Faidika na Kilimo Cha Umwagiliaji Kwa Kutumia Pampu za Solar Toka Simu Solar Tanzania.
TANROADS MARA YAENDELEA KUIMARISHA MIUNDOMBINU YA BARABARA KUVUTIA UWEKEZAJI
Na Ghati Msamba-Musoma
WAKALA barabara(Tanroads) mkoa wa Mara umesema utaendelea kuimalisha na kupitika kwa barabara ili kuwavutia wawekezaji.
Meneja wa Tanroads mkoa wa Mara mhandisi Vedastus Malibe amesema haya kwenye mdahalo wa kujadili fursa za mkoa wa Mara bora Kwa uwekezaji na kuishi uliofanyika
Mhandisi Marine amesema ili muwekezaji aweze kufanya shughuli zake vizuri kuna hitajika kuwa na uhakika wa miundombinu kwenye uaafirishaji ikiwemo barabara.
Pia amesema wakati wote watahakikisha barabara zinapitika ili kila mmoja aweze kufanya shughuli za kiuchumi wakiwemo wawekezaji ndani na nje.
" Waandishi wa Habari mnalo jukumu la kuhakikisha elimu juu ya ulimishaji wa kulinda miundombinu ya barabara inatolewa kwa jamii kutokana na umuhimu wake katika suala Zima la uwekezaji Katika kuwavutia wawekezaji".Amesema Mhandisi Maribe.
Amesema wapo watu ambao hawana nia njema na wamekuwa wakihujumu miundombinu ya barabara ambao wanapaswa kuelimishwa.
Meneja Maribe amewashukuru waandishi wa habari Kwa kumuarika katika Mdahalo huo na kuhakikisha kutoa ushirikiano wao katika kutekeleza majukumu ya kikazi.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa klabu ya Waandishi wa Habari mkoa wa Mara Mugini Jacob amemshukuru mkuu wa mkoa na wadau wengine kuwaunga mkono kwenye mdahalo huo ambao utakuwa endelevu
ARUSHA: RIDHIWANI KIKWETE ATOA WITO KWA MAAFISA RASILIMALI WATU KUTUMIA MIFUMO YA KIUTENDAJI KUTENDA HAKI.
Na Ghati Msamba
IMEELEZWA kuwa Mabadiliko ya kweli ya mienendo ya Kiutendaji miongoni mwa Maafisa Rasilimali Watu yataletwa na matumizi salama ya mifumo ya kazi Kwa watumishi
Naibu Waziri wa Utumishi na Utawala Bora Ridhiwani Kikwete ameyasema haya wakati alipokuwa akifunga Mkutano wa 11 wa wanachama wa Chama Cha Maafisa uliofanyika katika Ukumbi wa AICC , jijini Arusha.
Naibu Waziri Kikwete, ametoa ushauri huo wa mienendo ya Kiutendaji Kwa Maafisa hao kuendelea kutumia mifumo ya utendaji kazi ili kuwezesha haki na wajibu kutolewa kwa watumishi wa umma Katika RasilimaliWatu Tawala na Rasilimali Watu (AAPAM).
Akizungumza na watumishi hao katika siku ya mwisho ya Mkutano huo wa siku tatu, Waziri Kikwete aliwakumbusha watumishi hao mifumo mbalimbali iliyokwisha tengenezwa kuwezesha watumishi kukopa, kuhama na kupima utendaji kazi.
Katika hatua nyingine Naibu Waziri Kikwete amewaonya Maafisa hao juu ya tabia inayoendelea ya kutowatendea vyema watumishi wenzao wanaowaongoza na kwamba Kwa kufanya hivyo ni kuwa roho mbaya walizonazo Kwa baadhi ya Watendaji hao akitoa mfano wa Rorya na taratibu za upandishaji madaraja.
Aidha Naibu Waziri Kikwete amewataka watumishi hao kubadilika na badala yake kushirikiana waheshimiane na kupendana katika kutekeleza na kuendelea na utendaji wa majukumu ya kazi za umma na si vinginevyo.
PICHA: Mwandishi wa habari nguli Bw George Marato akiteta jambo na waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano Tanzania Mh Kassim Majaliwa katika moja ya mikutano mkoni Mara.
PROFESA NDAKIDEMI AISHAURI SERIKALI KUANZISHA SERA YA AFYA YA SELI MUNDU
Na Gift Mongi-Dodoma
Mbunge wa Jimbo la Moshi Vijijini Profesa Patrick Ndakidemi ametoa ushauri huo leo tarehe 08.11.2023 wakati akiuliza swali la nyongeza bungeni Dodoma kama ifuatavyo:
Pamoja na uwepo wa huduma ndogo kwa vipimo vya wagonjwa wa Seli Mundu hapa nchini, bado idadi ya wagonjwa ni kubwa, na Tanzania ni ya tano duniani na ya tatu barani Afrika kwa kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa wa Seli Mundu.
Je? Serikali haioni umuhimu wa kuwa na sera ya afya ya Seli Mundu itakayotoa maelekezo ya kuwahudumia wagonjwa hawa?
....
WAANDISHI WA HABARI MKOA WA KAGERA WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA KUZINGATIA MAADILI.
Na Angela Sebastian-Bukoba
Waandishi wa habari wa mkoa wa Kagera wametakiwa kufanya kazi kwa weledi,kufuata maadili ya Waandishi wa habari bila upendeleo na kutoshinikizwa na mtu yoyote ili kuandika habari za uongo zitakazohatarisha amani ya nchi yetu.
Akiongea na waandishi wa habari ambao ni wanachama wa chama cha waandishi wa habari mkoani humo (KPC) mkuu wa Wilaya ya Bukoba Elasto Siima katika maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani ambapo yalianza Mei 3 mwaka huu na kilele ni Mei 20, mwaka huu ambapo kwa mkoa wa Kagera imeadhimishwa leo.
"Kubalance ni wajibu wa mwandishi kufuatailia pande zote mbili mfano kunapokuwepo malalamiko kutoka pande zote,mfano pale unapolazimishwa useme hivi kwamba utalipwa kitu fulani lakini unajua unachosema siyo sahii hivyo timizeni majukumu yenu kwa weledi mliousomea na mlionao"
Siima amesema waandishi wa habari wa mkoa wa Kagera wamekuwa kichocheo cha maendeleo ya mkoa huo ndani na nje kutokana na kuandika habari za kuutangaza vyema huku akiwashauri waendelee kutoa ushirikiano huo na kuahidi kwamba Serikari ya Wilaya itaendelea kushirikiana nao ili kuleta maendeleo makubwa .
Kwa upande wa mwezeshaji Peter Matete ambaye ni mwenyekiti wa chama cha mawakili wa kujitegemea mkoani Kagera (TLS) wakati wa maadhimisho hayo ambapo alidadavua juu ya ya kauli mbiu ya siku hiyo ambapo amesema kuwa mtu yoyote kama hajasikilizwa anakuwa amenyimwa haki ya msingi ya mwanadamu ambayo anapsswa kuipata tangu anapozaliwa .
Naye mwenyekiti wa KPC Mbeki Mbeki amewashauri waandishi kufanya kazi kwa kufuata misingi mikuu ya mwandishi wa habari ambayo ni mustakabali wa haki.
Naye mdau wa habari ambaye pia ni makamu mwenyekiti wa chama kikuu cha ushirika mkoani humo (KCU 1990) Respicius John amewaomba waandishi wa habari kama wadau muhimu kuendelea kuelimisha wananchi hasa wakati huu tunapoelekea kwenye msimu wa 2023/2024 katika kutunza ubora wa zao
MBUNGE GHATI ZEPHANIA AIOMBA SERIKALI KUTATUA CHANGAMOTO YA UKOSEFU WA VIFAA TIBA NA MADAKTARI MKOANI MARA.
Na Emmanuel Chibasa.
Changamoto ya ukosefu wa Vifaa tiba pamoja na upungufu wa madaktari na Watoa huduma ya Afya katika hospitali, zahanati na vituo vya Afya ni Moja ya tatizo kuwa linalowakabili Wananchi wa Mkoa wa Mara kupata Huduma ya matibabu kama sera ya Afya inavyoelekeza.
Licha ya Serikali kujenga vituo vya afya 335 Kwa ajili ya Kutoa huduma ya Afya Kwa Wananchi wa Mkoa wa Mara lakini imeelezwa kuwa vituo hivyo vinashindwa Kutoa huduma stahiki kutokana na ukosefu wa Vifaa tiba, madaktari pamoja na Watoa huduma ya afya.
Kufuatia uwepo wa Changamoto hiyo Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mara Mhe.Ghati Zephania Chomete ametumia Kikao Cha bunge Cha tarehe 15 Mei 2023, katika Bunge la 12, Mkutano 11, Kikao cha 25 kupitia Bajeti ya Wizara ya Afya kueleza Changamoto wanazozipata Wananchi wa Mkoa wa Mara katika kupata Huduma za matibabu.
Akichangia katika Kikao hicho mbali na kueleza jitihada mbalimbali zilizofanywa na Serikali kuhakikisha Wananchi wanapata huduma bora lakini pia akaeleza Changamoto zinazo wakabili ikiwa ni pamoja na wananchi kutembea umbali mrefu zaidi ya 50 Km kwenda kutafuta huduma kutokana na virus vya afya na zahanati zilizojengwa kutokuwa na uwezo wa Kulaza, Kutoa huduma ya damu salama, kupiga X-ray, Utra- Sound na kufanya Operation Kwa Wananchi wa maeneo husika
KITUO CHA AFYA UMBWE KUPATA GARI LA WAGONJWA.
Na Gift Mongi-Dodoma
KutokaBungeni: Mbunge wa jimbo la Moshi vijijini Prof. Patrick Ndakidemi ameuliza swali la nyongeza kama ifuatavyo
"Kituo cha afya cha Umbwe ambacho ndio kituo pekee cha afya kwenye tarafa ya Kibosho hakina gari la kubeba wagonjwa. Je? Serikali ina mpango gani wa kutupatia gari la kubeba wagonjwa katika kituo hicho.?"
Akijibu swali hilo Naibu Waziri OR-TAMISEMI Dkt Festo Dugange(MB) amekiri kuwa kwa tarafa ya Kibosho kuna kituo cha afya kimoja na hakina gari ambapo katika mwaka huu wa fedha Mh. Rais ameahidi kupeleka magari ya wagonjwa katika halmashauri zote 184 ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
MLAO AVITAKA VYAMA VYA SIASA KUTUMIA MIKUTANO KUHAMASISHA SHUGHULI ZA KIUCHUMI
Na Angela Sebastian-Kagera
KAGERA: Mjumbe wa Halmashauri kuu Taifa (NEC) Ramadhan Mlao amevitaka vyama vya siasa kutumia vizuri uhuru waliopewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Samia Suluhu Hassani wa kufanya mikutano ya hadhara.
Ameyasema hayo akiwa mkoani Kagera kwenye ufunguzi wa kongamano la vijana mkoa huu lililofanyika kata ya Nshambya Wilaya ya Misenyi ambapo, baada ya ufunguzi huo vijana watandelea na kongamano hilo kwenye wilaya zao hadi April 5 mwaka huu kuelekea maadhimisho ya miaka 46 ya kuzaliwa CCM
Amesema siasa ni uchumi hawawezi kujenga chama bila kuimarisha uchumi kwa wanachama wao na kuwa vijana wana bahati chama chao ndicho kinaongoza serikali, kwa kuhakikisha hilo wanaona wakuu wa wilaya wameshiriki kongamano hilo.