GOOD ONE TV

GOOD ONE TV I am journalist

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi na utenguzi wa viongozi mbalimba...
08/01/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi na utenguzi wa viongozi mbalimbali. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka,

Mhe. Paul Christian Makonda (Mb.) ameteuliwa kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo. Kabla ya uteuzi huu, Mhe. Makonda alikuwa Naibu Waziri katika Wizara hiyo;

Mkuu wa Makampuni Binafsi ya Ulinzi na Polisi Wasaidizi Tanzania, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Ulrich Matei, Leo Janua...
07/01/2026

Mkuu wa Makampuni Binafsi ya Ulinzi na Polisi Wasaidizi Tanzania, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Ulrich Matei, Leo Januari 07, 2026, akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara kwa ajili ya ufunguzi wa mafunzo kwa Wakuu wa Polisi Jamii wa Mikoa, Vikosi na Wilaya.

Mikoa inayoshiriki katika Mafunzo hayo ni Mtwara, Lindi na Ruvuma.

AAH! SHEMEJI... ACHA!SEHEMU YA 01Aisha alijiona k**a mtu mwenye bahati ya mtende kwa kutongozwa na shemeji yake. Nafsi y...
06/01/2026

AAH! SHEMEJI... ACHA!

SEHEMU YA 01

Aisha alijiona k**a mtu mwenye bahati ya mtende kwa kutongozwa na shemeji yake. Nafsi yake ilikuwa njia panda; aliwaza amkubalie au amkatalie kwa kigezo cha undugu wa shemeji. Hata hivyo, akili yake iligubikwa na taswira ya utajiri wa shemeji yake huku akilinganisha na hali duni aliyokuwa nayo.

“Endapo nikikubali na dada akigundua, itakuwaje?” alijiuliza moyoni. “Aah! Lakini si amenitongoza mwenyewe? Siwezi kupiga teke fuko la pesa... Potelea mbali.”

Siku iliyofuata, Aisha alikutana na shoga yake kipenzi, Anita. Bila kusita, Aisha alimsimulia Anita kuhusu yaliyojiri kati yake na shemeji yake.

“Shoga yangu, basi ngoja nikupe mkanda kamili.”
Anita alichekelea kwa hamu. “Hapo ndipo ninapokupendea! Tukikutana barazani huchangamka kwa stori. Haya shoga, hebu nipe huo ubuyu.”

Aisha akaanza kuelezea, “Jana usiku wakati tunakula, dada aliwahi kushiba akaenda zake kulala. Sebuleni tukabaki mimi na shemeji tukipata chakula cha usiku. Basi shoga yangu, shemeji si ndio akaanza... ‘Ooh Aisha unajua wewe ni mzuri sana kuliko hata dada yako.’ Mimi nikabaki kucheka tu.

Dakika chache zikapita mara akaanza tena, ‘Aisha, najua wewe ni mtu mzima na unaweza kutunza siri. Mimi nataka uwe mpenzi wangu lakini dada yako asijue.’”

Aisha alivuta pumzi kidogo kisha akaendelea, “Shoga, nilishtuka! Kwani sikutegemea hata siku moja k**a shemeji atakuja kunitamkia maneno k**a yale, ukizingatia jinsi ninavyomheshimu.”

“Shuu! Atabeba mimba huyo!” Anita alidakia kwa mshangao uliochanganyika na furaha ya umbea. “Heshima hiyo weka pembeni, kwani yule ni baba yako mzazi?” Wote kwa pamoja waliangua vicheko vya umbea.

Anita akaendelea kumpa darasa, “Sasa sikiliza shoga yangu nikwambie; maisha ndiyo hayo yanaanza kukunyookea. Ukizingatia shemeji yako alivyo na utajiri, kumuacha ni sawa na kukataa kuolewa na mfalme ili uje kuwa malkia.”

📣🔈🔉SIMULIZI HII HAIJAFIKA MWISHO

Rais Magufuli k**a unamkumbuka weka ❤️❤️
06/01/2026

Rais Magufuli k**a unamkumbuka weka ❤️❤️

Ulinzi imara ndio  Msingi wa Amani.
03/01/2026

Ulinzi imara ndio Msingi wa Amani.

Askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) walionyesha kwa mafanikio ujuzi wao wa hali ya juu wa kurusha I...
03/01/2026

Askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) walionyesha kwa mafanikio ujuzi wao wa hali ya juu wa kurusha ICV, uliopatikana hatua kwa hatua kupitia mafunzo ya kina kwenye MIC & S.

03/01/2026

Salamu za kipekee kwa mashabiki wangu wapya chipukizi! Vallen Cosmas

Ukitaka kupanga uzazi  kwa njia asili  hii ni njia moja wapo  isiokua na madhara   zingatia tu  siku ya kwanza unapotoka...
31/12/2025

Ukitaka kupanga uzazi kwa njia asili hii ni njia moja wapo isiokua na madhara zingatia tu siku ya kwanza unapotoka bridi kunywa mbegu mbili siku ya kwanza na mbegu mbili siku ya pili hakuna mimba itakayoingia kwa bahati mbaya hata ukisex kwenye siku za hatari usijichanganye umeze ukiwa piriodi lakini sio njia ya kudum kwa maana nzima mwezi ujao lazima umeze kingine k**a hutaki kuonekana kwenye lamli na kamera za wanga tafta penye bwawa la maji chukua tonge dogo la ugari kiisha pachika mbegu mbili litamkie tonge tia mdomoni zama umeze kiisha ibuka nikitendo cha sekunde 3 nimeona niwaandikie fupi fupi kunawatu wavivu wa kusoma ndefu

Nahodha wa Ureno Cristiano Ronaldo anasema hatastaafu soka hadi afunge bao lake la 1,000 katika maisha yake ya soka.Mche...
31/12/2025

Nahodha wa Ureno Cristiano Ronaldo anasema hatastaafu soka hadi afunge bao lake la 1,000 katika maisha yake ya soka.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 40 alifunga mara mbili katika ushindi wa 3-0 wa Al-Nassr dhidi ya Al Akhdoud siku ya Jumamosi na kufikisha mabao 956 kwa klabu na nchi.

Mshambuliaji huyo katili wa Nyavu na ambaye alijiunga na Al-Nassr mwaka wa 2022, alisaini mkataba mpya wa miaka miwili na klabu hiyo ya Saudi Arabia Julai mwaka jana.

Ronaldo amefunga mabao 13 katika mechi 14 alizocheza msimu huu akiwa na Al-Nassr, ambao wako kileleni kwa pointi nne kwenye Msimamo wa Saudi Pro League.

Ronaldo anashikilia rekodi ya kufunga mabao mengi zaidi kwa Ureno (143) na Real Madrid (450), na ndiye mchezaji pekee aliyefunga mabao 100+ kwa vilabu vinne Manchester United, Real Madrid, Juventus na Al-Nassr.

Mshambuliaji huyo alisema mnamo Novemba kwamba Kombe la Dunia la 2026 nchini Marekani, Canada na Mexico litakuwa mchuano wake wa mwisho wa Kimataifa.

Alikuwa nahodha wa Ureno waliposhinda Euro 2016 nchini Ufaransa.

12/12/2025

Salamu za kipekee kwa mashabiki wangu wapya chipukizi! Vallen Cosmas, Abieremana Taratibu

Nikikuomba unitumie nauli nije mkoani kwenu utakubali? 🫵😉☺️🇹🇿🇰🇪🇩🇪🇧🇮
10/12/2025

Nikikuomba unitumie nauli nije mkoani kwenu utakubali? 🫵😉☺️🇹🇿🇰🇪🇩🇪🇧🇮

*"Utangazaji ni daraja la kuwasilisha ujumbe, kuleta mabadiliko na kuhamasisha jamii. Kwa sauti yako, unaweza kufikia mi...
10/12/2025

*"Utangazaji ni daraja la kuwasilisha ujumbe, kuleta mabadiliko na kuhamasisha jamii. Kwa sauti yako, unaweza kufikia mioyo na akili za watu, kuwapa habari muhimu, burudani, na maarifa. Tangaza kwa uwazi, kwa upole, na kwa moyo wa kuwahudumia wasikilizaji wako. Kila neno unalosema lina nguvu ya kuleta matumaini, kusimulia hadithi, na kuimarisha mshik**ano wa jamii. Usikose nafasi ya kuwa sauti ya mabadiliko."*

Address

Mwanza

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when GOOD ONE TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share