MOtownTV

MOtownTV Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from MOtownTV, TV Channel, smbegu7@gmail. com, Moshi.

MOtownTV(motownmadia) ni online television inayotoa Habari mbali mbali Siasa,Burudan, Michezo na Braking News YouTube Tunapatikana kwa jina la MOtown TV na Instagram pamoja na twitter Tunapatikana kajina Hilo Hilo la MOtown TV

17/08/2024

Reginald Mengi na safari ya ufukara mpaka utajiri

"Nimezaliwa katika umasikini wa kutupwa, lakini jambo hilo hata siku moja halikunikatisha tamaa," ni moja ya kauli ambazo Reginald Abraham Mengi alikuwa hacoki kuzisema kila alipopata wasaa wa kuzungumzia alipotokea maishani.

Reginald Mengi ni jina kubwa Tanzania na Afrika kwa ujumla, lakini wajua ametokea wapi.

Mengi alizaliwa wilayani Machame, Kilimanjaro, Tanzania mwaka 1942, akiwa mmoja wa watoto saba wa Bw Abhraham Mengi na Bi Ndeekyo Mengi.

"Familia yetu ilikuwa masikini sana, kila siku ilikuwa ni vita ya kupambana na umasikini. Tulimiliki sio zaidi ya ekari moja tukiishi kwenye vibanda vya udongo tukichanganyika na ng'ombe wachache na kuku. Ninaporudisha fikra na kutazama nyuma ni vigumu napatwa na ugumu wa kufikiri namna tulivyoweza kuishi katika hali ile," alipata kusema kwenye uhai wake.

Alianza safari yake kielimu shule katika shule ya msingi Kisereny Village Bush School, kisha akajiunga Nkuu District School, kisha Siha Middle School, na baadaye Old Moshi Secondary School. Kwa ufadhili wa Chama cha Ushirika kilichokuwa na nguvu ya kifedha ushawishi KNCU Mengi alisomeshwa masomo yake ya shahada ya kwanza ya uhasibu nchini Uingereza.

Baada ya masomo ughaibuni, Mengi alirudi Tanzania 1971 na kuajiriwa na kampuni ya Cooper and Lybrand Tanzania ( sasa Prince water house Cooper) mpaka mwaka 1989 alipoamua kujikita kwenye ujasiriamali

Baada ya kuachana na ajira, Mengi aliiboresha kampuni yake ya Industrial Projects Promotion Limited na baadae kufahamika zaidi k**a IPP Limited.

Kupitia IPP Limited Mengi alaianzisha kampuni mbalimbali na kufanya biashara kadha wa kadha kuanzia uzalishaji wa sabuni, soda, maji ya kunywa, madini, mafuta, gesi asilia na kilimo.

Hata hivyo, umaarufu mkubwa wa Mengi ni kutokana na kumiliki vyombo vya habari, kuanzia magazeti, vituo vya runinga na redio. Runinga yake ya ITV pamoja na kituo cha Redio One ni moja ya vituo vikubwa vya utangazaji huku magazeti yake ya Guardian na Nipashe yakiwa miongoni mwa magazeti makubwa zaidi Tanzania.

Mpaka umauti unamfika, Mengi alikuwa Mwenyekiti wa Wamiliki wa Vyombo Vya Habari Tanzania.

Mengi pia amekuwa akijitoa katika kusaidia wasionacho na wenye uhitaji kwenye jamii ikiwemo walemavu wa ngozi na kugharamia matibabu ya watoto wenye matatizo ya moyo nchini India.

Mwaka 2014, jarida maarufu la masuala ya fedha Forbes lilikadiria utajiri wa Mengi kuwa unafikia Dola milioni 560.

Mjane wa Mzee ni Jacqueline Ntuyabaliwe ambaye alipata kuwa Miss Tanzania mwishoni ma miaka ya 90.

Vitu vingine niaibu sio vya kusema Sheep Keep Quite 🀫We ni   gani unaupenda kwenye   ya
16/08/2024

Vitu vingine niaibu sio vya kusema Sheep Keep Quite 🀫
We ni gani unaupenda kwenye ya

Ikiwa wanazungumza juu ya maisha ya watu wengine mbele yako usicheke na wewe, watazungumza juu ya maisha yako kwa watu w...
12/08/2024

Ikiwa wanazungumza juu ya maisha ya watu wengine mbele yako usicheke na wewe, watazungumza juu ya maisha yako kwa watu wengine

πŸŽ₯

11/08/2024

Bongo 5 wamefanya mahojiano na Ndugu wa Aliyekuwa Mwanamuziki wa Bongo Fleva Man Dojo na kuelezea Chanzo cha Kifo cha Mkongwe wa muziki wa Bongo Fleva.

MOtownTV

09/08/2024

TOXIC Fuvu atetea penzi lake kwa mwanamuziki mwenzie Abby Chams anasema bado ajaona k**a kunaugumu wakuwa kwenye mahusiano na msanii uyo.

09/08/2024
06/08/2024

Polisi watoa taarifa hatua waliyofikia katika kuwasaka watu 5 waliomkaba/kumlawiti msichana wa Dar

Leo nimefurahi sana kukutana na Dada yangu Petty Mbuya alikuwa akikomenti kwenye kila post niliuokuwa napost ya habari a...
31/07/2024

Leo nimefurahi sana kukutana na Dada yangu Petty Mbuya alikuwa akikomenti kwenye kila post niliuokuwa napost ya habari ata zangu binafsi na hata wakati nipo nafanya kazi kwenye redio moshi alikuwa Shabiki yangu wambele kabisa.

Kitendo cha kuchkua simu yake na kuniandikia maoni yake na wakati mwingine ananiombea kwenye komenti zake mbalimbali hii kwangu naithamini sana na Ninamshukuru mimi pia ni fan wake mkubwa sana.

Sasa anabiashara yake Sinza unaweza kwenda kumsapoti kwenye Biashara yake ya kuuza nguo unakilabsababu ya kuwa mteja wake kwani ananguo za k**e zenye Viwango vya juu kabisa Duka lake lipo maeneo ya kitambaa cheupe pale sinza linaitwa Miss boutique Fashion

Tupo hapa  msikizeee hapo  akiongelea   πŸ“Έ
30/07/2024

Tupo hapa msikizeee hapo akiongelea

πŸ“Έ

AMEANDIKA ALIEKUWA MPIGA PICHA WA ZAMANI WA Diamond Platnumz πŸ‘‡πŸΎThe year ni 2014 saa 11 alfajiri studio kwa Nilipiga hii ...
07/07/2024

AMEANDIKA ALIEKUWA MPIGA PICHA WA ZAMANI WA Diamond Platnumz πŸ‘‡πŸΎ

The year ni 2014 saa 11 alfajiri studio kwa
Nilipiga hii picha akiwa amepitiwa na usingizi baada ya kukesha akirekodi NITASHINDA ft Chegge hiyo nyimbo inayo play

Likisha swala la studio Diamond aliku yuko serious sana.. lazima tukeshe huko.. hata k**a nyimbo kashirikishwa siyo yake ataikeshea na k**a bado hajaridhika lazima atarudi kesho yake even if mwenye nyimbo ka relax zake nyumbani

K**a ni u freemasonry unaosemagwa ambao mimi mda wangu wote pale sikuwahi uona basi itakua masharti walompaga ni kujitesa kwa kupiga Kazi saana

Asante, Mungu, kwa zawadi ya uhai na kwa fursa zote za kujifunza, kukua, na kutumikia zinazoambatana nami.Thank you, God...
21/06/2024

Asante, Mungu, kwa zawadi ya uhai na kwa fursa zote za kujifunza, kukua, na kutumikia zinazoambatana nami.

Thank you, God, for the gift of life and for all the opportunities to learn, grow, and serve that come with it.

Are you genuinely happy?
06/06/2024

Are you genuinely happy?

Barcelona imemfuta kazi rasmi kocha wao Xavi ingawa bado atakuwa sehemu ya benchi kwenye mchezo wa jumapili dhidi ya Sev...
24/05/2024

Barcelona imemfuta kazi rasmi kocha wao Xavi ingawa bado atakuwa sehemu ya benchi kwenye mchezo wa jumapili dhidi ya Sevilla.

Uongozi wa Barcelona umemaliza mazungumzo na Hans Flick l huwenda akatambulishwa k**a kocha mpya kuelekea msimu ujao

Watoto waliodharaulika sasa Mungu anawaketisha na waLiowaheshimu ,Mungu azidi kuwa upande wao, wako na Wetu Pia.
24/05/2024

Watoto waliodharaulika sasa Mungu anawaketisha na waLiowaheshimu ,Mungu azidi kuwa upande wao, wako na Wetu Pia.

Watoto waliodharaulika sasa Mungu anawaketisha na waLiowaheshimu ,Mungu azidi kuwa upande wako na Wetu Pia. πŸ’ͺ🏽Ni nchi ga...
24/05/2024

Watoto waliodharaulika sasa Mungu anawaketisha na waLiowaheshimu ,Mungu azidi kuwa upande wako na Wetu Pia.

πŸ’ͺ🏽

Ni nchi gani unatamani Mw.mungu akujaalie Ufike na Kwanini πŸ‘‡πŸΎ niambie hapa.

22/05/2024

🐁 Gharama ya maziwa ya panya inazidi $22,000 (zaidi ya milioni 50 za kitanzania) kwa lita moja tu .Maziwa ya panya hutum...
22/05/2024

🐁 Gharama ya maziwa ya panya inazidi $22,000 (zaidi ya milioni 50 za kitanzania) kwa lita moja tu .

Maziwa ya panya hutumika katika utengenezaji wa dawa. Panya wa k**e hutengeneza kimikali inayoitwa lactoferrin, ambayo hutumiwa katika utengenezaji wa dawa za kipekee.

Tupe mawazo yako πŸ‘‡πŸ‘‡

Your love, kindness, and compassion have touched my heart in ways I cannot express. I am forever grateful for the positi...
02/05/2024

Your love, kindness, and compassion have touched my heart in ways I cannot express. I am forever grateful for the positive impact you was have on my life. Dear brother, thank you for being my forever ✊🏾

Njia NZURI ya KUITHAMINI leo nikuangalia nyakati NGUMU ulizopita na MW.MUNGU akakuvusha.
22/04/2024

Njia NZURI ya KUITHAMINI leo nikuangalia nyakati NGUMU ulizopita na MW.MUNGU akakuvusha.

Mtangazaji Mahiri wa Clouds FM, Gadner G. Habash Amefariki Dunia Leo April 20, 2024.Gadner maarufu k**a β€˜Captain’ alieji...
20/04/2024

Mtangazaji Mahiri wa Clouds FM, Gadner G. Habash Amefariki Dunia Leo April 20, 2024.

Gadner maarufu k**a β€˜Captain’ aliejizolea Umaarufu Mkubwa kupitia Kipindi cha Jahazi, alikua amelazwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Jijini Dar es Salaam kutokana na kusumbuliwa na Pressure (Shinikizo la Damu).

MOtownTV

Ni kheri kutazama pembeni ukisonga mbele kuliko kutazama nyuma ukienda mbele.Maana maumivu ya majuto yanaumiza kuliko uv...
17/04/2024

Ni kheri kutazama pembeni ukisonga mbele kuliko kutazama nyuma ukienda mbele.

Maana maumivu ya majuto yanaumiza kuliko uvumilivu wa mapito, ajabu ni kuwa hata ukiyakumbuka maumivu huwezi kuyabadili.

Kimsingi yasiyowezekana ni yote uliyo yaamini na yanayowezekana ni yote unayo yanuia, na maamuzi ya haya mawili yapo katikati ya uso na kisogo cha kila mtu.

Ingawa kutazama pembeni bila kujua unavyo tazama ni kupoteza uelekeo wa unako elekea, basi bora kwenda unakoenda ukitazama vitakavyo simulika mbele.

Anyways, ni kheri kukosa macho kuliko kukosa uelekeo.✍️

cc

Ni kheri kutazama pembeni ukisonga mbele kuliko kutazama nyuma ukienda mbele.Maana maumivu ya majuto yanaumiza kuliko uv...
17/04/2024

Ni kheri kutazama pembeni ukisonga mbele kuliko kutazama nyuma ukienda mbele.

Maana maumivu ya majuto yanaumiza kuliko uvumilivu wa mapito, ajabu ni kuwa hata ukiyakumbuka maumivu huwezi kuyabadili.

Kimsingi yasiyowezekana ni yote uliyo yaamini na yanayowezekana ni yote unayo yanuia, na maamuzi ya haya mawili yapo katikati ya uso na kisogo cha kila mtu.

Ingawa kutazama pembeni bila kujua unavyo tazama ni kupoteza uelekeo wa unako elekea, basi bora kwenda unakoenda ukitazama vitakavyo simulika mbele.

Anyways, ni kheri kukosa macho kuliko kukosa uelekeo.✍️

MOtownTV

The best mirror is an old friend ishi sana kaka
15/04/2024

The best mirror is an old friend ishi sana kaka

Nobody is real in this world. Everyone has a dual face.|●|Hakuna mtu wa kweli katika ulimwengu huu.  Kila mtu ana sura m...
03/03/2024

Nobody is real in this world. Everyone has a dual face.
|●|
Hakuna mtu wa kweli katika ulimwengu huu. Kila mtu ana sura mbili.

Rais Mstaafu wa awamu ya pili wa Tanzania, Ally Hassan Mwinyi amefariki Dunia leo Februry 29,2024 saa 11:30 Jioni katika...
29/02/2024

Rais Mstaafu wa awamu ya pili wa Tanzania, Ally Hassan Mwinyi amefariki Dunia leo Februry 29,2024 saa 11:30 Jioni katika Hospitali Jijini Dar es salaam alipokuwa akipatiwa matibabu kwa ya ugonjwa wa Saratani ya Mapafu.

Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ametangaza msiba huo leo ambapo amesema Mzee Mwinyi alikuwa akipatiwa matibabu tangu November 2023 London Uingereza na baadaye kurejea Nchini na kuendelea na matibabu Mzena Hospital.

Rais Sami ametangaza siku saba za maombolezo kuanzia kesho kufuatia kifo hicho.

Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania, Edward Lowassa (70) amefariki dunia leo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete, Dar es S...
10/02/2024

Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania, Edward Lowassa (70) amefariki dunia leo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete, Dar es Salaam.

Taarifa ya kifo chake imetangazwa na Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango.

Picha TBConline

Nusu ya thamani ya uzuri wa kitu inapungua pale tu unapokipata..
06/02/2024

Nusu ya thamani ya uzuri wa kitu inapungua pale tu unapokipata..

Address

Smbegu7@gmail. Com
Moshi

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MOtownTV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Videos

Share

Category


Other TV Channels in Moshi

Show All

You may also like