Programu ya mafunzo ya ufundi imekuwa mkombozi kwa vijana, ikiwapa ujuzi wa vitendo wa kubuni maisha bora katika maeneo mbalimbali kama ushonaji, ufundi magari, na mengine ambayo yanawasaidia vijana kupata ajira au kuanzisha biashara zao baada ya kumaliza masomo.
katika kuunga mkono jitihada za serikali kuelekea uchumi wa viwanda kanisa katoliki la moyo safi wa bikira maria Arusha limeanzisha vyuo vya ufundi wa ushonaji na magari ambapo
Katika ufunguzi wa mkutano wa 4 wa chama cha ununuzi na ughavi Tanzania (APSP) uliofanyika katika ukumbi wa AICC, jijini Arusha wanachama kutoka taasisi mbalimbali wa sekta ya biashara wamekusanyika kwa lengo la kubadilishana mawazo na kujadili masuala muhimu yanayohusu maendeleo ya ununuzi na ughavi nchini.
Akihutubia mkutano huo, Mtendaji Mkuu wa mamlaka ya udhibiti na manunuzi ya umma (PSPR) Denis Sumbo amesisitiza kuwa serikali imeweka kipaumbele kwa vikundi maalum katika sekta ya biashara akifafanua kwa mwaka 2023/2024 jumla ya vikundi 210 vilifanikiwa kupata tuzo za zabuni zenye thamani zaidi ya bil 9.8 kwa lengo la kukuza wawekezaji wa ndani.
Kwa upande mwingine, mwenyekiti wa chama cha ununuzi na ughavi Tanzania (APSP) Emmanuel Urembo amesema mkutano huu ni fursa ya kuwakutanisha wanataaluma wa sekta hiyo ili kukuza weledi, nidhamu, na utaalamu utakaosaidia kuboresha makampuni ya wazawa na kuchangia maendeleo ya taifa kwa ujumla.
Aidha afisa mtendaji mkuu wa wakala wa usajili wa biashara na leseni (BRELA) Godfrey Nyaisa amesema changamoto nyingi zinawakumba wataalamu wa ununuzi na ughavi ni kukosa uzoefu wa kukabiliana na vikwazo.
Mwakilishi wa taifa kwenye mashindano ya mapishi ya Zambia yanayotarajiwa kufanyika 2025 Hamisa Rashidi ametoa elimu kuhusu jinsi ya kutumia mboga ya Biringanya katika maandalizi ya vyakula vya kisasa huku akisisitiza umuhimu wa kuongeza mboga hii katika lishe ya kila siku.
Haya yamejiri Katika maafali ya 12 ya wahitimu 264 wa Chuo cha ufundi stadi, hoteli, Ukarimu na Utalii cha VETA kilichopo jijini Arusha, huku wito ukitolewa kwa vijana kujituma na kuacha kusubiri ajira pekee.
Viongozi na wahadhiri wa chuo hicho walisisitiza kwamba elimu pekee haitoshi, bali ni muhimu kwa vijana kujitahidi kuwa wabunifu ili kufanikiwa katika maisha.
#veta #ElimuNiNguvu #kujituma
Matatizo ya afya ya akili yameendelea kuwa changamoto kubwa nchini na hivi karibuni taasisi ya Afya Huru imeanzisha mafunzo kwa maafisa rasilimali na wafanyakazi ili kupunguza madhara ya afya ya akili katika maeneo ya kazi.
Mafunzo haya ambayo yamefanyika New Arusha hotel yamejumuisha maafisa rasilimali watu kutoka maeneo mbalimbali yakiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha afya ya akili na kuboresha mazingira ya kazi kwa wafanyakazi.
Mratibu wa taasisi ya Akili Huru Bw. Jonas Biseko amesema wamejikita katika afya ya akili sana sana kwa sababu ni eneo ambalo wanahitaji kujenga uelewa kutokana na uelewa mdogo wa wafanyakazi kuhusiana na madhara yanayotokana na afya ya akili
Mtaalamu wa saikolojia Malick Shekimweri amesema kuwa matatizo ya afya ya akili yanaongezeka kwa kasi kubwa, na asilimia kubwa ya waathirika ni vijana. Amegusia athari za matatizo haya kwa uzalishaji kazini, akieleza kwamba hali ya kisaikolojia ya wafanyakazi inaathiri moja kwa moja utendaji wao kazini.
Kwa upande wake mkurugenzi wa taasisi ya Mtuwe Mama mzigo iliyopo jijini Arusha Ruth Allan amesema kuwa chanzo cha matatizo ya afya ya akili mara nyingi kinatokana na familia. Walezi ambao wamepitia matatizo ya kiuchumi na kijamii wanawaathiri watoto wao, na hii inaweza kupelekea matatizo ya afya ya akili kwa vizazi vijavyo.
Aidha Afisa rasilimali watu wa kampuni ya EACOP ya jijini Da es Salaam Lusajo Mwakalundwa ameongeza kuwa mafunzo ya afya ya akili yameongeza uelewa kuhusu matatizo haya katika maeneo ya kazi. Mafunzo haya ni hatua muhimu ya kuhakikisha wafanyakazi wanapata msaada wa kisaikolojia na kwamba mazingira ya kazi yanaboreshwa ili kupunguza shinikizo la kisaikolojia linaloweza kuleta matatizo ya afya ya akili.
#afya
#afyayaakili
Wadau wa maendeleo nchini hasa wale wanaozalisha bidhaa za ujenzi na mafundi wameaswa kutumia bidhaa zinazozalishwa nchini na kuzitumia kwenye miradi mikubwa inayotekelezwa nchini kwani zina ubora uliothibitishwa.
Afisa masoko mkuu wa kampuni ya kiboko Erhadi Mlyansi amesema watakwenda kufaidika kutokana na miradi inayoendelea hapa jijini Arusha ikiwemo ujenzi wa uwanja wa mpira.
Balozi wa kampuni ya kiboko Salim Ahmedy amewashauri mafundi kuwa na msimamo na kitu wanachokifanya ili iwe rahisi kuelewa na kufanikiwa zaidi.
Nae fundi rangi Aisen Uroki amewaasa wanawake waliozoea kukaa bila kufanya kazi waache mara moja kudharau kazi za ufundi kwani mafundi wa kike hupewa kipaumbele zaidi kazini.
Mkurugenzi wa wilaya ya Arusha Bw. Suleimani Msumi amewaomba wadau mbalimbali kuguswa na kusaidia familia zisizojiweza ili kupunguza ongezeko la watoto wa mtaani.
Hayo yamesemwa katika tukio la ugawaji wa vifaa kwa watu wa kuaminika kwenye jamii(Fitperson) zaidi ya 50 kwa kushirikiana na shirika la kusaidia watoto la SOS lililofanyika katika halmashauri ya wilaya ya Arusha miongoni mwa vifaa vilivyotolewa ni pamoja na madaftari, magodoro, blanket, Kalamu na vinginevyo.
Nae Afisa wa shirika la SOS Godlisten Mlay zaidi ya watoto 120 wameshasaidika katika halmashauri ya wilaya ya Arusha, halmashauri ya jiji la Arusha na halmashauri ya Karatu kwa kushirikiana na Ustawi wa jamii
Aidha Mkazi wa Arusha Ester Gabriel ameshukuru kwa msaada aliopewa na kuomba misaada kama hii iendelee kuwafikia ili kusaidia familia zinazoishi katika mazingira magumu.
Kwa upande wa mtoto Rahma Hamisi amesema Msaada huo unakwenda kuwasaidia wazazi wake kwa sababu mwanzo walishindwa kununua madaftari ya kujisomea na utamsaidia kusoma kwa bidii.
Taasisi ya Taifa ya Kudhibiti na Usimamizi wa Mionzi ambayo ni Tume ya Nguvu za Atomic Tanzania leo imeendesha mafunzo kwa watoa huduma na wakufunzi kutoka mikoa mbalimbali yanafanyika makao makuu ya kituo hicho kilichopo Njiro, Arusha kwa lengo la kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya mionzi katika huduma za afya.
Mafunzo hayo yatakayodumu kwa siku tano, kuanzia tarehe 2 hadi 6 December, yanahusisha wataalamu wapatao 60 kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania. Washiriki hao ni wakufunzi na watoa huduma zinazohusiana na vifaa vya uchunguzi kama X-ray, MRI na CT Scan.
Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo hayo Mkurugenzi wa Udhibiti na Usimamizi wa Mionzi, Tume ya Nguvu za Atomic Tanzania Justin Ngaile amesisitiza kuwa watoa huduma za afya wasiokuwa na sifa na utaalamu wa kutumia mionzi wanapaswa kuacha mara moja, kwani ni kosa la kisheria kufanya hivyo.
Kwa upande mwingine mkufunzi wa Chuo cha Mionzi Muhimbili, Catherine Malika amesema wamejifunza mbinu bora za kutoa huduma za mionzi na umuhimu wa usahihi katika matumizi ya vifaa vya uchunguzi.
Aidha, mkazi wa Arusha Sara Lothi ametoa ushuhuda wa kutia moyo kwa kusema kuwa huduma za mionzi zinazotolewa mahospitalini ni salama na zinasaidia sana katika utambuzi na matibabu, huku akisisitiza kuwa ni muhimu kwa jamii kuondoa hofu na mitazamo hasi kuhusu huduma hizi.
Mkurugenzi wa jiji la Arusha John Kayombo akiambatana na Hakimu mkazi mahakama ya mwanzo mkoa wa Arusha Salma Mwamende amewaapisha viongozi 924 katika hafla iliyofanyika jijini Arusha mara baada ya uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji kumalizika hivi karibuni.
Akizungumza mkurugenzi wa jiji la Arusha Bw. John Kayombo amewasisitiza viongozi hao kuwa sehemu ya maendeleo katika jamii pamoja na kusimamia miradi ya maendeleo na kuleta tabasamu kaa jamii wanazozisimamia.
Mara baada ya kiapo hicho viongozi waliochaguliwa katika maeneo yao wameagizwa kwenda kufanya kazi mara moja.
Zaidi ya vijana 50 kutoka taasisi za afya, bima na afya ya akili wamehudhuria mdahalo wa elimu ya Afya ya uzazi na haki Kwa vijana ulioandaliwa na Taasisi ya Bethani jijini Arusha ukiwa na lengo la kuwafanya kutambua afya ni msingi katika kuelekea maendeleo.
Mkurugenzi wa taasisi hiyo bwana Jimmy Pamba amesema wamefanya hivyo kwa dhamira ya kutuma ujumbe kwa serikali ,kaya na jamii ili kuwakumbusha vijana ambao ni robo tatu ya wakazi wa tanzania kujitambua katika kufanya maamuzi yaliyo sahihi sambamba na kuwasaidia vijana.
Aidha aliyekuwa muathirika wa madawa ya kulevya James Vincent amewaasa wazazzi kuwaepusha watoto na athari za madawa ya kulevya pamoja na kutenga muda wa kuzungumza wa watoto wao.
Mshiriki ambae ni msimamizi wa washauri wa watoto Sharifa Ally amesema yeye kama mama amenufaika na mdahalo huo na amejifunza kutenga muda kuongea na familia yake ili kuepusha changamoto kwa watoto.
Kampeni za uchaguzi wa serikali za mitaa zinatarajiwa kuanza rasmi leo tarehe 20 Novemba , ikiwa ni siku saba kabla ya uchaguzi wa serikali za mitaa.
Wagombea kutoka vyama vya siasa watafanya mikutano ya hadhara katika maeneo wanapogombania nafasi hizo ili kunadi sera zao na kutoa ahadi zitakazokwenda kuboresha huduma za kijamii
Je umejiandaa kwenda kuhudhuria kampeni za wagombea wako?
Tupe maoni yako
✍🏿@joseph_mukya
🎥@bonnie_layker
Katibu mkuu wizara ya mambo ya ndani ya nchi Ally Gugu ameagiza ujenzi wa miji kufuata kanuni za upangaji miji utakaozingatia huduma zinazotolewa na jeshi la zima moto na uokoaji na kuepuka ujenzi holela ili kutibu athari kabla hazijatokea.
Akizungumza kwenye kikao cha baraza la wafanyakazi la jeshi hilo kilichofanyika jijini Arusha Ally Gugu amehamasisha elimu kwa vijana mashuleni na wananchi kufika katika maeneo mbalimbali yanayotolewa elimu ya zimamoto na uokoaji kwa lengo la kujilinda pindi itokeapo janga.
Ubunifu wa watoto katika teknolojia zinazojibu changamoto kwa jamii
Watoto wana ubunifu usio na mipaka na mitazamo mipya inayowapa sifa kupata suluhisho za asili pale tunapowawezesha na kukuza ubunifu wao, tunafungua milango ya suluhisho bunifu kwa changamoto kubwa za leo
Tuwasaidie watoto kuunda mustakabali bora na endelevu.
#WabunifuWajao
#ubunifuwawatoto
#MawazoyaWatoto