Radio5tz

Radio5tz Radio 5 is one of Tanzania's most popular Swahili speaking radio station, broadcasting news and entertainment

News segment comprises of accurate; soft and hard local, international and national news. Entertainment segment encompasses Blues, Afro vibes and R&B, of both local (African) and international flavors that provide a rare source of relaxation in the hectic world we live in.

Shirikisho la Soka Afrika Caf Limesaini Mkataba na Kampuni ya Mafuta Total Energies Rais Wa Shirikisho hilo Dkt. Patrice...
28/01/2025

Shirikisho la Soka Afrika Caf Limesaini Mkataba na Kampuni ya Mafuta Total Energies Rais Wa Shirikisho hilo Dkt. Patrice Motsepe leo January 28,2025 mbele ya Waandishi wa Habari Jijini Dar Es Salaaam na Kampuni ya Mafuta ya Total Energies wamesaini Mkataba wa udhamini ambao utaanza mwaka huu 2025 mpaka 2028.
shughuli hii ya kuingia mkataba imefanyika kwenye hotel ya Hyatt Jijini Dar Es Salaam.

Cc.

Aliyekuwa mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM kwa miaka kumi, Khadija Omary Kopa, ameeleza kuwa anatarajia watoto wake, aki...
28/01/2025

Aliyekuwa mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM kwa miaka kumi, Khadija Omary Kopa, ameeleza kuwa anatarajia watoto wake, akiwemo binti yake Zuhura Othman (maarufu k**a Zuchu), kuwa kiongozi wa kisiasa. Khadija Kopa amesema kuwa mwanaye Zuchu awali hakuwa na mapenzi na siasa, lakini alijivutia na utendaji kazi wa Rais John Magufuli. Hivi sasa, anasema kuwa Rais Samia Suluhu Hassan pia anamvutia zaidi, na kutokana na hilo, Zuchu ameonyesha nia ya kujihusisha na siasa na sasa ni mwanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Cc.

Wanajeshi watatu wa Afrika Kusini wameuawa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, hali iliyosababisha Rais wa Afrika K...
28/01/2025

Wanajeshi watatu wa Afrika Kusini wameuawa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, hali iliyosababisha Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, kumwomba Rais Paul Kagame wa Rwanda kukutana na kupanga njia za kusaidia kusitisha mapigano yanayoendelea huko Kongo.

Wakati huo, Rais Kagame amedai kuwa Kongo wanajua ukweli wa hali ya mambo, lakini hawataki kusema. Kagame anasema chanzo kikuu cha vita ni juhudi za Wakongomani kutaka kuondoa kabila la Watutsi kutoka katika maeneo ya Mashariki mwa Kongo.

Rais Kagame anaamini kuwa inawezekana makabila haya mawili (ya Kongo na Rwanda) kuwa na nchi tofauti, jambo ambalo Kongo hawakutaka, kwani walikuwa na nia ya kulifukuza kabila hilo na kurudisha upande wa Rwanda, wakiamini kuwa kabila la Watutsi halipaswi kuishi nchini Kongo.


Cc.

Bei ya mayai nchini Marekani inakadiriwa kuongezeka kwa Asilimia 20% mwaka wa 2025, na kupita mfumuko wa bei wa jumla wa...
28/01/2025

Bei ya mayai nchini Marekani inakadiriwa kuongezeka kwa Asilimia 20% mwaka wa 2025, na kupita mfumuko wa bei wa jumla wa chakula.

Gharama ya mayai makubwa kadhaa ilipanda kutoka Dola za kimarekani 3.65 ambazo ni sawa na Tsh 9,282/= za kitanzania, mnamo Novemba, hadi Dola 4.15 sawa na Tsh 10,400/=, mnamo Desemba 2024,Wamarekani wanaweza kuendelea kutarajia bei ya juu ya mayai mwaka huu, makadirio mapya yanaonyesha, kutokana na mlipuko unaoendelea wa mafua ya ndege na mfumuko wa bei.


Cc.

Rapa   anakutana na matatizo ya kisheria baada ya kudaiwa kumwamuru mtu kumpiga mpiga picha kwa mlango wa gari.Mtu anaye...
28/01/2025

Rapa anakutana na matatizo ya kisheria baada ya kudaiwa kumwamuru mtu kumpiga mpiga picha kwa mlango wa gari.
Mtu anayeitwa anachukua hatua za kisheria dhidi ya rapa huyo kwa kudaiwa kumpiga, kulingana na kesi mpya iliyoripotiwa na TMZ. Kesi hiyo ilifunguliwa katika Mahak**a Kuu ya LA Jumatatu.
Hati za kesi za shambulio zinadai kwamba tukio hilo lilitokea mnamo Septemba 11, 2024, wakati Santos alipokuwa kwenye hafla ya kitabu ya rapa huyo Septemba huko The Grove, Los Angeles ili kupiga picha na video.
Santos anadai kwamba 50 Cent alikusudia kumtumia mtu kufanya kitendo hicho kwa niaba yake. Kesi ya shambulio pia inadai kwamba hakukuwa na sababu yoyote kwa mlango kufunguka mahali hapo, isipokuwa kwa kukusudia kumuumiza.


Cc.

Tanzania imepangwa Katika Kundi C kwenye Fainali za Afcon 2025. Baada ya Droo iliyofanyika usiku wa kuamkia leo January ...
28/01/2025

Tanzania imepangwa Katika Kundi C kwenye Fainali za Afcon 2025. Baada ya Droo iliyofanyika usiku wa kuamkia leo January 27,2025 huko Rabbat, Morocco.

Fainali hizo zinafanyika kwa mara ya 35 na zitaanza disemba Mwaka huu.

Ikimbukwe Tanzania inashiriki Fainali hizi kwa mara ya nne baada ya kufuzu mwaka 1980,2019,202 na sasa 2025.

Cc.

Leo kwenye     tunaye  tusikilize kupitia 105.7 Arusha/Moshi/Manyara/Singida91.3/Dsm/Pwani/Iringa/Zanzibar 88.6 dodoma 9...
27/01/2025

Leo kwenye tunaye

tusikilize kupitia 105.7 Arusha/Moshi/Manyara/Singida
91.3/Dsm/Pwani/Iringa/Zanzibar
88.6 dodoma
92.5 mwanza
Cc & music by

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amefungua Rasmi Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afr...
27/01/2025

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amefungua Rasmi Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika katika Ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC), Posta jijini Dar es Salaam Leo Januari 27, 2025 Hadi Januari 28, 2025 ambao unaotarajiwa kuhudhuriwa na zaidi ya marais 25 na mawaziri 60 kutoka nchi mbalimbali za Afrika.

Biteko ameanza hotuba yake kwa kuwakaribisha viongozi ambao wamehudhuria mkutano huo na kueleza kuwa k**a ambavyo Dar es Salaam ilitumika kwa mikutano ya ukombozi wa nchi mbalimbali za Kiafrika ndivyo ambavyo inatumika Leo kwenye mkutano huo muhimu kuhusu nishati.

Biteko amewataka wajumbe wa Mkutano huo kuhakikisha wanatumia vyema Mkutano huo k**a moja ya njia sahihi na muhimu ya kupata ufumbuzi wa uhakika wa tatizo la Nishati katika nchi za Afrika

Cc.

Tunapoumaliza mwaka 2024 na kuuanza mwaka 2025, tunawatakia heri ya mwaka mpya wenye mafanikio, furaha, na afya njema. A...
31/12/2024

Tunapoumaliza mwaka 2024 na kuuanza mwaka 2025, tunawatakia heri ya mwaka mpya wenye mafanikio, furaha, na afya njema. Asanteni kwa kuwa nasi mwaka 2024, na tunatarajia kuwa paroja nanyi zaidi mwaka huu. Mungu awabariki nyote!

Tunaposherehekea msimu huu wa Sikukuu, tunakutakia wewe msikilizaji wetu na familia yako amani, upendo, na furaha tele.
25/12/2024

Tunaposherehekea msimu huu wa Sikukuu, tunakutakia wewe msikilizaji wetu na familia yako amani, upendo, na furaha tele.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania naAmiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye ...
28/11/2024

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na
Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na Maafisa wanafunzi
waliotunukiwa Shahada ya Sayansi ya Kijeshi (BMS) kundi la 05/21 katika sherehe zilizofanyika katika Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi (TMA)
Monduli mkoani Arusha tarehe 28 Novemba, 2024

Bongo Top 20
10/11/2024

Bongo Top 20


🚲Join the Fun Ride at the Meru Off-Road Bike Tour, Season 3!This year, it’s all about enjoying the ride and having a gre...
21/10/2024

🚲Join the Fun Ride at the Meru Off-Road Bike Tour, Season 3!

This year, it’s all about enjoying the ride and having a great time!
Our Fun Ride is designed for casual riders who want to explore breathtaking views and experience adventure without the intensity of a tough race.

What makes the Fun Ride special?
Spectacular views of Lake Duluti
A relaxing Nature Walk
Scenic trails through Mt. Sakila
Swimming at Ngurudoto Mountain Lodge
A post-ride BBQ to chill out and enjoy great food!

And that’s not all! Even if you’re not cycling, we’ve got plenty of Kids’ games and fun activities for everyone to enjoy!

No participation fee!
Swimming & BBQ: Tsh. 30,000/=
Bike Rental (optional): Tsh. 20,000/=

🚲This ride is for everyone, so bring your friends, family, and energy for a day filled with fun, leisure, and adventure!

Date: Sunday, 27th October 2024
Starting Point: ABC Bike Shop, Maji ya Chai Finishing Point: Ngurudoto Mountain Lodge Time: 6 AM sharp

Reserve your spot now and make sure you don’t miss out on the fun! Contact 0752 094 123 for reservations.

Powered by

Spika wa Bunge la Seneti Amason Jeffah Kingi ametangaza kuondolewa madarakani kwa Naibu Rais Rigathi Gachagua na bunge h...
17/10/2024

Spika wa Bunge la Seneti Amason Jeffah Kingi ametangaza kuondolewa madarakani kwa Naibu Rais Rigathi Gachagua na bunge hilo.

Gachagua amekutwa na hatia ya mashtaka matano kati ya 11 ikiwemo ukiukaji wa katiba ya Kenya.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda amekutana na kuzungumza na Balozi wa Urusi nchini Tanzania Mhe. Andre...
17/10/2024

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda amekutana na kuzungumza na Balozi wa Urusi nchini Tanzania Mhe. Andrey Avetisyan na kukubaliana kuendelea kushirikiana katika kukuza Utalii wa Arusha na kuvutia wawekezaji wengi zaidi raia wa Urusi kuja kuwekeza Mkoani Arusha.

Kwenye mazungumzo yao, Mhe. Makonda amemuambia Balozi huyo wa Urusi kuwa Mkoani Arusha zipo Fursa mbalimbali za uwekezaji kwenye Hoteli za Kitalii, Kumbi za Mikutano, kwenye sekta ya Kilimo pamoja na uwekezaji kwenye usafiri wa Anga kutokana na mahitaji makubwa ya usafiri huo mkoani Arusha unaotokana na wageni na watalii wanaofika Mkoani Arusha.

Balozi Avetisyan kando ya Ratiba zake nyingine, Leo alhamisi Oktoba 17, 2024 anakutana na wafanyabiashara na Wawekezaji wa Kirusi waliopo Mkoani Arusha kwa lengo la kuwashirikisha fursa zilizopo Mkoani Arusha ambapo Mhe. Makonda pia ameahidi kushirikiana na Wawekezaji hao katika kurahisisha mazingira ya ufanyaji biashara Mkoani hapa na kusema kuwa Ofisi yake ipo wazi muda wote katika kuhudumia wageni na wenyeji wa Mkoa huo ulio muhimu kwa Utalii, biashara na shughuli mbalimbali za kidiplomasia.

Tunawatakia Heri ya kumbukizi ya miaka 25 ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
14/10/2024

Tunawatakia Heri ya kumbukizi ya miaka 25 ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Mapokeo Land Rover Festival 2024.
12/10/2024

Mapokeo Land Rover Festival 2024.

Address

Njiro Block J
Arusha
P.O.BOX15883

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio5tz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Radio5tz:

Videos

Share

Category