11/02/2025
JINSI YA KUIBA NYAMA KWENYE HOT POT.
01. Ingia jikoni,angalia kushoto na kulia K**a Kuna mtu anakuja.
02. Angalia mkao wa kijiko kimekaaje ili mda wakuondoka ukiache vile vile kilivyokaa usikigeuze, usifanye kosa kizembe.
03. Fungua hot pot pole pole ,usiache mfuniko upige kelele au uanguke(utashtukiwa).
04. Hesabu vipande vya nyama hakikisha vipo kuanzia vitano na kuendelea maana k**a vipo chini ya vitano ni rahisi mama kujua vipande vilivyopungua.
Sasa ni muda wa kuchukua mnofu anza kuutafuna...lakini K**a vipande viko chini ya vitano basi chukua kimoja kimoja na kung'ata robo afu kirudishe chukua kingine fanya hivyo hivyo kwa minofu yote(unang'ata kidogo unaacha kidogo)
05. wakati unakula, simamisha masikio yako vizuri kusikia k**a Kuna mtu anakuja (atakufuma), sasa fungua roho nyama ishuke, usiruhusu mchuzi ukudondokee kwenye nguo au kudondoka chini, na K**a mchuzi utakudondokea wahi haraka fua nguo...na ondoa ushahidi wowote jikoni.
06. Baada ya kula nawa mikono kwa sabuni na uinuse mara 6 K**a unahisi harufu Bado ipo nawa tena na tena..
07. Weka viganja kwa kuziba mdomo afu pumua kusikia K**a harufu ya nyama inatoka kinywani.
Usiwe na wasi wasi kuhusu Hilo,chukua tangawizi au au limao tafuna kuondoa harufu.
08. sasa toka jikoni K**a mtakatifu,maana uko salama
Kesho nitafundisha jinsi ya kumuiba MPENZI WA MTU.🫢🫢🫢🫢🫢🫢🫢