisha yako. Kumbukumbu nzuri na za ...
06/06/2024

Wakati Mwingine unaweza usione tumaini lolote mbele yako,machozi yatakuwa sehemu ya maisha yako. Kumbukumbu nzuri na za kufurahisha za miaka ya nyuma utatamani zirudi tena.

Wakati mwingine maisha hayawezi kukupa unachotaka sio kwamba hustahili kupata,ni kwasababu inabidi ukose inabidi upitie mateso,inabidi uchekwe na watu ili upate kilichobora zaidi ya unachotaka.Kuna ushindi mbele yako Mungu amekuandalia ndiomaana bado upo hai,usichoke kusubiri usichoke kujaribu,usikate tamaa na kuishia njiani ENDELEA MBELE 💪

Globify inakutakia siku i njema na yenye furaha na baraka wewe na familia yako.





Jiunge na channel yetu ya WhatsApp kwa kugusa kiungo hiki
https://whatsapp.com/channel/0029VaER90OEgGfVZhNXv00o

  YA LEOWakati mwingine unaweza kukatishwa tamaa kutokana na changamoto unazopitia,utatamani uache kuendelea na  safari ...
30/05/2024

YA LEO

Wakati mwingine unaweza kukatishwa tamaa kutokana na changamoto unazopitia,utatamani uache kuendelea na safari ya mafanikio yako. Kumbuka hata ndege hupaa angani licha ya upepo mkali,usikate tamaa endelea na safari.

inakutakia mchana mwema na wenye baraka kwako.






JIUNGE NA 'CHANNEL' YETU YA WHATSAPP KWA TAARIFA MBALIMBALI

Globify inaendelea kukupa nafasi ya kupata Taarifa na Elimu kwa ukaribu na urahisi zaidi kupitia Mtandao wa WhatsApp

Jiunge nasi kwa kubofya kiungo hiki

https://whatsapp.com/channel/0029VaER90OEgGfVZhNXv00o

Nahodha wa timu ya Taifa ya Tanzania, Mbwana Samatta, ameweza kumaliza msimu wa 2023/2024 kwa mafanikio makubwa baada ya...
20/05/2024

Nahodha wa timu ya Taifa ya Tanzania, Mbwana Samatta, ameweza kumaliza msimu wa 2023/2024 kwa mafanikio makubwa baada ya timu yake ya PAOK Thessaloniki kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Ugiriki. Katika mechi ya mwisho iliyochezwa jana, PAOK ilishinda kwa mabao 2-1 dhidi ya Aris Salonika ugenini, na hivyo kufikisha pointi 80 ambazo zimewafanya kuwa kileleni mwa ligi.

Hii ilikuwa ni hatua muhimu kwa Samatta na timu yake, huku AEK Athens ikimaliza msimu katika nafasi ya pili. Mafanikio haya ni ushahidi wa mchango mkubwa wa Samatta kwenye timu na umahiri wake uwanjani, ambao umeonekana katika kipindi chote cha msimu.

Kwa ushindi huu, PAOK imeongeza taji lingine kwenye kabati lao la mataji na Samatta anaendelea kuimarisha nafasi yake k**a mmoja wa wachezaji bora kutoka Tanzania.






Tembelea channel yetu ya WhatsApp kwa kugusa kiungo hiki
https://whatsapp.com/channel/0029VaER90OEgGfVZhNXv00o

Anaitwa Yuen Wah muigizaji maarufu wa Hong Kong, huyu mwamba ndio mkuu wa kitengo cha roho mbaya au unaweza kumuita msag...
18/05/2024

Anaitwa Yuen Wah muigizaji maarufu wa Hong Kong, huyu mwamba ndio mkuu wa kitengo cha roho mbaya au unaweza kumuita msaga sumu mkuu. Achana na yule Bill Drago wa Marekani, hiki chuma ukikiona k**a mtu mmoja mwenye minyoo ila mapigo yake k**a watu buku.

Anafinya ile mbaya huyu sina haja ya kumuelezea sana mliotazama Eastern Condors mtakua mashahidi, aliwakamua mavi wababe wote kina Sammo Hang, Yuen Biao mpaka wakakubali mziki

Kwa msiomfahamu huyu pia ndio alicheza kwenye ile movie ya yule mama mvuta fegi mwenye balaa ya Kung Fu Hustle akiwa sambamba na yule mama

Huyu jamaa ndiye aliyefanya wanaume wembamba k**a mimi admin wenu wa page hii maarufu zaidi kwa sasa tz "Dunia Ina Mambo" tuogopeke na kuheshimika duniani

Alisababisha wanaume wembamba tusichukuliwe oya oya kwamba kumbe tunaweza kuwa na balaa zito. Kwa sasa amekuwa mzee ana miaka 73, kwenye maisha yake amecheza movie zaidi ya 160 k**a staa, bedui

HAYA NDIO MAKABILA 125 YA TANZANIA​ ​ANDIKA NAMBA YA KABILA LAKO​ UWAJUE NDUGUZO1. Waalagwa (pia wanaitwa Wasi)2. Waakie...
18/05/2024

HAYA NDIO MAKABILA 125 YA TANZANIA​ ​ANDIKA NAMBA YA KABILA LAKO​ UWAJUE NDUGUZO

1. Waalagwa (pia wanaitwa Wasi)
2. Waakiek
3. Wameru
4. Waassa
5. Wabarabaig (pia wanaitwa Wamang’ati)
6. Wabembe
7. Wabena
8. Wabende
9. Wabondei
10. Wabungu (au Wawungu)
11. Waburunge
12. Wachagga(admin wenu wa page hii maarufu zaidi kwa sasa tz "Dunia Ina Mambo" pia ni mangi wa old moshi kidia)
13. Wadatoga
14. Wadhaiso
15. Wadigo
16. Wadoe
17. Wafipa
18. Wagogo
19. Wagorowa (pia wanaitwa Wafiome)
20. Wagweno
21. Waha (watan zangu wakopeshaji vyombo hawa)
22. Wahadzabe (pia wanaitwa Wahadza na Watindiga)
23. Wahangaza
24. Wahaya
25. Wahehe
26. Waikizu
27. Waikoma
28. Wairaqw (pia wanaitwa Wambulu)
29. Waisanzu
30. Wajiji
31. Wajita
32. Wakabwa
33. Wakaguru
34. Wakahe
35. Wakami
36. Wakara (pia wanaitwa Waregi)
37. Wakerewe
38. Wakimbu
39. Wakinga
40. Wakisankasa
41. Wakisi
42. Wakonongo
43. Wakuria
44. Wakutu
45. Wakw’adza
46. Wakwavi
47. Wakwaya
48. Wakwere (pia wanaitwa Wanghwele)
49. Wakwifa
50. Walambya
51. Waluguru
52. Waluo
53. Wamaasai
54. Wanyantuzu
55. Wamagoma
56. Wamakonde
57. Wamakua (au Wamakhuwa)
58. Wamakwe (pia wanaitwa Wamaraba)
59. Wamalila
60. Wamambwe
61. Wamanda
62. Wamatengo
63. Wamatumbi
64. Wamaviha
65. Wambugwe
66. Wambunga
67. Wamosiro
68. Wampoto
69. Wamwanga
70. Wamwera
71. Wandali
72. Wandamba
73. Wandendeule
74. Wandengereko
75. Wandonde
76. Wangasa
77. Wangindo
78. Wangoni
79. Wangulu
80. Wangurimi (au Wangoreme)
81. Wanilamba (au Wanyiramba)
82. Wanindi
83. Wanyakyusa
84. Wanyambo
85. Wanyamwanga
86. Wanyamwezi
87. Wanyanyembe
88. Wanyaturu (pia wanaitwa Warimi)
89. Wanyiha
90. Wapangwa
91. Wapare (pia wanaitwa Wasu)
92. Wapimbwe
93. Wapogolo
94. Warangi (au Walangi)
95. Warufiji
96. Warungi
97. Warungu (au Walungu)
98. Warungwa
99. Warwa
100. Wasafwa
101. Wasagara
102. Wasandawe
103. Wasangu
104. Wasegeju
105. Wasambaa
106. Washubi
107. Wasizaki
108. Wasuba
109. Wasukuma
110. Wasumbwa
111. Wamanyema
112. Watemi (pia wanaitwa Wasonjo)
113. Watongwe
114. Watumbuka
115. Wavidunda
116. Wavinza
117. Wawanda
118. Wawanji
119. Waware (inaaminika lugha yao imekufa)
120. Wayao
121. Wazanaki
122. Wazaramo
123. Wazigula
124. Wazinza
125. Wazyoba

Wewe ni kabila lipi hapo?


Follow channel yetu ya WhatsApp kwa kugusa kiungo hiko https://whatsapp.com/channel/0029VaER90OEgGfVZhNXv00o

Address

Masaki
Dar Es Salaam
14110

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Globify posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Globify:

Videos

Share