Msumba News Blog

Msumba News Blog Blog hii inajihusisha na machapisho ya kuhabarisha,kuelimisha na kuburudisha.

28/01/2025
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM Taifa) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu. Dkt. Samia Suluhu Hassan...
17/01/2025

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM Taifa) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) kilichofanyika Jijini Dodoma tarehe 17 Januari, 2025.

Mabasi ya Chama Cha Mapinduzi  yako hapa Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete yakiwa na kazi ya kuwasafirisha wajumbe wa...
17/01/2025

Mabasi ya Chama Cha Mapinduzi yako hapa Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete yakiwa na kazi ya kuwasafirisha wajumbe waliofika kwa ajili ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCM

Ukumbi wa JAKAYA KIKWETE CONVENTION CENTRE upo tayari kwa mkutano mkuu maalum wa CCM TAIFAEndelea kukaa karibu na kurasa...
16/01/2025

Ukumbi wa JAKAYA KIKWETE CONVENTION CENTRE upo tayari kwa mkutano mkuu maalum wa CCM TAIFA

Endelea kukaa karibu na kurasa zetu za mitandao ya kijamii tutakusogezea taarifa zote kutokea hapa Jijini Dodoma.

Karibu sana Dodoma Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi
15/01/2025

Karibu sana Dodoma Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi

BARABARA YA KM 18 MIANZINI-NGARAMTOKUKAMILIKA SEPTEMBAWaziri wa Ujenzi Abdallah Ulegaamemtaka Meneja wa Wakala wa Baraba...
08/01/2025

BARABARA YA KM 18 MIANZINI-NGARAMTOKUKAMILIKA SEPTEMBA

Waziri wa Ujenzi Abdallah Ulega
amemtaka Meneja wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), mkoa wa Arusha Eng. Reginald Massawe kumsimamia kikamilifu mkandarasi Stecol Corporation anaejenga barabara ya Mianzini-Ngaramtoni Km 18 kuhakikisha inakamilika ifikapo Septemba mwaka huu.

Akizungumza wakati akikagua maendeleo ya ujenzi huo amesisitiza kufanyakazi usiku na mchana mpaka mradi huo ukamilike kwa wakati ili kurahisisha usafiri na usafirishaji jijini Arusha.

Amesisitiza ujenzi wa Barabara katika miji na majiji uendane na uwekaji taa za barabarani zinazotumia jua (solar power), ili kupendezesha mitaa na kuiwezesha kupitika wakati wote.

"Mh.Rais Samia ametoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya barabara jijini Arusha hivyo hakikisheni kazi inafanywa kwa ubora, hatutakubali barabara iharibike baada ya muda mfupi ", "amesisitiza Ulega.

Aidha, Waziri huyo amemhakikishia mkuu wa mkoa wa Arusha Paul Makonda kuwa Serikali itazijenga barabara zote unganishi na wezeshi jijini Arusha ili kupunguza msongamano wa magari na kuendana na maandalizi ya mashindano ya kombe la mataifa ya Africa AFCON 2027.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Makonda ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya barabara jijini Arusha nakusisitiza itachochea ukuaji wa sekta ya utalii na kukuza uchumi wa watu jijini humo.

* *

WANANCHI SIMANJIRO WAIPA TANO SERIKALI UJENZI WA MIUNDOMBINUSimanjiroWAKAZI wa Wilaya ya Simanjiro wameipongeza Serikali...
06/01/2025

WANANCHI SIMANJIRO WAIPA TANO SERIKALI UJENZI WA MIUNDOMBINU

Simanjiro

WAKAZI wa Wilaya ya Simanjiro wameipongeza Serikali kupitia Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kwa kutatua kero ya muda mrefu ya barabara na madaraja wilayani humo.

Wakizungumza wakati wa ziara ya waandishi wa habari kutembelea miradi ya ujenzi wa miundombinu wilayani humo wakazi hao wamesema kabla ya ujenzi wa miundombinu hiyo walikuwa wakipata shida hasa kipindi cha mvua zilizokuwa zikisababisha mafuriko na kukata mawasiliano kutokana na kutokuwa na madaraja ya kutosha wilayani humo.

Bi. Angelina Makala mkazi wa Kijiji cha Lolotu wilayani humo anasema kipindi cha nyuma kabla ya ujenzi wa miundombinu hiyo walikuwa wanashindwa kwenda kwenye shughuli zao za kijamii kutokana na maji kujaa katika mito na kukatisha mawasiliano.

“Kipindi cha nyuma tulikuwa tunateseka, maana kipindi cha masika tunavuka maji tunaogelea kwenye maji na shule watoto hawaendi mpaka mafuriko yaishe. Lakini tangu hii barabara imejengwa huu ni mwaka wa tatu tunanufaika na hii barabara.

“Tunashukuru kwa sababu hata juzi hapa maji yalitoka, tumeona ni vema Mama Samia anatufanyia vizuri, mkandarasi aliyeshika hapa anajenga makalavati makubwa.” Alisema Angelina.

Naye, Bw. Cloud Losioki mkazi wa Orkesumet, wilayani Simanjiro anasema kwa mara ya kwanza mji wao umepata Barabara za lami ambazo zimesaidia kurahisisha usafiri pamoja na kuwaepusha na athari za kiafya ambazo awali zilikuwa zikisababishwa na vumbi kutokana na barabara kutokuwa na lami hivyo kuishukuru serikali kwa kuwapelekea mradi huo.

Amesema kukamilika mradi huo kutawasaidia kuwainua kiuchumi kutokana na maendeleo yatakayopatikana ikiwemo kusafirisha mazao na bidhaa nyingine kwa urahisi kwa kutumia barabara hizo.

“Tunafurahi kwa sababu ni kwa mara ya kwanza kabisa ndani ya mji wetu huu tunapata barabara ya lami, naamini kabisa kwamba kila mtu anafurahia sababu barabara ya lami inasaidia kupunguza vumbi, wakati mwingine tunakuwa na migahawa pembeni, k**a barabara ni za vumbi, vumbi yote zinaingia kwenye chakula wateja wanaathirika kutokana na vumbi na vitu k**a hivyo, unapopata barabara za lami mojawapo ya athari za kiafya zinapungua, lakini

Bodaboda nao wachangia milioni  1 kwa ajili ya fomu ya Rais Dkt SamiaMbunge wa Jimbo la Tanga Mjini Ummy Mwalimu amefany...
04/01/2025

Bodaboda nao wachangia milioni  1 kwa ajili ya fomu ya Rais Dkt Samia

Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini Ummy Mwalimu amefanya kikao na viongozi na madereva wa Bodaboda zaidi ya mia tano (500) kupitia Umoja wa Madereva wa Pikipiki na Bajaji  Wilaya ya Tanga (UWAPIBATA) kuzungumzia masuala ya maendeleo ya Bodaboda Tanga Mjini ambapo pamoja na mengineyo Bodaboda kupitia Mwenyekiti wao Mohamedi Chande walimuomba Mh Ummy kuwaunga mkono ili kutunisha Mfuko wao wa  kukopeshana pesa za Leseni kwa Bodaboda. 

Mhe Ummy alikubali ombi hilo na kuwachangia kiasi cha shilingi milioni 10 sambamba na kuwataka bodaboda wengi zaidi kujiunga katika Umoja huo ili kuweza kunufaika na fursa mbalimbali ili kufanya shughuli zao katika mazingira mazuri zaidi.

Wakati huo huo, Bodaboda wa Wilaya ya Tanga kupitia UWAPIBATA wamechangia shilingi miloni moja kwa ajili ya Fomu ya Urais wa Dkt Samia Suluhu Hassan kutokana na kazi nzuri za maendeleo kwa watu wa Tanga ikiwemo maboresho ya Bandari ya Tanga ambao yameongeza fursa za wateja kwa Bodaboda.

Mhe Ummy alimeshukuru Bodaboda kwa kuchangia Fomu ya Rais Dkt Samia Suluhu na amesema kuwa Mh Rais anastahili kutiwa moyo na kuungwa mkono. 

Aidha ameahidi atashirikiana nao bega kwa bega kutafuta kura za Rais Samia na pia kutafuta wadau mbalimbali ili kuboresha shughuli za bodobda. Sambamba na hilo Mhe Ummy alitoa ofa ya mafuta lita mbili kwa bodaboda wote waliohudhuria.

Shughuli hiyo ilihudhuriwa na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga Ndg.Meja mst.Hamisi Mkoba, katibu wa UVCCM Wilaya ya Tanga ndugu Salim Dede, viongozi wa bodaboda wakiongozwa na mwenyekiti wake ndg. Mohamed Chande.

Imetolewa na Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini.

Waziri  wa Ujenzi Abdallah Ulega amewataka Wakala wa Barabara  Tanzania (TANROADS), kuhakikisha unatoa kipaumbele kwa vi...
04/01/2025

Waziri  wa Ujenzi Abdallah Ulega amewataka Wakala wa Barabara  Tanzania (TANROADS), kuhakikisha unatoa kipaumbele kwa vijana wazawa katika ujenzi wa miradi ya barabara inayoendelea nchini ili kupata ajira, kukuza ujuzi na uchumi kwa Watanzania.

Akizungumza na wananchi wa Kata ya Ndungu wilayani Same katika hafla ya kumkabidhi Mkandarasi China Communication Construction Company (CCCC), anayejenga barabara ya Ndungu-Mkomazi KM 36 kwa kiwango cha lami Waziri Ulega amesema ujenzi wa barabara hii itaondoa kero ya usafiri na usafirishaji ya siku nyingi na kuimarisha shughuli za kilimo, utalii na biashara.

“Rais Samia ametoa zaidi ya  bilioni 59 kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii ili kuwakomboa wananchi kiuchumi hivyo ongezeni uzalishaji wa mpunga, tangawizi, ndizi na kukuza biashara kati ya Same, Korogwe na mikoa ya Tanga, Pwani na Dar es Salaam,” amesema Waziri Ulega.

Aidha, amewataka TANROADS kusimamia na kuhakikisha barabara hii inajengwa usiku na mchana kwa ubora uliokusudiwa.

“Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan amenituma Same nije niwatengezee barabara ili mlime tangawizi na mpunga kwa wingi kwa sababu anafahamu ninyi ni wachapakazi,” amesisitiza Ulega.

Amesema inatarajiwa kuwa shughuli za kiuchumi za wananchi wa Same na Korogwe zitaimarika hivyo amemhimiza  Mkuu wa mkoa na mkuu wa wilaya wahamasisheni vijana kuchangamkia fursa katika ujenzi huo.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu amesema ujenzi wa barabara hiyo inayopita kwenye eneo lenye idadi kubwa ya watu wilayani humo itarahisisha maisha na kuibua fursa nyingi za uchumi wa watu wa Same.

Mtendaji Mkuu wa TANROADS Eng. Mohamed Besta amesema barabara ya Ndungu-Mkomazi Km 36 ni sehemu ya barabara ya Same-Kisiwani-Mkomazi yenye urefu wa Km 100.5  ambayo ni barabara ya kimkakati inayounganisha mkoa wa Tanga na Kilimanjaro ambapo km 96.5 ziko mkoa wa Kilimanjaro na Km 4 ziko mkoa wa Tanga hivyo kukamilika kwake kutachochea  shughuli za kilimo, uvuvi, biashara na utalii  katika hifadhi ya mkomazi na milima ya Pare.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Ridhiwani Kikwete ameungana na ndugu, jama...
04/01/2025

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Ridhiwani Kikwete ameungana na ndugu, jamaa na marafiki katika mazishi ya Bw. Ernest Njama Kimaya aliyekuwa Mwenyekiti wa Shirikisho la vyama vya watu Wenye Ulemavu (SHIVYAWATA) na Mjumbe wa Baraza la Taifa la Ushauri Kwa Watu Wenye Ulemavu Leo tarehe 02 Januari, 2025.

Mazishi hayo yamefanyika katika Kijiji cha Mnyuzi Wilaya ya Wilaya ya Korogwe Mkoani Tanga. Akizungumza wakati akitoa salamu za Serikali, Waziri Kikwete alimshukuru Mungu kwa zawadi ya uhai wa Ndg. Kimaya ambaye alianza harakati za kutetea watu wenye mahitaji maalum toka akiwa na miaka 19 miaka ya 1990. Kimaya ambaye amewahi kushiriki katika harakati mbalimbali atakumbukwa kwa kazi nzuri aliyoifanya akiwa Mbunge wa Bunge maalum, mabadiliko ya sera zinazosimamia ustawi wa wenye mahitaji maalum, na mafanikio mbalimbali. Kwa upande mwengine Mh. Rais wa JMT , Dr. Samia Suluhu Hassan alitoa shilingi Milioni 3 k**a rambirambi kwa familia ya Ndg Kimaya zilizopokelewa na Binti yake Elizabeth Kimaya.

Marehemu Kimaya alifariki tarehe 30 Desemba, 2024 Jijini Dar es Salaam katika hospitali ya Ocean Road ambapo alikuwa akipatiwa matibabu.

MBUNGE WA CHALINZE MH.RIDHIWANI KIKWETE AMWOMBEA RAIS SAMIA SULUHU HASSANTumepata nafasi ya kuomba Dua ya kumshukuru Mwe...
02/01/2025

MBUNGE WA CHALINZE MH.RIDHIWANI KIKWETE AMWOMBEA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN

Tumepata nafasi ya kuomba Dua ya kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa zawadi nyingi alizotujaalia katika maisha yetu. Tumemshukuru Mwenyezi Mungu kwa ajili ya uhai , Afya na Neema alizotujaalia. Haya sio kwa Ujanja wetu ni kudra yake.

Tumemshukuru Mwenyezi Mungu kwa ajili ya Rais wetu, Dr. Samia Suluhu Hassan. Tumemshukuru na kumuombea Mh. Rais kwa Uongozi wake wenye mashiko na unaojali wananchi wake. Maendeleo tuliyoyapata, mafanikio yetu k**a Nchi, Utulivu, Amani , na Mshik**ano uliopo yote ni kazi yake Mh. Rais kwa Neema na Vipawa alivyojaliwa na Mwenyezi Mungu. Tunakushukuru Sana Mh. Rais tunapoukaribisha Mwaka mpya na kuendelea kukuombea Mungu.

Tunawaombea kheri wazee wetu, wazazi wetu, watoto na wake zetu . Allah awape huruma, mapenzi , na Malezi mema ili tuendelee kukua na kuleana pamoja.

Tumeiombea Nchi, kupatikane utulivu, Idumu amani na Upendi baina yetu. Tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kila jema analotujalia.

Mwenyezi Mungu atulinde sote na kutujalia amani na utulize. Mwenyezi Mungu ilinde Tanzania, Mwenyezi Mungu mlinde Rais Wetu.

RAIS SAMIA ARIDHIA UPANUZI BARABARA YA RANGI TATU HADI MKURANGAMbunge wa Jimbo la Mkuranga na Waziri wa Ujenzi, Abdallah...
01/01/2025

RAIS SAMIA ARIDHIA UPANUZI BARABARA YA RANGI TATU HADI MKURANGA

Mbunge wa Jimbo la Mkuranga na Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, ametangaza rasmi kuanza kwa mchakato wa upanuzi wa barabara kutoka Rangi Tatu hadi Mkuranga, baada ya kupata kibali kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika Jumanne, Desemba 31, 2024, katika Uwanja wa Shule ya Msingi Mwandege wilayani Mkuranga mkoani Pwani, Ulega amesema kuwa upanuzi wa barabara hiyo umekubalika ili kuondoa msongamano mkubwa unaosababisha adha kwa wananchi wa Mkuranga, Kibiti, Rufiji na maeneo yote ya ukanda wa Kusini.

"Rais Samia amenipa kibali cha upanuzi wa barabara hii na kuniruhusu kutangaza tenda ya kazi hiyo. Tayari fedha zipo, na tunakwenda kuitanua barabara kutoka Rangi Tatu kuja mpaka Kongowe na kuendelea. TANROADS na TARURA Mkoa wa Pwani wapo tayari kuanza kazi," amesema Ulega.

Ulega amebainisha kuwa msongamano katika barabara ya Rangi Tatu (Mkoani Dar es Salaam hadi Kongowe umekuwa kikwazo kikubwa kwa maendeleo ya ukanda wa Kusini hivyo maagizo ya Rais Samia yanaenda kuleta tumaini endelevu kwa watumiaji wa barabara hiyo kutoka Mkuranga.

"Maendeleo yetu yanachelewa sana kwa muda tunaotumia katika eneo hili. Mtu anaweza kuondoka Mkamba mapema, lakini akifika Mwandege kuelekea Kongowe, Dar es Salaam, anapoteza muda wa saa mbili au tatu. Hili lazima lifike mwisho," amesisitiza.

Kwa mujibu wa Waziri Ulega, Rais Samia alimpa jukumu la kuhakikisha tatizo hili linatatuliwa kwa haraka.

"Rais Samia amenituma, amenielekeza na kuniambia, 'Uliomba jambo hili, leo kijana wangu Ulega ninakukabidhi mfupa huo k**alizane nao mwenyewe sasa,' ameeleza Ulega.

*UJUMBE WA MWAKA MPYA 2025 KWA VIJANA WENZANGU WA KITANZANIA*Na Mohamed Ali Kawaida, _Mwenyekiti wa UVCCM Taifa_Ndugu vi...
31/12/2024

*UJUMBE WA MWAKA MPYA 2025 KWA VIJANA WENZANGU WA KITANZANIA*

Na Mohamed Ali Kawaida, _Mwenyekiti wa UVCCM Taifa_

Ndugu vijana wenzangu!

Tukiwa tunaanza safari ya mwaka mpya wa 2025, nipende kutumia fursa hii kuwatakia heri ya mwaka mpya, afya njema, na mafanikio tele. Mwaka mpya ni fursa mpya. Ni ukurasa mwingine wa kitabu cha maisha yetu, kitabu ambacho tunaendelea kukiandika sisi wenyewe kwa bidii na maarifa yetu.

Tunapokabiliana na changamoto mbalimbali, ni muhimu tukumbuke kwamba ushindi wetu haupo katika kushindana na wengine, bali katika juhudi zetu binafsi huku tukiwatakia mema wenzetu. Pia umoja na mshik**ano wetu k**a vijana ndiyo silaha yetu kubwa ya mafanikio.

Katika kipindi cha miaka miwili ya uongozi wangu k**a Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), nimeona kwa macho yangu nguvu, uthubutu, na bidii za vijana wa Kitanzania katika kulijenga taifa letu. Japokuwa changamoto zipo, lakini fursa ni nyingi mbele yetu, fursa ambazo tukiweza kuzitumia vizuri zitabadilisha maisha yetu na kuleta faida katika taifa letu. Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutufikisha hapa tulipo. Nawashukuru pia viongozi wenzangu wa UVCCM kutoka katika ngazi zote taifa hadi matawi na kila mwanachama ambaye amechangia mafanikio yetu.

_Vijana wenzangu, taifa letu linahitaji nguvu zetu, mawazo yetu, na maono yetu_. K**a alivyowahi kusema Nelson Mandela, *“It always seems impossible until it’s done.”* Tusikate tamaa. _Tusirudi nyuma. Kila hatua tunayochukua inachangia kujenga Tanzania yenye haki, maendeleo, na usawa_.

John F. Kennedy aliwahi kusema,
*"Ask not what your country can do for you, ask what you can do for your country."*
Kauli hii inatufundisha kwamba jukumu letu k**a vijana ni zaidi ya kusubiri, bali ni tuna paswa kuchukua hatua leo ili kuleta mabadiliko chanya leo na kesho.

Tunapojipanga kwa mwaka huu mpya wa 2025, ni lazima tuendelee kujitoa kwa bidii katika kazi, elimu, biashara, kilimo, siasa, na shughuli nyingine za uzalishaji. _Kila hatua tunayopiga leo ni msingi wa taifa lenye ustawi, umoja, na heshima kwa vizazi vya leo na kesho_.

*Mwaka 2025 ni mwaka wa ushindi kwa vijana wa Kitanzania pia tukumbuke ni mwaka wa Uchaguzi Mkuu wa Rai

Arusha Tanzania Usiku huu kuelekea Mkesha Mwaka Mpya  #2025    ♥️🎆🎉✨🎈🌹💐❤️❤️❤️👌🤗🙌👏😘🥰❤️❤️❤️🧿💃💃💃
31/12/2024

Arusha Tanzania Usiku huu kuelekea Mkesha Mwaka Mpya #2025

♥️🎆🎉✨🎈🌹💐❤️❤️❤️👌🤗🙌👏😘🥰❤️❤️❤️🧿💃💃💃

TANZANIA MWENYEJI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA HAMASA YA NISHATI SAFI JANUARI 2025.Tanzania inatarajiwa kuwa Mwenyeji wa M...
31/12/2024

TANZANIA MWENYEJI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA HAMASA YA NISHATI SAFI JANUARI 2025.

Tanzania inatarajiwa kuwa Mwenyeji wa Mkutano mkubwa wa Kimataifa kwaajili ya uhamasishaji wa matumizi ya nishati safi duniani, suala ambalo limechagizwa na Utashi wa Rais Samia Suluhu Hassan ambaye amekuwa kinara katika uhamasishaji wa matumizi ya nishati safi Nchini Tanzania na kote barani Afrika.

Kauli hiyo imetolewa leo Disemba 31, 2024 Wilayani Ruangwa mkoani Lindi na Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa, wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Hamasa ya matumizi ya nishati safi kwenye Mkoa huo, akiwataka watanzania kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutumia nishati safi ya kupikia.

Waziri Mkuu akizungumzia Faida ya matumizi ya nishati safi ambayo ni Gesi, Umeme pamoja na makaa ya mawe, amesema Nishati safi inalinda afya ya Watanzania, kulinda mazingira dhidi ya ukataji wa miti pamoja na kutoa ulinzi kwenye nishati endelevu.

WAZIRI MAVUNDE ASIMAMISHA UCHIMBAJI MADINI  KWENYE MTO ZILA KIJIJI CHA IFUMBO, WILAYANI CHUNYA-MBEYAWaziri wa Madini, An...
31/12/2024

WAZIRI MAVUNDE ASIMAMISHA UCHIMBAJI MADINI KWENYE MTO ZILA KIJIJI CHA IFUMBO, WILAYANI CHUNYA-MBEYA

Waziri wa Madini, Anthony Mavunde (Mb) amesimamisha shughuli za uchimbaji zilizokuwa zikifanywa na kampuni ya G & I Tech Mining Company Ltd kwa kipindi hichi cha masika na pia mpaka pale tathmini ya kitaalam ya mazingira itapokamilika juu ya shughuli za uchimbaji madini kwenye Mto Zila.

Ameyasema hayo Jana tarehe 30 Desemba, 2024 katika kijiji cha Ifumbo, Wilayani Chunya alipotembelea eneo la leseni ya mwekezaji ambalo lilivamiwa na wananchi na kusababisha mgogoro mkubwa na uharibifu wa mali za mwekezaji huyo.

"Tumetembelea maeneo yote mawili, na sote tumejionea hali halisi ya mazingira. Ni dhamira na maelekezo ya Mh Rais Dkt. Samia S. Hassan kuona shughuli zote za kiuchumi hususan za madini zinafanyika kwa utulivu bila kuleta migogoro na pasipo kuathiri mazingira ya eneo shughuli zinapofanyika.

Nimesikiliza hoja za wananchi juu ya uharibifu wa mazingira ya Mto Zila,serikali itaunda Timu ya wataalamu kufanya tathmini ya kina ya mazingira juu ya athari zinazoweza kutokea wakati wa uchimbaji wa madini na kwasasa shughuli zote za uchimbaji madini zisimame kipindi hichi cha masika k**a NEMC ilivyoelekeza.

Wizara ya Madini kwa kushirikiana na Watalaam wa Mazingira, wataalam wa Mkoa na wananchi katika muda mfupi ujao inakwenda kuunda Timu ya pamoja ya kufanya tathmini ili itueleze kitaalam iwapo shughuli hizi zinaweza kuendelea kufanyika pasipo athari kwenye mazingira ya Mto Zila.

Nitumie fursa hii kuwataka wananchi wote kuacha vitendo vya uvunjifu wa amani na kujichukulia sheria mkononi,tunalaani kitendo cha kuvamia na kuharibu mali za mwekezaji“Alisema Mavunde

Awali, akitoa maelezo ya utangulizi, Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mh. Mbarak Batenga alishukuru ujio wa Waziri wa Madini na kusisitiza kwamba sasa anaona mwanga ambao unakwenda kuleta s

Address

Arusha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Msumba News Blog posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Msumba News Blog:

Videos

Share