Kyela Fm Radio

Kyela Fm Radio Kyela Fm Radio Official Facebook Account
96.1 MHZ 📻
Sauti Yako, Mafanikio Yako.

Tunawatakia wasikilizaji wa Kyela Fm Radio na wafuatiliaji wote wa mitandao yetu ya kijamii Sikukuu ya Wapendanao yenye ...
14/02/2025

Tunawatakia wasikilizaji
wa Kyela Fm Radio
na wafuatiliaji wote wa mitandao yetu ya kijamii Sikukuu ya Wapendanao yenye upendo, Amani, na furaha tele. Muwe na wakati mzuri wa kusherehekea upendo na mshikamano na wale mnaowathamini, Upendo Udumu kila Siku .

🛑 Mara Baada ya Kufungwa Jana na Tabora united Msemaji wa Kagera Sugar Manzanzala ameongea na  kuwa Hadi sasa hajaamka k...
12/02/2025

🛑
Mara Baada ya Kufungwa Jana na Tabora united Msemaji wa Kagera Sugar Manzanzala ameongea na kuwa Hadi sasa hajaamka kwa sababu ya uchungu wa kupoteza Mechi Muhimu jana.

Kagera sugar ipo Nafasi ya 15 Mechi 18 Alama 12.

Mara Baada ya Kufungwa Jana na Tabora united Msemaji wa Kagera Sugar Manzanzala ameongea na kuwa Hadi sasa hajaamka kwa sababu ya uchungu wa ku...

🛑 Kijana mmoja mkazi wa kitongoji cha Ushirika kati, kata ya Mpuguso, wilayani Rungwe,Mkoani Mbeya anayekadiriwa kuwa na...
11/02/2025

🛑
Kijana mmoja mkazi wa kitongoji cha Ushirika kati, kata ya Mpuguso, wilayani Rungwe,Mkoani Mbeya anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka kati ya 20-25 amekutwa akiwa amefariki dunia kwa kujinyonga na kamba ndani ya nyumba yao.

Akizungumza na kituo hiki mapema hii leo February 11,2025 Diwani wa kata ya Mpuguso Japhet Mwakagugu amesema kuwa tukio hilo limetokea siku ya jana jumatatu majira ya mchana.

Kijana huyo aitwaye Ezma Mawazo enzi za uhai wake alikuwa akijishughulisha na biashara ya uchomaji nyama katika eneo la Stand ya ushirika Mjini.

Bado hakijafahamika chanzo cha kijana huyo kuchukua hatua ya kujinyonga kwakuwa hakuna taarifa yoyote aliyoiacha.

Kijana mmoja mkazi wa kitongoji cha Ushirika kati, kata ya Mpuguso, wilayani Rungwe,Mkoani Mbeya anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka kati ya 20-25 amekutwa a...

🛑 🛑Mabadiliko ya Makocha katika Klabu ya yanga  kumesababisha Wachezaji kutoelewa Mifumo ya Walimu Mapema  hii inaweza k...
11/02/2025

🛑 🛑
Mabadiliko ya Makocha katika Klabu ya yanga kumesababisha Wachezaji kutoelewa Mifumo ya Walimu Mapema hii inaweza kusababisha yanga isichukue Ubingwa wa Ligi kuu Msimu huu.

Benzo Sanga ×

Sikiliza Kyela Fm Radio 96.1 Ukiwa eneo lolote Nyanda za juu Kusini

🛑 🛑Siku kadhaa zimepita tokea kuwepo kwa Taarifa ya mtu mmoja kukutwa amekufa uwanja wa mchaga hapa wilayani Kyela .Hati...
10/02/2025

🛑 🛑
Siku kadhaa zimepita tokea kuwepo kwa Taarifa ya mtu mmoja kukutwa amekufa uwanja wa mchaga hapa wilayani Kyela .
Hatimae amejulikana kuwa ni Frances Mbukwa ambaye ni katibu mwenezi chama Cha Mapinduzi tawi la Mbugani kata Mbugani wilayani Kyela .

Wakizungumza kwa masikitiko makubwa viongozi wa chama na serikali pamoja na majirani wameipokea kwa masikitiko makubwa taarifa hiyo ya Ts jina marufu na kusema kuwa alikuwa ni Mtu wa watu na mwanachama mpiga kazi kwa kitongoji chake na kata kwa ujumla .
Kwa mujibu wa Tarifa kutoka kwa msemaji wa Familia ndugu Ts atazikwa kesho .

Nb.Jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi juu ya kifo Cha marehemu na kwa wenyeji wa Kyela nyumbani kwa marehemu ni karibu na kanisa la kasunga Mungu ailaze mahala pema peponi roho ya marehemu Amina .

Siku kadhaa zimepita tokea kuwepo kwa Taarifa ya mtu mmoja kukutwa amekufa uwanja wa mchaga hapa wilayani Kyela .Hatimae amejulikana kuwa ni Frances Mbukwa a...

Timu ya Sungura FC Bingwa wa ligi Daraja la Tatu Mkoa wa Mbeya, Kutoka Wilayani Kyela imenyang'anywa ushiriki wa ligi ya...
07/02/2025

Timu ya Sungura FC Bingwa wa ligi Daraja la Tatu Mkoa wa Mbeya, Kutoka Wilayani Kyela imenyang'anywa ushiriki wa ligi ya Mabingwa Wa Mikoa kwa Sababu ya kukosa Vyeti vya usajili wa Timu.

Akizungumza na Kipindi cha ​ hii leo Mwenyekiti wa Chama cha Mpira Mkoa wa Mbeya (MREFA) Ndugu Sadick Jumbe ameeleze kuwa Miongoni mwa Sababu iliyopelekea Sungura FC kutoenda Kushiriki ligi ya Mabingwa Wa Mikoa ni Kukosa cheti cha Usajili ilihali walikuwa na Namba ya usajili Jambo ambalo kanuni za FIFA hazirusu

Timu ya Sungura FC Bingwa wa ligi Daraja la Tatu Mkoa wa Mbeya, Kutoka Wilayani Kyela imenyang'anywa ushiriki wa ligi ya Mabingwa Wa Mikoa kwa Sababu ya kuko...

Kwa unavyoliona Kundi hilo unadhani Tutatoboa Kwenda Hatua inayofuata?1.TANZANIA2.UGANDA3.TUNISIA4.NIGERIAComment tutapi...
28/01/2025

Kwa unavyoliona Kundi hilo unadhani Tutatoboa Kwenda Hatua inayofuata?

1.TANZANIA
2.UGANDA
3.TUNISIA
4.NIGERIA

Comment tutapitia kwenye saa 10:00-01:00 Mchana.

🛑LIVE: Kyela fm Radio Tupo Live kwenye UCHAGUZI MKUU CHADEMA LEO MLIMANI CITY. 🛑 Sikiliza Kupitia   na Tizama Live Kupit...
21/01/2025

🛑LIVE: Kyela fm Radio Tupo Live kwenye UCHAGUZI MKUU CHADEMA LEO MLIMANI CITY. 🛑 Sikiliza
Kupitia na Tizama Live Kupitia Account yetu ya YOUTUBE Bofya 👇

Endelea kutufuatilia Kupitia Kyela Fm DigitalFacebook: KyelafmRadioInstagram: Kyelafmradio

Helloooo MWANAKWETU,👋 Baada ya vikao vya Muda mrefu vya mipango na mikakati Kwaajili ya  Mwaka 2025 Sasa HESABU ZIMEKUBA...
05/01/2025

Helloooo MWANAKWETU,👋 Baada ya vikao vya Muda mrefu vya mipango na mikakati Kwaajili ya Mwaka 2025 Sasa HESABU ZIMEKUBALI✅
Rasmi Kuanzia Juma 3 Hii 06/01/2025 Kyela FM Tumejiandaa vyakutosha Kuhakikisha Tunakupa Kampani MWANAKWETU kwakuwa nawe bega kwa bega katika Safari Yako kuelekea Ushindi.
Tumekubaliana Kuisikia SAUTI YAKO nakuitumia kushiriki Mchakato Wa kujenga msingi wa MAFANIKIO yako Kwa sababu Sasa tumeshaKUWA ZAIDI na safari yetu inasubiri kushiriki nawe HATUA yako nyingine...
Wewe na sisi tukiwa na mdundo mmoja, 2025 HATUA KWA HATUA. 📻

Tuambie Ukweli X-Mass ya mwaka huu Imekukuta Ukiwa Wapi!?
24/12/2024

Tuambie Ukweli X-Mass ya mwaka huu Imekukuta Ukiwa Wapi!?


Jeshi la Polisi Nchini limetoa onyo na kupiga marufuku maandamano yaliyotangazwa na Viongozi wa CHADEMA September 23,202...
13/09/2024

Jeshi la Polisi Nchini limetoa onyo na kupiga marufuku maandamano yaliyotangazwa na Viongozi wa CHADEMA September 23,2024 na kusema Mtu yeyote atakayeingia barabarani atakabiliwa vilivyo kwa mujibu wa sheria za Nchi.

Akiongea Mjini Moshi leo September 13,2024, Msemaji wa Polisi, David Misime amesema “September 11,2024 kupitia Vyombo vya Habari na Mitandao ya Kijamii walisikika Viongozi wa CHADEMA akiwemo Mwenvyekiti wa Chama hicho (Freeman Mbowe), akiwahamasisha Viongozi wa Dar es salaam kuingia barabarani kuanzia September 23,2024, Viongozi hao waliendelea kuhamasisha Wananchi wa Kanda mbalimbali Nchini kukutana Dar es salaam ili kuungana na Wakazi wa Dar es salaam kuingia barabarani”

“Hatua hiyo waliyofikia tunajiuliza na tunaendelea kufuatilia na kuchunguza kwanini wanataka kututoa kwenye reli ya hatua za kiupelelezi zinazoendelea baada ya Rais Samia kuviagiza Vyombo vya Uchunguzi vifanye uchungizi kisha wawasilishe uchunguzi kwake”

“Ikumbukwe mara kadhaa Viongozi na Wafuasi wa Chama hicho wamekuwa wakipanga, kuratibu mikakati mbalimbali na kutoa matamshi yenye lengo la kuleta vurugu Nchini ili kuharibu amani ya Nchi yetu kwasababu wanazozijua wenyewe”

“Jeshi la Polisi linatoa onyo kwa Viongozi wa Chama hicho kuacha kuendelea kuhamasisha Wananchi kujihusisha katika uhalifu huo na yoyote atakayeingia barabarani atakabiliwa vilivyo kwa mujibu wa sheria za Nchi, kwa maana hiyo maandamano hayo yamepigwa marufuku, naomba kurudia kwa maana hiyo maandamano hayo yamepigwa marufuku”

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema vitendo vya utekaji na mauaji vinavyoendelea nch...
13/09/2024

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema vitendo vya utekaji na mauaji vinavyoendelea nchini havikubaliki na yeyote na kuongeza kuwa vitendo hivyo vinafanywa na watu aliowaita ‘genge’ la wasioitakia mema nchi.

Dkt. Nchimbi amesema kutokana na hilo, CCM na vyama vya upinzani vinapaswa kuungana pamoja kupinga vitendo hivyo.
"...tunao wajibu mkubwa sana wa kuhakikisha kwamba tunaacha kunyoosheana vidole tunahakikisha kwamba uchunguzi wa kweli na wa kina unafanyika..."Emmanuel Nchimbi - Katibu Mkuu CCM

Idadi ya vifo hadi sasa nchini Vietnam vimefikia watu 152, maelfu ya watu wamehama kutoka makazi yao ya jiji, Wilaya 10 ...
13/09/2024

Idadi ya vifo hadi sasa nchini Vietnam vimefikia watu 152, maelfu ya watu wamehama kutoka makazi yao ya jiji, Wilaya 10 kati ya 30 ziko kwenye tahadhari ya mafuriko, vyombo vya habari vya serikali nchini Vietnam vimeripoti.

“Kuanzia Jumatatu [Septemba 23] sisi tutaingia barabarani kudai tunachoona ni uhai wa watu wetu waliopotezwa, vinginevyo...
13/09/2024

“Kuanzia Jumatatu [Septemba 23] sisi tutaingia barabarani kudai tunachoona ni uhai wa watu wetu waliopotezwa, vinginevyo serikali imechukua hatua za haraka na za makusudi kuwarejesha, watu kujiuzulu, na watu wote kuwajibika.” - Freeman Mbowe, Mwenyekiti CHADEMA

LATRA imesitisha Leseni ya kusafirisha abiria kwa kampuni ya mabasi ya KATARAMA Luxury kutokana na kuchezea kifaa cha ku...
13/09/2024

LATRA imesitisha Leseni ya kusafirisha abiria kwa kampuni ya mabasi ya KATARAMA Luxury kutokana na kuchezea kifaa cha kufuatilia mwenendo wa magari (VTD) kwa kuondoa kifaa kilichofungwa katika mabasi yake na kufunga kifaa kingine kilichosababisha utumaji wa taarifa potofu katika mfumo wa VTS.

Kosa hilo, lilibainika baada ya wataalamu kufanya uchunguzi na kubaini kuwa kosa hilo haliwezi kuvumilika na linahitaji uchunguzi Zaidi kufanyika na watuhumiwa kufikishwa Mahakamani kwa mujibu wa sheria.

Kampuni ya Katarama imekuwa ikiendelea na makosa hayo hata baada ya kusitishiwa leseni na kurejeshewa kwa mara kadhaa.

Kufuatia kikao hicho, Mamlaka imetoa onyo kali kwa makampuni ya usafirishaji ya ABOOD Bus Service, BM Coach na SUPER FEO na kuwataka wazingatie Sheria, Kanuni na taratibu zilizowekwa.

Kikao hicho kimefanyika Ofisi ya LATRA Dar es Salaam, Septemba na kuhudhuriwa wadau mbalimbali wakiwemo Chama cha wamiliki wa mabasi Tanzania (TABOA), Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, pamoja na Wamiliki na Wawakilishi wa Makampuni hayo.

Kilio na simanzi Vimetawala katika msiba wa mtoto Ufunuo Mwamlima aliyekuwa Mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika Shule...
13/09/2024

Kilio na simanzi Vimetawala katika msiba wa mtoto Ufunuo Mwamlima aliyekuwa Mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika Shule ya Sekondari Mpakani A iliyopo Halmashauri ya Mji Tunduma Mkoani Songwe ambaye amefariki baada ya kujichoma na kisu tumboni usiku wa kuamkia septemba 10 nyumbani kwao Mtaa wa Chapwa A.

Baba mkubwa wa Marehemu Fadhiri Mwamlima akizungumza kwa niaba ya Familia amesema kuwa usiku wa septemba 10 ,2024 wazazi walimuita kijana wao kumhoji juu ya matukio ya wizi wa hela kwenye kibanda chao ndipo kijana alikiri kuwa na chenji alizodai anaenda kuzichukua ili awaletee na baadaye walisikia kelele kutoka jikoni ambapo walipotoka walikuta kijana huyo amejichoma kisu na utumbo uko nje na alifariki wakati wakiwa njiani wakimpeleka hospitali kwaajili ya Matibabu.

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Chapwa A Steven Minga amethibitisha kutokea kwa tukio hilo huku Diwani wa kata hiyo Chapwa A, Amos Siame ametoa rai kwa wazazi na walezi kuendelea kuwa karibu na watoto wao ikiwemo kuwazuia kuangalia filamu ambazo zina maudhui ya kujiua ili kuwaondoa na dhana ya kufanya hivyo.

Mkuu wa jeshi la polisi nchi |GP Camillius Wambura amesema hali ya nchini ni shwari kutokana na umahiri wa jeshi la poli...
13/09/2024

Mkuu wa jeshi la polisi nchi |GP Camillius Wambura amesema hali ya nchini ni shwari kutokana na umahiri wa jeshi la polisi katika kupambana na uhalifu kwa kushirikiana na raia wema.

Akizungumza katika ufunguzi wa mkutano mkuu wa maofisa wakuu waandamizi wa jeshi la polisi uliofanyika katika shule ya polisi Moshi wenye lengo la kujadili na kutathmini mikakati ya jeshi hilo.

Kwa upande wake naibu waziri wa mambo ya ndani, Daniel Sillo amelipongeza jeshi la polisi kwa kulinda na kuhakikisha amani inaendelea kuimarika, huku akiwataka waendelee kuwa karibu na jamii katika kupata ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yao.

Address

Kyela
Mbeya
600

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kyela Fm Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Kyela Fm Radio:

Videos

Share