Greataziz

Greataziz Kukubali Kukosolewa na Kujifunza ni Sehemu ya Mabadiliko na Kukua kwa Binadamu

07/06/2024
My Daughter Was Born Today 🎈 More Years of Awesomeness SweetHeart, Dada Mkubwa🥰! Wishing The happiest Birthdays To The B...
10/02/2024

My Daughter Was Born Today 🎈 More Years of Awesomeness SweetHeart, Dada Mkubwa🥰! Wishing The happiest Birthdays To The Beautifu and coolest Daughter❤️ in The universe. Daddy Loves You.

The Garden 🌍 | Mandhari Murua
18/01/2024

The Garden 🌍 | Mandhari Murua

Miaka Inakimbia Sana, Nashukuru Mungu kwa Kuongeza Mwaka Mwingine.Heri Ya Siku Ya Kuzaliwa Kwangu.
01/01/2024

Miaka Inakimbia Sana, Nashukuru Mungu kwa Kuongeza Mwaka Mwingine.

Heri Ya Siku Ya Kuzaliwa Kwangu.

Ukiwa mwanaume fala fala huweziona k**a unateswa na mapenzi, kiuhalisia asilimia kubwa ya wana wanaoteswa na mepenzi ni ...
21/11/2023

Ukiwa mwanaume fala fala huweziona k**a unateswa na mapenzi, kiuhalisia asilimia kubwa ya wana wanaoteswa na mepenzi ni wale ambao.

1. Hawana kipato + insecurity za kuzidi.

2. Hawajui malengo yao ni nini katika maisha.

The later results to the former

K**a haujui malengo yako lazima ukose kuwa na kipato maana asilimia 90 ya malengo ya mwanaume ni kushika pesa.

Lengo likiwa mafanikio yako maana yake utapambana kupata kipato na hautokuwa na insecurity za ajabu.

K**a hauna malengo basi utapambania huyo mwanamke anaekuliza huku ukimuona ni wa maana kuliko hata maisha yako mwenyewe.

Ukipambania malengo yako, Trust me unapoteza energy ya kubembeleza mwanamke kila siku na hapa ndio unapata ile class ya ma broo tunaoambiwa.

UNADHARAU SANA na UNAJIONA SANA.

ThrowBack 2012 🧵🌍 😂 Sema Muda Umeenda Sana.
16/11/2023

ThrowBack 2012 🧵🌍 😂 Sema Muda Umeenda Sana.

*MABORESHO YA MITAALA AMBAYO YANAENDA KUBADILISHA MFUMO WETU WA ELIMU*1. Mtihani wa darasa la saba utafutwa. Mwanafunzi ...
06/11/2023

*MABORESHO YA MITAALA AMBAYO YANAENDA KUBADILISHA MFUMO WETU WA ELIMU*

1. Mtihani wa darasa la saba utafutwa. Mwanafunzi akianza darasa la kwanza lazima amalize kidato cha nne.

2. Kutakuwa mtihani wa upimaji wa kitaifa wa darasa la sita (Standard Six National Assessment).

3. Mwanafunzi atatakiwa asome fani fulani kabla hajamaliza kidato Cha nne ili aweze kujiajiri au kuajiriwa baada ya kumaliza.

4. Lugha ya kufundishia na kujifunzia itakuwa kiswahili, Kiingereza kitakuwa K**a somo kwa shule za Kiswahili medium na lugha ya kufundishia English, kiswahili kitakuwa K**a somo kwa shule za English medium.

5. Elimu ya msingi itakuwa miaka 6. Mwanafunzi ataanza darasa la kwanza akiwa na miaka 6, tofauti na ya sasa miaka 7.

7. Elimu ya awali mwanafunzi ataanza akiwa na miaka 5.

8. Masomo ya elimu ya msingi yatakuwa K*K, Jiografia, kiswahili, Sanaa na michezo, hisabati, sayansi, historia ya Tanzania na maadili, dini na kiingereza na stadi za kazi itachopekwa.

9. Kiingereza kitafundishwa kuanzia darasa la kwanza kwa shule za Kiswahili na kiswahili kitafundishwa kuanzia darasa la kwanza kwanza kwa shule za kiingereza.

10. Shule zenye uwezo zitafundisha walau somo moja la lugha za kigeni k**a kichina au kifaransa.

11. Sekondari kutakuwa na mikondo 2, mkondo wa jumla na amali (ufundi). Mwanafunzi atachagua kutokana na
uwezo, matakwa na malengo yake ya badae.

12. Mkondo wa amali (ufundi) utakuwa na fani za:
-kilimo na ufugaji
-umakenika
-biashara na ujasiriamali
-sanaa bunifu
-elimu ya michezo
-ufugaji wa nyuki
-uchimbaji wa madini
-urembo

13. Mwanafunzi wa mkondo wa amali atatakiwa kuchukua masomo manne (4) ya jumla na moja la fani.

14. Masomo ya jumla la wanafunzi wa amali ni:
-hisabati
-elimu ya biashara
-kiingereza
-historia ya Tanzania na maadili

15. Wahitimu wa amali watapata vyeti viwili yaani:
-cheti cha ujumla cha elimu ya sekondari (NECTA)
-cheti cha amali (NACTVET)

16. Kila shule itakuwa na wakala wa VETA ili kusimamia maswala ya ufundi.

17. Kila shule haitakuwa na mikondo zaidi ya miwili ya ufundi, hii ni kwaajili ya ufanisi na fani ziwe zinaendana na fursa za eneo husika.

18. Kutaanzishwa somo jipya la mawasiliano ya kitaaluma (academic communication) katika A-level na ualimu.

19. Coding itafundishwa shule ya msingi.

20. Information and Computer Studies (ICS) itabadilishwa na kuitwa Computer Science. Somo limesukwa upya.

21. Civics itaunganishwa na historia ya Tanzania na maadili kwa O-level.

22. O-level masomo ya lazima yatakuwa 6 badala 7 ya Sasa.

23. Katika O-level masomo ya Biology na Geography yatakuwa masomo ya kuchagua pia kwasababu maudhui yake yamekuwa kwenye masomo ya jiografia na sayansi ya shule ya msingi kwa mfano afya ya jamii, afya ya uzazi, magonjwa ambukizi nk.

24. Civics, maarifa ya jamii, uraia na maadili yamefutwa. Maudhui yake yameingia katika somo la historia ya Tanzania na maadili.

25. General Studies (GS) katika A-level itafutwa na maudhui yake yatawekwa katika somo la historia ya Tanzania na maadili na mawasiliano ya kitaaluma.

26. Kufuta baadhi ya masomo kumefanyika ili kuondoa tatizo la kujirudia rudia kwa maudhui.

27. Michepuo katika elimu ya O-level imeongezeka kutoka minne (4) hadi tisa (9). Michepuko iliyoongezeka ni:
-sanaa
-lugha
-muziki
-michezo
-TEHAMA

28. Masomo ya O-level yatakuwa:
-biology
-physics
-chemistry
-history
-geography
-historia ya Tanzania na maadili
-hisabati
-kiswahili
-english
-elimu ya biashara
-utunzaji wa taarifa za fedha
-computer science
-bible knowledge
-elimu ya dini ya kiislamu etc

29. Astashahada ya ualimu itafutwa kisha itaanzishwa Stashahada (diploma) ya elimu ya awali, ualimu wa msingi na ualimu wa elimu maalumu. Watakaosoma Stashahada watakuwa waliomaliza kidato cha sita na itasomwa kwa miaka miwili.

30. Walimu wa sekondari wote watakuwa na Shahada (degree). Kwasababu nchi nyingi ndio wanaenda muelekeo huu.
31. Vyuo vilivyokuwa vinatoa Stashahada (diploma) ya ualimu wa sekondari vitatumika kutoa continuous professional development.

Una Maoni Gani Kuhusu Maboresho Haya, Je Unadhani Yataleta Tija kwenye Elimu Yetu....!?

03/11/2023

LEO NAKUSHUSHIA BAADHI YA BIASHARA UNAZOWEZA KUFANYA KWA MTAJI MDOGO TU.

✒️ BUSINESS PLANS | MONEY MAKER

1. Advertiser Magazine Case Study & Fact Sheet
2. Agrovet Business Guide
3. Bank Agency Factsheet
4. Beef Butchery Guide
5. Boda Boda Info Pack
6. Bookshop Quick Guide
7. Bottled Water Business Guide
8. Building Materials Yard - Dynamics and Case Study
9. Car Wash Business Guide
10. Chapati Wholesale Case Study
11. Chemist Retail Business Guide
12. Chicken Butchery Guide
13. Chips and Chicken Guide
14. Cookie Mania
15. Corn Chips Quick Guide
16. Cosmetics Retail Business Guide
17. Courier Guide
18. Cyber Cafe Guide
19. Daycare Guide
20. Electrical Parts Retail Guide
21. Executive Barber Shop Guide 2018
22. Feasibility of Cooking Oil Filtering Service
23. Fish Supply to Hotels – Nairobi
24. Flower Business In Nairobi
25. FMCG Small Scale Distribution Quick Guide
26. Free Advertiser Magazine Quick Guide and Case Study
27. Fruit and Juice Parlour Guide
28. Gas(LPG) Retail Guide 2018
29. Gift Services Overview
30. Greenhouse Tomato Guide - Prodution & Market
31. Gym Business Guide
32. Hair Salon Plan
33. Handbag Rental Feasibility
34. Ice Lollies Quick Guide
35. Informal Money Lending Guide
36. Innerwear Quick Guide
37. Keg Bar Business Guide
38. Laundry Business Guide
39. Leather - Skin Trade
40. Local Bar Business Guide
41. Milk Distributorship & Industry Overview
42. Mitumba Retail Guide
43. Motorcycle Spare Parts Retail Guide
44. M-pesa Sub Agency Guide
45. Nails Making Guide
46. Non Woven Bags Making Guide
47. Paint Mixing Business Guide
48. Petrol Station (Independent) Guide
49. Plumbing Hardware Business Guide 2018
50. Pork Butchery & Eatery Guide 2018
51. Printing Business Guide 2018
52. Quick Guide To Supermarket Shelf Space
53. Second Hand Novels Guide
54. Sifted Maize Flour Guide
55. Slot Machines Quick Guide
56. Smokies & Eggs Vending Guide
57. Tents & Chair Leasing Business Guide
58. The Cake Packaging
59. Tiles Retail Business Guide
60. Timber Retail Business Guide
61. Wines and Spirits Retail
62. Sacco's and chamas
63. How to start a business from scratch.
64.Most 200 profitable business in Tanzania.
65. Import business in Tanzania
66.Bank agents business

Jaribu Biashara Mojawapo Kati ya Hizi.

Usidanganywe kufanya jambo lolote la kijinga kwa kutumia    ya "Sijali watu wanasema ninaishi maisha yangu" Ndio huwezi ...
14/10/2023

Usidanganywe kufanya jambo lolote la kijinga kwa kutumia ya "Sijali watu wanasema ninaishi maisha yangu" Ndio huwezi kumfurahisha kila mtu na huwezi kuishi maisha yako kufikia viwango vya kila mtu lakini kuwa na sifa nzuri bado ni jambo jema.

Ukiwa Angani, unaona Nyumba ndogo k**a size ya tofali na ukiwa chini kwenye nyumba unaona ndege ndogo k**a size ya njiwa...
10/10/2023

Ukiwa Angani, unaona Nyumba ndogo k**a size ya tofali na ukiwa chini kwenye nyumba unaona ndege ndogo k**a size ya njiwa.

Ndivyo matatizo yalivyo,tatizo linaonekana dogo kwa kadri linavyo kuwa mbali na wewe... likikufikia ndo unaona ukubwa wake halisi.

ELIMU YA MIKOPO BENKIKumekuwa na malalamiko na vilio kwa baadhi ya watumishi kuhusu mikopo wanayopewa na benki. Wengi wa...
30/09/2023

ELIMU YA MIKOPO BENKI

Kumekuwa na malalamiko na vilio kwa baadhi ya watumishi kuhusu mikopo wanayopewa na benki.

Wengi wao wanalaumu mikopo hiyo kuwa ni kandamizi kwao badala ya kuwapa unafuu imegekuka kuwakandamiza na kuyafanya maisha yao kuwa magumu.

Hapa tatizo sio mikopo inayotolewa na benki bali shida ipo kwenye elimu juu ya namna bora ya kukopa.

Kwa kukosa elimu hiyo, mtumishi wa umma unapokwenda kukopa benki afisa mikopo atakupa chaguo (option) ambalo litakuwa na faida zaidi kwa benki.

Mfano,
Mtumishi mwenye mshahara wa
Tsh.700,000/=baada ya makato
(take home)

Kwa mtumishi asiyekuwa na elimu ya mikopo, akifika benki atamuuliza afisa mikopo kwa mshahara wa laki 7 naweza kukopa kiasi gani??

Hapa afisa mikopo atakachoangalia kwanza ni chaguo lipi litaingizia benki faida kubwa zaidi!

Atapiga mahesabu, kuzingatia sheria ya 1/3 ya mshahara ibaki kwa mtumishi , atapata 2/3 ya 700,000/= ni k**a 466,666.67 hivi.

Sasa chukulia hapo muda wa chini uwe miaka mitano.

Atakwambia una uwezo wa kukopa hadi 19M, makatao yote itakuwa sawa na Tsh. 443,000 kwa mwezi.

Mtumishi asiyekuwa na elimu ya mikopo akiangalia mshahara wake anajikuta inabakisha 270,000.
Anamuuliza afisa mikopo nikichukuwa hiyo 19M kwa miaka nane je?

Anaambiwa ukichukuwa hiyo 19M kwa miaka nane kila mwezi utakatwa 325,000 na utabakiwa na 375,000/= kila mwezi.

Mtumishi asiye na elimu hii anakubali kuchukuwa 19M kwa miaka nane kwa sababu tu makato ni madogo.

*USICHOKIJUA SASA*

1. Ukichukuwa mkopo wa 19M kwa miaka
mitano marejesho yako ya Tsh 443,000/=
kila mwezi kwa miaka 5 ni sawa na
Tsh. 443,000×12×5= 26,580,000/= na hivyo
mkopo huo utakuwa umeipatia benki faida
ya Tsh 7,580,000.

2 Ukichukuwa kwa 19m kwa miaka nane kwa
marejesho ya Tsh. 325,000/= kila mwezi
utakuwa na jumla ya marejesho
Tsh. 325,000 ×12×8= Tsh.31,200,000/=
hivyo utaipatia benki faida ya 12,200,000.

K**a mkopo huu lengo lake kubwa ikiwa ni kuendeleza ujenzi wa nyumba, kwa hiyo unachukuwa hiyo 19M ndani ya miaka nane anaishia kwenye kufunga linta.

*KUMBE BASI*
Tunalopaswa kulielewa kwa sisi watumishi wa umma ni kuwa
-🖍Mkopo unaozidi miaka miwili na nusu hapo ni
kujiumiza wenyewe.

-🖍Mtumishi wa umma jitahidi ukope kwa
awamu mgawanyiko zenye muda mfupi
mfupi ili upate unafuu na uifurahie ajira yake.

Chukulia hii 19M ambayo mtumishi mwenye take home ya 700,000 ambaye alichagua kukopa kwa miaka nane, njia bora ni kuanza na 9.5M kwa miaka miwili na nusu tu ambapo atatakiwa kulipa 11.5M kwa makato ya 380,000 kwa mwezi. Riba ya miaka miwili na nusu atakuwa around 1,900,000.

Baada ya kuisha miaka miwili na nusu anachukuwa 9.5M nyingine.
Hapo riba ya miaka mitano itakuwa ni 3,800,000 badala 7,600,000 kwa muda ule ule wa miaka mitano.

Mwisho usikope kwa kufuata mkumbo.
Weka mipango yako kwa awamu ili kuweza kuitekeleza bila maumivu makali

HII ELIMU NI MKOMBOZI WA WATUMISHI
TAFADHALI SHARE NA WENGINE WANUFAIKE

Don’t Be Scared To Start Over, You Might like Your New Story Better.
04/09/2023

Don’t Be Scared To Start Over, You Might like Your New Story Better.

Don’t Be Scared To Start Over, You Might Like Your New Story Better
03/09/2023

Don’t Be Scared To Start Over, You Might Like Your New Story Better

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Greataziz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

  • Address
  • Alerts
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share

Maisha Ni Safari

Amigos Uthubutu Unakuja Pale Unaporuhusu Wazo Linalokuumiza Kichwa Likuumize Na Mikono Kulitimiza. Pindi Unapoanza Kuona Thamani Yako Utagundua Ni Vigumu Sana Kuendelea Kukaa Na Wasio Jithamini. MUNGU Akikupa Utajiri Wa Mali, Jitahidi Kuwa Maskini Wa Roho Waone Wasio Na Mali Kuwa Bado Binaadamu Wa Thamani Wewe Haukuzaliwa Navyo.

#BusaraZaMtaani #hekima #hekimayamtaani #busara #greataziz1 #greataziz