Savvy Media Live

Savvy Media Live MAONI YAKO FB,INSTAGRAM@SAVVY MEDIA LIVE. SIKILIZA SAVVY FM 105.3
LISTEN ONLINE: SAVVY FM ARUSHA.

  FLEVA SAVVY FM ARUSHA  Mgodi umetema tega sikio 105.3 Savvy Fm upate madini yanayopatikana Tanzania pekee.  tupo na   ...
15/01/2025

FLEVA SAVVY FM ARUSHA


Mgodi umetema tega sikio 105.3 Savvy Fm upate madini yanayopatikana Tanzania pekee.

tupo na

tupo na mwekezaji

tupo na

Usikose pia

Kwenye ni

Wachimbaji wako ni .g

Graphics by
Tembelea mitandao yetu ya kijamii ya Facebook Instagram na tweeter

Chama cha ACT Wazalendo kinapenda kuutangazia umma kuwa mchakato wa ndani ya Chama wa wanachama kujitokeza na kutangaza ...
15/01/2025

Chama cha ACT Wazalendo kinapenda kuutangazia umma kuwa mchakato wa ndani ya Chama wa wanachama kujitokeza na kutangaza nia ya kugombea nafasi mbalimbali kwenye uchaguzi mkuu 2025 umefunguliwa rasmi kuanzia tarehe 15 Januari, 2025.

Hatua hiyo ni utekelezaji wa agizo la Halmashauri Kuu ya Chama Taifa iliyoelekeza Chama kuweka utaratibu wa wanachama kutangaza nia ya kugombea nafasi za Udiwani, Udiwani Viti Maalum, Ubunge, Ubunge Viti Maalum na Urais.

Baadhi ya masuala muhimu ya kuzingatiwa kwenye mchakato huo ni pamoja na watiania kupaswa kujisajili kwenye orodha ya watiania kwenye ngazi husika kwa kujaza fomu maalum.

Taarifa ya ACT imewataja watia nia wa Udiwani na Udiwani wa Viti Maalum kujihusisha na ngazi ya Kata huku kwa wale wa Ubunge na Ubunge wa viti maalum kwenda ngazi ya Jimbo; na Watia nia wa Urais kufika Ofisi ya Makao Makuu kwa taratibu zaidi.

Pia viongozi wa Mikoa, Majimbo na Kata wameagizwa kuwaruhusu watiania kutumia Ofisi za Kata, Majimbo na Mikoa kutangaza nia zao huku ngazi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakiruhusiwa kutangaza nia kupitia Ofisi ya Makao Makuu ya Chama.





Shirika la Maasai Stove and Solar limegawa vifaa kwa  wanafunzi wa kidato cha kwanza kijiji cha Selela kata ya  Selela -...
15/01/2025

Shirika la Maasai Stove and Solar limegawa vifaa kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza kijiji cha Selela kata ya Selela -Monduli

Akiongoza zoezi hilo mkurugenzi wa shirika hilo ndugu KISIOKI MOITIKO amesema wanafunzi hao ni wale ambao Familia zao zimeshindwa gharama za vifaa vya shule.

Shirika hilo kwa kushirikiana na mwenyekiti wa kijiji hicho waliwatambua watoto zaidi ya 20 ambao wamepangiwa shule mbalimbali ndani ya wilaya ya Monduli ,ambao hawakuweza kufanikiwa kupata mahitaji yao .

Miongoni mwa vifaa vilivyotolewa na shirika hilo ni pamoja na Magodoro, Madaftari na Mabegi ya Madaftari , Matranka pamoja na ndoo.

Credit.

Familia ya Marehemu Jures Ngani mwanamuziki wa Mjengoni Band imefikia uamuzi wa kumzika leo Jumatano Januari 15,3025, ma...
15/01/2025

Familia ya Marehemu Jures Ngani mwanamuziki wa Mjengoni Band imefikia uamuzi wa kumzika leo Jumatano Januari 15,3025, maeneo ya DUKABOVU mkoani Arusha baada ya kufikia muafaka wa pande zote mbili wa kumsitiri ndugu yao.

Yote haya yanajiri baada yakutokea sintofahamu kati ya ndugu wa marehemu na mke wa marehemu kushindwa kuelewana wapi azikwe mwanamuziki huyo.

Mungu ailaze roho ya marehemu JURES MARDOSHER NGANI

Handeni kunani , ajali zaua watu 30 ndani ya siku 20: Habari kubwa Magazetini leo Jumatano Januari 15/2025
15/01/2025

Handeni kunani , ajali zaua watu 30 ndani ya siku 20: Habari kubwa Magazetini leo Jumatano Januari 15/2025




Ni upi mtazamo wako katika hili ... Dondosha komenti yako hapa ..      #
14/01/2025

Ni upi mtazamo wako katika hili ... Dondosha komenti yako hapa ..


#

Klabu ya  imefungiwa mechi mbili na kupunguzwa kuwa mechi moja kucheza bila mashabiki pamoja na faini ya dola elfu 40,00...
14/01/2025

Klabu ya imefungiwa mechi mbili na kupunguzwa kuwa mechi moja kucheza bila mashabiki pamoja na faini ya dola elfu 40,000 kutokana na vurugu zilizojitokeza katika mchezo dhidi ya CS Sfaxien uliofanyika disemba 15,2024.

14/01/2025
Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Mhe. Ester Mahawe amefariki dunia leo Januari 14, 2025 katika hospitali ya Rufaa ya kanda ya ka...
14/01/2025

Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Mhe. Ester Mahawe amefariki dunia leo Januari 14, 2025 katika hospitali ya Rufaa ya kanda ya kaskazini -KCMC Mkoani Kilimanjaro alipokuwa anapatiwa Matibabu.

Taarifa ya kifo chake imetangazwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Mohamed Mchengerwa kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan

"Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Mkuu wa Wilaya ya Mbozi mkoani Songwe Mhe. Ester Mahawe. Kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ninatoa pole kwa familia, Mkuu wa Mkoa wa Songwe, wafanyakazi na wananchi wote wa wilaya ya mbozi, ndugu, jamaa na mafariki kwa msiba huu. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi' amesema waziri Mchengerwa

Watu 11 wamefariki dunia wa Kijiji cha Chang’ombe kilichopo Kata ya Segera wilayani Handeni Mkoani Tanga  baada ya kugon...
14/01/2025

Watu 11 wamefariki dunia wa Kijiji cha Chang’ombe kilichopo Kata ya Segera wilayani Handeni Mkoani Tanga  baada ya kugongwa na lori lililokuwa limebeba saruji baada ya kupoteza uelekeo wakati walipojitokeza barabarani walipokuwa wakishanga ajali ya gari dogo aina ya tata .

Watu hao walijitokeza barabarani ili kuweza kutoa msaada kufuatia ajali ya barabarani ya gari dogo aina ya Tata ndipo walipokumbana na ajali hiyo iliyopelekea kupoteza maisha..

Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian lori hilo liliwagonga watu hao usiku wa kuamkia Januari 14,2025  na kusababisha vifo hivyo pamoja na majeruhi.

Lori hilo lenye namba za usajili T.680 BQW likiwa linatokea Tanga lilifeli breki na kuwagonga watu waliokuwepo pembezoni mwa barabara na kusababisha vifo vya watu 11 papo hapo na kujeruhi wengine 11.

Miili ya marehemu hao imehifadhiwa katika Hospitali ya wilaya ya Korogwe Magunga na majeruhi wanaendelea kupatiwa matibabu katika hospitali hiyo .

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa huyo alitoa pole kwa familia za marehemu na kuwatakia nafuu ya haraka majeruhi wote .

Mkuu huyo wa Mkoa alitoa wito kwa madereva na wamiliki wa vyombo vya moto kuhakikisha magari yao yanakuwa katika hali nzuri ya kiufundi ili kuepusha ajali za namna


.3

Laiti kila kitu kingekwenda k**a kilivyopangwa, basi leo mwili wa mwimbaji Jures Mardosher Ngani ungeagwa jijini Arusha,...
13/01/2025

Laiti kila kitu kingekwenda k**a kilivyopangwa, basi leo mwili wa mwimbaji Jures Mardosher Ngani ungeagwa jijini Arusha, kisha mazishi yangefanyika kesho Same, Kilimanjaro.

Jures, msanii wa Mjengoni Classic ya Arusha, alifariki dunia Januari 11, katika hospitali ya Mount Meru alipokuwa amelazwa kwa siku sita

Taarifa za awali za ratiba ya mazishi zilizotolewa juzi, zilionyesha kuwa Jures angezikwa Jumanne Januari 14, Same, eneo ambalo linadaiwa alilipendekeza mwenyewe wakati wa uhai wake.

Same ni ukweni kwa Jures na alilipenda eneo hilo baada ya kuhudhuria mazishi ya mama mkwe wake na ndipo alipomwambia mama watoto wake kuwa ikitokea ametangulia basi azikwe Same.

Inasemekana kikao cha mazishi kilichofanyika juzi Arusha kilikubaliana na wazo hilo la mazishi kufanyika Same ambapo maandalizi yalianza mara moja.

Lakini jana jioni mambo yakabadilika, baada ya Jumuiya ya Wacongo waishio Arusha kusema mazishi lazima yafanyike Arusha, kukawa na mabishano makubwa.

Wanaopinga mazishi kufanyika Same wanataka ushahidi utakaonyesha kuwa ni kweli marehemu alitaka akazikwe huko. Wanadai si desturi yao mwanaume kuzikwa ukweni.

Wengine wanakwenda mbali zaidi kwa kusema mwanamke hakuwa mke wa ndoa ingawa waliishi kinyumba kwa miaka mingi na kujaaliwa kupata watoto wawili.

Mwisho wa siku ikaamuliwa kuwa kila kitu kisimame hadi kaka wa marehemu atakapofika Arusha Jumanne hii akitokea kwao Congo (DRC).

Rais wa Mjengoni Classic, Digital Mkongya, ameithibitishia kuwa ni kweli kuna utata juu ya mji atakaozikwa Jures.

"Tunamsubiri kaka wa marehemu ambaye yuko njiani ameshavuka Kampala. Nadhani kesho mapema atawasili Arusha na naamini akishaongea na shemeji yetu (Mke wa marehemu), yatapatikana maamuzi yenye busara," ameeleza Digital.

Aidha, Digital amekiri kuwa Jures alikuwa akielewana sana na mama mkwe wake aliyezikwa Same, lakini kwa bahati mbaya hajawahi kuwaambia wasanii wenzake wala Mcongo yeyote kuwa angependa kuzikwa huko na hapo ndipo shida inapokuja kwani watu wanataka ushahidi.

Kwa upande wake mke wa marehemu amekiri kuwepo utata juu ya mazishi ya mumewe.

Sina ushahidi, lakini huo ndio wosia alionipa mume wangu wakati wa uhai wake .....
Credit: SAID MDOE

  FLEVA SAVVY FM ARUSHA  Mgodi umetema tega sikio 105.3 Savvy Fm upate madini yanayopatikana Tanzania pekee.  tupo na   ...
13/01/2025

FLEVA SAVVY FM ARUSHA


Mgodi umetema tega sikio 105.3 Savvy Fm upate madini yanayopatikana Tanzania pekee.

tupo na

tupo na mwekezaji

tupo na

Usikose pia

Kwenye ni

Wachimbaji wako ni .g

Graphics by
Tembelea mitandao yetu ya kijamii ya Facebook Instagram na tweeter




Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema  Miaka 61 ya Mapinduzi ni  Kumbukumb...
12/01/2025

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema Miaka 61 ya Mapinduzi ni Kumbukumbu ya Wananchi wa Zanzibar kujikomboa Kiuchumi ,Kisiasa na Kijamiì yaliyotokana na Madhila ya kutawaliwa.

Rais Dk.Mwinyi ameyasema hayo alipowahutubia Wananchi katika Kilele cha Maadhimisho ya Miaka 61 ya Mapinduzi Uwanja Wa Gombani, Pemba tarehe 12 Januari 2025.

Ameeleza kuwa Mafanikio Makubwa yamepatikana katika kufikia Malengo ya Mapinduzi ya Usawa, Wananchi kuwa Wanufaika wa Rasilimali na fursa sawa bila ya Upendeleo.

Rais Dk.Mwinyi amebainisha kuwa Serikali imeitafsiri dhana ya Mapinduzi kwa Kuleta Mageuzi ya Kiuchumi ,Kisiasa na Kijamii.

Aidha ameeleza kuwa Nchi imepata Mafanikio Makubwa katika kukuza Uchumi, Kuongeza Ukusanyaji wa Mapato na kudhibiti Matumizi yote.

Eneo jengine ambalo Dk ,Mwinyi amelielezea kuwa la Mafanikio ni Kuwawezesha Wananchi Kiuchumi Kuimarisha Miundombinu ya Barabara , Viwanja vya Ndege,Bandari, Nyumba za Makaazi ,Miundombinu ya Michezo, Huduma za Afya ,Umeme Elimu na Kuimarisha Demokrasia na Utawala Bora.

Halikadhalika amewasisitiza Wanasiasa ,Viongozi wa Dini na Wananchi kuwa Mstari wa mbele katika kudumisha Amani na Utulivu wa nchi ili Maendeleo Makubwa zaidi yapatikane.

Akizungumzia suala la Uchaguzi Dk.Mwinyi amesema ni wajibu wa kila Mwananchi Kuiombea Nchi Amani na Utulivu na Mshik**ano ili hatimae Nchi ifanye Uchaguzi wa Kidemokrasia,Uwazi na Misingi ya Kisheria.

Aidha , Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan ameshiriki Maadhimisho hayo, pamoja na Viongozi mbalimbali wa Serikali kitaifa kutoka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mabalozi wanaowakilisha Nchi zao nchini, Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Viongozi wa Dini na Vyama vya Siasa na Wananchi kutoka Mikoa ya Unguja na Pemba.

Usikose kusikiliza live kupitia savvyfm code ni moja 105.3
12/01/2025

Usikose kusikiliza live kupitia savvyfm code ni moja 105.3





Usikose kusikiliza live mtanange kati ya  na   kupitia savvyfm 105.4
12/01/2025

Usikose kusikiliza live mtanange kati ya na kupitia savvyfm 105.4


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa majaji wa Mahak**a ya Rufani, Wen...
10/01/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa majaji wa Mahak**a ya Rufani, Wenyeviti wa Bodi na kumpanga kituo cha kazi Balozi

Address

P. O. BOX 14070
Arusha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Savvy Media Live posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Videos

Share