DW Kiswahili

DW Kiswahili Tunakuletea yaliyomuhimu. Unatupa fikra yako: Jadiliana nasi habari kutoka Afrika na ulimwengu mzima.

 : Rais wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Joseph Kabila ametoa wito kukomeshwa kwa kile alichokiita "udiktet...
23/05/2025

: Rais wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Joseph Kabila ametoa wito kukomeshwa kwa kile alichokiita "udikteta" nchini humo siku moja tu baada ya kuondolewa kinga ya kutoshtakiwa.

"Udikteta lazima ukomeshwe, na demokrasia, utawala bora na ustawi wa kijamii lazima urejeshwe," Kabila amesema katika hotuba ya nadra iliyopeperushwa moja kwa moja kwenye mitandao.

23/05/2025
 : Watu wasiopungua 12 wamejeruhiwa, baadhi yao wakiwa hali mahututi baada ya kushambuliwa kwa kisu katika kituo kikuu c...
23/05/2025

: Watu wasiopungua 12 wamejeruhiwa, baadhi yao wakiwa hali mahututi baada ya kushambuliwa kwa kisu katika kituo kikuu cha treni mjini Hamburg.

Polisi ya Ujerumani imeandika kwenye mtandao wa kijamii wa X kwamba, "kulingana na taarifa za awali, mtu mmoja amewashambulia kwa kisu na kuwajeruhi watu kadhaa katika kituo kikuu cha treni."

Mshukiwa huyo tayari amek**atwa na vikosi vya usalama.

Hivi karibuni, Ujerumani imekumbwa na visa vya mashambulizi ya kisu.

 : Chama cha Rais wa zamani wa Kongo Joseph Kabila cha PPRD kimelaani hatua ya kuondolewa kinga ya kutoshtakiwa kwa kion...
23/05/2025

: Chama cha Rais wa zamani wa Kongo Joseph Kabila cha PPRD kimelaani hatua ya kuondolewa kinga ya kutoshtakiwa kwa kiongozi huyo.

Chama hicho kimeongeza kwamba hatua iliyochukuliwa dhidi ya Kabila inalenga kumdidimiza kisiasa na kuficha kile walichokiita "kufeli" kwa utawala wa Rais Felix Tshisekedi.

Baraza la Seneti nchini DRC lilipiga kura ya kumuondolea kinga ya kutoshtakiwa Joseph Kabila. Kabila anashutumiwa na serikali kwa kulisaidia kundi la waasi la M23.

Joseph Kabila aliiongoza Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kuanzia mwaka 2001 hadi 2019.

 : Mapigano kati ya jeshi la Sudan Kusini na wapiganaji wanaomuunga mkono mpinzani wake Rais Salva Kiir yamesababisha vi...
23/05/2025

: Mapigano kati ya jeshi la Sudan Kusini na wapiganaji wanaomuunga mkono mpinzani wake Rais Salva Kiir yamesababisha vifo vya takriban raia 75 tangu Februari.

Haya yamesemwa leo Ijumaa na Mkuu wa Tume ya Haki za binadamu ya Umoja wa mataifa Volker Turk.

 : Gazeti la The Bild nchini Ujerumani limechapisha ripoti inayoonyesha kwamba mji wa Leverkusen katika jimbo la North R...
23/05/2025

: Gazeti la The Bild nchini Ujerumani limechapisha ripoti inayoonyesha kwamba mji wa Leverkusen katika jimbo la North Rhine-Westphalia unaongoza kwa talaka nchini humo.

Takwimu katika mji huo zinasema, karibu ndoa 516 hufungwa kila mwaka, na katika muda huo huo talaka 467 hutolewa, ikimaanisha kuwa robo tatu ya ndoa huvunjika mjini humo.

Ila ndoa ni taasisi ya ajabu k**a wanavyosema wavyele, walioko nje wanataka kuingia ndani ilhali walioko ndani wanataka kutoka nje. Hii imekaaje?

23/05/2025

Adila Nassoro kutoka Tanzania aliyeamua kusimama katika pengo la kimya na unyanyapaa, akianzisha programu ya kipekee ya kuelimisha vijana kuhusu afya ya akili. Kupitia moyo wa huruma na kiu ya mabadiliko, ameunda jukwaa salama la mazungumzo, ambapo vijana wanaweza kuelewa, kueleza, na kujijenga upya bila hofu ya kuhukumiwa.

 : Mwanaharakati wa Kenya Boniface Mwangi aliyedaiwa kuwekwa kizuizini nchini Tanzania, akizungumza na waandishi wa haba...
23/05/2025

: Mwanaharakati wa Kenya Boniface Mwangi aliyedaiwa kuwekwa kizuizini nchini Tanzania, akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuachiliwa huru. Mwanaharakati huyo alipatikana katika eneo la Ukunda, kaunti ya Kwale pwani ya Kenya.

 : Mbunge wa Mbeya Mjini Dkt. Tulia Ackson ametangaza nia ya kuwania ubunge wa jimbo jipya la Uyole katika uchaguzi mkuu...
23/05/2025

: Mbunge wa Mbeya Mjini Dkt. Tulia Ackson ametangaza nia ya kuwania ubunge wa jimbo jipya la Uyole katika uchaguzi mkuu wa Oktoba, mwaka huu 2025.

Uamuzi wa Dkt. Ackson ambaye pia ni Spika wa Bunge la Tanzania, ameutoa wiki chache tu baada ya tume huru ya taifa ya uchaguzi INEC kutangaza majimbo nane mapya na kata tano mpya ambazo zitatumika katika uchaguzi mkuu wa Oktoba.

Mkoa wa Mbeya, Mbeya Mjini umegawanywa na kuanzishwa Uyole.

 : Katibu Mkuu wa chama cha upinzani cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA John Mnyika amedai kuwepo kwa juhudi za kudhoof...
23/05/2025

: Katibu Mkuu wa chama cha upinzani cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA John Mnyika amedai kuwepo kwa juhudi za kudhoofisha harakati za kudai mabadiliko ya kisiasa nchini Tanzania.

Akizungumza leo kwenye kikao cha chama hicho kilichofanyika Mikocheni-Dar es Salaam, Mnyika ameeleza kuwa watawala wanajaribu kubatilisha maamuzi ya Kamati Kuu ambayo yalifanyika baada ya uongozi mpya kuingia madarakani.

Waziri wa Katiba na sheria nchini Tanzania Dokta Damas Daniel Ndumbaro aliwasilisha bungeni hotuba ya mpango na makadiri...
23/05/2025

Waziri wa Katiba na sheria nchini Tanzania Dokta Damas Daniel Ndumbaro aliwasilisha bungeni hotuba ya mpango na makadirio ya mapato na matumizi ya wizara kwa mwaka wa fedha 2025/2026.

Katika hotuba yake alitoa takwimu zinazohusiana na masuala ya ndoa nchini humo. Takwimu hizo zinasema kuanzia Julai 2024 hadi Aprili 2025 wakala umesajili marejesho ya shahada za ndoa 35,052 ambayo ni sawa na asilimia 65 ya lengo.

Aliongeza katika kipindi cha Julai 2024- Aprili 2025 wakala umesajili na kutoa vyeti 675 vya talaka sawa na asilimia 116. Tujadiliane kwanini talaka zinaongezeka kwa sasa

23/05/2025

Kufuatia mkutano na Donald Trump katika ikulu ya White House, rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, anataka kuimarisha uhusiano wa kirafiki na Marekani, na pia kutuliza hofu kuhusu sheria tata ya mageuzi ya ardhi. Lakini Sheria ya Kisasa ya Kutaifisha Ardhi ni nini, na raia wa Afrika Kusini wana maoni gani kuihusu?

Adresse

Bonn
53113

Webseite

https://tinyurl.com/2bvkbetv

Benachrichtigungen

Lassen Sie sich von uns eine E-Mail senden und seien Sie der erste der Neuigkeiten und Aktionen von DW Kiswahili erfährt. Ihre E-Mail-Adresse wird nicht für andere Zwecke verwendet und Sie können sich jederzeit abmelden.

Service Kontaktieren

Nachricht an DW Kiswahili senden:

Teilen