Neno Litaendelea

Neno Litaendelea Neno Litaendelea (TTB Swahili) is a bible teaching (Gen- Rev) program from Trans World Radio Kenya.

Karibu kwa Safari ya Maandiko Inayoangazia Ukweli wa Neno la MunguJiunge nasi katika safari ya Biblia iliyojaa ufunuo, n...
04/06/2025

Karibu kwa Safari ya Maandiko Inayoangazia Ukweli wa Neno la Mungu
Jiunge nasi katika safari ya Biblia iliyojaa ufunuo, neema, na nguvu ya kiroho, ukiwa pamoja na Mchungaji Geoffrey Wanjala Munialo ana Dada Pamela Omwodo watumishi waliyeitwa kufundisha kwa uaminifu na uongozi wa Roho Mtakatifu.

πŸ“– β€œNeno lako ni taa ya miguu yangu, Na nuru ya njia yangu.”
Zaburi 119:105

Sikiliza Neno Litaendelea kila Jumatatu hadi Ijumaa Kupitia SIFA 107.7 FM VOI na Sifa FM Lamu saa 12:05 Asubuhi,
SIFA FM 101.1 ATOO, SIFA FM Marsabit SIFA FM Hekima - "Sauti Ya Busara" saa 11:00 Asubuhi

Neno Litaendelea  ni kipindi cha kiroho kinacholenga kufunza kwa kina Maandiko Matakatifu. Kipindi hiki hutoa mafundisho...
13/05/2025

Neno Litaendelea ni kipindi cha kiroho kinacholenga kufunza kwa kina Maandiko Matakatifu.
Kipindi hiki hutoa mafundisho ya Biblia yaliyo sahihi, yanayoeleweka kwa urahisi, na yanayohusiana na maisha ya kila siku.

Kila sehemu huongoza wasikilizaji kuelewa Neno la Mungu kwa uwazi na ukweli, na kuwasaidia kukua kiimani na kulitumia Neno hilo katika maisha yao ya kila siku..

πŸ‘‰ Je, unakisikiliza kipindi hiki kupitia kituo gani? Tuandikie hapo chini!

πŸ‘‰ Je, unakisikiliza kipindi cha Neno Litaendelea  kupitia kituo gani? Tuandikie hapo chini!Neno Litaendelea.......... ni...
13/05/2025

πŸ‘‰ Je, unakisikiliza kipindi cha Neno Litaendelea kupitia kituo gani?
Tuandikie hapo chini!

Neno Litaendelea.......... ni kipindi cha kiroho kinacholenga kufunza kwa kina Maandiko Matakatifu.

.................

Neno Litaendelea sasa lina endelea kubariki wengi kwa lugha ya Kiturkana
12/05/2025

Neno Litaendelea sasa lina endelea kubariki wengi kwa lugha ya Kiturkana

30/04/2025

Hata maneno yanapokosekana, Mungu husikia sauti ya moyo wako. πŸ’›πŸ™

❗️❗️❗️ Wasikilizaji wa Neno Litaendelea na vipindi vingine kutoka Trans World Radio Kenya kupitia kituo cha SIFA 107.7 F...
24/04/2025

❗️❗️❗️ Wasikilizaji wa Neno Litaendelea na vipindi vingine kutoka Trans World Radio Kenya kupitia kituo cha SIFA 107.7 FM VOI wa andaa mkesha wa SIFA Night.

"Kila sauti ilipoimba, anga lilibadilika, mioyo ilifunguka, mikono ikainuliwa, na mbingu zikajibu. Kile kilichoishi tu kwenye mawimbi ya redio sasa kilikuwa hai ana kwa ana: injili, halisi na ya dhati, ikitamba kanisani na kusikika hadi usiku kucha. Kanisa halikuweza kuwatosha waumini. Waabudu walijaa hadi nje, wakiwa wamesimama chini ya mwanga wa mwezi, wameunganishwa na kiu ya uwepo wa Mungu.........endelea kusoma ↓↓
https://sifafm.co.ke/usiku-wa-sifa-kijiji-cha-sofia-chamulika-kwa-ibada/?

Tangu wimbo wa kwanza ulipopaa k**a uvumba kuelekea mbinguni, sauti ziliungana kwa sifa, maombi yakapiga ngurumo angani, na mioyo ikaelekezwa tena kwa...

22/04/2025

Kwa mioyo yenye huzuni, sisi katika shirika la K- Trans World Radio Kenya watayarishi wa kipindi cha Neno Litaendelea pamoja na vituo vya redio vya SIFA FM tunaungana na familia ya Kikristo duniani kote kuomboleza kifo cha Papa Francis, aliyeitwa na Bwana saa chache tu baada ya kutoa baraka zake za mwisho za Urbi et Orbi katika Uwanja wa Mtakatifu Petro. (Video hapa chini)

Papa Francis alikuwa mchungaji wa kweli wa amani, aliyeongoza kwa unyenyekevu, huruma, na imani isiyotetereka. Sauti yake iliwatetea kwa ujasiri maskini, waliopuuzwa, na umoja katika Kristo.

Tunapotafakari maisha na urithi wake, tunawaombea faraja na nguvu ndugu zetu Wakatoliki duniani kote. Mfano wake na uendelee kututia moyo kuenenda katika upendo na huduma.

"Heri wale wanaoomboleza, kwa kuwa watafarijika." β€” Mathayo 5:4

πŸŽ₯ Video kwa hisani ya Vatican News

"Neno Litaendelea" ni kipindi cha kila siku kinacholenga kuwafundisha wasikilizaji Neno la Mungu kwa undani na ufunuo wa...
07/04/2025

"Neno Litaendelea" ni kipindi cha kila siku kinacholenga kuwafundisha wasikilizaji Neno la Mungu kwa undani na ufunuo wa kiroho.

Kupitia mafundisho ya Biblia, kipindi hiki huleta matumaini, imani, na kuelewa kwa kina kuhusu ahadi na upendo wa Mungu. Kikiwa kina pepea kupitia vituo vya Sifa FM kila siku ya wiki.

Jiunge naye Pamela Omwodo na Mchungaji Geoffrey Wanjala Munialo na ujifunze mengi.

Na Neno Litaendelea .............................

19/03/2025

: Mithali 21- Moyo wa binadamu..

na Neno Litaendelea

13/03/2025

Florence Wangare ni Mwalimu wa Sunday School na ni Msikilizaji wa Neno Litaendelea kupitia SIFA FM Marsabit. Mwalimu Florence akiri kuwa kando na kipindi kumjenga kiimani kimekuwa k**a daraja ya kumwezesha kufikisha mafundisho kwa watoto wa Sunday School. Hivyo basi hata kwa watoto bado Neno Litaendelea

Je unasikiliza Neno litaendelea, na una ushuhuda ? tuma ujumbe kupitia inbox au [email protected]

Kwa habari kuhusu huduma na jinsi kazi ya Bwana linaendelea soma jarida la TWR K- Trans World Radio Kenya
07/03/2025

Kwa habari kuhusu huduma na jinsi kazi ya Bwana linaendelea soma jarida la TWR K- Trans World Radio Kenya

This quarter, we’ve witnessed incredible growth, both in our programs and in the lives touched by the message of Christ. We’re excited to share these stories with you, as...

26/02/2025

Ushuhuda wa huduma

Address

Producer Neno P. O. Box 21514 Nairobi
Nairobi
00505

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Neno Litaendelea posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Neno Litaendelea:

Share

Category