Magnet News

Magnet News Powered by IPO SIKU MEDIA{ISM}

MAgnet News-Spark the News, Magnetize Minds.

MAGNET ICT CENTRE WANATAFUTA WANAGENZI WA PACKAGESJe, unatafuta huduma za computer?? Magnet ICT Centre wako hapa kukupa ...
15/01/2025

MAGNET ICT CENTRE WANATAFUTA WANAGENZI WA PACKAGES
Je, unatafuta huduma za computer?? Magnet ICT Centre wako hapa kukupa huduma zote unazohitaji! Tunakupa huduma k**a vile; Photocopy, printing, typesetting, binding, lamination pia tuko na online services zikiwemo E-Citizen, HELB, KRA, Passports, NTSA na zinginezo, pia tunatoa Mafunzo ya kompyuta kuanzia shilingi 2500, jiunge nasi leo hii...
Kumbuka ofisi zetu kwa sasa zimehamishwa kutoka St Mary`s Kibomet hadi katikati ya mji wa Kitale. Tutembelee leo hii pale Midtown Business Centre(Nyuma ya Vision Gate Hotel ama Nyuma ya M-Oriental Bank)

Sasa waweza tupata kwa urahisi kuliko awali.

Karibu sana.

ISM~Your Getaway to Digital Excellence.

 Mojawapo ya changamoto kuu katika taifa kwa vijana limekuwa ajira licha ya hilo viongozi ambao awali walihudumu katika ...
15/01/2025


Mojawapo ya changamoto kuu katika taifa kwa vijana limekuwa ajira licha ya hilo viongozi ambao awali walihudumu katika nyadhfa mbali mbali katika serikali zilizopita wanaonekana wakipata nafasi na kupendekezwa kuhudumu katika nyadfha mbali mbali je unafikiri kigezo kikuu ni kipi? Je ni uzoefu wao wa kazi ikilinganishwa na walio wageni katika huduma za serikali??

KIKI ZA MASTAA ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ"Harmonize ni mtoto mdogo sana sema alifanikiwa kuingia kwenye Record label iliyopata mafanikio makubwa...
14/01/2025

KIKI ZA MASTAA ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ
"Harmonize ni mtoto mdogo sana sema alifanikiwa kuingia kwenye Record label iliyopata mafanikio makubwa Afrika, Ila sio wakushindanisha na kaka zetu Diamond na Alikiba, Ila Nyie Watangazaji Ni Miyeyusho na Mnazingua Maana nyie ndo mnamshindanisha yuke Mtoto na wakubwa." Maneno ya Baraka the Prince.

 Klabu ya Simba SC, imepatiwa adbabu na Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) kufuatia vurugu zilizojitokeza katika mch...
14/01/2025


Klabu ya Simba SC, imepatiwa adbabu na Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) kufuatia vurugu zilizojitokeza katika mchezo wao dhidi ya CS Sfaxien uliofanyika Disemba 15, 2024.

CAF imeifungia klabu hiyo mechi moja kucheza bila mashabiki pamoja na faini ya Dola elfu 40,000.

KIKI ZA MASTAA ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅMwimbaji wa nyimbo za injili Christina shusho alifunguka kwamba star wa muziki wa bongo fleva Harmonize...
14/01/2025

KIKI ZA MASTAA ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ
Mwimbaji wa nyimbo za injili Christina shusho alifunguka kwamba star wa muziki wa bongo fleva Harmonize aliwai kumuomba kolabo wakiwa studio.

"Harmonize aliniletea project kali tukiwa studio nikamwambia ngoja nikaombe, nilivyoenda kuomba sikurudi tena, ila project ipo wakati ukifika tutaimba." Alisema - Christina shusho.

 MASHINDANO YA CHAN YAAHIRISHWA HADI AUGUST 2025Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF) Limeahirisha mashindano ya CHAN A...
14/01/2025


MASHINDANO YA CHAN YAAHIRISHWA HADI AUGUST 2025

Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF) Limeahirisha mashindano ya CHAN Ambayo yalitarajiwa kuanza Mwezi February katika Nchi za Tanzania,Kenya na Uganda .

Ukosefu wa utayari wa Miundo mbinu na Vifaa ni sababu kuu ambazo CAF imezitaja zilizopelelekea kusogeza Mbele mashindano Haya.

MUTURI AZIDI KUIANIKA SERIKALIโ€œNikiwa nimesimama nje ya pazia, nilimsikia Rais akimuuliza Noordin Haji k**a anamshikilia...
14/01/2025

MUTURI AZIDI KUIANIKA SERIKALI
โ€œNikiwa nimesimama nje ya pazia, nilimsikia Rais akimuuliza Noordin Haji k**a anamshikilia mwanangu, Noordin alithibitisha kwamba ni kweli alikuwa amemshikilia mwanangu na Rais alimuagiza amwachie Leslie mara moja, Noordin akajibu kuwa Leslie ataachiwa ndani ya saa moja. . Leslie aliachiliwa baada ya saa moja." Waziri Justin Muturi.

Aliyekuwa Gavana wa kaunti ya Nairobi Mike Sonko alikutana na aliyekuwa naibu wake Polycarp Igathe katika mtaa wa Runda ...
14/01/2025

Aliyekuwa Gavana wa kaunti ya Nairobi Mike Sonko alikutana na aliyekuwa naibu wake Polycarp Igathe katika mtaa wa Runda jijini Nairobi, Wawili hao walikutana kwenye sherehe ya kuajindaa kwa harusi ya kitamaduni ya mwanawe Polycarp Igathe, Matilda Igathe na mchumba wake Luios Muihengi Kimanzi.

Sherehe hizo ziliwaleta pamoja ndugu, jamaa pamoja na marafiki wakiwemo vigogo mashuhuri kutoka sehemu tofautitofauti.

Sonko ambaye anajulikana kuwa na uwezo wa kununua mivinyo za bei ghali alimuzawadi Polycarp Igathe na pombe aina Johnnie Walker King George V edition inayogharimu thamani ya Ksh 76,000 kwa chupa moja.

Akipokea zawadi hiyo Igathe alimushukuru Sonko akisema โ€œ hii pombe ya walker king imeletwa na bosi wangu , Gavana wangu sonkoree. Sasa wewe ni rafiki yangu , umekuja na familia ya kimani umekua mkoo, tukikutaa uko inje wewe ndo unalipa bill.

KIKI ZA MASTAA ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅMsanii na mjasiriamali kutoka Tanzania, Diamond Platnumz amewatayarisha kisaikolojia mashabiki wake kuh...
14/01/2025

KIKI ZA MASTAA ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ
Msanii na mjasiriamali kutoka Tanzania, Diamond Platnumz amewatayarisha kisaikolojia mashabiki wake kuhusu ujio wa albamu yake mpya.

Kupitia kwa Instagram yake siku chache zilizopita, msanii ambaye anamiliki chombo cha Habari cha Wasafi na lebo ya WCB Wasafi alifichua kwamba ataangusha magoma ya kipekee katika albamu yake ijayo.

Diamond alithibitisha kwamba albamu hiyo itatoka kabla ya mwezi Mtukufu wa Ramadhan, akiipaisha kuwa yenye itawakumbusha mashabiki wake kwa nini yeye ni โ€˜simbaโ€™ Msanii huyo alisema kwamba licha ya wengi kuona ngoma zake za miaka miwili iliyopita โ€“ Zuwena na Yatapita k**a ngoma bora kutoka kwake, ngoma mpya zilizopo katika albamu hiyo zitawafanya kuona hizo nyimbo mbili k**a uchafu tu.

โ€œAlbamu mpya ya Bongo Fleva kabla ya mwezi mtukufu wa Ramadhani. Achana na Zuwena, Yatapita, hizo ni uchafu,โ€ Diamond aliandika, Nataka niwakumbushe nini kilifanya nikapendwa,โ€ Platnumz aliongeza huku akisisitiza kwamba albamu hiyo itakuwa na upekee wa ngoma za Bongo Fleva pekee bila mchanganyiko wa mtindo mwingine wa muziki.

Msanii huyo licha ya kufanya vizuri katika miaka ya hivi karibuni, amekuwa mkimya sana likija ni suala la kuachia albamu, kwani mara ya mwisho alitoa albamu ilikuwa mwaka 2022 alipoachia EP ya FOA.
Tangu alipoachia ngoma hizo mbili ambazo sasa ameita uchafu, Diamond ameonekana kutoka nje ya mdundo wa Bongo Fleva na nyingi ya ngoma ambazo ameachia ni za mdundo wa Amapiano.

 Waziri wa Utumishi wa Umma Justin Muturi yuko katika afisi za makachero wa  DCI katika Kituo cha Polisi cha Kilimani ku...
14/01/2025


Waziri wa Utumishi wa Umma Justin Muturi yuko katika afisi za makachero wa DCI katika Kituo cha Polisi cha Kilimani kurekodi taarifa kuhusu kutekwa nyara kwa mwanawe mwaka jana.

 Waziri mteule wa kilimo na mifugo Mutahi Kagwe ameweka wazi kuwa utajiri wake ni wa thamani ya karibu shilingi milioni ...
14/01/2025


Waziri mteule wa kilimo na mifugo Mutahi Kagwe ameweka wazi kuwa utajiri wake ni wa thamani ya karibu shilingi milioni 842 za Kenya.

Mutahi ameweka haya wazi alipokuwa akipigwa msasa ili kutathmini iwapo anastahili kuongoza wizara hiyo.

Waziri mteule wa ICT William Kabogo amekanusha kuhusika katika biashara ya dawa za kulevya, k**a ilivyodaiwa na aliyekuw...
14/01/2025

Waziri mteule wa ICT William Kabogo amekanusha kuhusika katika biashara ya dawa za kulevya, k**a ilivyodaiwa na aliyekuwa waziri wa Usalama wa Ndani Goerge Saitoti mwaka wa 2010.
Kabogo amekanusha madai hayo wakati akihojiwa na k**ati ya Bunge ya taifa inayowapiga msasa mawaziri wateule.

 ๐”๐ฌ๐ก๐ข๐ซ๐ข๐ค๐š ๐ฐ๐š ๐‘๐ข๐ ๐š๐ญ๐ก๐ข ๐ง๐š ๐๐š๐ญ๐ž๐ฆ๐›๐ž๐ฒ๐š, ๐ฎ๐ค๐จ ๐ง๐ฃ๐ข๐š๐ง๐ข ๐ฎ๐ง๐š๐ค๐ฎ๐ฃ๐š?USHIRIKIANO wa kisiasa kati ya aliyekuwa Naibu wa Rais Rigathi Gac...
14/01/2025


๐”๐ฌ๐ก๐ข๐ซ๐ข๐ค๐š ๐ฐ๐š ๐‘๐ข๐ ๐š๐ญ๐ก๐ข ๐ง๐š ๐๐š๐ญ๐ž๐ฆ๐›๐ž๐ฒ๐š, ๐ฎ๐ค๐จ ๐ง๐ฃ๐ข๐š๐ง๐ข ๐ฎ๐ง๐š๐ค๐ฎ๐ฃ๐š?

USHIRIKIANO wa kisiasa kati ya aliyekuwa Naibu wa Rais Rigathi Gachagua na Gavana wa Trans Nzoia George Natembeya unanukia baada ya gavana huyo kuashiria kuwa yuko tayari kushirikiana na kiongozi huyo.

Kwenye mahojiano Jumatatu na redio ya Kameme FM inayopeperusha matangazo yake kwa lugha ya Gikuyu, gavana huyo alisema ataendelea kushirikiana na eneo la Mlima Kenya kisiasa kwani alipandishwa vyeo katika utawala wa mkoa kutokana na ushawishi wa watu wa eneo hilo.

Alieleza kuwa watu k**a marais wa zamani Mwai Kibaki na Uhuru Kenyatta, aliyekuwa mkuu wa Utumishi wa Umma Francis Kimemia na mshauri wa rais kuhusu masuala ya usalama Monica Juma, walimsaidia kupanda ngazi kutoka afisa wa cheo cha chini hadi akawa Kamishna wa Ukanda wa Bonde wa Ufa 2022.

โ€œIkiwa mtu anaamini kuwa ninafaa kuwa adui wa mtu kutoka Mlima Kenya kwa sababu ya tofauti zake na mtu huyo, ajue anaota mchana,โ€ Bw Natembeya akasema.

Gavana huyo alisema wakereketwa wa serikali wanampiga vita kisiasa, kiasi cha kupanga hoja ya kumtimua afisini, kutokana na uhusiano wake na Bw Gachagua na uamuzi wake kuendelea kukosoa utawala huu wa Rais William Ruto.

โ€œWanataka kunitimua kutokana na msimamo wangu kisiasa. Waendelee na mipango hiyo kwani itanipa nafasi nzuri ya kwenda mashinani kutetea maslahi ya umma, nikishirikiana wa Gachagua na wazalendo wengine,โ€ akasema.

Gavana Natembeya alidai Kiongozi wa Wengi Kimani Ichungโ€™wah ni miongoni mwa wadhamini wakuu wa mikutano ya kumwondoa afisini.
Hata hivyo, alimpuuzilia mbali Mbunge huyo wa Kikuyu k**a โ€œmtu anayepayuka tu ilhali hana hekima yoyoteโ€.

Mnamo Januari 3, Bw Ichungโ€™wah alimshambulia hadharani Bw Natembeya wakati wa mazishi ya mamake Spika wa Bunge Moses Wetangโ€™ula katika Kaunti ya Bungoma kwa kuihusisha serikali na visa vya utekaji nyara wa Wakenya.

โ€œWewe Gavana Natembeya haufai kulalamikia utekaji nyara ilhali rafiki yako Rigathi Gachagua ndiye anaendeleza utekaji huo ili ailaumu serikali. Ulihudumu k**a Kamishna wa Ukanda katika utawala uliopita wakati mamia ya watu walitekwa na kuuawa katika Bonde la Kerio kisha miili yao ikatupwa katika Mto Yala. Je, ulithamini maisha ya raia wakati huo?โ€ Ichungโ€™wah akauliza kwa hasira mbele ya Bw Natembeya aliyehudhuria hafla hiyo.

Mazishi hayo pia yalihudhuriwa na Rais William Ruto.

Siku moja baada ya kushambuliwa kwa Gavana Natembeya, Bw Gachagua alimpa moyo huku akimtaka kutokubali kuyumbishwa na vitisho k**a hivyo.

โ€œNdugu yangu Gavana Natembeya. Tafadhali usikubali watetezi hao wa udhalimu na wenye matusi wakuzuie kuwahudumia watu wa kaunti ya Trans nzoia. Watu hawa wamekodiwa kukushambulia ili kumfurahisha mkubwa wao,โ€ Bw Gachagua akamwambia.

Naibu huyo wa rais wa zamani alimshauri Natembeya asiogope kuongea ukweli, akiongeza kuwa anashambuliwa na wandani wa Rais Ruto kwa sababu analeta mabadiliko katika jamii.

โ€œNa usiogope kupaza sauti yako ukitetea raia wa Kenya kwa sababu huo ndio wajibu wako k**a kiongozi,โ€ Bw Gachagua akaongeza.

Gavana Natembeya, aliyechaguliwa kwa tiketi ya chama cha Democratic Action Party of Kenya (DAP-K), amekuwa akihimiza umoja wa jamii ya โ€˜Mulembeโ€™ huku akiwakosoa viongozi wakuu eneo hilo, Bw Wetangโ€™ula na Mkuu wa Mawaziri Musalia Mudavadi kwa kutosaidia kukuza eneo hilo kimaendeleo.

Kando na kumtetea Bw Natembeya, Bw Gachagua na wandani wake, wamemwalika gavana huyo katika mikutano kadhaa maeneo ya Mlima Kenya, hali ambayo imeibua tetesi kuhusu uhusiano wake na mbunge huyo wa zamani wa Mathira.

Mchanganuzi wa masuala ya kisiasa Martin Andati anasema bado ni mapema kubashiri iwapo ushirikiano wa kisiasa kati ya Gavana Natembeya na Bw Gachagua utayumbisha siasa nchini kuelekea uchaguzi mkuu wa 2027.

โ€œBw Natembaye ambaye ameanzisha vuguvugu la Tawe, angali mchanga katika siasa. Isitoshe, ameonyesha wazi kwamba bado anapania kutetea kiti chake cha ugavana 2027. Kwa hivyo, huenda akajishughulisha zaidi na juhudi za kutetea kiti hicho badala ya kumsaidia Gachagua katika ajenda yake ya kuangusha Rais Ruto 2027." anaeleza.

 NYANI WAWAUMA WAKAAZI KITALEWakaazi wa mtaa wa Lessos viungani mwa mji wa Kitale kaunti ya Trans Nzoia wameingiwa na ho...
14/01/2025


NYANI WAWAUMA WAKAAZI KITALE
Wakaazi wa mtaa wa Lessos viungani mwa mji wa Kitale kaunti ya Trans Nzoia wameingiwa na hofu baada ya watu 15 kuumwa na tumbili wakali katika muda wa miezi miwili. Wahasiriwa, ambao tayari wamepata chanjo ya kushonwa na kichaa cha mbwa, wanasalia na wasiwasi juu ya uwezekano wa maambukizo kutoka kwa magonjwa yanayopitishwa na nyani.

Mashambulizi hayo yamewalazimu wenyeji wengi kusalia majumbani, huku wale wanaoendesha biashara wakisalia katika hali ya tahadhari. Wengine wanaamini kuwa tabia isiyo ya kawaida ya nyani hao huenda ilichochewa na uharibifu wa msitu ulio karibu.

Maafisa wa KWS walithibitisha kisa hicho na kuripoti kuwa nyani wanne wameangamizwa huku mipango ikiendelea ya kumk**ata mmoja ili kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu ili kubaini iwapo ana magonjwa hatari. Wakaazi wanaomba hatua za haraka kuzuia mashambulizi zaidi na kuhakikisha usalama wao.

 Wizara ya Mambo ya Ndani imetangaza kuwa Wakenya hawatalazimika kutembelea vituo vya polisi kuanzia Aprili mwaka huu ku...
14/01/2025


Wizara ya Mambo ya Ndani imetangaza kuwa Wakenya hawatalazimika kutembelea vituo vya polisi kuanzia Aprili mwaka huu kuripoti kesi baada ya mkutano kati ya katibu katika wizara hiyo Raymond Omollo na Balozi wa EU nchini Kenya.

Serikali pia itaanzisha mfumo wa kidijitali kushughulikia faini za trafiki na kutekeleza kitabu cha matukio ya kidijitali k**a sehemu ya juhudi hizi.

Wakenya 25 bado hawajulikani walipo wakikisiwa kutoweka mwezi June mwaka jana, KNHRC inasema visa 85 vya utekaji nyara v...
14/01/2025

Wakenya 25 bado hawajulikani walipo wakikisiwa kutoweka mwezi June mwaka jana, KNHRC inasema visa 85 vya utekaji nyara vimerekodiwa katika kipindi hicho.

 Shule ya mtakatifu Gabriel Isongo katika kaunti  ya kakamega imefanikiwa kuwapeleka wanafunzi watano kwenye vyuo vikuu ...
14/01/2025


Shule ya mtakatifu Gabriel Isongo katika kaunti ya kakamega imefanikiwa kuwapeleka wanafunzi watano kwenye vyuo vikuu Kati ya wanafunzi 176 walioukalia mtihani wa kitaifa mwaka wa 2024.

Ikumbukwe mwaka uliopita wazazi wa shule hiyo walimfurusha Mwalimu mkuu kutokana na matokea duni mwaka wa 2023.

 Mamlaka ya ukusanyaji ushuru nchini KRA inalenga kukusanya mapato ya ushuru ya Shilingi Trilioni 2.7  katika mwaka wa k...
14/01/2025


Mamlaka ya ukusanyaji ushuru nchini KRA inalenga kukusanya mapato ya ushuru ya Shilingi Trilioni 2.7 katika mwaka wa kifedha unaoanza Julai, kutoka kwa makadirio ya Shilingi Trilioni 2.3, kufuatia kurejeshwa kwa hatua muhimu za ushuru.

Address

Kitale

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Magnet News posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Magnet News:

Videos

Share

Category