12/01/2025
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema Miaka 61 ya Mapinduzi ni Kumbukumbu ya Wananchi wa Zanzibar kujikomboa Kiuchumi ,Kisiasa na Kijamiì yaliyotokana na Madhila ya kutawaliwa.
Rais Dk.Mwinyi ameyasema hayo alipowahutubia Wananchi katika Kilele cha Maadhimisho ya Miaka 61 ya Mapinduzi Uwanja Wa Gombani, Pemba tarehe 12 Januari 2025.
Ameeleza kuwa Mafanikio Makubwa yamepatikana katika kufikia Malengo ya Mapinduzi ya Usawa, Wananchi kuwa Wanufaika wa Rasilimali na fursa sawa bila ya Upendeleo.
Rais Dk.Mwinyi amebainisha kuwa Serikali imeitafsiri dhana ya Mapinduzi kwa Kuleta Mageuzi ya Kiuchumi ,Kisiasa na Kijamii.
Aidha ameeleza kuwa Nchi imepata Mafanikio Makubwa katika kukuza Uchumi, Kuongeza Ukusanyaji wa Mapato na kudhibiti Matumizi yote.
Eneo jengine ambalo Dk ,Mwinyi amelielezea kuwa la Mafanikio ni Kuwawezesha Wananchi Kiuchumi Kuimarisha Miundombinu ya Barabara , Viwanja vya Ndege,Bandari, Nyumba za Makaazi ,Miundombinu ya Michezo, Huduma za Afya ,Umeme Elimu na Kuimarisha Demokrasia na Utawala Bora.
Halikadhalika amewasisitiza Wanasiasa ,Viongozi wa Dini na Wananchi kuwa Mstari wa mbele katika kudumisha Amani na Utulivu wa nchi ili Maendeleo Makubwa zaidi yapatikane.
Akizungumzia suala la Uchaguzi Dk.Mwinyi amesema ni wajibu wa kila Mwananchi Kuiombea Nchi Amani na Utulivu na Mshik**ano ili hatimae Nchi ifanye Uchaguzi wa Kidemokrasia,Uwazi na Misingi ya Kisheria.
Aidha , Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan ameshiriki Maadhimisho hayo, pamoja na Viongozi mbalimbali wa Serikali kitaifa kutoka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mabalozi wanaowakilisha Nchi zao nchini, Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Viongozi wa Dini na Vyama vya Siasa na Wananchi kutoka Mikoa ya Unguja na Pemba.