24/10/2025
💢🎙 Na….. Neno Litaendelea 📻
❗️Tangu mwaka 1992, Neno Litaendelea (Thru The Bible – Swahili) limeendelea kugusa maisha ya watu wengi katika vizazi mbalimbali, likiwaongoza wasikilizaji kwa uaminifu kupitia Maandiko Matakatifu kuanzia Mwanzo hadi Ufunuo.
Kuanzia siku za awali kwenye Redio KBC na TWR Shortwave, hadi sasa kupitia majukwaa mengi ikiwemo Sifa FM inayofikia maeneo mengi ndani na nje ya Kenya, ujumbe umebaki ule ule. Neno la Mungu halitarudi bure.
Maisha yamebadilishwa, imani imeimarishwa, na tumaini limefufuliwa katika familia nyingi barani Afrika na kwingineko.
Faida hii kubwa imewezekana kupitia ushirikiano wenye nguvu kati ya Trans World Radio na Thru The Bible (TTB) mashirika mawi zilizounganishwa na dhamira moja: kufikisha Neno la Mungu mpaka miisho ya dunia.
Hivi karibuni tulipata heshima ya kuwapokea timu kutoka TTB, tukijadiliana njia mpya za kuimarisha na kupanua ushirikiano huu ili kuhakikisha Injili inaendelea kuwafikia watu kwa lugha wanayoielewa vyema zaidi.
🎤Katika TWR Kenya, tumebarikiwa kuwa na timu yenye kujitolea ya wataalamu wa vyombo vya habari na washirika wa huduma wanaofanya kazi bila kuchoka kutengeneza vipindi vya kimaandiko na kimaendeleo vinavyotoa taarifa, kuhamasisha, na kubadilisha maisha.
Tukiwa na uzoefu wa zaidi ya miaka 49 katika utangazaji, tupo tayari kuhudumia huduma za injili, makanisa, na mashirika yanayotamani kuleta athari kamili katika jamii.
🤝 Tunakuarika kushirikiana nasi. Pamoja, tunakuza ujumbe.
Pamoja, tunaleta faida ya milele. 🎙💢
📧 Wasiliana nasi leo: [email protected] 🌐 Tembelea: www.twr.co.ke