Radio5tz

Radio5tz Radio 5 is one of Tanzania's most popular Swahili speaking radio station, broadcasting news and entertainment

News segment comprises of accurate; soft and hard local, international and national news. Entertainment segment encompasses Blues, Afro vibes and R&B, of both local (African) and international flavors that provide a rare source of relaxation in the hectic world we live in.

Wapenzi wasikilizaji wetu,Katika kipindi hiki kitakatifu cha Pasaka, tunapenda kuwashukuru kwa upendo na usikivu wenu wa...
19/04/2025

Wapenzi wasikilizaji wetu,

Katika kipindi hiki kitakatifu cha Pasaka, tunapenda kuwashukuru kwa upendo na usikivu wenu wa kila siku. Tunawatakia nyote heri ya Pasaka, yenye amani, upendo, faraja na baraka tele kwa familia zenu.

Pasaka iwe ni wakati wa kutafakari, kusameheana na kuungana kwa upendo k**a jamii moja.

Tunaendelea kuwa nanyi bega kwa bega, tukileta habari, burudani na maarifa.

Heri ya Pasaka!

Leo ni Ijumaa Kuu, siku adhimu katika kalenda ya Wakristo duniani, tukikumbuka mateso, kifo na sadaka kuu ya Bwana wetu ...
17/04/2025

Leo ni Ijumaa Kuu, siku adhimu katika kalenda ya Wakristo duniani, tukikumbuka mateso, kifo na sadaka kuu ya Bwana wetu Yesu Kristo pale msalabani – tendo la upendo usio na mipaka kwa ajili ya wokovu wa wanadamu.

Katika tafakari hii ya kiroho, Radio 5 FM tunawakumbusha wasikilizaji wetu wote umuhimu wa msamaha, toba ya kweli, na upendo kwa jirani. Iwe ni muda wa kutafakari maisha yetu binafsi, kuhuisha imani, na kujitoa kwa matendo mema kwa manufaa ya jamii.

Ijumaa Kuu ni darasa la unyenyekevu, uvumilivu, na matumaini. Ni siku ya ukimya wa nafsi, lakini yenye sauti kubwa ya neema na huruma.

Tunawatakia wasikilizaji wetu wote Ijumaa Kuu yenye baraka, utulivu, na tafakari yenye tija.

Lala vizuri amka Mpya na
02/04/2025

Lala vizuri amka Mpya na

“ inawatakia Waislamu wote Eid Ul-Fitr Mubarak! Mwenyezi Mungu akubali swaum na ibada zenu, na awajalie amani, upendo na...
30/03/2025

“ inawatakia Waislamu wote Eid Ul-Fitr Mubarak! Mwenyezi Mungu akubali swaum na ibada zenu, na awajalie amani, upendo na mafanikio. Furahia sikukuu yako!

14/03/2025
Leo, tunasherehekea nguvu, ustahimilivu, na mafanikio ya wanawake kote duniani.
08/03/2025

Leo, tunasherehekea nguvu, ustahimilivu, na mafanikio ya wanawake kote duniani.

Mkurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini Wizara ya Nishati, Bi. Anita Ishengoma amesema katika utekelezaji wa majukumu ya k...
01/03/2025

Mkurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini Wizara ya Nishati, Bi. Anita Ishengoma amesema katika utekelezaji wa majukumu ya kisekta Wizara ya Nishati imetoa fursa za usawa kwa wanawake.

Bi. Ishengoma ameyasema hayo katika kuelekea kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo huadhimishwa kila tarehe 8 Machi ambapo nchini itaadhimishwa kitaifa mkoani Arusha.

"Usawa hapa wizarani unazingatiwa kutokana na uwepo wa idadi kubwa ya wanawake katika ngazi ya maamuzi ambayo inafikia 5." Amesema Bi. Ishengoma

Amesema kuwa uwepo wa uwiano wa jinsia unatoa fursa sawa kwenye maamuzi katika ngazi za juu katika kutekeleza majukumu ya ki sekta.

Katika kuelekea Siku ya Wanawake Duniani ameasa Wanawake kuendelea kuchangamkia fursa zilizopo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Serikali itaendelea kutunga Sera rafiki z...
27/02/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Serikali itaendelea kutunga Sera
rafiki zitakazowezesha ushiriki wa sekta binafsi katika upatikanaji wa nishati safi ya kupikia kwa bei nafuu.

Ameyasema hayo leo Februari 27, 2025 akiwa wilayani Muheza katika muendelezo wa ziara yake mkoani Tanga ambapo amezindua zoezi la ugawaji wa mitungi ya gesi ya kupikia kwa wananchi wa Mkoa wa Tanga.

“Tumeanza kutoa ruzuku kwa wale wote wenye miradi ya gesi ambao wanachakata na kuifanya gesi kuwa nishati”. Amesema Rais Samia

Ameongeza kuwa, Serikali pia inatoa ruzuku hadi kwenye majiko ya umeme ili kuwezesha watanzania wengi zaidi kutumia nishati safi ya kupikia.

Amepongeza ubunifu wa teknolojia mbalimbali ambazo zinakwenda kubana matumizi katika kutumia nishati safi ya kupikia.

Amesema lengo la Serikali ni kulinda afya za watumiaji wa Nishati za kupikia pamoja na mazingira.

Aidha, Rais Samia ameitaka Wizara ya Nishati kuendelea kuusimamia mkakati wa nishati safi ya kupikia ili kuweza kufikia lengo la asilimia 80 ya watanzania kutumia nishati safi ya kupikia kufikia mwaka 2034.

Katika hatua nyingine, Rais Samia amesema upatikanaji wa umeme maeneo ya vijijini uwe zaidi ya kuwasha taa na kuchaji simu bali utumike pia katika shughuli za kiuchumi.

Awali Naibu Waziri Nishati, Mhe. Judith Kapinga alimpongeza Rais Samia.kwa kukubali kuzindua programu ya ugawaji mitungi ya gesi ya ruzuku 452,445.

Mhe. Kapinga alisema mpango.huo jumuishi utasaidia kupunguza uharibifu wa mazingira na kupunguza athari za kijamii kiafya na kiuchumi.

“Mhe. Rais programu yako hii imezaa matunda, tunapoelekea mwaka mmoja wa utekelezaji wa mkakati huu wa nishati safi ya kupikia k**a Taifa tumepiga hatua sana”. Amesema Mhe. Kapinga

Ameeleza kuwa, kupitia sekta binafsi usambazaji gesi kabla ya Mkakati ulikuwa ni asilimia kumi hadi 11 kwa mwaka ila kwa sasa ukuaji wa kampuni hizo ni asilimia 50 hadi 60 kwa mwaka.

Aliongeza kuwa kiashiria Kingine cha ukuaji wa matumizi ya nishati safi ni ongezeko la masoko vijijini lakini hamasa kubwa ya nishati safi ya kupikia imekuja pia kutokana na uwepo wa umeme kwani ukuaji wa matumizi ya umeme umeongezeka.

 : Utekelezaji wa Kampeni ya Mtu ni AfyaHost:  &
25/02/2025

: Utekelezaji wa Kampeni ya Mtu ni Afya

Host: &

Jeshi la Polisi katika mkoa wa Mwanza limekanusha taarifa zinazosambaa mtandaoni zikilihusisha jeshi hilo kuhusika na tu...
19/02/2025

Jeshi la Polisi katika mkoa wa Mwanza limekanusha taarifa zinazosambaa mtandaoni zikilihusisha jeshi hilo kuhusika na tukio la kutoweka kwa Katibu wa BAVICHA mkoa wa Mwanza Amani Mohamed Manengelo.

Akizungumza na vyombo vya habari jijini Mwanza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Wilbrod Mutafungwa amesema mpaka sasa jeshi hilo linawashikilia na linaendelea kuwahoji watu watatu akiwemo mwanamke mmoja anayefahamika kwa jina la Pendo kuhusiana na tukio la kutoweka kwa katibu na katika mahojiano ambayo watu hao wamehojiwa hakuna sehemu walipolitaja jeshi la polisi kuhusika na tukio hilo.

Katika hatua nyingine Kamanda Mutafungwa amewaomba wananchi wa mkoa huo kuendelea kutoa taarifa kwa jeshi hilo ili kufanikisha upatikanaji wa Amani.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt.  , ameonya vikali wanachama wanaotafuta uteuzi wa udiwani, uwakili...
19/02/2025

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. , ameonya vikali wanachama wanaotafuta uteuzi wa udiwani, uwakilishi na ubunge kwa njia zisizo halali, akisisitiza kuwa chama hakitasita kuwaengua wale watakaokiuka Katiba, Kanuni na maadili ya CCM kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025.

Akizungumza jijini Dodoma wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa makatibu wa matawi na kata kutoka Wilaya ya Dodoma, Balozi Nchimbi alisema baadhi ya wanachama wameanza kampeni kabla ya muda rasmi kwa kutumia mbinu k**a kuanzisha mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs), kufadhili matukio ya kijamii k**a kumbukumbu za misiba na sherehe za ndoa, pamoja na kushinikiza vikao vya chama kuwapitisha bila kupingwa.

“Tayari tumeshuhudia baadhi ya wabunge na madiwani wakitafuta mbinu za kuhakikisha wanapitishwa bila kupingwa. Wengine wanahamasisha matamko ya vikao, huku baadhi wakihudhuria matukio yenye lengo la kujitambulisha mapema kwa wapiga kura. Wapo wanaowapa posho wahudhuriaji wa mikutano wakiwa wamevaa sare za CCM ili kuonesha wanaungwa mkono. Tunawataka waache mara moja. CCM ina mfumo madhubuti wa kufuatilia mwenendo wa wanachama wake, na kumbukumbu hizi zote zinahifadhiwa. Wanaweza kushangaa majina yao yakiwekwa pembeni,” alisema.

Balozi Nchimbi aliwataka madiwani na wabunge walioko madarakani kuacha kupuuza majukumu yao kwa kisingizio cha maandalizi ya uchaguzi, akisema chama kitafanya tathmini kwa kila mgombea kulingana na utendaji wake, si kwa uwezo wa kutoa fedha kwa wapiga kura.

“Tumeshuhudia watu wakichaguliwa lakini wanakaa miaka mitano bila kufanya kazi kwa sababu wanajua wapiga kura wachache wa ndani ya chama watakaowarudisha tena madarakani. Mfumo wetu mpya unalenga kumchagua mgombea kwa misingi ya kazi zake, si kwa kutumia rushwa au mbinu za kificho. Tunataka ukichaguliwa ukafanye kazi kwa wananchi,” alisisitiza. Inaendelea….

Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini,  , amesema kuwa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo,  alimweleza kuwa hana tena hamu ya kugo...
19/02/2025

Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, , amesema kuwa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, alimweleza kuwa hana tena hamu ya kugombea nafasi hiyo kutokana na kazi kubwa inayofanywa na Rais Dkt.

Akizungumza leo Februari 19, 2025 jijini Arusha wakati wa hafla ya uhamasishaji wa kutoa elimu ya nishati safi kwa viongozi wa baraza la wazee Arusha, sambamba na kuwaeleza mafanikio ya serikali ya awamu ya sita katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo Jijini humo

Gambo amesema kuwa Lema alimueleza kuwa ingawa yeye ni mpinzani, hawezi kusema hadharani, lakini anatambua juhudi kubwa zinazofanywa na Rais Samia.

Address

Njiro Block J
Arusha
P.O.BOX15883

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio5tz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Radio5tz:

Share

Category