TBCArusha

TBCArusha TBC Arusha 92.1MHz FM owned by

OUR LIVE STREAM LINKS

tbcarusha921.radiostream321.com

tbcarusha921.radiostream12345.com

tbcarusha921.radiostream123.com

02/01/2026

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imeendesha mafunzo maalum kwa watendaji wa vituo vya kupiga kura kuelekea uchaguzi mdogo wa udiwani wa Kata ya Kirua Vunjo Magharibi, Wilaya ya Moshi Vijijini mkoani Kilimanjaro. Mafunzo hayo yamewahusisha wasimamizi wa vituo, makarani pamoja na wasaidizi wa uchaguzi, yakilenga kuwajengea uwezo wa kusimamia zoezi la upigaji kura kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za uchaguzi.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Afisa Uchaguzi wa Jimbo la Vunjo, Lucas Msele, amesema mafunzo hayo ni muhimu katika kuhakikisha uchaguzi mdogo unafanyika kwa haki, uwazi na kwa kuzingatia misingi ya kisheria.

Washiriki wameeleza kufaidika na mafunzo waliyopata, hususan katika matumizi ya vifaa vya uchaguzi, utunzaji wa siri ya kura na taratibu za siku ya uchaguzi, huku uchaguzi mdogo wa udiwani wa Kata ya Kirua Vunjo Magharibi ukitarajiwa kufanyika tarehe 5 Januari 2026.

02/01/2026

Unajua Mitandao ya kijamii inalinda vipi taarifa zako binafsi ?

Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi inawajibu wa kusimamia ulinzi wa taarifa binafisi katika kampuni na majukwaa ya miramdao ya kijamii Nchini.

Mkuu wa mahusiano na Mawasiliano Tume ya Ulinzi Binafsi Nchini Innocent Mungy amesema wanaendelea kutoa Elimu kwa Maafisa Ulinzi wa Taarifa binafsi katika Taasisi na kampuni mbalimbali ikiwa ni pamoja na Kampuni za Mitandao ya Kijamii ili kuhakikisha Usalama na faragha kwa watumiaji wa mitandao hiyo.

Endelea kusikiliza 92.1 kwa habari,Elimu na burudani.

02/01/2026
31/12/2025

Katika makabidhiano hayo, CPA Makalla ameuagiza uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha kuhakikisha malipo hayo yanafanyika kwa wakati.

Hundi hiyo ya Mfano ya bilioni mbili imekabidhiwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha CPA Amos Makalla ambaye amesema Serikali inaendelea kuboresha miundombinu mbalimbali ili kukuza uchumi wa wananchi, hususan kupitia sekta za utalii na biashara na ameitaka Halmashauri ya Jiji la Arusha kusimamia kikamilifu ulipaji wa fidia kwa wananchi waliopisha mradi huo.

Naye Afisa Mipango Miji wa Jiji la Arusha amewashukuru wananchi kwa ushirikiano wao katika kupisha utekelezaji wa mradi huo wa kimkakati, akiwahakikishia kuwa malipo ya fidia yataendelea kulipwa kwa wakati uliopangwa.

Baadhi ya wananchi walipokea Hundi ya malipo wamesema imekua furaha na faraja kuanza mwaka 2026, kwani wanaamini pesa hizo watazitumia katika maendeleo yao.

🇹🇿

31/12/2025

Wananchi wa moshi wanatarajia kunufaika na gari la kubebea wagonjwa, hasa kwa wale waliokuwa wakilazimika kutumia usafiri usio salama au kusubiri muda mrefu kabla ya kufikishwa hospitalini.

Mbunge wa Jimbo la Moshi mjini IBRAHIM SHAYO amezindua gari Hilo maalum la kubebea wagonjwa kwa lengo la kuboresha huduma za afya na kupunguza changamoto za usafiri kwa wagonjwa,

Gari hilo la kubebea wagonjwa limezinduliwa katika Hospitali ya Mawenzi iliyopo mkoani kilimanjaro. likiwa ni sehemu ya juhudi za serikali ya Tanzania kwa kuhakikisha wananchi wanapata huduma za afya kwa wakati na kwa usalama zaidi.

Aidha Mganga mkuu wa mkoa, ambaye alimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa, akaeleza kuwa hatua hiyo ni mfano wa ushirikiano mzuri kati ya viongozi na serikali.

Kwa uzinduzi wa gari hili la kubebea wagonjwa, wananchi wa Jimbo la Moshi mjini wanatarajia kuimarika kwa huduma za afya, huku viongozi wakisisitiza matumizi sahihi ya rasilimali hiyo kwa manufaa ya jamii kwa ujumla.

31/12/2025

Jumla ya wagonjwa 500 wamepatiwa huduma katika kambi ya matibabu ya vipimo bure inayoendelea iliyowekwa na taasisi ya moyo ya JKCI ya  Dar es salaam katika hospitali ya Arusha Lutheran Medical  Center (ALMC)liyopo jijini Arusba waliyoingia nayo ubia ikiwa ni hatua za mwanzo kuelekea kuanzisha huduma zkiwemo za kibngwa zitakazokuwa zinasimamiwa na JKCI  kuanzia  january 1 2026 kwa kipindi cha  miaka 20.

Mkurugenzi mtendaji wa taasisi ya JKCI Dkt. Peter Kisenge amesema   taasisi hiyo imejioanga kuifanya hospitali hiyo kuwa kitovu matibabu ya magonjwa ya moyo na mengine ambayo itakuwa ni kuvutio cha utalii tiba pamoja na kuimarisha vifaa tiba vya kisasa  pamoja na miundo mbinu ili kuwa na huduma bora.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, CPA Amos Makalla, amekabidhi hundi ya fidia ya shilingi bilioni mbili kwa wananchi waliopisha ma...
31/12/2025

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, CPA Amos Makalla, amekabidhi hundi ya fidia ya shilingi bilioni mbili kwa wananchi waliopisha maendeleo ya mradi wa ujenzi wa Uwanja wa AFCON unaojengwa Jijini Arusha.

Hundi hiyo ya Mfano ya bilioni mbili imekabidhiwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha CPA Amos Makalla ambaye amesema Serikali inaendelea kuboresha miundombinu mbalimbali ili kukuza uchumi wa wananchi, hususan kupitia sekta za utalii na biashara na ameitaka Halmashauri ya Jiji la Arusha kusimamia kikamilifu ulipaji wa fidia kwa wananchi waliopisha mradi huo.

Kwa upande wao, wananchi waliopokea hundi hiyo ya fidia wameonesha furaha yao na kuiomba Serikali kuhakikisha malipo yote yanakamilika kwa wakati k**a ilivyoahidiwa.

Mbali na kukabidhi hundi hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Arusha amekagua maendeleo ya ujenzi wa uwanja huo, ambapo hadi sasa umefikia asilimia 70 ya utekelezaji, na unatarajiwa kukamilika mwezi Juni mwaka 2026.

🇹🇿

30/12/2025

Maonyesho ya utalii wa magari ya zamani mchanganyiko yanayojulikana k**a Kilimanjaro Classic Car Show yamefanyika mkoani Kilimanjaro, yakilenga kukuza utalii, historia ya magari pamoja na michezo ya magari ya zamani.

Huo ni mkusanyiko uliowaleta pamoja wapenzi wa magari ya zamani, na wadau wa utalii, kushuhudia maonyesho ya kipekee ya Kilimanjaro Classic Car Show, tukio lililounganisha utalii, historia na burudani.

Katika kilele cha maonyesho hayo tuzo ya Gari Bora la Zamani la Mwaka 2025 ilitolewa kwa washiriki walioonesha ubora wa hali ya juu katika utunzaji, muonekano na historia ya magari yao, ambapo washindi wa nafasi ya kwanza na ya pili walikuwa na haya.

Akizungumza wakati wa maonyesho hayo, mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Moshi mjini Godfrey Mnzava amesema Serikali kwa kushirikiana na waandaaji itazidi kuweka mikakati ya kuboresha tamasha lijalo, ili liwe la kuvutia zaidi na lenye mabadiliko makubwa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa African Sports Agency Company Limited Joseph Mselle amesema lengo kuu ni kuanzisha jukwaa la kudumu litakalokuza utalii, kuhifadhi historia ya magari ya zamani na kuutangaza utamaduni wa michezo ya magari nchini.

Maonyesho ya Kilimanjaro Classic Car show yanatarajiwa kufanyika kila mwaka, yakiwa na lengo la kuongeza thamani ya utalii na urithi wa magari ya zamani nchini.
#ɢᴏᴠɪʀᴀʟ

28/12/2025

Baada ya Tume huru ya Uchaguzi nchini kutangaza kurudiwa kwa uchaguzi wa ubunge katika Jimbo la Siha mkoani Kilimanjaro, chama Cha NRA kimeanza ramsi kampeni zake jimboni humo kwa kumnadi mgombea ubunge Anna Kipembela ambapo wamewataka wanachi kudumisha amani kuelekea uchaguzi huo huku kikiahidi kuwatumikia kwa kuboresha miundombinu pamoja na kukuza uchumi.

Katika kuwahakikishia wananchi hao amani na utulivu,mkuu wa mkoa huo Nurdin Babu amewataka wananchi kujitokeza na kushiriki uchaguzi huo kwani hali ya usalama ni ya kutosha swala lililotiliwa mkazo pia aliyekuwa mgombea wa nafasi ya urais kupitia chama cha NRA Almasi Hassan Kisabya akisisitiza amani.

Uchaguzi huo wa marudio unatarajiwa kufanyika rasmi Tarehe 30 December 2025, na macho ya wananchi sasa yako kwenye mchakato huu muhimu wa kidemokrasia.

28/12/2025

Mwenyekiti wa UVCCM Moshi vijijini Mkoani Kilimanjaro,Juvenali Shirima amesema Wizara ya Vijana imekuja na dira mpya yenye lengo la kuwaunganisha vijana, kuwajengea uzalendo na kuwawezesha kiuchumi bila kujali tofauti za kisiasa, kidini au kikanda.

Aidha Shirima amewataka vijana kuwa mstari wa mbele kulinda amani na kushiriki kikamilifu katika mipango ya serikali, akibainisha kuwa utulivu wa taifa ni nguzo muhimu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

20/12/2025

Zaidi ya watoa huduma 90 kutoka katika vituo mbalimbali vya afya nchiniwamepatiwa mafunzo yaliyoandaliwa na Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzani (TAEC)jijini Arusha kwa lengo la kuwajengea uwezo zaidi katika kuhudumia wagonjwa na wateja wao ili kuwapa vipimo sahihi vya mionzi na kuepuka madhara pale vinapozidishwa.

17/12/2025

Wataalamu wa dawa na vifaa tiba katika halmashauri mbalimbali nchini wametakiwa kutumia utaalamu wao katika kufanya ukaguzi na kuhakikisha kuwa wanaendelea kuwa na soko la bidhaa bora na salama ili kuhakikisha wanapambana na utandawazi ambao unatajwa kuwa janga kubwa duniani   linalochangia uwepo wa dawa duni na bandia.

 

Akifungua kikao kazi cha wataalamu hao jijini Arusha ,mwakilishi wa mganga mkuu wa mkoa wa Arusha, Dkt. Revocatus Ndyekobora amesema ushirikiano wa kiutendani uliopo kati ya mamlaka ya dawa na vifaa tiba(TMDA) na TAMISEMI  hususani mkoa wa Arusha kwa kuzingatia  mwongozo wa kutekeleza kanuni za kukasimu baadhi ya madaraka na majukumu ya TMDA na Halmashauri  kumechangia kusogeza huduma bora kwa wananchi.

Address

Arusha Chini

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TBCArusha posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to TBCArusha:

Share