Neno Litaendelea

Neno Litaendelea Neno Litaendelea (TTB Swahili) is a bible teaching (Gen- Rev) program from Trans World Radio Kenya.

❗️❗️ Mzunguko Kamili wa Huduma  🎙️🎙️Mwaka 1987, kijana aitwaye Ruben Kigame alitembelea studio za TWR K- Trans World Rad...
10/10/2025

❗️❗️ Mzunguko Kamili wa Huduma 🎙️🎙️

Mwaka 1987, kijana aitwaye Ruben Kigame alitembelea studio za TWR K- Trans World Radio Kenya kurekodi albamu yake ya kwanza kabisa ya injili: “What a Mighty God We Have.” ♫♫

Wakati huo haukuzaa tu muziki wa kudumu, bali pia ulizindua huduma ambayo imegusa mioyo ya watu wengi vizazi hadi vizazi.

Miaka 38 baadaye, Dkt. Ruben Kigame amerejea tena. Safari hii kupitia mitambo ya redio ya SIFA FM, mojawapo ya huduma za redio za TWR Kenya. Katika mahojiano ya kugusa moyo, alishiriki safari yake kutoka ulimwengu wa muziki hadi kwenye uongozi wa kitaifa na hamu yake ya kuhudumia Kenya k**a Rais wa Sita mwaka 2027.

Alizungumza kwa msisitizo kuhusu maadili yanayomwongoza : imani, uadilifu, na haki. Pamoja na maono yake ya kuona Kenya isiyo na ufisadi, upendeleo, na ukosefu wa ajira kwa vijana.
Aidha, aliweza kujibu maswali kutoka kwa wasikilizaji kupitia kipindi “Miereka ya Siasa” kinachoendeshwa na Lion Obimbo na Ian Odhiambo.

“Sauti kuu ya busara lazima isikike. Kizazi hiki na kijacho vinastahili nchi iliyobadilika. Mabadiliko yanaanza na sisi,” alisema.

Kwetu sisi TWR Kenya, ilikuwa ni ukumbusho wenye nguvu kwamba mbegu zilizopandwa kupitia utangazaji wa injili bado zinaendelea kuzaa matunda hadi leo.

Kutoka kurekodi nyimbo za imani hadi sasa kuzungumza kuhusu mageuzi ya taifa, ujumbe wa Mungu wa tumaini unaendelea kudumu. 🙏

Iwe ni kupitia muziki, mahubiri, au programu za kijamii na kimaendeleo, TWR Kenya itaendelea kujitolea kubadilisha maisha na kutangaza Habari Njema kwa vizazi vyote.

📻 “Kuzungumza tumaini, ukweli, na mabadiliko kwa mataifa.”
Na Neno Litaendelea

Ushuhuda wa Msikilizaji wa Neno Litaenedelea “Sina fursa ya kuhudhuria mikutano ya kanisani, lakini kupitia redio yangu ...
08/10/2025

Ushuhuda wa Msikilizaji wa Neno Litaenedelea

“Sina fursa ya kuhudhuria mikutano ya kanisani, lakini kupitia redio yangu napokea Neno la Mungu moja kwa moja nyumbani kwangu,” .....Katika maeneo yenye barabara mbaya, makanisa machache na rasilimali haba, redio inakuwa madhabahu, na kila nyumba inakuwa hekalu la ibada.

In places where roads are rough, churches are few, radio becomes the pulpit, & every home becomes a sanctuary.

22/09/2025

🖥❗️❗️ Ukweli wa Injili – Wakolosai 1:1-8
Kipindi cha MATUMAINI

Injili ya kweli maana yake nini?
Katika somo hili la kwanza kutoka Wakolosai 1:1-8, tunachunguza msingi wa imani yetu: Imani kwa Kristo, Tumaini la Mbingu, na Upendo kwa Watakatifu.

Kupitia simulizi ya wanaume wawili waliokumbwa na mto mkali, tunajifunza jinsi maamuzi kuhusu Injili yanavyoamua hatima ya maisha yetu. Mtume Paulo anatufundisha kwamba Kristo pekee ndiye msingi wa wokovu Habari Njema ya kweli.

❤️ Imani ya kweli daima inaleta tumaini na kuzaa tunda la upendo.

👉 Usikose kuitazama makala haya wenye mafundisho ya Biblia kwa lugha Kiswahili, yaliyokusudiwa kukusaidia kukua katika imani ukiwaletewa na Heralds of Hope na TWR K- Trans World Radio Kenya.
https://www.youtube.com/watch?v=AIxbObYS5vU

| | |

🎤Enzi zile…....💙💙🎙📻Unakumbuka pale ulipokuwa unasikia sauti hii?👉 “Ni mimi, Mchungaji wako Geoffrey Wanjala Munialo… na ...
09/09/2025

🎤Enzi zile…....💙💙
🎙📻Unakumbuka pale ulipokuwa unasikia sauti hii?

👉 “Ni mimi, Mchungaji wako Geoffrey Wanjala Munialo… na Neno litaendelea!” 📻

Maneno haya yalipenya masikioni na kuingia moyoni, yakikufikia popote ulipokuwa—kwenye redio ya kijijini, mjini, au ukiwa safarini.

Ni kumbukumbu ya nyakati ambazo Neno la Mungu liliendelea kutufikia bila kikomo.

Na leo, bado tunasema kwa hakika: Neno litaendelea!

Neno La Siku kutoka kwa Mchungaji Geoffrey Wanjala Munialo wa Neno Litaendelea akiwa katika Gereza la Manyani."Hujakamilika kuumbwa Mungu anakujua tayari"

Shukrani kwa WashirikaKupitia ushirikiano wenu, tumefanikisha kuwafikia familia nyingi kwa Biblia na vitabu vya kujifunz...
27/08/2025

Shukrani kwa Washirika
Kupitia ushirikiano wenu, tumefanikisha kuwafikia familia nyingi kwa Biblia na vitabu vya kujifunza Neno la Mungu hata katika maeneo yaliyo mbali na upeo wa matangazo yetu. Neno la Mungu linaendelea kusonga na kubadilisha maisha, katika sehemu ambazo pengine hatungeweza kufika peke yetu. Asanteni kwa kufanya hili liwezekane!
Pamoja tunathibitisha kuwa Neno Litaendelea. Ikiwa bado hujawa mshirika, tunakukaribisha ujiunge nasi katika huduma hii ya kusambaza Neno la Mungu kwa kila nyumba na kila moyo

Tungefurahia sana kusikia kutoka kwako! Tafadhali shiriki nasi jinsi Neno Litaendelea  imekuwa baraka katika maisha yako...
05/08/2025

Tungefurahia sana kusikia kutoka kwako! Tafadhali shiriki nasi jinsi Neno Litaendelea imekuwa baraka katika maisha yako.

Such feedback truly warms our hearts.
Neno Litaendelea continues to transform lives, one soul at a time, through the powerful teaching of God’s Word.

We are humbled and grateful to witness how His truth transcends boundaries, bringing healing, hope, and restoration to all who listen.

You can tune in to the Neno program through Sifa FM Kenya and be part of what God is doing.

We’d love to hear from you! Tell us how the program has blessed or impacted your life.

Kipindi cha Neno Litaendelea kimeendelea kutoa mafundisho ya kina ya Maandiko Matakatifu yanayogusa mioyo na kubadilisha...
29/07/2025

Kipindi cha Neno Litaendelea kimeendelea kutoa mafundisho ya kina ya Maandiko Matakatifu yanayogusa mioyo na kubadilisha maisha.

Kwa zaidi ya miaka kumi, kipindi hiki kimewaongoza wasikilizaji kwa uaminifu kupitia Neno la Mungu, kikiwasaidia wengi kukua katika imani na upendo kwa Kristo.

📖 Neno Litaendelea hupeperushwa hewani kila siku kupitia vituo vyote vya Sifa FM , kikifikia na kuinua watu kutoka jamii mbalimbali kote nchini.

Tunamshukuru Mungu kwa maisha yanayoendelea kubadilishwa kupitia kipindi hiki.

TWR K- Trans World Radio Kenya  watayarishaji wa kipindi cha Neno Litaendelea  inamkaribisha Dkt. Njoki Chege k**a Mkuru...
25/07/2025

TWR K- Trans World Radio Kenya watayarishaji wa kipindi cha Neno Litaendelea inamkaribisha Dkt. Njoki Chege k**a Mkurugenzi Mtendaji katika makabidhiano ya kihistoria ya uongozi yaliyojaa imani, maono, tumaini, na kukumbatia matarajio ya siku za usoni ya utangazaji wa injili kwa njia ya kidijitali.

TWR Kenya welcomes Dr. Njoki Chege as the Director in a historic leadership handover filled with faith, vision, hope and embracing prospects of the digital......

23/07/2025
Mabadiliko uongozini katika shirika la TWR K- Trans World Radio Kenya
14/07/2025

Mabadiliko uongozini katika shirika la TWR K- Trans World Radio Kenya

01/07/2025

SIFA NA KAZI naye DAN JUMA
Unategea ukiwa wapi sema nasi
0724-601-810 / 0731-233-283
Neno Litaendelea
Radio Injili


30/06/2025

Wakati ambapo maisha yalionekana kuwa ya kutokuwa na uhakika na siku za usoni hazieleweki, msikilizaji mmoja alipata tumaini mahali pa kushangaza....kupitia kipindi cha redio. Neno Litaendelea, kutoka K- Trans World Radio Kenya kupitia KBC Radio Taifa, Sauti Ya Mkenya wakati huo, kilikuwa nguzo ya kiroho katika ujana wake.
Kilichoanza k**a faraja ya kimya kupitia masafa ya redio, baadaye kilikua wito wa ujasiri. Leo hii, yeye ni mchungaji katika Kanisa la Jordan Gospel huko Kawangware, akisimama kwa ujasiri mbele ya waumini, jambo ambalo hakuweza hata kulifikiria wakati akiwa mwanafunzi mwenye haya na asiyejiamini. Hadithi yake ni ushuhuda wa uaminifu wa Mungu, nguvu ya Neno Lake, na umuhimu ya huduma ya vyombo vya habari.
Tazama jinsi Neno Litaendelea lilivyokuwa na nafasi muhimu katika kubadilisha hofu kuwa imani, na kimya kuwa sauti yenye nguvu kwa Kristo.

Address

Producer Neno P.O. Box 21514 Nairobi
Nairobi
00505

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Neno Litaendelea posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Featured

Share

Category