Neno Litaendelea

Neno Litaendelea Neno Litaendelea (TTB Swahili) is a bible teaching (Gen- Rev) program from Trans World Radio Kenya.

01/07/2025

SIFA NA KAZI naye DAN JUMA
Unategea ukiwa wapi sema nasi
0724-601-810 / 0731-233-283
Neno Litaendelea
Radio Injili


30/06/2025

Wakati ambapo maisha yalionekana kuwa ya kutokuwa na uhakika na siku za usoni hazieleweki, msikilizaji mmoja alipata tumaini mahali pa kushangaza....kupitia kipindi cha redio. Neno Litaendelea, kutoka K- Trans World Radio Kenya kupitia KBC Radio Taifa, Sauti Ya Mkenya wakati huo, kilikuwa nguzo ya kiroho katika ujana wake.
Kilichoanza k**a faraja ya kimya kupitia masafa ya redio, baadaye kilikua wito wa ujasiri. Leo hii, yeye ni mchungaji katika Kanisa la Jordan Gospel huko Kawangware, akisimama kwa ujasiri mbele ya waumini, jambo ambalo hakuweza hata kulifikiria wakati akiwa mwanafunzi mwenye haya na asiyejiamini. Hadithi yake ni ushuhuda wa uaminifu wa Mungu, nguvu ya Neno Lake, na umuhimu ya huduma ya vyombo vya habari.
Tazama jinsi Neno Litaendelea lilivyokuwa na nafasi muhimu katika kubadilisha hofu kuwa imani, na kimya kuwa sauti yenye nguvu kwa Kristo.

At a time when life felt uncertain and the future unclear, one young listener found hope in the most unexpected place, a...
28/06/2025

At a time when life felt uncertain and the future unclear, one young listener found hope in the most unexpected place, a radio program. Neno Litaendelea , produced by Trans World TWR K- Trans World Radio Kenya and aired by KBC Radio Taifa, Sauti Ya Mkenya at that time, became a spiritual anchor during his teenage years. What began as quiet encouragement through the airwaves eventually grew into a bold calling.

Today, he is a pastor at Jordan Gospel Church in Kawangware, standing confidently before congregations. Something he never imagined possible as a shy, unsure high school student. His story is a testimony of God's faithfulness, the power of His Word, and the impact of media ministry.

Read and watch the video of how Neno Litaendelea played a vital role in transforming fear into faith, and silence into a powerful voice for Christ.

One of the greatest transformations I experienced was in my confidence. I used to be extremely shy. I feared standing in front of people or even being seen

Heri ya Siku ya akinababa kwa mababa wote!Tunapowasherehekea leo, tunakumbushwa maneno ya Mithali 20:7 – “Mwenye haki hu...
15/06/2025

Heri ya Siku ya akinababa kwa mababa wote!
Tunapowasherehekea leo, tunakumbushwa maneno ya Mithali 20:7 – “Mwenye haki huenenda katika unyofu wake; watoto wake wamebarikiwa baada yake.”

Asanteni kwa upendo wenu, uongozi na imani. Mungu aendelee kuwatia nguvu muendelee kuwa mwanga kwa familia zenu.

Karibu kwa Safari ya Maandiko Inayoangazia Ukweli wa Neno la MunguJiunge nasi katika safari ya Biblia iliyojaa ufunuo, n...
04/06/2025

Karibu kwa Safari ya Maandiko Inayoangazia Ukweli wa Neno la Mungu
Jiunge nasi katika safari ya Biblia iliyojaa ufunuo, neema, na nguvu ya kiroho, ukiwa pamoja na Mchungaji Geoffrey Wanjala Munialo ana Dada Pamela Omwodo watumishi waliyeitwa kufundisha kwa uaminifu na uongozi wa Roho Mtakatifu.

📖 “Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na nuru ya njia yangu.”
Zaburi 119:105

Sikiliza Neno Litaendelea kila Jumatatu hadi Ijumaa Kupitia SIFA 107.7 FM VOI na Sifa FM Lamu saa 12:05 Asubuhi,
SIFA FM 101.1 ATOO, SIFA FM Marsabit SIFA FM Hekima - "Sauti Ya Busara" saa 11:00 Asubuhi

Neno Litaendelea  ni kipindi cha kiroho kinacholenga kufunza kwa kina Maandiko Matakatifu. Kipindi hiki hutoa mafundisho...
13/05/2025

Neno Litaendelea ni kipindi cha kiroho kinacholenga kufunza kwa kina Maandiko Matakatifu.
Kipindi hiki hutoa mafundisho ya Biblia yaliyo sahihi, yanayoeleweka kwa urahisi, na yanayohusiana na maisha ya kila siku.

Kila sehemu huongoza wasikilizaji kuelewa Neno la Mungu kwa uwazi na ukweli, na kuwasaidia kukua kiimani na kulitumia Neno hilo katika maisha yao ya kila siku..

👉 Je, unakisikiliza kipindi hiki kupitia kituo gani? Tuandikie hapo chini!

👉 Je, unakisikiliza kipindi cha Neno Litaendelea  kupitia kituo gani? Tuandikie hapo chini!Neno Litaendelea.......... ni...
13/05/2025

👉 Je, unakisikiliza kipindi cha Neno Litaendelea kupitia kituo gani?
Tuandikie hapo chini!

Neno Litaendelea.......... ni kipindi cha kiroho kinacholenga kufunza kwa kina Maandiko Matakatifu.

.................

Neno Litaendelea sasa lina endelea kubariki wengi kwa lugha ya Kiturkana
12/05/2025

Neno Litaendelea sasa lina endelea kubariki wengi kwa lugha ya Kiturkana

Hata maneno yanapokosekana, Mungu husikia sauti ya moyo wako. 💛🙏
30/04/2025

Hata maneno yanapokosekana, Mungu husikia sauti ya moyo wako. 💛🙏

❗️❗️❗️ Wasikilizaji wa Neno Litaendelea na vipindi vingine kutoka Trans World Radio Kenya kupitia kituo cha SIFA 107.7 F...
24/04/2025

❗️❗️❗️ Wasikilizaji wa Neno Litaendelea na vipindi vingine kutoka Trans World Radio Kenya kupitia kituo cha SIFA 107.7 FM VOI wa andaa mkesha wa SIFA Night.

"Kila sauti ilipoimba, anga lilibadilika, mioyo ilifunguka, mikono ikainuliwa, na mbingu zikajibu. Kile kilichoishi tu kwenye mawimbi ya redio sasa kilikuwa hai ana kwa ana: injili, halisi na ya dhati, ikitamba kanisani na kusikika hadi usiku kucha. Kanisa halikuweza kuwatosha waumini. Waabudu walijaa hadi nje, wakiwa wamesimama chini ya mwanga wa mwezi, wameunganishwa na kiu ya uwepo wa Mungu.........endelea kusoma ↓↓
https://sifafm.co.ke/usiku-wa-sifa-kijiji-cha-sofia-chamulika-kwa-ibada/?

Tangu wimbo wa kwanza ulipopaa k**a uvumba kuelekea mbinguni, sauti ziliungana kwa sifa, maombi yakapiga ngurumo angani, na mioyo ikaelekezwa tena kwa...

22/04/2025

Kwa mioyo yenye huzuni, sisi katika shirika la K- Trans World Radio Kenya watayarishi wa kipindi cha Neno Litaendelea pamoja na vituo vya redio vya SIFA FM tunaungana na familia ya Kikristo duniani kote kuomboleza kifo cha Papa Francis, aliyeitwa na Bwana saa chache tu baada ya kutoa baraka zake za mwisho za Urbi et Orbi katika Uwanja wa Mtakatifu Petro. (Video hapa chini)

Papa Francis alikuwa mchungaji wa kweli wa amani, aliyeongoza kwa unyenyekevu, huruma, na imani isiyotetereka. Sauti yake iliwatetea kwa ujasiri maskini, waliopuuzwa, na umoja katika Kristo.

Tunapotafakari maisha na urithi wake, tunawaombea faraja na nguvu ndugu zetu Wakatoliki duniani kote. Mfano wake na uendelee kututia moyo kuenenda katika upendo na huduma.

"Heri wale wanaoomboleza, kwa kuwa watafarijika." — Mathayo 5:4

🎥 Video kwa hisani ya Vatican News

"Neno Litaendelea" ni kipindi cha kila siku kinacholenga kuwafundisha wasikilizaji Neno la Mungu kwa undani na ufunuo wa...
07/04/2025

"Neno Litaendelea" ni kipindi cha kila siku kinacholenga kuwafundisha wasikilizaji Neno la Mungu kwa undani na ufunuo wa kiroho.

Kupitia mafundisho ya Biblia, kipindi hiki huleta matumaini, imani, na kuelewa kwa kina kuhusu ahadi na upendo wa Mungu. Kikiwa kina pepea kupitia vituo vya Sifa FM kila siku ya wiki.

Jiunge naye Pamela Omwodo na Mchungaji Geoffrey Wanjala Munialo na ujifunze mengi.

Na Neno Litaendelea .............................

Address

Producer Neno P. O. Box 21514 Nairobi
Nairobi
00505

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Neno Litaendelea posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Neno Litaendelea:

Share

Category