Kusini Yetu Online Tv

Kusini Yetu Online Tv Ukarasa maalum wa habari utakaokuweza kupata taarifa zote zinazotokea ndani na nje ya Tanzania.

Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia ijulikanayo k**a Samia Legal Aid Campaign, imeendelea kuwafikia wananchi kat...
28/01/2025

Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia ijulikanayo k**a Samia Legal Aid Campaign, imeendelea kuwafikia wananchi katika Halmashauri mbalimbali za Mkoa wa Mtwara.

Katika Halmashauri ya Mji Nanyamba Mkoani Mtwara, wananchi wameendelea kupata huduma baada ya watendaji wa Kampeni hiyo kufika katika vijiji vya Malongo, Majengo na Njengwa.

Wakizungumza na vyombo vya habari wananchi hao wameeleza kufurahiswa na huduma hiyo ya msaada wa kisheria inayoambatana na elimu, wakisema kuwa imewasaidia kujua haki zao na masuala mengine ya kisheria yaliyokuwa yakiwasumbua kwa muda mrefu.

Aidha Wananchi hao walimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia kwa ubunifu huo ambao wamesema umewafikia kwa wakati muafaka ambao wana haja ya kuzifahamu haki zao za kisheria.

"Kampeni hii ni muhimunsana, na vitu k**a hivi vingekuja mapema tusingekuwa na migogoro ikiwemo ya ardhi,ndoa,mirathi na dhuluma zingine wanazofanyiwa wananchi" ameeleza Hassan Dadi mkazi wa Kijiji cha Malongo Nanyanba TC.

Mratibu wa kampeni hiyo katika Halmashauri ya Nanyamba Bwn. Christopher Kabado amewataka wananchi kuendelea kujitokeza na kupata huduma ambazo ameeleza kuwa zinatolewa bure na inaratibiwa na Wizara ya katiba na Sheria.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara-Mikindani Mwalimu Hassan Nyange kupitia mfuko wa elimu ameahidi kutoa fedha Shilingi mi...
28/01/2025

Mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara-Mikindani Mwalimu Hassan Nyange kupitia mfuko wa elimu ameahidi kutoa fedha Shilingi milioni arobaini na tatu laki tano tisini ( 43,590,000) kwa shule 11 za Serikali za Kutwa kwa ajili ya mahitaji ya kambi kwa wanafunzi wa kidato cha nne.

Mkurugenzi anatoa fedha hizo ikiwa ni mkakati mmoja wapo wa kuweka mazingira mazuri ya kujisomea kwa wanafunzi na kujiandaa vema kwenye mtihani wao wa kumaliza Elimu ya Sekondari ili Kuongeza ufaulu na kufuta daraja sifuri.

Hayo yamesemwa katika Kongamano la elimu lililofanyika katika viwanja vya Mashujaa, lenye lengo la kuhamasisha ufaulu na kuweka mikakati ya kuondoa daraja sifuri.

Amewataka Wakuu wa Shule kukaa na wazazi kuwahimiza michango ya kambi na kupongeza kuwa, Halmashauri inaendelea kupambana kuhakikisha kambi inaleta tija.

Vile vile amewaasa wanafunzi wa kidato cha nne kutopoteza muda kwa kuangalia tamthilia zisizo na maana badala yake wasome vitabu mbalimbali vitakavyo wasaidia kuongeza maarifa

Shule zitakazohusishwa na mgao huo ni pamoja na Shule ya Sekondari ya Shangani, Rahaleo, Mangamba, Sino Tanzania Friendship, Sabasaba, na Naliendele.

Shule nyingine ni Shule ya Sekondari ya Umoja, Bandari, Mikindani, Chuno na Mitengo Sekondari.

Mkuu wa mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Kenan Sawala, amewataka Wanafunzi wa kidato cha nne kusoma kwa bidii na kuhakikish...
27/01/2025

Mkuu wa mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Kenan Sawala, amewataka Wanafunzi wa kidato cha nne kusoma kwa bidii na kuhakikisha wanafanya vyema katika mitihani yao ili kujitengenezea kesho iliyo bora.

Kanali Sawala amesema hayo leo Januari 27, 2025 wakati akipngea na wanafunzi wa kidato cha nne, katika viwanja vya Mashujaa Manispaa ya Mtwara Mikindani, akiwa kwenye Kongamano la Elimu kwa Wanafunzi wa Kidato cha Nne, lililoandaliwa na ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara Mkindani.

Amewataka wanafunzi wa k**e kutoshawishika kujiingiza katika mahusiano yatayowapelekea kupata mimba za mapema huku akiwataka wavulana kutofuata mkumbo wa kujiunga na vikundi vya uhalifu.

Kadhalika Kanali Sawala, amempongeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara Mikindani Mwl.Hassan Nyange kwa jitihada zake kwenye usimamizi wa Miradi mbalimbali inayogusa sekta tofauti ikiwemo elimu, afya na nyinginezo.

Kwa upande wa Mkurugenzi wa Manisapaa hiyo Mwl. Hassan Nyange amesema matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne yaliyotoka hivi karibuni, Manispaa hiyo imepata ufaulu nzuri ambapo kwa Shule zote za Serikali na zile za Binafsi, waliopata daraja Sifuri 61, jambo linatoa hamasa kwake kuhakikisha matokeo yajayo hakuna mwanafunzi atayepata daraja hilo.

Nao Wanafunzi walioshiriki Kongamano hilo akiwemo Yusra Hamis kutoka Sekondari ya Sino amesema amefurahishwa na uwepo wa Kongamano hilo huku wakiomba jambo hilo lifanyike mara kwa mara kwani maneno yanayozungumzwa na Viongozi yanawatia moyo.

Kongamano hilo limewakutanisha Wanafunzi 2,130 wa Kidato cha Nne wa Shule 20 za Sekondari zilizopo ndani ya Manispaa ya Mtwara-Mikindani.


Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani imefanya kongamano la elimu kwa wanafunzi wa kidato cha nne, leo Januari 27,...
27/01/2025

Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani imefanya kongamano la elimu kwa wanafunzi wa kidato cha nne, leo Januari 27, 2025, katika uwanja wa Mashujaa.

Kongamano hili limejumuisha shule 20 kutoka shule mbalimbali za serikali na binafsi wapatao 2130, na limehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali Patrick Sawala, na Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Abdallah Mwaipaya.

Kauli mbiu ya kongamano hilo ni: "Ufaulu Manispaa ya Mtwara - Mikindani Bila Daraja 0 Inawezekana", ikilenga kuhamasisha wanafunzi kuwa na moyo wa bidii na juhudi ili kufikia mafanikio katika masomo yao.

Lengo kuu la kongamano hili ni kutoa motisha na mbinu za ufaulu kwa wanafunzi, sambamba na kuwaelimisha juu ya umuhimu wa kujitolea kwa bidii katika kujifunza.


Mkuu wa mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Kenan Sawala,  amewaongoza wakazi wa mkoa huu, kwenye zoezi maalum la kukata keki ...
27/01/2025

Mkuu wa mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Kenan Sawala, amewaongoza wakazi wa mkoa huu, kwenye zoezi maalum la kukata keki kwa ajili ya kusherehekea kumbikizi ya kuzaliwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, ambaye leo Januari 27, 2025 anatimiza miaka 65 ya kuzaliwa.

Rais Samia Suluhu Hassan alizaliwa Januari 27, 1960 katika kijiji cha Kizimkazi mkoa wa Kusini Unguja, visiwani Zanzibar.

Zoezi hilo lilifanyika kwenye viwanja vya Mashujaa, Manispaa ya Mtwara-Mikindani, ambalo kumefanyika kongamano la elimu kwa wanafunzi wa kidato cha nne.


Mbunge wa Jimbo la Mchinga Mkoani Lindi Mama Salma Rashid kikwete, amesema wananchi wa Jimbo hilo wamejipanga kikamilifu...
27/01/2025

Mbunge wa Jimbo la Mchinga Mkoani Lindi Mama Salma Rashid kikwete, amesema wananchi wa Jimbo hilo wamejipanga kikamilifu kuhakikisha Chama cha Mapinduzi (CCM), kinapata ushindi wa kishindo katika Uchaguzi Mkuu utakayofanyika mwaka huu.

Mama Salma Kikwete ameyasema hayo alipokuwa anazungumza katika kikao maalumu na mabalozi zaidi ya 300 uliofanyika Katika tarafa ya Mchinga huko manispaa ya Lindi.

Amesema kikao hicho cha mabalozi wa Jimbo hilo la Mchinga ni mahususi kwa ajili ya kupeana mikakati na mipango ya halmashauri ili kuhakikisha wananchi wanajitokeza kujiandikisha katika Daftari la kudumu la Wapiga Kura.

Amesema Katika kuhakikisha chama hicho kinashinda kwa kishindo ni muhimu kuwepo na Wapiga Kura wa kutosha ambao watapiga Kura na kukichagua chama hicho siku ya uchaguzi utakapofika.

Zoezi la uandikishaji na uboreshaji wa Daftari la kudumu la Wapiga Kura kwa Mkoa wa Lindi litaanza Januari 28 na kutamalizika February 3 mwaka huu.

Imeandaliwa na Hadija Omary-Lindi

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko amesema baada ya kupata uhuru mwaka 1960, Nchi za Afrika zimepig...
27/01/2025

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko amesema baada ya kupata uhuru mwaka 1960, Nchi za Afrika zimepiga hatua kubwa katika kuzalisha na kusambaza umeme kwa wananchi wao.

Dk. Biteko amesema hayo leo Januari 27 kwenye Mkutano wa nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika ‘Mission 300’ unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es salaam.

Naibu Waziri Mkuu amesema lengo kuu la mkutano huo kuitishwa ni kufikia lengo la kuongeza upatatikanaji wa umeme kwa angalau watu milioni 300 barani Afrika katika miaka mitano ijayo.

“Inasikitisha kwamba idadi ya Waafrika ambao hawana umeme inakadiriwa kuwa milioni 571.kutokana na hali hii, Mkutano huu uliitishwa, ukiwa na lengo kubwa lakini linaloweza kufikiwa la kuongeza upatikanaji wa umeme kwa angalau watu milioni 300 barani Afrika katika miaka mitano ijayo,” amesema kiongozi huyo.

Katika hatua nyingine, amesema ili kuunga mkono mpango wa Mission 300 Mikataba ya Kitaifa ya Nishati iliyobuniwa na nchi kumi na nne (14) za majaribio itatoa mfumo wa hatua zilizoratibiwa ili kufungua uwekezaji wa ziada kutoka kwa serikali, washirika wa maendeleo, wahisani, na sekta binafsi katika kufikia malengo ya upatikanaji wa nishati.

Kampeni ya Kitaifa ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia imezinduliwa rasmi mkoani Mtwara, ikiwa ni hatua muhimu katika ku...
24/01/2025

Kampeni ya Kitaifa ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia imezinduliwa rasmi mkoani Mtwara, ikiwa ni hatua muhimu katika kuimarisha upatikanaji wa haki kwa wananchi.

Uzinduzi wa kampeni hiyo umefanyika leo katika uwanja wa Nangwanda, Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani, na kuhudhuriwa na mgeni rasmi, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali Patrick Sawala.

Katika hotuba yake, Kanali Sawala amewataka wananchi wa Mtwara kujitokeza kwa wingi ili kupata huduma za kisheria zitakazotolewa bure, huku akisisitiza kuwa hii ni fursa muhimu kwa kila mmoja kushiriki katika kutatua migogoro ya kisheria.

Kanali Sawala ameeleza kuwa kampeni hii itasaidia kuongeza uelewa kuhusu haki za binadamu, hasa haki za wanawake na watoto, na itajikita zaidi katika kutatua changamoto zinazowakabili wananchi, ikiwa ni pamoja na masuala ya ukatili wa kijinsia na haki za familia.

Lengo kuu la kampeni ni kuimarisha upatikanaji wa haki kwa wananchi, kuongeza uelewa wa haki za binadamu, na kutoa msaada wa kisheria kwa jamii, wakiwemo manusura wa ukatili wa kijinsia. Aidha, kampeni hii inatarajiwa kuelimisha umma kuhusu sheria na masuala ya utawala bora, ambayo yatasaidia kuongeza amani na utulivu mkoani Mtwara.

Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Sheria kwa Umma kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Abdulrhaman Mshamu, amesema kuwa kampeni hii mkoani Mtwara itadumu kwa siku kumi na kuwa ni sehemu ya mfululizo wa kampeni zilizofanyika katika mikoa mingine 11 tangu mwaka 2023, na mikoa sita inayoendesha kampeni hiyo nchini.

Kwa upande wake, Jaji Mfawidhi wa Mahak**a Kuu Kanda ya Mtwara, Rose Ebrahim, amesisitiza kuwa Mahak**a inashirikiana kikamilifu na serikali katika kuhakikisha kuwa haki inapatikana kwa wananchi kwa wakati, na kuwa kampeni hii ni muhimu katika kufanikisha malengo ya haki ya mwananchi.

Wananchi waliohudhuria uzinduzi huo wameelezea furaha yao kwa kupewa huduma ya kisheria kwa urahisi, wakiamini kuwa kampeni hii itasaidia kutatua changamoto mbalimbali za kisheria walizokuwa wakikabiliana nazo kwa muda mrefu.

Kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia (Samia Legal Aid campaign) itaanza utoaji huduma za kisheria kwa wakazi wa m...
23/01/2025

Kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia (Samia Legal Aid campaign) itaanza utoaji huduma za kisheria kwa wakazi wa mkoa wa Mtwara katika halmashauri tisa za mkoa huo kuanzia Januari 24 hadi Februari 2, mwaka huu.

Kwa mujibu wa Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, ambaye Mkurugenzi Msaidizi Huduma za Sheria kwa Umma, Abdulrhaman Mshamu ameeleza kuwa lengo kuu la Kampeni hiyo ni kulinda na kukuza upatikanaji wa haki kwa wote kupitia huduma ya msaada wa kisheria nchini.

Amefafanua kuwa, kampeni imejikita katika kutoa elimu ya kisheria kwa wananchi hususan katika masuala ya ukatili wa kijinsia, migogoro ya ardhi, mirathi, usuluhishi wa migogoro kwa njia mbadala, na masuala yahusuyo haki za binadamu kwa ujumla.

"Utekelezaji wa kampeni hii ni utekelezaji wa sheria ya Msaada wa kisheria namba 21 ya mwaka 2017 iliyotoa wajibu kwa serikali kuhakikisha inafikisha huduma za kisheria kwa wananchi wote" ameeleza

Mikoa 11, imefikiwa na Kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia tangu kuanza mwaka 2023 na mwaka huu 2025 inaendelea katika mikoa sita ikiwemo mkoa wa Mtwara.

Waratibu 100 wa Kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia (Samia Legal Aid campaign) kutoka halmashauri tisa za mkoa w...
23/01/2025

Waratibu 100 wa Kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia (Samia Legal Aid campaign) kutoka halmashauri tisa za mkoa wa Mtwara wamepatiwa mafunzo ya utekelezaji wa kampeni hiyo kuelekea kuanza kwa utoaji huduma ya kisheria kwa wakazi wa mkoa huo ambayo yataanza Januari 24 hadi Februari 2, mwaka huu.

Akiongea wakati wa kuzindua mafunzo hayo Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara Bi. Bahati Geuzye amewataka waratibu hao kuhakikisha kwamba mafunzo wanayopatiwa kuhusiana na kampeni hiyo yanakuwa chachu na kuwawezesha kuwahudumia wananchi ambao kwa kiasi kikubwa wamekuwa na uhitaji wa kupata huduma za msaada wa kisheria ili kuwasaidia kutatua changamoto mbalimbali za kisheria zinazowakabili.

Bi. Geuzye amesisitiza kuwa, wananchi watakapokuwa na uelewa wa masuala hayo ya kisheria kutasaidia kuondoa migogoro iliyopo baina yao na kufuata taratibu rasmi za kisheria katika masuala mbalimbali.

Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, ambaye Mkurugenzi Msaidizi Huduma za Sheria kwa Umma, Abdulrhaman Mshamu ameeleza kuwa lengo kuu la Kampeni ni kulinda na kukuza upatikanaji wa haki kwa wote kupitia huduma ya msaada wa kisheria nchini.

Amefafanua kuwa, kampeni imejikita katika kutoa elimu ya kisheria kwa wananchi hususan katika masuala ya ukatili wa kijinsia, migogoro ya ardhi, mirathi, usuluhishi wa migogoro kwa njia mbadala, na masuala yahusuyo haki za binadamu kwa ujumla.

"Utekelezaji wa kampeni hii ni utekelezaji wa sheria ya Msaada wa kisheria namba 21 ya mwaka 2017 iliyotoa wajibu kwa serikali kuhakikisha inafikisha huduma za kisheria kwa wananchi wote" ameeleza

Mikoa 11, imefikiwa na Kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia tangu kuanza mwaka 2023 na mwaka huu 2025 inaendelea katika mikoa sita ikiwemo mkoa wa Mtwara.



Mahak**a ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani, imemuhukumu John Christopher Kambanga (44), Mkazi wa Msufini Ml...
19/01/2025

Mahak**a ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani, imemuhukumu John Christopher Kambanga (44), Mkazi wa Msufini Mlandizi kwenda jela maisha kwa kosa la kulawiti, mtoto wa miaka 10 kitendo ambacho ni kinyume cha Sheria na maadili ya jamii.

Hakimu Mkazi wa Wilaya ya Kibaha Mhe. Felister Ngw'elu amesema kuwa tukio hilo lilitokea tarehe Mei 5, 2024 huko Msufini Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani.

Amesema kuwa John Christopher amehukumiwa kifungo hicho cha maisha jela baada ya ushahidi upande wa Jamhuri kukamilika pasi na shaka na kumtia hatia kwa kosa hilo.

Zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Mtwara Kuanza Januari 28, mwaka huu ambapo wananchi wenye changa...
19/01/2025

Zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Mtwara Kuanza Januari 28, mwaka huu ambapo wananchi wenye changamoto mbalimbali ikiwemo ya kuhama maeneo na mengineyo watapata nafasi ya kubadilisha taarifa zao.

Hayo yameelezwa Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Mhe. Jaji Rufaa Jacobs Mwambegele, wakati akizungumza na wadau wa uchaguzi mkoani Mtwara.

Katika mkutano huo, Mhe. Mwambegele alitangaza ratiba ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura katika mkoa wa Mtwara, ambapo zoezi hilo litaanza tarehe 28 Januari, 2025 na kumalizika tarehe 03 Februari, 2025.

Uboreshaji wa daftari hili utahusisha mikoa ya Mtwara, Lindi na Ruvuma, na utatekelezwa katika Halmashauri za Wilaya ya Madaba, Namtumbo na Tunduru.

Zoezi hili ni muhimu kwa kuhakikisha kwamba Daftari la Kudumu linakuwa sahihi na linakidhi mahitaji ya uchaguzi ujao.


Meli iliyobeba watalii kutoka nchi mbalimbali ikiwemo Uingereza, Costa Rica, Scotland, Australia  na Afrika Kusini, imew...
19/01/2025

Meli iliyobeba watalii kutoka nchi mbalimbali ikiwemo Uingereza, Costa Rica, Scotland, Australia na Afrika Kusini, imewasili katika Bandari ya Kilwa kwa lengo la kufanya shughuli za utalii kwenye vivutio mbalimbali vya utalii vilivyopo Kilwa Kisiwani.

Kwa mujibu wa nahodha wa meli hiyo, Paul Mchwampaka ambaye ni mkuu wa kitengo cha ubaharia kutoka Bandari ya Mtwara, amesema kuwa meli hiyo ijilikanayo kwa jina la Highdridean Sky imetoka katika visiwa vya Shelisheli na imekuja na watalii takribani 98 na mabaharia 81.

Afisa Utalii Daraja la Pili, Lembolos Ndengea ambaye ni afisa utalii kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Kanda ya Kusini Mashariki amesema kuwa ujio wa meli hiyo ni mwanzo wa kuanza kwa msimu wa utalii ambao huanza mwezi Januari hadi Aprili kila mwaka.

Ameongeza kuwa hadi sasa tayari meli saba za kitalii zimethibitisha kuja katika Bandari ya Kilwa kwa ajili kufanya shughuli za utalii.

Kwa mujibu wa Kanuni ya 15(20)(c) ya Kanuni za Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura za mwaka 2024, Tume ya Tai...
16/01/2025

Kwa mujibu wa Kanuni ya 15(20)(c) ya Kanuni za Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura za mwaka 2024, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeweka utaratibu maalum wa kuwawezesha wafungwa na wanafunzi waliohukumiwa kifungo cha chini ya miezi sita pamoja na mahabusu kuandikishwa k**a wapiga kura.

Hayo yamebainishwa leo Januari 16 na Kaimu Mkurugenzi wa Uchaguzi Bi. Giveness Aswile katika Mkutano wa Tume na wadau wa Uchaguzi kuhusu Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la wapiga kura uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi.

Hatua hii inalenga kuhakikisha kuwa makundi haya yanapata fursa ya kushiriki kikamilifu katika mchakato wa kidemokrasia, sambamba na haki yao ya kikatiba ya kushiriki uchaguzi.

Kwa upande wa Tanzania Bara, jumla ya vituo 130 vya kuandikisha wapiga kura vimeanzishwa ndani ya magereza mbalimbali huku kwa upande wa Zanzibar, vituo 10 vya kuandikishia vimewekwa kwenye vyuo vya mafunzo.

Utaratibu huu unaonyesha dhamira ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya kuhakikisha kuwa kila Mtanzania anayeweza kisheria anapata fursa ya kushiriki katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2024 bila kikwazo chochote, ikiwemo wale walioko katika maeneo ya magereza na vyuo vya mafunzo.

Imeandaliwa na Hadija Omary-Lindi

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa taarifa ya uwepo wa Kimbunga Dikeledi katika Bahari ya Hindi mwambao wa pw...
14/01/2025

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa taarifa ya uwepo wa Kimbunga Dikeledi katika Bahari ya Hindi mwambao wa pwani ya Msumbiji.

Katika taarifa yake, iliyotolewa leo Jumanne Januari 14, 2025 mamlaka hiyo inaeleza kuwa, mifumo ya hali ya hewa inaonesha kimbunga hicho kwa sasa kipo mwambao wa pwani ya Msumbiji na kinatarajiwa kurejea katika Rasi ya Msumbiji leo alasiri.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, kimbunga hicho hakiashirii uwezekano wa kusababisha athari za moja kwa moja hapa nchini.

“Hata hivyo, kutokana na ukaribu wa maeneo ambayo Kimbunga Dikeledi kipo sambamba na maeneo ya kusini mwa nchi yetu, upo uwezekano mdogo wa matukio ya vipindi vifupi vya mvua kubwa katika maeneo ya pwani ya kusini hususan katika mikoa ya Lindi na Mtwara kwa siku ya leo Januari 14, 2025,”inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Wavulana wawili ambao ni  Mapacha wamefikisha mahak**ani kwa tuhuma za kumuua Mama yao mzazi kwa imani za kishirikina, w...
13/01/2025

Wavulana wawili ambao ni Mapacha wamefikisha mahak**ani kwa tuhuma za kumuua Mama yao mzazi kwa imani za kishirikina, wilani Masasi, mkoani Mtwara.

Watuhumiwa hao wawili, Danford Steven Seif na Daniel Steven Seif, mapacha wa umri wa miaka 24, wametiwa mbaroni kwa tuhuma za kumuua mama yao, Upendo Methew Mayaya (42), baada ya kumshambulia kwa jembe na mwichi kwenye paji lake la uso.

Kulingana na Kamanda wa Polisi mkoani hapa SACP Issa J.Suleiman kwenye taarifa yake kwa Waandishi wa Habari kuwa, chanzo cha mauaji hayo ni masuala ya imani za kishirikina.

Aidha Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara limefanikiwa kuzuia uhalifu kupitia operesheni na misako iliyoendeshwa katika kipindi cha mwisho wa mwaka 2024.

Katika operesheni hiyo, wamek**ata wahalifu 25 wakiwemo watuhumiwa wa mauaji, kulawiti, wizi, na uhalifu mwingine, pamoja na kupata pombe haramu na dawa za kulevya.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara ameshukuru wananchi kwa ushirikiano wao na kuwataka kuendelea kutoa taarifa za uhalifu ili kudumisha usalama katika jamii.

Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Kundo Mathew ameweka jiwe la msingi katika mradi wa uchimbaji visima na ujenzi miundombinu...
12/01/2025

Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Kundo Mathew ameweka jiwe la msingi katika mradi wa uchimbaji visima na ujenzi miundombinu rahisi wa shilingi milioni 325 katika vijiji vitano wilayani Ruangwa Mkoani Lindi.

Mradi huo wa uchimbaji wa visima na ujenzi wa miundombinu rahisi katika vijiji vitano  ambavyo havina huduma ya maji ni program maalum ya Serikali ya uchimbaji visima 900 inayotekelezwa nchi mzima katika Majimbo yote ya uchaguzi.

Akizungumza mara baada ya kukagua na kuweka jiwe la msingi katika kisima cha maji huko katika kijiji cha Mmawa Mhandisi Kundo ametoa maelekezo kwa wakala wa maji na usafi wa mazingira kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati.

Amesema mpaka kufikia tarehe 31 mwezi huu maeneo yote ambayo hayajakamilika kutoa huduma yaanze kutoa huduma k**a dhamira ya Serikali ilivyotarajia .

Pia ameeleza kuwa Serikali ya Rais Samia inaendelea kutoa fedha za kutosha kwa ajili ya utekelezaji wa mradi ya maji lengo ni kuhakikisha wanqnchi wote wanapata huduma hiyo kwa ukaribu zaidi

Hata hivyo amemtaka Mhandisi wa maji kuhakikisha anafanya maboresho katika baadhi ya maeneo  ikiwa pamoja na mita na presha ya utokaji wa maji kwenye mabomba.

Kwa upande wake meneja wa Ruwasa wilaya ya Ruangwa Lawrence Mapunda amesema mradi huo unaltekelezwa kwa kutumia force akaunti ujenzi wake wa miundombinu umefikia asilimia 85.
Imeandaliwa na Hadija Omary-Lindi

Waziri wa Ujenzi, Mhe. Abdallah Ulega ametoa miezi mitatu kwa Mkandarasi  M/s China Railway 15 Bureau Group  Cooperation...
11/01/2025

Waziri wa Ujenzi, Mhe. Abdallah Ulega ametoa miezi mitatu kwa Mkandarasi M/s China Railway 15 Bureau Group Cooperation anayejenga Barabara ya Nachingwea-Ruangwa-Nanganga (KM 106), kukamilisha ujenzi wa daraja la Lukuledi.

Agizo hilo amelitoa leo wakati akikagua barabara na madaraja katika barabara hiyo na kusisitiza kuwa fedha zipo hivyo ni wajibu wa mkandarasi kuongeza kasi ili wana Ruangwa na Nachingwea wanufaike na mradi huo.

"Mtendaji Mkuu wa TANROADS simamieni mradi huu ukamilike kwa wakati na ujengwe kwa ubora ili udumu kwa muda na kuwawezesha wananchi wa wilaya za Ruangwa na Nachingwea kunufaika kwa kuyafikia masoko ya mazao yao kwa urahisi,” amesema Waziri Ulega.

Amesema ujenzi wa barabara hiyo uendane na uwekaji taa za barabarani ili kuondoa giza na kuchochea ukuaji wa miji na hivyo kuwawezesha wananchi kufanya biashara muda wote.

"Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ameelekeza katika miradi hii vijana na wanawake wa maeneo inapopita miradi hii wapewe kipaumbele kwa kazi wanazoweza kuzifanya ili wanufaike kiuchumi,”amesisitiza Waziri Ulega.

Address

1050
Mtwara

Telephone

+255682907172

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kusini Yetu Online Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Kusini Yetu Online Tv:

Videos

Share