28/05/2025
Ronaldinho Gaucho 🗣️: "Wakati Messi aliponilipia dhamana nikiwa gerezani na nikaachiliwa, nilikuwa katika hali mbaya, nilimtembelea mazoezi ya Barcelona na kumshukuru. Alinipa jezi ya Barcelona iliyosainiwa na yeye na baadhi ya wachezaji wa Barcelona, ​​aliniambia, "Unaweza kuiuza. Niliwasiliana na tovuti ya [jina kapuni]. Watainunua kutoka kwako, najua hutaki kuchukua pesa kutoka kwangu lakini hii ni njia nzuri," baada ya Siku moja, tovuti iliniita, lakini nilikataa.
"Niliwaambia, “Hii ni zawadi kutoka kwa rafiki yangu, na sitaiuza.” lakini nilishangaa kuona nimetumiwa Fedha kutoka kwenye tovuti (website) hiyo bila kuwauzia jezi.
"Nilipiga simu kwenye tovuti na kuwaambia, "Niliwaambia, sitaki kuiuza. Kwa nini mmehamisha pesa hizo kwenye akaunti yangu?" Meneja akaniambia, "Messi, ndiye alituomba hivi, alitupa jezi nyingine inayofanana na hiyo"
"Machozi yalinitoka. Sitasahau alichonifanyia baada ya kusalitiwa na kila mtu, Messi hakatai shukrani. Ndio maana mambo yanaenda sawa katika maisha yake kwa sababu moyo wake ni safi sana" Alisema Ronaldinho