Michuzi TV

Michuzi TV Karibu Michuzi Blog a.k.a Globu ya Jamii the most read Swahili blog on Earth

http://issamichuzi.blo

When I started this blog at Finlandia Hall in Helsinki, Finland, on Septermber 28, 2005, my aim was to bridge the news and information gap for the benefit of Tanzanians in the Diaspora. Since I was the first Tanzanian blogger operating from Tanzania ( http://issamichuzi.blogspot.com/2005_09_01_archive.html) about 4 years elapsed before others started blogging. Therefore I boast of millions of fait

hful old and new followers who have made Michuzi the most read Swahili blog on earth. Moreso its the top most blog with authoritative and authentic content.

 Rais Samia usiku wa kuamkia leo wakati wa ibada ya mkesha ya kuusubiri mwaka mpya wa 2025 katika kanisa la ngome ya Yes...
01/01/2025



Rais Samia usiku wa kuamkia leo wakati wa ibada ya mkesha ya kuusubiri mwaka mpya wa 2025 katika kanisa la ngome ya Yesu linaloongozwa na mchungaji kiongozi Kuhani Musa alipiga simu na kuongea na mchungaji pamoja na waumini wa Kanisa hilo huku akiwatakia heri ya mwaka mpya 2025.

Aidha Rais Samia ameahidi kuchangia kiasi cha shilingi milioni mia moja katika ujenzi wa kanisa hilo unaoendelea.

 Watumiaji wa bidhaa za mafuta ya petroli nchini wameuanza mwaka mpya wa 2025 kwa shangwe ya kuendelea kupata unafuu  be...
01/01/2025



Watumiaji wa bidhaa za mafuta ya petroli nchini wameuanza mwaka mpya wa 2025 kwa shangwe ya kuendelea kupata unafuu bei za bidhaa hizo kwa mwezi Januari 2025.

Taarifa iliyotolewa na EWURA, leo Jumatano, mosi, imeonesha bei za mwezi huu kuendelea kushuka ambapo petroli kwa lita imeshuka kwa sh. 105, dizeli kwa sh. 135 na mafuta ya taa bei imepungua kwa shilingi 15 kwa mafuta yaliyopokelewa bandari ya Dar es Salaam ikilinganishwa na bei za mwezi Desemba 2024.

Kwa upande wa mafuta yaliyopokelewa bandari ya Tanga, bei ya petroli pia imeshuka kwa sh. 105 kwa lita, dizeli sh. 136 na mafuta ya taa sh. 135 huku bandari ya Mtwara bei ya petroli kwa lita ikipungua kwa sh. 42, dizeli sh. 129 na mafuta ya taa sh. 157.

Ahueni hiyo inatokakana na kuendelea kuimarika thamani ya shilingi dhidi ya fedha za kigeni zinazotumika kuagiza mafuta nje ya nchi ambapo wastani wa kubadilisha fedha za kigeni umepungua kwa asilimia 11.27.

Ikumbukwe pia kwamba, bei za bidhaa za mafuta aina ya petroli zimeendelea kushuka mfululizo kwa takribani miezi mitano kuanzia mwezi Septemba 2024.

 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amewataka watanzania wote kuhakikisha wanatumia nis...
31/12/2024



Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amewataka watanzania wote kuhakikisha wanatumia nishati safi ya kupikia k**a njia mahususi ya kutunza na kulinda mazingira pia kuokoa uharibifu wa misitu.

Katika tamasha maalumu la azimio la Kizimkazi lililofanyika mkoani Lindi wilaya ya Ruangwa leo tarehe 31 Disemba, 2024 Waziri Mkuu Majaliwa amebainisha kuwa uhamasishaji wa matumizi ya nishati safi ya kupikia ni ajenda ya kimataifa inayofanyika kwa lengo la kuimarisha afnya za wananchi na kuongeza wigo wa upatikanaji wa nishati endelevu.

Aidha, Waziri Mkuu ameongeza kwa kusema kuwa "Baada ya jumuiya za kimataifa kuanzisha kampeni hii Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan alikuwa wa kwanza kuibeba na kuileta nchini Tanzania kwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa vitendo jambo ambalo limeongeza msukumo na kukuza matumizi ya nishati safi hasa katika maeneo ya vijijini"

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) amesaini Kitabu cha M...
31/12/2024



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) amesaini Kitabu cha Maombolezo Ubalozi wa India nchini kufuatia kifo cha Waziri Mkuu Msataafu wa India, Mhe. Manmohan Singh, kilichotokea Desemba 26, 2024

Waziri Kombo aliwasili ubalozini hapo Desemba, 31, 2024 na kupokewa na Balozi wa India nchini, Mhe. Bishwadip Dey.

Balozi Kombo aliwasilisha salamu za pole kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo alimweleza Hayati Manmohan k**a kiongozi mahiri aliyeimarisha uhusiano mzuri na Tanzania katika mihula miwili ya utawala wake kuanzia mwaka 2004 hadi 2014.
Katika kipindi hicho cha ungozi wake Hayati Manmohan aliwahi kufanya ziara nchini Tanzania wakati wa Serikali ya awamu ya nne iliyokuwa ikiongozwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete..

 Waziri wa Madini, Anthony Mavunde (Mb) amesimamisha shughuli za uchimbaji zilizokuwa zikifanywa na kampuni ya G & I Tec...
31/12/2024



Waziri wa Madini, Anthony Mavunde (Mb) amesimamisha shughuli za uchimbaji zilizokuwa zikifanywa na kampuni ya G & I Tech Mining Company Ltd kwa kipindi hichi cha masika na pia mpaka pale tathmini ya kitaalam ya mazingira itapokamilika juu ya shughuli za uchimbaji madini kwenye Mto Zila.

Ameyasema hayo katika kijiji cha Ifumbo, Wilayani Chunya alipotembelea eneo la leseni ya mwekezaji ambalo lilivamiwa na wananchi na kusababisha mgogoro mkubwa na uharibifu wa mali za mwekezaji huyo.

"Tumetembelea maeneo yote mawili, na sote tumejionea hali halisi ya mazingira. Ni dhamira na maelekezo ya Mh Rais Dkt. Samia S. Hassan kuona shughuli zote za kiuchumi hususan za madini zinafanyika kwa utulivu bila kuleta migogoro na pasipo kuathiri mazingira ya eneo shughuli zinapofanyika.

Nimesikiliza hoja za wananchi juu ya uharibifu wa mazingira ya Mto Zila,serikali itaunda Timu ya wataalamu kufanya tathmini ya kina ya mazingira juu ya athari zinazoweza kutokea wakati wa uchimbaji wa madini na kwasasa shughuli zote za uchimbaji madini zisimame kipindi hichi cha masika k**a NEMC ilivyoelekeza.

Wizara ya Madini kwa kushirikiana na Watalaam wa Mazingira, wataalam wa Mkoa na wananchi katika muda mfupi ujao inakwenda kuunda Timu ya pamoja ya kufanya tathmini ili itueleze kitaalam iwapo shughuli hizi zinaweza kuendelea kufanyika pasipo athari kwenye mazingira ya Mto Zila.

Nitumie fursa hii kuwataka wananchi wote kuacha vitendo vya uvunjifu wa amani na kujichukulia sheria mkononi,tunalaani kitendo cha kuvamia na kuharibu mali za mwekezaji“Alisema Mavunde

Awali, akitoa maelezo ya utangulizi, Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mbarak Batenga alishukuru ujio wa Waziri wa Madini na kusisitiza kwamba sasa anaona mwanga ambao unakwenda kuleta suluhisho la kudumu katika mgogoro baina ya mwekezaji na wananchi wa kijiji cha Ifumbo na kuwa serikali ngazi ya wilaya itaendelea kusimamia sheria na kanuni ili kuhakikisha eneo hilo linakuwa salama muda wote.

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na  Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe.Geor...
30/12/2024



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe.George Simbachawene ametoa wito kwa Watanzania wenye sifa za kujiandikisha katika Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, kujitokeza kwa wingi katika vituo ili kupata Kitambulisho cha Mpiga Kura kitakachowawezesha kupata haki ya kuchagua Viongozi katika Uchaguzi Mkuu ujao .

Pia, Mhe.Simbachawene amewataka Watumishi wa Umma nchini kuhakikisha wanatumia haki yao kujiandikisha kwenye daftari hilo ili kuwawezesha kuchagua viongozi akiwemo Rais, Wabunge pamoja na Madiwani kwenye uchaguzi huo .

Mhe.Simbachawene ametoa wito huo leo Jumatatu Desemba 30, 2024 mara baada ya kuboresha taarifa zake kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura katika Kituo cha Wapiga Kura kilichopo Kata ya Pwaga Wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma.

Amesema kitendo cha kwenda kuboresha taarifa katika kituo husika kwa Mtumishi wa Umma ni kujihakikishia usahihi wa taarifa zake pamoja na uhakika wa mahali atakapopigia kura.

“ Nimefika hapa ndani ya muda mfupi nimeboresha taarifa zangu ambapo nimepata kitambulisho kipya kitakachoniwezesha kutumia haki yangu ya kidemokrasia muda utakapowadia wa
kuchagua na kuchaguliwa ”, amesema Mhe.Simbachawene.

Katika hatua nyingine Mhe.Simbachawene ameipongeza Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kwa kuboresha zoezi hilo na kufanya kazi kwa weledi inayoimarisha Demokrasia nchini huku akisifu jinsi zoezi hilo linavyoendesha kwa umakini na uharaka ili kuwawezesha wananchi kuendelea na shughuli zingine za kujiingizia kipato

Aidha, Mhe.Simbachawene amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa kinara wa kuendelea kuimarisha Demokrasia nchini na kuendelea kuiwezesha Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.

 Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) mstaafu, Jaji Frederick Werema (69), amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa Muhimb...
30/12/2024



Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) mstaafu, Jaji Frederick Werema (69), amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) akipokuwa akipatiwa matibabu.

Taarifa ya kifo chake imethibitishwa na Katibu wa Halmashauri ya Walei, Parokia ya Mtakatibu Martha Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, Salome Ntaro.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Jaji Werema amefariki dunia mchana wa leo, Jumatatu Desemba 30, 2024 katika hospitali hiyo, huku taratibu nyingine zikiendelea kupangwa na umma utajulishwa.

“Kwa masikitiko makubwa nimepokea taarifa ya kifo cha mwenyekiti wetu wa Parokia ya Martha Jaji na Mwanasheria Mkuu mstaafu, mzee wetu Frederick Werema, kilichotokea mchana wa leo katika Hospitali ya Muhimbili,” ameeleza Salome katika taarifa hiyo.

Mbali na ubobezi katika taaluma ya sheria unaojulikana na wengi, Jaji Werema amewahi kuwa Mwalimu wa Shule ya Sekondari Shaaban Robert, jijini Dar es Salaam kati ya mwaka 1979 hadi 1980.

Sambamba na nafasi hiyo, pia amekuwa wakili tangu mwaka 1984 hadi 2006 na baadaye 2009 aliteuliwa kuwa AG, nafasi aliyohudumu hadi mwaka 2014 alipojiuzulu.

Pia, amewahi kuwa Jaji wa Mahak**a Kuu katika Divisheni ya Biashara.

Kufuatia msiba huo Rais Samia ametoa salamu za pole kwa ndugu jamaaa na marafiki...:-

Repost from

Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mstaafu, Mheshimiwa Jaji Mstaafu Frederick Werema. Ninatoa pole kwa familia, Mheshimiwa Jaji Mkuu, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Majaji, ndugu, jamaa na marafiki.

Nawaombea kwa Mwenyezi Mungu awajalie subra na imani katika kipindi hiki cha kuomboleza msiba huu, na ailaze roho ya mpendwa wetu huyu mahali pema peponi.

Amina.

 Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko leo Desemba 30, 2024 ameshiriki Kikao cha Kamati ya Siasa...
30/12/2024



Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko leo Desemba 30, 2024 ameshiriki Kikao cha Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Geita, kilichofanyika katika Ukumbi wa CCM Wilaya ya Bukombe.

 *RAIS DKT. SAMIA AMLILIA MAREHEMU MHESHIMIWA JAJI MWANAISHA KWARIKO* WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Desemba 30, 2024 ...
30/12/2024



*RAIS DKT. SAMIA AMLILIA MAREHEMU MHESHIMIWA JAJI MWANAISHA KWARIKO*

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Desemba 30, 2024 amemwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye mazishi ya Mheshimiwa Mwanaisha Kwariko ambaye alikuwa Jaji wa Mahak**a ya Rufani na Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.

Akitoa Salama pole kwa waombolezaji nyumbani kwa marehemu Kondoa, Mkoani Dodoma, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Rais Dkt. Samia ameguswa na kifo cha Mheshimiwa Mwanaisha kwani alikuwa ni moja ya majaji wa mahak**a ya rufani wenye uwezo mkubwa katika nafasi zote alizozitumikia.

Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Marehemu Mheshimiwa Mwanaisha alikuwa kiongozi aliyetekeleza wajibu wake kwa weledi na uadilifu “Msiba huu kwetu ni mzito, jukumu letu Wanakondoa, Watanzania, Majaji na wajumbe wa Tume ni kuendelea kumuombea kwa Mwenyezi Mungu”

Aidha, Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa kila mmoja kuenzi yote mazuri aliyoyafanya Mheshimiwa Mwanaisha katika kipindi chake chote cha utumishi wa umma kwani kufanya hivyo kutakuwa ni njia nzuri ya kuweka kumbukumbu ya kazi zake.

Kwa upande wake, Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahimu Juma amesema kuwa Mheshimiwa Mwanaisha Kwariko aliishi kiapo cha Uhakimu kwa kutoa huduma kwa wananchi ikiwemo kutatua migogoro kwa uadilifu bila upendeo wowote,

“Mheshimiwa Mwanaisha alikuwa na ubinadamu na utu, maisha yake yalikuwa ni yakusaidia watu wengine, sisi tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwani uhai wake umetusaidia sana katika shughuli mbalimbali za kimahak**a”

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Mhe. Jaji (Rufani) Jacobs Mwambegele amesema kuwa Mheshimiwa Mwanaisha ameondoka katika kipindi ambacho tume ilikuwa inamuhitaji hasa katika kipindi hiki ambacho tume hiyo ipo katika mchakato wa kuboresha daftari la kudumu la wapiga kura kuelekea uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani

 Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amefanya ziara katika wilaya ya Kigamboni kujionea maendeleo ya miradi ya ujenzi wa ba...
30/12/2024



Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amefanya ziara katika wilaya ya Kigamboni kujionea maendeleo ya miradi ya ujenzi wa barabara na kutoa maelekezo kwa mkandarasi anayetekeleza mradi huo, kampuni ya Nyakemore Engineering Group, ili kuhakikisha kazi zinakamilika kwa wakati na ubora wa hali ya juu.

Akiwa katika eneo la Kigamboni Mnadani, Waziri Ulega ameeleza kuwa barabara hiyo ni muhimu kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi, hivyo ni lazima marekebisho yake yakamilike haraka.

Amesisitiza umuhimu wa kuhakikisha barabara haifungwi kabisa wakati wa ujenzi ili kuepusha athari kwa shughuli za kijamii, na kwa wananchi wanaokwenda kufuata huduma za kijamii ikiwemo huduma za afya, masoko, ofisi za umma.

“Ni lazima barabara iwe inapitika hata wakati wa ujenzi ili wananchi waendelee kupata huduma muhimu. Tunataka kazi hii ikamilike ifikapo Januari 30, 2025, na nitakuja kukagua na kuifungua rasmi. Mkandarasi anapaswa kufanya kazi usiku na mchana, kuongeza wataalamu, vibarua, na vifaa ili kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati na na changamoto ya msongamano inatatuliwa haraka,” alisema Ulega.

Aidha, Waziri Ulega ameagiza kuwekwa utaratibu wa kudhibiti kasi ya malori yanayopita katika barabara ya Kigamboni, ili kuhakikisha usalama wa watumiaji wa barabara.

Pia amesisitiza umuhimu wa kujenga vituo vya mabasi kandokando ya barabara hiyo ili kuimarisha usafiri kwa wananchi.

Waziri Ulega amemtaka mkandarasi kutumia njia za ubunifu ili kuondoa msongamano wa magari katika eneo la Kigamboni Mnadani na maeneo mengine na kuhakikisha shughuli za ujenzi haziathiri ratiba za kila siku za wakazi wa eneo hilo.

 Washukiwa  wawili wanaotuhumiwa na kesi ya mauaji ya mtoto wa mfanyabiashara  jijini Dodoma Zainab Zenngo almaarufu 'Jo...
30/12/2024



Washukiwa wawili wanaotuhumiwa na kesi ya mauaji ya mtoto wa mfanyabiashara jijini Dodoma Zainab Zenngo almaarufu 'Jojo' Graison Kanyenye (6) wamefikishwa mahak**ani leo jijini Dodoma.

Mtoto wa mfanyabiashara huyoanadaiwa kuuawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani wakati mama yake akiwa matembezini usiku wa kuamkia Desemba 25, 2024.

Heri ya Kumbukizi ya Siku ya Kuzaliwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko
30/12/2024

Heri ya Kumbukizi ya Siku ya Kuzaliwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko

 Rais wa zamani wa Marekani Jimmy Carter amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 100, kituo alichoanzisha kimethibitisha....
30/12/2024



Rais wa zamani wa Marekani Jimmy Carter amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 100, kituo alichoanzisha kimethibitisha.

Mkulima huyo wa zamani wa karanga aliishi muda mrefu kuliko rais yeyote katika historia ambapo alisherehekea siku yake ya kuzaliwa ya 100 mnamo Oktoba.

Kituo cha Carter, ambacho kinatetea demokrasia na haki za binadamu kote duniani, kilisema alifariki Jumapili mchana nyumbani kwake huko Plains, Georgia.

Mwanademokrasia huyo alihudumu k**a rais kuanzia mwaka 1977 hadi 1981, kipindi ambacho kilikumbwa na migogoro ya kiuchumi na kidiplomasia.

Baada ya kuondoka Ikulu ya White House na viwango vya chini vya idhini, sifa yake ilirejeshwa kupitia kazi ya kibinadamu ambayo ilimletea Tuzo ya Amani ya Nobel.

"Baba yangu alikuwa shujaa, sio kwangu tu bali kwa kila mtu anayeamini katika amani, haki za binadamu, na upendo usio na ubinafsi," mwanawe, Chip Carter, alisema katika taarifa.

"Dunia ni familia yetu kwa sababu ya jinsi alivyoleta watu pamoja, na tunakushukuru kwa kuheshimu kumbukumbu yake kwa kuendelea kuishi imani hizi za pamoja."

Carter - ambaye kabla ya kuwa rais alikuwa gavana wa Georgia, luteni katika jeshi la wanamaji la Marekani na mkulima - ameacha watoto wake wanne, wajukuu 11 na vitukuu 14.

Mkewe, Rosalynn, ambaye alikuwa walioana miaka 77, alikufa mnamo Novemba 2023.

 Waziri wa Ujenzi, Mheshimiwa Abdallah Ulega, ametembelea eneo la daraja la Mzinga Mbagala wilaya ya Temeke mkoani Dar e...
29/12/2024



Waziri wa Ujenzi, Mheshimiwa Abdallah Ulega, ametembelea eneo la daraja la Mzinga Mbagala wilaya ya Temeke mkoani Dar es Salaam, kukagua maandalizi ya ujenzi wa miradi mikubwa inayolenga kupunguza msongamano wa magari katika eneo hilo.

Miradi hiyo ni upanuzi wa barabara kutoka Mbagala Rangi Tatu hadi Kongowe yenye urefu wa Kilometa 3.8 kwa kiwango cha lami na ujenzi wa daraja jipya la Mzinga.

Akizungumza na waandishi wa habari, Waziri Ulega amesema miradi hii ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kutatua changamoto za msongamano jijini Dar es Salaam.

“Tumepokea maelekezo mahususi kutoka kwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha msongamano mkubwa unaoathiri watumiaji wa barabara katika eneo hili unakwisha. Watanzania wanapoteza hadi masaa matatu kwenye foleni. Tunakwenda kujenga barabara sita, mbili kati ya hizo zitakuwa maalum kwa mabasi yaendayo haraka (BRT), na daraja la Mzinga litapanuliwa kuwa na urefu wa mita 60,” alisema Ulega.

Ameongeza kuwa Serikali itahakikisha miradi hiyo inatekelezwa kwa viwango vya juu kwa kuwapa kazi wakandarasi wenye uwezo mkubwa.

Kwa mujibu wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mhandisi Mohamed Besta, amesema ujenzi wa daraja la Mzinga unafadhiliwa na Benki ya Dunia (World Bank), ambapo benki hiyo imetoa takribani dola za Kimarekani milioni 70 kupitia Mpango wa Dharura (Crisis Response Window).

“Manunuzi ya miradi hii yanatarajiwa kukamilika Januari 31, 2025, na mkandarasi atapatikana Februari 2025. Ujenzi wa barabara ya kilomita 3.8 na daraja la Mzinga utaanza mara moja” alisema Besta.

Daraja la sasa la Mzinga lenye urefu wa mita 45 na upana wa mita 9 litaongezewa njia mbili kila upande na sehemu ya mabasi yaendayo haraka, huku barabara ya Mbagala Rangi Tatu hadi Kongowe ikipanuliwa kuwa na njia sita pamoja na maeneo ya watembea kwa miguu na waendesha pikipiki.

Mhandisi John Mkumbo ambaye ni Meneja wa TANROADS Mkoa wa Dar es Salaam, amesema fidia ya shilingi bilioni 12.6 tayari inalipwa kwa wananchi wanaopisha mradi huo.

Kwa upande

 ALIYEKUWA Diwani wa kata ya Bendera wilayani Same mkoani Kilimanjaro kupitia chama cha Chadema mwaka 2015-2020, Michael...
27/12/2024



ALIYEKUWA Diwani wa kata ya Bendera wilayani Same mkoani Kilimanjaro kupitia chama cha Chadema mwaka 2015-2020, Michael Mcharo (52), anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani humo kwa kosa la mauaji ya Edson Shangari (59), mkulima kwa kumpiga risasi tatu mwilini mwake.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, SACP Simon Maigwa alisema kuwa, tukio hilo limetokea Disemba 26 mwaka huu majira ya saa tatu na nusu asubuhi huko kitongoji cha Kaloleni Kijiji cha Bendera kata ya Bendera.

Alisema kuwa, mtuhumiwa huyo alimpiga marehemu risasi tatu, moja mkono wa kushoto, kifuani kushoto na shavu la kushoto ambapo chanzo ni ugomvi baina yao uliotokana na mgogoro wa shamba tangu mwaka 2022.

Kamanda huyo alidai kuwa, mgogoro huo haukupatiwa ufumbuzi hadi tukio lilipotokea juzi.

Aliendelea kudai kuwa, marehemu alikuwa anaelekea shambani kwake na akiwa njiani hatua chache kabla ya kufika shambani alikutana na mtuhumiwa ambaye alimshambulia kwa kumpiga risasi tatu nakumsababishia kifo.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika kituo cha afya cha Ndungu kusubiria uchunguzi wa Daktari.

Kwa mujibu wa baadhi ya wananchi ambao wa kata ya Bendera ambao hawakutaka majina yao kuandikwa walidai kuwa, Diwani huyo mstaafu mara kadhaa amekuwa akitumia nguvu kuchukua mali za watu hasa kipindi chake alipokuwa kiongozi huku mara kwa mara amekuwa akiwatishia wananchi.

“Huyo baba tunashukuru sana leo amek**atwa maana wananchi wote kwenye hii kata tulikuwa tunamuogopa sana na mara nyingi amekuwa akitisha wananchi na wakati mwingine anatumia nguvu kuzulumu wananchi mali hata hilo shamba ambalo alikuwa analigombea na marehemu sio lake sisi tunajua lakini sasa tulikuwa tunaogopa kueleza ukweli” alisema mmoja wa wananchi wa kata ya Bendera.

 WATU tisa wamefariki Dunia baada ya gari aina ya Noah walilokuwa wakisafiria kutoka Tarakea wilayani Rombo kugongana us...
26/12/2024



WATU tisa wamefariki Dunia baada ya gari aina ya Noah walilokuwa wakisafiria kutoka Tarakea wilayani Rombo kugongana uso kwa uso na basi la Ngasere lililokuwa likitokea Dodoma kuelekea Rombo.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Mwenyekiti wa ulinzi na usalama ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Rombo, Raymond Mangwalla alisema kuwa tukio hilo limetokea jana majira ya jioni katika maeneo ya Tarakea.

Alisema kuwa, katika ajali hiyo watu tisa ambao ni wakiume watano na wakike wanne waliokuwa katika Noah walifariki Dunia papo hapo huku mpaka sasa yupo majeruhi mmoja ambaye amekimbizwa hospitali ya Huruma kwa matibabu.

Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa, chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi ambapo Dereva wa Noah alikuwa akilipita gari jingine ndipo alipokutana na basi na Ngasere na kugongana nalo uso kwa uso.

MWISHO.

 Mtoto Grayson Kanyenye (6) anadaiwa kuuawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani wakati mama yake akiwa matembezini usiku...
26/12/2024



Mtoto Grayson Kanyenye (6) anadaiwa kuuawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani wakati mama yake akiwa matembezini usiku wa kuamkia jana, Jeshi la polisi limesema mwili wa mtoto huyo ulikutwa ndani ya nyumba ukiwa na majeraha shingoni.

Kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma, George Katabazi amesema jana Disemba 25, 2024 kuwa tukio limetokea saa moja kamili asubuhi katika mtaa wa Bwawani, Ilanzo Extension jijini Dodoma nyumbani kwa Ofisa Uvuvj wa Mtera, Hamis Mohamed ambaye anatajwa kuwa mpenzi wa mama wa mtoto huyo anayetambulika kwa jina la Jojo.

Kamanda wa polisi amesema Hamis na Mama wa mtoto huyo walitoka kwenda matembezini na kumuacha mtoto huyo chini ya uangalizi wa dereva bodaboda wa Ilazo Extension anayetambulika k**a Kelvin Gilbert ambaye walimfahamu kupitia huduma ya usafiri anayoitoa kwa familia hiyo.

"Kelvin Gilbert aliachiwa mtoto huyo amwangalie, wakati Hamis na mama yake walipoondoka kwenda matembezini, lakini waliporudi saa moja kamili asubuhi walikuta mtoto Graison Kanyenye Mabuya amepigwa kichwani na kitu kizito kwenye paji la uso, huku akiwa na majeraha shingoni" amesema Kamanda wa polisi.

Aidha familia ya ya mtoto huyo imetoa taarifa kwamba mazishi ya Greyson Kanyenye aliyefariki Tar 25/12/2024 yatafanyika Leo Alhamis Tarehe 26/12/2024 kwenye Makaburi ya kilimo kwanza ,kwa Malanga yakitanguliwa na ibada itakayofanyika kuanzia saa sita mchana nyumbani kwa Mama wa Mtoto barabara ya Waziri Mkuu karibu na kituo cha mafuta cha Emirates.

 Zaidi ya wafungwa 1,500 wametoroka katika gereza moja nchini Msumbiji, wakitumia fursa ya machafuko ya kisiasa yanayoen...
26/12/2024



Zaidi ya wafungwa 1,500 wametoroka katika gereza moja nchini Msumbiji, wakitumia fursa ya machafuko ya kisiasa yanayoendelea yaliyochochewa na matokeo ya uchaguzi yenye utata, polisi wamesema.

Watu 33 waliuawa na 15 kujeruhiwa katika mapigano na walinzi, mkuu wa polisi Bernardino Rafael aliambia mkutano na waandishi wa habari.

Maandamano yalizuka siku ya Jumatatu kujibu mahak**a ya juu zaidi ya Msumbiji ikithibitisha kwamba chama tawala cha Frelimo, kilichokuwa madarakani tangu mwaka 1975, kilishinda uchaguzi wa rais wa Oktoba.

Bw Rafael alisema makundi ya waandamanaji wanaoipinga serikali yalikaribia gereza hilo katika mji mkuu Maputo siku ya Jumatano. Wafungwa walitumia machafuko hayo kuangusha ukuta na kutoroka, alisema.

Msumbiji imekumbwa na machafuko tangu uchaguzi uliozozaniwa mwezi Oktoba. Matokeo rasmi yalionyesha mgombea urais wa chama tawala cha Frelimo, Daniel Chapo, akishinda.

Maandamano mapya yalizuka siku ya Jumatatu, wakati mahak**a ya kikatiba ilipoamua kuwa Chapo alishinda uchaguzi huo, huku ikirekebisha tofauti yake ya ushindi.

Matokeo ya awali ya mwezi Oktoba yalisema Daniel Chapo alipata asilimia 71 ya kura dhidi ya mpinzani wake mkuu Venâncio Mondlane aliyepata 20%. Mahak**a sasa imeamua kwamba alishinda 65% dhidi ya 24% ya Mondlane.

Address


Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00

Telephone

+255713422313

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Michuzi TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Michuzi TV:

Videos

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Opening Hours
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Videos
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share