Neno Litaendelea

Neno Litaendelea Neno Litaendelea (TTB Swahili) is a bible teaching (Gen- Rev) program from Trans World Radio Kenya.

Kadri mwaka unavyokaribia kuhitimishwa, tunamshukuru Mungu kwa uaminifu wake na kusherehekea msaada thabiti wa washirika...
17/12/2025

Kadri mwaka unavyokaribia kuhitimishwa, tunamshukuru Mungu kwa uaminifu wake na kusherehekea msaada thabiti wa washirika wetu wanaofanikisha huduma hii, pamoja na nguvu ya jamii tunazoshirikiana nazo kote Kenya na kwingineko.

Toleo hili jipya la jarida letu linaangazia simulizi zenye kugusa mioyo, maisha yaliyobadilika, familia zilizoimarishwa, na jamii zilizoinuliwa kupitia utangazaji unaozingatia imani na programu za maendeleo za Trans World Radio Kenya na SIFA FM. Kila hatua ya mafanikio inaakisi kujitolea kwa timu yetu na imani ya washirika wanaotembea nasi katika safari hii.

Kuanzia Kakuma na Lodwar hadi Marsabit, Garissa, Wajir, Mandera, Voi na Lamu, ushirikiano wenu unawezesha ujumbe wa tumaini kufika kuvuka mandhari na mipaka.

Karibu utembee nasi tunapoendelea kusambaza tumaini, utangazaji mmoja kwa wakati mmoja.

📖 Soma au Pakua Jarida kupitiahttps://twr.co.ke/wp-content/uploads/2025/12/Trans-World-Radio-Kenya-Newsletter-Issue-2-2025-.pdf

❗️❗️ USHUHUDA WA  NENO LITAENDELEA Wakati wa safari ya hivi karibuni kutoka Mombasa hadi Nairobi, mmoja wa wafanyakazi w...
10/12/2025

❗️❗️ USHUHUDA WA NENO LITAENDELEA
Wakati wa safari ya hivi karibuni kutoka Mombasa hadi Nairobi, mmoja wa wafanyakazi wetu alikutana na msikilizaji ambaye alionekana mwenye furaha kubwa alipojua kuwa huyo mfanyakazi anahudumu katika shirika inayotayarisha kipindi cha Neno Litaendelea. Akiwa amejawa na shangwe, alijitambulisha k**a Cheruyiot kutoka Bonde la Ufa na huu hapa ni ushuhuda wake.

“Neno Litaendelea ni miongoni mwa vipindi vinavyosikilizwa sana katika Bonde la Ufa. Kinatia moyo, kinafundisha, na kututia nguvu kila siku. Nimefuatilia kipindi hiki kwa muda mrefu, na kupitia safari hii ya kupitia Biblia, nimejifunza kutokata tamaa. Mungu ametumia kipindi hiki kuninenea moyoni.”

“Mungu awabariki Pastor Geoffrey Wanjala Munialo na Sister Pamela Omwodo. Nikikutana nao leo, sijui hata ningewapa nini kuwalipa kwa yale ambayo huduma yao imefanya katika maisha yangu.”

“Huko Kericho, ambako wengi ni wakulima wa majani chai, unawakuta watu wakifanya kazi mashambani wakiwa wamewasha redio, wote wakisikiza kipindi hicho hicho, japokuwa kupitia vituo tofauti. Hata wamepanga kazi zao kulingana na muda wa matangazo. Hii ni ya kipekee, na inaonyesha kuwa Neno Litaendelea linabadilisha maisha kwa kulifundisha Neno la Mungu, kutoa tumaini na kutia mioyo nguvu.”

“Trans World Radio Kenya, nawaheshimu sana nawavulia kofia.”

🙏 Tunamshukuru Mungu kwa ushuhuda k**a wa Vincent.
Neno Litaendelea linaendelea kugusa maelfu kote Kenya, likifundisha kwa uaminifu Maandiko kuanzia Mwanzo hadi Ufunuo na kuleta tumaini katika nyumba, mashamba na mioyo ya watu.

Utukufu kwa Mungu pekee. Na Neno Litaendelea!

02/12/2025

Aliyekuwa Meneja Mkuu wa vituo vya Sifa FM Pamela Omwodo akizungumza wakati wa hafla ya kumuaga Mwanzilishi wa vituo vya Sifa Fm nchini Kenya ambaye pia amehudumu k**a Mkurugenzi Mkuu wa TWR K- Trans World Radio Kenya Dr.Bernice Gatere.

😍💃🎊 ASANTENI KWA KUFANYA TUKIO HILI LISILOSAHULIKA❗️ 🎊 (Picha Kwa Wingi)Ilikuwa alasiri ya heshima, furaha na kumbukumbu...
01/12/2025

😍💃🎊 ASANTENI KWA KUFANYA TUKIO HILI LISILOSAHULIKA❗️ 🎊 (Picha Kwa Wingi)

Ilikuwa alasiri ya heshima, furaha na kumbukumbu tamu tuliposherehekea safari ya huduma ya zaidi ya miaka 30 ya Dkt. Bernice Gatere katika TWR Kenya na Sifa FM. Asante kwa wote mliohudhuria, na kwa waliotuma salamu na kuomba radhi—tulihisi upendo wenu.

Hatugeweza kuwaleta wote ukumbini, lakini msijisikie mmetengwa. Ninyi bado ni familia ya TWR Kenya & Sifa FM.

Ukumbi ulijaa familia, marafiki, wafanyakazi wa sasa na wa zamani, bodi ya sasa na iliyopita, washirika wa huduma na hata tukapata kujuimuika tamu kwa waliostaafu awali. Tunawashukuru pia Mchungaji Geoffrey Wanjala Munialo na Dada Pamela Omwodo wa Neno Litaendelea kwa uwepo wao.

Tulicheka, tulilia, na tukajawa na shukrani tukisherehekea urithi wa imani na utumishi. Dkt. Njoki alituhakikishia kuwa mwanga huu wa huduma utaendelea kung’aa.

Tuliwaheshimu pia wajumbe wa Bodi wanaostaafu:
Rev. Ambrose Nyangao–EBS, Bw. Morris Peter Kinyanjui, Bw. Jomo Gatundu, na Bi. Stella Mutegi.

💙📻 Urithi uendelee, na huduma isonge mbele!

27/11/2025

Big Opportunity for Creative Teams!
Trans World Radio (TWR) Kenya will mark 50 years in 2026, and we’re seeking a professional production team to create a 50th Anniversary Documentary and Commemorative Coffee Table Book.

If your company excels in impactful storytelling, high-quality visuals, and meaningful projects, we invite you to submit your proposal.
Join us in capturing five decades of hope, faith, and transformation across Kenya.

For more information visit
https://lnkd.in/dyRHxxhy

👉 For more information visit https://twr.co.ke/request-for-proposals-documenting-five-decades-of-broadcasting-hope-in-kenya/

24/11/2025

SIFA NA KAZI
Ayubu anaonyesha uaminifu wa Mungu kupitia mateso na urejesho. Tuma maoni/ushuhuda kwa 0724 601 810
^MK
Neno Litaendelea
Africa Gospel Church, Kenya - AGC

📛 Kwenye Kivuli cha Vifo vya Shakahola: Wakati Redio Ilipogeuka Kuwa U*i wa U*ima wa Ukweli 📻♨️Kutoka kwa makaburi ya Sh...
05/11/2025

📛 Kwenye Kivuli cha Vifo vya Shakahola: Wakati Redio Ilipogeuka Kuwa U*i wa U*ima wa Ukweli 📻

♨️Kutoka kwa makaburi ya Shakahola hadi kwenye misitu ya Kwa Bi Nzaro, maumivu ya udanganyifu bado yapo lakini pia kuna tumaini. Kupitia Trans World Radio Kenya na SIFA FM, vipindi k**a Neno Litaendelea (Thru the Bible), Matumaini Heralds of Hope, Dorothy’s Devotion na Jamvi la Gumzo vinafanya zaidi ya kutangaza tu, vinaokoa maisha.

🔘Familia ambazo hapo awali zilikuwa zimefungwa katika mafundisho ya uongo sasa zimesimama imara katika ukweli wa Neno la Mungu.
Waendeshaji na wapanda pikipiki, akina mama, na vijana wanagundua kwamba imani ya kweli huleta uzima si kifo.

Katika moyo wa Kwa Bi Nzaro, tunakutana na John Mjimba, msikilizaji ambaye simulizi lake linatukumbusha kuwa ukimya ni hatari, na kwamba fundisho sahihi huokoa maisha.

❗️Soma ushuhuda wenye nguvu wa John kupitia kiungo hiki 👇

The tragedy of Shakahola and Kwa Bi Nzaro reminds us that silence is deadly. Where truth is absent, deception thrives. Where the Gospel is not taught, false prophets rise.

01/11/2025

🌟 Hello November! A Month of Purpose, Passion & Possibilities! 🌟
“As we step into November, let’s run with purpose! Together, we can shape a generation through the SIFA FM SIFA 107.7 FM VOI Super Cup. Where talent meets hope, and hope wins. Join us in making the difference!” ⚽

The SIFA FM Super Cup happening December 1-6 is more than just football, it’s a movement that brings together youth, communities, and listeners across our regions to inspire hope, nurture talent, and promote positive change.

💪 Why it Matters:
⬛️It provides a platform for young people to showcase their God-given talents.
🟩It strengthens community bonds through healthy competition and mentorship.
🟦It connects thousands of fans, listeners, and brands in a celebration of unity and purpose.

🤝 How You Can Be Part of It: ❗️
🔘Partner or Sponsor through our Gold, Silver, or Bronze packages and position your brand before thousands of passionate fans.

🔷Give in-kind support equipment, merchandise, refreshments, or services are welcome!

🔶Sign up for exhibition space to showcase your products or services to a diverse audience during the tournament.

Let’s make this November one to remember. One where faith, community, and football come together to inspire hope!

📞 For partnership and exhibition opportunities, contact us via email [email protected] or or call 0734 939928 today.

💢🎙 Na….. Neno Litaendelea 📻❗️Tangu mwaka 1992, Neno Litaendelea (Thru The Bible – Swahili) limeendelea kugusa maisha ya ...
24/10/2025

💢🎙 Na….. Neno Litaendelea 📻

❗️Tangu mwaka 1992, Neno Litaendelea (Thru The Bible – Swahili) limeendelea kugusa maisha ya watu wengi katika vizazi mbalimbali, likiwaongoza wasikilizaji kwa uaminifu kupitia Maandiko Matakatifu kuanzia Mwanzo hadi Ufunuo.

Kuanzia siku za awali kwenye Redio KBC na TWR Shortwave, hadi sasa kupitia majukwaa mengi ikiwemo Sifa FM inayofikia maeneo mengi ndani na nje ya Kenya, ujumbe umebaki ule ule. Neno la Mungu halitarudi bure.
Maisha yamebadilishwa, imani imeimarishwa, na tumaini limefufuliwa katika familia nyingi barani Afrika na kwingineko.

Faida hii kubwa imewezekana kupitia ushirikiano wenye nguvu kati ya Trans World Radio na Thru The Bible (TTB) mashirika mawi zilizounganishwa na dhamira moja: kufikisha Neno la Mungu mpaka miisho ya dunia.

Hivi karibuni tulipata heshima ya kuwapokea timu kutoka TTB, tukijadiliana njia mpya za kuimarisha na kupanua ushirikiano huu ili kuhakikisha Injili inaendelea kuwafikia watu kwa lugha wanayoielewa vyema zaidi.

🎤Katika TWR Kenya, tumebarikiwa kuwa na timu yenye kujitolea ya wataalamu wa vyombo vya habari na washirika wa huduma wanaofanya kazi bila kuchoka kutengeneza vipindi vya kimaandiko na kimaendeleo vinavyotoa taarifa, kuhamasisha, na kubadilisha maisha.

Tukiwa na uzoefu wa zaidi ya miaka 49 katika utangazaji, tupo tayari kuhudumia huduma za injili, makanisa, na mashirika yanayotamani kuleta athari kamili katika jamii.

🤝 Tunakuarika kushirikiana nasi. Pamoja, tunakuza ujumbe.
Pamoja, tunaleta faida ya milele. 🎙💢

📧 Wasiliana nasi leo: [email protected] 🌐 Tembelea: www.twr.co.ke

❗️❗️ Mzunguko Kamili wa Huduma  🎙️🎙️Mwaka 1987, kijana aitwaye Ruben Kigame alitembelea studio za TWR K- Trans World Rad...
10/10/2025

❗️❗️ Mzunguko Kamili wa Huduma 🎙️🎙️

Mwaka 1987, kijana aitwaye Ruben Kigame alitembelea studio za TWR K- Trans World Radio Kenya kurekodi albamu yake ya kwanza kabisa ya injili: “What a Mighty God We Have.” ♫♫

Wakati huo haukuzaa tu muziki wa kudumu, bali pia ulizindua huduma ambayo imegusa mioyo ya watu wengi vizazi hadi vizazi.

Miaka 38 baadaye, Dkt. Ruben Kigame amerejea tena. Safari hii kupitia mitambo ya redio ya SIFA FM, mojawapo ya huduma za redio za TWR Kenya. Katika mahojiano ya kugusa moyo, alishiriki safari yake kutoka ulimwengu wa muziki hadi kwenye uongozi wa kitaifa na hamu yake ya kuhudumia Kenya k**a Rais wa Sita mwaka 2027.

Alizungumza kwa msisitizo kuhusu maadili yanayomwongoza : imani, uadilifu, na haki. Pamoja na maono yake ya kuona Kenya isiyo na ufisadi, upendeleo, na ukosefu wa ajira kwa vijana.
Aidha, aliweza kujibu maswali kutoka kwa wasikilizaji kupitia kipindi “Miereka ya Siasa” kinachoendeshwa na Lion Obimbo na Ian Odhiambo.

“Sauti kuu ya busara lazima isikike. Kizazi hiki na kijacho vinastahili nchi iliyobadilika. Mabadiliko yanaanza na sisi,” alisema.

Kwetu sisi TWR Kenya, ilikuwa ni ukumbusho wenye nguvu kwamba mbegu zilizopandwa kupitia utangazaji wa injili bado zinaendelea kuzaa matunda hadi leo.

Kutoka kurekodi nyimbo za imani hadi sasa kuzungumza kuhusu mageuzi ya taifa, ujumbe wa Mungu wa tumaini unaendelea kudumu. 🙏

Iwe ni kupitia muziki, mahubiri, au programu za kijamii na kimaendeleo, TWR Kenya itaendelea kujitolea kubadilisha maisha na kutangaza Habari Njema kwa vizazi vyote.

📻 “Kuzungumza tumaini, ukweli, na mabadiliko kwa mataifa.”
Na Neno Litaendelea

Ushuhuda wa Msikilizaji wa Neno Litaenedelea “Sina fursa ya kuhudhuria mikutano ya kanisani, lakini kupitia redio yangu ...
08/10/2025

Ushuhuda wa Msikilizaji wa Neno Litaenedelea

“Sina fursa ya kuhudhuria mikutano ya kanisani, lakini kupitia redio yangu napokea Neno la Mungu moja kwa moja nyumbani kwangu,” .....Katika maeneo yenye barabara mbaya, makanisa machache na rasilimali haba, redio inakuwa madhabahu, na kila nyumba inakuwa hekalu la ibada.

In places where roads are rough, churches are few, radio becomes the pulpit, & every home becomes a sanctuary.

🎤Enzi zile…....💙💙🎙📻Unakumbuka pale ulipokuwa unasikia sauti hii?👉 “Ni mimi, Mchungaji wako Geoffrey Wanjala Munialo… na ...
09/09/2025

🎤Enzi zile…....💙💙
🎙📻Unakumbuka pale ulipokuwa unasikia sauti hii?

👉 “Ni mimi, Mchungaji wako Geoffrey Wanjala Munialo… na Neno litaendelea!” 📻

Maneno haya yalipenya masikioni na kuingia moyoni, yakikufikia popote ulipokuwa—kwenye redio ya kijijini, mjini, au ukiwa safarini.

Ni kumbukumbu ya nyakati ambazo Neno la Mungu liliendelea kutufikia bila kikomo.

Na leo, bado tunasema kwa hakika: Neno litaendelea!

Neno La Siku kutoka kwa Mchungaji Geoffrey Wanjala Munialo wa Neno Litaendelea akiwa katika Gereza la Manyani."Hujakamilika kuumbwa Mungu anakujua tayari"

Address

Producer Neno P. O. Box 21514 Nairobi
Nairobi
00505

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Neno Litaendelea posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category