Ndago Television

Ndago Television Above & Beyond

Hayo yamesemwa leo Jumapili Januari 28, 2024 na Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam, Mrisho Mrisho wakati akitoa ufaf...
29/01/2024

Hayo yamesemwa leo Jumapili Januari 28, 2024 na Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam, Mrisho Mrisho wakati akitoa ufafanuzi kuhusu madai ya uwepo wa msongamano bandarini kutokana na kutofanya kazi kwa baadhi ya gati.

Mrisho amethibitisha kuwa, gati zote zinafanya kazi na kwa sasa meli zinaendelea kuhudumiwa katika gati zote.

Ameendelea kwa kusema kuwa, kwa leo pekee (Januari 28, 2024) kuna meli 13 kwenye gati zote kuanzia gati namba 0 hadi gati 11 zikiendelea kuhudumiwa na meli 31 zikiwa zinasubiri kuhudumiwa.

Bw. Mrisho ameongeza kuwa, kwa upande wa gati za Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA), terminal l kuna meli zipatazo 10 zikiendelea kuhudumiwa ambazo zimebeba shehena mbalimbali

“Pale gati namba 0 kuna meli ya MV Yangze 32 inapakua, gati namba 1 kuna meli ya MV Loa Fortune inahudumiwa, gati namba 2
kuna MV African Macaw, huku gati namba 3 kukiwa kuna meli ya MV Tong Da na meli zote hizi zinapakua mizigo mchanganyiko” alisema Bw. Mrisho na kuongeza

“Gati namba 4 hivi sasa kuna meli ya MV Fearless, gati namba 5 kuna MV Anassa, gati namba 6 na 7 kuna MV MSC Nora III, pale KOJ I kuna meli ya MT NCC Abha, KOJ II kuna meli ya MT Lubersac na mwisho pale SPM kuna meli ya MT Torm Hannah ikiendelea kupakua”

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndugu. Paul Makonda amekemea vikali t...
29/01/2024

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndugu. Paul Makonda amekemea vikali tabia ya baadhi ya Viongozi na Watumishi wa Chama na Serikali wanaotembea vifua mbele angali hawatekelezi majukumu yao na kupelekea Wananchi kuichukia Serikali na Chama Cha Mapinduzi kinachoogozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waandishi wa habari kuelezea masuala mba...
25/01/2024

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waandishi wa habari kuelezea masuala mbalimbali ya ziara yake nchini Indonesia tarehe 25 Januari, 2024. Pembeni ni mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Indonesia Mhe. Joko Widodo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akinawishwa mikono na Rais wa Jamhuri ya Indonesia Mhe....
25/01/2024

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akinawishwa mikono na Rais wa Jamhuri ya Indonesia Mhe. Joko Widodo mara baada ya kupanda mti wa kumbukumbu katika viwanja vya Makazi ya Rais huyo Bogor Presidential Palace tarehe 25 Januari,2024.

24/01/2024
Lissu kwenye Maandamano
24/01/2024

Lissu kwenye Maandamano

Address

Sakina Kwa Idd
Arusha
P.OBOX11988

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ndago Television posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Ndago Television:

Share

Category